Siri ya Lowassa yavuja

Siri ya Lowassa yavuja

Haki ya nani hii nchi hatutakaa tuendelee kama mibunge inayochaguliwa ndo aina ya Msukuma saa ngapi tutapata maendeleo? Yaani mbunge mzima hajui hata utaratibu wa kumpata waziri Mkuu? Aibu yenu wana Geita kama mtapeleka Bomu bungeni, hili litamzidi hata Prof. MAJI Marefu!
 
Huyu jamaa ana akili ndogo, kikatiba waziri mkuu lazima awe mbunge wa kuchaguliwa. Sasa sumaye anagombea jimbo gani? Ni bahati mbaya tuna wanasiasa wasiojitambua hata kidogo!

Halafu anasema eti ni mwaka wa 'kanda ya ziwa kutoa rais'! Kumbe uraisi tunapokezana kikanda? Haya maneno yanaonekana kama mepesi, lakini tuna-inject sumu mbaya kwa wananchi!
 
Msukuma anadai kwamba EL akichaguliwa, ataunda serikali iliojaa watu wa ukanda wa kaskazini. Labda nimuelewe kwamba anapinga swala la Ukanda. Ni vyema.

Lakini aliendelea kusema kwamba "sasa ni wakati wa kanda ya ziwa kutoa rais" wa JMT.

Naona anajikanyaga mwenyewe!

Mimi ni msukuma wa mwanza lakn kura yangu ni ya UKAWA tuuu! Sina uadui na Mh. Magufuli bali adui yangu ni CCM. Kwani CCM amenifanya niwe katka hali hii ya UMASKINI kwa kunitengenezea mazingira ya kiunyonyaji katka mchakato mzima wa upangaji na uhalalishaji wa bei ya Pamba(ambalo ndilo zao kuu la biashara kwetu) . Bei ya Pamba ni sh. 600 hadi 800 kwa kilo mpaka sasa hv, wakati bei ya bidhaa kama bati, mfuko wa simenti , baiskeli, nguo,.... n.k zinazidi kupanda kila siku na kila mwaka. Ni mwaka 2010 tu ndo bei ilipanda hadi kufikia sh. 1200 kwa kilo baada ya hapo bei ikashuka tena hadi leo ni 600 au sh. 720 kama una mikokoteni mitatu au zaidi iliyojaa Pamba.
Kama nitapigia Kura yangu CCM basi nitakuwa nimetoa uthibitisho tosha kabsa kuwa mm ni Lofa na mpumbavu wa kuibiwa Pamba kwa sh. 600 kwa kilo tangu mwaka 2005. Hapa hakuna cha kushabikia ukabila wala ukanda. Nahitaji mabadiliko ya Chama na siyo mtu. Hata kama Mh. Magufuli ni msukuma mwenzangu lakn mm nimeshachoka na CCM.... Hivyo kura yangu iko UKAWA na siyo CCM.

Nimeshachoka kudanganywa na CCM acha nione na uongo wa chama kingine ila siyo uongo wa CCM.
Mm ni MWALIMU pia MKULIMA wa zao la Pamba..... lakn kwa kada zangu hizi mbili hakuna hata kada moja ambayo serikali ya CCM imethamini JASHO langu (kweli mm nitakuwa lofa na mpumbavu kama nitaendelea kumpa kura yangu CCM kwa ngazi zote kuanzia umonita wa darasa hadi rais wa nchi )

Mkulima wa zao la Pamba kanda ya ziwa na mwalmu wa sekondari anayeathirika na mfumo wa kiunyonyaji wa chama cha CCM, kama ambavyo wengi tunadhulumiwa JASHO letu na CCM, chondechonde amka tupambane na huyu adui yetu CCM.... Ukabila na ukanda isiwe kisingizio au kigezo cha kumrudisha madarakani CCM. Kumbuka ndugu yetu magufuli hata kama tutampitisha hataruhusiwa na wazee wa chama kuufumua na kuupanga upya mfumo wa CCM. Tabia ya CCM kutuimbia mashairi mazuri ya ILANI yao kipindi cha kampeni lakn utekelezaji wake 34%, tuseme sasa basi imetosha (msukuma mwenzetu usitulaumu kwa hili) ....hapa TANZANIA KWANZA ukanda na ukabila baadae. Hatuchagui mtemi au chifu wa wasukuma bali tunachagua mtemi au chifu wa watanzania wote (bara na
zanzibar).

Chondechonde watanzania wenzangu (hasa wanaothirika na mfumo wa CCM) uchaguzi wa mwaka huu kwa pamoja na kwa sauti moja tuseme CCM basiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii. Kufanikisha hili (kumuondoa CCM), kura yako pigia chama na siyo mtu (kwani watu ni walewale na mapungufu yao hayana tofauti kubwa sana).
 
Waziri mkuu tangu akawa hatokani na wabunge wa kuchaguliwa? Mmatufanya wajinga? Subirini hukumu yenu mamaye zenu maccm.
 
Huyu jamaa anasema Lowassa atamteua Sumaye kuwa Waziri Mkuu. Sumaye si mbunge na wala hagombei ubunge. Waziri Mkuu ni lazima awe mbunge wa kuchaguliwa, kwa mujibu wa katiba na definitions za Tume ya Uchaguzi.

Huyo Sumaye atakuwaje Waziri Mkuu bila ya kuwa na jimbo la uchaguzi aliloshinda?
 
Huyu Jose Msukuma pamoja na yule jaluo wa Rorya ni walanguzi na wafanya magendo wakubwa. Ndio siri ya utajiri wao. CCM ni kichaka chao cha kujificha
 
Sumaye waziri mkuu tena aaaaargh jamani. Tanzania yangu mbona hivyo? Mpiga madili Mbowe form 6 failure ndiyo waziri wa fedha? Poor Tanzania! Nakuombea sana kikombe hiki na kikupite!
 
Msukuma ana shida.... yaani hana la kumsema el.... anatafuta kukubalika ndani ya ccm asionekane msaliti....eti Sumaye awe waziri mkuu... kwa katiba ipi....
Umeonaa? Ccm ni wamechanyikiwa hawana pakushika miti yote inateleza
 
Sumaye waziri mkuu tena aaaaargh jamani. Tanzania yangu mbona hivyo? Mpiga madili Mbowe form 6 failure ndiyo waziri wa fedha? Poor Tanzania! Nakuombea sana kikombe hiki na kikupite!

Tumia akili yako kidogo kufanya utafiti , Sumaye atawezaje kuwa Waziri Mkuu kwa katiba iliyopo?
 
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita, Joseph Msukuma amesema ana siri kubwa ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuhamia Chadema na kupewa nafasi ya kugombea urais akiwakilisha vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Msukuma alisema yeye alikuwa miongoni mwa timu ya watu 11 iliyokuwa na mkakati wa kumsaidia Lowassa kushinda katika kura za maoni za kuomba kuteuliwa kugombea urais ndani ya CCM, ambapo alikatwa na kuhamia Chadema.

Alitoa kauli hiyo kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za mgombea ubunge wa Jimbo la Geita Mjini, Costantine Kanyasu uliofanyika juzi kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Nyankumbu.

Alidai kuwa baada ya Lowassa kukatwa wananchi wengi walianza kusema ana mpango wa kuhamia Chadema ili kumfuata, lakini alisisitiza kwamba hana mpango huo kwani ana siri nzito kuhusu mgombea huyo wa Ukawa.

Msukuma ambaye ni mgombea wa CCM Jimbo la Geita Vijijini, alidai kuwa hadi sasa mpango wa Lowassa kama atashinda kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kumteua Waziri Mkuu mstaafu aliyehamia Chadema, Frederick Sumaye kuwa waziri mkuu katika serikali yake.

Alisema mpango wake mwingine ni kumteua Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe kuwa Waziri wa Fedha, vyeo ambavyo alidai ni kugawiana kutokana na ukanda ili waunde Serikali.

“Mimi nilizunguka nchi nzima na Lowassa, nikiwa miongoni mwa timu ya watu 11 iliyokuwa ikimpigia debe ashinde, najua mipango yake mingi, namsubiri aje Geita aropoke hapo ndiyo atamjua Msukuma ni nani, nitatoa siri zake zote,” alisema Msukuma huku akishangiliwa na wananchi.

Aliwataka wananchi kumpuuza mgombea huyo wa Ukawa na badala yake wananchi waelekeze nguvu zao kumchagua mgombea urais wa CCM, Dk. John Magufuli huku akisisitiza kuwa ni muda wa Kanda ya Ziwa kumtoa rais.
Matata

Aliyewahi kuwa Meya wa Jiji la Mwanza kupitia Chadema, Henry Matata naye ametoboa siri baada ya kudai alijiunga na chama hicho akiwa pandikizi kutoka CCM na kwamba alichokipata kinatosha.

“Mimi nilikuwa pandikizi wa CCM ndani ya Chadema, baada ya kuona Mbowe natekeleza Ilani ya CCM katika kipindi changu cha Uongozi wakanifukuza,” alidai Matata.

Aliongeza kuwa akiwa Chadema amekaa humo na kujua matatizo na siri zote za chama hicho pamoja na matatizo yote ya Mbowe.

Hata hivyo, aliwataka wanachama wa CCM Wilaya ya Geita ambao bado wamegawanyika kutokana na makovu ya uchaguzi wa kura za maoni kuvunja makambi ili kujihakikishia ushindi katika jimbo hilo la Geita.

Mgombea

Mgombea ubunge wa Jimbo la Geita, Costantine Kanyasu alisema akichaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Geita atahakikisha makapi ya mawe yanayosadikika kuwa na dhahabu katika Mgodi wa Geita maarufu kwa jina la Magwangala yanatolewa kwa wananchi.

Alisema kilio kikubwa cha wananchi wa Geita hasa vijana wachimbaji wadogo ni Magwangala na kuahidi kama atapata ridhaa hiyo atapambana kufa au kupona ili kuhakikisha mawe hayo yanatolewa kama inavyofanyika katika migodi ya Kahama na Nyamongo.

Kanyasu alisema kero kubwa kwa wananchi wa Geita ni tatizo la maji ambalo limekuwepo kwa kipindi kirefu na kudai kwamba kabla ya kuomba ridhaa alikuwa anafuatilia tatizo hilo ambalo limeanza kutatuliwa na Serikali.

“Mimi mkinipa nafasi hii nitahakikisha stendi inakuwa ya kisasa..ni muda mrefu stendi yetu mmekuwa mkiilalamikia…mvua zikinyesha yanakuwa majaluba ya mpunga..nawaahidi nitahakikisha tunakuwa na stendi inayoendana na hadhi ya mkoa wetu,” alisema.

Aliongeza kuwa atahakikisha Kituo cha Afya Nyankumbu kinapatiwa gari la wagonjwa ili kuondoa kero ya kutegemea gari la Hospitali ya Wilaya ya Geita hali inayochagia vifo kwa wagonjwa.

Aliwaomba wananchi wamchague yeye pamoja na mgombea urais, Dk. Magufuli ambaye anaamini kwa uchapakazi wake Geita itabadilika na kuwa mkoa unaofanana na rasilimali iliyopo.

Dk Slaa

Katika hatua nyingine, aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya za Same, Magu na Misenyi, Mhandisi Elias Maarugu (70) amemlipua aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa kuwa si msafi wala mwadilifu akisema asiwadanganye Watanzania.

Alidai kuwa Dk. Slaa hana tofauti na dikiteta na kwamba alikuwa mzigo kwa chama hivyo wananchi wapuuze kauli zake ambazo amezitoa hivi karibuni kuhusu Lowassa.

“Slaa si mwadilifu. Ameendesha chama kwa mabavu kwa sababu alikuwa hatoi nafasi kwa wanachama kujitetea ambayo ni haki ya mtu kufanya hivyo,” alidai Maarugu wakati akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Bukoba na kuongeza;

“Alinisingizia kuwa nimehongwa fedha na kunitaka nitoe majibu ndani ya wiki mbili nilifanya hivyo lakini alinijibu kwamba suala langu linashughulikiwa na sekretarieti ya chama kumbe ulikuwa uongo mtupu. Ni muongo na hana uadilifu wowote,” alidai.

Chanzo: Jambo leo

kwakuwa na wewe mlikuwa mkizunguka wote,na ww alikuahidi nini
 
​Usaliti ni kitu kibaya wewe Msukuma nilikusikia ukitamka Dodoma kuwa akikatwa patachimbika leo ni wewe wa kutuambia siri za Lawasa hakika usaliti ni kitu kibaya sana na nina hakika jibu lako utalipata hapahapa duniani!!
 
Lowasa ndiye.......

Huyo msukuma akajambe tu alale na ubunge atauskia kwenye bomba
 
Back
Top Bottom