Kuna jambo la kujifunza kwenye habari hii:
1. CHADEMA kumbe wanatetea maslahi yao binafsi, na tunaposema maslahi yao tuna maana ya viongozi wa CHADEMA kwa sababu wangekuwa wanatetea na wafuaasi wao wote, basi Baregu angeitikia witowa kuitwa kwenye Kamati kuu kwa vile naye ni mmoja wa wale ambao angenufaika na wito huo, lakini kwa kutambua kuwa kuitwa kwake kulikuwa ni kwa ajili ya wachache akaona mbali;
2. Kwa nini Baregu anasema yeye ni muumini wa serikali moja wakati CHAMA chake kimezunguka nchi zima kutafuta maoni juu ya rasimu ya katiba mpya, bali kuhubiri serikali tatu? Yawezekana kabisa mikakati hii serikali tatu ndani ya CDM ilianza hata kabla ya kuundwa kwa kamati ya Katiba lakini mzee wa watu akaa nalo moyoni kwa vile hakuwa na pa kulisemea. Ni dhahiri kabisa kauli ya BAREGU inalenga kuimarisha muungano wakati harakati za CDM kutumia nguvu nyingi sana kunadi serikali tatu inalenga kuuvunja muungano jambo ambalo linadhihirishwa na kauli mbalimbali za makada wa CDM mfano LISSU alivyosema juzi kuwa CUF ni chma cha WAZANZIBARI.