MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,213
- 22,277
Wakuu leo nipo kisomi zaidi kuongelea hili suala la kitaifa.
Wote ni mashahidi wa matokeo ya kidato cha nne mwaka 2020 yalivyosheheni division 1.7 karibu kila shule. St Francis Mbeya ilikuwa nazo nyingi sana. Kama ni za kweli na za haki nawapongeza NECTA, Waalimu, Wanafunzi, Wazazi na wote waliohusika kupatikana. Hakika ni matokeo ya kimbunga.
Ila mimi nina mashaka makubwa na matokeo hayo. Kwa tuliosoma miaka ya nyuma hadi mwanzoni mwa miaka ya 2000 mtakuwa mashahidi ilivyokuwa ngumu kupata Division One za 7,8 na 9. Sisi tuliziita one za digit. Ni wakali wachache walikuwa wakizipata. Matokeo yakitoka one zinakuwa nyingi ila za 7 ni chache mno. Kwa mfano Ilboru, Mzumbe na Kibaha zilikuwa zinatoa one nyingi mno ila hizo za 7 ilikuwa ngumu kuwepo nyingi.
Na waliokuwa wakizipata walikuwa ni wale magenius wa ukweli au wale ambao walikuwa na bidii ya kusoma karibu muda wote. Kuna majamaa walikimbiza kuanzia o-level hadi UDSM. Sisi wengine tulipiga tu One za kawaida. Wengi kuanzia one ya 12 hadi 17. Je, miaka ile wanafunzi hawakuwa na akili kama wa sasa? Hawakuwa na jitihada kuliko wa sasa?
Kwangu mimi inawezekana kweli zimepatikana kihalali. Pia nahisi zile tetesi za baraza "kupanua goli" ni za kweli. Kama kweli walipanua goli itakuwa jambo la kusikitisha mno. Ni kujidanganya. Mimi kwa leo nimepost tu wasiwasi wangu ila muda utatupa majibu sahihi kuhusu hawa watoto wetu.
Wote ni mashahidi wa matokeo ya kidato cha nne mwaka 2020 yalivyosheheni division 1.7 karibu kila shule. St Francis Mbeya ilikuwa nazo nyingi sana. Kama ni za kweli na za haki nawapongeza NECTA, Waalimu, Wanafunzi, Wazazi na wote waliohusika kupatikana. Hakika ni matokeo ya kimbunga.
Ila mimi nina mashaka makubwa na matokeo hayo. Kwa tuliosoma miaka ya nyuma hadi mwanzoni mwa miaka ya 2000 mtakuwa mashahidi ilivyokuwa ngumu kupata Division One za 7,8 na 9. Sisi tuliziita one za digit. Ni wakali wachache walikuwa wakizipata. Matokeo yakitoka one zinakuwa nyingi ila za 7 ni chache mno. Kwa mfano Ilboru, Mzumbe na Kibaha zilikuwa zinatoa one nyingi mno ila hizo za 7 ilikuwa ngumu kuwepo nyingi.
Na waliokuwa wakizipata walikuwa ni wale magenius wa ukweli au wale ambao walikuwa na bidii ya kusoma karibu muda wote. Kuna majamaa walikimbiza kuanzia o-level hadi UDSM. Sisi wengine tulipiga tu One za kawaida. Wengi kuanzia one ya 12 hadi 17. Je, miaka ile wanafunzi hawakuwa na akili kama wa sasa? Hawakuwa na jitihada kuliko wa sasa?
Kwangu mimi inawezekana kweli zimepatikana kihalali. Pia nahisi zile tetesi za baraza "kupanua goli" ni za kweli. Kama kweli walipanua goli itakuwa jambo la kusikitisha mno. Ni kujidanganya. Mimi kwa leo nimepost tu wasiwasi wangu ila muda utatupa majibu sahihi kuhusu hawa watoto wetu.