Kwa Dodoma mie nilikwenda 2018 nikawakubali sana
Suma Lodge. Yaani niliwakubali sana tu. Ila sijui kwa sasa 2020 kama bado wako vizuri vilevile.
Ila kuna mgesti mmoja m-bovu sana uko karibu na Police Central ndo bodaboda alinipeleka usiku usiku huo kama saa sita hivi ndo nimewasili, yaani walinikera maana walichukua hela yangu reception kwanza halafu ndo wakanipeleka chumbani. Godoro jembaba kama chapati yaani chaga unazisikia. Halafu eti maji ya kuogea kwenye ndoo. Tukagombana sana wakagoma kurudisha hela yangu. Nikaondoka usiku huo huo nikaanza kutembea kwa mguu barabarani sijui hata naenda wapi. Ndo nikakutana na bodaboda mwingine nikamwelezea tatizo langu akaniambia ngoja nikupeleke Guest nzuri. Akanipeleka
Suma Lodge.
Aisee nilifurahi sana kwa mambo niliyoyakuta
Suma Lodge. Bei poa (ilikuwa Tshs. 15,000/- tu, chumba kisafi na maji ya moto ya kwenye shower. Halafu asubuhi unapewa na chai ya watu wawili ya maziwa, mkate mmoja mzima wa silesi, mayai ya kukaanga, na unakaa kwenye kibaraza fulani kizuri unakunywa chai huku unapigwa na upepo.
Kwa nje inaonekana namna hii
View attachment 1537669
Na hapo ndo kibarazani asubuhi ukiwa unakunywa chai inapendeza sana
View attachment 1537672