Siri Ya Mtungi.

Siri Ya Mtungi.

Tamthilia imetengenezwa vizuri, inaeleweka kwa ufasaha, ina flow kwa mpango mzuri, na inatia hamasa kuiagalia. Labda kwa wale wanaoona tatizo la kuiangalia na watoto je haina age-restriction? Kuna weza wekwa alama ya PG-parental guidance kama kuna mahala panahitaji, kama mnataka kujitofautisha na hao mnao waita bongowood- ambao naona wanatoa burudani kwa viwango vyao ndio maana ni "maarufu sana" kwa watanzania wengine--tukiweza tafiti chambua kwanini wanapendwa pengine tutaondoa mtazamo 'hasi' juu yao na kuwakubali 'wao' kama 'wao'.
Na hili la swahiliwood vs bongowood' , bongomovie' ndio kitu gani?
 
Tamthilia imetengenezwa vizuri, inaeleweka kwa ufasaha, ina flow kwa mpango mzuri, na inatia hamasa kuiagalia. Labda kwa wale wanaoona tatizo la kuiangalia na watoto je haina age-restriction? Kuna weza wekwa alama ya PG-parental guidance kama kuna mahala panahitaji, kama mnataka kujitofautisha na hao mnao waita bongowood- ambao naona wanatoa burudani kwa viwango vyao ndio maana ni "maarufu sana" kwa watanzania wengine--tukiweza tafiti chambua kwanini wanapendwa pengine tutaondoa mtazamo 'hasi' juu yao na kuwakubali 'wao' kama 'wao'.
Na hili la swahiliwood vs bongowood' , bongomovie' ndio kitu gani?
madogo, sijakusoma ndugu yangu hapo.
umezungumzia vitu kadhaa!

Ni kweli ni tamthiliya nzuri sana, kama nilivyosema awali nadhani kama umeiangalia pia tutakubaliana.

Suala la age limit nadhani sasa hichi ni kitu ambacho tete, kwamba kuna viwango vinavyokubaliwa na mabaraza kwamba Tamthiliya ya kuangaliwa na "TV za UMMA" zinatakiwa ziweje!! Naamini hawa jamaa wamezingatia viwango hivyo sababu wadau waliohusika na kazi hii ni wadu ambao wamekuwa wakifanya kazi za namna hii kwa mda mrefu na kwa ubora uliovutia kundi la wapenzi wa kazi za namna hiyo.

Ukipata nafasi cheki hawa Wafadhili wa Siri ya Mtungi, na kazi ambazo weshafanya.

Kwa binafsi sijaona kitu cha kuwa cha kuhitaji Age Limit kiasi hicho kwa Tamthiliya hii kwa mpaka sasa ilipofikia, labda huko mbeleni kama itaendelea kuonyeshwa!

Hayo mengine ya Bongowood sijui, Bongomovie na Swahiliwood nadhani tu hujanielewa sehemu.
Sizungumzii umaarufu wa watu, mi nazungumzia Sanaa na Vifaa vyake na namna inavotakiwa ifanyike, na mara zote inavyofanyika kama inavyotakiwa huwa inaleta tofauti na msisimko wa aina yake.
 
Last edited by a moderator:
Hahahahaaaaaaa!... Ni kweli tulifika sehemu tukazinguana, hata hivyo
wiki hiyo hiyo nikapata kazi nyingine kutoka kwenye taasisi moja ya Canada
ambapo nililazimika kusafiri kwenda kutengeneza documentary ambayo ilinichukua
takriban miezi mitatu.

Kuhusiana na kazi hii ya 'Siri ya Mtungi' panapo majaaliwa nitaandika
makala maalum ikiwa kama somo maalum kwa watengeneza filamu wetu...

lol, nilijua tu nyie wasanii lazima myumbishane !

Ndio maana sikukuona kwenye EFF, that May 11-15! Ndio ulikuwa upo na hao jamaa au tulipoteana tu ukumbini??

Poa, nasubiri mambo matamu kutoka pande hizo za hao jamaa "wapya".

Sijawahi kupata muda kuitazama tamthilia hii lakini kwa kuona vionjo humu ndani imenipa mzuka niitafute!
Mwalimu, naamini umeichek leo EATV.

Duma kalikoroga kwa mlimbwende Nusura, naamini Mzee Kizito ndio anapopigia bao hapo.....
Huyu Mzee anaujua sana uchawi wa mabinti lol
 
Last edited by a moderator:
Precisely mkuu,inaonekana ni tamthilia nzuri sana!
TUKUTUKU vipi umepata chance ya kuichek leo kupitia EATV??

Sijui tatizo lipo wapi ila inaonekana watu wengi sana hawanataarifa za hii kitu, pamoja na jitihada zote za jamaa kujitangaza....

Sijui tatizo lipo wapi kwenye upokeaji wa taarifa!!
 
Last edited by a moderator:
lol, nilijua tu nyie wasanii lazima myumbishane !
Ndio maana sikukuona kwenye EFF, that May 11-15! Ndio ulikuwa upo na hao jamaa au tulipoteana tu ukumbini??
Poa, nasubiri mambo matamu kutoka pande hizo za hao jamaa "wapya".

Unajua, mara nyingi tukikubaliana jambo basi lifanyike on time na kwa kufuata misingi.
Lakini zikishaanza longolongo mara nyingi mimi huamua kujitoa na kufanya shughuli zingine.
Huo ndiyo msimamo wangu..
 
Unajua, mara nyingi tukikubaliana jambo basi lifanyike on time na kwa kufuata misingi.
Lakini zikishaanza longolongo mara nyingi mimi huamua kujitoa na kufanya shughuli zingine.
Huo ndiyo msimamo wangu..

Kweli Mkuu, huo msimamo ni makini sana......

Japo sielewi watu wazima mlishindwana wapi ila naamini ilikuwa ni kwa heri tu!

Kazi uliyoiacha huku nyuma haikuwa mbaya sana, miongoni mwetu wengine bado tumeona tunu kwa vijana wetu.....

Naisubiri kwa hamu sana hiyo kazi uliyoifanya na hao jamaa wengine!
 
tamthiliya bomba kabisa, inanishawishi kufuatilia sanaa za ndani baada ya watu wa Bongo movie kuharibu
 
sehemu yoyote akishagusa mzungu mara nyingi huwa sion ufanisi wa mwafrika. Kwenye hiyo tamthilia ni wazungu wanaongoza. Wabantu wanachezeshwa. Fungu linatoka vyanzo vya kuaminika. Ingekuwa ni zao la kampuni ya nyumbani tungeweza kusema habari nyingine. Kwa kifupi ni nzuri kwa kuwa imegharamiwa
 
TUKUTUKU vipi umepata chance ya kuichek leo kupitia EATV??

Sijui tatizo lipo wapi ila inaonekana watu wengi sana hawanataarifa za hii kitu, pamoja na jitihada zote za jamaa kujitangaza....

Sijui tatizo lipo wapi kwenye upokeaji wa taarifa!!

Tatizo ni media inayotumika. Sina hakika kama ndio sababu ya kurushwa itv au inarushwa kote. Halafu yaelekea una taarifa za ndani kuhusu hii tamthiliya. Unahusika?
 
Last edited by a moderator:
TUKUTUKU vipi umepata chance ya kuichek leo kupitia EATV??

Sijui tatizo lipo wapi ila inaonekana watu wengi sana hawanataarifa za hii kitu, pamoja na jitihada zote za jamaa kujitangaza....

Sijui tatizo lipo wapi kwenye upokeaji wa taarifa!!

Niliiangalia kama mara mbili hivi haikunishawishi kabisa . . . sijaangalia tena!
 
sehemu yoyote akishagusa mzungu mara nyingi huwa sion ufanisi wa mwafrika. Kwenye hiyo tamthilia ni wazungu wanaongoza. Wabantu wanachezeshwa. Fungu linatoka vyanzo vya kuaminika. Ingekuwa ni zao la kampuni ya nyumbani tungeweza kusema habari nyingine. Kwa kifupi ni nzuri kwa kuwa imegharamiwa
Raia Fulani, nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani. Hata wachangiaji
na wafuatiliaji wa kazi hii nawashauri kuwa wasiangalie ubora tu wa picha,
waangalie mambo mengi ambayo kuhusiana na tamaduni zetu, utagundua
kuwa kwa kuwa kazi imeandaliwa na wazungu basi mambo mengi yanakosa
uhalisia wa Kiafrika bali yanakuwa yanabeba uzungu mwingi, japo Waafrika
wamehusishwa katika utengenezaji huu, hii ni kutokana na kutoshiriki kikamilifu
katika ngazi ya maamuzi; mfano aina ya mapenzi yaliyomo humo, mtazamo wa
wapenzi nk. Nimewahi kuandika makala kuhusiana na mtazamo wa Wazungu
kwa Waafrika
(ambayo unaweza kuisoma kwa ku-click hapo kwenye title) jinsi
ambavyo wazungu wamekuwa wakituchukulia Waafrika. Anyway, sitaki kuiongelea
sana kazi hii 'Siri ya Mtungi', wadau waifuatilie huenda wataburudika zaidi...
 
Raia Fulani, nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani. Hata wachangiaji
na wafuatiliaji wa kazi hii nawashauri kuwa wasiangalie ubora tu wa picha,
waangalie mambo mengi ambayo kuhusiana na tamaduni zetu, utagundua
kuwa kwa kuwa kazi imeandaliwa na wazungu basi mambo mengi yanakosa
uhalisia wa Kiafrika bali yanakuwa yanabeba uzungu mwingi, japo Waafrika
wamehusishwa katika utengenezaji huu, hii ni kutokana na kutoshiriki kikamilifu
katika ngazi ya maamuzi; mfano aina ya mapenzi yaliyomo humo, mtazamo wa
wapenzi nk. Nimewahi kuandika makala kuhusiana na mtazamo wa Wazungu
kwa Waafrika
(ambayo unaweza kuisoma kwa ku-click hapo kwenye title) jinsi
ambavyo wazungu wamekuwa wakituchukulia Waafrika. Anyway, sitaki kuiongelea
sana kazi hii 'Siri ya Mtungi', wadau waifuatilie huenda wataburudika zaidi...
Mkuu nimeicheki makala. umechimba sana. naona hapa kwenye siri ya mtungi wanayaendeleza yale ya CFU. Japo sijaiangalia sana, ni wazi kuwa mapenzi ndani ya hii tamthiliya yamejaa uthubutu uliokaribia kupitiliza kiasi kwamba kwa mwafrika kumwomba penzi binti au mwanamke wa kiafrika ni jambo rahisi tu. Siku zote mzungu amependa kuwa juu kwa kila jambo hata nje ya mipaka yake kwa kisingizio cha 'kufanya utafiti' juu ya jambo husika
 
Kila nikiangalia haijanishawishi kabisa, naona tumeshaharibiwa na umagharibi alafu mnataka kuturudisha tulikotokea wakati hakuna hata future. Nafikiri mngeanzia hapa tulipo alafu ndo mtubadilishie hapo, sijui labda huko mbele kuna jipya.
 
Dah mkuu naona umetokelezea hatimaye, vipi za masiku?? Na heri ya Mwaka mpya!

sehemu yoyote akishagusa mzungu mara nyingi huwa sion ufanisi wa mwafrika. Kwenye hiyo tamthilia ni wazungu wanaongoza. Wabantu wanachezeshwa. Fungu linatoka vyanzo vya kuaminika. Ingekuwa ni zao la kampuni ya nyumbani tungeweza kusema habari nyingine. Kwa kifupi ni nzuri kwa kuwa imegharamiwa

Sijui kwanini toka naanzisha hii sred tu nilijua kuna mtu ataleta hoja za "wazungu" lol....
Naona wadau karibia wote mnamsimamo unaofanana juu ya hichi kitu maana nina kijana wangu mtaani naye ni mdau sana wa tasnia toka mwanzo nimemwambia acheki hii kazi kakazana oohh wazungu wazungu!!

Miaka yote tupo sisi kama sisi "wabantu" na tasnia yetu, na wote tunajua nini tumekuwa tunafanya, Bishop Hiluka kaandika wee kukosoa na kurekebisha lakini wapi, kazi zetu tunazijua wenyewe mpaka sasa.

Kosa hasa la hao "wazungu" ni nini hapo?
Kuwa na uwezo na kugharamia kukamilisha walichoona wao kinafaa kwa kupitia sanaa yetu?

Tatizo ni media inayotumika. Sina hakika kama ndio sababu ya kurushwa itv au inarushwa kote. Halafu yaelekea una taarifa za ndani kuhusu hii tamthiliya. Unahusika?
Raia Fulani ushaanza uoga wako wa kunihisia vitu ambavyo havipo, mi pia ni raia fulani tu ambaye nina mguso wa kipekee na hizi sanaa.
 
Last edited by a moderator:
Niliiangalia kama mara mbili hivi haikunishawishi kabisa . . . sijaangalia tena!

Ni sawa tu kama hujaiangalia na wala hutaiangalia tena.....

Hata kazi kubwa za sanaa duniani hazikuwahi kuwapendeza watu wote, kuwa huru tu!
 
Sijui kwanini toka naanzisha hii sred tu nilijua kuna mtu ataleta hoja za "wazungu" lol....
Naona wadau karibia wote mnamsimamo unaofanana juu ya hichi kitu maana nina kijana wangu mtaani naye ni mdau sana wa tasnia toka mwanzo nimemwambia acheki hii kazi kakazana oohh wazungu wazungu!!

Miaka yote tupo sisi kama sisi "wabantu" na tasnia yetu, na wote tunajua nini tumekuwa tunafanya, Bishop Hiluka kaandika wee kukosoa na kurekebisha lakini wapi, kazi zetu tunazijua wenyewe mpaka sasa.
Kosa hasa la hao "wazungu" ni nini hapo?
Kuwa na uwezo na kugharamia kukamilisha walichoona wao kinafaa kwa kupitia sanaa yetu?

Mkuu, hili suala la wazungu na waafrika ni suala/jambo ambalo lipo sana
hata kama hatutakubali, sitaki kuingia kwenye mjadala huo lakini kuna
mambo yanayohusiana na hili yaliyonifanya nijiondoe pale...
 
Raia Fulani, nakubaliana na wewe kwa kiasi fulani. Hata wachangiaji
na wafuatiliaji wa kazi hii nawashauri kuwa wasiangalie ubora tu wa picha,
waangalie mambo mengi ambayo kuhusiana na tamaduni zetu, utagundua
kuwa kwa kuwa kazi imeandaliwa na wazungu basi mambo mengi yanakosa
uhalisia wa Kiafrika bali yanakuwa yanabeba uzungu mwingi, japo Waafrika
wamehusishwa katika utengenezaji huu, hii ni kutokana na kutoshiriki kikamilifu
katika ngazi ya maamuzi; mfano aina ya mapenzi yaliyomo humo, mtazamo wa
wapenzi nk. Nimewahi kuandika makala kuhusiana na mtazamo wa Wazungu
kwa Waafrika
(ambayo unaweza kuisoma kwa ku-click hapo kwenye title) jinsi
ambavyo wazungu wamekuwa wakituchukulia Waafrika. Anyway, sitaki kuiongelea
sana kazi hii 'Siri ya Mtungi', wadau waifuatilie huenda wataburudika zaidi...

Najua una uzoefu katika haya masuala, wala siwezi kubishana na wewe juu ya hivi vitu, nadhani nipo kwenye nafasi ya kujifunza zaidi ili kuielewa tasnia.
Ninaweza kukubaliana na baadhi ya vitu juu "wazungu" (japo sijasoma hiyo makala, nitaisoma mda wa baadae).....

Labda twende kwa mifano, unaweza kunisimulia kama kulikuwa na madhara yoyote kwa kazi kubwa kama Neria na Yellow Card ??

Na vipi kuhusu Chumo??

Nadhani nikiisoma hiyo makala yako nitajua cha kukuambia zaidi!

Hilo suala utamaduni wetu nahofia tunalitumia wakati mwingine katika namna isiyo halisi, nina uhakika leo hii kwa asilimia kubwa sana katika jamii za kitanzania ni jamii chache sana zinafuata hicho tunachoita utamaduni wa watanzania!!

Mkuu kumbuka huko juu umeeleza kuwa jamaa mlishindana kwenye masuala fulani fulani kwenye ukamilishaji wa hii kazi, so huoni kuwa ni rahisi sana mtu kusema kuwa upo biased kwa sababu hiyo???
 
Najua una uzoefu katika haya masuala, wala siwezi kubishana na wewe juu ya hivi vitu, nadhani nipo kwenye nafasi ya kujifunza zaidi ili kuielewa tasnia.
Mkuu kumbuka huko juu umeeleza kuwa jamaa mlishindana kwenye masuala fulani fulani kwenye ukamilishaji wa hii kazi, so huoni kuwa ni rahisi sana mtu kusema kuwa upo biased kwa sababu hiyo???

Mkuu, jouneGwalu, nimeshaweka msimamo wangu kutoingia sana kwenye suala la wazungu
kwa kuogopa isije ikaonekana kama unavyosema. Lakini mimi sina chuki na hawa jamaa, bado
ni rafiki zangu na nitafanya nao tena kazi japo kwa mikataba maalum na kawaida yangu kama
nitaona sikubaliani na mazingira yaliyopo huwa najiondoa ili nisiwakwaze wengine au kuharibu
kazi. Naweza kusema kuwa najivuna sana kwa hawa jamaa kuamua kuichukua ripoti yangu ya
utafiti na kuitumia kwani wazo la kuanzisha Swahiliwood lilitokana na ripoti hiyo, hii ni kwa mujibu
wa kauli zao wenyewe.

Lakini bado nasisitiza nilichokisema kuhusu mtazamo wa wazungu kwa waafrika nikiwa siwalengi
hawa bali wazungu wote, na hii makala niliiandika miaka mitano iliyopita kabla hata sijapata
nafasi ya kufanya na taasisi hii na wala sikuwa na wazo kama siku moja wangeniita na kutaka
nifanye nao kazi. Sikatai kuna mambo mengi nimejifunza kupitia wao ingawa pia kuna matatizo
nimeyapata kutokana na kufahamiana nao...
 
Mkuu, hili suala la wazungu na waafrika ni suala/jambo ambalo lipo sana
hata kama hatutakubali, sitaki kuingia kwenye mjadala huo lakini kuna
mambo yanayohusiana na hili yaliyonifanya nijiondoe pale...

Siwezi kukataa, nadhani nikikataa nitakuwa mtu wa ajabu sana.

Hicho kitu kipo kwenye masuala yote tu bro, kwenye kazi huko maviwandani hadi katika usimamizi wa siasa za dunia.

Hivyo tusitegemee kitu cha tofauti sana kwenye hata ili la sanaa, nadhani tungekuwa wajanja labda tungeweza kujipanga na namna ya kubaki na ujuzi hata wakiondoka.

Ila huu ubishi wa kibongo tutaendelea tu na kazi zetu hizi, tutaandika makala hadi mwisho.

Mi naunga mkono sanaa zinazozingatia viwango bila kujali wazungu au weusi ndio maana nashiriki matamasha yote ninapokuwa na nafasi iwe Sauti za Busara, iwe ZIFF au EFF nk nk nk...

Tunavitu vya kujifunza, tena kujifunza kwa vitendo moja kwa moja na kila mtu kwenye eneo lake
 
Back
Top Bottom