Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,395
- 13,272
Nimegundua kumbe kuna agenda ya siri kwa watu fulani wa makundi fulani walioko na nafasi fulani kisiasa kwa vyama tofauti kutaka serikali tatu ili vyeo viwe vingi , vyeo kibao , serikali kibao ofisi kibao , semina kibao, safari kibao , posho kibao , sadakalawe amina, mwenye kupata apate mwenye kukosa akose! kumbe madaraka matamu jamani hata wale waliopita nao wanayataka.
Zikiwa serikali tatu, uongo hata kama ulistaafu miaka hamsini iliyopita ila kwa CV yako uongo hukosi nawewe japo Naibu Waziri.
Ila serikali zote kama kawaida zitaendeshwa kwa kodi zetu na majasho yetu.
Mwenye masikio na asikie.
Ni mtazamo tu wa mimi kijana nisietaka kusikia mawazo ya wazee na sina chama wala itikadi wala manifesto.
Mwenye busara huongea inapobidi, mjinga huongea ili mradi!