Mkuu umenikumbusha hili tatizo lilishamkumba Tyler Perry (ambae studios zilikuwa zinataka kubalisha movies zake na zilimwambia movies zake ni tofauti na wenyewe walivyotaka..) ila jamaa hakukata tamaa wala hakubadilisha mfumo wake bali alianzisha studio yake na kutoa movies zake mwenyewe.. (kwahiyo labda swali lije kwenye ugumu wa kusambaza movie mwenyewe na ku-promote mwenyewe bila kutegemea wasambazaji) nina uhakika ugumu utakuwa mwanzo tu ila ukishajenga jina watu watakufuata.., pia word of mouth na trailers za hapa na pale zinaweza zikakusaidia kwenye promo..; labda swali gumu zaidi hivi low budget movie kwa Tanzania na kwa kutumia unknown actors inaweza ikagharimu kiasi gani hadi mtu ushindwe kutoa kitu bila kushirikisha mdosi ?
Kuna kipindi fulani walikuja wataalam wa filamu watatu, wawili kutoka Hollywood
na mmoja kutoka Australia kwa ajili ya kufanya reasearch katika film industry ya
Bongo, hii ilikuwa ni project maalum hasa kuangalia kama inaweza kufanya kazi
baada ya Kenya kuprove failure kwenye commercial films. Bahati nzuri walikuwa
na taarifa zangu, nikatafutwa na kujiunga nao. Tulisafiri zaidi ya mikoa nane na miji
yote mikubwa yenye pilikapilika ya Tanzania.
Hivyo nikaamua kuitumia nafasi hiyo pia kufanya utafiti na kuandika ripoti yangu
ambayo ilijumuisha kuanzia script hadi distribution. Siku ukiihitaji naweza kukupatia
ripoti ya utafiti wangu niliyoipa jina la "The Perspective of the Film and
Television Industry in Tanzania" ambayo nimeshaifanyia presentation kwenye
maeneo mbalimbali, hii ndiyo iliyokuja kuzaa wazo la Swahiliwood baada ya
Taasisi ya Media for Development International-Tanzania (MFDI-Tanzania)
chini ya John Riber kuamua kuifanyia kazi. Hawa MFDI ndiyo watengenezaji
wa filamu ya Chuo na hii tamthilia ya 'Siri ya Mtungi' tunayoijadili hapa.
Katika utafiti wangu huo ambao baadaye niliamua kujiingiza kwenye biashara
ya usambazaji na kusambaza filamu mbili za "Naomi 1" na "Naomi 2" kwa kushirikiana
na kampuni ya Studio KVS, hii ilikuwa ni kufanya utafiti kwa vitendo. Mambo
niliyogundua ni kwamba ili uweze kupata mafanikio unahitaji kuwa na mtaji mkubwa
kwani wauzaji wa rejareja walioko mikoani watakuuzia kazi yako vizuri kama utakuwa
unatoa kazi mara kwa mara (ikiwezekana kila wiki), kinyume na hapo huwa wanauza
lakini wanakuwa wasumbufu kulipa hadi wasikie unatoa nyingine...
Ni kweli usemayo ila niliona interview moja ya Samuel Jackson akasema yeye huwa anaangalia script na anakwenda kuifanyia kazi na kurudi na kushauriana na mtunzi/director kuhusu hiyo script husasan kwenye Dialogue yeye mwenye hupenda kuweka maneno yake na kuboresha kwahio nadhani cha muhimu nadhani ni kwa director; script writer na actor wote kufanya kazi pamoja mwanzo mpaka mwisho kwa kukubaliana sio kila mtu kufanya kazi kivyake.
Sipingani sana na wewe ingawa wakati nasomea masuala ya uandishi wa script
(creative writing) tulifundishwa kuwa: Script nzuri inaweza kutoa filamu mbovu
lakini script mbovu kamwe haiwezi kutoa filamu nzuri. Naamini unaweza kupata
product nzuri kutokana na script mbovu endapo mtashirikiana (hasa kama ni kundi
la watu wenye weledi) kuiboma na kuiboresha vizuri. Hii itatokana na muongozaji
endapo hatakuwa overall incharge (maana wengine huwa hawataki kushauriwa)...