Siri Ya Mtungi.

Siri Ya Mtungi.

Sijaiona hii kitu bado naona shughuli zimeingiliana..

Ila hawa jamaa inabidi wajue kwamba hata ukiwa na product nzuri vipi bila promotion ni kazi bure..

Sijui kwanini wasiamue hata kurusha episodes za mwanzo mwanzo youtube ili watu waweze kuangalia kwa wakati wao (hata kama itakuwa ni against contract na ITV) lakini ikiwepo online hata episodes za mwanzo zitawavutia wengine hata walio nje kuweza kuona (unless otherwise hii kitu inaweza kushika kasi na watu kuitambua baada ya miaka kadhaa ambapo huenda itakuwa imeshaanza kuchuja)
 
Sijaiona hii kitu bado naona shughuli zimeingiliana..
Ila hawa jamaa inabidi wajue kwamba hata ukiwa na product nzuri vipi bila promotion ni kazi bure..
Sijui kwanini wasiamue hata kurusha episodes za mwanzo mwanzo youtube ili watu waweze kuangalia kwa wakati wao (hata kama itakuwa ni against contract na ITV) lakini ikiwepo online hata episodes za mwanzo zitawavutia wengine hata walio nje kuweza kuona (unless otherwise hii kitu inaweza kushika kasi na watu kuitambua baada ya miaka kadhaa ambapo huenda itakuwa imeshaanza kuchuja)

Ki ukweli wamejitahidi sana kujitangaza, matangazo yao yapo
sehemu nyingi mno hadi humu Jamii Forums, pia wana page kule
facebook na hata youtube...
 
Ki ukweli wamejitahidi sana kujitangaza, matangazo yao yapo
sehemu nyingi mno hadi humu Jamii Forums, pia wana page kule
facebook na hata youtube...

Mkuu simaanishi banners hapa na pale au trailer huku na kule naamisha going the whole nine yards..

Mfano hizo episodes ambazo zimeshatoka ITV ana hasara gani kuzirusha bure youtube (full episode) ili kuwanasa watu wakishaonja ili waendelee kutazama ?

Mfano Spartacus (Starz waliamua kuna season fulani kutoa youtube full episodes mbili za mwanzo ili watu waangalie.., baada ya hapo wakaacha guess what baada ya hapo mtu utake usitake unatune kwenye TV uone nini kinaendelea).., hivyo basi since bongo wengi internet ni anasa (hata hawa ITV au watunzi au wahusika wa hii kitu wanaweza wakavujisha dvds mitaani za episodes za mwanzo ambazo zimeshaonyeshwa au kuamua tu kusambaza mitaani episodes za mwanzo)
 
Leo nilikuwa naongea na dada mmoja aliyekuwa akiitazama hii tamthiliya na akasema kuwa hajapenda jinsi wasanii wanavyoongea mechanically. Wamemezeshwa script na wanaongea kama vile wanaogopa kukosea wakati katika uhalisia hayo sio maongezi, tena ya kiafrika. Hii naifananisha na filamu ya chumo. ​Nadhani waliotengeneza siri ya mtungi ndio waliotengeneza chumoLeo nilikuwa naongea na dada mmoja aliyekuwa akiitazama hii tamthiliya na akasema kuwa hajapenda jinsi wasanii wanavyoongea mechanically. Wamemezeshwa script na wanaongea kama vile wanaogopa kukosea wakati katika uhalisia hayo sio maongezi, tena ya kiafrika. Hii naifananisha na filamu ya chumo. ​Nadhani waliotengeneza siri ya mtungi ndio waliotengeneza chumo
 



duma-door.jpg
kizito-vert.jpg


Wa kwanza kulia hilo ni Mwalimu na msanii mzuri sana pale chuo cha sanaa Bwagamoyo kwa kweli jamaa ana kipaji
 
Dah mkuu naona umetokelezea hatimaye, vipi za masiku?? Na heri ya Mwaka mpya!



Sijui kwanini toka naanzisha hii sred tu nilijua kuna mtu ataleta hoja za "wazungu" lol....
Naona wadau karibia wote mnamsimamo unaofanana juu ya hichi kitu maana nina kijana wangu mtaani naye ni mdau sana wa tasnia toka mwanzo nimemwambia acheki hii kazi kakazana oohh wazungu wazungu!!

Miaka yote tupo sisi kama sisi "wabantu" na tasnia yetu, na wote tunajua nini tumekuwa tunafanya, Bishop Hiluka kaandika wee kukosoa na kurekebisha lakini wapi, kazi zetu tunazijua wenyewe mpaka sasa.

Kosa hasa la hao "wazungu" ni nini hapo?
Kuwa na uwezo na kugharamia kukamilisha walichoona wao kinafaa kwa kupitia sanaa yetu?


Raia Fulani ushaanza uoga wako wa kunihisia vitu ambavyo havipo, mi pia ni raia fulani tu ambaye nina mguso wa kipekee na hizi sanaa.
Duh! kama huo ni uoga na uoga utakuwaje? Kosa la wazungu ni kutuaminisha kuwa wao wanajua tamaduni zetu. Kwamba tamthiliya ya kiafrika ina mahadhi ya kizungu. Uongeaji ule kiukweli sio. Nimependa sana kazi ya CREW. Pia nawe usiogope kuhusishwa na jambo unalolitetea. Nilidhani nawe uko kwenye crew ili nami nije kuiba ujuzi huko maana wamejipanga
 

Wa kwanza kulia hilo ni Mwalimu na msanii mzuri sana pale chuo cha sanaa Bwagamoyo kwa kweli jamaa ana kipaji

Huyo mzee hata acting yake imenifurahisha sana.....

Umeona jana kaitisha kikao cha familia kuwapa taarifa za ujio wa mke wa nne lol, bimkubwa acha awashe moto na kikao kikaisha utamu.
Kwa mfano kwenye suala la huyu mzee na jinsi anavyofanya mambo yake sijui huo "uzungu" wanao dai hawa wadau wangu hapa JF upo wapi!!!
 
Leo nilikuwa naongea na dada mmoja aliyekuwa akiitazama hii tamthiliya na akasema kuwa hajapenda jinsi wasanii wanavyoongea mechanically. Wamemezeshwa script na wanaongea kama vile wanaogopa kukosea wakati katika uhalisia hayo sio maongezi, tena ya kiafrika. Hii naifananisha na filamu ya chumo. ​Nadhani waliotengeneza siri ya mtungi ndio waliotengeneza chumo

Roho inaniuma sana ninapokuwa na wadau wanaojua na bado wanatetea vitu tu ilimradi kushinda ligi, ila uzuri wa kitu kizuri hata ukikipinga bado utajichanganya tu hebu cheki hapo chini ulivyotoa comment nzuri.... lol

Nimependa sana kazi ya CREW. Pia nawe usiogope kuhusishwa na jambo unalolitetea. Nilidhani nawe uko kwenye crew ili nami nije kuiba ujuzi huko maana wamejipanga

Pamoja saaaaana bro!
 
Roho inaniuma sana ninapokuwa na wadau wanaojua na bado wanatetea vitu tu ilimradi kushinda ligi, ila uzuri wa kitu kizuri hata ukikipinga bado utajichanganya tu hebu cheki hapo chini ulivyotoa comment nzuri.... lol



Pamoja saaaaana bro!

Kuna usemi usemao mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Hawa jamaa hawawezi kuwa kamili kiivyo. Crew nimeikubali sana. Cast nimeikubali pia. Labda upande wa maandalizi ya script maana kama nilivyosema cast wako mechanical sana. Dialogue nazo wamezidisha kupanga kiasi hakuna ule mtelezo katika hali halisi. Labda ndio aina tofauti ya muundo wa script toka kwa hao...
 
Roho inaniuma sana ninapokuwa na wadau wanaojua na bado wanatetea vitu tu ilimradi kushinda ligi

Mkuu, Wachina wana msemo wao kuwa: "kama kila mnapokutana huwa mnakubaliana
kwa kila jambo basi baadhi yenu wana matatizo ya kufikiri". Ni kawaida kutofautiana
hasa ukizingatia kuwa kila mmoja ana angle anayoitumia kuangalia jambo. Binafsi naweza
kusema kuwa in terms of equipments, quality, cast, story na jinsi ya mgawanyo wa kazi
jamaa wamejitahidi sana kwa kuwa walijiandaa kabla ya kuanza kazi. Bajeti yao ni kubwa
mno kwa kuwa walipata funds kutoka kwenye taasisi mbalimbali za nchini kwao (Marekani)
na hapa nchini.

Pamoja na uzuri wa kazi husika lakini hilo la uzungu ki ukweli limo sana. Llilikuwemo hata
kwenye filamu ya chumo kwa kutuwekea mashindano ya vijana wawili (Sharo na Mlela)
kumgombea binti (Jokate) huku baba wa binti ndiye akiwa referee.

Tukirudi kwenye tamthilia hii, sioni kama ina tofauti sana na tamthilia zingine za nje hasa
linapokuja suala la maudhui na matumizi ya movements: mfano mdogo ukiwa kwa wapenzi
na mikao yao; kwa mfano sisi (Waafrika) hatuna desturi ya kupeana visogo unapoongea na
mpenzi wako, lakini humo ni kawaida kumuona binti kusimama akiwa kasimama kampa kisogo
mpenzi wake halafu wanaongea. Au pale mtu anapomuuliza rafiki yake "vipi ulitumia kondomu?"
wakati tamthilia hii inaangaliwa na watu wa rika zote wakiwemo watoto wadogo. Kwangu mimi
haya ni mapungufu ya kimaadili, hata kama ni utandawazi lakini bado hatujafikia huko. Pia
usishangae kuona jamaa anamletea mpenzi wake maua akiwa kayaficha mgongoni na kusema
"surprise!".

Kwa hiyo kama wadau wanapinga ni kwa sababu wao hawaangalii ubora wa picha au sauti tu,
au kumwangalia mtu mmoja mmoja kama huyo mzee Nkwabi wa Bagamoyo, bali katika angle
waliyoitumia kuna vitu vinawaudhi kiasi cha kuwafanya wasiyaone hata hayo mazuri mengine.

Mwisho, kila mtu huwa ana hobbies (vitu avipendavyo) na vitu asivyovipenda, na huwa
tunatofautiana katika mitazamo, hivyo anaweza asiyaone kabisa hayo unayoyasema wewe
kuwa ni mazuri. Najua wanakukera lakini ukweli utabaki kuwa hivyo...
 
Duh! kama huo ni uoga na uoga utakuwaje? Kosa la wazungu ni kutuaminisha kuwa wao wanajua tamaduni zetu. Kwamba tamthiliya ya kiafrika ina mahadhi ya kizungu. Uongeaji ule kiukweli sio. Nimependa sana kazi ya CREW. Pia nawe usiogope kuhusishwa na jambo unalolitetea. Nilidhani nawe uko kwenye crew ili nami nije kuiba ujuzi huko maana wamejipanga

Duh labda sijaelewa wakuu ndio maana nashindwa kuelewa huu mjadala na uhusiano baina ya wazungu (na ubovu au ubora wa kazi zetu), nadhani hapa ni kusingizia uwepo wa bunduki kwa mauaji badala ya aliyeitumia hio bunduki..

Sijaelewa kama unasema kwamba watu hawaangilii kazi zetu sababu sio za kizungu au waigizaji wanaigiza uzungu.., kama ni hivyo nadhani tunawaonea hao wazungu (kwa ufupi ni mediocrity ya wanasaa na kazi mbovu za kurashiarashia za wabongo ndio zinazosababisha kazi mbovu)

Nimeangalia kazi nyingi za sehemu tofauti na hata kuna kazi za huko huko kwa wazungu ambazo nyingi naacha kuziangalia sababu tu ni mbovu na sio sababu nyingine.., pia kuna kazi za watu wa kawaida mfano wa-Brazil walipotoa The City of God (kuonyesha reality ya nchini kwao kazi ilipendwa dunia nzima bila kujali ni wapi ilitoka) au kuna kazi nzuri kutoka Afrika Kusini n.k.

Nadhani hapa tunaweza kujikuta tunatumia neno Uzalendo kulazimishana kuangalia makapi sababu tu yametoka nyumbani au ni vijana wa nyumbani ndio wametoa hayo makapi (tatizo kubwa na wabongo ni over-acting na hii sidhani kama walifundishwa au wanaiga hao wazungu) sababu hata hao hawafanyi hivyo

Samahani kama sijaelewa huu uhusiano wa kuwalaumu wazungu au kazi za wazungu kwa kutoa kazi zetu mbovu (labda sijakueleweni au nimekosea) mnamaanisha nini
 
Tukirudi kwenye tamthilia hii, sioni kama ina tofauti sana na tamthilia zingine za nje hasa
linapokuja suala la maudhui na matumizi ya movements: mfano mdogo ukiwa kwa wapenzi
na mikao yao; kwa mfano sisi (Waafrika) hatuna desturi ya kupeana visogo unapoongea na
mpenzi wako, lakini humo ni kawaida kumuona binti kusimama akiwa kasimama kampa kisogo
mpenzi wake halafu wanaongea. Au pale mtu anapomuuliza rafiki yake

usishangae kuona jamaa anamletea mpenzi wake maua akiwa kayaficha mgongoni na kusema
"surprise!".

Mkuu hivi haya siku hizi hayatokei kwenye hii karne ya dot.com na hawa vijana wetu ? kama mtu ana-act kama sharobaro (kama wenyewe wanavyojiita unategemea kwenye ku-act abadilike awe kama mstaarabu fulani au mtoto mwenye malezi ?

Kwahio mkuu ingawa na mimi naona kasoro nyingi sana kwenye Bongo Movie hadi kupelekea nisiziangalie sana lakini nadhani kwa mfano hapo juu tutakuwa tumewaonea.., nadhani hapo labda tuwalaumu watunzi kwanini wasitengeneze na filamu zinazohusu sana maisha ya watanzania na mila na desturi ili nazo ziingie sokoni sababu unajua watu wanaangalia soko na huu usharobaro ndio soko la vijana wetu (kwahio watengeneze na tamthiliya za familia na nyingine zinazohusu mila zetu)
 
Mkuu, Wachina wana msemo wao kuwa: "kama kila mnapokutana huwa mnakubaliana
kwa kila jambo basi baadhi yenu wana matatizo ya kufikiri". Ni kawaida kutofautiana
hasa ukizingatia kuwa kila mmoja ana angle anayoitumia kuangalia jambo. Binafsi naweza
kusema kuwa in terms of equipments, quality, cast, story na jinsi ya mgawanyo wa kazi
jamaa wamejitahidi sana kwa kuwa walijiandaa kabla ya kuanza kazi. Bajeti yao ni kubwa
mno kwa kuwa walipata funds kutoka kwenye taasisi mbalimbali za nchini kwao (Marekani)
na hapa nchini.

Pamoja na uzuri wa kazi husika lakini hilo la uzungu ki ukweli limo sana. Llilikuwemo hata
kwenye filamu ya chumo kwa kutuwekea mashindano ya vijana wawili (Sharo na Mlela)
kumgombea binti (Jokate) huku baba wa binti ndiye akiwa referee.

Tukirudi kwenye tamthilia hii, sioni kama ina tofauti sana na tamthilia zingine za nje hasa
linapokuja suala la maudhui na matumizi ya movements: mfano mdogo ukiwa kwa wapenzi
na mikao yao; kwa mfano sisi (Waafrika) hatuna desturi ya kupeana visogo unapoongea na
mpenzi wako, lakini humo ni kawaida kumuona binti kusimama akiwa kasimama kampa kisogo
mpenzi wake halafu wanaongea. Au pale mtu anapomuuliza rafiki yake "vipi ulitumia kondomu?"
wakati tamthilia hii inaangaliwa na watu wa rika zote wakiwemo watoto wadogo. Kwangu mimi
haya ni mapungufu ya kimaadili, hata kama ni utandawazi lakini bado hatujafikia huko. Pia
usishangae kuona jamaa anamletea mpenzi wake maua akiwa kayaficha mgongoni na kusema
"surprise!".

Kwa hiyo kama wadau wanapinga ni kwa sababu wao hawaangalii ubora wa picha au sauti tu,
au kumwangalia mtu mmoja mmoja kama huyo mzee Nkwabi wa Bagamoyo, bali katika angle
waliyoitumia kuna vitu vinawaudhi kiasi cha kuwafanya wasiyaone hata hayo mazuri mengine.

Mwisho, kila mtu huwa ana hobbies (vitu avipendavyo) na vitu asivyovipenda, na huwa
tunatofautiana katika mitazamo, hivyo anaweza asiyaone kabisa hayo unayoyasema wewe
kuwa ni mazuri. Najua wanakukera lakini ukweli utabaki kuwa hivyo...
Yani umeeleza vizuri mno! We ni mchambuzi wa kweli. Gwalu nae inabidi aanze kuitazama hii tamthiliya kwa jicho la tatu. Halafu kumbe nilipatia kufikiri kuwa hawa ndio waandaaji wa chumo? Kiukweli zinafanana MNO! Pozi ni zile zile. kukakamaa kwa stori ni kule kule... Ila bado naendelea kukiri kuwa CREW iko njema
 
Duh labda sijaelewa wakuu ndio maana nashindwa kuelewa huu mjadala na uhusiano baina ya wazungu (na ubovu au ubora wa kazi zetu), nadhani hapa ni kusingizia uwepo wa bunduki kwa mauaji badala ya aliyeitumia hio bunduki..

Sijaelewa kama unasema kwamba watu hawaangilii kazi zetu sababu sio za kizungu au waigizaji wanaigiza uzungu.., kama ni hivyo nadhani tunawaonea hao wazungu (kwa ufupi ni mediocrity ya wanasaa na kazi mbovu za kurashiarashia za wabongo ndio zinazosababisha kazi mbovu)

Nimeangalia kazi nyingi za sehemu tofauti na hata kuna kazi za huko huko kwa wazungu ambazo nyingi naacha kuziangalia sababu tu ni mbovu na sio sababu nyingine.., pia kuna kazi za watu wa kawaida mfano wa-Brazil walipotoa The City of God (kuonyesha reality ya nchini kwao kazi ilipendwa dunia nzima bila kujali ni wapi ilitoka) au kuna kazi nzuri kutoka Afrika Kusini n.k.

Nadhani hapa tunaweza kujikuta tunatumia neno Uzalendo kulazimishana kuangalia makapi sababu tu yametoka nyumbani au ni vijana wa nyumbani ndio wametoa hayo makapi (tatizo kubwa na wabongo ni over-acting na hii sidhani kama walifundishwa au wanaiga hao wazungu) sababu hata hao hawafanyi hivyo

Samahani kama sijaelewa huu uhusiano wa kuwalaumu wazungu au kazi za wazungu kwa kutoa kazi zetu mbovu (labda sijakueleweni au nimekosea) mnamaanisha nini
Actually umeelewa angalau. haimaanishi tulazimishe kuangalia kazi za kwetu japo mbovu. Kwanza tuna mapungufu katika uandikaji wa stori zenyewe. Pili hatuna utaalam wa kutosha kama wazungu. Tatu bajeti zetu finyu sana. haijawahi kutokea hapa mtu akatengeneza filamu iliyogharimu mil 50. sasa kitu kama chumo na siri ya mtungi ni zaid ya mil 200 hivi. Hayo ndio yanayowafanya hawa wenzetu kuja kuamini kuwa hata itikadi na tamaduni zetu wanaweza kuzilipia
 
Najua wanakukera lakini ukweli utabaki kuwa hivyo...

Hapana Mkuu hapo umekosea!

Labda sio kwa mimi, mi naielewa sana JF.

Hamna kitu binafsi hapa, hivyo ni sawa kila mtazamo, ila kila mtazamo hauwezi kunitoa kwenye kile nilichokiona mimi japo sijaribu kuwaleta watu kwangu.

Najua tunaweza kujaza hizi kurasa tukisema tupitie kila pembe ya sanaa hii....

Katika kujenga hoja mtu mwerevu hutumia kila aina ya dhana hata kama katika hali halisi hicho kitu hakipo wala hakitekelezeki. Hicho ndio nimekiona kwa wadau wangu wengi wanaoipinga kazi hii, ndio maana hapo awali nkatolea mfano wa hoja inayojengwa ya "utamaduni wa mtz au muafrika"

Pia ndio maana nkasema "wadau wanaojua", nikimaanisha wenye utashi wa kisanaa na wanaojua kuwa fasihi hii inahusisha sana "ubunifu", "uumbaji" na "mawazo" (imaginations??)

Sasa ndio maana nashangaa vitu vinavyokomaliwa hapa.

Hebu we mwenyewe angalia unazungumzia suala la mkao wa wapenzi, kweli??
 
Hapana Mkuu hapo umekosea!
Hebu we mwenyewe angalia unazungumzia suala la mkao wa wapenzi, kweli??
Mkuu, labda tutafute focus maana tumekuwa tukiongelea vitu vingi mno,
ungependa tujikite kwenye kuangalia nini? Inawezekana naongea vitu vingi
nikajikuta naacha mada ya msingi ambayo wewe umeikusudia. Suala la
mapenzi nililoliongelea lina maana sana unapotaka kuzama kwenye maudhui.
Haya niliyoyaongea kwenye tamthilia hii ndiyo nimekuwa nikiyapigia kelele haya
kwenye movie zetu. Tena yameshakuwa ni kitu cha kawaida siku hizi. Anyway,
labda tuongelee nini...
 
Mkuu, labda tutafute focus maana tumekuwa tukiongelea vitu vingi mno,
ungependa tujikite kwenye kuangalia nini? Inawezekana naongea vitu vingi
nikajikuta naacha mada ya msingi ambayo wewe umeikusudia. Suala la
mapenzi nililoliongelea lina maana sana unapotaka kuzama kwenye maudhui.
Haya niliyoyaongea kwenye tamthilia hii ndiyo nimekuwa nikiyapigia kelele haya
kwenye movie zetu. Tena yameshakuwa ni kitu cha kawaida siku hizi. Anyway,
labda tuongelee nini...
Tuongelee maudhui yaliyoko kwenye script pamoja na uwasilishaji wa hiyo script. Tuachane na technical part of it
 
Mkuu hivi haya siku hizi hayatokei kwenye hii karne ya dot.com na hawa vijana wetu ? kama mtu ana-act kama sharobaro (kama wenyewe wanavyojiita unategemea kwenye ku-act abadilike awe kama mstaarabu fulani au mtoto mwenye malezi ?

Kwahio mkuu ingawa na mimi naona kasoro nyingi sana kwenye Bongo Movie hadi kupelekea nisiziangalie sana lakini nadhani kwa mfano hapo juu tutakuwa tumewaonea.., nadhani hapo labda tuwalaumu watunzi kwanini wasitengeneze na filamu zinazohusu sana maisha ya watanzania na mila na desturi ili nazo ziingie sokoni sababu unajua watu wanaangalia soko na huu usharobaro ndio soko la vijana wetu (kwahio watengeneze na tamthiliya za familia na nyingine zinazohusu mila zetu)
Mkuu, makosa mawili hayawezi kuhalalisha jambo. Huu usharobaro na
hayo mengine unayoyasema ni mambo ambayo nimekuwa nikiyapigia
kelele kila siku. Sote tunayajua matatizo makubwa yaliyopo kwenye
movie zetu za Bongo ambazo kiukweli nyingi (90%) sijawahi kuziangalia
japo mimi ni mdau mkubwa. Siziangalii kwa kuwa najua nitakerekwa baada
ya kuziangalia, hivyo tusipende kulinganisha Bongo movie na kazi za watu
wenye weledi, waliojiandaa kwa kila hali na waliowekeza gharama kubwa.
Kwa hiyo unataka kuniambia kama Bongo Movie wanafanya mambo haya basi
hata wenye weledi ni ruksa kuyafanya?

Lakini pia ukumbuke kuwa kila kazi ya sanaa huwa ina mazuri yake na mabaya
yake, hata hizo Bongo Movie zinaweza kuwa mbaya 99% lakini kukawa na zuri
japo 1%. ambayo tutalazimika kujifunza kupitia hiyo 1%. Vivyo hivvyo kwenye
kazi nzuri kama hii tamthilia inayoongelewa hapa pia kuna mazuri na mabaya hata
kama ni 0.5%, kumbuka kuwa kila mtu huwa anatafuta angle yake ya kuangalia kitu.
Si lazima wote tukubali au tuyaiongelee mazuri tu lakini pia tunaweza kukubaliana
kutokubaliana. Hii inatusaidia kujua mengine ambayo pengine wengine tulikuwa hatuyajui,
hii ndiyo maana ya mjadala.

Mi nadhani hili ni jukwaa huru, kila mmoja ana utashi wake na maoni yake kwa kile
anachokiamini ili mradi tu atumie staha katika kuwasilisha maoni yake bila kuwakera
wachangiaji wengine. Naheshimu sana maoni yako.

Mwisho, labda niweke wazi, binafsi waliotengeneza hii kazi ni rafiki zangu,
nimeshafanya nao kazi, pia nilikuwa na mkataba nao wa script ambao umekwisha
December 31, 2012, na sasa niko huru lakini kuna kazi nyingine tumekubaliana kufanya
baadaye mwaka huu kama Mungu akipenda na kama tutafikia makukubaliano. Haya
ninayoyachangia humu huwa nawaeleza hata wao wenyewe physically, bila unafiki wala
kuongopeana na wao huwa wananipa ufafanuzi, na mwisho wa siku tunamaliza mjadala...
 
Mkuu, makosa mawili hayawezi kuhalalisha jambo. Huu usharobaro na
hayo mengine unayoyasema ni mambo ambayo nimekuwa nikiyapigia
kelele kila siku.
Mkuu sijasema kwamba hakuna makosa ila hayo uliyosema ni makosa sioni kama ni makosa.., different strokes for different folks na sababu movies zinareflect jamii tunayoishi basi since vijana wetu ndio wanavyoishi mitaani kwanini hata wabunifu wabadilishe ?, ndio kuna watu wanaoishi kwa maadili tofauti basi watunzi watengeneze movies za maadili tofauti pia.., hii ni kama watu wanaosema nyimbo nyingi ni za mapenzi (kama basi nyimbo nyingi ni za mapenzi ubaya haupo kwenye nyimbo za mapenzi bali ni wingi wake) kuna themes tofauti na ubaya haupo kwenye themes labda upo kwa watunzi kusahau themes zenye mafunzo na utamaduni wetu (ingawa hata hizo themes nyinginezo sio mbaya sababu zina nafasi yake)

Sote tunayajua matatizo makubwa yaliyopo kwenye
movie zetu za Bongo ambazo kiukweli nyingi (90%) sijawahi kuziangalia
japo mimi ni mdau mkubwa. Siziangalii kwa kuwa najua nitakerekwa baada
ya kuziangalia, hivyo tusipende kulinganisha Bongo movie na kazi za watu
wenye weledi, waliojiandaa kwa kila hali na waliowekeza gharama kubwa.
Kwa hiyo unataka kuniambia kama Bongo Movie wanafanya mambo haya basi
hata wenye weledi ni ruksa kuyafanya
?
Na mimi pia sijaangalia hizi movies na muda mwingi naona matatizo yapo kwenye plot mbovu wala hazina substance..., yaani story nyepesi nyepesi ambapo naona kwenye nchi yenye historia na utamaduni mkubwa kuna Gap kubwa sana kwa watunzi kuweza kupata stories za nguvu.. (tatizo sio acting pekee, bali ni utunzi mbovu na story nyepesi nyepesi) na mimi suala la gharama naona kama ni kisingizio tu kuna movies zilikuwa blockbuster kwa kutumia pesa ya kawaida tu, alafu mkuu nadhani hatujaelewana kwenye issue ya mambo ya weledi (nimesema kama actor ana-potray Sharobaro au kijana wa sasa wa mtaani) unategemea ata-act tofauti na kujifanya mtu wa weledi.., kwahio mkuu hapa kosa ni watunzi na wanaoandika script kutokutoa movies za weledi (sio kwamba kila movie ambayo haina weledi ni mbaya)
Mwisho, labda niweke wazi, binafsi waliotengeneza hii kazi ni rafiki zangu,
nimeshafanya nao kazi, pia nilikuwa na mkataba nao wa script ambao umekwisha
December 31, 2012, na sasa niko huru lakini kuna kazi nyingine tumekubaliana kufanya
baadaye
mwaka huu kama Mungu akipenda na kama tutafikia makukubaliano. Haya
ninayoyachangia humu huwa nawaeleza hata wao wenyewe physically, bila unafiki wala
kuongopeana na wao huwa wananipa ufafanuzi, na mwisho wa siku tunamaliza mjadala...

Naam sasa kumbe hapa ndio tumegundua ubaya na tatizo la hii tasnia yetu kutokuwa na movies za kutosha zenye themes tofauti na zenye stories zilizokwenda shule.., sababu nyie mnaoandika script zinapwaya.., mkuu umeshaandaa movies ngapi au script ngapi zenye utamaduni na weledi kama wewe unaosema..? nina uhakika ukiandika kama hii watu wataangalia na kuna Gap kubwa kwenye soko la movies kama hizi.. (kwahio kosa sio hizi movies ambazo zipo sokoni, kosa ni ukosekanaji wa hizo movies nyingine unazosema).., Sio kwamba natetea Bongo Movies huwa zinaniboa ila kinachoni-put off ni overacting, story mbovu, na movies kufanana fanana na zinakuwa kama ngonjera na maigizo (reality hakuna kabisa) ila ulichosema ni kosa (kuongea kwa kuangalia pengine au kumpa mtu flowers na kusema surprise nadhani kwa lugha ya wenzetu wanasema "To make a Mountain from a Mole Hill"
 
Naam sasa kumbe hapa ndio tumegundua ubaya na tatizo la hii tasnia yetu kutokuwa na movies za kutosha zenye themes tofauti na zenye stories zilizokwenda shule.., sababu nyie mnaoandika script zinapwaya.., mkuu umeshaandaa movies ngapi au script ngapi zenye utamaduni na weledi kama wewe unaosema..? nina uhakika ukiandika kama hii watu wataangalia na kuna Gap kubwa kwenye soko la movies kama hizi..
Mkuu, nakubaliana na wewe katika mambo mengi ila pengine tofauti yetu ni lugha
tunazoongea pengine zinatofautiana japo ujumbe unabaki kuwa ni uleule, kwa mfumo
wa soko la filamu Tanzania kama utafuata weledi kwa kiwango kikubwa unaweza
usitengeneze filamu, labda tamthilia kwa kuwa hazihitaji fadhila za wahindi kuzisambaza.
hivyo kwa mfumo huu unatufanya baadhi yetu kutupwa nje ya soko. Nimeshaandika script
kadhaa kwa soko la Bongo na hata kwa soko la nje, ila bahati mbaya sana kwa product
za Bongo (Bongo Movie) nyingi huwa ni tofauti sana na script yenyewe. Hii ni kwa sababu
mwenye kui-transform script into movie ni director ambaye inategemea weledi wake au angle
atakayoitumia katika kuitafsiri script into movie.

Mimi huiangalia sinema kwa mambo makuu matano: Script nzuri, Waigizaji wazuri, Wapigapicha
wazuri, Muongozaji mzuri na Mhariri mzuri. Naamini script ni sawa na msingi imara wa nyumba
unaotokana na ramani nzuri (stori). Kama script haitakuwa mzuri hata filamu haiwezi kuwa nzuri
kabisa, hii inamaanisha kuwa kwa script mbovu hata ukimleta muigizaji mzuri duniani hawezi
kucheza katika kiwango tulichozoea kumuona akicheza.

Waigizaji ni sawa na matofali yanayotumika katika ujenzi wa nyumba, huku wapigapicha
ni kama simenti na maji kwa ajili ya kujengea nyumba. Muongozaji ndiye fundi mjenzi,
anayepaswa kuchanganya vizuri simenti, maji na mchanga ili kupata kile kinachotakiwa.

Bahati nzuri tasnia yetu imebarikiwa kuwa na waigizaji wengi wazuri, wapigapicha wengi
wazuri na hata wahariri wengi wazuri, lakini inakosa waandishi wazuri wa script na waongozaji
wazuri wa filamu. Hii haimaanishi kuwa hakuna kabisa waandishi au waongozaaji wazuri hapa
nchini, wapo wengi tu wenye uzoefu na elimu ya kutosha katika uandishi na uongozaji wa filamu,
tatizo ni mfumo mbovu unaowafanya kutupwa nje ya ulingo wa soko la filamu kwa kuwa
hawathaminiki, hawatumiki wala hawapewi heshima inayostahili.

Script limekuwa tatizo kubwa kwenye filamu zetu, hasa kwa kuwa ni moja ya vipengele muhimu
sana katika uandaaji wa filamu na michezo ya kuigiza inabebwa na dhana ya kuwa script ni hatua
ya mwanzo, ni ramani ya kutuongoza kutoka kwenye wazo (concept) hadi final edit.

Lakini watazamaji walio wengi hukimbilia kumlaumu mwandishi wa script pindi filamu inapokuwa
mbaya, ikisababishwa na kutoelewa nani hasa mwenye jukumu la kuhakikisha filamu inakuwa nzuri.
Hapa ndipo script inapokuwa chanzo cha mahusiano mazuri au mabaya (a love-hate relationship)
kati ya mwandishi na timu ya uzalishaji, hasa muongozaji wa filamu.

Uhusiano mbaya huja pale muongozaji wa filamu anapoamua kubadili baadhi ya matukio ndani ya script,
wakati mwingine hubadili sehemu kubwa ya script bila hata kumshirikisha mwandishi na hivyo kuvuruga
mtiririko mzima wa stori. Kitendo hiki kinaweza kusababisha kuzalishwa filamu yenye hadithi tofauti
kabisa na iliyoandikwa mwanzo ingawa jina la mwandishi litabaki lilelile. Haya yamekuwa yakitokea sana,
binafsi yamenikuta na nimeshawahi kushuhudia yakitokea hata kwa waandishi na waongozaji wakubwa
duniani.

Filamu ni zao la muongozaji na wala si la mtayarishaji, mwandishi au muigizaji kama ambavyo wengine
wanadhani. Muongozaji wa filamu anapaswa kuwa mbunifu na kiungo muhimu kati yake na timu ya
uzalishaji. Muongozaji anawajibika katika kutafsiri script iliyoandikwa kwenye karatasi na kuihamishia
katika picha halisi na sauti kwenye skrini – na anapaswa kuiona taswira halisi na kutafsiri mtindo na
muundo wa filamu hiyo, na hivyo kufanya kazi zote mbili kama kiongozi wa timu na msimulizi kwa
kutoa picha halisi.

Tatizo kubwa lililopo kwenye tasnia ya filamu hapa Tanzania ni kwa waongozaji wetu wa filamu
kudhani kuwa kazi ya uongozaji wa filamu ni kujua: "standby... action... cut!" na kusahau kuwa
muongozaji ndiye anayepaswa kumtengeneza mhusika kwa kutegemea muongozo unasemaje.
Kama muigizaji atashindwa kuvaa uhalisia, hilo sio kosa lake ni kosa la muongozaji na hutafsiri
uwezo wa muongozaji ulipokomea.

Sasa nikirudi kwenye swali lako la msingi: kutokana na mfumo wa soko la sasa, ukweli sina
hata movie moja niliyowahi kuandaa lakini kuna movie nyingi ambazo niliandika script au
kufanya kazi kama consultant, sound expert au director. Sasa sijui unahitaji kuziona filamu
zilizotokana na script nilizoandika au unahitaji kuziona script nilizoandika?...
 
Back
Top Bottom