Sina shaka na Tundu Lissu, nina shaka na Katiba ya chama chake

CHEF

JF-Expert Member
Nov 4, 2013
222
122
Ndugu wapendwa salaam, leo wakati nawaza nani wa kumpigia kura, pamoja na kuona TAL anaweza kuongoza nikiwa na maana ya kusimamia katiba na Sheria za nchi kuongoza kama Rais jambo ambalo ni udhaifu wa mgombea wa CCM JPM , wakati udhaifu wa TAL ni kwamba tusitegemee maendeleo makubwa ya kiuchumi kama anayoyafanya JPM tofauti na usawa katika sheria na katiba mpya jambo ambalo muhimu sana kwa kizazi hiki na kijacho.

Haya twende kwenye maada kuu ambayo jinsi katiba ya chadema inavyo kinzana kusimamia uchumi wa nchi,
Katiba ya Chadema inasema inaitikadi ya mrengo wa kati wakiwa na maana wao sio mabepari wala wajamaa.

1601036125307.png


Hivyo hivyo chadema wanasema wanaamini katika soko huru yaani FREE MARKET ECONOMY, kitu ambacho msingi wake ni ubepari (CAPITALIST), kwa hiyo CHADEMA wanataka kutupeleka kwenye ubepari?

1601037106163.png


Hili suala la ubepari limethibitishwa tena na TAL alipokuwa anasema serikali yake itabaki kuwa msimamizi tu wa masuala ya kiuchumi lakini uchumi wote utendeshwa na wananchi wenyewe, hapa akiwa na maana kutakuwa na free market economy ambayo itaendeshwa by demand and supply forces. Huu ni ubepari kabisa, hili suala kwa Tanzania yetu bado hatujafikia , yaani kama ndio CHADEMA wanategemea kuendesha uchumi hivi kutakuwa na athari zifuatazo:

1. Kutaongeza tofauti kubwa sana kati ya wasio nacho na wenye nacho (income gap)

2. Watanzania bado hawajaelimika vyakutosha kwa hiyo watauza ardhi kwa urahisi kwa wenye nacho na kubaki kuwa masikini daima

3. Maisha kubadilika kwa asiye ncho itakuwa ndoto

4. Kutokea kwa machafuko kama Afrika kusini maana wageni watashika uchumi wakati wenyeji wakiwa hohe hahe.


Kwa maelezo haya nafikiri CHADEMA wanatakiwa wakae na kuitafakari katiba yao , baada ya hapo waje waombe ridhaa ya kuongoza nchi.

CHADEMA bado hawajaijua nchi yao na aina ya wananchi wake, tafadhali , chonde, chonde chonde tunahitaji mabadiliko lakini sio kwa katiba hii ya chadema itatupeleka pabaya.
 
..mtoa mada inaelekea huna shaka na TL, na huna shaka na katiba ya chama chake.

..Nakushauri ubadilishe kichwa cha habari cha mada yako ili kifanane na hoja uliyojenga.
 
... acheni kunyanyasa wananchi; acheni kunyanyasa wafanyabiashara! Duniani kote mchangiaji mkuu wa pato la taifa na mwajiri mkuu ni sekta binafsi. Mnapoivuruga sekta binafsi haileweki mnataka nini kama sio kulivuruga taifa.
 
Acha upotoshaji!! Nani kakwambia kwenye free market economy kuna gape kubwa kati walio Nacho na wasio nacho?

Mbona kwenye mfumo wa sasa wa Ccm kuna tofauti kubwa sana kati ya walio Nacho na wasio nacho??? Hujui ndani ya Tanzania hii kuna watu wanakunywa maji ya tope??? Hujui ndani ya Tanzania hii kuna watu wanalala kwenye mabox kwenye masoko??? Hujui ndani ya Tanzania hii kuna watu hata kula yao ni tabu?

Free Market economy maana yake ni uchumi huru unaotoa fursa kwa kila mtu anayefanya kazi ya halali na anayejituma kweli kufanikiwa.

Ndani ya free market economy creativity yako tu inaweza kukutoa bila kutegemea serikali au taasisi zake. Ndani ya free market economy akili ni mtaji ambapo kitu kidogo tu kinaweza kumtajirisha mtu. Ndani ya free market economy sekta binafsi ndo kipaumbele Kwa iyo ajira ziko nyingi, biashara iko nyingi na mafanikio yako mengi.

Mtatoa sana nyuzi za kuichafua chadema na Sera zake lakini uzuri ni kuwa hamtafanikiwa!
 
Hiyo no katiba ya chama Chao wakishinda watakuwa na kula kiapo cha kulindakatiba ya nchi kwahiyo hoja yako. Itafakari na Kama Ni hivyo CCM imetutawala muda mrefu lakini hawajawahi kututawala na katiba yao
 
Tanzania ni nchi ya kibepari toka 1995 alipoingia Ben.
Na moja wa mabeberu nchi hii ni Jiwe na kampuni yake akina Sumaye,Lowassa,rostam,Mo dewji nk
 
Tanzania ni nchi ya kibepari toka 1995 alipoingia Ben.
Na moja wa mabeberu nchi hii ni Jiwe na kampuni yake akina Sumaye,Lowassa,rostam,Mo dewji nk
NAfikiri bado hujajua vizuri tofauti kati ya Socialism economy, Mixed economy & capitalist economy
 
Hiyo no katiba ya chama Chao wakishinda watakuwa na kula kiapo cha kulindakatiba ya nchi kwahiyo hoja yako. Itafakari na Kama Ni hivyo CCM imetutawala muda mrefu lakini hawajawahi kututawala na katiba yao
Kiongozi ataongoza kulingana na imani ya chama chake, imani ya chama chake ni kama dini katika siasa
 
Acha upotoshaji!! Nani kakwambia kwenye free market economy kuna gape kubwa kati walio Nacho na wasio nacho?

Mbona kwenye mfumo wa sasa wa Ccm kuna tofauti kubwa sana kati ya walio Nacho na wasio nacho??? Hujui ndani ya Tanzania hii kuna watu wanakunywa maji ya tope??? Hujui ndani ya Tanzania hii kuna watu wanalala kwenye mabox kwenye masoko??? Hujui ndani ya Tanzania hii kuna watu hata kula yao ni tabu?

Free Market economy maana yake ni uchumi huru unaotoa fursa kwa kila mtu anayefanya kazi ya halali na anayejituma kweli kufanikiwa.

Ndani ya free market economy creativity yako tu inaweza kukutoa bila kutegemea serikali au taasisi zake. Ndani ya free market economy akili ni mtaji ambapo kitu kidogo tu kinaweza kumtajirisha mtu. Ndani ya free market economy sekta binafsi ndo kipaumbele Kwa iyo ajira ziko nyingi, biashara iko nyingi na mafanikio yako mengi.

Mtatoa sana nyuzi za kuichafua chadema na Sera zake lakini uzuri ni kuwa hamtafanikiwa!
Nimeandika hoja nne, na hujaweza kujibu hata moja, angalia mfano Afrika kusini halafu uje na majibu
 
Hakuna,hakujawahi kuwa na haitatokea nchi ya kibepari kabisa duniani,kajifunze zaidi.
 
Ndugu wapendwa salaam, leo wakati nawaza nani wa kumpigia kura, pamoja na kuona TAL anaweza kuongoza nikiwa na maana ya kusimamia katiba na Sheria za nchi kuongoza kama Rais jambo ambalo ni udhaifu wa mgombea wa CCM JPM , wakati udhaifu wa TAL ni kwamba tusitegemee maendeleo makubwa ya kiuchumi kama anayoyafanya JPM tofauti na usawa katika sheria na katiba mpya jambo ambalo muhimu sana kwa kizazi hiki na kijacho.

Haya twende kwenye maada kuu ambayo jinsi katiba ya chadema inavyo kinzana kusimamia uchumi wa nchi,
Katiba ya Chadema inasema inaitikadi ya mrengo wa kati wakiwa na maana wao sio mabepari wala wajamaa.

View attachment 1580480

Hivyo hivyo chadema wanasema wanaamini katika soko huru yaani FREE MARKET ECONOMY, kitu ambacho msingi wake ni ubepari (CAPITALIST), kwa hiyo CHADEMA wanataka kutupeleka kwenye ubepari?

View attachment 1580490

Hili suala la ubepari limethibitishwa tena na TAL alipokuwa anasema serikali yake itabaki kuwa msimamizi tu wa masuala ya kiuchumi lakini uchumi wote utendeshwa na wananchi wenyewe, hapa akiwa na maana kutakuwa na free market economy ambayo itaendeshwa by demand and supply forces. Huu ni ubepari kabisa, hili suala kwa Tanzania yetu bado hatujafikia , yaani kama ndio CHADEMA wanategemea kuendesha uchumi hivi kutakuwa na athari zifuatazo:

1. Kutaongeza tofauti kubwa sana kati ya wasio nacho na wenye nacho (income gap)

2. Watanzania bado hawajaelimika vyakutosha kwa hiyo watauza ardhi kwa urahisi kwa wenye nacho na kubaki kuwa masikini daima

3. Maisha kubadilika kwa asiye ncho itakuwa ndoto

4. Kutokea kwa machafuko kama Afrika kusini maana wageni watashika uchumi wakati wenyeji wakiwa hohe hahe.


Kwa maelezo haya nafikiri CHADEMA wanatakiwa wakae na kuitafakari katiba yao , baada ya hapo waje waombe ridhaa ya kuongoza nchi.

CHADEMA bado hawajaijua nchi yao na aina ya wananchi wake, tafadhali , chonde, chonde chonde tunahitaji mabadiliko lakini sio kwa katiba hii ya chadema itatupeleka pabaya.
Enzi hizi watz sio wale wa kupewa ma tshet tena oversize na kofia.

Walio ongozwa kwa kuburuzwa. Tunshitaji kiongozi atakayewajali na kuuheshimu utu wa mabosi zake (wapiga kura).

Watanzania hawata mchagua mfalme asiyependa kukosolewa na waliomuajiri bali kupenda kukosolewa na waliomuajiri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom