Siongozi Genge la wasaka URAIS - Mbowe

Siongozi Genge la wasaka URAIS - Mbowe

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/298724-kura-ya-maoni-zitto-vs-dr-slaa-23.html#post4413384

Duh Mkuu Molemo wewe ndiye sponsor wa hii kura ya maoni? Wekeni basi kura ya maoni kati ya Mbowe na Zitto na kati ya Mbowe na Dr. Slaa.
 
Last edited by a moderator:
Amewajibu vyema wanao hangaika usiku na mchana kuwachonganisha viongozi wa cdm kwa suala la urais!
 
Mbowe ni puppet anasubiri baba mkwe ampe mwongozo ndio atamke, Zitto ni jeshi la mtu mmoja hawamuwezi mwaka huu lazima kamasi na jasho la pua liwatoke.
 
Mbowe ni puppet anasubiri baba mkwe ampe mwongozo ndio atamke, Zitto ni jeshi la mtu mmoja hawamuwezi mwaka huu lazima kamasi na jasho la pua liwatoke.

Maabdishi yako yanaonyesha upeo wako wa kufikiri.Unatia huruma...
 
Badala ya kukaa kwenye vikao vyao na kushauriana nini cha kusema wanakuja kwenye vyombo vya habari na kuleta mipasho. Hii ni wazi kabisa zitto anajibiwa hapa.

kwa nini sio shibuda?????
 
Teh teh teh!na vipi kuhusu agenda yake ya siri yakumpiku slaa kugombea urais 2015?wakati slaa akijua mbowe anamsapoti kumbe jamaa nae anajipanga kumzunguka!kiongozi wa mkakati huo akiwa lema eti kwakuamini kwamba 2015 wananchi watachagua chama na sio mtu.mnajidanganya!japo namuamini mbowe kwa 15%,slaa 1.5% , kamanda zitto 99.999% ambapo kwa mathematisians kama mimi if you convert that percentage u get 100%.zitto tunakuamini kamanda utaondoa ghilba ya ukuskazini chadema.teh teh teh mbowe amchezea rafu slaa,siasa bwana!
15% + 1.5%= 16.5%
100-16.5%=83.5%( 86%)
hesabu ni janga la kitaifa.......
 
badly hulijui ulisemalo na wala humjui tuntemeke zaidi ya kuijuwa hiyo id tu, mtu ambaye anamiliki id 16 hapa jf kwa ajili ya kueneza chuki na uchochezi unataka kunishawishi kwamba ana hoja gani? Kama ungekuwa unamfahamu huyu ni kiongozi mwandamizi wa chadema makao makuu ungebaki mdomo wazi na usingethubutu kuandika ulichoandika, hapa tunatunza tu ile kanuni ya jf ya name calling.

natamani sana kumjua huyu jamaa jilipue tu mkuu utujuze au nipm.
 
Matunda ya M4C tumeyaona na hata chama cha mabwepande wameyaona na yanawatesa sasa.
 
Reading between the lines, naona hapa anayepashwa hii mipasho ni Zito Kabwe....Chadema wanaanza kutumia mafuta yao kujikaanga. My take, it was unwise for Mbowe to make such statement for it cements the perception kwamba kuna mgogoro mkubwa Chadema.

Ni namna unavyoiangalia hoja, unaweza ukatoka na mawazo mengi ingawa ujumbe mahususi ni Focus ya chama sasa hivi ni kuwaunganisha wananchi.....Sio viongozi na wabunge wote wa CDM wanapiga M4C cuz kuna majukumu mengine pia ya majimboni na kitaifa na mengineyo mengi ambayo lazima yasimamiwe
 
Duh Mkuu Molemo wewe ndiye sponsor wa hii kura ya maoni? Wekeni basi kura ya maoni kati ya Mbowe na Zitto na kati ya Mbowe na Dr. Slaa.

Mkuu Kimbunga,
Kamanda Mbowe ameshasema kamwe asihusishwe na mambo ya Urais kwa sasa.Hataki kuingia kwenye historia ya kuwagawa wanachama kwa uroho wa madaraka.
Kukujibu kuhusu kura ya maoni inayoendelea hapa JF nadhani aliyeweka amewaweka Dr Slaa na Zitto kwa sababu wana-CDM wanamheshimu Dr Slaa kama shujaa na "RAIS" wao huku Zitto akiwa amewekwa kutokana na tamaa yake ya Urais ambayo kila mmoja anaijua.
 
Last edited by a moderator:
Hata mimi naamini Uenyekiti wa Mbowe CDM ni mpango wa Mungu kuona Ukombozi wetu Watanzania unapatikana. Laiti kama yale Mapandikizi ndio yangepata Uenyekiti kwa pesa ya akina Rostam CDM saa hizi ingekuwa historia.

Nimekuwa nikibishana na watu waliokuwa wakiunganisha Mbowe na ukaribu wake na Familia ya Mtei kuliko uwezo wake binafsi.Mtei alifanya maamuzi ya kama mfanya biashara.Unapoanza biashara unahitaji dedicated people,smart na wasio na njaa za kugombea mafanikio kidogo yanayopatikana njiani.Mbowe wanamjua wapiga Kura wake wa Hai.Huwa ni mtu mwenye msimamo, anaheshimu watu sana, ni jasiri hakuna kipimo.Huwa ni mtu apendaye akitoa msaada ufanye kazi husika.Waliowahi kwepesha wanamjua , naona hata wapenda longo longo wanatamani sana aitwe dictator.

Mbowe amepata majaribu mengi ila hajapoteza integrity yake.Chagangamoto nyingi kama za kuvamiwa na polisi, ulinzi wa Kura etc. Kuna mazingira unaona kabisa angewekwa "mzee wa Liwalo na Liwe".Nadhani tungekuwa sasa hivi kama Syria.Kuna maeneo unaweza ona kabisa kuwa CCM wanapoteza akili na ku push to the limit vurugu zianze,tena vurugu ambazo zikianza kuzimika ni utawala kuondoka.Ila mbowe anameza uamuzi mgumu wa kukabiliana na wanachama wanaotaka atoe ruhusa tuu.

Ukitaka jua Mbowe na timu nzima ya CDM ni wachapa kazi ,angalia uchaguzi uliopita,hawa jamaa walikuwa wakipigana majimbo kadhaa kwa muda huo kuhakikisha kura haziibwi.Jimbo lake la Hai, Arusha,Moshi majimbo kadhaa, wakiwa na Mzee Ndesa.
 
Hii nchi ni laini kama maini "Joshua Nassari"

teh teh.... hata ukiwauliza wawekezaji watasema hivyohiyo.Unapata leseni moja,unaishia msituni.hawakukumbuki tena.Labda uwe unafanya kazi wanazopenda chukulia sifa.Nayo pia huwa wanapropose misamaha yenye .....kwanini isiwe laini.Ila ni ngumu kwa raia wa kawaida
 
Nimekuwa nikibishana na watu waliokuwa wakiunganisha Mbowe na ukaribu wake na Familia ya Mtei kuliko uwezo wake binafsi.Mtei alifanya maamuzi ya kama mfanya biashara.Unapoanza biashara unahitaji dedicated people,smart na wasio na njaa za kugombea mafanikio kidogo yanayopatikana njiani.Mbowe wanamjua wapiga Kura wake wa Hai.Huwa ni mtu mwenye msimamo, anaheshimu watu sana, ni jasiri hakuna kipimo.Huwa ni mtu apendaye akitoa msaada ufanye kazi husika.Waliowahi kwepesha wanamjua , naona hata wapenda longo longo wanatamani sana aitwe dictator.

Mbowe amepata majaribu mengi ila hajapoteza integrity yake.Chagangamoto nyingi kama za kuvamiwa na polisi, ulinzi wa Kura etc. Kuna mazingira unaona kabisa angewekwa "mzee wa Liwalo na Liwe".Nadhani tungekuwa sasa hivi kama Syria.Kuna maeneo unaweza ona kabisa kuwa CCM wanapoteza akili na ku push to the limit vurugu zianze,tena vurugu ambazo zikianza kuzimika ni utawala kuondoka.Ila mbowe anameza uamuzi mgumu wa kukabiliana na wanachama wanaotaka atoe ruhusa tuu.

Ukitaka jua Mbowe na timu nzima ya CDM ni wachapa kazi ,angalia uchaguzi uliopita,hawa jamaa walikuwa wakipigana majimbo kadhaa kwa muda huo kuhakikisha kura haziibwi.Jimbo lake la Hai, Arusha,Moshi majimbo kadhaa, wakiwa na Mzee Ndesa.

Nakushukuru kwa mchango wako mkuu..!
 
ZITTO KASHAANZA TAYARI...... Wengine wapo kimya.. Hii inaonyesha jinsi gani anatamaa kama za kikwete alivyokuwa anataka urais
 
Back
Top Bottom