Morogoro: Zaidi ya Wanafunzi 10,000 hawajaripoti Kidato cha Kwanza hadi sasa

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
WANAFUNZI zaidi ya sh 10,000 kati ya 56,827 walichaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza katika Shule za Sekondari za Serikali mkoani Morogoro hawajaripoti na kusajiliwa hadi kufikia Februari 23, mwaka huu (2024).

Taarifa hiyo iliyotolewa na Ofisa Elimu Taaluma mkoa huo, Hildegard Saganda wakati akiwa kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Morogoro, imeeleza kuwa hadi kufikia Februari 23 idadi ya wanafunzi walioripoti na kusajiliwa shuleni ilikuwa 46,775 sawa na asilimia 82 kati yao wavulana ni 22,203 na wasichana ni 24,572.

Ametaja halmashauri zenye wanafunzi wengi kuwa ni Kilosa ambao waliochanguliwa ni 11,156 wakati walioripoti hadi kipindi hicho walikuwa 8,990 sawa na asilimia 81 ikifuatiwa na Manispaa ya Morogoro waliochanguliwa ni 9,885 na walioripoti 7,502 sawa na asilimia 76.
 
Aisee teena kama Ifakara watoto wanaacha shule bila sababu za msingi hali ni mbaya sana kwenye swala la elimu kule.
 
50% Ndoa za utotoni,
25% Ajira za utotoni,
25% Kukosa mwamko wa elimu/umasikini.

Hiyo ni tathmini yangu kwa kadiri ninavyoufahamu Mkoa huo.
 
Hapa sababu kuu ni dhana ya ukosefu wa ajira,wazazi walitegemea wakisomesha mtoto lazima aajiriwe,lakini walivyoona tatizo la ajira,wazazi wengi hawawapeleki watoto shule,na watoto nao wamejazana maneno mengi mtaani kwamba ukienda shule unapoteza muda,ukirudi unakuta wenzio tunamagari.ko hili ni tatizo.kabisa
 
WANAFUNZI zaidi ya sh 10,000 kati ya 56,827 walichaguliwa kujiunga na masomo ya kidato cha kwanza katika Shule za Sekondari za Serikali mkoani Morogoro hawajaripoti na kusajiliwa hadi kufikia Februari 23, mwaka huu (2024).

Taarifa hiyo iliyotolewa na Ofisa Elimu Taaluma mkoa huo, Hildegard Saganda wakati akiwa kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Morogoro, imeeleza kuwa hadi kufikia Februari 23 idadi ya wanafunzi walioripoti na kusajiliwa shuleni ilikuwa 46,775 sawa na asilimia 82 kati yao wavulana ni 22,203 na wasichana ni 24,572.

Ametaja halmashauri zenye wanafunzi wengi kuwa ni Kilosa ambao waliochanguliwa ni 11,156 wakati walioripoti hadi kipindi hicho walikuwa 8,990 sawa na asilimia 81 ikifuatiwa na Manispaa ya Morogoro waliochanguliwa ni 9,885 na walioripoti 7,502 sawa na asilimia 76.
Watanzania, tumieni hii kama fursa ya kuwa na maafisa usafirishaji na maafisa ubashiri wa kutosha kwa ajili ya uchumi wa nchi
 
Pia kuna kundi jingine la watoto wanaosoma private schools ambao huchaguliwa shule za Kayumba.Hawa nao huwa hawaripoti katika shule husika badala yake huendelea na private secondary schools.
 
Back
Top Bottom