Inawezekana kuna mambo ya kishirikina ndani yaki, lastime kuna waliokuwa wanasema yule kiongozi wa Mwenge at last lazima anakufa sijui kama lina ukweli hili.
Kuna wazee fulani pale Kilimanjaro maeneo ya Kiboriloni(kwa sasa hawapo tena) walikuwa wakisikia mwenge unakuja Moshi walikuwa wanaondoka maeneo ya hapo wanaenda huko milimani suala ni kwamba wasiuone tu huo mwenge mpaka utakapoondoka na wanasema walikuwa wakiamini kwamba ukiuona Mwenge unaweza kupata nuksi, balaa, mikosi na vilevile kuna mambo makubwa ya kishirikina yanafanyika.
Sisi vijana wa leo tujiulize Mwenge una faida gani kwa mwananchi na nchi wa/ya Tanzania?
Kwanini uwe mjinga? Kwanini usitumie akili? Kwanini ufikirie kuwa kunamashetani?
Mwenge wa Uhuru haunaconnection na imani ya aina yote.
Halafu baadae utasema kumpigia saluti raisi ni kumuabudu.
Dhana ya mwenge wa uhuru ni kuwamulika wanyonyaji wote na kuleta mshikamano.
Hivi umezaliwa mwaka gani vile?
Ondoa imani potofu ndani ya akili zako.
Kwani wazee kuchinja mbuzi au kondoo ndio kuabudi mashetani?
Hiyo ni ishara ya furaha na Mlima kilimanjaro ndio mrefu kuliko yote Africa.
Hauna jipya zaidi ya kuabudu mashetani. Kuna taarifa rasmi kuwa Mwenge huo unapofika Rombo-Kilimanjaro hufanyiwa tambiko mbalimbali ili kulinda viongozi wa nchi.
Taarifa zinaonesha kuwa kuna Wazee maalum wameandaliwa kule Rombo kwa ajili ya matambiko haya kila mwaka.Mmoja wa wazee hao aitwaye Mzee Malamsha amenithibitishia hicho.
Kwenye matambiko hayo,kafara hutolewa.Na kadhalika na kadhalika.Ndio maana,kila mwaka Mwenge wa Uhuru lazima ukimbizwe Mkoa wa Kilimanjaro na kufika Wilaya ya Rombo.
Mwenge huu ni wa kuupiga vita. Unaleta laana zaidi ya baraka. Unatubakisha kama nchi kwenye kuabudu mizimu badala ya kusonga mbele kimaendeleo.
Laana za Mwenge huu ndizo zinazotufanya tusieendelee. Ni muda sasa wa kuachana na imani hizi za kishirikina kwa kuachana na Mwenge huu.
Sijakuelewa Akili ya grade C ama D ndio ikoje hiyo ?