Sina imani na Division 1.7 wanazopata wanafunzi siku hizi kidato cha nne

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Mar 29, 2012
10,213
22,277
Wakuu leo nipo kisomi zaidi kuongelea hili suala la kitaifa.

Wote ni mashahidi wa matokeo ya kidato cha nne mwaka 2020 yalivyosheheni division 1.7 karibu kila shule. St Francis Mbeya ilikuwa nazo nyingi sana. Kama ni za kweli na za haki nawapongeza NECTA, Waalimu, Wanafunzi, Wazazi na wote waliohusika kupatikana. Hakika ni matokeo ya kimbunga.

Ila mimi nina mashaka makubwa na matokeo hayo. Kwa tuliosoma miaka ya nyuma hadi mwanzoni mwa miaka ya 2000 mtakuwa mashahidi ilivyokuwa ngumu kupata Division One za 7,8 na 9. Sisi tuliziita one za digit. Ni wakali wachache walikuwa wakizipata. Matokeo yakitoka one zinakuwa nyingi ila za 7 ni chache mno. Kwa mfano Ilboru, Mzumbe na Kibaha zilikuwa zinatoa one nyingi mno ila hizo za 7 ilikuwa ngumu kuwepo nyingi.

Na waliokuwa wakizipata walikuwa ni wale magenius wa ukweli au wale ambao walikuwa na bidii ya kusoma karibu muda wote. Kuna majamaa walikimbiza kuanzia o-level hadi UDSM. Sisi wengine tulipiga tu One za kawaida. Wengi kuanzia one ya 12 hadi 17. Je, miaka ile wanafunzi hawakuwa na akili kama wa sasa? Hawakuwa na jitihada kuliko wa sasa?

Kwangu mimi inawezekana kweli zimepatikana kihalali. Pia nahisi zile tetesi za baraza "kupanua goli" ni za kweli. Kama kweli walipanua goli itakuwa jambo la kusikitisha mno. Ni kujidanganya. Mimi kwa leo nimepost tu wasiwasi wangu ila muda utatupa majibu sahihi kuhusu hawa watoto wetu.
 
Div. Kipindi cha maggu ziliwekwa kumfurahisha tu ila ukweli vijana ni watupu mno wengi ni wafuasi wa nyau fc (mbumbumbu)

Shule niliyosoma haijawahi kuwa na dv 1 zaidi ya 20 kwa mwaka mmoja ila chini ya maggu ilipiga 1 zaidi ya 40 tena wakiwa wamekaa likizo ya korona zaidi ya miezi 2 nikajua n katika kumfurahisha mwamba
 
unazungumza ukweli... Mimi sitaki kusema yangu ya mwaka 1999 lakini ilikuwa kazi kupata single digit.. Japo mi kusoma kwangu ilikuwa kawaida.. Na sio shule za kipaji maalum.

Elimu kipindi hiki naona ina siasa na ipo diluted Sana.

Ushauri:
  • Serikali iwajali waalimu..
  • Serikali iajiri walimu wenye vipaji na taaluma nzuri ya kufundisha
  • Mitaala ibadilike iyendane na mwenendo wa Dunia
  • Masomo yenye nwelekeo wa sayansi na ufundi yapewe kipaumbele
  • Siasa zitolewe kwenye elimu hasa siasa za kusifia sifia kila wakati
 
Mimi mwenyewe nilipasua Enzi hizo lakini sijaona faida yake..Unaweza kuta mwenye 4 akaanzisha kampuni Na mwenye singo digit akafa anazungusha bahasha maofisini...kumbuka hata Albert Einstein alikuwa Anafeli darasani Na alisema "everyone is a genius" Kwa namna Yake mwenyewe tu...cha msingi Ni vijana wengi Zaidi wafike chuo.

Halafu elimu sio kitu complicated kihivyo..We hujiulizi kwanini hapa bongo div3 husomi udaktari lakini ukienda china unasoma??Je elimu ya Tz Iko juu kuliko China?
 
Sio wivu ni jambo la kushangaza ukilitazama vizuri.
Tatizo Ni ukosefu WA ajira Na upungufu wa shule Na vyuo Tu...lakini hivyo vingekuwepo vya kutosha hata Hayo madaraja yangeondolewa ingekuwa Kila anayesoma anafaulu tu
 
Kutakuwa na shida mahali, kuna kipindi nilichukua hadi paper ya hesabu ya mwaka X katika kuhakikisha kweli vijana wanapata hii misonge ya namba kihalali au ni mafekeche zinafanyika.
 
Zile one simple sana kizipiga mkuu. Ungesoma english medium ungepiga tu. Alafu inaonekana hata watoto wako home work ufuatilii home work. Mtoto wa darasa la nne anasoma science ya form three kwann usipige one?
 
Back
Top Bottom