Siri ya Mwenge wa Uhuru


unachosema mkuu acheche kina ukweli, nakumbuka 2007 nilikuwa najitolea kufundisha shule flani kijijini kwetu, mwenge ukaja kuzindua jengo la bweni la wasichana, nilipewa assignment ya kuandaa ndoo ya mchanga na kuupeleka staff room, baada ya mwenge kufika ulioelekwa ofisini kisha ukazungukwa na wanajeshi, then ulizimwa halafu wakamwaga majivu na(mchanga?) kwenye mfuko, kisha wakaweka tena mchanga kidogo kutoka kwenye ile ndoo kwenye ule mwenge, ukawashwa shuguli za uzinduzi zikaendelea. nilipouliza hakuna aliyenipa jibu zaidi ya kusema kuwa baada ya kuhitimisha mbio za mwenge mchanga ule na majivu yale yaliyokusanywa nchi nzima huwekwa kwenye chombo kimoja na kusemewa vineno hv, then hutupwa baharini, ati ili kudumisha muungano...
 
Hao watu wa Rombo wanapenda sana matambiko, kila Dec lazima wakatambike.... Mwenge wa Uhuru unaendeleza tabia chafu na matumizi mabaya ya rasilimali....hivi nao huwa wanatengewa mil18 kutibiwa kama watapata ukimwi?
 

Kuna wanyonyaji zaidi ya viongozi wa CCM? Mbona hawajamulikwa? We umekaririshwa tu ili kujibu mitihani, hutumii akili zako kupambanua mambo. Hivi huwezi kujiuliza ni kwa nini sehemu unapolala mwenge uvunjaji wa sheria huwa ni sawa tu? Wauza bangi, gongo, mirungi sambamba na watumiaji huwa hawabughudhiwi. Ni kweli kabisa Mwenge una kila chembe ya kishetani; kwanza huanza kwa kuchangisha wafanyabiashara fedha ambazo matumizi yake huwa hayajulikani; eti mafuta ya mwenge .... UPUUZI MTUPU.
 
ni kwel mwenge unahusishwa na iman za kshetan,kama upo kwa ajil ya kumulika wanyonyaji kwann ufanyiwe tambiko?na wanyonyaj ndio wahucka wakuu wa mbio za mwenge,,,vijana 2natakiwa kuwa makin na hii isue.MABADILIKO YANAANZA KWA VIJANA..God blec tz.
 

Ñi ushirikina mtupu
 
mwenge uwekwe kwenye jumba la makumbusho hakuna haja ya kuutembeza nchi nzima.
 
Nimemsikiliza Nyambari Nyangwine akijustify umuhimu wa Mwenge wa Uhuru, lakini kimsingi mawazo yake yamenifanya nijihoji kama vitabu anayoandika anaandika yeye au anaandikiwa. Mojawapo ya justification aliyotoa ni kwamba "Mwenge wa Uhuru unaleta Faraja". Mheshimiwa huyu hajui mchango mkubwa wa mikesha ya mwenge wa uhuru katika mmomonyoko wa maadili na maambukizi ya VVU...Ufuska huongezeka zaidi wakati wa mbio wa mwenge! Hata Mtu mwenye akili ya grade C hata D anaweza kujiuliza je VVU ndiyo faraja anayoiongelea Nyangwine inayotokana na Mwenge?

Pili, mheshimiwa huyu amedhihirisha uwezo mdogo wa kufikiri kwa kutojua maana ya msanii- kwake mwandishi wa vitabu -academic, novel n.k ndiye msanii! Mwanamuziki siyo msanii! Je mheshimiwa huyu anao uwezo mzuri wa kufikiri?

Tuupeleke Mwenge Makumbusho ya Taifa!
 
huyu Nyambali Nyangwine anatafuta kijinafasi serikalini mana siku hizi vitabu vyake havisomwi hivyo anakosa pesa na hana pa kukimbilia zaidi ya kujipendeza kwa mi-CCM,usiwaze nyambari ukatibu mkuu wizara ya elimu unakusubiri ila cjui lini maana hilo lichama lenu ndo tunaelekea kulizika
 
Sijakuelewa Akili ya grade C ama D ndio ikoje hiyo ?
 
Huu mwenge ulitakiwa uweunawashwa wakati wa ufunguzi wa shule, barabara, reli, hospitali au miradi mikubwa mipya. Ukiwasha mwenge inaleta maana!
 
Sijakuelewa Akili ya grade C ama D ndio ikoje hiyo ?

Yaani akili ya kawaida tu maana ya Grade B na A ni watu wenye uwezo mkubwa sana wa kuhoji mambo na Grade D kushuka chini ni watu wa "Ndiyo mzee bila kuhoji"
 
Mwenge ni kitu gani?..ni dini ya ccm?...ni matambiko ya ccm?...Azimio la Arusha liko wapi? Je, Mwenge una maana kuliko Azimio la Arusha?...liko wapi azimio letu?...nauliza maadili ya kizalendo yaliyomo humo ndani, yako wapi? mwenge hauna tija..zamani ulikuwa unamlika wahujumu uchumi nchini,je umemlika na kupelekea kukamatwa,kufilisiwa aua kufungwa jera wangapi?...ina maana hawapo wahujum uchumi nchini "mafisadi" ?...MWENGE NI DINI YA CCM, waseme misingi ya imani au ushirikina ndani yake...hauna mantiki ya uchumi,maadili ya utumishi wa uma, kijamii au vyovyote vile au ni ngoma ya kienyeji ya watanzania. Hebu nipe manufaa ambayo ni tangible..weka hapa nione kama huwezi chagua kati hayo niliyoanisha hapo na ukubaline na mimi....
 
Enyi kizazi cha upinzani mwenge ni ishara ya nuru itakayo mulika mpaka nje ya tanzania. Kizazi hiki huamini ishara zaidi kuliko maneno. Nyerere ni yohana mbatizaji aliyekuja kuwaandaa watu wampokee Kristo. Alichofanya ni kuuandaa mapito ya bwana. Wala hakuwa mkorofi, babu zenu ndio wakorofi, walitamani wanaume badala ya wanawake. Anayekujibu ni KRISTO aitwaye MASIHI
 
kuwasha Mwenge*2 na kuuweka kilimanjaro! umurike hata nje ya mipaka yetu ulete tumaini. pale ambapo hakuna matumaini, upendo...............huo ulikuwa ni wimbo tuliimba enzi zile....... sasa Mwenge umekosa lengo imebaki ni mwenge wa viongozi leo upo MEATU unazindua miradi. eti mwenge unazindua miradi. sielewi kama hilo ni lengo kuu la mwenge. tunateketeza raslmali za nchi kwa kigezo cha kuzindua miradi. shughuli za halmashauri zinakwama, viongozi wote wa taifa,wilaya,mkoa hadi vijiji wanashindwa kufanya kazi za maana kuzindua miradi tu. Tunapiga hatua moja na kurudi nyuma hatua kumi. MALI YA UMMA haina mwenye. Huo mwenge bora upelekwe jumba la makumbusho. miradi kama kweli ipo imalizake na huo mkwanja wa kujaza mafuta, kulipana posho, na kuteketeza raslimali zetu tufanyie mambo ya msingi. hatuuelewi mwenge kabisa upo kwa malengo yapi anayejua lengo la mwenge kwa sasa afunguke.
 
Watumishi hulazimishwa kuuchangia kila mwaka

"Nchi ngumu hii"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…