Simulizi ya kweli: Mwanamke jini

Simulizi ya kweli: Mwanamke jini

SEHEMU YA 03




ILIPOISHIA
Nikaangaza macho yangu kumtazama. Nikamkumbuka. Alikuwa ni yule msichana niliyekutana naye sinema siku ile.
“Oh nzuri! Hujambo?” nilijibu salamu yake.
“Sijambo. Leo tumekutana tena”
“Imekuwa kama bahati. Nilikuwa natoka kununua kitabu”
“Mimi pia nimekuja kununua kitabu. Nilikuwa nahitaji kitabu cha “Mashimo Saba ya Malme Suleiman”
“Vimeisha. Kilikuwa kimebaki kimoja tu nilichonunua mimi” nikamwambia.
“Kumbe wewe pia ulikuja kununua kitabu hicho hicho?”
“Nilikuja kununua kitabu hicho”
Nikakitoa kile kitabu na kumuonesha.
Akakishika na kukitazama.
“Una umuhimu nacho sana kwa leo na kesho?” akaniuliza.
“Ni kwa ajili ya kujisomea tu”
“Basi naomba uniazime kwa siku mbili tu halafu nitakurudishia”
Sikuwa na sababu yoyote ya kukataa. Nilihisi yule msichana alikuwa akikihitaji zaidi.
“Nitakuazima, sasa sijui nitakipata vipi?”
SASA ENDELEA
“Keshokutwa nitakuwa majestic Cinema, utakuja?” akaniuliza.
“Ninaweza kuja kwa ajili yako tu”
“Basi njoo usiku saa mbili na nusu hivi utanikuta nakusubiri pale nje”
“Kutakuwa na picha gani?”
“Picha nzuri ya James Bond”
“Inaitwaje?”
“Dk No”
“Inarudia. Nakumbuka Dk No ndio picha ya kwanza ya James Bond, ilitoka kwa mara ya kwanza mwaka 1961”
“Sijui. Mimi sikuwahi kuiona lakini ni ya Seen Conary mwenyewe?”
“Mimi pia sikuwahi kuiona ila niliisikia tu. Mbabe wake ni Seen Conary mwenyewe”
“Nimekuuliza hivyo kwa sababu kuna mtu mwingine anakuja kwenye picha za James Bond anaitwa Roger Moor”
“Ile ni ya Seen Conary si Roger Moor”
“Huyo ndiye ninayemtaka mimi”
“Basi mimi nitafika hapo Majestic Cinema keshokutwa”
“Asante kaka, ngoja niingie humu dukani nione kama nitapata vitabu vingine vya hadithi”
‘Sawa”
Msichana akaingia mle dukani na mimi nikapanda pikipiki yangu na kuondoka.
SASA ENDELEA
Yule msichana alikuwa ameniambia nikutane naye kesho kutwa saa mbili usiku nje ya Majestic Cinema. Ilipofika siku hiyo niliondoka nyumbani kwangu saa mbili usiku kuelekea Majestic Cinema kufuatia kitabu changu. Nilipofika ilikuwa saa mbili na nusu kama tulivyoahidiana na msichana huyo ambaye sikuwahi hata kumuuliza jina lake.
Nikamkuta amesimama mbele ya mlango wa jumba hilo akiwa na mavazi yake yale yale, baibui jeusi la kiiran na hijabu.
“Niko hapa nakusubiri” akaniambia.
“Nimeshakuona”
“Vipi hali yako?”
“Mimi sijambo, sijui wewe”
“Mimi mzima tu, karibu”
“Asante”
Msichana alikuwa ameshika tikiti mbili mkononi. Akanipa tikiti moja.
“Nimekukatia tikiti uingie”
“Mbona mimi sikupanga kuangalia sinema” nikamwambia huku nikipokea ile tikiti.
“Hukupanga? Si nilikwambia juzi…”
“Wewe ndio ulisema utakuja sinema, mimi nilikuwa nije kuchukua kile kitabu tu”
“Kwa vile nimeshakukatia, ingia tu tuangalie pamoja”
Wakati akiniambia hivyo watu walikuwa wanatoka ndani ya jumba hilo. Onesho la jioni lilikuwa limekwisha.
Tulisimama kwa pembeni kuwapisha watu hao, walipomalizika na sisi tukaingia. Tulitafuta siti zetu, tulipozipata tukaketi. Saa tatu kamili trela ikaanza. Baada ya trela kwisha msichana alitoka. Baadaye alirudi akiwa na chupa mbili za soda na pakiti mbili za njugu.
“Chukua’
Akanipa chupa moja ya soda na pakiti moja ya njugu.
“Asante”
Onesho la sinema likaanza. Tukaitazama filamu ya Dk No mwanzo hadi mwisho. Mara kwa mara msichana huyo alikuwa akimshangilia James Bond kutokana na ujanja wake wa kipelelezi. Filamu ilipomalizika tukatoka.
“Si utanipeleka nyumbani?” msichana akaniuliza tulipokuwa nje ya jumba hilo.
“Kitabu kiko wapi?” nikamuuliza.
“Nilikisahau nyumbani, nitakwenda kukupa huko huko”
Nikaguna kimoyomoyo kwa vile ahadi yetu haikuwa hivyo. pikipiki yangu na kuiwasha.
“Panda twende” nikamwambia.
Msichana ambaye alionesha alikuwa mzoevu wa kupanda pikipiki alikaa nyuma yangu akauzungusha mkono wake kwenye tumbo langu. Nikatia gea na kuiondoa pikipiki.
“Unaitwa nani?” Msichana huyo akaniuliza.
“Naitwa Amour na wewe unaitwa nani?”
“Naitwa Zena, unaishi wapi?”
“Ninaishi Mabawa”
“Unafanya kazi wapi?”
“Nafanya kazi shirika la STC”
“Nimefurahi sana kukufahamu Amour”
“Na mimi pia nimefurahi kukufahamu”
Tukaendelea kuzungumza hili na lile mpaka tukafika Mikanjuni. Safari hii alinifikisha hadi katika nyumba aliyokuwa anaishi. Lilikuwa jumba zuri la kifahari. Ingawa eneo hilo lilikuwa giza, jumba hilo lilikuwa linawaka taa ya umeme.
“Mimi naishi hapa” Msichana akaniambia huku akishuka kwenye pikipiki.
Nilikuwa nikilitupia macho lile jumba, nikataka kumuuliza alikuwa amepangisha chumba au alikuwa akiishi kwao. lakini nilishindwa kumuuliza ili asione ninayachunguza maisha yake.
“Nimepaona” nikamjibu.
“Karibu ndani” akaniambia.
“Asante”
“Karibu” Msichana akanisisitizia.
“Hapa panatosha” nikamwambia nikiwa nimekaa kwenye pikipiki yangu.
“Unataka uishie nje, si vizuri. Tuingie ndani. Ninaishi peke yangu tu usiogope”
“Unaishi peke yako humu ndani?” nikamuuliza.
“Nimejenga mwenyewe kutokana na biashara zangu na ninaishi mwenyewe. Msichana aliniambia huku akifungua geti.
“Karibu”
Kwa jinsi alivyokuwa akinibembeleza ilibidi nishuke kwenye pikipiki. Niliposhuka tu msihana aliishika pikipiki yangu akaikokokota na kuiingiza ndani, nikawa namfuata nyuma.
Tulipoingia ndani msichana aliiegesha pikipiki kando ya mti mkubwa uliokuwa umeota katika ua wa jumba hilo. Aliiacha pikipiki akaenda kufunga geti.
“Karibu” akaniambia huku akitangulia kwenda kwenye mlango wa kuingilia kwenye jumba hilo. Nikamfuata.
JAMAA AMESHAINGIA NDANI YA NYUMBA YA MWANAMKE HUYO AMBAYE HAMJUI. Je Nini kitatokea?
 
SEHEMU YA 04


Ilipoishia
Nilikuwa nikilitupia macho lile jumba, nikataka kumuuliza alikuwa amepangisha chumba au alikuwa akiishi kwao. lakini nilishindwa kumuuliza ili asione ninayachunguza maisha yake.
“Nimepaona” nikamjibu.
“Karibu ndani” akaniambia.
“Asante”
“Karibu” Msichana akanisisitizia.
“Hapa panatosha” nikamwambia nikiwa nimekaa kwenye pikipiki yangu.
“Unataka uishie nje, si vizuri. Tuingie ndani. Ninaishi peke yangu tu usiogope”
“Unaishi peke yako humu ndani?” nikamuuliza.
“Nimejenga mwenyewe kutokana na biashara zangu na ninaishi mwenyewe. Msichana aliniambia huku akifungua geti.
“Karibu”
Kwa jinsi alivyokuwa akinibembeleza ilibidi nishuke kwenye pikipiki. Niliposhuka tu msichana aliishika pikipiki yangu akaikokokota na kuiingiza ndani, nikawa namfuata nyuma.
Tulipoingia ndani msichana aliiegesha pikipiki kando ya mti mkubwa uliokuwa umeota katika ua wa jumba hilo. Aliiacha pikipiki akaenda kufunga geti.
“Karibu” akaniambia huku akitangulia kwenda kwenye mlango wa kuingilia kwenye jumba hilo. Nikamfuata.
SASA ENDELEA
Alifungua mlango akanikaribisha tena, tukaingia ndani. Tulitokea kwenye sebule pana iliyokuwa na makochi ya chini chini ambayo hutumiwa zaidi na watu wenye asili ya kiarabu. Ilikuwa sebule iliyonakishiwa na kupendeza.
“Karibu ukae” akaniambia.
Nikaa kaa kwenye kochi mojawapo.
“Nikuletee kinywaji gani, cha moto au cha baridi” akaniuliza.
“Hapana, sihitaji kinywaji chochote” nikamwambia.
Msichana akanitazama na kukunja uso kisha akaondoka hapo sebuleni. Nikajua kuwa amekwenda kunichukulia kitabu changu ili niondoke.
Baadaye kidogo akarudi. Alikuwa ameshika chano kilichokuwa na kijibiika kidogo na vikombe viwili vya kahawa. Chano hicho pia kilikuwa na kisahani kilichokuwa na tende.
Akakiweka chini mbele yangu.
Yeye mwenyewe alikuwa amevua baibui na kubaki na dera la mikono mirefu lililoziba kabisa miguu yake. Dera hilo lilikuwa limedariziwa nyuzi zilizokuwa zikimemeta kama hariri.
Pia alikuwa ameiondoa hijabu na badala yake alijitanda mtandio mwepesi uliokuwa unaonya. Uso wake uliweza kuonekana vizuri. Nywele zake ndefu za maboga kama za kiarabu zilikuwa zimefikia kwenye mabega yake.
“Karibu” akaniambia na kuongeza.
“Kunywa kahawa kidogo. Kahawa inachangamsha”
Sikupenda kuikataa ile takirima ingawa nilimwambia sikuhitaji kinywaji chochote.
Msichana akaketi chini karibu yangu akachukua kile kibirika na kunimiminia kahawa kisha akajimiminia na yeye.
Alichukua kikombe hicho akaionja kahawa kisha akakirudisha chini na kuokota tende moja na kuitia midomoni.
Na mimi niliokota tende kwanza, nikaitia midomoni kisha nikainua kikombe cha kahawa kusukumizia.
“Wewe una asili ya kiarabu?” nikamuuliza.
“Nimechanganya uarabu na uswahili”
‘Muarabu ni baba yako au mama yako?”
“Baba yangu ni muarabu wa Ajemi, mama yangu ndio amechanganya. Zamani tulikuwa tunaishi Zanzibar”
“Sasa wazazi wako wako wapi?” nikamuuliza baada ya kutoa kokwa ya tende mdomoni.
“Iweke hapo kwenye sinia” aliniambia akinionesha kile chano.
Nikaiweka ile kokwa kwenye chano hicho kisha nikaokota tende nyingine.
“Baba yangu yuko Zanzibar na mama yangu yuko Ajemi” akaniambia.
“Kwa hiyo wewe unaishi hapa peke yako?” nikamuuliza.
“Ninaishi peke yangu” Msichana akanikubalia kwa haraka.
“Uliniambia hii nyumba uliijenga mwenyewe kwa biashara zako, unashughulika na biashara gani?”
“Ninauza madini”
“Madini gani?”
“Madini ya kila aina”
“Unayapata wapi?”
“Baba yangu ananiletea kutoka Zanzibar”
“Yeye anayapata wapi?”
Msichana akabetua mabega yake.
“Sijui anayapata wapi”
“Ninavyojua mimi Zanzibar hakuna madini”
“Hayatoki Zanzibar, anayapata kutoka nje ya Zanzibar lakini sio Afrika ila mahali penyewe sipafahamu na hajawahi kuniambia”
“Ndiyo yamekuwezesha kujenga nyumba hii?”
“Ndiyo”
“Hongera sana. Sasa kwanini unaishi peke yako?”
“Sijapata mwenzangu wa kuishi naye”
Kahawa aliyonitilia kwenye kikombe nikaimaliza. Akataka kuniwekea nyingine, nikamwambia.
“Imetosha, asante sana”
“Ngoja nikakuchukulie kitabu chako” akaniambia huku akiinuka. Macho yangu yalimsindikiza hadi alipotoka mlangoni.
Kusema kweli baada ya msichana huyo kuondoka sikujua tena kilichotokea kwani usingizi ulinipitia hapo hapo bila kutarajia. Nikalala fofofo.
Nilipokuja kuzinduka nilijikuta nimekaa peke yangu mahali pale pale nilipokuwa. Kile chano cha kahawa na tende kilikuwa kimeondolewa. Kwa kutaka kujua ilikuwa ni saa ngapi nilitazama saa yangu ya mkononi, nikaona ilikuwa saa tisa kasorobo ya usiku.
Nikashituka sana kuona nilikuwa nimelala nyumbani kwa msichana huyo hadi muda huo. Nikataka kuinuka ili nimuite mwenyeji wangu ambaye sikujua alikuwa wapi.
Kabla ya kuinuka nikaisikia sauti yake ikitoke nje ya dirisha la kile chumba. Kisha nilisikia sauti nyingine ya kiume ikijibishana naye. Sauti ile ya kiume ikanishitua kwa sababu yule mwanamke aliniambia alikuwa akiishi peke yake mle ndani.
Nikapenua pazia nakuchungulia uani. Nikaiona pikipiki yangu niliyokuwa nimeiegesha kando ya mti. Mbele ya pikipiki niliona kitu kama kisima cha maji. Wakati tunaingia mle ndani kisima hicho sikukiona.
Maji yaliyokuwa kwenye kisima hicho yalikuwa mekundu kama damu na yalikuwa yakitoa harufu ya damu ya binaadamu mpaka nikahisi yalikuwa ni damu kweli.
Ndani ya kile kisima kulikuwa na watu wawili waliokuwa wakioga na ndio waliokuwa wakizungumza. Mmoja akatoka na kusimama kando ya kisima hicho. Mara moja nikatambua kuwa ni yule mwenyeji wangu lakini safari hii alikuwa na umbile la kutisha sana.
Kwanza nywele zake zilikuwa nyingi na ndefu zilizoteremka na kumfikia kiunoni. Zilikuwa nywele nyeupe kama mvi za bi kikongwe. Yeye mwenyewe ngozi yake ilibadilika na kuwa nyeupe kama ya mzungu. Macho yake yalikuwa ya kijivu na mboni zake zilikuwa nyembamba na zilizosimama kama mboni za paka.
Bado alikuwa ameota manyoya marefu mwili mzima. Nikagundua kwenye miguu yake hakuwa na vitanga vya miguu kama walivyo binaadamu wote bali alikuwa na kwato nyeusi kama za farasi au punda. Hakuwa amevaa chochote. Alikuwa uchi wa mnyama!
Mwenzake naye akatoka kwenye kisima. Yeye alikuwa mwanaume lakini alikuwa na umbile kama la yule msichana. Miguu yake pia ilikuwa na kwato.
Walikuwa wakizungumza kwa lugha ambayo sikuielewa. Kwa kweli nilishituka sana. Nikapata hofu na uoga mpaka mwili wangu ukawa unatetemeka.
Nikahisii kwamba yule msichana aliyenikarisha mle ndani hakuwa binaadamu bali alikuwa jini na pale alikuwa akizungumza na jini mwenzake.
Nikatengeza mawazo kwamba huenda msichana yule aliniingiza katika nyumba ile kwa hila ili wanidhuru kwani ile damu iliyokuwa kwenye kile kisima ilikuwa ni ya binaadamu kama mimi. Na bila shaka waliingizwa mle ndani na kuuawa kikatili.
Hapo ndipo nilipochanganyikiwa nikajua kwamba dakika zangu za kuishi zilikuwa zimekaribia kwisha.
Itaendelea
 
SEHEMU YA 05

ILIPOISHIA
Ndani ya kile kisima kulikuwa na watu wawili waliokuwa wakioga na ndio waliokuwa wakizungumza. Mmoja akatoka na kusimama kando ya kisima hicho. Mara moja nikatambua kuwa ni yule mwenyeji wangu lakini safari hii alikuwa na umbile la kutisha sana.
Kwanza nywele zake zilikuwa nyingi na ndefu zilizoteremka na kumfikia kiunoni. Zilikuwa nywele nyeupe kama mvi za bi kikongwe. Yeye mwenyewe ngozi yake ilibadilika na kuwa nyeupe kama ya mzungu. Machoyake yalikuwa ya kijivu na mboni zake zilikuwa nyembamba na zilizosimama kama mboni za paka.
Bado alikuwa ameota manyoya marefu mwili mzima. Nikagundua kwenye miguu yake hakuwa na vitanga vya miguu kama walivyo binaadamu wote bali alikuwa na kwato nyeusi kama za farasi au punda. Hakuwa amevaa chochote. Alikuwa uchi wa mnyama!
Mwenzake naye akatoka kwenye kisima. Yeye alikuwa mwanaume lakini alikuwa na umbile kama la yule msichana. Miguu yake pia ilikuwa na kwato.
Walikuwa wakizungumza kwa lugha ambayo sikuielewa. Kwa kweli nilishituka sana. Nikapata hofu na uoga mpaka mwili wangu ukawa unatetemeka.
Nikahisii kwamba yule msichana aliyenikarisha mle ndani hakuwa binaadamu bali alikuwa jini na pale alikuwa akizungumza na jini mwenzake.
Nikatengeza mawazo kwamba huenda msichana yule aliniingiza katika nyumba ile kwa hila ili wanidhuru kwani ile damu iliyokuwa kwenye kile kisima ilikuwa ni ya binaadamu kama mimi. Na bila shaka waliingizwa mle ndani na kuuawa kikatili.
Hapo ndipo nilipochanganyikiwa nikajua kwamba dakika zangu za kuishi zilikuwa zimekaribia kwisha.
SASA ENDELEA
“Nitatokaje humu ndani?” nikajiuliza.
Nililirudisha lile pazia. Nikaenda kwenye mlango na kutoka ukumbini. Ukumbi ulikuwa kiza. Sikuweza kuona kitu. Sikuelekea upande wa uani tulikoingilia, nikalekea mlango wa mbele. Nilitaka nitoka kwa kutumia mlango huo bila Zena na mwenzake kujua. Pikipiki yangu nilikuwa nimeshaisamehe.
Kwa muda ule pikipiki haikuwa na umuhimu kwangu, kilichokuwa muhimu illikuwa ni kujisalimisha roho yangu. Nilijiambia kama nitafanikiwa kutoka mle ndani na kukimbia nitakuwa nimeweza kujisalimisha kuuawa.
Nikawa natembea haraka haraka ili niwahi kutoka kabla sijagunduliwa. Kwa sababu ukumbi ulikuwa kiza nikakumba kitu kama meza iliyokuwa imewekwa ukumbini. Niliikumba kwa nguvu hadi ikatoa mlio wa kuburuzika.
Hapo hapo nikasikia sauti ya Zena ikiuliza.
“Amour unanitafuta?”
Sikujibu kitu, nikaikwepa ile meza na kundelea kwenda mbele sasa kwa haraka zaidi.
“Amour unaondoka?” Sauti ya Zena ikasikika tena.
Sikujibu. Nikaendelea kwenda. Sasa nilikuwa nahema kwa hofu. Mdomo nilikuwa nimeuacha wazi huku mikono yangu ikiwa mbele ili niweze kuugusa mlango nitakapoufikia.
“Amour usiondoke, nisubiri”
Sauti ya Zena ilizidi kunichanganya. Ndani ya moyo wangu nikawa naomba Mungu anisalimishe.
“Yarabi nisitiri…Yarabi nisitiri…”
Mara moja nikaufikia mlango. Nikawa naupapasa haraka haraka mpaka nikaushika ufunguo uliokuwa umeachwa kwenye kitasa, nikaufungua kisha nikauvuta mlango. Mlango haukufunguka.
Nikagundua kuwa kulikuwa na vifungulio vingine vilivyokuwa chini ya na juu ya mlango. Nikapeleka mkono wangu juu na kupapasa. Nikapata kifungulio kimojawapo nikakivuta chini.
“Amour umeona nini?” Sauti ya Zena sasa ikasikika kutokea mlango wa uani.
Bila shaka alikuwa akinichungulia kupitia mlango huo. Sikutaka hata kugeuka nyuma kumtazama. Nikainama chini ili nifungue kifungulio kingine kilichokuwa chini.
“Amour usiondoke!” Zena aliendelea kuniambia.
Aliposikia nafungua kile kifungulio cha mlango cha chini akaniambia.
“Hebu nisubiri”
Sasa nikazisikia hatua zake akinifuata kwa mwendo wa haraka. Kwa vile miguu yake ilikuwa na kwato, kwato hizo zilisikika kama za farasi wa kwenye sinema, “Kwa…kwa…kwa…”
Mwili ukanisisimka. Nikajiambia sasa nakufa.
Nikauvuta mlango. Licha ya kufungua vifungulio vya juu na chini. Mlango haukufunguka.
Kwato za Zena zilikuwa zimeshanikaribia. Akili yangu iliunda picha nikikabwa na mwanamke huyo wa kijini na kunifyonza damu yangu kupitia kenye tundu za pua yangu…
Mkono wa Zena wenye kucha ndefu ukanishika kwenye bega. Nikaukutua…
“We Amour nini…?” akaniambia kwa hamaki baada ya kuukutua mkono wake.
Niliuvuta tena ule mlango kwa nguvu. Safari hii ukafunguka. Zena alikuwa ameshanishika shati kwa nyuma. Nikapiga hatua kutoka nje. Zena akaliachia shati.
“We Amour…utaona!” akaniambia.
Nilikuwa nimeshavuka kizingiti cha mlango.
“Hutakwenda popote” Sauti ya Zena iliyokuwa na hasira ikasikika nyuma yangu.
Wakati napiga hatua kutoka nje niliona nimetokea nje ya ile nyumba lakini Zena aliponiambia “Hutakwenda popote” nikaona nimetokea kwenye eneo jingine ambalo sikulielewa. Lile jumba la Zena sikuliona tena. Nikajiona kama nimo ndani ya pango la kutisha lenye njia nyembamba ya kupita.
Vile nilivyokuwa nakimbia niliendelea kukimbia ndani ya hilo pango nikiifuata ile njia nyembamba. Kwenye kuta za mawe za lile pango kulikuwa kumewekwa mishumaa iliyokuwa inawaka.
Kadiri nilivyokimbia nilikutana na njia zingine zilizonichanganya. Sikuweza kujua nishike njia ipi. Kadhalika kulikuwa na mashimo yaliyokuwa yakifuka moshi. Wakati nakimbia niligundua nilikuwa nikizunguka tu ndani ya pango hilo
kwani nilikuwa nikitokea mahali pale pale nilipoanzia kukimbia.
Nikajaribu kushika njia nyingine ambayo nilihisi ingeweza kunitoa ndani ya pango hilo, nikajikuta nimetokea kwenye mlango kama mlango wa nyumba. Nikaufungua ule mlango na kuchungulia ndani. Nikaona kumesakafiwa na kulikuwa na kuta kama za nyumba. Kuta hizo zilikuwa zimepakwa rangi ya samawati.
Nikaingia ndani na kukutana na hewa safi yenye harufu ya mawaridi. Sasa nilikuwa kwenye ukumbi mpana ambao haukuwa na kitu chochote. Nilitembea kwenye ukumbi huo uliokuwa kimya huku nikiwa nimejaa hofu.
Sikujua nilikuwa nimetokea katika nyumba gani na inayoshi nani. Mazingira yaliyonifikisha hapo yalinifanya nipate hofu. Nilikuta mlango uliokuwa wazi, nikaingia katika huo mlango. Nilimkuta mzee mmoja aliyevaa shuka nyeupe akiwa ameketi kwenye mswala.
Alikuwa amejifunga kilemba kirefu kama muarabu. Mwenyewe pia alionekana kama muarabu. Alikuwa na ndevu ndefu na sharafa.
Wakati naingia katika hicho chumba alichokuwemo, mzee huyo alikuwa ameinama akisoma kitabu. Kitabu chenyewe kilikuwa ni kile nilichomuazima Zena.
Nikasimama mbele yake na kumtazama. Mzee alikuwa akiendelea kufungua karasa.
Nikamuamkia.
“Shikamoo mzee”
Mzee akainua kichwa na kunitazama. Macho yake yalikuwa madogo ya kijivu.
“Marahaba” akaniitikia. Sauti yake ilikuwa na lafidhi ya kiarabu.
“Mzee samahani, naomba msaada wako” nikamwambia.
“Msaada gani?”
“Mimi sijui nilivyofika hapa, ninaomba unioneshe njia ya kutoka nje”
“Unasema hujui ulivyofika hapa?”
“Sijui, nimejiona tu nikitokea katika nyumba hii”
“Kwani unatoka wapi?”
“Ninatoka katika nyumba ya msichana mmoja ambaye nilimuazima kitabu changu, wakati ule natoka nikaona nimetokea kwenye pango. Baadaye tena naona nimetokea kwenye nyumba hii”
“Wakati unatoka ulimuaga mwenyeji wako?”
“Sikumuaga”
“Kwanini hukumuaga?”
Hapo nikanyamaza kimya, sikuwa na jibu. Nilishindwa kumueleza niliyoyaona kwa sababu yule mzee naye sikujua alikuwa ni nani.
Pakapita kimya cha sekunde kadhaa. Yule mzee alikuwa akinitazama akisubiri jibu langu na mimi nilikuwa nikimtazama uso wangu ukiwa umenywea ukionesha sikuwa na jibu.
“Ulifanya kosa kutomuaga mwenyeji wako na ndio sababu unahangaika. Siku nyingine usirudie kosa kama hilo” Yule mzee akaniambia.
Akanyamaza kimya kisha akanimabia.
JAMAA HAJIELEWI YUKO WAPI. JE HUYO MZEE NI NANI NA ATAMWAMBIA NINI JAMAA HUYO? WEWE UNAFIKIRI KITU GANI KITAMTOKEA JAMAA HUYO
 
SEHEMU YA 06

ILIPOISHIA
“Mzee samahani, naomba msaada wako” nikamwambia.
“Msaada gani?”
“Mimi sijui nilivyofika hapa, ninaomba unioneshe njia ya kutoka nje”
“Unasema hujui ulivyofika hapa?”
“Sijui, nimejiona tu nikitokea katika nyumba hii”
“Kwani unatoka wapi?”
“Ninatoka katika nyumba ya msichana mmoja ambaye nilimuazima kitabu changu, wakati ule natoka nikaona nimetokea kwenye pango. Baadaye tena naona nimetokea kwenye nyumba hii”
“Wakati unatoka ulimuaga mwenyeji wako?”
“Sikumuaga”
“Kwanini hukumuaga?”
Hapo nikanyamaza kimya, sikuwa na jibu. Nilishindwa kumueleza niliyoyaona kwa sababu yule mzee naye sikujua alikuwa ni nani.
Pakapita kimya cha sekunde kadhaa. Yule mzee alikuwa akinitazama akisubiri jibu langu na mimi nilikuwa nikimtazama uso wangu ukiwa umenywea ukionesha sikuwa na jibu.
“Ulifanya kosa kutomuaga mwenyeji wako na ndio sababu unahangaika. Siku nyingine usirudie kosa kama hilo” Yule mzee akaniambia.
SASA ENDELEA
Akanyamaza kimya kisha akanimabia.
“Mlango huu hapa, nenda zako”
Alinionesha mlango uliokuwa ubavuni kwake.
“Asante sana, nashukuru” nikamwambia huku nikivuta hatua kuelekea kwenye mlango huo.
Mzee alikuwa akinitazama.
Niliufungua ule mlango nikatazama nje na kutoka. Nilipotoka nikajiona niko nje ya nyumba ya Zena! Jambo hilo lilinipa mshangao lakini nilishukuru nikaanza kutoka mbio nikiwa pekupeku. Sikukumbuka tena ile pikipiki yangu.
Nilikimbia kwa miguu nikiwa peke yangu usiku ule katika njia iliyokuwa na vichaka vinavyotisha. Vivuli vya miti iliyokuwa ikitikiswa na upepo vilizidi kunitisha lakini sikuwa na la kufanya, nilikuwa nimeshajitolea.
Baada ya nusu saa nikawa nimefika kwenye barabara ya lami nikakata kushoto na kuendelea kukimbia. Nilipokuwa ninakikaribia kituo cha polisi cha Mabawa nikaanza kuchoka. Nguvu zilikuwa zimeniishia kabisa.
Nilisimama huku nikitweta. Nikatazama nyuma. Kulikuwa kimya. Kile kituo cha polisi kilinipa matumaini nikaanza kutembea taratibu. Nilikipita kituo hicho nikaendelea kutembea hadi nikafika nyumbani kwangu.
Nilifungua mlango nikaingia nyumbani kwangu. Mwili wote ulikuwa unaniuma. Shati langu lilikuwa limeloa kwa jasho. Nilivua nguo nikaenda kuoga. Niliporudi chumbani kwangu nikasikia dirisha langu linagongwa.
Nilikuwa nimeshazima taa na kupanda kitandani. Nikatega masikio yangu kusikiliza. Dirisha liliendelea kugongwa.
“Amour! Amour!” Sauti ya kiume ikawa inaita jina langu.
Nilijaribu kuifikiria ilikuwa sauti ya nani lakini sikuweza kutambua ilikuwa sauti ya nani miongoni mwa watu niliokuwa nawafahamu. Nikaamua kunyamaza kimya.
Sauti ile ikaendela.
“Amour fungua mlango nimekuletea viatu vyako na funguo za pikipiki yako”
Nilishituka niliposikia maneno yale nikajua mtu aliyekuwa akiniita alitoka kule kwa Zena ambako niliacha pikipiki yangu na viatu vyangu.
Nikajiambia kwa vyovyote vile atakuwa si mtu bali ni jini. Hofu yangu ilianzaa tena upya. Moyo ukaanza kunienda mbio.
Dirisha liliendelea kugongwa na ile sauti ikaendelea kuniambia nifungue mlango nichukue viatu vyangu pamoja na funguo za pikipiki yangu niliyoiacha kwa Zena.
Sikujibu chochote, nikaendelea kubaki kimya.
Baada ya muda kidogo ile sauti ikapotea, kukawa kimya. Nikasubiri kuona kama kutatokea kitu chochote, sikuona kitu. Nikaendelea kuwa macho huku hofu ikiwa imenitawala hadi nikapitiwa na usingizi.
Nilichelewa sana kuamka asubuhi. Nilishukuru kuwa ilikuwa ni jumapili siku ambayo ni ya mapumziko, vinginevyo ningechelewa kufika kazini.
Mara tu niliposhuka kitandani nilitazama saa. Ilikuwa saa mbili na robo. Nikatoka nje nikiwa nimejifunga taulo. Wakati nafungua mlango wa mbele nikaona viatu vyangu nilivyoviacha kwa yule msichana, vimewekwa mbele ya mlango wangu pamoja na funguo za pikipiki yangu. Nikashituka.
Wakati huo mpangaji mwenzangu wa upande wa pili alikuwa anatoa pikipiki yake. Nikamuita.
“Alphonce!”
Alphonce akanifuata na kunisalimia.
“Kuna tatizo limenitokea” nikamwambia.
“Tatizo gani?” akaniuliza.
“Unaviona hivi viatu?”
“Ninaviona”
“Sasa njoo ndani nikueleze mkasa ulionitokea jana usiku”
Alphone akiwa amepatwa na mshangao aliigesha pikipiki yake karibu na mlango wangu akaingia ndani. Nilimkaribisha sebuleni kwangu. Vile viatu na funguo za pikipiki yangu nilikuwa nimeviondoa pale mlangoni.
“Haya nieleze kuna nini?” Alphonce akaniuliza.
Nikamueleza ule mkasa ulionitokea usiku uliopita uliosababisha nirudi nyumbani kwangu usiku nikiwa pekupeku.
“Wakati nimerudi niko chumbani kwangu, nikasikia sauti ya mtu kwenye dirisha akiniambia ameniletea viatu vyngu na funguo za pikipiki. Kwa kweli sikumjibu. Nilinyamaza kimya”
Wakati ninamueleza Alphonce alikuwa ameshangaa kweli kweli.
“Halafu ikawaje?” akaniuliza.
“Baada ya kunyamaza kimya ile sauti sikuisikia tena, sasa hii leo asubuhi nafungua mlango nakuta viatu vyangu na funguo za pikipiki yangu vimewekwa mbele ya mlango wangu”
“Una maana yule mwanamke alikuwa ni jini?”
“Alikuwa jini”
“Na huyo aliyekuletea hivyo viatu na funguo ni nani?”
“Sijui, lakini watakuwa ni wamoja”
“Unajua mimi huwa nazisikia habari za majini lakini siamini kama kuna viumbe hao. Unaonaje kama tutakwenda mimi na wewe kwenye hiyo nyumba?’
“Mimi nilikuwa nimepanga kwenda polisi kwa sababu ya pikipiki yangu”
“Twende huko Mikanjuni kwanza, kama pikipiki yako hutaipata ndio utakwenda polisi kwa ajili ya kupata msaada zaidi”
“Sawa. Subiri nivae tutoke”
“Nitakusubiri”
Nikanyanyuka na kuingia chumbani kwangu. Baada ya nusu saa nikatoka nikiwa nimeshavaa.
“Twende” nikamwambia Alphonce.
Tukatoka. Alphonce alinipakia kwenye pikipiki yake tukaelekea Mikanjuni. Nilimuelekeza mahali ilikokuwa ile nyumba ya yule msichana, tukaenda hadi mahali hapo lakini jambo la ajabu lililotokea ni kuwa ile nyumba hatukuiona. Badala yake tuliona eneo lote lilikuwa makaburi matupu ya watu wa zamani.
Nikapatwa na mshangao. Wakati naangalia angalia nikaiona pikipiki yangu ikiwa kando ya mti. Mti huo ndio ule uliokuwa uani mwa nyumba ya Zena. Kando yake palikuwa na kisima ambacho yule msichana na mwenzake walikuwa wakioga.
Wakati ule kile kisima hakukuwepo tena, badala yake tuliona dimbwinl maji ya mvua.
“Pikipiki yangu ile pale!” nikamwambia Alphonce ambaye naye alikuwa ameshangaa.
“Sasa mbona iko kwenye makaburi na hapana nyumba?” akaniuliza.
“Na mimi ndio nashangaa. Ile pikipiki niliiweka uani mwa hiyo nyumba niliyokwambia. Ule mti unaouona ulikuwa uani na lile dimbwi la maji kilikuwa ni kisima”
“Hebu twende pale karibu”
JE WAKIFIKA HAPO KARIBU WATAONA NINI?
 
SEHEMU YA 07


ILIPOISHIA
Nikanyanyuka na kuingia chumbani kwangu. Baada ya nusu saa nikatoka nikiwa nimeshavaa.
“Twende” nikamwambia Alphonce.
Tukatoka. Alphonce alinipakia kwenye pikipiki yake tukaelekea Mikanjuni. Nilimuelekeza mahali ilikokuwa ile nyumba ya yule msichana, tukaenda hadi mahali hapo lakini jambo la ajabu lililotokea ni kuwa ile nyumba hatukuiona. Badala yake tuliona eneo lote lilikuwa makaburi matupu ya watu wa zamani.
Nikapatwa na mshangao. Wakati naangalia angalia nikaiona pikipiki yangu ikiwa kando ya mti. Mti huo ndio ule uliokuwa uani mwa nyumba ya Zena. Kando yake palikuwa na kisima ambacho yule msichana na mwenzake walikuwa wakioga.
Wakati ule kile kisima hakukuwepo tena, badala yake tuliona dimbwinl maji ya mvua.
“Pikipiki yangu ile pale!” nikamwambia Alphonce ambaye naye alikuwa ameshangaa.
“Sasa mbona iko kwenye makaburi na hapana nyumba?” akaniuliza.
“Na mimi ndio nashangaa. Ile pikipiki niliiweka uani mwa hiyo nyumba niliyokwambia. Ule mti unaouona ulikuwa uani na lile dimbwi la maji kilikuwa ni kisima”
“Hebu twende pale karibu”
SASA ENDELEA
Tukaenda hadi pale ilipokuwa pikipiki yangu. Karibu yake palikuwa na kaburi la zamani. Lilikuwa limejengewa kiukuta kilichoandikwa jina la Zena binti Ashraf.
Tarehe aliyokufa pia iliandikwa pamoja na tarehe aliyozikwa. Alikufa tarehe kumi mwezi wa kwanza mwaka 1920.
“Yule msichana aliniambia anaitwa Zena na hili kaburi lina jina la Zena, sasa hata sielewi” nikasema.
Nikamsikia Alphonce akitoa mguno. Hakusema chochote. Nikaiangalia pikipiki yangu.
“Ichukue tuondoke, huku Tanga kuna mambo ya ajabu sana”
Nikatia ufunguo na kuikokota hadi kwenye barabara ya vumbi. Nilipoiwasha ikawaka.
“Twenzetu” Alphonce akaniambia huku akipanda pikipiki yake.
Nikapanda pikipiki yangu, tukaondoka.Tukiwa njiani tunarudi tulikuwa tunazungumza.
“Jana ulikunywa pombe?” Alphonce akaniuliza.
“Mimi situmii ulevi wa aina yoyote”
“Sasa ilikuwaje, wewe umeniambia uliingia katika nyumba lakini pale ni makaburini?”
“Yaani pamebadilika. Ilikuwa ni nyumba. Yale makaburi hayakuwepo, ndio nayaona sasa”
“Ni miujiza mikubwa lakini shukuru Mungu umenusurika na pikipiki yako umeipata”
“Aisee nashukuru sana. Na yule mwanamke nikimuona nitamkimbia mbali sana. Sitataka anikaribie, anaweza kutoa roho yangu”
“Mimi sasa naamini kweli majini wapo na wanajigeuza binaadamu”
Tulipofika Mabawa mimi nilielekea nyumbani kwangu, Alphonce akaenda kwenye shughuli zake.
Siku ile nilishinda nikiwa na mawazo ya yule msichana. Kwa kweli alikuwa amenitia hofu sana. Sikutaka nikutane naye tena. Ili kujiondoa wasi wasi niliwaeleza mkasa ule watu mbali mbali niliokuwa nawafahamu akiwemo kaka yangu. Wote walinipa matumaini wakaniambia hakutakuwa na madhara yoyote yatakayonitokea.
Baada ya wiki mbili nilikuwa narudi nyumbani kwangu kutoka kazini. Nilikuwa naendesha pikipiki yangu taratibu. Tukio lile la wiki mbili zilizopita nilikuwa nimeshaanza kulisahau.
Wakati nikiwa katika barabara ya Pangani nikikaribia kwenye mzunguko wa barabara nne uliokuwa eneo la mabanda ya papa nikamuona msichana amesimama kando ya barabara akinipungia mkono. Nilipomtupia macho mara moja nikatambua alikuwa ni Zena! Moyo ulinishituka sana.
Hapo hapo nikaongeza mwendo. Nilitakiwa nisimame kwenye mzunguko huo wa barabara nne uliokuwa mbele yangu. Lakini sikusimama. Gari lililokuwa linakuja kutoka upande wangu wa kushoto ambalo nilitakiwa nilipishe lilinikwepa na kwenda kugonga nguzo ya umeme na kisha kuingia kwenye mfereji wa maji ya mvua.
“Nguzo hiyo iling’oka, waya za umeme zikatikisika na kutoa cheche za moto. Mimi nikaendelea kwenda mbio na kushika barabara ya Pangani kabla ya kuingia katika eneo nililokuwa ninaishi.
Nilipofika nyumbani niliingiza pikipiki yangu ndani nikakaa sebuleni na kuanza kuwaza. Nilijua kuwa nilikuwa nimesababisha ajali kutokana na kuvunja sheria za barabarani baada ya kumuona yule msichana.
Kwa vile nilikuwa na hakika kwamba namba za usajili za pikipiki yangu zilionekana, nilijiambia sitaitimia tena pikipiki yangu hadi lile tukio litakaposahalika.
Zikapita tena wiki mbili. Nilikuwa siitumii tena ile pikipiki yangu kwa kuogopa kukamatwa na polisi. Siku hiyo nilikuwa niko kazini nikawaona polisi wawili wa usalama barabarani wakiingia. Mfanyakazi wa kwanza waliyekutana naye niikuwa mimi.
Wakanisalimia na kuniambia walikuwa wanamtaka Amour.
Amour nilikuwa ni mimi.
Nikasita kuwajibu. Badala yake nikawauliza.
“Amour nani?”
“Hatujui anaitwa Amour nani, kwani hapa kuna Amour wangapi?”
“Kuna Amour mmoja tu”
“Yuko wapi?”
“Ni mimi”
“Sasa mbona hutuambii, unatuuliza maswali. Pikipiki yako iko wapi?”
“Mmejuaje kama nina pikipiki”
“Tumeelekezwa. Tafadhali tuambie”
“Iko nyumbani”
“Ina namba hizi?”
Polisi huyo alinionesha kikaratasi kilichokuwa kimeandikwa namba za usajili za pikipiki yangu.
“Ndiyo” nikamkubalia polisi huyo baada ya kukiangalia kile kikaratasi.
“Tunakuhitaji wewe na hiyo pikipiki yako”
“Mimi nina nini na pikipiki yangu ina nini?” nikawauliza.
“Uliwahi kufanya makosa ya barabarani wiki mbili zilizopita”
“Sijawahi kufanya kosa lolote labda mmeifananisha pikipiki yangu”
“Tutajua huko kituo cha polisi. Kwa sasa tutaondoka na wewe twende nyumbani kwako tuichukue hiyo pikipiki, twende nayo kituo cha polisi”
Sikuwa na la kupinga. Nikakakamatwa. Polisi hao ambao walikuja na gari lao walinipakia kwenye gari hilo, nikaenda nao nyumbani kwangu.
Niliwatolea pikipiki yangu, walipoiona tu wakasema ndiyo waliyokuwa wanaitafuta kwa karibi wiki mbili.
Nikafikishwa kituo cha polisi. Huko ndiko nilikoelezwa kuwa tarehe fulani siku fulani nilisababisha ajali eneo la Mabanda ya Papa baada ya kuendesha pikipiki kwa uzembe na kuvunja sheria za barabarani.
Nikaelezwa kuwa kutokana na uzembe wangu wa kutosimama mahali ambapo nilipaswa kusimama ili nipishe gari lililokuwa linatoka kuliani kwangu, nilisababisha gari hilo aina ya Toyota Landa Cruiser linikwepe na kugonga nguzo ya umeme na kutumbukia kwenye mfereji.
Ingawa nilijitahidi kukana kosa hilo nilifikishwa mahakamani baada ya kulala ndani kwa siku moja. Katika mahakama ya Chumbageni nikashitakiwa kwa makosa matatu.
Kosa la kwanza lilikuwa kuendesha kwa uzembe, kosa la pili kusababisha ajali na kosa la tatu kuharibu mali na kulitia hasara shirika la Umeme iliyokadiriwa kufikia shilingi milioni kumi na mbili.
Niliyakana mashitaka yote na kumuomba hakimu anipe dhamana. Ndugu zangu walikuwa wamejitokeza kutaka kuniwekea dhamana.
HAYA JAMANI MNAYAONA MAMBO HAYO! NI MAKUBWA. SIJUI KAMA JAMAA ATAPEWA DHAMANA.
 
SEHEMU YA 08



ILIPOISHIA
Polisi huyo alinionesha kikaratasi kilichokuwa kimeandikwa namba za usajili za pikipiki yangu.
“Ndiyo” nikamkubalia polisi huyo baada ya kukiangalia kile kikaratasi.
“Tunakuhitaji wewe na hiyo pikipiki yako”
“Mimi nina nini na pikipiki yangu ina nini?” nikawauliza.
“Uliwahi kufanya makosa ya barabarani wiki mbili zilizopita”
“Sijawahi kufanya kosa lolote labda mmeifananisha pikipiki yangu”
“Tutajua huko kituo cha polisi. Kwa sasa tutaondoka na wewe twende nyumbani kwako tuichukue hiyo pikipiki, twende nayo kituo cha polisi”
Sikuwa na la kupinga. Nikakakamatwa. Polisi hao ambao walikuja na gari lao walinipakia kwenye gari hilo, nikaenda nao nyumbani kwangu.
Niliwatolea pikipiki yangu, walipoiona tu wakasema ndiyo waliyokuwa wanaitafuta kwa karibi wiki mbili.
Nikafikishwa kituo cha polisi. Huko ndiko nilikoelezwa kuwa tarehe fulani siku fulani nilisababisha ajali eneo la Mabanda ya Papa baada ya kuendesha pikipiki kwa uzembe na kuvunja sheria za barabarani.
Nikaelezwa kuwa kutokana na uzembe wangu wa kutosimama mahali ambapo nilipaswa kusimama ili nipishe gari lililokuwa linatoka kuliani kwangu, nilisababisha gari hilo aina ya Toyota Landa Cruiser linikwepe na kugonga nguzo ya umeme na kutumbukia kwenye mfereji.
Ingawa nilijitahidi kukana kosa hilo nilifikishwa mahakamani baada ya kulala ndani kwa siku moja. Katika mahakama ya Chumbageni nikashitakiwa kwa makosa matatu.
Kosa la kwanza lilikuwa kuendesha kwa uzembe, kosa la pili kusababisha ajali na kosa la tatu kuharibu mali na kulitia hasara shirika la Umeme iliyokadiriwa kufikia shilingi milioni kumi na mbili.
Niliyakana mashitaka yote na kumuomba hakimu anipe dhamana. Ndugu zangu walikuwa wamejitokeza kutaka kuniwekea dhamana.
SASA ENDELEA
Hakimu aliruhusu dhamana iliyokuwa na masharti magumu. Hata hivyo ndugu zangu walimudu masharti yote waliyopewa wakanitoa.
Shauri hilo lilikuwa limeahirishwa kwa wiki moja. Nilipoachiwa kwa dhamana ndugu zangu walinipeleka nyumbani kwa mama yetu ambaye wakati huo alikuwa yuko hai. Nikawaeleza mkasa uliokuwa umenitokea kuanzia kisa kile cha Zena aliponipeleka nyumbani kwake hadi siku ile nilipomuona tena na kusababisha ile ajali.
Mama yangu na ndugu zangu walishangaa waliposikia kisa hicho.
“Inabidi uende kwa mganga, huyo jini atakuletea matatizo” Mama akaniambia.
“Tatizo la Amour nikuwa ana usiri sana, kwanini hakutueleza tangu mapema?” kaka yangu akanilaumu.
“Sikujua kama yangekuwa makubwa kiasi hiki?’ nikajitetea.
Jioni ya siku ile nikapelekwa kwa mganga mmoja aliyekuwa akiishi Mnyanjani. Nilikuwa mimi, mama yangu na kaka Abdul.
Tukamueleza mganga tatizo langu. Mganga akatazama ramli kisha akatuambia.
“Amour amekumbwa na jini anaitwa Ummi Subian, ni jini wa kike ambaye amemfanyia vitisho na kumsababishia kukabiliwa na kesi”
“Huyo jini ataendelea kumfuata tena?’ Mama yangu akamuuliza mgamga.
“Alilolitaka huyo jini ameshalipata, hatamfuata tena kwa sababu anajua atafungwa. Hii kesi imemkalia vibaya” Mganga akasema.
“Sasa tunataka kuizima hii kesi, itawezekana?’ Abdul akamuuliza mganga.
“Itawezekana. Hakuna kisichowezekana”
“Tunataka utufanyie hiyo kazi, itagharimu shilingi ngapi?”
“Itgharimu shilingi laki moja na mbuzi mweusi”
“Punguza kidogo. Shilingi laki moja hatuna”
“Sipunguzi. Kama nilivyowambia hii kesi imekaa vibaya. Kazi inayotakiwa ni kubwa”
“Haya, tutatoa hiyo shilingi laki moja”
“Ninataka na mbuzi mweusi na kipande cha kaniki. Siku muafaka wa kazi yenu ni jumamosi”
“Kwa hiyo tuje jumamosi” Abdul akamuuliza.
“Mje siku ya jumamosi saa mbili asubuhi pamoja na hivyo vitu”
“Sawa. Tumekuelewa.
Tukaondoka.
Siku ya jumamosi tukaenda tena kwa mganga huyo. Tulienda na gari aina ya Toyota ya wazi. Tulikuwa tumepakia mbuzi tuliyekuwa tumeagizwa.
Tulipofika, wasaidizi wa mganga huyo walitupokea tukakaribishwa ndani. Baada ya muda kidogo mganga akaanza kazi. Kazi ilianzia pale nyumbani kisha ikahamia makaburini.
Yule mbuzi alichinjwa akavalishwa ile kaniki na kuzikwa kwenye kaburi.
Mganga akatuambia.
“Kesi nimeshaizika”
“Sasa nitaachiwa au..” nikamuuliza.
“Utakwenda kusikia huko huko lakini kwa upande wangu hakuna kesi tena”
“Tunashkuru kama itakuwa hivyo” Mama akamwambia mganga.
Tuliporudi nyumbani kwa mganga tulimpa ile shilingi laki moja aliyotaka tukaondoka.
Nilipata matumaini sana, ingawa sikuwa na uzoevu na mambo ya kwenda kwa waganga. Tarehe ya kesi ilipowadia nilifika mahakamani nikasomewa tena mashitaka yangu, nikayakana.
Hakimu akasema alikuwa tayari kuanza kusikiliza shauri hilo. Upande wa mashitaka ukaeleza kwamba ulikuwa na mashahidi ambao walikuwa tayari kutoa ushahidi wao.
Hakimu akataka mashahidi hao waanze kuitwa ili watoe ushidi wao.
Akaitwa shahidi wa kwanza ambaye ni dereva wa Toyota iliyogonga nguzo ya umeme.
Akaeleza jinsi tukio zima lilivyotokea.
Baada ya kumaliza kutoa ushidi wake ikafika zamu yangu ya kumuuliza maswali.
“Unamjua huyo mtu aliyekuwa akiendesha hiyo pikipiki?” nikamuuliza.
“Ninamjua” akajibu.
“Ni nani?”
“Ni wewe”
“Nani alikwambia kwamba ni mimi?”
“Nilikuona mwenyewe”
“Ulipata muda gani wa kuniona na kunikariri wakati umesema gari lako liliingia kwenye mfereji na mimi nilikimbia?”
“Nilikuona kabla”
“Sasa mimi nakwambia siye huyo mtu, mmenifananisha tu”
“Ni wewe”
Baada ya mtu huyo kutoa ushahidi wake aliitwa shahidi mwingine, muuza machungwa katika eneo la Mabanda ya Papa.
Kumbe yeye ndiye aliyekuwa amewatajia polisi namba za pikipiki yangu. Siku ile ya ajali aliniona na aliiona pikipiki yangu. Akaieleza mahakama kuwa amekuwa akiniona mara kwa mara nikipita na pikipiki katika eneo lile.
Huku akiongozwa na Mwendesha Mashitaka wa serikali shahidi huyo aliiambia mahakama kuwa siku na tarehe hiyo alikuwa akiuza machungwa yake jirani na Barabara ya Pangani katika eneo hilo la Mabanda ya Papa.
“Nini kilitokea?” Mwendesha Mashitaka akamuuliza.
“Ilitokea ajali”
“Ilitokea ajali gani? Hebu tueleze”
“Kulikuwa na pikipiki moja inakuja kutoka barabara ya Taifa. Ile pikipiki ilitakiwa isimame kwenye mzunguko wa barabara nne uliopo pale lakini haikusimama”
“Baada ya hapo nini kilitokea?’
“Kulikuwa na gari aina ya Toyota Land Cruicer likitokea Gofu, lilikuwa linapita kwenye ule mzunguko likalazimika kuikwepa ile pikipiki. Katika kuikwepa pikipiki, gari hilo lilikwenda kugonga nguzo ya umeme”
“Baada ya kugonga nguzo ya umeme lilikwenda wapi?”
“Liliingia kwenye mfereji”
“Ni athari gani ilitokea baada ya nguzo ya umeme kugongwa?”
“Kwanza nguzo yenyewe ilivunjika halafu baadhi ya nyaya zilikatika na nyingine zilitoa cheche za moto hali iliyosababisha mfadhaiko mkubwa”
“Wakati tukio hilo linatokea, mwenye pikipiki alisimama”
“Hapana, hakusimama. Alipita moja kwa moja na kuendelea na safari yake”
“Wewe uliiona hiyo pikipiki?’
“Ndiyo niliiona”
“Ilikuwa ni aina gani”
“Kama sikosei ilikuwa aina ya Honda ya rangi nyeusi”
“Namba yake ya usajili uliiona”
“Niliiona”
Akaitaja. Ilikuwa ndio namba ya pikipiki yangu.
DUH! JAMAA NDIO AMEKWISHA! HEBU FUATILIA HAPO KESHO UJUE NINI KITATOKEA?
 
SEHEMU YA 09


ILIPOISHIA
“Kulikuwa na pikipiki moja inakuja kutoka barabara ya Taifa. Ile pikipiki ilitakiwa isimame kwenye mzunguko wa barabara nne uliopo pale lakini haikusimama”
“Baada ya hapo nini kilitokea?’
“Kulikuwa na gari aina ya Toyota Land Cruicer likitokea Gofu, lilikuwa linapita kwenye ule mzunguko likalazimika kuikwepa ile pikipiki. Katika kuikwepa pikipiki, gari hilo lilikwenda kugonga nguzo ya umeme”
“Baada ya kugonga nguzo ya umeme lilikwenda wapi?”
“Liliingia kwenye mfereji”
“Ni athari gani ilitokea baada ya nguzo ya umeme kugongwa?”
“Kwanza nguzo yenyewe ilivunjika halafu baadhi ya nyaya zilikatika na nyingine zilitoa cheche za moto hali iliyosababisha mfadhaiko mkubwa”
“Wakati tukio hilo linatokea, mwenye pikipiki alisimama”
“Hapana, hakusimama. Alipita moja kwa moja na kuendelea na safari yake”
“Wewe uliiona hiyo pikipiki?’
“Ndiyo niliiona”
“Ilikuwa ni aina gani”
“Kama sikosei ilikuwa aina ya Honda ya rangi nyeusi”
“Namba yake ya usajili uliiona”
“Niliiona”
Akaitaja. Ilikuwa ndio namba ya pikipiki yangu.
SASA ENDELEA
“Je aliyekuwa akindesha pikipiki hiyo ukimuona unaweza kumtambua?”
“Naweza kumtambua”
“Yuko hapa mahakamani?”
“Ndiyo yupo. Ni yule pale”
Akaninyooshea kidole mimi.
“Asante sana”
Baada ya mtu huyo kumaliza kutoa ushahidi wake, niliambiwa kama nina maswali nimuulize.
“Unajua hapa Tanga kuna pikipiki ngapi za aina ya Honda?” nikamuuliza.
“Ziko nyingi”
“Ambazo ni rangi nyeusi kama pikipiki yangu?’
“Ziko nyingi”
“Unawezaje kuzitofautisha?”
“Kivipi?”
“Nina maana una uhakika gani kama pikipiki ulioiona ni yangu na si ya mtu mwingine?’
“Wewe unapita pale kila siku na pikipiki yako. Pikipiki yako ninaijua na wewe mwenyewe ninakujua”
“Je nikikwambia kwamba sikuwa mimi bali alikuwa mtu mwingine utakataa?’
“Ndiyo nitakataa”
“Sasa mimi nakwambia sikuwa mimi?”
“Alikuwa nani?”
“Sijui”
Yule mtu akanyamaza.
Mwendesha Mashitaka akasimama na kumuuliza yule mtu.
“Mtu uliyemuona siku hiyo ndiye huyo hapo au siye?”
“Ndiye yeye” shahidi akajibu.
Mwendesha Mashitaka kakaa.
Kesi ikaahirishwa kwa juma moja.
Kipindi kile cha kesi ile kilinifanya niwe mnyonge sana. Nilijiuliza kama nitatakiwa nilipe faini au fidia ya uharibifu uliotokea, nitalipa nini? Kwa vile uharibifu ulikuwa mkubwa niliamni fidia yake pia itakuwa kubwa. Nilijiuliza nitapata wapi pesa za kulipa fidia hiyo ambayo kwa vyovyote vile ingekuwa ni mamilioni ya pesa.
Kila wakati nilikuwa nikimlaani yule msichana wa kijini aliyenisababishia matatizo yale. Niliomba nisikutane naye tena milele na milele.
Siku ya kesi ilipowadia nillifika mahakamani. Upande wa Mashitaka uliendelea kupeleka mashahidi. Safari hii aliyesimamishwa kizimbani kutoa ushahidi alikuwa polisi wa usalama barabarani aliyepima ile ajali iliyotokea.
Alitoa vielelezo yake ikiwa ni pamoja na ramani ya ajali aliyokuwa ameichora.
Ramani hiyo ilionesha kuwa nilifanya kosa la kutosimama katika alama ya L iliyokuwa kwenye mzunguko wa barabara nne uliopo eneo la Mabanda ya Papa.
Ramani hiyo iliendelea kuonesha kwamba wakati nafanya kosa hilo kulikuwa na gari aina ya Toyota Land Cruiser likitokea upande wangu wa kulia ambalo nilipaswa kulipisha lipite lakini sikufanya hivyo.
Hivyo gari hilo lililazimika kunikwepa na kwenda kugonga nguzo ya umeme inayomilikiwa na shirika la umeme na kuivunja.
Katika ushidi wake polisi huyo alieleza kwamba nguzo ya umeme niliyoivunja pamoja na nyaya zilizokatika zina thamani ya shilingi milioni kumi.
Akaeleza kwamba ili kurudisha mfumo wa upatikanaji umeme katika eneo hilo shirika la umeme litalazimika kutoa shilingi milioni kumi na tatu ikiwa ni pamoja na gharama ya ufundi.
“Pesa hizo zitapaswa zilipwe na mshitakiwa kwa sababu alifanya kosa hilo kwa uzembe na kutozingatia sheria za barabarani” akasema.
Hapo ndipo moyo wangu ulipotaharuki. Nitazitoa wapi shilingi milioni kumi na tatu za kuwalipa shirika la umeme? Nikajiuliza.
Polisi huyo alipomaliza kutoa ushahidi wake, hakimu aliniambia kama nina swali nimuulize.
Nilikuwa nimefadhaika sana kiasi kwamba sikuweza kuuliza swali lolote lakini niliona kukaa kimya kutaionesha mahakama kuwa kweli nilitenda kosa, nikamuuliza polisi huyo.
“Hiyo ramani uliyoitoa aliichora nani?”
“Niliichora mimi”
“Unapochora ramani ya ajali kama ile unapata maelezo kutoka kwa nani?”
“Kutoka kwa wale wahusika wa ajali na mashahidi”
“Kwa maoni yako mimi ni muhusika wa ajali?’
“Ndiyo”
“Nilikuwepo wakati unachora ramani hiyo?”
“Hukuwepo”
“Je niliweka saini yangu kuonesha kuwa nimekubaliana na ulichokichora?”
“Saini yako haipo”
“Kwa maana hiyo ni kwamba ramani uliyochora sikubaliani nayo”
“Kwanini saini yake haipo?” hakimu akamuuliza polisi huyo.
“Ni kwa sababu wakati tunachora ramani, yeye mwenyewe hakuwepo” Polisi huyo akajibu.
“Alikuwa wapi?”
“Alikuwa mafichoni, yaani baada ya kusababisha ile ajali alikimbia. Tulimpata wakati tukiwa tumeshachora ramani”
“Jibu umelisikia?” hakimu akaniuliza.
“Nimelisikia lakini halinihusu mheshimiwa, wananihusisha tu na hiyo ajali lakini sikuhusika mimi”
“Ushahidi umetolewa hapa kuwa ni wewe” Polisi huyo aliyekuwa akitoa ushahidi aliniambia.
“Sikubaliani na ushahidi huo” nikamjibu.
“Wewe mwenyewe umeonekana na kutambuliwa, pikipiki yako imeonekana na kutambuliwa na namba ya usajili ya pikipiki yako pia imeonekana na kutambuliwa, sasa unakataa nini?”
“Kwa vile sikuhusika lazima nikatae”
“Una swali jingine” hakimu akanuiliza.
“Sina swali jingine” nikamjibu.
Hakimu aliandika kisha akaamuru aitwe shahidi mwingine.
Shahidi aliyeitwa baada ya hapo alikuwa afisa wa shirika la umeume.
Ushahidi alioutoa ulihusu uharibifu uliosababishwa na ajali hiyo. Alitoa takwimu za gharama kama alizozitoa shahidi aliyemaliza kutoa ushahidi wake. Alipomaliza kutoa ushahidi huo nilimuuliza.
“Ulimuona mtu aliyesababisha ajali hiyo?’
“Sikumuona” akajibu. Ndilo jibu nililokuwa nalitaka.
“Kwa hiyo hujui ni nani aliyesababisha ajali hiyo?”
“Nimeambiwa kuwa ni wewe”
“Nimeshasema kuwa sikuwa mimi”
“Kama si wewe kwanini walikukamata?”
“Walinikamata kwa makosa. Wao ni binaadamu wanaweza kukosea”
Jibu hilo liliwafanya baadhi ya watu waliokuwa wakisikiliza shauri hilo kucheka kimya kimya.
“Mahakama ndio itajua kama ulikamatwa kwa makosa”
“Lakini kwa maoni yako kama mimi sikuhusika bado nitalazimika kulipia gharama uliyoitaja?”
“Suala hilo tunaliachia mahakama”
“Sawa”
ITAENDELEA JINI SEHEMU YA 9
SIMULIZI ZA FAKI A FAKI
MWANAMKE JINI 9
ILIPOISHIA
“Kulikuwa na pikipiki moja inakuja kutoka barabara ya Taifa. Ile pikipiki ilitakiwa isimame kwenye mzunguko wa barabara nne uliopo pale lakini haikusimama”
“Baada ya hapo nini kilitokea?’
“Kulikuwa na gari aina ya Toyota Land Cruicer likitokea Gofu, lilikuwa linapita kwenye ule mzunguko likalazimika kuikwepa ile pikipiki. Katika kuikwepa pikipiki, gari hilo lilikwenda kugonga nguzo ya umeme”
“Baada ya kugonga nguzo ya umeme lilikwenda wapi?”
“Liliingia kwenye mfereji”
“Ni athari gani ilitokea baada ya nguzo ya umeme kugongwa?”
“Kwanza nguzo yenyewe ilivunjika halafu baadhi ya nyaya zilikatika na nyingine zilitoa cheche za moto hali iliyosababisha mfadhaiko mkubwa”
“Wakati tukio hilo linatokea, mwenye pikipiki alisimama”
“Hapana, hakusimama. Alipita moja kwa moja na kuendelea na safari yake”
“Wewe uliiona hiyo pikipiki?’
“Ndiyo niliiona”
“Ilikuwa ni aina gani”
“Kama sikosei ilikuwa aina ya Honda ya rangi nyeusi”
“Namba yake ya usajili uliiona”
“Niliiona”
Akaitaja. Ilikuwa ndio namba ya pikipiki yangu.
SASA ENDELEA
“Je aliyekuwa akindesha pikipiki hiyo ukimuona unaweza kumtambua?”
“Naweza kumtambua”
“Yuko hapa mahakamani?”
“Ndiyo yupo. Ni yule pale”
Akaninyooshea kidole mimi.
“Asante sana”
Baada ya mtu huyo kumaliza kutoa ushahidi wake, niliambiwa kama nina maswali nimuulize.
“Unajua hapa Tanga kuna pikipiki ngapi za aina ya Honda?” nikamuuliza.
“Ziko nyingi”
“Ambazo ni rangi nyeusi kama pikipiki yangu?’
“Ziko nyingi”
“Unawezaje kuzitofautisha?”
“Kivipi?”
“Nina maana una uhakika gani kama pikipiki ulioiona ni yangu na si ya mtu mwingine?’
“Wewe unapita pale kila siku na pikipiki yako. Pikipiki yako ninaijua na wewe mwenyewe ninakujua”
“Je nikikwambia kwamba sikuwa mimi bali alikuwa mtu mwingine utakataa?’
“Ndiyo nitakataa”
“Sasa mimi nakwambia sikuwa mimi?”
“Alikuwa nani?”
“Sijui”
Yule mtu akanyamaza.
Mwendesha Mashitaka akasimama na kumuuliza yule mtu.
“Mtu uliyemuona siku hiyo ndiye huyo hapo au siye?”
“Ndiye yeye” shahidi akajibu.
Mwendesha Mashitaka kakaa.
Kesi ikaahirishwa kwa juma moja.
Kipindi kile cha kesi ile kilinifanya niwe mnyonge sana. Nilijiuliza kama nitatakiwa nilipe faini au fidia ya uharibifu uliotokea, nitalipa nini? Kwa vile uharibifu ulikuwa mkubwa niliamni fidia yake pia itakuwa kubwa. Nilijiuliza nitapata wapi pesa za kulipa fidia hiyo ambayo kwa vyovyote vile ingekuwa ni mamilioni ya pesa.
Kila wakati nilikuwa nikimlaani yule msichana wa kijini aliyenisababishia matatizo yale. Niliomba nisikutane naye tena milele na milele.
Siku ya kesi ilipowadia nillifika mahakamani. Upande wa Mashitaka uliendelea kupeleka mashahidi. Safari hii aliyesimamishwa kizimbani kutoa ushahidi alikuwa polisi wa usalama barabarani aliyepima ile ajali iliyotokea.
Alitoa vielelezo yake ikiwa ni pamoja na ramani ya ajali aliyokuwa ameichora.
Ramani hiyo ilionesha kuwa nilifanya kosa la kutosimama katika alama ya L iliyokuwa kwenye mzunguko wa barabara nne uliopo eneo la Mabanda ya Papa.
Ramani hiyo iliendelea kuonesha kwamba wakati nafanya kosa hilo kulikuwa na gari aina ya Toyota Land Cruiser likitokea upande wangu wa kulia ambalo nilipaswa kulipisha lipite lakini sikufanya hivyo.
Hivyo gari hilo lililazimika kunikwepa na kwenda kugonga nguzo ya umeme inayomilikiwa na shirika la umeme na kuivunja.
Katika ushidi wake polisi huyo alieleza kwamba nguzo ya umeme niliyoivunja pamoja na nyaya zilizokatika zina thamani ya shilingi milioni kumi.
Akaeleza kwamba ili kurudisha mfumo wa upatikanaji umeme katika eneo hilo shirika la umeme litalazimika kutoa shilingi milioni kumi na tatu ikiwa ni pamoja na gharama ya ufundi.
“Pesa hizo zitapaswa zilipwe na mshitakiwa kwa sababu alifanya kosa hilo kwa uzembe na kutozingatia sheria za barabarani” akasema.
Hapo ndipo moyo wangu ulipotaharuki. Nitazitoa wapi shilingi milioni kumi na tatu za kuwalipa shirika la umeme? Nikajiuliza.
Polisi huyo alipomaliza kutoa ushahidi wake, hakimu aliniambia kama nina swali nimuulize.
Nilikuwa nimefadhaika sana kiasi kwamba sikuweza kuuliza swali lolote lakini niliona kukaa kimya kutaionesha mahakama kuwa kweli nilitenda kosa, nikamuuliza polisi huyo.
“Hiyo ramani uliyoitoa aliichora nani?”
“Niliichora mimi”
“Unapochora ramani ya ajali kama ile unapata maelezo kutoka kwa nani?”
“Kutoka kwa wale wahusika wa ajali na mashahidi”
“Kwa maoni yako mimi ni muhusika wa ajali?’
“Ndiyo”
“Nilikuwepo wakati unachora ramani hiyo?”
“Hukuwepo”
“Je niliweka saini yangu kuonesha kuwa nimekubaliana na ulichokichora?”
“Saini yako haipo”
“Kwa maana hiyo ni kwamba ramani uliyochora sikubaliani nayo”
“Kwanini saini yake haipo?” hakimu akamuuliza polisi huyo.
“Ni kwa sababu wakati tunachora ramani, yeye mwenyewe hakuwepo” Polisi huyo akajibu.
“Alikuwa wapi?”
“Alikuwa mafichoni, yaani baada ya kusababisha ile ajali alikimbia. Tulimpata wakati tukiwa tumeshachora ramani”
“Jibu umelisikia?” hakimu akaniuliza.
“Nimelisikia lakini halinihusu mheshimiwa, wananihusisha tu na hiyo ajali lakini sikuhusika mimi”
“Ushahidi umetolewa hapa kuwa ni wewe” Polisi huyo aliyekuwa akitoa ushahidi aliniambia.
“Sikubaliani na ushahidi huo” nikamjibu.
“Wewe mwenyewe umeonekana na kutambuliwa, pikipiki yako imeonekana na kutambuliwa na namba ya usajili ya pikipiki yako pia imeonekana na kutambuliwa, sasa unakataa nini?”
“Kwa vile sikuhusika lazima nikatae”
“Una swali jingine” hakimu akanuiliza.
“Sina swali jingine” nikamjibu.
Hakimu aliandika kisha akaamuru aitwe shahidi mwingine.
Shahidi aliyeitwa baada ya hapo alikuwa afisa wa shirika la umeume.
Ushahidi alioutoa ulihusu uharibifu uliosababishwa na ajali hiyo. Alitoa takwimu za gharama kama alizozitoa shahidi aliyemaliza kutoa ushahidi wake. Alipomaliza kutoa ushahidi huo nilimuuliza.
“Ulimuona mtu aliyesababisha ajali hiyo?’
“Sikumuona” akajibu. Ndilo jibu nililokuwa nalitaka.
“Kwa hiyo hujui ni nani aliyesababisha ajali hiyo?”
“Nimeambiwa kuwa ni wewe”
“Nimeshasema kuwa sikuwa mimi”
“Kama si wewe kwanini walikukamata?”
“Walinikamata kwa makosa. Wao ni binaadamu wanaweza kukosea”
Jibu hilo liliwafanya baadhi ya watu waliokuwa wakisikiliza shauri hilo kucheka kimya kimya.
“Mahakama ndio itajua kama ulikamatwa kwa makosa”
“Lakini kwa maoni yako kama mimi sikuhusika bado nitalazimika kulipia gharama uliyoitaja?”
“Suala hilo tunaliachia mahakama”
“Sawa”
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 10


ILIPOISHIA
Hakimu aliandika kisha akaamuru aitwe shahidi mwingine.
Shahidi aliyeitwa baada ya hapo alikuwa afisa wa shirika la umeme.
Ushahidi alioutoa ulihusu uharibifu uliosababishwa na ajali hiyo. Alitoa takwimu za gharama kama alizozitoa shahidi aliyemaliza kutoa ushahidi wake. Alipomaliza kutoa ushahidi huo nilimuuliza.
“Ulimuona mtu aliyesababisha ajali hiyo?’
“Sikumuona” akajibu. Ndilo jibu nililokuwa nalitaka.
“Kwa hiyo hujui ni nani aliyesababisha ajali hiyo?”
“Nimeambiwa kuwa ni wewe”
“Nimeshasema kuwa sikuwa mimi”
“Kama si wewe kwanini walikukamata?”
“Walinikamata kwa makosa. Wao ni binaadamu wanaweza kukosea”
Jibu hilo liliwafanya baadhi ya watu waliokuwa wakisikiliza shauri hilo kucheka kimya kimya.
“Mahakama ndio itajua kama ulikamatwa kwa makosa”
“Lakini kwa maoni yako kama mimi sikuhusika bado nitalazimika kulipia gharama uliyoitaja?”
“Suala hilo tunaliachia mahakama”
“Sawa”
SASA ENDELEA
Baada ya shahidi huyo kumaliza kutoa ushahidi wake hakimu aliahirisha kesi kwa wiki moja.
Nilikuwa nikienda kazini kama kawaida ila pikipiki yangu ndiyo ilikuwa imezuiwa na polisi. Wakati mwingine nilikuwa nikijipa moyo kuwa nitashinda kesi na wakati mwingine nilikata tamaa. Niliona jela ilikuwa inaningoja kwa vile sikuwa na pesa za kulipa faini wala kulipia gharama za shirika la umeme.
Siku ya kesi ikawadia. Upande wa mashitaka ukaeleza kuwa ulikuwa umemaliza mashahidi wake. Na mimi nikatakiwa nipeleke mashahidi kama nilikuwa nao.
Nikasema kwamba sikuwa na shahidi. Kesi ikaahirishwa tena ili kuupa nafasi upande wa mashitaka kuandaa maelezo ya mwisho ya kuishawishi mahakama inione kuwa nina hatia. Na pia kunipa nafasi mimi ya kuandaa utetezi wangu baada ya kusema kuwa sikuwa na shaahidi.
Kuahirishwa kwa kesi hiyo kulifanywa kwa wiki mbili. Wiki mbili zikapita kwa haraka, tukakutana tena mahakamani.
Upande wa mashitaka ukatoa maelezo yake ya mwisho ya kuionesha mahakama kuwa nilikuwa na hatia.
Mwendesha Mashitaka alisema “ Ushahidi uliotolewa hapa umethibitisha bila kuacha shaka yoyote kuwa kosa aliloshitakiwa mshitakiwa limetendeka na aliyehusika ni mshitakiwa aliyeko kizimbani”
Akaendelea.
“Ushahidi wa raia mwema muuza machungwa katika eneo la Mabanda ya Papa umethibitisha wazi kuwa mshitakiwa hakusimama mahali ambapo alitakiwa asimame ili kupisha magari na pikipiki zinazotoka upande wake wa kulia na hivyo kusababisha gari lililokuwa linapita, kufunga breki ghafla na kusababisha ajali”
“Ushahidi wa polisi wa usalama wa barabarani umethibitisha kuwa baada ya ajali kutokea mshitakiwa alikimbia na alikuja kukamatwa baada ya wiki mbili”
Mwendesha Mashitaka akaendelea kueleza.
“Kukamatwa kwake kuliwezeshwa na msamaria mwema aliyekuwa akiuza machungwa katika eneo hilo ambaye aliwatajia polisi namba ya pikipiki hiyo pamoja na muhusika mwenyewe”
Baada ya hapo Mwendesha Mashitaka alitaja vifungu vya sheria za usalama barabarani ambavyo alidai nilivikiuka na kuieleza mahakama kuwa nilistahili kupewa adhabu kali ikiwemo kulipia gharama za za shirika la umeme.
Mwendesha Mashitaka huyo alikwenda mbali zaidi akataja adhabu ya kifungo nilichostahili kwa kosa langu ni kwenda jela miaka mitano au kulipa faini siyopungua shilingi milioni kumi pamoja na kulipa ghrama za uharibu niliousababisha.
Hakujua ni jinsi gani alikuwa amenishitua na hakujua ni jinsi gani nilikuwa nikimlaani kwa kutaka kuniharibia maisha yangu. Hapo hapo niliona uso wangu ukifadhaika kama vile tayari nilikuwa nimeshahukumiwa.
Baada ya maelezo marefu ya Mwendesha Mashitaka, hakimu alinitaka nijitetee. Nikaanza kujitetea.
“Mheshimiwa hakimu licha ya maelezo marefu ya Mwendesha Mashitaka ya kutaka nifungwe na kulipa faini, bado ninaisisitizia mahkama yako kuwa si mimi niliyetenda kosa. Mimi nimefananishwa tu kwa bahati mbaya. Mimi sijavunja sheria yoyote ya barabarani”
Nikaendelea kueleza.
“Nilishangaa sana nilipoona nakamatwa na kuambiwa nimesababisha ajali. Jambo hilo si kweli. Mashahidi wote waliokuja kutoa ushahidi dhidi yangu ni waongo wakubwa, wamerubiniwa na polisi ili nipatikane na hatia. Kwa hiyo naiomba mahakama yako inione sina hatia na iniachie huru”
Hakimu aliandika maelezo yangu kisha akapanga tarehe ya kutoa hukumu.
Wakati niko uraiani nikisubiri hukumu yangu, nilikonda kwa mawazo. Ningekuwa ni mtu mwenye uwezo wa kulipa faini na kulipia gharama zilizotakiwa, nisingejali. Lakini nillikuwa masikini niliyekuwa nikitegemea mshahara wa kila mwezi ambao mimi mwenyewe pia haukunitosha.
Nilijiambia kama nitafungwa miaka mitano maisha yangu yatakuwa yameharibika. Nitakapotoka hapo nitakuwa sina kazi, sina bazi. Nitakuwa ninaanza maisha upya nikiwa sina uhakika wa kupata kazi mahali pengine.
Pia sikuwa na uhakika kuwa nitaweza kukaa gerezani kwa miaka mitano. Itakuwa ni kifo. Si ajabu nikarudishwa nikiwa maiti.
Katika kipindi hicho nikuwa naswali na kuomba Mungu. Nilimkumbuka Mungu sana.
Lakini sikuacha kumfikiria yule msichana wa kijini aliyenisababishia lile balaa. Nilikuwa nikijiambia kama si yeye balaa lile lisingenitokea.
Niliwahi kueleza kwamba nilikwenda kwa mganga kuroga ile kesi. Katika kipindi hicho cha kusubiri hukumu nilikwenda tena kwa waganga wasiopungua watatu.
Niliambiwa kulikuwa na mganga mmoja wa kimakonde aliyekuwa akiishi Kijiji cha Kigombe wilaya ya Muheza ambaye alikuwa hodari wa kuzima kesi, nikaenda na kaka yangu.
Baadaye tena nilikwenda kwa mganga mwingine aliyekuwa wilaya ya Mkinga. Alikuwa sharifu aliyekuwa akitumia uganga wa vitabu. Akanifanyia visomo vya kuzima kesi.
Mganga wa tatu alikuwa Pangani. Yeye alikwenda kunifanyia kafara baharini akanitabiria kwamba nitapata misukosuko mingi lakini nitakuja kuwa tajiri.
Siku moja kabla ya hukumu niliota ndoto ya kutisha. Ndoto ile ilikuwa kama inanitabiria kifungo. Niliota mzee mmoja aliyevaa nguo nyeupe akiniambia kuwa uganga niliofanya ulikuwa wa bure.
Kwa pembeni yangu nilimuona yule msichana wa kijini amesimama akinicheka. Alikuwa amebeba mkoba uliokuwa umeja kinyesi ambacho alikuwa akikichota na kunirushia, mpaka mwili wangu wote ukatapakaa kinyesi.
Hapo hapo nikaona nimesimamishwa kwenye kizimba. Hakimu akaniambia amenitia hatiani na kunihukumu kifungo cha miaka saba jela bila faini na kunitaka nililipe shirika la umeme shilingi milioni kumi na tano.
Nikamuona mama yangu ambaye alikuwa hapo mahakamani akiangua kilio.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 11


ILIPOISHIA
Katika kipindi hicho nikuwa naswali na kuomba Mungu. Nilimkumbuka Mungu sana.
Lakini sikuacha kumfikiria yule msichana wa kijini aliyenisababishia lile balaa. Nilikuwa nikijiambia kama si yeye balaa lile lisingenitokea.
Niliwahi kueleza kwamba nilikwenda kwa mganga kuroga ile kesi. Katika kipindi hicho cha kusubiri hukumu nilikwenda tena kwa waganga wasiopungua watatu.
Niliambiwa kulikuwa na mganga mmoja wa kimakonde aliyekuwa akiishi Kijiji cha Kigombe wilaya ya Muheza ambaye alikuwa hodari wa kuzima kesi, nikaenda na kaka yangu.
Baadaye tena nilikwenda kwa mganga mwingine aliyekuwa wilaya ya Mkinga. Alikuwa sharifu aliyekuwa akitumia uganga wa vitabu. Akanifanyia visomo vya kuzima kesi.
Mganga wa tatu alikuwa Pangani. Yeye alikwenda kunifanyia kafara baharini akanitabiria kwamba nitapata misukosuko mingi lakini nitakuja kuwa tajiri.
Siku moja kabla ya hukumu niliota ndoto ya kutisha. Ndoto ile ilikuwa kama inanitabiria kifungo. Niliota mzee mmoja aliyevaa nguo nyeupe akiniambia kuwa uganga niliofanya ulikuwa wa bure.
Kwa pembeni yangu nilimuona yule msichana wa kijini amesimama akinicheka. Alikuwa amebeba mkoba uliokuwa umejaa kinyesi ambacho alikuwa akikichota na kunirushia, mpaka mwili wangu wote ukatapakaa kinyesi.
Hapo hapo nikaona nimesimamishwa kwenye kizimba. Hakimu akaniambia amenitia hatiani na kunihukumu kifungo cha miaka saba jela bila faini na kunitaka nililipe shirika la umeme shilingi milioni kumi na tano.
Nikamuona mama yangu ambaye alikuwa hapo mahakamani akiangua kilio.
SASA ENDELEA
Nilipozinduka usingizini niliona jasho limenitoka mwili mzima na moyo ulikuwa ukinienda mbio.
Niliwasha taa kisha nikalaani. Saa yangu ilionesha ilkuwa saa kumi alfajiri. Sikulala tena. Mawazo yangu yote yalikuwa kwenye kufungwa. Nilijua kuwa ile ndoto ilkuwa imenibashiria kifungo ambacho ningepambana nacho siku ile.
Asubuhi kulipokucha nilipanga vitu vyangu vizuri kwa kujua kuwa ninakwenda kufungwa. Nilipomaliza nilikwenda kuoga, nikarudi kuvaa.
Nilihakikisha kila kitu nimekiweka sawa ndipo nilipotoka. Nilikwenda nyumbani kwa mama yangu barabara ya tisa ambako nilimkuta kaka yangu akinisubiri.
Baada ya kusalimiana nao, nililetewa chai nikanywa. Kwa sababu ya fadhaa niliyokuwa nayo nilikunywa kikombe kimoja tu na silesi tatu za mkate.
Kaka yangu akaitazama saa yake.
“Inakaribia kuwa saa mbili sasa” akasema.
Na mimi nikatazama saa yangu.
“Twendeni. Muda umekaribia sana” nikawambia.
“Ngoja nikuombee Mungu” Mama akaniambia.
Nilitaka kuwaeleza kuhusu ile ndoto niliyoota lakini nikoana hakukuwa na haja. Kaka yangu angeona niliota kwa sababu ya uoga wa kufungwa, wakati yeye siku zote alikuwa akiniambia niache uoga kwa vile alikuwa akiamini kuwa ningeshinda ile kesi.
Mama yangu akaniombea dua iliyonipa faraja sana. Baada ya dua yake ndefu akatuambia.
“Sasa twendeni”
Tukatoka. Tulipanda teksi iliyotupeleka mahakamani. Tuliingia ndani ya mahakama tukakaa kusubiri hakimu aingie.
Muda ulipowadia hakimu aliingia. Sauti ya koooort ikasikika. Watu wote tukasimama kutoa heshima ya mahakama kisha tukaketi pamoja na hakimu.
Jalada la kesi yangu ndilo lililoitishwa kwanza. Lilipotajwa jina langu nikasimama na kupanda kizimbani.
Hakimu akaniambia kwamba siku ile ndio angesoma hukumu ya kesi yangu. Nikamwambia “Sawa”
Nilikuwa nimeshajitolea kwa lolote litakalotokea, kufungwa au kuachiwa huru.
Hakimu alianza kutaja kesi iliyokuwa inanikabili. Akaeleza kwamba nilikana mashitaka niliyoshitakiwa na hivyo hukumu yake ilitegemea sana ushahidi uliotolewa mahakamani.
Hakimu aliendelea kuuchambua ushidi huo uliotolewa na mashahidi wa upande wa mashitaka kuanzia shahidi wa kwanza hadi wa mwisho.
Mwisho wa maelezo yake hakimu alisema, ameridhika kwamba ushahidi huo ulikuwa wa kweli na haukuwa na shaka yotote licha ya mimi mshitakiwa kuupinga.
Hakimu alipofika hapo nilishituka nikajiambia ubashiri wa ndoto niliyoota sasa ulikuwa unatimia.
Miguu ilianza kunitetemeka lakini nilijikaza kiume. Nikajiambia wanaofungwa pia ni binaadamu kama mimi.
“Kwa sababu hiyo nimekutia hatiani mshitakiwa katika makosa yote uliyoshitakiwa” hakimu akasema kisha akanitazama.
“Mshitakiwa uliopo mbele yangu ninakuhukumu kifungo cha miaka mitatu au ulipe faini ya shilingi milioni sita. Na pia ninakuamuru ulilipe shirika la umeme shilingi milioni kumi na tano kutokana na hasara uliyolisababishia shirika hilo”
Moyo wangu ulishituka na miguu yangu ikazidi kutetemeka.
“Utatumikia kifungo au utalipa faini pamoja na kulifidia shirika la umeme?’ Hakimu akaniuliza.
Sikuwa hata na la kujibu, ndipo nilipomuona msichana mmoja miongoni mwa watu waliokuwa wakisikiliza hukumu yangu akinyanyuka.
“Mheshimiwa nitamlipia faini mshitakiwa pamoja na gharama aliyotakiwa kulipa” akasema.
Nikamtazama vizuri msichana huyo.
Unadhani alikuwa nani?
Alikuwa Zena. Yule msichana ambaye nilimgundua kuwa ni jini!
“Utamlipia wewe faini ya shilingi milioni sita na shilingi milioni kumi na tano za kulilipa shirika la umeme?’ Hakimu akamuuliza.
“Ndiyo mheshimiwa”
“Unazo hapo?”
“Ndiyo mheshimiwa”
“Haya nenda kalipe”
Msichana huyo aliyekuwa ameweka begani mkoba wa rangi ya samli, alitoka kwenye mabenchi ya kukalia mahakamani akaongozwa na polisi kulekea sehemu ya kulipia pesa.
Wakati akitembea watu wote walikuwa wamegeuza uso wakimtazama. Pengine ni mimi peke yangu niliyejua kuwa hakuwa binaadamu, bali alikuwa jini aliyekuwa akijigeuza binaadamu.
Mama yangu na kaka yangu ambao walikuwepo hapo mahakamani wakiwa wameketi katika safu za mbele pia walikuwa wamepigwa na butwaa wakimtazama yule msichaana bila kumuelewa.
Polisi mwingine alinishusha mimi kizimbani na kunipeleka pale mahali ambapo Zena alitakiwa kunilipia faini na gharama za shirika la umeme.
Kitendo kile cha Zena kilikuwa kimenishitua na kunishangaza sana. Kwanza sikuwa nikijua kwamba alikuwepo pale mahakamani na kama alikuwepo sikujua alijuaje kuwa nilikuwa na kesi na kwamba siku ile ningetakiwa kulipa pesa hizo.
Nikasimamishwa karibu naye. Alikuwa amevaa baibui la kiiran lililonakishiwa mistari ya rangi ya samli. Alikuwa amejitia manukato yaliyokuwa yakisikika. Wakati ameuweka moba wake juu ya meza na kufungua zipu nilimuona kama adui ambaye ghafla amegeuka na kuwa mkombozi wangu.
Siku za nyuma nilikuwa nikijiambia nitakapomuona popote nitamkimbia. Lakini siku ile sikuweza kumkimbia kwani yeye sasa alikuwa kama kimbilio langu.
Baada ya kufungua mkoba wake alitia mkono ndani ya mkoba huo na kutoa mabunda ya noti nyekundu na kuyaweka juu ya meza. Nilihesabu jumla ya mabunda ishirini na moja ambayo aliyatoa.
“Hizo hapo shilingi milioni ishirini na moja. Milioni sita za faini na shilingi milioni kumi na tano za shirika la umeme” akasema.
Pesa hizo zilihesabiwa na kuthibitishwa kuwa zilikuwa ni kiasi kilichotakiwa.
Itaendelea...
 
SEHEMU YA 12


ILIPOISHIA
Msichana huyo aliyekuwa ameweka begani mkoba wa rangi ya samli, alitoka kwenye mabenchi ya kukalia mahakamani akaongozwa na polisi kulekea sehemu ya kulipia pesa.
Wakati akitembea watu wote walikuwa wamegeuza uso wakimtazama. Pengine ni mimi peke yangu niliyejua kuwa hakuwa binaadamu, bali alikuwa jini aliyekuwa akijigeuza binaadamu.
Mama yangu na kaka yangu ambao walikuwepo hapo mahakamani wakiwa wameketi katika safu za mbele pia walikuwa wamepigwa na butwaa wakimtazama yule msichaana bila kumuelewa.
Polisi mwingine alinishusha mimi kizimbani na kunipeleka pale mahali ambapo Zena alitakiwa kunilipia faini na gharama za shirika la umeme.
Kitendo kile cha Zena kilikuwa kimenishitua na kunishangaza sana. Kwanza sikuwa nikijua kwamba alikuwepo pale mahakamani na kama alikuwepo sikujua alijuaje kuwa nilikuwa na kesi na kwamba siku ile ningetakiwa kulipa pesa hizo.
Nikasimamishwa karibu naye. Alikuwa amevaa baibui la kiiran lililonakishiwa mistari ya rangi ya samli. Alikuwa amejitia manukato yaliyokuwa yakisikika. Wakati ameuweka mkoba wake juu ya meza na kufungua zipu nilimuona kama adui ambaye ghafla amegeuka na kuwa mkombozi wangu.
Siku za nyuma nilikuwa nikijiambia nitakapomuona popote nitamkimbia. Lakini siku ile sikuweza kumkimbia kwani yeye sasa alikuwa kama kimbilio langu.
Baada ya kufungua mkoba wake alitia mkono ndani ya mkoba huo na kutoa mabunda ya noti nyekundu na kuyaweka juu ya meza. Nilihesabu jumla ya mabunda ishirini na moja ambayo aliyatoa.
“Hizo hapo shilingi milioni ishirini na moja. Milioni sita za faini na shilingi milioni kumi na tano za shirika la umeme” akasema.
Pesa hizo zilihesabiwa na kuthibitishwa kuwa zilikuwa ni kiasi kilichotakiwa.
SASA ENDELEA
Pamoja na pesa hizo kulipwa, utaratibu wa kuachiwa kwangu ulichukua karibu saa nzima. Wakati natoka katika jengo la mahakama sasa nikiwa huru nilikuwa nimefuatana na Zena. Mama yangu na kaka yangu walikuwa nyuma. Bado walikuwa hawajui yule msichana alikuwa nani.
Tulipotoka nje ya mahakama Zena akaniambia.
“Ningependa nikutane na wewe leo saa kumi na moja jioni katika bustani ya Uhuru Park”
Wakati ule nilijihisi kuwa mdogo kama piritoni, nikamwambia.
“Sawa”
“Timiza ahadi”
“Nitatimiza’
“Sawa. Mimi nakwenda zangu”
Zena akaondoka na kuniacha. Mama na kaka yangu wakafika nilipokuwa nimesimama.
“Yule msichana ni nani?” kaka akaniuliza.
Zena alikuwa ameshakata kona na kutupotea.
“Yule si ndiye msichana aniliyewambia”
“Yupi?”
“Si ndiye yule jini mwenyewe aliyenipeleka kule Mikanjuni siku ile”
Mama na kaka walishituka.
“Kumbe ndiye yule!” Kaka akasema kwa mshangao.
“Sasa mbona amekulipia pesa?’ Mama akaniuliza.
“Sijui mwenyewe”
“Alikuwa anakueleza nini?” aliuliza kaka.
“Ameniambia nikutane naye Bustani ya Uhuru Park leo saa kumi na moja jioni”
Nilipowambia hivyo mama yangu aliguna.
“Mkutane kwa ajili gani?” akaniuliza.
Nikabetua mabega yangu.
“Sijui. Ameniambia hivyo tu”
“Na wewe umemjibu nini?” Kaka akaniuliza.
“Nimemwambia nitakwenda kukutana naye”
“Usiende peke yako, tutakwenda sote. Mimi pia nataka kumuona” Kaka akasema.
“Ni vizuri mwende nyote, asiende peke yake” Mama alisisitiza.
“Sawa. Tutakwenda pamoja” nikawambia.
Baada ya hapo tukaondoka. Tulikwenda kupanda teksi tukarudi nyumbani kwa mama.
Hatua ile ya kuachiwa huru na mahakama ilinifariji sana kwani tayari nilikuwa ninakwenda kufungwa. Yule mwanamke wa kijini ambaye ndiye aliyenitia katika tatizo lililonikabili aliibuka kama mkombozi wangu bila mimi kutarajia.
Nilipata wasiwasi aliponiambia nikutane naye katika bustani ya uhuru. Nikawa najiuliza alikuwa anataka nini tena wakati ile kesi ilikuwa imeshakwisha. Na kama ni uhusiano wetu ulikuwa haupo tena.
Kusema kweli sikupenda tena kuwa karibu na yule msichana. Kitendo cha kumkubalia kukutana naye kilitokana na hofu tu. Nilishindwa kumkatalia. Angeweza kunizushia tatizo jingine.
Nilikaa kwa mama hadi saa kumi na moja jioni. Kaka aliondoka tangu saa tisa akarudi dakika chache kabla ya saa kumi na moja.
“Naona muda umewadia” akaniambia nakuongeza.
“Twenzetu”
“Sawa. Twende”
Tukamuaga mama na kuondoka. Tulipanda tena teksi ikatupeleka Bustani ya Uhuru ambayo ilikuwa karibu na baharini. Kutoka barabara ya tisa hadi mahali hapo ulikuwa mwendo wa karibu kilometa mbili.
Bustani ya Uhuru ilikuwa katika eneo la mijini kabisa. Enzi hizo tulizoea kukuita uzunguni.
Ilikuwa bustani nzuri ya kupendeza yenye eneo la mita kumi hivi za mraba. Mbali ya kuzungushiwa ukuta mfupi ilikuwa na mti ya vivuli na viti vilivyotengezwa kwa saruji.
Mida kama ile ya jioni watu mbalimbali hupenda kufika katika bustani hiyo kupunga upepo au kupumzika.
Tulipofika, tayari watu walikuwa wakionekana wamejilisi katika kila kona. Tulipata kiti kilichokuwa kitupu chini ya mti mmoja tukakaa.
Niliangaza macho yangu kila upande kuona kama yule mwanamke ameshafika lakini sikumuona. Walikuwepo watu wengine tu.
“Naona bado hajafika” Nikamwambia kaka ambaye alitazama saa yake.
“Saa kumi na moja bado” akaniambia.
“Bado dakika ngapi?’
“Bado dakika mbili”
“Basi atafika sasa hivi”
Tukasubiri.
Saa kumi na moja ikafika. Hatukuona mtu. Dakika zikaendelea kwenda. Kila wakati kaka yangu alikuwa akitazama saa yake. Haukupita muda mrefu akaniambia.
“Sasa ni saa kumi na moja na nusu”
Na mimi nikatazama saa yangu. Ni kweli ilikuwa saa kumi na moja na nusu.
Nikaangaza macho yangu kila upande.
“Mbona hatokei?” nikajiuliza lakini kwa sauti iliyosikika.
“Labda ameghairi”
“Yeye alinisisitiza kwamba nisivunje ahadi”
“Basi tuendelee kusubiri, anaweza kutokea”
Tukaendelea kusubiri hadi saa kumi na mbili jioni.
“Sidhani kama atakuja tena” Kaka akaniambia.
“Basi twenzetu”
“Twenzetu”
Tukanyanyuka.
“Ametupotezea muda wetu bure” Kaka akasema.
“Nashukuru pia hivyo ambavyo hakutokea’
Kaka akacheka.
“Kwanini useme hivyo?’
“Yule mwanamke mimi nilishapanga nisikutane naye tena!”
“Lakini ndiye aliyekuokoa”
“Kwani yale matatizo si ameniletea yeye!”
Tulikuwa tumeshatokea barabarani.
“Naona turudi kwa miguu tu” nikamwambia kaka.
Tukarudi kwa miguu.
Tulipofika nyumbani kwa mama, mama akatuuliza.
“Mlikutana naye?”
“Hakuja” nikamjibu.
“Tumekaa mpaka tumechoka” Kaka akaongeza.
“Kwanini asije na alikwambia mkutane hapo saa kumi na moja”
“Labda amebadili mawazo” nikamwambia.
“Ndiyo vizuri”
Itaendelea
 
SEHEMU YA 13


ILIPOISHIA
Tukaendelea kusubiri hadi saa kumi na mbili jioni.
“Sidhani kama atakuja tena” Kaka akaniambia.
“Basi twenzetu”
“Twenzetu”
Tukanyanyuka.
“Ametupotezea muda wetu bure” Kaka akasema.
“Nashukuru pia hivyo ambavyo hakutokea’
Kaka akacheka.
“Kwanini useme hivyo?’
“Yule mwanamke mimi nilishapanga nisikutane naye tena!”
“Lakini ndiye aliyekuokoa”
“Kwani yale matatizo si ameniletea yeye!”
Tulikuwa tumeshatokea barabarani.
“Naona turudi kwa miguu tu” nikamwambia kaka.
Tukarudi kwa miguu.
Tulipofika nyumbani kwa mama, mama akatuuliza.
“Mlikutana naye?”
“Hakuja” nikamjibu.
“Tumekaa mpaka tumechoka” Kaka akaongeza.
“Kwanini asije na alikwambia mkutane hapo saa kumi na moja”
“Labda amebadili mawazo” nikamwambia.
“Ndiyo vizuri”
SASA ENDELEA
“Mimi pia nimemwambia kaka ni vizuri kama hakuja, simuhitaji. Namuona kama nduli”
“Ni nduli kweli. Angekuharibia maisha yako” Mama akaniambia.
“Lakini haikuwa vibaya kumsikiliza kujua alitaka kukwambia nini” Kaka akaniambia.
“Basi yameshapita”
Baada ya hapo mimi na kaka tulimuaga mama na kuondoka. Kaka alikwenda kwake na mimi nikarudi nyumbani kwangu Msambweni.
Nilipofika nilioga. Nilipomaliza kuoga nilikaa sebuleni na kujiwazia.
Mpaka muda ule nilikuwa siamini kama niliachiwa na mahakama na nilikuwa huru.
Niliona hivyo kwa sababu kuachiwa kwangu kulikuwa kwa miujiza sana. Kila aliyekuwa akisikiliza ile hukumu alijua kuwa nafungwa kwani nisingeweza kupata zile pesa zilizotakiwa.
Lakini yule mwanamke alishajua kuwa ningetakiwa kulipa pesa zile na pia alijua kuwa nisingekuwa nazo, hivyo akaja nazo na kusubiri hukumu.
Kwa upande mwingine nilikuwa sijajua nia ya yule msichana. Sikujua alikuwa akitaka nini kwangu kwani hatukuwahi kuwa na makubaliano yoyote tuliyokubalina.
Wakati niko katika lindi la mawazo sebuleni kwangu simu yangu ya mezani iliyokuwa pembeni mwa sebule ikaita. Ilinishitua sana. Simu hiyo ilikuwa haipigwi mara kwa mara. Wakati ule hakukuwa na waswahili wengi waliokuwa wakimiliki simu hivyo mawasiliano ya simu yalikuwa madogo sana.
Nikanyoosha mkono wamgu na kukinyakua chombo cha simu cha kusemea.
“Hallow!” nikasema nikiwa simjui aliyenipigia.
“Hallow!” Sauti nyembamba ya mwanamke ikajibu kutoka kwenye simu.
“Amour hapa, nani mwenzangu?”
“Unazungumza na Zena”
Moyo wangu ukashituka.
“Nani…Zena?”
“Ndiyo Zena”
Nilishajua kuwa huenda alikuwa yule msichana wa kijini lakini nilitaka kuthibitisha.
“Zena nani?”
“Ohoo umenisahau leo. Nilikwambia tukutane saa kumi na moja jioni katika bustani ya Uhuru”
“Ndiyo nilifika na nilikusubiri lakini wewe hukutokea”
“Ninajua kwamba ulifika na ulinisubiri lakini mimi sikutokea”
“Kwanini?”
“Umeniudhi”
“Nimekuudhi?”
“Ndiyo”
“Nimekuudhi kwa vipi?”
“Ulikuwa pamoja na nani?”
Nikasita kidogo kabla ya kumjibu.
“Nilikuwa na kaka yangu”
“Kaka yako mimi namjua?”
“Hapana, hunjui”
“Sasa ulikuja na kaka yako kwa ajili ya nini?”
“Alikuwa amenisindikiza tu”
“Lakini tulikubaliana tukutane mimi na wewe. Kwanini ulimleta kaka yako?” Hapa Zena alisema kwa ukali kidogo.
Nikanyamaza.
“Sasa uliyevunja ahadi ni mimi au wewe?” Zena akaniuliza.
Sikumjibu kitu.
“Sema ni wewe. Mimi nilipoona umekuja na mwenzako kinyume na makubaliano yetu sikujitokeza”
“Basi nisamehe”
“Nimeshakusamehe ila kuna kitu nataka kukwambia”
“Fika tena kesho saa nne asubuhi pale Uhuru Park”
“Utakuja?”
“Ndiyo nitakuja”
“Sawa, basi nitafika”
“Kwaheri”
Simu ikakatwa.
Niliuweka mkono wa simu nikawa najiuliza, msichana huyo aliipata wapi namba yangu ya simu. Sikukumbuka kama niliwahi kumtajia namba yangu ya simu. Kitendo kile cha kunipigia kilikuwa kimenishitua na kunishangaza.
Sasa nikawa nimetambua sababu ya Zena kutofika mahali ambapo tuliahidiana kukutana. Kumbe ilikuwa ni kwa sababu nilikwenda na kaka wakati yeye hakupenda awepo mtu mwingine.
Nikawa nimeshapata wasiwasi, nikavaa nguo na kutoka. Nilikwenda kwa mama yangu nikamueleza.
Mama akaniambia niende nikamueleze kaka yangu aliyekuwa akiishi eneo la Chuda, nikaenda. Ilikuwa karibu saa tatu usiku.
Kaka aliponiona akashituka.
“Vipi ndugu yangu?” akaniuliza.
“Yule mwanamke amenipigia simu” nikamwambia.
“Kumbe ulimpa namba yako?” akaniuliza.
“Hapana, sikumpa”
“Aliipata wapi?”
Nikabetua mabega yangu.
Sijui. Hata mimi mwenyewe nimeshangaa”
“Amekwambia nini?”
“Ameniambia hakutokea kwa sababu nilikwenda pale nikiwa na wewe”
“Yaani alitaka uwe peke yako?”
“Ndiyo hivyo”
“Kumbe alituona tuko wawili!”
“Bila shaka”
“Sasa amekwambiaje?”
“Ameniambia tukutane tena kesho saa nne”
“Kwani anataka nini?”
“Sijajua”
“Sasa wewe umeamuaje?”
“Nataka ushauru wako”
“Mimi nakushauri nenda”
“Basi nitakwenda”
“Kwa sababu hujui anataka kukwambia nini. Pengine anataka kukwambia kitu cha maana kwako”
“Ni kweli”
“Huwezi jua, anaweza kukupa utajiri”
“Unasema kweli kaka?”
“Wewe nenda kamsikilize, usiogope”
“Sawa. Nitakwenda”
Baada ya kuzungumza na kaka kwa dakika kadhaa nikamuaga.
“Basi kaka mimi narudi nyumbani”
Itaendelea
 
SEHEMU YA 14


ILIPOISHIA
“Ameniambia hakutokea kwa sababu nilikwenda pale nikiwa na wewe”
“Yaani alitaka uwe peke yako?”
“Ndiyo hivyo”
“Kumbe alituona tuko wawili!”
“Bila shaka”
“Sasa amekwambiaje?”
“Ameniambia tukutane tena kesho saa nne”
“Kwani anataka nini?”
“Sijajua”
“Sasa wewe umeamuaje?”
“Nataka ushauru wako”
“Mimi nakushauri nenda”
“Basi nitakwenda”
“Kwa sababu hujui anataka kukwambia nini. Pengine anataka kukwambia kitu cha maana kwako”
“Ni kweli”
“Huwezi jua, anaweza kukupa utajiri”
“Unasema kweli kaka?”
“Wewe nenda kamsikilize, usiogope”
“Sawa. Nitakwenda”
Baada ya kuzungumza na kaka kwa dakika kadhaa nikamuaga.
“Basi kaka mimi narudi nyumbani”
SASA ENDELEA
“Acha nikusindikize”
Kaka akanisikindikiza hadi eneo la stendi ya mabasi, tukaachana.
Siku iliyofuata nikajiandaa kwenda kukutana na yule msichana. Nilipotoka nyumbani nilikwenda nyumbani kwa mama. Nikamjulisha kwamba ndio ninakwenda kukutana na yule msichana wa kijini.
“Jana nilipokwambia uende ukakutane na kaka yako ulikwenda?” Mama akaniuliza.
“Nilikwenda nikamjulisha akaniambia niende nikakutane naye”
“Na wewe mwenyewe umeridhika?”
“Sina la kufanya mama, inabidi niende nikamsikilize”
“Basi omba Mungu. Mungu atakusaidia”
“Sawa mama”
Saa tatu na nusu nikaondoka nyumbani kwa mama. Kwa sababu ya kihoro nilichokuwa nacho hata chai sikuwahi kunywa. Kusema kweli sikujisikia kunywa chai.
Nilipofika katika bustani ya Uhuru ilikuwa saa nne kasoro dakika tano. Nikakaa mahali pale pale nilipokaa na kaka jana yake.
SASA ENDELEA
Nikaanza kutupia macho watu waliokuwa wakipita barabarani hasa wasichana nikitazamia ningemuona Zena akiwa mmojawao.
Dakika zikandelea kupita. Zena sikumuona. Mara kwa mara nilikuwa nikitazama saa yangu. Hakukuwa na siku ambayo saa ilinishughulisha kama siku ile. Kila baada ya muda mfupi nilikuwa nilitazama saa.
Mpaka inafika saa nne kasoro dakika moja niliinua uso wangu nikawa ninaangalia barabarani upande ambao nilitarajia kuwa Zena angetokea. Niliangalia kwa shauku yenye hofu kwa kujua kuwa muda wowote ningemuona Zena.
Kutoka saa nne kasoro dakika moja nilianza kuhesabu sekunde kwani dakika hazikuwepo tena.
Nilianza kuhisi baridi ya hofu ikininyemelea mwilini. Sikujua yule msichana atakapotokea atanieleza nini. Ile picha ya kumuona siku ile akiwa na miguu ya kwato na mwili wenye manyoya kama wa shetani ilianza kunijia akilini mwangu. Picha hiyo ndiyo iliyonitisha na kunikumbusha mkasa mzima ulionitokea siku ile.
Ghafla niliona teksi ikisimama kando ya barabara jirani na bustani ya uhuru. Ilikuwa teksi ya rangi nyeupe na sikujua ni kwanini niliikodolea macho.
Mara nikamuona msichana mrembo akishuka. Alikuwa amevaa dera la mikono mirefu lenye ushungi uliofinika kichwa chake na kuteremka hadi usawa wa kiuno chake.
Alikuwa amevaa miwani ya jua iliyoficha uso wake lakini midomo yake iliyokolezwa rangi ya waridi ilitokeza na kuonekana waziwazi.
Mara tu aliposhuka kwenye teksi alianza kutembea kuelekea katika lango la bustani ya uhuru kwa hatua za taratibu.
Zilinichukua sekunde kama tano hivi kumtambua. Alikuwa ni Zena!
Ile akili yangu iliponiambia kuwa ni Zena, moyo wangu ulipiga kwa nguvu mara moja kisha ukatulia. Nikaona waziwazi pumzi zangu zimebadilika. Nilikuwa ninahema kwa nguvu. Nikawa nashindana na mapafu yangu kuyazuia ili nisionekane kuwa ninapumua hivyo.
Zena alishaingia kwenye eneo la bustani, akawa anatembea kuelekea mahali nilipokuwa kwa mwendo ule ule wa taratibu. Alionekana wazi kuwa mtu mwenye ahadi adhimu.
Wakati anazidi kunikaribia, upande mmoja wa akili yangu ulishindwa kuamini kuwa yule msichana alikuwa ni jini. Alikuwa mzuri sana.
“Asalaam alay kum” akanisalimia aliponikaribia kabla ya kuketi kando yangu.
Hapo hapo niliskia harufu ya manukato aliyokuwa amejitia na hewa ya mahali hapo ikawa ni ya mawaridi.
“Wa alayka salaam” nikamuitikia huku nikijaribu kutabasamu ili kuficha fadhaa niliyokuwa nayo usoni.
Alipoona ninatabasamu na yeye akatabasamu.
“Ninaitwa Zena” akaniambia ingawa sikuwa nimemuuliza jina.
Akaongeza. “Habari ya tangu jana?”
“Nzuri. Sijui yako wewe”
“Mimi mzima. Tukikutana kama hivi hatuna budi kumshukuru Mungu”
“Ni kweli”
Msichana akajiweka sawa na kuutoa mkoba wake uliokuwa umezibwa na ushungi wake aliokuwa amejitanda. Akaufungua na kukitoa kile kitabu changu nilichomuazima siku ile.
“Nimekurudishia kitabu chako ulichokuwa umeniazima” akaniambia huku akinipa kitabu hicho.
Wakati nakipokea akaniambia.
“Samahani kwa kukucheleweshea kitabu chako”
“Bila samahani. Nilikuwa nimeshakisahau kutokana na misuko suko”
“Pole”
“Asante”
Msichana akageukia upande wangu. Ilikuwa vyema kuwa alivaa miwani, vinginevyo angenipa wakati mgumu kutazamana naye.
“Ni kwaninini siku ile uliondoka nyumbani bila kuniambia, ukaacha pikipiki yako na viatu vyako?” akaniuliza.
“Siku ile nilitishika sana. Nilikuona katika umbo tofauti kabisa!” nikamwambia.
Zena akacheka. Alipofanya hivyo haiba ya uso wake ilibadilika na kuwa ya kupendeza zaidi.
“Uliniona katika umbo gani?” akaniuliza.
“Mwili wako ulikuwa na manyoya marefu na miguu yako ilikuwa na kwato kama ya punda. Kwa kweli nilipatwa na uoga mkubwa”
“Ndiyo maana siku ile uliponiona kule Mabanda ya Papa ukaongeza mwendo mpaka ikatokea ile ajali?”
“Kumbe unajua. Ni kweli niliongeza mwendo baada ya kukuona wewe”
Msichana akacheka tena.
“Hukupaswa kunikimbia. Iile umbo uliloniona nalo nyumbani siku ile ndilo umbo langu kwa maana mimi si binaadamu bali ni jini”
“Nilishafahamu kuwa wewe si binaadamu. Binaadamu hawezi kuwa na umbo kama lile”
“Nimefurahi kama umenielewa, kwa hiyo usiniogope tena”
“Kukuogopa ni lazima kwa sababu sijakuzoea”
“Taratibu tu utanizoea. Mimi nimekuwa na wewe kwa miaka mingi bila wewe mwenyewe kujua”
“Umekuwa na mimi kwa miaka mingi?”
“Ndiyo. Naweza kusema tangu ukiwa kijana mdogo”
“Ulikuwa uko wapi?”
“Nilikuwa na wewe”
“Sijawahi kukuona”
JAMANI MMEYASIKIA MANENO HAYO?! MWANAMKE WA KIJINI KAMHUSUDU BINAADAMU! MAKUBWA!!!! KWELI DUNIANI KUNA MAMBO! SIJUI MAZUNGUMZO YAO YATAENDELEAJE?
 
SEHEMU YA 15


ILIPOISHIA
Zena akacheka. Alipofanya hivyo haiba ya uso wake ilibadilika na kuwa ya kupendeza zaidi.
“Uliniona katika umbo gani?” akaniuliza.
“Mwili wako ulikuwa na manyoya marefu na miguu yako ilikuwa na kwato kama ya punda. Kwa kweli nilipatwa na uoga mkubwa”
“Ndiyo maana siku ile uliponiona kule Mabanda ya Papa ukaongeza mwendo mpaka ikatokea ile ajali?”
“Kumbe unajua. Ni kweli niliongeza mwendo baada ya kukuona wewe”
Msichana akacheka tena.
“Hukupaswa kunikimbia. Iile umbo uliloniona nalo nyumbani siku ile ndilo umbo langu kwa maana mimi si binaadamu bali ni jini”
“Nilishafahamu kuwa wewe si binaadamu. Binaadamu hawezi kuwa na umbo kama lile”
“Nimefurahi kama umenielewa, kwa hiyo usiniogope tena”
“Kukuogopa ni lazima kwa sababu sijakuzoea”
“Taratibu tu utanizoea. Mimi nimekuwa na wewe kwa miaka mingi bila wewe mwenyewe kujua”
“Umekuwa na mimi kwa miaka mingi?”
“Ndiyo. Naweza kusema tangu ukiwa kijana mdogo”
“Ulikuwa uko wapi?”
“Nilikuwa na wewe”
“Sijawahi kukuona”
SASA ENDELEA
“Ni kweli. Sikutaka unione wala kujitambullisha kwako kwa sababu muda wa wewe kunitambua mimi ulikuwa haujafika”
Nikaguna. Lakini niliguna moyoni mwangu.
“Siku ile niliyokuazima kitabu ndio siku ambayo nilipanga kujitokeza rasmi kwako”
Nikabaki kimya nikimsikiliza. Maneno yake yalikuwa yameshitua akili yangu.
“Samahani kwa matatizo yote yaliyokutokea ambayo kwa namna moja au nyingine niliyasababisha mimi. Haikuwa kusudio langu kukusumbua bali nililazimika kufanya vile ili uweze kunitambua” Zena aliendelea kuniambia.
“Umeniambia kwamba wewe ni jini, ni jini wa aina gani na unaishi wapi?” nikamuuliza ili niweze kumuelewa vizuri.
“Mimi ni jini wa ukoo wa Ummi Subian, yaani nimechanganya kabila mbili, upande mmoja ni ruhani na upande mwingine ni subian. Yaani ninatumia bara na pwani lakini zaidi mila zangu ni za kipwani”
Nilidhani alikuwa amemaliza. Akaendelea.
“Umeniuliza ninaishi wapi. Kwetu ni Sham na kwa hapa Afrika Mashariki maskani zangu zipo katika eneo lote hili la pwani ya Afrika Mashariki kuanzia Somalia, Kenya na Tanzania.
“Niliwahi kukwambia jina langu ninaitwa Zena. Baba yangu anaitwa Jabalkeys na mama yangu ni Ummi Mariam. Huko ujinini mimi natambulika kama Zainush binti Jabalkeys”
Alipofika hapo Zena alinitazama akaniuliza.
“Umenielewa vizuri?”
“Nimekuelewa” nikamjibu.
“Kuna kitu kimoja nataka nikwambie” akaniambia.
“Niambie”
“Nimekuchunuka na ninataka uwe mume wangu. Ninakuahidi kuwa nitakupa utajiri”
Nikashituka.
“Kama wewe ni jini, nitawezaje kuwa mume wako?” nikamuuliza.
“Majini huoana na binaadamu. Kama huamini nenda kwa bibi yako aliyemzaa baba yako, muulize baada ya kuachika yeye mume wake alioa mke gani?”
“Una maana gani, una maana kwamba babu yangu alioa jini?” nikamuuliza kwa mshangao.
“Nataka uende ukamuulize yeye, akueleze”
“Sawa. Nitakwenda kumuuliza”
“Tutakutana lini tena?”
“Niambie wewe”
“Unadhani ni lini utakuwa na jibu?”
“Labda keshokutwa”
“Basi nitakutafuta”:
“Sawa”
Zena akafungua mkoba wake. Nilikuwa namtazama pembeni mwa macho yangu.
Nikaona akitoa kitita cha noti nyekundu. Nilizikisia zilikuwa zaidi shilingi milioni moja. Akanipa bila kuzihesabu.
“Chukua hizo zitakusaidia” akaniambia.
“Asante sana” nikamwambia.
Zena akafunga mkoba wake na kunitazama huku akitabasamu.
“Una kitu chochote unataka kuniambia?” akaniuliza.
“Hapana, sina kitu cha kukwambia”
“Basi tuagane uende zako na mimi niende zangu”
“Mimi nashukuru tu kukutana na wewe”
Huku tabasamu likiendelea kutawala usoni kwake akaniambia.
“Asante”
Akanyanyuka.
“Kwaheri” akaniaga na kuondoka.
Nikiwa bado nimekaa nilimtazama wakati akienda zake. Alivuka viti kadhaa kabla ya kutokea kwenye njia iliyokuwa ndani ya bustani. Kulikuwa na vijana wawili waliokuwa wamekaa katika kiti kimoja nyuma yetu. Walikuwa na baskeli waliyokuwa wameiegesha mbele ya kiti walichokuwa wamekaa.
Walipomuona yule msichana Zena anaondoka waliinuka wakapakiana kwenye baskeli na kumfuata.
Wakati wanampita, yule kijana aliyekuwa amepakiwa nyuma aliuvuta mkoba wa Zena akauchomoa na kuuchukua. Zena alipogutuka vijana hao walimpita na baskeli na kukimbia.
Zena akabaki amesimama akiwatazama vijana hao kwa hasira. Mkoba wake ulikuwa umekwenda!
Nikanyanyuka kwenye kiti na kumfuata haraka. Wale vijana walikuwa wameshafika barabarani wakaelekea upande wa Chumbageni kwa mwendo wa kasi.
“Wamepora mkoba wako?” nikamuuliza.
“Basi waache tu, huwezi kuwafanya kitu” Zena alisema. Sauti yake ilikuwa tulivu lakini ilionesha ghadhabu.
“Wale vijana walikuwa wamekaa muda mrefu nyuma yetu, kumbe walikuwa na lao wanalongojea”
“Hakuna tatizo”
Nilikuwa nafuatana naye kuelekea kwenye lango la kutokea kwenye bustani hiyo.
“Dah!....”
“Usijali, waache tu. Mimi nakwenda zangu”
Ile teksi iliyomleta Zena ikatokea tena na kusimama mahali pale pale pa mwanzo.
Zena akaifuata na kujipakia. Teksi ikaondoka. Niliisindikiza kwa macho hadi ilipokata kona.
“Majini pia wanapanda teksi!” nikajisemea moyoni mwangu kisha nikaanza kutembea kwa miguu kurudi nyumbani.
MAMBO HAYO!!!!
 
SEHEMU YA 16

ILIPOISHIA
Nikanyanyuka kwenye kiti na kumfuata haraka. Wale vijana walikuwa wameshafika barabarani wakaelekea upande wa Chumbageni kwa mwendo wa kasi.
“Wamepora mkoba wako?” nikamuuliza.
“Basi waache tu, huwezi kuwafanya kitu” Zena alisema. Sauti yake ilikuwa tulivu lakini ilionesha ghadhabu.
“Wale vijana walikuwa wamekaa muda mrefu nyuma yetu, kumbe walikuwa na lao wanalongojea”
“Hakuna tatizo”
Nilikuwa nafuatana naye kuelekea kwenye lango la kutokea kwenye bustani hiyo.
“Dah!....”
“Usijali, waache tu. Mimi nakwenda zangu”
Ile teksi iliyomleta Zena ikatokea tena na kusimama mahali pale pale pa mwanzo.
Zena akaifuata na kujipakia. Teksi ikaondoka. Niliisindikiza kwa macho hadi ilipokata kona.
“Majini pia wanapanda teksi!” nikajisemea moyoni mwangu kisha nikaanza kutembea kwa miguu kurudi nyumbani.
SASA ENDELEA
Kile kitendo cha wale vijana kilikuwa kimefadhaisha akili yangu.
Sikurudi nyumbani moja kwa moja, nilikwenda nyumbani kwa kaka. Aliponiona tu akaniuliza.
“Ulifika huko Uhuru Park?”
“Nimefika na nimekutana naye”
“Enhe amekueleza nini?”
“Kwanza amenirudishia hiki kitabu changu nilichokuwa nimemuazima siku ile kisha akaniomba msamaha kwa usumbufu wowote ambao niliupata kutokana na yeye”
“Enhe…?”
“Baada ya hapo akanithibitishia
mwenyewe kwamba yeye ni jinni. Akaniambia kwamba nisimuogope kwani hatakuwa na madhara na mimi. Lakini la msingi aliloniambia ni kuwa anataka niwe mume wake…”
“Mume wake kivipi?”
“Nafikiri anataka tuoane”
“Eh…utamuweza kweli mke wa kijini? Kumbe ana makubwa!”
“Nimemuuliza kwani majini wanaoana na binaadamu? Akaniambia niende nikamuulize bibi mzaa baba, eti baba yangu baada ya kumuacha yeye alioa mke gani?”
“Alikuwa na maana gani?”
“Ameniambia nikamuulize tu halafu nije nimpe jibu”
“Kumbe anamjua pia bibi yetu?”
“Ameniambia amekuwa na mimi tangu nikiwa mdogo lakini hakuwa amejitokeza, kwa hiyo familia yetu atakuwa anaijua”
“Itakubidi hayo maneno ukamueleze mama”
“Nitakwenda kumueleza”
“Twende kwake sasa hivi”
Tukatoka na kaka kwenda nyumbani kwa mama. Tulienda kwa miguu. Njiani tulikuwa tukiendelea kuzungumza.
“Ameniambia kama nitaoana naye atanipa utajiri”
“Hilo si tatizo, tatizo ni kuwa na mke jini” Kaka akaniambia.
Nikajua suala hilo lilikuwa limemshitua na yeye.
Tulipofika nyumbani kwa mama, nikamueleza mazungumzo yote tuliyozungumza na Zena. Mama naye akashituka.
“Hebu nenda ukamuulize bibi yako kuhusu huyo babu yako usikie atakueleza nini lakini nakushauri usikubali kuoana na huyo mwanamke hata kama atakupa utajiri” Mama akaniambia.
“Mimi sijakubali, bado niko kwenye utafiti”
“Wewe ni binaadamu huwezi kuishi na mwanamke ambaye ni jini” Mama aliendelea kunisisitizia.
“Nitazingatia ushauri wako na nitakwenda kwa bibi hapo kesho” nikamwambia.
Bibi mwenyewe alikuwa akiishi Mwambani, mwendo wa kama kilometa kumi kutoka Tanga mjini. Kitongoji hicho kipo upande wa Kaskazini mwa jiji la Tanga katika barabara inayoelekea wilaya ya Pangani.
Siku ya pili yake nikaenda huko Mwambani kwa kutumia pikipiki yangu. Nilipofika nilimkuta bibi yuko barazani mwa nyumba yake akisuka ukili wake. Ingawa alikuwa kikongwe sana lakini bado alikuwa akijiweza kiasi kwamba alikuwa anaweza kusuka ukili wake.
Nilikuwa nimemnunulia kilo tano za sukari, nikampa.
Baada ya kuulizana hali nilimwambia licha ya kwenda kumsalimia pia nilikuwa na shida yangu.
“Shida gani?” akaniuliza.
“Nilikuwa nataka kujua eti baada ya wewe kuachana na marehemu mume wako yaani babu yangu, babu alioa mke mwingine?”
“Ndio alioa”
“Enhe niambie alimuoa nani?”
“Inasemekana alioa mke wa kijini, alikuwa akiitwa Zena na huyo Zena ndiye aliyefanya babu yako aniache mimi. Lakini mimi sikuwahi kumuona”
Nikashituka niliposikia maneno yale.
“Alimpata wapi huyo mke wa kijini?” nikamuuliza.
“Alimchunuka tu akamwambia aniache mimi amuoe yeye. Babu yako akakubali kuniacha kwa ajili ya kupata utajiri”
“Na ni kweli alipata utajiri?”
“Alipata utajiri mkubwa sana lakini siku chache kabla ya kufa kwake utajiri wote ulipotoea na huyo mke wake alitoweka pia”
“Wakati huo alikuwa umeshamzaa baba?”
“Baba yako alikuwa ameshazaliwa pamoja na kaka yake Abdul yaani baba yako mkubwa ambaye alifariki nchi za nje”
“Sasa baada ya babu kuoa mke wa kijini, nani aliwalea kina baba?”
“Aliniachia nao mimi, nikawalea hadi wakawa wakubwa”
Nikanyamaza kimya nikijiuliza kama Zena anayemsema bibi ndiye yule anayetaka nioane naye.
“Kwanini umeniuliza hivyo?” Bibi aliniuliza na kunizindua.
“Nimekuuliza tu bibi, kuna mzee mmoja alikuwa akifahamiana na marehemu babu, alinieleza kuhusu kisa hicho ndio nikaona nije nikuulize” nikamdanganya bibi. Sikutaka kumueleza ukweli kwamba kuna mwanamke wa kijini alinituma nimuulize.
“Ulikuwa huamini?”
“Nilikuwa siamini lakini baada ya wewe kunithibitishia sasa ninaamini”
“Wakati babu yako anakufa, watu walishangaa kuona mali yote aliyokuwa nayo imepotea. Na yule mke wake naye hakuonekana tena. Alitoweka wiki moja kabla ya kifo cha babu yako”
“Na huyo babu na mke wake walikuwa wakiishi maisha ya aina gani?”
“Waliishi maisha ya kawaida tu lakini mke wake alikuwa hajitokezi katika shughuli za watu”
“Babu alipokuacha uliona uchungu sana bibi?”
“Kwa kweli niliumia sana kwa sababu sikuwa nimemtenda kosa lolote na bado nilikuwa nampenda babu yako”
“Pole sana bibi”
“Oh! Wanipa pole leo wakati mambo yameshapita zamani!”
“Lakini bibi uliona babu alifanya jambo la busara kuoa mwanamke wa kijini?”
“Alilazimishwa na yule jini na aliahidiwa kupata utajiri. Kuna mganga mmoja aliniambia kama babu yako asingeniacha yule jini angeniua”
“Eh kumbe ni viumbe hatari kiasi hicho!”
“Ndivyo nilivyoambiwa, sijui kama ningeuliwa kweli”
Pakapita ukimya wa sekunde kadhaa. Bibi alikuwa akiendelea kusuka ukili wake na mimi nilikuwa nikiumiza kichwa kwa kuwaza. Hatimaye nikauondoa ule ukimya.
“Kwa mfano mimi nikipata mke wa kijini, unanishaurije nioane naye?” nikamuuliza.
Bibi akacheka.
“Bibi mbona unanicheka?”
“Unanichekesha. Huyo mke wa kijini utampata wapi?”
“Kwani babu alimpata wapi?”
“Yule ni mpaka akuchunuke mwenyewe”
“Sawa. Je akinichunuka na kuniambia anataka tuoane, nikubaliane naye?”
“Hayo ni mawazo yako sasa, mimi nikushauri nini?”
“Unaweza kunishauri kwamba nioane naye au la”
“Hilo sio jambo la kushauriwa, ni uamuzi wako na huyo jini kama utampata. Kwani na wewe unataka kupata utajiri?”
“Hakuna asiyetaka utajiri bibi”
“Angalia sana, utajiri mwingine una matatizo. Ni bora uishi masikini hivyo hivyo”
Baada ya kimya kingine kifupi nikamuaga bibi. Wakati nataka kuondoka nikampa shilingi elfu ishirini. Bibi akanishukuru.
“Haya bibi nakwenda” nikamuaga bibi na kupanda pikipiki yangu.
“Uende salama, nisalimie wenzako”
“Nitakusalimia”
JE JAMAA ATACHUKUA UAMUZI GANI? HEBU ENDELEA KUFUATILIA HADITHI HII
 
SEHEMU YA 17


ILIPOISHIA
Pakapita ukimya wa sekunde kadhaa. Bibi alikuwa akiendelea kusuka ukili wake na mimi nilikuwa nikiumiza kichwa kwa kuwaza. hatimaye nikauondoa ule ukimya.
“Kwa mfano mimi nikipata mke wa kijini, unanishaurije nioane naye?” nikamuuliza.
Bibi akacheka.
“Bibi mbona unanicheka?”
“Unanichekesha. Huyo mke wa kijini utampata wapi?”
“Kwani babu alimpata wapi?”
“Yule ni mpaka akuchunuke mwenyewe”
“Sawa. Je akinichunuka na kuniambia anataka tuoane, nikubaliane naye?”
“Hayo ni mawazo yako sasa, mimi nikushauri nini?”
“Unaweza kunishauri kwamba nioane naye au la”
“Hilo sio jambo la kushauriwa, ni uamuzi wako na huyo jini kama utampata. Kwani na wewe unataka kupata utajiri?”
“Hakuna asiyetaka utajiri bibi”
“Angalia sana, utajiri mwingine una matatizo. Ni bora uishi masikini hivyo hivyo”
Baada ya kimya kingine kifupi nikamuaga bibi. Wakati nataka kuondoka nikampa shilingi elfu ishirini. Bibi akanishukuru.
“Haya bibi nakwenda” nikamuaga bibi na kupanda pikipiki yangu.
“Uende salama, nisalimie wenzako”
“Nitakusalimia”
SASA SONGA NAYO
Nikawasha pikipiki yangu na kuondoka. Wakati narudi mjini mawazo yalikuwa yamesonga katika kichwa changu kuhusu yale maneno aliyonieleza bibi.
Sikuwa nikijua kama babu yangu alimuacha mke wake na kuoa mke wa kijini. Kwa vile babu mwenyewe alikufa zamani habari zake zilikuwa zimeshahaulika.
Lakini nilijiuliza Zena alijuaje habari ile? Nikawa na shaka sana kwamba huyo Zena aliyetajwa na bibi ndiye Zena yule yule.
Nikakumbuka kwamba aliniambia alikuwa na mimi kwa miaka mingi isipokuwa hakuwa amejitokeza kwangu hivyo nilikuwa sijui kama nina jini aliyenichunuka.
Pamoja na kufahamu ukweli wote huo bado nilikuwa na mtihani mgumu mbele yangu, mtihani wa kukubali kuoana na Zena kama alivyoniambia au kumkataa.
Mpaka muda ule naondoka kwa bibi sikuwa na uamuzi wowote. Nilitegemea kupata ushauri kwa kaka yangu na kwa mama yangu.
Nilikwenda moja kwa moja nyumbani kwa kaka. Nikamwambia.
“Ninatoka Mwambani kwa bibi”
“Umezungumza naye?” akaniuliza kwa shauku.
“Nimezungumza naye na anawasalimia”
“Amekuelezaje kuhusu madai ya babu kuoa mke wa kijini?”
“Amesema ni kweli, babu alioa mke wa kijini baada ya kumuacha yeye”
Kaka akashituka.
“Kumbe babu alioa mke wa kijini!”
“Tena alikuwa anaitwa Zena, jina lile lile la huyu anayenifuata mimi”
Kaka alikuwa amepigwa na butwaa.
Nikamueleza kwa kirefu maelezo ya bibi ambayo yalimshangaza sana.
“Isije kuwa jini huyo ndiye huyu huyu amejitokeza tena”
“Hata mimi nimekuwa nikijiuliza swali hilo hilo”
“Huyo bibi alikwambia aliwahi kumuona?’
“Ameniambia hakuwahi kumuona”
“Mimi nadhani jini mwenyewe ndiye huyo huyo, amejitokeza kwako”
“Inawezekana lakini nitakuja kumuuliza tupate uhakika”
“Sasa umeamua nini?”
“Bado ninakabiliwa na maswali mengi. Ninahitaji ushauri wenu ili niweze kuamua”
“Nenda nyumbani umueleze mama, usikilize atakwambia nini”
“Kwa upande wako unanishauri nini?”
“Hili ni suala la kujadiliana sote kwa pamoja lakini kwanza nenda kamueleze mama tusikie kauli yake”
“Sawa. Nitakwenda kumueleza mama”
Baada ya kuzungumza kirefu na kaka nikaondoka nyumbani kwake na kwenda nyumbani kwa mama.
Wakati nafika nyumbani, mama alikuwa amelala. Mjukuu wake alikwenda kumuamsha chumbani. Alipoamka akaja sebuleni.
“Shikamoo” nikamwamkia.
“Marahaba. Habari za huko?” Mama akaniuliza.
“Huko ni kwema. Natoka Mwambani kwa bibi?”
“Ndio ulikwenda kumuuliza kuhusu babu yako?”
“Nimemuuliza ameniambia kwamba babu yetu alimuacha yeye akaoa mke wa kijini”
“Unaniambia ukweli mwanangu?” Mama akaniuliza kwa mshituko.
“Ameniambia bibi mwenyewe”
“Kumbe babu yako alioa mke wa kijini?”
“Alioa, na bibi anasema waliishi pamoja hadi babu alipofikiwa na umauti, yaani wiki moja kabla ya babu kufariki jini huyo alitoweka”
“Kama ni hivyo inaelekea babu yenu alikuwa mtu hatari sana!”
“Bibi ameniambia babu alipomuoa jini huyo alipata utajiri mkubwa, yaani yule jini alimpa utajiri lakini alipokufa utajiri wake ukapotea”
“Hata kama alipata utajiri, si jambo la kukubaliana nalo kirahisi”
“Sasa kitu ambacho kimenitisha ni kuwa huyo jini alikuwa anaitwa Zena kama jini huyu anayenifuata mimi!”
“Isije kuwa ndiye jini huyo huyo. Kwanini alikuwambia uende ukamuulize bibi yako”
“Inawezekana ndiye jini huyo huyo”
“Sasa sikiliza mwanangu, huyo jini epukana naye mara moja!”
“Kwanini mama?”
“Atakuharibia maisha yako, kama ni kuoa oa binaadamu mwenzako si jini”
“Kwa hiyo unanishauri hivyo?”
“Inawezekana ni ushauri au ni amri yangu na naomba unisikilize”
“Sawa, nitakusikiliza. Nilitaka tu nijue una maoni gani”
“Atakapokufuata tena mwambie mimi siwezi kukuoa wewe, nitaoa binaadamu mwenzangu. Kwani majini madume hakuna mpaka akufuate wewe!”
“Ndio nashangaa!”
“Huyo mke wa kijini kweli utamuonesha kwa wa watu, uwambie mke wangu huyu!”
“Hiwezekani”
“Kwanza watu watakushangaa na hawatakuja kwako. Mimi pia sitakuja”
Mama alikuwa amekasirika, sikutaka tena kumjibu kitu. Nikanyamaza kimya.
“Upuuzi mtupu! Amekutia katika misuko suko chungu nzima halafu uje uishi naye kama mke wako, kwanza hao watoto mtakaozaa watakuwa ni watoto wa aina gani...epukama na huyo shetani asikuletee mikosi. Kama ndiye huyo aliyeolewa na babu yako atokomee huko huko alikokuwa. Mimi simtaki!” Mama aliendelea kuniambia kwa hasira.
“Sawa mama nimekusikia”
Nilipoondoka kwa mama nikarudi nyumbani kwangu. Kusema kweli nilikuwa na mawazo mengi sana. Maneno ya mama yalikuwa yameingia akilini mwangu na wakati huo huo nilikuwa nafikiria endapo nitamueleza yule jini kwamba siwezi kuoana naye atanifanya nini.
Wakati naendelea kutafakari nikasikia mlango wangu wa mbele unabishwa. Nikanyanyuka na kwenda kuufungua.
Nilimuona mzee mmoja aliyekuwa amevaa koti jeusi na kanzu ya darizi pamoja na baraghashia. Nikamuamkia.
“Shikamoo mzee?”
“Marahaba, waonaje hali yako?”
“Nzuri, karibu”
“Asante. Nadhani hunifahamu?” akaniuliza.
“Ndiyo sikufahamu mzee wangu”
“Ninaishi mtaa wa pili. Kuna mwanangu mmoja ndiye aliyenielekeza hapa kwako”
“Una tatizo gani?” nikamuuliza kistaarabu.
“Unakumbuka jana majira ya saa nne asubuhi mpaka tano ulikuwa wapi?”
“Nilikuwa maeneo ya mjini”
“Bila shaka ulikuwa umekaa katika Bustani ya Uhuru na msichana mmoja?”
“Ndio nilikuwa nimekaa hapo”
“Nimeambiwa kwamba wakati yule msichana uliyekuwa naye anaondoka, kuna vijana wawili waliokuwa na baiskeli walimpora yule msichana mkoba wake na kukimbia nao, ni kweli?’
“Ni kweli’
“Yule mzee alinyamaza kimya akitafakari kwa sekunde zisizopungua tano kisha akaniuliza.
“Huyo msichana ni nani wako?”
“Tunafahamiana tu, tulikuwa tumekaa tunazungumza”
“Sasa nataka kukueleza kitu kimoja. Mmoja wa wale vijana waliompora huyo msichana ni mwanangu. Jana usiku aliporudi nyumbani hatukulala”
“Kwanini?”
“Yule kijana alipoingia chumbani mwake tulisikia anapiga kelele. Mimi nikaenda kumuuliza ana matatizo gani, akaniambia kwamba kila anapopitiwa na usingizi anamuona mwanamke anampiga bakora. Nikamuuliza ni mwanamke gani huyo, ndio akanieleza kwamba kuna mwanamke walimpora mkoba wake na ndiye huyo anayemuona anampiga bakora.
“Hiyo hali iliendelea hadi asubuhi, kila akifumba macho tu anamuona, anamtandika. Bakora zimeota mgongoni mwake. Huyo mwanamke haonekani, anamuona yeye tu pale anapolala.
“Hii asubuhi tukaenda kwa huyo mwenzake, kumbe na yeye hali ni hiyo hiyo. Amepigwa bakora usiku kucha. Bakora zimeota kwenye mgongo wake. Kwa kweli nimewagombesha sana wale vijana kwa kututia aibu sisi wazazi wao kwa kujihusisha na vitendo vya kihalifu wakiwa bado wadogo, kuibia watu, kupiga watu na kuvuta bangi. Imebidi niwaulize ni mwanamke gani huyo waliyempora mkoba wake ndipo mwanangu aliponielekeza kwako. Kumbe alikuwa anakufahamu.
“Sasa mwanangu nimekuja, nakuomba unioneshe yule mwanamke nimlipe ule mkoba wake na nimuombe radhi ili wale vijana waondokewe na ile hali”
Yale maneno aliyonieleza yule mzee yalinishangaza na kunishitua. Wakati yule mzee ananieleza mimi nilikuwa natokwa na jasho.
“Kwani mpaka hii asubuhi wanaendelea kuchapwa bakora?’ nikamuuliza.
“Labda wakae bila kusinzia au kulala. Wanapolala kidogo tu tayari wanapiga kelele wanasema wanachapwa. Ni mpaka hii asubuhi hawajalala tangu jana wako macho tu. Wameshadhoofika. Kama hii hali itaendelea watakufa”
“Mzee wangu nikwambie ukweli, yule mwanamke tulikutana pale pale. Sijui anapoishi na sidhani kama nitamuona tena”
MMMH! MAMBO HAYO!!! LOH KUMBE YULE MWANAMKE BALAA!!! KWAKWELI ANATISHA!!!
 
SEHEMU YA 18


ILIPOISHIA
“Yule mzee alinyamaza kimya akitafakari kwa sekunde zisizopungua tano kisha akaniuliza.
“Huyo msichana ni nani wako?”
“Tunafahamiana tu, tulikuwa tumekaa tunazungumza”
“Sasa nataka kukueleza kitu kimoja. Mmoja wa wale vijana waliompora huyo msichana ni mwanangu. Jana usiku aliporudi nyumbani hatukulala”
“Kwanini?”
“Yule kijana alipoingia chumbani mwake tulisikia anapiga kelele. Mimi nikaenda kumuuliza ana matatizo gani, akaniambia kwamba kila anapopitiwa na usingizi anamuona mwanamke anampiga bakora. Nikamuuliza ni mwanamke gani huyo, ndio akanieleza kwamba kuna mwanamke walimpora mkoba wake na ndiye huyo anayemuona anampiga bakora.
“Hiyo hali iliendelea hadi asubuhi, kila akifumba macho tu anamuona, anamtandika. Bakora zimeota mgongoni mwake. Huyo mwanamke haonekani, anamuona yeye tu pale anapolala.
“Hii asubuhi tukaenda kwa huyo mwenzake, kumbe na yeye hali ni hiyo hiyo. Amepigwa bakora usiku kucha. Bakora zimeota kwenye mgongo wake. Kwa kweli nimewagombesha sana wale vijana kwa kututia aibu sisi wazazi wao kwa kujihusisha na vitendo vya kihalifu wakiwa bado wadogo, kuibia watu, kupiga watu na kuvuta bangi. Imebidi niwaulize ni mwanamke gani huyo waliyempora mkoba wake ndipo mwanangu aliponielekeza kwako. Kumbe alikuwa anakufahamu.
“Sasa mwanangu nimekuja, nakuomba unioneshe yule mwanamke nimlipe ule mkoba wake na nimuombe radhi ili wale vijana waondokewe na ile hali”
Yale maneno aliyonieleza yule mzee yalinishangaza na kunishitua. Wakati yule mzee ananieleza mimi nilikuwa natokwa na jasho.
“Kwani mpaka hii asubuhi wanaendelea kuchapwa bakora?’ nikamuuliza.
“Labda wakae bila kusinzia au kulala. Wanapolala kidogo tu tayari wanapiga kelele wanasema wanachapwa. Ni mpaka hii asubuhi hawajalala tangu jana wako macho tu. Wameshadhoofika. Kama hii hali itaendelea watakufa”
“Mzee wangu nikwambie ukweli, yule mwanamke tulikutana pale pale. Sijui anapoishi na sidhani kama nitamuona tena”
SASA ENDELEA
Mzee akashituka na kujishika kichwa.
“Mimi nilidhani unajuana na huyo mwanamke. Basi wale vijana hawatakuwa na maisha tena” Mzee akasema kisha akaniuliza.
“Unasema kweli, hujuani naye kabisa?’
“Sijuani naye mzee wangu, siwezi kukudanganya. Tulikutana pale pale, kila mmoja alikuja kivyake na aliondoka kivyake’
Mzee aliduwaa kwa sekunde zisizopungua kumi, alipozinduka aliniuliza.
“Hivi mwanangu utanisaidiaje na balaa hili?”
“Mzee wangu sina namna yoyote ya kukusaidia”
“Tuseme yule mwanamke alikwenda kwa mganga kuwaroga wale vijana?”
“Kwa waswahili hilo jambo linawezekana lakini siwezi kujua”
“Sasa nifanyeje?”
Sikumjibu yule mzee. Alionesha wazi alikuwa amechanganykiwa. Alipoona nipo kimya, aligeuka bila kuniaga na kushuka kwenye baraza ya nyumba yangu. Nikamsikia akisema peke yake.
“Kama hawatakoma, hawatakoma tena!”
Alipofika chini ya baraza ndipo alipokumbuka kuniaga.
“Haya kwaheri mwanangu” akaniambia.
Nilimuangalia yule mzee hadi alipokata kona mtaa wa pili, lakini mawazo yangu yalikuwa kwa Zena. Kitendo kile cha kuwatandika wale vijana bakora kilionesha kuwa mwanamke yule wa kijini alikuwa wa hatari.
Nilikumbuka wakati wale vijana wamempora mkoba wake alionekana mtulivu ingawa alionesha kuwa na hasira. Aliniambia “Waache tu” kumbe alikuwa na lake alilokuwa amelipanga.
Japokuwa niliwahurumia hao vijana lakini sikujua ningempata wapi huyo Zena ili nimwambie awasamehe hao vijana. Na hata kama ningekutana naye na kumwambia hivyo sikudhani kama angenisikia.
Nilirudi ndani na kuendelea kujiwazia. Nilihisi kwamba hata mimi maisha yangu yangeweza kuwa katika hatari kama nitakataa kumuoa Zena na kwa kweli hata hapo nitakapokutana naye nitashindwa kumueleza ukweli kwamba sikubaliani na matakwa yake ya kumuoa.
Kwa vyovyote vile yule mwanamke anaweza kunidhuru!
Nilipowaza hivyo nilitoka tena. Nikafunga mlango wangu na kuondoka na pikipiki yangu, nikaenda nyumbani kwa mama.
Kitendo cha kurudi tena kwa mama kilimshitua, akaniuliza.
“Kulikoni?”
“Nimerudi tena” nikamwambia.
“Ndio mana nimekuuliza kulikoni?”
Nikamueleza mama kile kisa cha yule jini kuwatandika bakora wale vijana waliomuibia mkoba wake.
“Baba wa mmoja wa wale vijana ameniambia hao vijana hivi sasa wako taabani wanamtafuta yule msichana wamuombe msamaha” nikamwambia.
Mama naye alishituka.
“Yaani wanapolala ndio wanamuona huyo msichana anawatandika bakora?”
“Ndio mama, na inakuwa usiku kucha na mchana kutwa. Miili ya wale vijana imeota makora migongoni”
“Huyo jini ni mbaya sana”
“Sasa nimefikiri hata mimi anaweza kuja kuniletea madhara kama nitakataa kumuoa”
“Ni kweli, sasa nikupeleke kwa mganga”
“Wapi?”
“Kule Mnyanjani, ni hodari sana kwa majini”
“Ndio maana nimekuja ili tushauriane kwenda kwa huyo mganga, vinginevyo naweza kupata balaa”
“Sasa nikupeleke lini?”
“Leo, twende leo”
“Saa ngapi?’
“Maliza kazi zako nitakufuata saa tisa twende”
“Sawa. Basi njoo hapo saa tisa twende”
Tulipokubaliana na mama nikaondoka. Wakati nafika nyumbani kwangu nikakutana na yule mzee akiondoka.
“Nimegonga mlango, nimeona kimya. Nilikuwa naenda zangu” akaniambia.
“Nilitoka kidogo”
“Nimekuja kukujulisha kuwa yule mwanangu ameshafariki dunia”
Nikashituka.
“Eh ameshafariki!”
“Amefariki kama nusu saa hivi iliyopita akiwa kwa mganga. Tulikuwa tumempeleka kwa mganga baada ya mateso kumzidia”
“Poleni sana jamani. Yule mwenzake naye anaendeleaje?’
“Sijapata habari zake. Nimekuja kukwambia hivyo, kwaheri mwanangu”
Mzee huyo akaondoka. Nilipata hofu sana. Sikuweza hata kuingia ndani. Niliona kama vile nitakutana na jini huyo, nikageuza pikipiki na kurudi kwa mama.
Nilipofika nilimuhadithia lile tukio la kufa kwa mmoja wa wale vijana.
“Nimekuja nikusubri hapa hapa, sikuingia hata nyumbani kwangu” nikamwambia.
Chakula cha mchana nilikula pale pale kwa mama. Baada ya kula ndipo tulipoondoka. Nilimpakia mama kwenye pikipiki tukaelekea huko Mnyanjani.
Wakati huo eneo hilo la Mnyanjani lilikuwa kama kitongoji cha mji huo. Likiwa karibu na ufukwe wa Bahari ya Hindi, lilikuwa moja ya maeneo ya kiasili ya mji wa Tanga yenye historia iliyosheheni utamaduni wa jiji hilo.
Eneo hilo hivi sasa limebadilika na kuwa na nyumba za kisasa na kuwa sehemu ya jiji hilo.
Ili ufike Mnyanjani unapita vitongoji kadhaa pamoja na viunga vya minazi. Ni mwendo wa karibu kilometa kumi.
Mama alinionesha nyumba ya mganga huyo iliyokuwa imejengwa kwa miti na udongo na kuezekwa makuti ya minazi.
Tukasimama na kubisha mlango.
“Karibuni” tukasikia sauti ya kiume ikitukaribisha.
Tukaingia ndani. Ukumbi ulikuwa giza. Kulikuwa na mwanga hafifu uliotokea kwenye mlango wa nje na wa uani.
Mganga mwenyewe alikuwa amekaa kwenye jamvi lililokuwa limetandikwa pale ukumbini. Alikuwa akikatakata mizizi ya dawa.
“Karibuni” akatuambia tena huku akitutazama.
“Tumeshakaribia” mama akamwambia na kisha kumuuliza hali.
Mimi nikamuamkia. “Shikamoo”
“Marahaba. Karibuni mkake kwenye jamvi”
Tukakaa kwenye jamvi.
“Tumekuja tuna shida” Mama akaanza kumwambia mzee huyo aliyekuwa amevaa kikoi cha rangi nyeupe.
“Shida gani?”
MAMBO YAMEFIKA KWA WAGANGA. JE MGANGA HUYO ATAWEZA KUPAMBANA NA MWANAMKE HUYO WA KIJINI AMBAYE AMESHAONESHA SI WA KUCHEZEA?
 
SEHEMU YA 19



ILIPOISHIA
Wakati huo eneo hilo la Mnyanjani lilikuwa kama kitongoji cha mji huo. Likiwa karibu na ufukwe wa Bahari ya Hindi, lilikuwa moja ya maeneo ya kiasili ya mji wa Tanga yenye historia iliyosheheni utamaduni wa jiji hilo.
Eneo hilo hivi sasa limebadilika na kuwa na nyumba za kisasa na kuwa sehemu ya jiji hilo.
Ili ufike Mnyanjani unapita vitongoji kadhaa pamoja na viunga vya minazi. Ni mwendo wa karibu kilometa kumi.
Mama alinionesha nyumba ya mganga huyo iliyokuwa imejengwa kwa miti na udongo na kuezekwa makuti ya minazi.
Tukasimama na kubisha mlango.
“Karibuni” tukasikia sauti ya kiume ikitukaribisha.
Tukaingia ndani. Ukumbi ulikuwa giza. Kulikuwa na mwanga hafifu uliotokea kwenye mlango wa nje na wa uani.
Mganga mwenyewe alikuwa amekaa kwenye jamvi lililokuwa limetandikwa pale ukumbini. Alikuwa akikatakata mizizi ya dawa.
“Karibuni” akatuambia tena huku akitutazama.
“Tumeshakaribia” mama akamwambia na kisha kumuuliza hali.
Mimi nikamuamkia. “Shikamoo”
“Marahaba. Karibuni mkae kwenye jamvi”
Tukakaa kwenye jamvi.
“Tumekuja tuna shida” Mama akaanza kumwambia mzee huyo aliyekuwa amevaa kikoi cha rangi nyeupe.
“Shida gani?”
SASA ENDELEA
Mama akamueleza mkasa mzima. Yule mganga naye alishangaa akasema.
“Huyo atakuwa Ummi Subian au Kamari wa Subian”
“Tunataka aondoke kwa mwanangu, asimfuate fuate tena”
“Ngoja nimtazame nijue ni jini gani”
Mganga akachukua kitabu akakifungua kisha akatazama saa yake.
“Ni saa nane sasa” alisema peke yake kisha akatazama kwenye kitabu.
“Aliyetawala muda huu ni Zuhra Kadhi Lhawaiju” Mganga aliendelea kujisemea kisha akatutazama.
“Huyu mwanamke wa kijini ni ruhani aliyechanganya na usubian”
“Yeye mwenyewe pia aliniambia hivyo hivyo” nikamkubalia mganga huyo.
“Hawa majini ni ving’ang’anizi sana na ni wabishi, akitaka jambo lake ni mpaka alitimize”
“Lakini ataweza kumuacha huyu mwanangu?” Mama akamuuliza kwa wasiwasi.
“Ni kazi kubwa. Huyu jini ni wa kurithi, zamani aliwahi kuwa na babu yake huyu kijana”
“Ni kweli, bibi yangu alinieleza leo” nikamwambia mganga huyo.
“Alikuelezaje?”
“Aliniambia kuwa babu yangu alikuwa na mke wa kijini, anaitwa Zena”
Mganga akamtazama mama.
“Unasikia. Sasa kumtoa jini wa aina hii inataka kazi kubwa, si kazi ndogo”
“Sasa tufanyeje?” Mama akamuuliza.
“Nitahitaji mbuzi watatu, wa rangi nyeupe, rangi nyeusi na rangi mchanganyiko” Mganga alituambia kisha akatuuliza.
“Mtaweza kuwapata?”
“Watapatikana” nikajibu mimi.
“Mbali na hao mbuzi watatu, mnipatie maji ya bahari lita tatu, mchanga wa pwani unaofikia kilo moja na kipande cha mti kilichotoka katika eneo lililopiganwa vita”
“Hicho kipande cha mti tutakipata wapi?” nikamuuliza.
“Najua hiki kitawapa tabu, nitawapatia mimi”
“Huo mchanga wa pwani na maji ya bahari pia ungetusaidia wewe, tunaona hapa ni karibu na bahari”
“Gharama yake itakuwa shilingi elfu kumi na tano”
“Sawa.Tutatoa”
“Hao mbuzi watatu pia mnaweza kuwapata hapa hapa kama mtataka”
“Watakuwa kiasi gani?”
“Kila mbuzi mmoja ni shilingi elfu arobaini”
“Kwa hiyo kwa mbuzi watatu itakuwa shilingi laki moja na ishirini elfu”
“Ingiza na hizi elfu kumi na tano za vifaa”
“Zitakuwa laki moja na hamsini na tano elfu”
“Na kazi yangu shilingi laki moja”
“Jumla laki mbili na hamsini na tano elfu”
“Hizo pesa zikipatikana, njooni niwafanyie kazi yenu”
“Pesa zipo lakini zipo nyumbani, labda utupe muda nikazichukue” nikamwambia mganga huyo.
“Hizo pesa nikizipata leo, kwanza nitashughulikia kupata hivyo vitu, Kesho saa mbili asubuhi ndio nitakushughulikia wewe mwenyewe”
“Sawa. Sasa acha turudi. Baadaye nitakuja na hizo pesa.
Baada ya kukubaliana na mganga huyo tuliondoka. Nilimpakia mama kwenye pikipiki nikamrudisha nyumbani kwake kisha mimi nikaenda nyumbani kwangu kuchukua hizo pesa. Zilikuwa ni pesa zile zile alizonipa Zena.
Nilitia mfukoni shilingi laki tatu nikaondoka tena na pikipiki kwenda Mnyanjani. Nilipofika nilimpa yule mganga shilingi laki mbili na hamsini na tano elfu.
“Sasa nenda, uje kesho saa mbili asubuhi, utakuta kila kitu kipo tayari” Mganga akaniambia.
“Sasa nilikuwa na ombi moja” nikamwambia.
“Ndio”
“Nina wasiwasi huyo jini anaweza kunifuata hii leo kutokana na hivi ambavyo nataka kumshughulikia, sasa itakuwaje?
“Nitakupa hirizi, kuwa nayo mfukoni hadi hapo kesho”
“Nikiwa na hiyo hirizi hatanifuata?’
“Abadani. Hawezi kukufuata”
“Basi nipatie hiyo hirizi’
Hirizi yenyewe ilikuwa imeshatayarishwa tayari. Mganga akanipatia. Nikaichukua na kuitia mfukoni.
Nikatoka na kupanda pikipiki yangu. Sasa kidogo moyo wangu ulikuwa na matumaini. Ile hofu niliyokuwa nayo ya kukutana na Zena ilikuwa imenitoka.
Wakati nakaribia kulitoka eneo la Mnyanjani, niliona mtu amesiamama pembeni mwa barabara chini ya mti wa mwembe. Nilipoukaribia mwembe huo nilishituka nilipoona mtu mwenyewe alikuwa Zena. Alikuwa amesimama kama aliyekuwa akisubiri mtu.
Nikaongeza mwendo ili kumkwepa na nikajifanya sikumuona. Wakati pikipiki imeshika kasi nikahisi kama kulikuwa na kitu nyuma yangu. Nikageuza uso wangu kutazama nyuma. Nilishituka tena. Alikuwa ni Zena aliyekuwa amekaa kwenye siti ya nyuma ya pikipiki yangu!
Sikuweza kujua alipakiaje kwenye pikipiki yangu wakati alikuwa amesimama kwenye mti ambao nilikwishaupita, tena nikienda kwa kasi. Kutokana na mshituko nilioupata mikono yangu ilitetereka nikajikuta ninaanguka na pikipiki. Mimi na Zena tukawa chini!
Nikainuka haraka. Lakini Zena alikuwa mwepesi zaidi. Nilimkuta tayari ameshasimama.
DUH! JAMAA AMEKWAMA! KAPEWA HIRIZI LAKINI JINI KAMTOKEA HIVYO HIVYO. Sijui itakuwaje?
 
SEHEMU YA 20



ILIPOISHIA
Hirizi yenyewe ilikuwa imeshatayarishwa tayari. Mganga akanipatia. Nikaichukua na kuitia mfukoni.
Nikatoka na kupanda pikipiki yangu. Sasa kidogo moyo wangu ulikuwa na matumaini. Ile hofu niliyokuwa nayo ya kukutana na Zena ilikuwa imenitoka.
Wakati nakaribia kulitoka eneo la Mnyanjani, niliona mtu amesiamama pembeni mwa barabara chini ya mti wa mwembe. Nilipoukaribia mwembe huo nilishituka nilipoona mtu mwenyewe alikuwa Zena. Alikuwa amesimama kama aliyekuwa akisubiri mtu.
Nikaongeza mwendo ili kumkwepa na nikajifanya sikumuona. Wakati pikipiki imeshika kasi nikahisi kama kulikuwa na kitu nyuma yangu. Nikageuza uso wangu kutazama nyuma. Nilishituka tena. Alikuwa ni Zena aliyekuwa amekaa kwenye siti ya nyuma ya pikipiki yangu!
Sikuweza kujua alipakiaje kwenye pikipiki yangu wakati alikuwa amesimama kwenye mti ambao nilikwishaupita, tena nikienda kwa kasi. Kutokana na mshituko nilioupata mikono yangu ilitetereka nikajikuta ninaanguka na pikipiki. Mimi na Zena tukawa chini!
Nikainuka haraka. Lakini Zena alikuwa mwepesi zaidi. Nilimkuta tayari ameshasimama.
SASA ENDELEA,
“Inua pikipiki yako” akaniambia.
Nikiwa nimetahayari nikaushika usukani wa pikipiki na kuiinua.
“Isimamishe” akaniambia tena.
Nikaiwekea standa.
“Unatoka wapi?”
“Mimi?’
“Jamani kwani nazungumza na nani?”
“Natoka kule…”
“Wapi?”
“Mnyanjani”
“Kufanya nini?”
Nikatunga uongo.
“Kumsalimia mjomba wangu”
Zena akanitazama kwa karibu nusu dakika bila kuniambia chochote. Bila shaka aligundua kuwa nilikuwa namdanganya. Wakati Zena akinitazama jasho jembamba lilikuwa linanitoka. Nilikuwa nikilihsi likitiririka kwenye uti wa mgongo wangu.
Nilikuwa najiuliza yule mganga alinipa hirizi akaniambia nikiwa nayo mfukoni Zena hatanifuata, mbona niko naye hapa?
“Humo mfukoni umetia nini?” Sauti ya Zena ikanishitua.
Alikuwa akiutazama mfuko wa suruali yangu ambao nilitia ile hirizi.
“Wapi?” nikamuuliza tena nikijifanya sikumuelewa.
“Nimekuuliza humo mfukoni mwako umetia nini?” Zena akaniuliza tena sasa kwa sauti ya ukali kidogo.
“Sijatia kitu, ni pesa zangu tu” nikamjibu.
“Hebu tia mkono wako mfukoni” akaniambia.
Nikatia mkono kwenye mfuko mwingine.
“Sio huo, tia kwenye mfuko huu”
Zena alinionesha mfuko huo kwa kidole chake.
Nikatia mkono kwenye mfuko huo.
“Hebu toa hicho kitu ulichokigusa”
Bila kupenda niliitoa ile hirizi.
“Hebu nioneshe”
Nikamuonesha, hata haikumshtua.
Akaishika na kuiweka kwenye kiganja chake kisha akanitazama.
“Nini hii?’ akaniuliza kwa dharau.
Sikumjibu. Nilikuwa nimefadhaika sana.
“Wewe unajidanganya sana, sikujua kama unaweza kuwa mpumbavu kiasi hicho. Shika hirizi yako” akaniambia.
Nikaichukua ile hirizi.
“Itupe kule!” akaniambia akinionesha kitu kilichokuwa kando yetu.
Nikaitupa. Ningefanyaje? Sikuwa na la kufanya. Hirizi yenyewe haikumtisha hata kidogo. Bora kuitupa tu.
“Nipakie twende zetu” akaniambia akiwa ameridhika kwa kile kitendo cha kuitupa ile hirizi.
Sikutaka hata kumuuliza twende wapi, nikawasha pikipiki iliyokuwa imezimika kisha nikaipanda. Zena akakaa nyuma yangu. Nikatia gea na kuondoka.
Nilikuwa naendesha pikipiki huku natetemeka mpaka Zena akaniuliza.
“Unatetemeka nini?”
“Sitetemeki” nikamjibu huku nikijua kuwa nilikuwa natetemeka.
Akanyamaza kimya. Hakunisemesha kitu mpaka tulipoingia mjini.
“Nishushe hapa” akaniambia mara tu tulipoipita hospitali ya Makorora.
Nikashukuru kusikia kauli hiyo. Nilikuwa nikihisi kama nimepakia chatu nyuma yangu. Nikaisimamisha pikipiki haraka na kushusha mguu wangu.
Zena akashuka.
“Niache hapa hapa. Wewe nenda zako” akaniambia.
Ingawa sauti yake ilikuwa tulivu lakini uso wake ulikuwa umekasirika. Nikamuona anavuka barabara na kuelekea upande wa hospitali ya Makorora.
Nikatia gea na kuiondoa pikipiki yangu taratibu. Sikutazama nyuma tena. Nilipofika kwenye mzunguko wa barabara ya Pangani nilikata kulia nikaelekea nyumbani kwa mama. Sikutaka kwenda nyumbani kwangu ingawa palikuwa karibu na hapo.
Nilipofika nyumbani kwa mama nikamueleza tukio zima lililokuwa limenitokea. Mama akashituka.
“Sasa huyo shetani amekwenda wapi?” akaniuliza.
“Sijui amekwenda wapi. Nimemuacha karibu na hospitali ya Makorora”
“Ina maana alikufutilia kule kwa mganga”
“Nafikiri. Amejua kuwa nimepewa hirizi na akaona iko mfukoni mwangu”
“Sasa itakuwaje?”
“Hata sijui. Hapa mwili wote unanitetemeka”
“Sasa ungerudi umueleze yule mganga”
“Unanishuri nirudi tena kwa yule mganga?”
“Ndio. Umueleze habari yote. Yeye ndio atajua la kufanya”
“Sasa twende sote. Yule jini asije akanifuata tena”
“Ngoja twende”
Dakika chache baadaye mimi na mama yangu tukawa kwenye pikipiki tukielekea Mnyanjani kwa yule mganga. Tulipofika pale mahali nilipoanguka na pikipiki nilimuonesha mama.
“Mahali tulipoanguka ni hapa” nikamwambia.
“Na huyo jini mwenyewe ulimuona amesimama wapi?”
“Alikuwa amesimama kwenye mti ule pale”
Nikamuonesha mti wa mwembe nilipomuona Zena amesimama.
“Inaonekana alikuwa akikufuatilia wewe” Mama akaniambia.
Tulipofika nyumbani kwa mganga tulikuta vilio vimetawala ndani ya nyumba huku nyumba yenyewe imeja watu hadi nje.
“Kuna nini?” nikamuuliza mama kabla ya kushuka kwenye pikipiki.
“Ngoja tuulize” Mama akaniambia.
Tulishuka kwenye pikipiki. Mtu mmoja alipotuona tulikuwa wageni akatufuata.
“Karibuni” akatuambia.
“Tumeshakaribia” Mama akamjibu.
“Habari za hapa?” nikamuuliza.
“Hapa si kwema, tumepata msiba” yule mtu akatuambia.
“Msiba wa nani?”
“Msiba wa huyu bwana aliyekuwa anaishi katika nyumba hii”
Nikatazamana na mama yangu kisha nikaendelea kumuuliza yule mtu.
“Sisi tunachojua ni kuwa mwenye nyumba hii ni yule mganga wa kienyeji”
“Niye huyo huyo aliyefariki”
Nikatazamana tena na mama yangu, sasa kwa mshituko.
“Dakika chache tu zilizopita si nilikuwa naye hapa?” nikauliza.
“Kufariki kwake kulikuwa kwa miujiza sana. Niliambiwa alikuwa akizungumza na mteja wake mmoja aliyefika na pikipiki, nafikiri ulikuwa wewe”
“Nadhani nilikuwa mimi kwani si muda mrefu sana nilipoondoka hapa”
“Basi mara tu ulipoondoka, yule mganga aliingia chumbani mwake. Mke wake alikuwa jikoni akasikia sauti ya mume wake akipiga kelele kuwa anakabwa na mwanamke. Mpaka mke wake anaingia chumbani alimkuta ameshakufa”
“Nikaguna na kumtazama mama.
“Mama umelisikia hilo tukio?”
“Nimelisikia” Mama akajibu kwa sauti iliyonywea kisha akaniambia.
“Basi twende zetu”
“Nilikuwa nimempa pesa kwa ajili ya kunifanyia kazi yangu ambayo tulipatana aifanye kesho lakini nitamsamehe” nikasema.
“Ulimpa kiasi gani?’ yule mtu akaniuliza.
“Kama laki mbili hivi. Lakini nitasamehe”
“Kama umeamua kuzisamehe ni jambo zuri”
“Poleni sana kwa msiba huo” nikamwambia na kupanda kwenye pikipiki yangu.
“Haya kwaheri baba” Mama akumuaga yule mtu kabla ya kukaa nyuma yangu. Tukaondoka.
WASOMAJI WANGU, MAMBO HAYO! MGANGA AMESHAUAWA! NAFIKIRI JAMAA HATAKUWA NA UJANJA TENA! LAKINI HADITHI INAENDELEA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom