Mafanikio ya Mtu yako katika Uhaminifu

Mafanikio ya Mtu yako katika Uhaminifu

Mwl Mwakujonga

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2023
Posts
356
Reaction score
707
Leo nilipata nilipata nafasi ya kutafakari habari kutoka Njombe kutoka katika mitandao ya kijamii

Mkuu wa Mkoa wa Njombe katika ujumbe ambao alikuwa anatoa alilielezea kisa cha kijana mmoja ambaye alipewa kazi ya kukusanya maparachichi kutoka kqa wakulima na mfanyabiashara wakiasia.

Mfanyabiashara huyo alimpa mtaji wa kiasi cha Tshs 100 Milioni kwa ajili ya kuanza kazi ya kukusanya maparachichi kijana huyo mara baada ya kupewa mtaji huo badala ya kukusanya parachichi alipotea na fedha za watu na hakuna alichofanya na pesa za watu.

Habari hiyo ilinishikitisha sana, kutokana na jinsi mtu anavyoweza kupoteza kesho yake kaa tamaa ya leo.

Mungu akitaka kukutoa kiwango kimoja kwenda atakuingiza kwenye mtihani na miongoni mwa mitihani ambayo Mungu anatoa kwa watu wake ni mtihani wa uaminifu

Unaposoma habari za Daniel katika kitabu cha Daniel, Daniel alifanikiwa kuwa kiongozi katika nchi ya ugeni sio kwa sababu alikuwa na akili sana kuliko wengine hapana Daniel aliwazidi wenzake kitu kimoja tu ambacho ni uaminifu

Mfalme alifanya tathimini ya utendaji kazi wa watumishi wake na akabaini kwamba hakuna mwaminifu kama
Daniel katika kazi watumishi wake akampandisha cheo.

Basi Danielii huyo alipata sifa kuliko wakubwa na maliwali, kwa kuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaazimu kumweka juu ya ufalme wote.

Basi mawaziri na maamiri wakatafuta sana kupata sababu za kumshitaki Danielii kwa habari za mambo ya ufalme; lakini hawakuweza kuona sababu wala kosa; kwa maana alikuwa mwaminifu, wala halikuonekana kosa wala hatia ndani yake. Danieli 6:4_4.

Umesoma habari za Yusufu mwana wa Yakobo, Yusufu kilichomsaidia kuwa Waziri Mkuu katika nchi ya Misri ni uaminifu wake

Yusufu wakati anafanya kazi kwa Potifa alikutana na mtihani wa uaminifu juu ya mke wa potifa, kijana mwingine angeona kuwa ndio fursa ya kufanikiwa kwa kutembea na mke wa bosi wake, lakini Yusufu akaona huu ni mtengo kutoka kwa Mungu aksema maneno aya

Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu? Mwanzo 39:9

Yusufu alimwabia yule mama sijui kama alimwelewa? yule mama aliona kwakuwa wako wawili hakuna mtu atakaye toa siri kwa mumewe, lakini Yusufu aliona wako watatu ndio maana akasema nifanyaje ubaya huu mkubwa ni mkose Mungu?

Je unapokuwa pekee yako au umepewa fedha utakuwa mwaminufu au utahamua kupotea na fedha za watu

Mtu yoyote ambaye sio mwaminifu ni mtu ambaye hajui kesho yake, Yusufu akiwa kijana mdogo aliota ndoto ya kwamba hiko siku hatakuwa waziri mkuu na ndoto hiyo hakuiacha

Tunapokuwa watoto kila mmoja anakuwa na ndoto yake na zingine tunapewa na watu , unasikia huyu mtoto atakuwa mtumishi wa Mungu au huyu mtoto atakuwa mfanyabiashara mkubwa

Zile ndoto ambazo tunakuwa nazo utotoni wengi hatuzifati na tunaingia katika vishawishi vya shetani

Mungu pekee ndiye aliyekupangia maisha bora na ya mafanikio pekee na sio shetani na kazi ya shetani ni kukutengenezea mazingira ili umkose Mungu na Mungu asikusaidie

Yule kijana wa parachichi alipata kazi ya kubadirisha maisha yake , inawezekana kila siku alikuwa anamwomba Mungu amsaidie kuwa na kipato cha uhakika cha kubadirisha maisha yake na familia yake na Mungu ni mwaminifu akamleta mfanyabishara wa kumsaidia lakini kutokana na tamaa kijana akapoteza baraka zake

Habari kama hizi sio mara ya kwanza kuziskia ziko nyingi mtu anapewa duka kufanya kazi ya kuuza duka la mtu badala ya kufanya kazi kwa uhaminifu unakuwa wakwanza kumwibia na kupelekea mweye duka kufirisika au kushindwa kuendelea na biashara

Unaposhindwa kuwa mwaminifu kwa mali za watu Mungu hawezi kukupa ya kwako

Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.Luka 19:17

Uaminifu unajengwa , uaminifu sio kitu kinashuka kutoka mbinguni hapana uaminifu ni tabia ambayo inajengwa, ili uwe mwanifu kwa vitu vikubwa kuwa mwaminifu katika kidogo

Umepewa kazi na mtu fanya kazi kwa uaminifu hata kama malipo ni madogo

Kuna katabia kwa watu kutumia kigezo kwa kuwa kazi ina malipo madogo basi ni lazima nisiwe mwaminifu hapana kama unaona malipo ni madogo omba kuongezewa, kama haujapata tafuta sehemu nyingine

Na mara nyingi kazi ambayo inakuwa na kipato kidogo inakuwa na ushawishi sana na inawezekana ayo mazingira ya kazi yanaweza kuwa ni sehemu ya mwajiri kutafuta mtu mwaminifu kwa ajili ya kumpa majukumu makubwa zaidi ukashidwa huo mtihani kwa tamaa ndogo

Siku zote kumbuka neno hili

Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.

Luka 16:10

Tengeneza uhaminifu katika vitu vidogo na makubwa yatakuja kwako, Yusufu angefeli mtihani wa uhaminifu leo hii tusingekuwa na habari ya Yusufu kama waziri mkuu kwa sababu alishinda

Popote unapoaminiwa kufanya kazi iwe kazi ya kumtumikia Mungu au kazi ya kaisari hakikisha unafanya kazi kama unafanya kwa Bwana

Lo lote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo, kama kwa Bwana, wala si kwa wanadamu. Wakolosai 3:23
 
Ni rahisi sana mhubiri au mtu mwenye hela kuketi kwenye kochi na kuhubiri uaminifu. Lakini ukweli mchungu ni kwamba underpayment breeds corruption.

Unakuta mtu anapewa duka la mamilioni lakini mshahara wake ni laki moja na nusu, huku ana mke na watoto na kodi ya nyumba inamkabili. Utu unashindwana na njaa wakati mwingine. Kama waajiri wanataka uaminifu wa 100%, lazima walipe mishahara inayokidhi mahitaji ya binadamu.
 
Basi wale waliofanya kwa wahindi na matajiri wangekuwa matajiri.

Acha kuwa mjinga wa mwisho.
 
Ni rahisi sana mhubiri au mtu mwenye hela kuketi kwenye kochi na kuhubiri uaminifu. Lakini ukweli mchungu ni kwamba underpayment breeds corruption.

Unakuta mtu anapewa duka la mamilioni lakini mshahara wake ni laki moja na nusu, huku ana mke na watoto na kodi ya nyumba inamkabili. Utu unashindwana na njaa wakati mwingine. Kama waajiri wanataka uaminifu wa 100%, lazima walipe mishahara inayokidhi mahitaji ya binadamu.
Kabla ya kuanza hiyo kazi hakujua mshahara wake utakua kiasi gani?

Acha kutafuta justification ya kutetea tabia ya wizi,

Wewe mtu akikuibia kisha akasema kakuibia coz ana njaa,utaona ni sawa? Hakuna justification ya kuhalalisha wizi.
 
Kabla ya kuanza hiyo kazi hakujua mshahara wake utakua kiasi gani?

Acha kutafuta justification ya kutetea tabia ya wizi,

Wewe mtu akikuibia kisha akasema kakuibia coz ana njaa,utaona ni sawa? Hakuna justification ya kuhalalisha wizi.
Usininukuu vibaya, sijatetea wala siyo lengo langu kuhalalisha wizi kama unavyodai.

Tunachojadili hapa sio uhalali wa wizi, tunajadili human behavior na mazingira yanayochochea uhalifu. Kujua mshahara kabla ya kazi hakumzuii mtu kubadilika akiona mamilioni mbele yake. Tamaa haitaji justification, inahitaji udhibiti na mifumo imara.
 
Usininukuu vibaya, sijatetea wala siyo lengo langu kuhalalisha wizi kama unavyodai.
Wabongo bhana,hua mnapenda sana kukimbilia kweny kujitetea kwa kusema "Ulininukuu vibaya" umetetea wizi,wala usikatae hilo,

Hakuna justification ya kuhalalisha wizi,mshahara hautoshi kwani ulilazimishwa kuifanya hiyo kazi? Wizi ni wizi tu.
Tunachojadili hapa sio uhalali wa wizi, tunajadili human behavior na mazingira yanayochochea uhalifu.
Mwizi ni mwizi tu,wizi ni tabia,wangapi wapo maofisini na mishahara mikubwa lakini wanaiba? Mwizi hata akiwa na milioni,akiiona elfu 10 ataiiba tu coz wizi ni tabia yake,
Kujua mshahara kabla ya kazi hakumzuii mtu kubadilika akiona mamilioni mbele yake.
Ndio huo huo wizi ninao usema sasa,
Tamaa haitaji justification, inahitaji udhibiti na mifumo imara.
Hiyo sio tamaa bali ni tabia ya mtu,sio kila mtu atakua na huo wizi wa kijinga,kwani hakuna watu waaminifu? Kwahiyo ukiona mamilioni ya watu ndio uwaze kuiba?
 
Ni rahisi sana mhubiri au mtu mwenye hela kuketi kwenye kochi na kuhubiri uaminifu. Lakini ukweli mchungu ni kwamba underpayment breeds corruption.

Unakuta mtu anapewa duka la mamilioni lakini mshahara wake ni laki moja na nusu, huku ana mke na watoto na kodi ya nyumba inamkabili. Utu unashindwana na njaa wakati mwingine. Kama waajiri wanataka uaminifu wa 100%, lazima walipe mishahara inayokidhi mahitaji ya binadamu.
Kuna watu wanalipwa mamilioni katika nchii hii na bado ni wezi kwa hiyi tabua ya uhalifu aina kiwango cha fedha , kadri fedha inapoongezeka na matamanio yanaongezeka , tujifunze kuishi katika vipato vyetu
 
Wabongo bhana,hua mnapenda sana kukimbilia kweny kujitetea kwa kusema "Ulininukuu vibaya" umetetea wizi,wala usikatae hilo,

Hakuna justification ya kuhalalisha wizi,mshahara hautoshi kwani ulilazimishwa kuifanya hiyo kazi? Wizi ni wizi tu.

Mwizi ni mwizi tu,wizi ni tabia,wangapi wapo maofisini na mishahara mikubwa lakini wanaiba? Mwizi hata akiwa na milioni,akiiona elfu 10 ataiiba tu coz wizi ni tabia yake,

Ndio huo huo wizi ninao usema sasa,

Hiyo sio tamaa bali ni tabia ya mtu,sio kila mtu atakua na huo wizi wa kijinga,kwani hakuna watu waaminifu? Kwahiyo ukiona mamilioni ya watu ndio uwaze kuiba?
Nadhani hatutoelewana hapa, sina cha kuongeza.
 
Kuna watu wanalipwa mamilioni katika nchii hii na bado ni wezi kwa hiyi tabua ya uhalifu aina kiwango cha fedha , kadri fedha inapoongezeka na matamanio yanaongezeka , tujifunze kuishi katika vipato vyetu
Uko sahihi, unatakiwa ujue pia huwezi kujua roho ya mtu kwa kumuangalia usoni. Huwezi kujua nani ameridhika na nani ni mlafi mpaka umpe hela.
 
Uaminifu sio kwa ajili ya mtu mmoja, leo hii waafrica wengi tunakwenda nchi za watu ila ukijitambulisha unatoka nchi flani unapata kazi kwa sababu wanajua watu wa nchi hiyo ni waaminifu ila ukitaja nchi nyingine ambayo watu wake sio waaminifu unakosa kazi.

Tuwe waaminifu sio kwa ajili yetu pekee na vizazi vijavyo, mfano Mwl Nyerere kutokana na uaminifu w Mwalimu wototo wake wanapata sifa kutoka na uaminifu wa baba yake

Kuna watu wanapata kazi sio kwamba wanajua kazi hapana ila sifa za wazazi wao kwamba walikuwa ni watu waaminifu wanapata upendeleo kwa hiyo unapopoteza uaminifu leo sio kwa ajili yako pekee ni pamoja na watoto wako

Ulishawai kusikia kuna watu wakienda kuomba kazi hawatumia majina ya wazazi wao au hawataki kujitambulisha kwa majina ya wazazi wao, ni kwa sababu wazazi wao walikosa uaminifu


Uaminifu wa Yusufu ulimfungulia mlango wa ndugu zake wote kupata kaI kwa faraoa kwa sababu ya Yusufu

Hata kwenye mausiano pia ndoa nyingi zinakufa kwa kukosa uaminifu, kwa hiyo tunatakiwa kuwa waaminifu katika kila eneo
 
Nadhani hatutoelewana hapa, sina cha kuongeza.
Sio hatutoelewana,mimi nimeongea ukweli ulivyo,sema wewe ndio hutaki kuelewa ili usimamie ulichokisema ambacho wewe unaona kua upo sahihi,

Mtu mwizi wala hahitaji mpaka aone mamilioni,hata elfu 10 tu ataiiba.
 
Wabongo bhana,hua mnapenda sana kukimbilia kweny kujitetea kwa kusema "Ulininukuu vibaya" umetetea wizi,wala usikatae hilo,

Hakuna justification ya kuhalalisha wizi,mshahara hautoshi kwani ulilazimishwa kuifanya hiyo kazi? Wizi ni wizi tu.

Mwizi ni mwizi tu,wizi ni tabia,wangapi wapo maofisini na mishahara mikubwa lakini wanaiba? Mwizi hata akiwa na milioni,akiiona elfu 10 ataiiba tu coz wizi ni tabia yake,

Ndio huo huo wizi ninao usema sasa,

Hiyo sio tamaa bali ni tabia ya mtu,sio kila mtu atakua na huo wizi wa kijinga,kwani hakuna watu waaminifu? Kwahiyo ukiona mamilioni ya watu ndio uwaze kuiba?
Nakuunga mkono. Kuna baadhi ya watu huko TPA, TRA, Ngorongoro wanalipwa vizuri ila ndo wezi kupindukia. Wizi ni tabia ya mtu.
 
Andiko zuri but imagine Potiphar's wife trying to seduce me...😀😫!!!... uaminifu wangu ungekuwa shakani
 
Sio hatutoelewana,mimi nimeongea ukweli ulivyo,sema wewe ndio hutaki kuelewa ili usimamie ulichokisema ambacho wewe unaona kua upo sahihi,

Mtu mwizi wala hahitaji mpaka aone mamilioni,hata elfu 10 tu ataiiba.
Nimekuelewa sana, hoja yangu ilikuwa ni kwamba underpayment breeds corruption muda mwingine kwa experience yangu, na hoja yangu haikuwa msaafu bali ni mtazamo wangu Mkuu.

Kwahiyo kunikosoa ni sawa kabisa na ndiyo maana ya kufanya mjadala.
 
Leo nilipata nilipata nafasi ya kutafakari habari kutoka Njombe kutoka katika mitandao ya kijamii

Mkuu wa Mkoa wa Njombe katika ujumbe ambao alikuwa anatoa alilielezea kisa cha kijana mmoja ambaye alipewa kazi ya kukusanya maparachichi kutoka kqa wakulima na mfanyabiashara wakiasia.

Mfanyabiashara huyo alimpa mtaji wa kiasi cha Tshs 100 Milioni kwa ajili ya kuanza kazi ya kukusanya maparachichi kijana huyo mara baada ya kupewa mtaji huo badala ya kukusanya parachichi alipotea na fedha za watu na hakuna alichofanya na pesa za watu.

Habari hiyo ilinishikitisha sana, kutokana na jinsi mtu anavyoweza kupoteza kesho yake kaa tamaa ya leo.

Mungu akitaka kukutoa kiwango kimoja kwenda atakuingiza kwenye mtihani na miongoni mwa mitihani ambayo Mungu anatoa kwa watu wake ni mtihani wa uaminifu

Unaposoma habari za Daniel katika kitabu cha Daniel, Daniel alifanikiwa kuwa kiongozi katika nchi ya ugeni sio kwa sababu alikuwa na akili sana kuliko wengine hapana Daniel aliwazidi wenzake kitu kimoja tu ambacho ni uaminifu

Mfalme alifanya tathimini ya utendaji kazi wa watumishi wake na akabaini kwamba hakuna mwaminifu kama
Daniel katika kazi watumishi wake akampandisha cheo.

Basi Danielii huyo alipata sifa kuliko wakubwa na maliwali, kwa kuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaazimu kumweka juu ya ufalme wote.

Basi mawaziri na maamiri wakatafuta sana kupata sababu za kumshitaki Danielii kwa habari za mambo ya ufalme; lakini hawakuweza kuona sababu wala kosa; kwa maana alikuwa mwaminifu, wala halikuonekana kosa wala hatia ndani yake. Danieli 6:4_4.

Umesoma habari za Yusufu mwana wa Yakobo, Yusufu kilichomsaidia kuwa Waziri Mkuu katika nchi ya Misri ni uaminifu wake

Yusufu wakati anafanya kazi kwa Potifa alikutana na mtihani wa uaminifu juu ya mke wa potifa, kijana mwingine angeona kuwa ndio fursa ya kufanikiwa kwa kutembea na mke wa bosi wake, lakini Yusufu akaona huu ni mtengo kutoka kwa Mungu aksema maneno aya

Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu? Mwanzo 39:9

Yusufu alimwabia yule mama sijui kama alimwelewa? yule mama aliona kwakuwa wako wawili hakuna mtu atakaye toa siri kwa mumewe, lakini Yusufu aliona wako watatu ndio maana akasema nifanyaje ubaya huu mkubwa ni mkose Mungu?

Je unapokuwa pekee yako au umepewa fedha utakuwa mwaminufu au utahamua kupotea na fedha za watu

Mtu yoyote ambaye sio mwaminifu ni mtu ambaye hajui kesho yake, Yusufu akiwa kijana mdogo aliota ndoto ya kwamba hiko siku hatakuwa waziri mkuu na ndoto hiyo hakuiacha

Tunapokuwa watoto kila mmoja anakuwa na ndoto yake na zingine tunapewa na watu , unasikia huyu mtoto atakuwa mtumishi wa Mungu au huyu mtoto atakuwa mfanyabiashara mkubwa

Zile ndoto ambazo tunakuwa nazo utotoni wengi hatuzifati na tunaingia katika vishawishi vya shetani

Mungu pekee ndiye aliyekupangia maisha bora na ya mafanikio pekee na sio shetani na kazi ya shetani ni kukutengenezea mazingira ili umkose Mungu na Mungu asikusaidie

Yule kijana wa parachichi alipata kazi ya kubadirisha maisha yake , inawezekana kila siku alikuwa anamwomba Mungu amsaidie kuwa na kipato cha uhakika cha kubadirisha maisha yake na familia yake na Mungu ni mwaminifu akamleta mfanyabishara wa kumsaidia lakini kutokana na tamaa kijana akapoteza baraka zake

Habari kama hizi sio mara ya kwanza kuziskia ziko nyingi mtu anapewa duka kufanya kazi ya kuuza duka la mtu badala ya kufanya kazi kwa uhaminifu unakuwa wakwanza kumwibia na kupelekea mweye duka kufirisika au kushindwa kuendelea na biashara

Unaposhindwa kuwa mwaminifu kwa mali za watu Mungu hawezi kukupa ya kwako

Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.Luka 19:17

Uaminifu unajengwa , uaminifu sio kitu kinashuka kutoka mbinguni hapana uaminifu ni tabia ambayo inajengwa, ili uwe mwanifu kwa vitu vikubwa kuwa mwaminifu katika kidogo

Umepewa kazi na mtu fanya kazi kwa uaminifu hata kama malipo ni madogo

Kuna katabia kwa watu kutumia kigezo kwa kuwa kazi ina malipo madogo basi ni lazima nisiwe mwaminifu hapana kama unaona malipo ni madogo omba kuongezewa, kama haujapata tafuta sehemu nyingine

Na mara nyingi kazi ambayo inakuwa na kipato kidogo inakuwa na ushawishi sana na inawezekana ayo mazingira ya kazi yanaweza kuwa ni sehemu ya mwajiri kutafuta mtu mwaminifu kwa ajili ya kumpa majukumu makubwa zaidi ukashidwa huo mtihani kwa tamaa ndogo

Siku zote kumbuka neno hili

Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia.

Luka 16:10

Tengeneza uhaminifu katika vitu vidogo na makubwa yatakuja kwako, Yusufu angefeli mtihani wa uhaminifu leo hii tusingekuwa na habari ya Yusufu kama waziri mkuu kwa sababu alishinda

Popote unapoaminiwa kufanya kazi iwe kazi ya kumtumikia Mungu au kazi ya kaisari hakikisha unafanya kazi kama unafanya kwa Bwana

Lo lote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo, kama kwa Bwana, wala si kwa wanadamu. Wakolosai 3:23
Mkuu ni UAMINIFU
 
Back
Top Bottom