MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,185
- 24,051
Wewe kwa akili yako unadhani sheria ni msahafu wa maneno ya Mungu kwamba binadamu hawezi kutabadilisha?Mtu anagombea urais anajinadi kwa kufuta posho za wafanyakazi. Hivi Magufuli hajui posho za safari semina mafunzo n.k ziko kisheria? Hili sio jambo la kujivunia hata kidogo. Au autuambie hizo posho za mawaziri ni tatizo kwenye serikali hii ya kwao tutamwelewa. Halafu raisi anajinadi kwa sera . Hivi kweli kupunguza au kuondoa kabisa posho za wafanyakazi ni sera au kipaumbele cha Rais ajeye 2015? Magufuli anatakiwa ajue tofauti ya utendaji wa serikali na miongozo yake na sera ya nchi. Huwezi kujinadi kwa vitu vidogo namna hii halafu ukaniambia wewe una uwezo wa kuwa Rais.
Sasa kama utafuta posho za mawaziri ina maana sisi wafanyakzi wa kawaida utatufanyaje? Yaani hata tukisaifri kikazi tujitegemee posho ?
Anaposema atafuta ina maana atapeleka mswaada bungeni ili itungwe sheria myingine itakayofuta posho za wafanyakazi na mawaziri.
Half knowledge is more dangerous than ignorance!