Sishauri mtu kusoma PhD OUT

Sishauri mtu kusoma PhD OUT

Mara kadhaa huku kwenye makundi sogozi ya OUT nimekuwa nikiwapa za uso kwa watumishi wake kukosa weledi, hawana customer care kabisa.

Halafu wanakera sana tabia yao ya kutoa matokeo nusu nusu, kwa mfano ikiwa hawaja kuwekea matokeo ya somo moja utasota sana hadi kuja kuwekewa, ukiwajulisha wahusika hawatatui kwa wakati mara wasipokee simu, na hata ukiwacheki WhatsApp utaishia kuchezea blue tick tu.

Kinachochekesha zaidi kwamba wewe ambaye hujawekewa matokeo ndio uwape taarifa ya 'missing results' wao wenyewe sijui hawana mifumo ya kutambua au vipi...!! Wanachofanya hakiakisi maana ya CHUO HURIA, matarajio yangu ilikuwa kuona chuo hiki kinakuwa mstari wa mbele kiteknolojia lakini bado wapo analoji.

OUT mnachosha.!!
 
kuna wengine ni punda aisee,bila kiboko hawatimizi majukumu yao

watu wa aina hiyo wakibanwa kisawasawa lazima waite udikteta
Mh. Mwendazake ndiyo yaliyomkuta.

Taasisi kama hiyo ya "Chuo Kikuu Huria Tz" na nyingine za serikali ni majanga yani.

Watu wanajikuta sana utadhani walilazimishwa kuomba hizo nafasi za kazi.
 
Katika makosa niliyofanya katika maisha ni kujiunga na masomo ya PhD pale Open University of Tanzania. Ningelijua ningeeda UDSM. Kwa matatizo ninayopitia sishauri mtu akasome PhD pale OUT.

Chamgamoto nilizopitia ni kama ifuatavyo:

1. Supervisor kutojibu email zangu au hata sms kwa zaidi ya mwaka mmoja.

2. Supervisor kukaa kimya bila kupitia proposal kwa zaidi ya mwaka mzima na Wala hajali. Unamtumia kazi zaidi ya mara kumi ila hajibu na yupo kimya kana kwamba hakujui.

3. Process ya kubadilisha supervisor ni ngumu Sana, unaweza kukaa mwaka mzima unahangaika tu. Nilijaza fomu ya kubadilisha supervisor wakaa kimya, nilipowakomalia wakanipa fomu nyingine, stori ikaishia hapo.

4. Yule mdada au secretary wa ofisi ya post graduate research wa OUT ana dharau Sana. Ukimpigia simu hapokei na hata akipokea akajua ni wewe ana kata simu yako. Yule dada ni shida Sana.

5. Kwa sisi tulioko mikoani ni shida kusoma PhD OUT. Hawajali kabisa. Na ukisema usafiri kwenda huko Dar utazungushwa mpaka uchoke. Nimeenda Dar kituoni kwao pale Biafra ni shida tu hakuna la maana la kunisaidia.

Kutokana na OUT kunisumbua kwa muda wa miaka mitatu huku ada yangu wamekula ila kunisaidia kwao wanaona mzigo au usumbufu kwakweli ni Bora niache kusoma hiyo PhD nifanye mambo mengine. Ila wamenipotezea muda, hiyo miaka mitatu imeenda Bure. Yani miaka mitatu unahangaika na proposal haijawahi kusahishwa hata kusomwa tu na supervisor. Ukienda ofisini kwao Biafra unaambiwa supervisor wako hayupo amesafiri.

7. Kwa kweli OUT mnakatisha tamaa, mtu anakuwa kama hasomi PhD. Kama uwezo wa kusimamia tafiti za wanafunzi wa PhD hapo si mnamwambia mwanafunzi atafute chuo kingine kuliko kupoteza muda wa mtu.
OUT ni chuo cha Walimu na wafanyakaz wa Halmashaur hakina Weledi wowote...pale lbda kama unataka upoteze muda wako kasome pale
 
Mkuu sijui unafeli wapi? Unasoma PhD na unalalamika upo serious kweli? Unafikiri supervisor wanakula email?
Tengeneza na weka mazingira supervisor wako akutambue na siku moja moja akupigie simu akijidai amekosea au anataka kukusalimia tu!
Nilitaka nimshauri hivi hivi mkono mtupu haulambwi. Sikuhizi hadi kwenye misiba kuna rushwa. Mc anapewa rushwa ilimradi aseme natambua uwepo wa Adverse effect. Hasa hasa wanasiasa.
 
Pole sana mdau! Machungu uliyo nayo NDIYO yaliyonipata! Mimi nilimaliza miaka mitano bila kufanya presentation ya proposal. Yaani unatuma proposal kwenye email jamaa hajibu chochote! Unapiga simu weee lakini wapi! Mwisho nikaamua kuapply chuo kingine, Ada niliyolipa pale kama M3.5 ikaenda bure kabisa! Kwa Sasa nasoma chuo kingine vizuri kabisa hapa hapa TZ! Kile chuo hakina mfumo wa kumonitor masupervisor! Wanapuyanga tu kama wanavyojisikia! NI AIBU SANA KWA CHUO KIKUBWA KAMA KILE KUSHINDWA KUWASIMAMIA WAAJIRIWA WAKE WAFANYE KAZI WALIYOANJIRIWA KUFANYA.
 
Katika makosa niliyofanya katika maisha ni kujiunga na masomo ya PhD pale Open University of Tanzania. Ningelijua ningeeda UDSM. Kwa matatizo ninayopitia sishauri mtu akasome PhD pale OUT.

Chamgamoto nilizopitia ni kama ifuatavyo:

1. Supervisor kutojibu email zangu au hata sms kwa zaidi ya mwaka mmoja.

2. Supervisor kukaa kimya bila kupitia proposal kwa zaidi ya mwaka mzima na Wala hajali. Unamtumia kazi zaidi ya mara kumi ila hajibu na yupo kimya kana kwamba hakujui.

3. Process ya kubadilisha supervisor ni ngumu Sana, unaweza kukaa mwaka mzima unahangaika tu. Nilijaza fomu ya kubadilisha supervisor wakaa kimya, nilipowakomalia wakanipa fomu nyingine, stori ikaishia hapo.

4. Yule mdada au secretary wa ofisi ya post graduate research wa OUT ana dharau Sana. Ukimpigia simu hapokei na hata akipokea akajua ni wewe ana kata simu yako. Yule dada ni shida Sana.

5. Kwa sisi tulioko mikoani ni shida kusoma PhD OUT. Hawajali kabisa. Na ukisema usafiri kwenda huko Dar utazungushwa mpaka uchoke. Nimeenda Dar kituoni kwao pale Biafra ni shida tu hakuna la maana la kunisaidia.

Kutokana na OUT kunisumbua kwa muda wa miaka mitatu huku ada yangu wamekula ila kunisaidia kwao wanaona mzigo au usumbufu kwakweli ni Bora niache kusoma hiyo PhD nifanye mambo mengine. Ila wamenipotezea muda, hiyo miaka mitatu imeenda Bure. Yani miaka mitatu unahangaika na proposal haijawahi kusahishwa hata kusomwa tu na supervisor. Ukienda ofisini kwao Biafra unaambiwa supervisor wako hayupo amesafiri.

7. Kwa kweli OUT mnakatisha tamaa, mtu anakuwa kama hasomi PhD. Kama uwezo wa kusimamia tafiti za wanafunzi wa PhD hapo si mnamwambia mwanafunzi atafute chuo kingine kuliko kupoteza muda wa mtu.
kwa usalama wa mwili na akili waachie ada ukaombe chuo kingine kama
lakini tujikumbushe haya kwa mwanafunzi anayesoma Phd chuo bora na chenye mifumo safi ya technology
mwanafunzi anafatiliwa kabisa hatua kwa hatua kuhusu thesis yake au dissertation yake
mwalimu nae anafatiliwa zaidi kuona kuwa wanafunzi wake wanakamilisha kwa wakati dissertation zao
uongozi wa chuo unafatilia kila hatua na kama mwanafunzi anaonekana kuchelewa unaulizwa sababu nini upo pale kukamilisha ndoto zake na sio kufeli ndio maana mwl akiona unafeli anakurekebisha hizi ndio hatua muhimu kabisa kwa vyuo bora duniani nafikiri kwa afrika hakuna
basi tuyaache hayo acha kusoma hapo omba vyuo hivi nmezipanga kwa mpangilio
  1. ESAMI Home • ESAMI
  2. The Nelson Mandela African Institution of Science and Technology (NM-AIST)
  3. UDSM
  4. UDOM
  5. SAUT
ila kama una nafasi omba za ulaya
 
Back
Top Bottom