Sangarara
JF-Expert Member
- Sep 29, 2011
- 13,104
- 5,665
Wakati nakubaliana nawe kwa 70% sidhani ni busara kutatua mgogoro wa mbio za urais kupitia magazeti. Sitaki kuamini kwamba busara za Mbowe ni kutumia gazeti kuwapelekea vijembe viongozi wenzake na kama amefikia hatua hiyo nashawishika kuamini kwamba njia za kawaida na zabusara zimegonga mwamba na kwamba the crisis is full blown!!
Hakuna kijembe pale, AMETOA AUTHORITATIVE STATEMENT, Labda itaonekana kama ni kijembe kutokana na kauli nyepesi kama za wauza kahawa tulizozizoea kutoka kwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaji, DR, Kanali ,Dhaifu Jakaya Mrisho Kikwete.
Mbowe hajalalamika lalamika na leo ametudhibitishia kwamba ukimya wake haukumaanisha kukwepa kirusi cha migogoro, hakuhairisha wala kusogeza mbele tatizo ili lije litatuliwe na wengine, au lijimalize lenyewe, amepiga ngumi ya kichwa, mliokuwa na ndugu kwenye hilo gari la urais nendeni mkatambue ndugu, hali za majeruhi sio nzuri, wameumizwa vubaya sana.