Mkulima hahitaji serikali tatu anachotaka ni serikali moja itakayompa uhuru wa kumiliki ardhi na kulima popote na kuuza popote
Mfanyabiashara anachotaka ni serikali moja yenye sheria za biashara na kodi za aina moja na taratibu za aina moja zinazomwezesha kufanya biashara popote bila bughudha ya aina yoyote
Mfanyakazi angependa kuwe na serikali moja ambapo yuko huru kufanya kazi popote na kwa viwango sawia vya mishahara na marupurupu
Mvuvi angependa serikali moja inayomwezesha kuvua popote na kujiuzia popote
Kiongozi wa dini angependa serikali moja yenye sheria moja ambayo inamwezesha yeye kutangaza dini yake na kuabudisha popote bila vikwazo
Mwanafunzi angependa awe huru kusoma popote na kupata mkopo wa kusoma popote
Lakini wanasiasa ndio wanataka serikali tatu ili wawe na nyimbo zao,majeshi yao,balozi zao,na vyeo vyao vya kisiasa na mafungu yao ya kugawana mapato yatokanayo na kukamua kodi wanyonge
Wakili wa kujitegemea angependa serikali moja ya kumwezesha kufanya kazi zake popote bila vikwazo ndani ya nchi moja.
Mfugaji wa kuhama hama angependa serikali moja inayoruhusu yeye kujichungia mifugo yake popote penye malisho mazuri ya mifugo yake
Hivi hiyo tume ya Warioba ina uhakika kuwa wananchi ndio wanataka serikali tatu?
Mimi baada ya kuwahoji wanachi wa kawaida wengi wameruka kuwa hilo la serikali tatu anayelijua vizuri ni huyo warioba na tume yake na hao wanasiasa wa UKAWA.
Wataka serikali tatu wanaotoa hadi mapovu ni wanasiasa ambao wanaishi kwa kutegemea siasa tu na wanaofaidika na ulaji kodi za wananchi ila wanajaribu kutumia wananchi kama ngao ya ubaradhuli wao.
Chadema na CUF wanajua kuwa si rahisi wao kushika nchi ikiwa moja kwa sababu CUF ina nguvu sana Zanzibar lakini bara haina nguvu hivyo nchi ikiwa moja wanajua hawatapata kura bara na CHADEMA wanaona kukiwa na serikali moja watakwama kwa kuwa wana nguvu sana Tanzania bara lakini Zanzibar hawana nguvu hivyo kukitokea uchaguzi kukiwa na serikali moja wanajua watakwama. Hivyo makundi haya mawili ya CUF na CHADEMA yanapigania serikali tatu kwa kuota ndoto za Alnacha kuwa zikipatikana basi CUF itashika Zanzibar CHADEMA tashika BARA na CCM itaambulia hako kaserikali ka muungano kasikokuwa na NGUVU wala raslimali bali kanategemea michango ya washirika.
Ukweli ndio huo wanasiasa ndio wanataka serikali tatu na warioba akaona muhimu kuwasikiliza hao na akayaita eti ndio maoni ya wananchi sio kweli.
Katika vitu vya aibu ambavyo tume imefanya ni kuchukua maoni ya wanasiasa kuhusu serikali tatu na kuyaita maoni ya wananchi .Ni aibu kwa tume. Najisikia vibaya tume kwa hili imekula posho ZA KODI ZA WANANCHI bure kabisa.
You are really a SUPER EAGLE, kama lilivyo jina lako... you have got an excellent Eagle's view of things and the way they are in Tanzania right now. HONGERA SANA MKUU for hitting the nail right on the HEAD.!!!!
Nimeipenda analysis yako which is very true and objective: wanasiasa ndio wanaoharibu mchakato wa katiba mpya kwa malengo yao ya kujifaidisha wenyewe. They do not have wananchi or their interests at hear AT ALL... na hii ni kwa both UKAWA and CCM.
Hao wachangiaji wengine wanaopinga post hii either ni katika kundi la wanaotarajia kunufaika na serikali 3 au 2, au ni MISUKULE na KENGE tu wanaofata msafara kiushabiki bila kujua unakwenda wapi na utawasaidiaje!!!
Inasikitisha kuwa siku hizi karibu kila mtu ni mshabiki tu esp. wa upinzani na wanafata upepo unaovumishwa na viongozi wao lakin hawajitambui..hata hapa JF wako wengi UTOA MAPOVU tu kutetea KILA KITU wanachoambiwa na viongozi wao wa siasa.
Sasa hao UKAWA wanaotaka serikali 3:
- Je mkulima, mfugaji, mwanafunzi, wastaafu, private sector, etc etc (tuseme mwananchi wa kawaida) ananufaika vipi kiuchumu na serikali 3????? Mbona Tume ya Warioba haijatuletea hiyo analysis?
- NAPINDA kwa nguvu zangu zote propaganda ya Tume kuwa "hayo ni maoni ya wananchi" hao waliowahoji wana-represent % ngapi ya wananchi zaidi ya 40 mill ya watanzania??? Statistician yeyote ukianalyze hizo data za Waryoba utakuta kuwa ni very very STATISTICALLY INSIGNIFICANT kuweza kuwa representative of the population!!!!
- Kwa mantiki ya data kuwa statistically insignificant, hata UKAWA NI invalid kwani hiyo rasimu kiukweli huwezi kusimama na ujasiri na kupiga kifua kusema ni ya "wananchi"
- Ili kujua kuwa hata Tume ilikuwa na ajenda zake zilizojificha cha kujinufaisha kwa serikali 3, kwa nini hadi leo TUME IMESHAMALIZA KAZI LAKINI HAWATULII KILA SIKU KWENYE MAKONGAMANO KUTETEA HIYO RASIMU? Kuna nini hapa???
- Kama UKAWA interest yao sio ya kisiasa ya serikali 3 kwa nini HAWATAKI KURUDI BUNGENI KUJADILI VIFUNGU VINGINE AMBAVYO SIO VYA MUUNDO WA SERIKALI bali vina-touch maisha ya kawaida ya wananchi? Kwani RASIMU NI MUUNDO WA SERIKALI TU?
- Wengine wanasema serikali 3 sio kuongeza vyeo: WRONG; kumkuba kuja kwa serikali tatu kutalazimu kuwepo kwa several Oversight institutions ambazo rasimu imesema lazima ziwe created: katika mahakama, ulinzi, tume ya ajira, na utitiri wa commissions kibao!
MIMI nilishastuka zamani nio ovu na selfish ya UKAWA katika mchakato huu, ila wengine wengi hawajijui na wanatumiwa kama madekio kwa ajili ya wanasiasa.