SIMULIZI RIWAYA
JF-Expert Member
- Feb 19, 2022
- 415
- 1,275
DON'T SHOUT
(usipige kelele)
Sehemu ya...............01
Mtunzi: Saul David
Tel : +255756862047
E-mail: saulstewarty@gmail.com
****
EPISODE 01...
"Moto, moto, jamani motooooo"
"Moto, kuna mtu ndani, motooooo"
Sauti hizi za makelele zilipasua anga zikitokea katika chuo kimoja kikubwa kilichojengwa kisasa pembezoni mwa jiji la Dar es salaam.
Wingu kubwa la moshi lilikuwa limetanda hewani kutokana na moto mkubwa uliokuwa ukiunguza jengo moja chuoni hapo, wanafunzi waliokuwa katika hostel zao walikurupuka na kuanza kutoka nje kwa kasi, huku wengine wakichungulia kutoka juu ghorofani kuangalia kilichokuwa kikiendelea.
Wote walishuhudia namna jengo moja la maktaba lilivyokuwa likiteketea kwa moto mkali.
"Jamani msaidieni Sophia alikuwa humo ndani hajatoka msaidieniii " alizungumza mwanafunzi mmoja wa kike hali akionyesha wasiwasi mkubwa aliokuwa nao.
Wanafunzi wa kike wenye moyo mwepesi waliaanza kupiga kelele zaidi huku wakiita jina la Sophia, na wengine wakiangua kilio.
Wanafunzi wa kiume nao walibaki katika hali ya kujiuma uma hakuna aliyethubutu kunyanyua mguu wake kujitoka katikati ya lile jengo lililokuwa tayari limeshika moto pande zote, wote walihofia usalama wa maisha yao.
Wanafunzi walizidi kukusanyika huku taarifa za kuwemo kwa Sophia mle ndani zikizidi kusambaa kwa kasi. Kelele zilizidi mara alipofika mwanafunzi mmoja wa kiume ambae ndiye haswa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Sophia pale chuoni aliitwa john
"Shem John njoo Sophy yuko ndani atakufa jamaniii" mwanamke mmoja alipiga kelele huku akimkimbilia john na kuanza kumvuta mkono.
John alipigwa na butwaa kwa sekunde kadhaa hali akionyesha kushitushwa na habari hizo.
"Sophia, Sophia yupo humu ndani" aliuliza
" ndiyoo, alikuwa humu ndani"
Wanafunzi wote waligeuka na kuanza kumtazama john huku kila mmoja akiwa na matumaini kuwa ni lazima angefanya jambo kumsaidia mpenzi wake.
John alipiga hatua taratibu kusogea kwenye lile jengo lililo kuwa likiteketea kwa moto. Jonh aliutazama ulemoto ambao ulikuwa ukiwaka haswa, kisha akageuka kutazama nyuma akaona wanafunzi wote wamenyamaza kimya wanamuangalia hasa wanafunzi wa kike.
Akageuka tena na kuutazama ule moto
" Aah hapana nitakufa bure" John alijisemea kimoyomoyo kisha akageuka na kuanza kurudi.
"Hebu subirini, kwani mm..mm..mmeshapiga simu zimamoto"
Aliuliza john hali akipatwa na kigugumizi cha ghafula.
"Ndiyo walisema wako njiani lakini tunashangaa mpaka sasa hawajafika bado"
"Kwa hiyo...." Alisema john lakini kabla hajamalizia sentensi yake mara alipita mtu mmoja kwa kasi akiwa amejifunika blanket nzito akakimbia na kujitosa moja kwa moja ndani ya ule moto akaingia ndani ya jengo la maktaba.Kelele za hapa na pale zilisikika huku kila mmoja akisema lake.
Wanafunzi karibu wote wa chuo hicho walikuwa wakitazama tukio hilo, wakati huo ving'ora vya magari ya zimamoto vilianza kusikika jirani kabisa na chuo hicho na punde magari manne ya zima moto yalifika na haraka shughuli ya kuzima moto ilianza.
Baada ya dakika Kama mbili hivi yule mtu aliyejitosa kwenye moto alitoka akiwa amembeba Sophia mgongoni na kujifunika lile blanket lake ambalo lilikuwa limeshika moto kDa chini.
Wale zimamoto walimpokea na kuanza kumpa huduma ya kwanza na kwa bahati nzuri binti huyo mrembo Sophia hakuwa ameungua ila tu alizidiwa kwa kushindwa kupumua kutokana na moshi mwingi uliokuwamo mle ndani.
"Yusto, Yusto, Yustoooo"
"Jamani we kaka asantee"
"Mmmh wewe kweli mwanaume"
"Muangalieni anaonekana jasiri hadi raha jamani"
Hizi zilikuwa ni sifa kutoka kwa wanafunzi wa kike zilizokuwa zikimwendea mwanafunzi mwenzao Yusto aliyejitosa kumsaidia Sophia.
Sifa hizi zilikuwa ni mwiba mkali kwa John aliyekuwa bado ameduwaa baada ya kushindwa kumsaidia mwanamke wake, alijihisi amedhalilishwa kupita kiasi na hii ingemtengenezea skendo kubwa hapo chuoni.
John alikuwa ni mtu mwenye majivuno
John alikuwa ni mtu mwenye majivuno makubwa chuoni hapo alikuwa na pesa na alipenda sifa na kujifanya yupo juu kuliko wanafunzi wengine wote, pesa zake zilimpa jeuri na kumdharau kila aliyekuwa mbele yake, alifanya matukio mengi ya ajabu na wala hakujali.
John aliondoka kinyonge huku akimtazama Yusto kwa macho makali Yusto nae alimuangalia bila kupepesa macho kisha akatabasamu kitendo kilichomfanya John akasiriki zaidi.
"Subiri nitakuonyesha, masikini mkubwa wewe mimi ndio Master Joo sijawahi kushindwa" alisema john kwa sauti ya chini huku akiuma meno yake kwa hasira akaondoka.
*****
Yusto alionekana akitembea taratibu baada ya kutoka kwenye tukio la moto sasa alikuwa akirejea chumbani kwake, Mara simu yake iliingia ujumbe mfupi wa maandishi akaufungua na kuusoma.
"NIMEKUONA YUSTO NI WEWE, ASANTE KWA KUNISAIDIA LAKINI KWA NINI UNANITESA HIVI YUSTO KAMA HUNIPENDI KWA NINI UMEKUJA KUNISAIDIA"
Huu ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Sophia, Yusto alisimama kwa dakika kadhaa huku akitafakari ajibu nini. baada ya sekunde chache akaandika meseji kumjibu
"HAKIKISHA UMEPUMZIKA, ALAFU JOHN HAJAPENDA SIJUI UNATAKA MPAKA ANIUWE, SI UNAMJUA LAKINI"
aliituma sms hiyo kisha akarudisha simu mfukoni na kuanza tena kutembea lakini mara alisita na kusimama ni kama vile aliona kitu, akaanza kupiga hatua akielekea kwenye darasa moja akaingia ndani.
"Wewe umekaa humu inamaana hujasikia kama nje kuna moto" Yusto aliuliza kwa ukali kidogo huku akimuangalia mwanamke mmoja aliyekuwa amekaa mbele yake na kumpa mgongo.
Yusto alimuangalia juu hadi chini, mwanamke huyo alikuwa mrefu kiasi rangi yake kama chotara si mwafrika si mwarabu, kichwani alikuwa na nywele ndefu zilizofika mgongoni.
Sehemu kubwa ya mgongo wake ulikuwa wazi kutokana na nguo aliyokuwa ameivaa, hivyo Yusto aliweza kuishuhudia vizuri ngozi laini ya mwanadada huyo aliyekuwa pia amevaa sketi fupi iliyokaa vizuri kwenye hips zake na kubana kwenye kiuno chake chembamba.
Mapaja ya mwanadada huyo yalikuwa wazi kwa sehemu kubwa jambo lililomfanya Yusto kutaka kuiona sura ya mwanadada huyo ambae hadi dakika hiyo hakuwa amezungumza wala kugeukaa.
"ii..ina..inamaana hunisikii" Yusto aliuliza tena kwa mara ya pili lakini safari hii akionyesha kupatwa na kigugumizi kiasi.
Yule dada aligeuka taratibu kisha akatazama na Yusto uso kwa uso. Yusto alijikuta mapigo yake ya moyo yanaanza kwenda kasi ghafula sura nzuri ya mwanamke huyo ilizidi kumuweka kwenye wakati mgumu alikuwa ni mrembo, mrembo kupindukia, ni kweli chuoni hapa kulikuwa na warembo wengi lakini hakuna hata mmoja aliyewahi kumshitua Yusto kwa kiwango hicho hii ilikuwa ni mara yake ya kwanza hadi yeye mwenyewe alijishangaa.
"Nini hiki, Huyu mwanamke ni nani?" alijiuliza Yusto, ni kweli ilikuwa ni mara yake ya kwanza kukutana na mwanafunzi huyo mgeni.
Yule dada alimtazama Yusto kuanzia juu hadi chini na alipofikisha macho yake kwenye kiuno cha Yusto akatabasamu na kumtazama Yusto usoni.
Yusto aliweza kuuona mwanya ambao ulizidi kuupambamba uzuri wa dada huyo mrembo.
Yusto hakuelewa nini kimemfanya dada huyo atabasamu taratibu aliinama na kujitazama ndipo alipogundua kuwa zipu ya suruali yake ilikuwa wazi.
Aliduwaa kwa sekunde kadhaa kisha akamtazama tena yule dada ambae alikuwa bado ametabasamu.
"Hi" alisema yule dada.
DON'T SHOUT
(Usipige kelele)
Sehemu ya......................02
Mtunzi: Saul David
Tel: +255756862047
Email: saulstewarty@gmail.com
Episode 02
UTANGULIZI (kwa wasomaji wapya)
Moto mkubwa unawaka na kuunguza jengo la maktaba ndani yake akiwemo binti mmoja mrembo anaeitwa Sophia, John ambae ndiye mpenzi wa sophia anashindwa kufanya lolote kumsaidia mpenzi wake lakini anatokea kijana mwingine(Yusto) anaejitosa katikati ya moto huo na kumsaidia Sophia jambo linalomkasirisha sana John anajikuta anaweka kisasi kizito kwa Yusto.
Baada ya purukushani hizo kuisha Yusto akiwa chuoni hapa anakutana na mwanamke mrembo kupindukia ambae hakuwahi kumuona kabla.
ILIPOISHIA...
Yusto hakuelewa nini kimemfanya dada huyo atabasamu taratibu aliinama na kujitazama ndipo alipogundua kuwa zipu ya suruali yake ilikuwa wazi.
Aliduwaa kwa sekunde kadhaa kisha akamtazama tena yule dada ambae alikuwa bado ametabasamu.
"Hi" alisema yule dada.
SONGA NAYO...
"Hi, mambo vipi" alijibu Yusto huku akitazama pembeni kwa aibu kisha akafunga zipi ya suruali yake haraka haraka. "Poa, pole ulikuwa unazima moto?"
" Aah hapana tulikuwe tu pale tunaangalia"
"Mimi naogopa sana moto ndo maana sijaenda hata kutazama" Alisema yule dada huku akimuangalia Yusto kwa macho ya kumdadisi, macho hayo ya kudeka yalimfanya Yusto ashindwe kujiamini akabaki katika hali ya kujiumauma wala hakujua azungumze nini na mrembo huyo, mara simu yake iliita.
Akachukua na kutazama jina la mpigaji
'FRANK'
haraka akaipokea
" Uko wapi wewe, boss yupo hapa nje ya geti anatuita njoo haraka" ilikuwa ni sauti ya Frank akizungumza upande wa pili kisha akakata simu.
Taarifa hii ilimshtua kidogo Yusto haraka akatoka bila hata kumuaga yule dada.
Yusto alitembea upesi hadi alipotoka nje kabisa ya chuo hicho mbele yake aliona gari nyeusi ikiwa imepaki pembeni ya barabara, gari hiyo haikuwa ngeni machoni kwa Yusto, aliifuata taratibu akafungua mlango wa nyuma akaingia.
Ndani ya gari hilo alimkuta tayari Frank rafiki yake amekwisha ingia nakukaa siti ya nyuma, mbele alikuwepo dereva pamoja na mzee mmoja aliayevaa suti nyeusi uso wake ukiwa umekunjamana.
"Hivi ninyi mnataka kazi hamtaki" aliuliza yule mzee kwa sauti ya kukwaruza.
"Tunataka bosi" Yusto na Frank walijibu kwa pamoja hali wakionyesha unyenyekevu wa hali ya juu.
"Sasa kwa nini mmekuwa wazembe, tumewaleta hapa kama walinzi wa siri ndani ya hiki chuo mnatakiwa kufanya kazi, hii ni biashara inaushindani kama biashara nyingine
hiki ni chuo kikubwa Tanzania nzima mmiliki wa hiki chuo anamaadui kibao ambao hawataki kuona akifanikiwa, wanamtafuta kila kona ili waharibu sifa ya hiki chuo, angalia tarehe 9 wanafunzi wote wameumwa matumbo wakaharisha tatizo ikaonekana ni chakula, tarehe 15 maji yalikata ghafula, tarehe 21 kukatokea short ya umeme vitu vya wanafunzi vikaungua na wengine kidogo wafe, leo tena maktaba imeungua vitabu na vitu vyote vya muhimu vimewaka moto na ninyi mpo mshahara manachukua hivi mnafikiri haya matukio yote yametokea bahati mbaya tuu" Alifoka yule mzee.
"Hapana bosi"
"Sasa kama hapana ninyi kazi yenu ni nini, mko hapa kama walinzi wa siri kulinda usalama sasa matukio yote haya yanatokea ninyi mnakuwa wapi, au mnapenda kusoma?, kama ndio wewe Yusto nasikia kunamtihani gani sijui umekuwa wa kwanza hii ndo kazi iliyokuleta hapa?"
" Hapana bosi ila tulipoanza kazi tulikuwa tunafeli sana ikabidi tukazane pia kusoma wasije kutushtukia lakini pia tungefeli zaidi tungefukuzwa hata chuo"
"Acha wendawazimu wewe sisi wenyechuo ndio tumekuleta hapa nani anaweza kukufukuza, hebu fanyeni kazi pelelezeni mjue nyuma ya haya matukio yote kuanzia tarehe 9 kuna nini sawa"
"Sawa bosi"
"Msisahau kwamba hii ni vita, tuliwaweka kambini miezi 8 mkapata mafunzo sio kwamba tulikuwa tunapoteza mda, haya shika hii"
Alisema yule mzee kisha akachomoa bastola ndogo mbili akampa Yusto moja na Frank moja.
"Hatutaki ujinga tena, nimetumwa kuja kuwapa onyo la mwisho sasa tusikie tena tukio la ajabu, nawapa siku 7 tu mnipe report ni nani yuko nyuma ya haya matukio kwa heri".
Walimaliza mazungumzo kisha Yusto na Frank wakashuka kwenye gari na kuondoka wakawa wanarejea chuoni huku kila mmoja akiwaza namna atakavyoanza kukabiliana na majukumu hayo.
"Unajua Yusto ni kweli tumejisahau sana haya matukio yamefuatana yani ni ndani ya mwezi huu mmoja sio bure, mbona mwanzo hali ilikuwa shwari tu eti kunani jamaa?"
"Tumepewa siku saba tu, nategemea utaniambia tuanzie wapi acha maswali ya kijinga?" Alisema Yusto hali akiwa amekunja sura yake.
Wakati wamefika kwenye geti la kuingia chuoni kwa mara nyingine tena Yusto akamuona yule dada waliyemkuta darasani anakuja upande wao, sasa aliweza kumuona vizuri namna mwanamke huyo alivyoumbika kuanzia juu hadi chini, alikuwa na shepu nzuri ya kuvutia na alitembea kwa madaha sana.
Walikutana na mwisho wakapishana bila hata kusalimiana, harufu ya marashi mazuri aliyopulizia dada huyo ndiyo iliyobaki kwenye pua za Yusto na Frank.
"Oya huyu ni nani?" Aliuliza Yusto
"Haa! inamaana humjui huyu demu anaitwa Caren, ni femas sana hapa chuoni kila mtu anamjua, nakwambia wanaume wanajigongagonga hapo lakini anawatolea nje, hadi Master Joo kachemka"
"Eeh John huyu mpenzi wa Sophia?"
"Sasa je, si ndo maana anataka kumtema Sophia kisa Caren, lakini Caren nae kakaza sijui ana nini huyo dada"
"Mmh unajua John anamtesa sana Sophia, kwanza umesikia leo kashindwa kumchomoa kwenye moto mle maktaba"
"Nimeskia kamanda wewe ndo ulimtoa sophia mle kwenye moto hongera, naona bado unamuelewa sana fanya mpango basi au unamuogopa John"
"Aah wapi hiyo sio sababu"
" Dah nasikia John kazuia mwanaume yoyote kumsogelea Caren yani kashakuwa demu wake tayari na hajampata, yule jamaa bangi zinamuharibu wallah"
"Kwani huyo Caren katokea wapi na anamda gani hapa chuoni"
" Amehamia tarehe 7 mwezi huu anawiki kama 3 tuu"
Alijibu Frank kauli iliyowasha taa nyekundu kwenye kichwa cha Yusto akasimama
" umesema tarehe 7?"
"Ndio kwani vipi?" aliuliza Frank akiwa haelewi Yusto ameshanganzwa na nini lakini mara akaelewaa.
" Aah kweli Yusto, inamaana baada ya Caren kuja ndo haya matukio yameanza kutokea hapa chuoni kuanzia hiyo tarehe 9, mmmh inawezekana kweli akawaa..." Alisema Frank huku akitafakari zaidi.
" Nakata uniletee taarifa za huyu mwanamke sasa hivi utanikuta room kwangu" Alisema Yusto
*****
Dakika 10 baada Yusto alikuwa ndani ya chumba chake amekaa, na Mara mlango ukafunguliwa akaingia Frank.
"Vipi umepata" Yusto aliuliza kwa bashasha
"Ndiyo huyu dada anaitwa Caren Pius Mwanandota, anamiaka 20 alikuja hapa chuoni tarehe 7, anaishi floor ya pili chumba namba 59, anatabia ya kutoka nje ya chuo mara kwa mara akiwa peke yake hata sasa hayupo amewaaga marafiki zake anaenda shopping hizo ndo taarifa nilizopata mpaka sasa" alisema Frank na bila kupoteza muda Yusto alichukua koti lake lenye rangi nyeusi akalivaa kisha akatoka nje kwa kasi akawa anaelekea upande zilipokuwa hostel za wanawake.
Frank alitoka nje na kumsindikiza kwa macho.
" aah huyu jamaa nae hatuliagi, anakurupuka tuu" alisema Frank kisha akageuka kuingia ndani lakini mara alishtuka na kugeuka tena nyuma.
"Mungu wangu Caren kurudi" alisema Frank huku akimuangalia Caren aliyekuwa anatembea kwa kasi kidogo kuelekea kwenye vyumba vyao.
JE, NINI KITAFUATA?
CAREN NI NANI?
VIPI KUHUSU JOHN, SOPHIA?
NINI HATIMA YA CHUO HIKI?
(usipige kelele)
Sehemu ya...............01
Mtunzi: Saul David
Tel : +255756862047
E-mail: saulstewarty@gmail.com
****
EPISODE 01...
"Moto, moto, jamani motooooo"
"Moto, kuna mtu ndani, motooooo"
Sauti hizi za makelele zilipasua anga zikitokea katika chuo kimoja kikubwa kilichojengwa kisasa pembezoni mwa jiji la Dar es salaam.
Wingu kubwa la moshi lilikuwa limetanda hewani kutokana na moto mkubwa uliokuwa ukiunguza jengo moja chuoni hapo, wanafunzi waliokuwa katika hostel zao walikurupuka na kuanza kutoka nje kwa kasi, huku wengine wakichungulia kutoka juu ghorofani kuangalia kilichokuwa kikiendelea.
Wote walishuhudia namna jengo moja la maktaba lilivyokuwa likiteketea kwa moto mkali.
"Jamani msaidieni Sophia alikuwa humo ndani hajatoka msaidieniii " alizungumza mwanafunzi mmoja wa kike hali akionyesha wasiwasi mkubwa aliokuwa nao.
Wanafunzi wa kike wenye moyo mwepesi waliaanza kupiga kelele zaidi huku wakiita jina la Sophia, na wengine wakiangua kilio.
Wanafunzi wa kiume nao walibaki katika hali ya kujiuma uma hakuna aliyethubutu kunyanyua mguu wake kujitoka katikati ya lile jengo lililokuwa tayari limeshika moto pande zote, wote walihofia usalama wa maisha yao.
Wanafunzi walizidi kukusanyika huku taarifa za kuwemo kwa Sophia mle ndani zikizidi kusambaa kwa kasi. Kelele zilizidi mara alipofika mwanafunzi mmoja wa kiume ambae ndiye haswa alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Sophia pale chuoni aliitwa john
"Shem John njoo Sophy yuko ndani atakufa jamaniii" mwanamke mmoja alipiga kelele huku akimkimbilia john na kuanza kumvuta mkono.
John alipigwa na butwaa kwa sekunde kadhaa hali akionyesha kushitushwa na habari hizo.
"Sophia, Sophia yupo humu ndani" aliuliza
" ndiyoo, alikuwa humu ndani"
Wanafunzi wote waligeuka na kuanza kumtazama john huku kila mmoja akiwa na matumaini kuwa ni lazima angefanya jambo kumsaidia mpenzi wake.
John alipiga hatua taratibu kusogea kwenye lile jengo lililo kuwa likiteketea kwa moto. Jonh aliutazama ulemoto ambao ulikuwa ukiwaka haswa, kisha akageuka kutazama nyuma akaona wanafunzi wote wamenyamaza kimya wanamuangalia hasa wanafunzi wa kike.
Akageuka tena na kuutazama ule moto
" Aah hapana nitakufa bure" John alijisemea kimoyomoyo kisha akageuka na kuanza kurudi.
"Hebu subirini, kwani mm..mm..mmeshapiga simu zimamoto"
Aliuliza john hali akipatwa na kigugumizi cha ghafula.
"Ndiyo walisema wako njiani lakini tunashangaa mpaka sasa hawajafika bado"
"Kwa hiyo...." Alisema john lakini kabla hajamalizia sentensi yake mara alipita mtu mmoja kwa kasi akiwa amejifunika blanket nzito akakimbia na kujitosa moja kwa moja ndani ya ule moto akaingia ndani ya jengo la maktaba.Kelele za hapa na pale zilisikika huku kila mmoja akisema lake.
Wanafunzi karibu wote wa chuo hicho walikuwa wakitazama tukio hilo, wakati huo ving'ora vya magari ya zimamoto vilianza kusikika jirani kabisa na chuo hicho na punde magari manne ya zima moto yalifika na haraka shughuli ya kuzima moto ilianza.
Baada ya dakika Kama mbili hivi yule mtu aliyejitosa kwenye moto alitoka akiwa amembeba Sophia mgongoni na kujifunika lile blanket lake ambalo lilikuwa limeshika moto kDa chini.
Wale zimamoto walimpokea na kuanza kumpa huduma ya kwanza na kwa bahati nzuri binti huyo mrembo Sophia hakuwa ameungua ila tu alizidiwa kwa kushindwa kupumua kutokana na moshi mwingi uliokuwamo mle ndani.
"Yusto, Yusto, Yustoooo"
"Jamani we kaka asantee"
"Mmmh wewe kweli mwanaume"
"Muangalieni anaonekana jasiri hadi raha jamani"
Hizi zilikuwa ni sifa kutoka kwa wanafunzi wa kike zilizokuwa zikimwendea mwanafunzi mwenzao Yusto aliyejitosa kumsaidia Sophia.
Sifa hizi zilikuwa ni mwiba mkali kwa John aliyekuwa bado ameduwaa baada ya kushindwa kumsaidia mwanamke wake, alijihisi amedhalilishwa kupita kiasi na hii ingemtengenezea skendo kubwa hapo chuoni.
John alikuwa ni mtu mwenye majivuno
John alikuwa ni mtu mwenye majivuno makubwa chuoni hapo alikuwa na pesa na alipenda sifa na kujifanya yupo juu kuliko wanafunzi wengine wote, pesa zake zilimpa jeuri na kumdharau kila aliyekuwa mbele yake, alifanya matukio mengi ya ajabu na wala hakujali.
John aliondoka kinyonge huku akimtazama Yusto kwa macho makali Yusto nae alimuangalia bila kupepesa macho kisha akatabasamu kitendo kilichomfanya John akasiriki zaidi.
"Subiri nitakuonyesha, masikini mkubwa wewe mimi ndio Master Joo sijawahi kushindwa" alisema john kwa sauti ya chini huku akiuma meno yake kwa hasira akaondoka.
*****
Yusto alionekana akitembea taratibu baada ya kutoka kwenye tukio la moto sasa alikuwa akirejea chumbani kwake, Mara simu yake iliingia ujumbe mfupi wa maandishi akaufungua na kuusoma.
"NIMEKUONA YUSTO NI WEWE, ASANTE KWA KUNISAIDIA LAKINI KWA NINI UNANITESA HIVI YUSTO KAMA HUNIPENDI KWA NINI UMEKUJA KUNISAIDIA"
Huu ulikuwa ni ujumbe kutoka kwa Sophia, Yusto alisimama kwa dakika kadhaa huku akitafakari ajibu nini. baada ya sekunde chache akaandika meseji kumjibu
"HAKIKISHA UMEPUMZIKA, ALAFU JOHN HAJAPENDA SIJUI UNATAKA MPAKA ANIUWE, SI UNAMJUA LAKINI"
aliituma sms hiyo kisha akarudisha simu mfukoni na kuanza tena kutembea lakini mara alisita na kusimama ni kama vile aliona kitu, akaanza kupiga hatua akielekea kwenye darasa moja akaingia ndani.
"Wewe umekaa humu inamaana hujasikia kama nje kuna moto" Yusto aliuliza kwa ukali kidogo huku akimuangalia mwanamke mmoja aliyekuwa amekaa mbele yake na kumpa mgongo.
Yusto alimuangalia juu hadi chini, mwanamke huyo alikuwa mrefu kiasi rangi yake kama chotara si mwafrika si mwarabu, kichwani alikuwa na nywele ndefu zilizofika mgongoni.
Sehemu kubwa ya mgongo wake ulikuwa wazi kutokana na nguo aliyokuwa ameivaa, hivyo Yusto aliweza kuishuhudia vizuri ngozi laini ya mwanadada huyo aliyekuwa pia amevaa sketi fupi iliyokaa vizuri kwenye hips zake na kubana kwenye kiuno chake chembamba.
Mapaja ya mwanadada huyo yalikuwa wazi kwa sehemu kubwa jambo lililomfanya Yusto kutaka kuiona sura ya mwanadada huyo ambae hadi dakika hiyo hakuwa amezungumza wala kugeukaa.
"ii..ina..inamaana hunisikii" Yusto aliuliza tena kwa mara ya pili lakini safari hii akionyesha kupatwa na kigugumizi kiasi.
Yule dada aligeuka taratibu kisha akatazama na Yusto uso kwa uso. Yusto alijikuta mapigo yake ya moyo yanaanza kwenda kasi ghafula sura nzuri ya mwanamke huyo ilizidi kumuweka kwenye wakati mgumu alikuwa ni mrembo, mrembo kupindukia, ni kweli chuoni hapa kulikuwa na warembo wengi lakini hakuna hata mmoja aliyewahi kumshitua Yusto kwa kiwango hicho hii ilikuwa ni mara yake ya kwanza hadi yeye mwenyewe alijishangaa.
"Nini hiki, Huyu mwanamke ni nani?" alijiuliza Yusto, ni kweli ilikuwa ni mara yake ya kwanza kukutana na mwanafunzi huyo mgeni.
Yule dada alimtazama Yusto kuanzia juu hadi chini na alipofikisha macho yake kwenye kiuno cha Yusto akatabasamu na kumtazama Yusto usoni.
Yusto aliweza kuuona mwanya ambao ulizidi kuupambamba uzuri wa dada huyo mrembo.
Yusto hakuelewa nini kimemfanya dada huyo atabasamu taratibu aliinama na kujitazama ndipo alipogundua kuwa zipu ya suruali yake ilikuwa wazi.
Aliduwaa kwa sekunde kadhaa kisha akamtazama tena yule dada ambae alikuwa bado ametabasamu.
"Hi" alisema yule dada.
DON'T SHOUT
(Usipige kelele)
Sehemu ya......................02
Mtunzi: Saul David
Tel: +255756862047
Email: saulstewarty@gmail.com
Episode 02
UTANGULIZI (kwa wasomaji wapya)
Moto mkubwa unawaka na kuunguza jengo la maktaba ndani yake akiwemo binti mmoja mrembo anaeitwa Sophia, John ambae ndiye mpenzi wa sophia anashindwa kufanya lolote kumsaidia mpenzi wake lakini anatokea kijana mwingine(Yusto) anaejitosa katikati ya moto huo na kumsaidia Sophia jambo linalomkasirisha sana John anajikuta anaweka kisasi kizito kwa Yusto.
Baada ya purukushani hizo kuisha Yusto akiwa chuoni hapa anakutana na mwanamke mrembo kupindukia ambae hakuwahi kumuona kabla.
ILIPOISHIA...
Yusto hakuelewa nini kimemfanya dada huyo atabasamu taratibu aliinama na kujitazama ndipo alipogundua kuwa zipu ya suruali yake ilikuwa wazi.
Aliduwaa kwa sekunde kadhaa kisha akamtazama tena yule dada ambae alikuwa bado ametabasamu.
"Hi" alisema yule dada.
SONGA NAYO...
"Hi, mambo vipi" alijibu Yusto huku akitazama pembeni kwa aibu kisha akafunga zipi ya suruali yake haraka haraka. "Poa, pole ulikuwa unazima moto?"
" Aah hapana tulikuwe tu pale tunaangalia"
"Mimi naogopa sana moto ndo maana sijaenda hata kutazama" Alisema yule dada huku akimuangalia Yusto kwa macho ya kumdadisi, macho hayo ya kudeka yalimfanya Yusto ashindwe kujiamini akabaki katika hali ya kujiumauma wala hakujua azungumze nini na mrembo huyo, mara simu yake iliita.
Akachukua na kutazama jina la mpigaji
'FRANK'
haraka akaipokea
" Uko wapi wewe, boss yupo hapa nje ya geti anatuita njoo haraka" ilikuwa ni sauti ya Frank akizungumza upande wa pili kisha akakata simu.
Taarifa hii ilimshtua kidogo Yusto haraka akatoka bila hata kumuaga yule dada.
Yusto alitembea upesi hadi alipotoka nje kabisa ya chuo hicho mbele yake aliona gari nyeusi ikiwa imepaki pembeni ya barabara, gari hiyo haikuwa ngeni machoni kwa Yusto, aliifuata taratibu akafungua mlango wa nyuma akaingia.
Ndani ya gari hilo alimkuta tayari Frank rafiki yake amekwisha ingia nakukaa siti ya nyuma, mbele alikuwepo dereva pamoja na mzee mmoja aliayevaa suti nyeusi uso wake ukiwa umekunjamana.
"Hivi ninyi mnataka kazi hamtaki" aliuliza yule mzee kwa sauti ya kukwaruza.
"Tunataka bosi" Yusto na Frank walijibu kwa pamoja hali wakionyesha unyenyekevu wa hali ya juu.
"Sasa kwa nini mmekuwa wazembe, tumewaleta hapa kama walinzi wa siri ndani ya hiki chuo mnatakiwa kufanya kazi, hii ni biashara inaushindani kama biashara nyingine
hiki ni chuo kikubwa Tanzania nzima mmiliki wa hiki chuo anamaadui kibao ambao hawataki kuona akifanikiwa, wanamtafuta kila kona ili waharibu sifa ya hiki chuo, angalia tarehe 9 wanafunzi wote wameumwa matumbo wakaharisha tatizo ikaonekana ni chakula, tarehe 15 maji yalikata ghafula, tarehe 21 kukatokea short ya umeme vitu vya wanafunzi vikaungua na wengine kidogo wafe, leo tena maktaba imeungua vitabu na vitu vyote vya muhimu vimewaka moto na ninyi mpo mshahara manachukua hivi mnafikiri haya matukio yote yametokea bahati mbaya tuu" Alifoka yule mzee.
"Hapana bosi"
"Sasa kama hapana ninyi kazi yenu ni nini, mko hapa kama walinzi wa siri kulinda usalama sasa matukio yote haya yanatokea ninyi mnakuwa wapi, au mnapenda kusoma?, kama ndio wewe Yusto nasikia kunamtihani gani sijui umekuwa wa kwanza hii ndo kazi iliyokuleta hapa?"
" Hapana bosi ila tulipoanza kazi tulikuwa tunafeli sana ikabidi tukazane pia kusoma wasije kutushtukia lakini pia tungefeli zaidi tungefukuzwa hata chuo"
"Acha wendawazimu wewe sisi wenyechuo ndio tumekuleta hapa nani anaweza kukufukuza, hebu fanyeni kazi pelelezeni mjue nyuma ya haya matukio yote kuanzia tarehe 9 kuna nini sawa"
"Sawa bosi"
"Msisahau kwamba hii ni vita, tuliwaweka kambini miezi 8 mkapata mafunzo sio kwamba tulikuwa tunapoteza mda, haya shika hii"
Alisema yule mzee kisha akachomoa bastola ndogo mbili akampa Yusto moja na Frank moja.
"Hatutaki ujinga tena, nimetumwa kuja kuwapa onyo la mwisho sasa tusikie tena tukio la ajabu, nawapa siku 7 tu mnipe report ni nani yuko nyuma ya haya matukio kwa heri".
Walimaliza mazungumzo kisha Yusto na Frank wakashuka kwenye gari na kuondoka wakawa wanarejea chuoni huku kila mmoja akiwaza namna atakavyoanza kukabiliana na majukumu hayo.
"Unajua Yusto ni kweli tumejisahau sana haya matukio yamefuatana yani ni ndani ya mwezi huu mmoja sio bure, mbona mwanzo hali ilikuwa shwari tu eti kunani jamaa?"
"Tumepewa siku saba tu, nategemea utaniambia tuanzie wapi acha maswali ya kijinga?" Alisema Yusto hali akiwa amekunja sura yake.
Wakati wamefika kwenye geti la kuingia chuoni kwa mara nyingine tena Yusto akamuona yule dada waliyemkuta darasani anakuja upande wao, sasa aliweza kumuona vizuri namna mwanamke huyo alivyoumbika kuanzia juu hadi chini, alikuwa na shepu nzuri ya kuvutia na alitembea kwa madaha sana.
Walikutana na mwisho wakapishana bila hata kusalimiana, harufu ya marashi mazuri aliyopulizia dada huyo ndiyo iliyobaki kwenye pua za Yusto na Frank.
"Oya huyu ni nani?" Aliuliza Yusto
"Haa! inamaana humjui huyu demu anaitwa Caren, ni femas sana hapa chuoni kila mtu anamjua, nakwambia wanaume wanajigongagonga hapo lakini anawatolea nje, hadi Master Joo kachemka"
"Eeh John huyu mpenzi wa Sophia?"
"Sasa je, si ndo maana anataka kumtema Sophia kisa Caren, lakini Caren nae kakaza sijui ana nini huyo dada"
"Mmh unajua John anamtesa sana Sophia, kwanza umesikia leo kashindwa kumchomoa kwenye moto mle maktaba"
"Nimeskia kamanda wewe ndo ulimtoa sophia mle kwenye moto hongera, naona bado unamuelewa sana fanya mpango basi au unamuogopa John"
"Aah wapi hiyo sio sababu"
" Dah nasikia John kazuia mwanaume yoyote kumsogelea Caren yani kashakuwa demu wake tayari na hajampata, yule jamaa bangi zinamuharibu wallah"
"Kwani huyo Caren katokea wapi na anamda gani hapa chuoni"
" Amehamia tarehe 7 mwezi huu anawiki kama 3 tuu"
Alijibu Frank kauli iliyowasha taa nyekundu kwenye kichwa cha Yusto akasimama
" umesema tarehe 7?"
"Ndio kwani vipi?" aliuliza Frank akiwa haelewi Yusto ameshanganzwa na nini lakini mara akaelewaa.
" Aah kweli Yusto, inamaana baada ya Caren kuja ndo haya matukio yameanza kutokea hapa chuoni kuanzia hiyo tarehe 9, mmmh inawezekana kweli akawaa..." Alisema Frank huku akitafakari zaidi.
" Nakata uniletee taarifa za huyu mwanamke sasa hivi utanikuta room kwangu" Alisema Yusto
*****
Dakika 10 baada Yusto alikuwa ndani ya chumba chake amekaa, na Mara mlango ukafunguliwa akaingia Frank.
"Vipi umepata" Yusto aliuliza kwa bashasha
"Ndiyo huyu dada anaitwa Caren Pius Mwanandota, anamiaka 20 alikuja hapa chuoni tarehe 7, anaishi floor ya pili chumba namba 59, anatabia ya kutoka nje ya chuo mara kwa mara akiwa peke yake hata sasa hayupo amewaaga marafiki zake anaenda shopping hizo ndo taarifa nilizopata mpaka sasa" alisema Frank na bila kupoteza muda Yusto alichukua koti lake lenye rangi nyeusi akalivaa kisha akatoka nje kwa kasi akawa anaelekea upande zilipokuwa hostel za wanawake.
Frank alitoka nje na kumsindikiza kwa macho.
" aah huyu jamaa nae hatuliagi, anakurupuka tuu" alisema Frank kisha akageuka kuingia ndani lakini mara alishtuka na kugeuka tena nyuma.
"Mungu wangu Caren kurudi" alisema Frank huku akimuangalia Caren aliyekuwa anatembea kwa kasi kidogo kuelekea kwenye vyumba vyao.
JE, NINI KITAFUATA?
CAREN NI NANI?
VIPI KUHUSU JOHN, SOPHIA?
NINI HATIMA YA CHUO HIKI?