Kuangalia mpira na
Wanawake.
Wana maswali.....
>Mbona hawa Brazil
hawamchezeshi Neymar ??
:aliumia mechi iliyopita, hawezi
kucheza
>mbona hawajamkodi MESSI??
:hairuhusiwi kukodi..
>kwann asihamie Brazili?,..
:izo sio nyumba za kupanga
kwamba anahamia tu,mpaka uwe
una uraia wa Nchi yako.
>mbona hadi wanawake
wanacheza umo uwanjani?
:wapo wapi hao wanawake
>sihawo wa Brazil wenye nywele
ndefu?
:hapana hawo ni Wanaume,mmoja
anaitwa David Luiz,na huyo
mwingine WILLIUM
>Mbona hao wengine wanapiga
Penalty tano wenyewe?eti Refa
anapendelea?
:hakuna Penalty hapo ni
magoli,Brazil wamezidiwa
wanafungwa..
>Eti mbona Goli 7 ni nyingi na ni
Dk ya 80, kwann refa hamalizii tu
hapo si bingwa alishajulikana.
::sheria ya mpira mpaka Dk 90
zitimie..
>Huu si mpira wa miguu??
::Ndio we,nyie mnaonaje?
>mbona huyo mwingine anadaka
na mikono?
:huyo ni kipa
>kwann huyu Kipa wa Brazil
asikimbie na mpira adi goli
jingine alafu afunge apunguze
magoli au hajui huo ujanja?
Aaaaaaa jamani