Sipo hapa kuitetea CHADEMA - Baregu

Sipo hapa kuitetea CHADEMA - Baregu

mzee slaa akisikia msimamo wa baregu anatamani ammeze kwa kuwa yeye anapenda kuabudiwa.
 
Ukisoma falsafa vizuri inakusaidia kujenga hoja na kuitetea hata kama itakuwa ni kwa nchi yako ilimradi hoja yako iwe na misingi makini ...Kwa hili CDM tukubali hoja ya mwenzetu ili itupatie nafasi ya kuwabana na wengine wanaofata misimamo ya vyama badala ya matakwa ya wananchi walio wengi na ambao kimsingi hawana hata vyama...
katiba ni ya watanzania katika hili tuache siasa ambazo hazitalisaidia Taifa hili huko twendako
 
Kwa mtizamo wangu Prof kaonyesha kiwango kidogo cha ufahamu,
Katika hili kwanza alitakiwa kuwasikiliza kwanza ,ili aweze kuthibitisha kama hicho alichokifikiri ndicho walichomuitia.Kwani huwa hatukatai wito bali tunakataa neno.Na pengine haya majibu alitakiwa awape kulekule walikomuita.Lakini kuja nayo public na kutangaza ,naona ni usanii wa aina fulani wa kujitengenezea umaarufu, ili baadae ajione shujaa, na si ajabu siku ukimsikia karudi CCM.

Jambo la pili ,hili suala liliishapita siku nyingi ,kwa nini analirudiarudia kama mfano sehemu tofautitofauti kuna ajenda gani?

Kwangu mimi Huyu Prof,japo namuheshimu sana ,lakini kwenye hili napaswa kumuweka kwenye mabano,kama ana ajenda binafsi tutaiona mbele ya safari.
 
Waeleze hao wanaoshindwa kusoma na kuanalise. Kwanza hii kitu kilitokea mwaka jana wakati CDM walipotishia kujito kwenye mchakato na ikajadiliwa sana humu. Mleta thread kachukua kasentence kamoja na kuafanya kama vile DCM wanataka kumshinikiza awe pale kwa manufaa yao.

Hakuna mahali au siku ambayo tumesikia kuwa CDM wanataka hivyo. Hata Warioba aliwahi kuwaonya CCM na hii alijadiliwa hapa.

umesoma gazeti la majira lakini?
 
Nadhani viongozi wa CHADEMA walijaribu kutingisha kiberiti wakakuta kimejaa njiti.

Tanzania imebakiwa na wanasiasa wachache sana wanaofanya kazi kulingana na Sheria, kanuni, miiko na misingi ya kazi zao.

Prof. Baregu alionyesha kama ni mmoja wa wanasiasa hao.
 
Hilo ndo jambo la msingi, kwenye tume tunahitaji UTANZANIA wala siyo UCCM wala UCHADEMA!!!
 
Kwa wale ambao hawatasoma gazeti hii ndiyo habari kamili ya Prof. Baregu:
Amesema CHADEMA walimtaka afike kwenye Kamati kuu lakini aliwagomea kwa sababu alitambua alichokuwa akikifanya, kilikuwa kwa manufaa ya watanzania si chama chake. "Mimi skuapa kuitetea CHADEMA hata kama ni kada wake bali niliapa kuitetea Tanzania na wananchi wake, vyama vya siasa vinaweza kufa lakini Tanzania haiwezi , itaendelea kuwepo milele hivyo lazima tuheshimu hilo." alisema Prof Baregu. Baregu aliongeza kuwa yeye ni muumini wa serikali moja.

sasA huyu afanywe kwama mansour wa ccm kwa kwenda kinyume na chama atimuliwe chadema
 
Kwani ni wapi tulisema yupo kwenye tume kutetea msimamo wa CHADEMA?

Mkuu. Tatizo kuna watu wanaangalia mambo kiushabiki sana bila mantiki, Chadema kuna mambo ya msingi sana tunayaunga mkono kwenye rasimu ya katiba ambayo mwenyekiti wake ni Warioba. haimaanishi kuwa kwa kuwa tunayaunga mkono basi tunamuunga mkono Warioba kwenye kila kitu na hiyo haimaanishi kuwa kwa kuwa kuna mambo tunayaunga mkono kutoka kwa Warioba basi tunaunga mkono ccm kwa kuwa Warioba ni kada wa ccm. Kinyume chake kwa Baregu.
 
Huyu kaja kuwapotezea muda nanyi mnaanza kuwaka bila kuwaza.Haya yalijitokeza mwanzoni sana wakati Baregu akisema maneno haya .Leo huyu kaamua kuwapotezea muda kwa kuleta kipande kidogo watu wameanza kulipuka .Mbona aweki habari nzima ?Ushabiki wa kijinga this is not news any more yalishapita ilikuwa pale mwanzoni Kamati ilipo mtaka ajitoe akajibu haya .
 
Tatizo ni pesa na si Utanzania anavyoda, mabilioni yanamkengeusha Baregu!!!!!!!!
 
Kwa wale ambao hawatasoma gazeti hii ndiyo habari kamili ya Prof. Baregu:
Amesema CHADEMA walimtaka afike kwenye Kamati kuu lakini aliwagomea kwa sababu alitambua alichokuwa akikifanya, kilikuwa kwa manufaa ya watanzania si chama chake. "Mimi skuapa kuitetea CHADEMA hata kama ni kada wake bali niliapa kuitetea Tanzania na wananchi wake, vyama vya siasa vinaweza kufa lakini Tanzania haiwezi , itaendelea kuwepo milele hivyo lazima tuheshimu hilo." alisema Prof Baregu. Baregu aliongeza kuwa yeye ni muumini wa serikali moja.

Pamoja na msimamo wake huu mzuri (namuunga mkono 100%) angefika tu kuwasikiliza hao wna kamati kuu wenziye hoja zao na kuwapa msimamo wake.......kuwakwepa ni upungufu wa kimsimamo kwa upande mwingine
 
Kuna jambo la kujifunza kwenye habari hii:
1. CHADEMA kumbe wanatetea maslahi yao binafsi, na tunaposema maslahi yao tuna maana ya viongozi wa CHADEMA kwa sababu wangekuwa wanatetea na wafuaasi wao wote, basi Baregu angeitikia witowa kuitwa kwenye Kamati kuu kwa vile naye ni mmoja wa wale ambao angenufaika na wito huo, lakini kwa kutambua kuwa kuitwa kwake kulikuwa ni kwa ajili ya wachache akaona mbali;
2. Kwa nini Baregu anasema yeye ni muumini wa serikali moja wakati CHAMA chake kimezunguka nchi zima kutafuta maoni juu ya rasimu ya katiba mpya, bali kuhubiri serikali tatu? Yawezekana kabisa mikakati hii serikali tatu ndani ya CDM ilianza hata kabla ya kuundwa kwa kamati ya Katiba lakini mzee wa watu akaa nalo moyoni kwa vile hakuwa na pa kulisemea. Ni dhahiri kabisa kauli ya BAREGU inalenga kuimarisha muungano wakati harakati za CDM kutumia nguvu nyingi sana kunadi serikali tatu inalenga kuuvunja muungano jambo ambalo linadhihirishwa na kauli mbalimbali za makada wa CDM mfano LISSU alivyosema juzi kuwa CUF ni chma cha WAZANZIBARI.

Kwani mtu akigoma kuitikia mwito wa kamati ambayo ni moja ya vyombo vya utendaji wa chama ambacho yeye ni mwananchama na kiongozi ndipo anapoonekana mzalendo? Kwanini mwandihi unatuletea habari nusunusu? Kama aliitwa kweli na kuigomea kamati ina maana alijua nini kamati ingemwambia? Hapa ndipo ninapopata shida na habari hii na kuiona kama uvumi maana kama ni kweli Profesa aliitwa na kamati na kwa bahati nzuri akapewa agenda za kikao na akakataa kuhudhuria amejinyima fursa ya kuwa Profesa na mwalimu mzuri maana angweza kutumia agenda hizo kutoa elimu kwa viongozi wengine wa CDM na Watanzania kwa ujumla. Kama anaamini siasa ni kukubali kutokukubaliana angekwenda akawasikiliza na kuifikia doctrine ya agree to disagree. Mimi naona hiki alichokifanya ni kuwa megalomenic
 
Na wajumbe ambao ni makada wa CCM, tuna uhakika gani kama hawatazingatia maslahi ya chama chao? Isije kuwa kwa Chadema tu wakati wenzake wa CCM wanapeta tu, Hatutamuelewa kwa kweli.
 
kama slaa na mbowe wana ubavu wamfukuze baregu kama madiwani wa arusha. Baregu ameidharau kamati kuu ya chdm
 
Back
Top Bottom