Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Juzi kati nilijikuta napatanisha ugomvi fulani wa mtu na demu (sijui mchumba?) wake. Case ilikuwa mwanaume analalamika kuwa kila ikishafika usiku wa saa nne(hawaishi pamoja), sim ya demu inakuwa bize sana. Analalamika pia kuwa wakiwa pamoja mara zote, ama dem anazima simu au anaweka silent bila vibration, na sio simu zote zinapokelewa au msg zote zinajibiwa. Mara kadhaa jamaa anasema kuwa akiwa anachat na dem kwenye simu, sometimes anatumiwa wrong msgs kutoka kwa huyo dem wake ambazo akiziangalia maudhui yake yake zinaashiria wazi kuwa zilikuwa zinaenda kwa mwanaume mwingine na zina harufu ya mapenzi. Kikubwa zaidi ni kuwa jamaa anasema akimshtukiza dem wakakutana, dem hampi simu hadi adelete msg zote, na zipo namba nyingi kasev bila kuandika jina kwenye sim yake. Kutokana na ushahidi huo wa kimazingira, jamaa anaona kabisa uaminifu kwa dem wake haupo.
Hata hivyo kwa upande wa dem yeye anadai kuwa ni kwel sim yake inakuwaga bize usiku kwani anamwazimaga dada yake aongee kama hana vocha. Anakubali pia kuwa anazimaga sim akiwa na jamaa yake kwa sababu hapendi usumbufu toka kwa mashosti na wafanyakazi wenzake. Kiufupi ni kuwa malalamiko yote ya jamaa dem anakubali lakini anayapangua kwa kutoa reasons fulani.
Tulijadili mgogoro huo, na japo hakukuwa na ushahidi kuwa dem anamcheat jamaa, lakini nililazimika kumshauri dem kuwa sio tu lazima uaminifu uwepo, bali unatakiwa kuonekana upo. Asikubali kujenga mazingira tatanishi kwa kuwa tu ana kisingizio na haachi ushahidi.
Yapo mambo ambayo tusipoyahandle vizuri hata kama sio kwa nia mbaya yanaweza kuleta matatizo katika ndoa/mahusiano.
Kuchat na simu, Kupokea simu unapopigiwa, jinsi unavyoongea na simu, muda wa kurudi nyumbani, marafiki zako nk, ni mambo ambayo yanaweza kujenga mazingira ya kutokuaminiwa.
Kwangu mi nasema, "ni bora usiwe mwaminifu ukaonekana mwaminifu, kuliko kuwa mwaminifu lakini huonekani mwaminifu"...
Take care.... AIDS is there...
Hata hivyo kwa upande wa dem yeye anadai kuwa ni kwel sim yake inakuwaga bize usiku kwani anamwazimaga dada yake aongee kama hana vocha. Anakubali pia kuwa anazimaga sim akiwa na jamaa yake kwa sababu hapendi usumbufu toka kwa mashosti na wafanyakazi wenzake. Kiufupi ni kuwa malalamiko yote ya jamaa dem anakubali lakini anayapangua kwa kutoa reasons fulani.
Tulijadili mgogoro huo, na japo hakukuwa na ushahidi kuwa dem anamcheat jamaa, lakini nililazimika kumshauri dem kuwa sio tu lazima uaminifu uwepo, bali unatakiwa kuonekana upo. Asikubali kujenga mazingira tatanishi kwa kuwa tu ana kisingizio na haachi ushahidi.
Yapo mambo ambayo tusipoyahandle vizuri hata kama sio kwa nia mbaya yanaweza kuleta matatizo katika ndoa/mahusiano.
Kuchat na simu, Kupokea simu unapopigiwa, jinsi unavyoongea na simu, muda wa kurudi nyumbani, marafiki zako nk, ni mambo ambayo yanaweza kujenga mazingira ya kutokuaminiwa.
Kwangu mi nasema, "ni bora usiwe mwaminifu ukaonekana mwaminifu, kuliko kuwa mwaminifu lakini huonekani mwaminifu"...
Take care.... AIDS is there...