Kanungila Karim
JF-Expert Member
- Apr 29, 2016
- 20,746
- 25,662
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 36:
Aliondoka asubuhi akiwa hana habari ya safari. Baadaye mchana alirudi akaniambia kuwa atakuwa na safari.
“Utaondoka saa ngapi? Nikamuuliza haraka.
“Nitaondoka usiku. Hivi sasa gari iko bandarini inapakia mzigo.”
“Hapa nyumbani utaondoka saa ngapi?”
“Nimekuja kuchukua begi langu, nikiondoka ndiyo nimeondoka. Sitarudi tena.” SASA ENDELEA…
“Poa,” nikajisemea.
Hivyo ndivyo nilivyokuwa nataka.
“Hutawahi kula chakula?” nikajidai kumuuliza.
“Kwani umeshapika?”
“Ndiyo ninapika.”
“Sitakisubiri, acha niende. Nitakula hukohuko.”
“Hao matajiri zenu wanapenda kuwapa taarifa za ghafla sana. Ilitakiwa wakwambie mapema kuwa utakuwa na safari.”
“Ndiyo kazi zetu zilivyo. Tumeshazoea.”
“Poa. Safari njema.”
Musa alichukua begi lake akatia vitu alivyovitaka kisha akaniaga. Wakati anatoka nikamuuliza:
“Kondomu zako huzihitaji tena?”
Musa aligeuka mara moja akanitazama kisha akasema:
“We’ acha mzaha wako.”
Nilisimama kunako mlango nikamtazama alivyokuwa akitembea kuelekea kwenye kituo cha daladala. Wakati namtazama mawazo ya Mustafa yakaanza kunijia.
Nikarudi ndani na kufunga mlango. Niliketi kwenye sebule nikajiambia kuwa sitapika tena. Nitakwenda kupika kwa Mustafa.
Nilisubiri yapite masaa mawili nikatia baadhi ya vitu vyangu kwenye mkoba wangu kisha nikatoka. Sikuchukua nguo. Nilikwishahamishia kwa Mustafa baadhi ya nguo zangu na viatu. Nilichukua vitu vidogovidogo tu ambavyo Mustafa asingeweza kuvizingatia.
Kabla ya kwenda Mbezi nilipitia sokoni nikanunua vitu ambavyo nilihitaji kupika. Nilipofika Mbezi Mustafa alikuwa hayupo. Kwa vile nilikuwa na funguo zangu nikafungua mlango na kuingia ndani.
Niliingia chumbani nikabadili nguo kisha nikazima simu yangu na kuiweka kwenye chaji ili Mustafa akija aone simu iko kwenye chaji. Sikutaka anipigie wala sikutaka Musa anipigie.
Baadaye nikatoka chumbani na kuelekea jikoni na kuanza kupika.
Yalikuwa majira ya saa kumi na moja Mustafa aliporudi nyumbani na kunikuta nimeketi sebuleni nikiangalia CD ya filamu ya Kihindi.
“Mbona hukunifahamisha kama umeshakuja?” akaniuliza.
“Kwani ulitaka kuleta msichana wako?”
“Mishi acha mzaha wako, una ‘surprise’ za ajabu sana. Halafu nilikupigia ukawa hupatikani.”
“Simu ilikuwa kwenye chaji. Mimi mwenyewe nilikuwa jikoni napika.”
“Kwani ulikuja saa ngapi.”
“Tangu saa sita niko hapa.”
Nilimdanganya. Muda niliofika, saa sita ilikuwa imeshapita.
“Umepika nini?”
“Nimepika wali na nyama.”
Nilipomwambia hivyo Mustafa aliinuka na kuelekea chumbani. Baadaye alirudi tena sebuleni. Alionekana alikuwa anatoka kuoga.
Tukaendelea na mazungumzo.
Kabla ya mwezi mmoja kukamilika Mustafa akaenda India. Alipoondoka tu nikarudi kwa Musa. Musa aliporudi kutoka Burundi alinikuta nipo nyumbani.
Kwa vile safari zake nyingi zilikuwa za Burundi, alipoondoka tena kwenda Burundi nikahamia Mbezi kwa Mustafa. Mustafa alikaa India kwa wiki nzima. Aliporudi alinikuta nipo nyumbani kwake.
Baada ya mwezi mmoja nikajikuta nina mimba. Sikujua ile mimba ilikuwa ni ya nani lakini nilikisia kuwa ilikuwa ya Mustafa. Nikaitambulisha mimba yangu kwa waume wote wawili. Kila mmoja akajua nina mimba na mimba ni yake.
Kwa vile waume wangu wote wawili walikuwa wakisafiri nje ya nchi na wakiwa huko hukaa kwa zaidi ya wiki. Niliendelea kutumia mtindo uleule wa kuhamia kwa mwanaume mmoja pindi mwenzake anaposafiri.
Kwa bahati njema walikuwa wakisafiri kwa nyakati tofauti hivyo kuniwezesha mimi kuweza kuwa kwa mwanaume mmoja pale mwenzake anapokuwa hayupo. Ile mimba iliendelea hadi ikatimiza miezi tisa. Hakukuwa na mwanaume wangu yeyote aliyegundua kuwa mimba hiyo ilikuwa ya watu wawili.
Kuna siku Mustafa alikuwa amekwenda China kununua bidhaa. Lakini Musa alikuwepo na nilikuwa nyumbani kwake. Musa akaniambia kwamba anataka asafiri lakini anasita kwa sababu naweza kuumwa na uchungu wakati wowote na nitakuwa peke yangu.
Wakati akiniambia hivyo Mustafa alishanipigia simu kunijulisha kuwa anarudi kesho yake.
Nikamwambia Musa kuwa anaweza kwenda safari.
“Mimi nitakwenda kwa shangazi.”
“Shangazi ataweza kukuhudumia?” akaniuliza.
“Kwa nini asiweze. Yeye mwenyewe ameniambia niende.”
“Kama ameshakwambia basi unaweza kwenda, acha mimi niende safari.”
Siku ile Musa akaondoka. Sikwenda kwa shangazi. Musa alipoondoka nikaenda Mbezi kwa Mustafa.
Mustafa alirudi siku iliyofuata na siku hiyohiyo nikaumwa na uchungu. Mustafa alinikimbiza na gari hospitali. Nikajifungua usiku mtoto wa kiume. Alikuwa amefanana sana na Mustafa.
Mustafa alikuja hospitali asubuhi akamkuta mtoto ameshazaliwa. Akampa jina hapohapo.
“Mwanangu ataitwa Amani,” akaniambia.
Nikatabasamu na kumuuliza:
“Umempa jina la nani wako?”
“Ni jina la babu yangu mzaa mama yangu,” akaniambia.
Je, nini kiliendelea?
Aliondoka asubuhi akiwa hana habari ya safari. Baadaye mchana alirudi akaniambia kuwa atakuwa na safari.
“Utaondoka saa ngapi? Nikamuuliza haraka.
“Nitaondoka usiku. Hivi sasa gari iko bandarini inapakia mzigo.”
“Hapa nyumbani utaondoka saa ngapi?”
“Nimekuja kuchukua begi langu, nikiondoka ndiyo nimeondoka. Sitarudi tena.” SASA ENDELEA…
“Poa,” nikajisemea.
Hivyo ndivyo nilivyokuwa nataka.
“Hutawahi kula chakula?” nikajidai kumuuliza.
“Kwani umeshapika?”
“Ndiyo ninapika.”
“Sitakisubiri, acha niende. Nitakula hukohuko.”
“Hao matajiri zenu wanapenda kuwapa taarifa za ghafla sana. Ilitakiwa wakwambie mapema kuwa utakuwa na safari.”
“Ndiyo kazi zetu zilivyo. Tumeshazoea.”
“Poa. Safari njema.”
Musa alichukua begi lake akatia vitu alivyovitaka kisha akaniaga. Wakati anatoka nikamuuliza:
“Kondomu zako huzihitaji tena?”
Musa aligeuka mara moja akanitazama kisha akasema:
“We’ acha mzaha wako.”
Nilisimama kunako mlango nikamtazama alivyokuwa akitembea kuelekea kwenye kituo cha daladala. Wakati namtazama mawazo ya Mustafa yakaanza kunijia.
Nikarudi ndani na kufunga mlango. Niliketi kwenye sebule nikajiambia kuwa sitapika tena. Nitakwenda kupika kwa Mustafa.
Nilisubiri yapite masaa mawili nikatia baadhi ya vitu vyangu kwenye mkoba wangu kisha nikatoka. Sikuchukua nguo. Nilikwishahamishia kwa Mustafa baadhi ya nguo zangu na viatu. Nilichukua vitu vidogovidogo tu ambavyo Mustafa asingeweza kuvizingatia.
Kabla ya kwenda Mbezi nilipitia sokoni nikanunua vitu ambavyo nilihitaji kupika. Nilipofika Mbezi Mustafa alikuwa hayupo. Kwa vile nilikuwa na funguo zangu nikafungua mlango na kuingia ndani.
Niliingia chumbani nikabadili nguo kisha nikazima simu yangu na kuiweka kwenye chaji ili Mustafa akija aone simu iko kwenye chaji. Sikutaka anipigie wala sikutaka Musa anipigie.
Baadaye nikatoka chumbani na kuelekea jikoni na kuanza kupika.
Yalikuwa majira ya saa kumi na moja Mustafa aliporudi nyumbani na kunikuta nimeketi sebuleni nikiangalia CD ya filamu ya Kihindi.
“Mbona hukunifahamisha kama umeshakuja?” akaniuliza.
“Kwani ulitaka kuleta msichana wako?”
“Mishi acha mzaha wako, una ‘surprise’ za ajabu sana. Halafu nilikupigia ukawa hupatikani.”
“Simu ilikuwa kwenye chaji. Mimi mwenyewe nilikuwa jikoni napika.”
“Kwani ulikuja saa ngapi.”
“Tangu saa sita niko hapa.”
Nilimdanganya. Muda niliofika, saa sita ilikuwa imeshapita.
“Umepika nini?”
“Nimepika wali na nyama.”
Nilipomwambia hivyo Mustafa aliinuka na kuelekea chumbani. Baadaye alirudi tena sebuleni. Alionekana alikuwa anatoka kuoga.
Tukaendelea na mazungumzo.
Kabla ya mwezi mmoja kukamilika Mustafa akaenda India. Alipoondoka tu nikarudi kwa Musa. Musa aliporudi kutoka Burundi alinikuta nipo nyumbani.
Kwa vile safari zake nyingi zilikuwa za Burundi, alipoondoka tena kwenda Burundi nikahamia Mbezi kwa Mustafa. Mustafa alikaa India kwa wiki nzima. Aliporudi alinikuta nipo nyumbani kwake.
Baada ya mwezi mmoja nikajikuta nina mimba. Sikujua ile mimba ilikuwa ni ya nani lakini nilikisia kuwa ilikuwa ya Mustafa. Nikaitambulisha mimba yangu kwa waume wote wawili. Kila mmoja akajua nina mimba na mimba ni yake.
Kwa vile waume wangu wote wawili walikuwa wakisafiri nje ya nchi na wakiwa huko hukaa kwa zaidi ya wiki. Niliendelea kutumia mtindo uleule wa kuhamia kwa mwanaume mmoja pindi mwenzake anaposafiri.
Kwa bahati njema walikuwa wakisafiri kwa nyakati tofauti hivyo kuniwezesha mimi kuweza kuwa kwa mwanaume mmoja pale mwenzake anapokuwa hayupo. Ile mimba iliendelea hadi ikatimiza miezi tisa. Hakukuwa na mwanaume wangu yeyote aliyegundua kuwa mimba hiyo ilikuwa ya watu wawili.
Kuna siku Mustafa alikuwa amekwenda China kununua bidhaa. Lakini Musa alikuwepo na nilikuwa nyumbani kwake. Musa akaniambia kwamba anataka asafiri lakini anasita kwa sababu naweza kuumwa na uchungu wakati wowote na nitakuwa peke yangu.
Wakati akiniambia hivyo Mustafa alishanipigia simu kunijulisha kuwa anarudi kesho yake.
Nikamwambia Musa kuwa anaweza kwenda safari.
“Mimi nitakwenda kwa shangazi.”
“Shangazi ataweza kukuhudumia?” akaniuliza.
“Kwa nini asiweze. Yeye mwenyewe ameniambia niende.”
“Kama ameshakwambia basi unaweza kwenda, acha mimi niende safari.”
Siku ile Musa akaondoka. Sikwenda kwa shangazi. Musa alipoondoka nikaenda Mbezi kwa Mustafa.
Mustafa alirudi siku iliyofuata na siku hiyohiyo nikaumwa na uchungu. Mustafa alinikimbiza na gari hospitali. Nikajifungua usiku mtoto wa kiume. Alikuwa amefanana sana na Mustafa.
Mustafa alikuja hospitali asubuhi akamkuta mtoto ameshazaliwa. Akampa jina hapohapo.
“Mwanangu ataitwa Amani,” akaniambia.
Nikatabasamu na kumuuliza:
“Umempa jina la nani wako?”
“Ni jina la babu yangu mzaa mama yangu,” akaniambia.
Je, nini kiliendelea?