'Single mothers' wana tabia ya kubadili gia angani

'Single mothers' wana tabia ya kubadili gia angani

Mkuu kama hakushirikishi hayo hapo kuna walakini....hapo hakuna mapenzi tena

Nishawahi kuwa a mmoja yalikua kama haya yako mkuu ndo maana nakushauri usepe kabla ya kuumizwa
Mkuu nitafanya hivyo. Hakuna jinsi.
 
Wakuu kwema?

Huu uzi ninauandika huku nikiwa na maumivu makali ya nafsi yaliyosababishwa na (single mother) Miezi kama 7 iliyopita kuna (single mother) nilimpenda na nikajua sasa hapa nimefika mwisho wa safari yangu ya kusaka mke. Kiukweli mwanzoni hata yeye alikuwa haamini kama kweli nimempenda na nia ya kumuoa.

Alifurahi na kunionyesha upendo. Kama mwezi mmoja hivi umepita ndo kaanza kutia supu nazi. Mawasiliano yamekuwa shida na pia kanipa taarifa rasmi kwamba tuwe kwanza marafiki kabla ya kuoana maana hayupo sawa kisaikolojia kwa sasa. Nikashtuka na kujiuliza hii kuwa marafiki si ni sawa na kurudi mwanzo maana tulishafikia hatua ya kupanga tuoane lini?Kuna wazo linanijia kwamba labda jamaa aliyemzalisha karudisha majeshi. Nimemuuliza kakana na kudai ni mambo yake mengine tu.

Wakuu nionavyo mimi hawa (single mother) kuwa nao kimahusiano lolote laweza hasa kurudiana na jamaa yake wa mwanzo. Ukiwa na (single mother) jua suala la gia kubadilishwa angani sio geni.

Nishaurini huyu mwanamama nimvumilie hadi hapo atakapokuwa sawa kisaikolojia au nipite zangu hivi?
Sasa wewe umetuhumu na kuhukumu halafu unaomba ushauri? Ondoa hizo tuhuma kwanza na usihukumu halafu ndio ushauriwe. Ni vigumu kwa hali hiyo ukashauriwa na kukubali
 
Huu mstari una uhusiano wa karibu na sababu zinazopelekea baadhi ya wanawake kuwa single mothers;

Mithali 21:9
Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini, kuliko katika nyumba pana na mwanamke mgomvi.
 
Wewe ndio unampa kichwa mwenye mtoto a nashindwa kuendelea na family yake. Pia wewe nidhaifu unashindwa kuchukua fresh unavizia aliyejuruhiwa.

Kati ya michango ya JF iliyowahi nifurahisha huu dah naupa namba 1, kama umenigusa kiasi
 
Kwa jinsi wanaume wanavyoukandia usingle mother nashangaa kuona mabinti wanaendelea kujizalia tu kila kukicha. Kuna mdada mmoja nilitaka kumuoa miaka kama minne iliyopita akanikatalia kata kata eti hataki kuolewa bora ajizalie maana wanaume hawafai. Baada ya kuzalishwa last year ameanza kunitafuta ati ndo wakati wake muafaka wa kuolewa. Nilipiga chini nikamblock shenzy type ulipokuwa hujazaa unaniona sifai umezalishwa ndo unaniona wa maana. Wadada acheni kudanganyika hakuna mwanaume anapenda kuoa single mother ni bora kuoa mjane siyo single mother.
 
Mzazi mwenzake yuko mkoa wa mbali. Anamzungumzia mwenzake kama mtu ambaye mapenzi nae yalishaisha na hana mpango tena. Msimamo wake ni kuwa kuna mambo yake mengine yanamsibu.

Hujawajua wanawake bado wewe!
 
Kwa jinsi wanaume wanavyoukandia usingle mother nashangaa kuona mabinti wanaendelea kujizalia tu kila kukicha. Kuna mdada mmoja nilitaka kumuoa miaka kama minne iliyopita akanikatalia kata kata eti hataki kuolewa bora ajizalie maana wanaume hawafai. Baada ya kuzalishwa last year ameanza kunitafuta ati ndo wakati wake muafaka wa kuolewa. Nilipiga chini nikamblock shenzy type ulipokuwa hujazaa unaniona sifai umezalishwa ndo unaniona wa maana. Wadada acheni kudanganyika hakuna mwanaume anapenda kuoa single mother ni bora kuoa mjane siyo single mother.

Sanyingine sijui wanawake huwa tunawaza nn
 
Huyo Hana mapenzi na wewe anatafuta sababu ya kukuacha.! Na kaipata
 
Wakuu kwema?

Huu uzi ninauandika huku nikiwa na maumivu makali ya nafsi yaliyosababishwa na (single mother) Miezi kama 7 iliyopita kuna (single mother) nilimpenda na nikajua sasa hapa nimefika mwisho wa safari yangu ya kusaka mke. Kiukweli mwanzoni hata yeye alikuwa haamini kama kweli nimempenda na nia ya kumuoa.

Alifurahi na kunionyesha upendo. Kama mwezi mmoja hivi umepita ndo kaanza kutia supu nazi. Mawasiliano yamekuwa shida na pia kanipa taarifa rasmi kwamba tuwe kwanza marafiki kabla ya kuoana maana hayupo sawa kisaikolojia kwa sasa. Nikashtuka na kujiuliza hii kuwa marafiki si ni sawa na kurudi mwanzo maana tulishafikia hatua ya kupanga tuoane lini?Kuna wazo linanijia kwamba labda jamaa aliyemzalisha karudisha majeshi. Nimemuuliza kakana na kudai ni mambo yake mengine tu.

Wakuu nionavyo mimi hawa (single mother) kuwa nao kimahusiano lolote laweza hasa kurudiana na jamaa yake wa mwanzo. Ukiwa na (single mother) jua suala la gia kubadilishwa angani sio geni.

Nishaurini huyu mwanamama nimvumilie hadi hapo atakapokuwa sawa kisaikolojia au nipite zangu hivi?
Ndugu mi nakushauri ufanye uamuzi mgumu kabla hujamuweka ndani maana kwa hali hiyo lazima atakuwa na mtu tena.
 
Hao single mother wanakuwa wamezalishwa na nani? majina ya hao waliowazalisha wanaitwa vipi......unaweza kukuta anayekashifu SM mwenyewe ana wadada amewatelekeza na ......hayo yanayosemwa kuhusu kurudiana hata hao ambao hawakuwa na watoto waliwaacha kwenye mapipa wanaweza kuendeleza mahusiano....kama umeanzisha mahusiano na SM jiamini sio unakuwa na wasiwasi hata kushindwa kutimiza wajibu wako.....
 
Back
Top Bottom