Simulizi ya kweli: Mwanamke jini

Simulizi ya kweli: Mwanamke jini

SEHEMU YA 21


ILIPOISHIA
Nikatazamana tena na mama yangu, sasa kwa mshituko.
“Dakika chache tu zilizopita si nilikuwa naye hapa?” nikauliza.
“Kufariki kwake kulikuwa kwa miujiza sana. Niliambiwa alikuwa akizungumza na mteja wake mmoja aliyefika na pikipiki, nafikiri ulikuwa wewe”
“Nadhani nilikuwa mimi kwani si muda mrefu sana nilipoondoka hapa”
“Basi mara tu ulipoondoka, yule mganga aliingia chumbani mwake. Mke wake alikuwa jikoni akasikia sauti ya mume wake akipiga kelele kuwa anakabwa na mwanamke. Mpaka mke wake anaingia chumbani alimkuta ameshakufa”
“Nikaguna na kumtazama mama.
“Mama umelisikia hilo tukio?”
“Nimelisikia” Mama akajibu kwa sauti iliyonywea kisha akaniambia.
“Basi twende zetu”
“Nilikuwa nimempa pesa kwa ajili ya kunifanyia kazi yangu ambayo tulipatana aifanye kesho lakini nitamsamehe” nikasema.
“Ulimpa kiasi gani?’ yule mtu akaniuliza.
“Kama laki mbili hivi. Lakini nitasamehe”
“Kama umeamua kuzisamehe ni jambo zuri”
“Poleni sana kwa msiba huo” nikamwambia na kupanda kwenye pikipiki yangu.
“Haya kwaheri baba” Mama akumuaga yule mtu kabla ya kukaa nyuma yangu. Tukaondoka.
SASA ENDELEA
“Mama umeona mambo hayo!” nikamwambia mama wakati ninaendesha pikipiki kurudi mjini.
“Nimeona. Kwa kweli ni kifo cha kushangaza sana”
“Mimi nadhani ni yule jini amekuja kumuua yule mganga”
“Itakuwa ndiye yeye, kwa sababu alisema kuna mwanamke anamkaba. Sasa alikuwa mwanamke yupi kama sio yule jini?”
“Sasa haya yamekuwa mapambano!”
“Tutatafuta mganga mwingine”
“Sasa usalama wangu utakuwa wapi? Nimeshashuhudia watu wawili waliouawa leo. Yule kijana aliyekuwa anatandikwa na huyu mganga. Bado kuna na yule kijana mwingine. Naona pia atakuwa ameshakufa”
“Tukifika tutakwenda kulizungumza vizuri hili suala pamona na kaka yako”
“Sasa nimeshaona huyu mwanamke ni wa hatari”
Nilimpeleka mama nyumbani kwake kisha nikaenda Chuda kumchukua kaka.
Nilimueleza kwa kifupi hayo matukio.
“Mama ameniambia nije nikuchkue twende tukayazungumze haya mambo”
Ule muhutasari wa habari niliomueleza kaka tayari ulikuwa.
Nikampakia kwenye pikipiki yangu tukaondoka.
Tulipofika nyumbani kwa mama tukalizungumza lile suala ambalo kaka lilimshitua sana.
“Kumbe yule jini ni hatari sana. Tulivyomuona pale mahakamani siku ile alionekana ni msichana mpole sana” Kaka akasema kwa mshangao.
“Lile umbile ulilomuona nalo ni la kujipachika, si umbile lake halisi. Katika umbile lake halisi anatisha” nikamwambia kaka.
“Kwa kweli inabidi muepukane haraka, sasa tutafanyaje wakati mtaalamu muliyemtegemea ndio ameuawa kwanza?”
“Itakuja kuwa yeye!” Mama akamalizia akimaanisha mimi.
“Sasa tufanyeje jamani, jua linakuchwa hili!” nikawahimiza wenzangu.
“Hapa la kufanya ni kumuona mganga mwingine haraka iwezekanavyo” Kaka akashauri.
“Bila kupata mganga mwingine, mimi leo sitalala, nina hofu” nikawambia.
“Usijali, tutkwenda kwa mganga wa Amboni. Yeye pia namfahamu. Ni hodari” Mama akasema.
“Sasa twende sasa hivi kwa sababu jua linakuchwa”
“Ingekuwa kaka yako anapafahamu angekupeleka lakini itabidi nikupeleke mimi”
“Mpeleke tu halafu mtakuja kunijulisha” Kaka akamwambia mama.
Dakika chache baadaye tulikuwa tumetoka nje, nilimpakia mama kwenye pikipiki. Kaka yangu naye akaondoka kurudi kwake kwa miguu.
Amboni ni kitongoji cha mji wa Tanga kinachokuwa kwa haraka. Kipo katika barabara ya Horohoro inayokwenda Mombasa nchini Kenya. Kutoka Tanga hadi Amboni ulikuwa mwendo upatao kilometa nane hivi.
Kitongoji hicho kimepata umaarufu kutokana na mapango yaliyoko katika eneo hilo, maarufu kama Mapango ya Amboni.
Wakati tunafika Amboni jua lilikuwa limeshakuchwa. Matumaini yangu yalikuwa madogo sana kupata huduma katika muda ule. Hofu yangu kubwa ilikuwa ni kwa usiku. Kama Zena alikusudia kunifanyia jambo baya lolote, nilijua kuwa alikuwa akisubiri usiku nikiwa niko nyumbani peke yangu.
Hapo Amboni palikuwa na eneo linaitwa Mafuriko. Eneo hilo liliwahi kupata mafuriko makubwa katika miaka ya nyumba na kusababisha kupewa jina hilo.
Mganga tuliyemuendea alikuwa akiishi katika eneo hilo. Kwa vile mama aliwahi kufika kwa mganga huyo katika siku za nyuma hatukusumbuka kuuliza. Tulikwenda moja kwa moja kwenye nyumba yake.
Tulikuta mzee aliyeketi barazani mwa nyumba hiyo akivuta Mtemba. Alikuwa amekaa kwenye kiti cha uvivu kando ya mlango wa nyumba yake.
Kumbe alikuwa ndiye mganga mwenyewe tuliyemuendea.
Tulisaliana naye. Mama akamwambia kuwa tulikuwa tumemfuata yeye.
“Karibuni ndani” akatuambia.
Nikapata matumaini kidogo.
Mganga huyo alikuwa na chumba chake maalum cha uganga. Tulipoingia katika chumba hicho alitukaribisha kwenye majamvi, yeye mwenyewe aliketi kwenye kigoda kidogo kilichokuwa kwenye pembe moja ya ukuta.
“Habari za huko mtokako?” akatuuliza.
“Habari si nzuri. Tuna matatizo” Mama akamwambia.
“Matatizo gani?”
“Ni matatizo ambayo si ya kawaida. Huyu niliyenaye hapa ni mwanangu. Yeye ndiye anayehusika na hayo matatizo….”
Mama akamueleza matatizo yaliyokuwa yametupeleka. Mganga akatuambia.
“Subirini kidogo niwaite wenyewe muwaeleze”
Akamuita mke wake. Mwanamke huyo alipokuja alimwambia amletee moto. Baada ya muda kidogo mwanamke huyo alileta makaa ya moto kwenye chetezo ambacho alikiweka mbele ya mganga huyo.
“Niletee mavumba yangu na shuka yangu” Mganga akaendelea kumuagiza.
Mwanamke huyo alikwenda pembeni mwa chumba hicho ambako kulikuwa na meza iliyokuwa na vitabu pamoja na vichupa na vikopo kopo. Alichukua kikopo kimoja, akatungua na shuka moja ya rangi nyeupe iliyokuwa imetundikwa kwenye ukuta.
Alikwenda navyo kwa mganga akakiweka kile kikopo mbele yake kisha akamfinika ile shuka pale alipokuwa amekaa.
“Na wewe ukae hapa hapa, usiondoke” Mganga akamwambia mwanamke huyo.
Mwanamke huyo akakaa karibu yetu.
Mganga alikisogeza kile chetezo cha moto karibu yake kisha akakifungua kile kikopo kilichokuwa na mavumba akachota kidogo na kuyatia kwenye ule moto kisha akajifinika shuka vizuri ili ule moshi uliokuwa unafuka uingie ndani ya ile shuka.
Baada ya sekunde chache yule mganga akaanza kusema maneno niliyodhani kuwa yalikuwa ya lugha ya Kijerumani.
Nilisikia maneno kama “Dachi…pontia…n
a mengine ambayo sikuweza kuyakariri.
Wakati huo uso wake alikuwa ameufunika ndani ya shuka. Ghafla akafunua shuka na kuutoa uso wake. Alikisogeza kile chetezo pembeni kisha akatutazama.
“Dachi…jerumani nimekuja hapa” akasema lakini hatukuelewa maana ya maneno yale.
Mke wa mganga akatueleza.
“Anasema yeye ni jini wa Kijerumani anaitwa Dachi, amekuja kuwasikiliza”
“Sawa, tumemuelewa” Mama akamjibu.
“Asalaam aleykum” mganga akaendelea kwa kutupa salamu.
“Wa alaykumu salaam” tukamuitikia.
“Nini shida yenu?”
“Mwanangu anasumbuliwa na jini mwanamke” Mama akamwambia.
“Mwanao yuko wapi?”
“Huyu kijana niliyenaye hapa”
“Oh mwano amepata mchumba wa kijini, anaitwa Zainush”
Mgnga huyo alipotuambia hivyo mimi na mama tukatazamana. Tulitazamana kwa mshangao kwa jinsi alivyoweza kujua lile jina la Zena ambalo hatukuwa tumelitaja.
“Mwanangu hataki mchumba wa kijini, tunataka aondoke asimfuate tena mwanangu” Mama akamwambia.
ENDELEA KUFUATILIA
 
SEHEMU YA 22


ILIPOISHIA
Baada ya sekunde chache yule mganga akaanza kusema maneno niliyodhani kuwa yalikuwa ya lugha ya Kijerumani.
Nilisikia maneno kama “Dachi…pontia…n
a mengine ambayo sikuweza kuyakariri.
Wakati huo uso wake alikuwa ameufunika ndani ya shuka. Ghafla akafunua shuka na kuutoa uso wake. Alikisogeza kile chetezo pembeni kisha akatutazama.
“Dachi…jerumani nimekuja hapa” akasema lakini hatukuelewa maana ya maneno yale.
Mke wa mganga akatueleza.
“Anasema yeye ni jini wa Kijerumani anaitwa Dachi, amekuja kuwasikiliza”
“Sawa, tumemuelewa” Mama akamjibu.
“Asalaam aleykum” mganga akaendelea kwa kutupa salamu.
“Wa alaykumu salaam” tukamuitikia.
“Nini shida yenu?”
“Mwanangu anasumbuliwa na jini mwanamke” Mama akamwambia.
“Mwanao yuko wapi?”
“Huyu kijana niliyenaye hapa”
“Oh mwano amepata mchumba wa kijini, anaitwa Zainush”
Mgnga huyo alipotuambia hivyo mimi na mama tukatazamana. Tulitazamana kwa mshangao kwa jinsi alivyoweza kujua lile jina la Zena ambalo hatukuwa tumelitaja.
“Mwanangu hataki mchumba wa kijini, tunataka aondoke asimfuate tena mwanangu” Mama akamwambia.
SASA ENDELEA
“Yule jini ni mkorofi, ameshaua watu watatu” Mganga huyo aliendelea kutuambia.
Tukatazamana tena na mama. Mama hakulieleza suala hilo la watu waliouawa, yaani yule mganga wa Mnyanjani na wale vijana wawili walioiba mkoba wa Zena.
Tukawa tunajiuliza amelijuaje tukio hilo la kuuawa kwa yule mganga na wale vijana.
Kama ambaye aliyagundua mawazo yetu, mganga huyo akacheka.
“Huyo jini anakufuata wewe kila wakati, ameshapata wasiwasi. Anajua unataka kumfukuza” akatuambia.
Alinyamaza kimya kisha akaendelea.
“Lakini mimi haniwezi, naweza kumpiga makofi mara moja”
“Sasa utatusaidiaje?” nikamuuliza mganga huyo.
“Mimi naweza kumuita halafu nitamfunga kamba, hataweza kukufuata tena”
“Utamuita lini?” nikamuuliza tena.
“Nitamuita kesho”
“Sasa leo akija kunidhuru usiku?”
“Nitamzuia” Mganga akaniambia kisha akaitenga shuka na kunyanyuka.
“Nisubirini hapa hapa” akatuambia na kutoka.
Tulisubiri kwa karibu nusu saa. Mke wake alituambia kuwa mganga huyo alikuwa amekwenda kuchuma dawa makaburini.
Aliporudi alikuwa ameshika rundo la majani, akampa mke wake.
“Yaroweke kwenye maji” alimwambia.
Mke wake aliyekuwa ameketi na sisi aliinuka na kuyachukuaa yale majani.
“Changanya na huu mvuje” Mganga aliendelea kumwambia mke wake huku akielekea kwenye meza iliyokuwa na chupa na makopokopo. Alichukua kopo mojawapo akachota kiasi cha mvuje uliokuwa umesagwa na kumpa mke wake.
Baada ya hapo mganga alirudi kwenye kigoda chake.
“Nimekutayarishia dawa ambayo utakwenda kuoga na nyingine utajifukiza” akaniambia.
“Sawa. Kwa hiyo nitakwenda kuoga nyumbani?”
“Hapana. Utaoga hapa hapa na utajifukiza hapa hapa”
“Sawa”
Baada ya kama dakika tano hivi mke wa mganga alirudi akiwa amebeba ndoo ya maji ambayo aliitia yale majan.
“Tayari” akasema.
“Sasa nenda kamuwekee chooni” Mgnaga akamwambia.
Mwanamke huyo akaibeba tena ndoo hiyo na kutoka nayo.
Mganga akanitazama.
“Mfuate, utakwenda kuyaoga yale maji yote” akaniambia.
Nikanyanyuka na kumfuata yule mwanamke. Tulitoka uani mwa ile nyumba. Mwanamke huyo aliingia kwenye choo akaiweka ile ndoo kisha akatoka.
“Haya nenda sasa’ akaniambia.
Nikaingia kwenye kile choo. Nilivua nguo nikazitundika kwenye mlango wa choo. Niliona kata iliyokuwa imetiwa kwenye ndoo nyingine niliyoikuta mle chooni, nikaichukua na kujimwagia yale maji. Yalikuwa yakinuka harufu mbaya sana isiyovumilika.
Lakini kwa vile nilikuwa na shida nilivumilia hivyo hivyo. Nilipomaliza nilijifuta futa maji kwa mikono kisha nikavaa nguo zangu na kutoka na ile ndoo ambayo niliiacha pale uani.
Nilienda kule chumbani kwa mganga huku maji yakiwa yametosa shati langu.
“Umeshaoga?” Mganga akaniuliza.
“Nimeoga” nikamjibu.
“Umemaliza maji yote?”
“Nimeyamaliza yote”
“Sasa bado dawa ya kujifukiza” Mganga aliniambia kisha akawageukia mke wake na mama yangu.
“Hebu mpisheni ajifukize dawa” akawambia.
Mama yangu na yule mwanamke wakatoka.
Mganga akanipa shuka.
“Vaa shuka. Vua nguo zako kisha chutama ujifukize dawa”
Nikajifunga ile shuka kiunoni kisha nikavua suruali yangu pamoja na shati. Mganga alinisogezea kile chetezo cha moto. Akakitia aina fulani ya dawa ya unga. Chetezo kikawa kinatoa moshi.
Nilikuwa nimeshachutama. Ile shuka ndio nilijifunika kukinga ule moshi uingie mwilini mwangu. Harufu yake ilifanana na yale maji niliyooga.
Wakati ule moshi ukinipata mwilini. niliisikia sauti ya mganga akisema maneno kwa lugha ambayo sikuweza kuijua huku akilitaja jina la Zainush.
Moshi ulipokwisha, mganga aliniambia nininuke na nivae nguo zangu. Nikainuka na kuvaa nguo.
“Sasa kazi yako imekwisha kwa leo, rudi nyumbani ila kesho asubuhi uje tena” Mganga akaniambia.
“Hii kazi yaa leo ni shilingi ngapi?” nikamuuliza mganga huyo.
“Kwa leo utanipa shilingi elfu ishirini”
“Nikatoa shilingi elfu ishirini na kumpa mganga huyo.
“Sasa mnaweza kwenda zenu”
“Yule jini hataweza kunifuata tena leo?” nikamuuliza.
Mganga akatikisa kichwa.
“Hawezi kukufuata. Hiyo harufu unayonuka hataweza hata kukusogelea”
“Nashukuru sana’
“Ila kumbuka kitu kimoja. Ukifika nyumbani usioge tena. Lala hivyo hivyo”
“Sawa”
Baada ya kumalizana na mganga huyo nilitoka ukumbini. Mama yangu alikuwa amekaa na mke wa mganga, nikamwambia.
“Twenzetu”
“Umeshamaliziwa?” Mama akaniuliza.
“Tayari”
Mama akamuga mwenzake kisha akaingia kwenye kile chumba alichokuwemo mganga akaagana naye kisha akatoka.
Tulitoka nje tukapanda pikipiki na kuondoka.
“Dawa inanuka kweli!” nikamwambia mama.
“Dawa za kufukuza mashetani ndivyo zilivyo, vumilia tu”
Nilipomfikisha mama nyumbani kwake, nikaenda Msambweni nilikokuwa nikiishi.
Licha ya kuwa na hofu sikuona tatizo lolote usiku ule. Nikalala hadi asubuhi.
Wakati naamka, shuka za kitanda na ile niliyojifinika zilikuwa zikinuka ile harufu ya dawa za mganga. Niliziondoa kitandani nikatandika zingine kisha nikaenda kuoga. Licha ya kujisugua kwa sabauni zaidi ya mara moja, ile harufu bado nilikuwa nikiisikia mwilini mwangu.
Nilikwenda mkahawani nikanywa chai kisha nikapanda pikipiki yangu na kuelekea Chuda kwa kaka yangu.
Nilipofika nilimueleza nilivyoshughulikiwa na yule mganga na alivyonieleza kuwa niende tena siku ile.
“Jana usiku yule mwanamke hakukufuata?” akaniuliza.
“Sikumuona lakini nadhani kama nisingekwenda kwa yule mganga wa Amboni, angenifuata. Naamini zile dawa ndizo zilizomzuia”
“Sasa leo utaakwenda na mama au utakwenda peke yako?”
“Nitakwenda kumsikiliza mama, kama atasema twende tutakwenda”
“Hata kama atakwambia uende peke yako wewe nenda tu, ukirudi utakuja kunieleza”
“Sawa kaka”
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 23


ILIPOISHIA
Mama akamuga mwenzake kisha akaingia kwenye kile chumba alichokuwemo mganga akaagana naye kisha akatoka.
Tulitoka nje tukapanda pikipiki na kuondoka.
“Dawa inanuka kweli!” nikamwambia mama.
“Dawa za kufukuza mashetani ndivyo zilivyo, vumilia tu”
Nilipomfikisha mama nyumbani kwake, nikaenda Msambweni nilikokuwa nikiishi.
Licha ya kuwa na hofu sikuona tatizo lolote usiku ule. Nikalala hadi asubuhi.
Wakati naamka, shuka za kitanda na ile niliyojifinika zilikuwa zikinuka ile harufu ya dawa za mganga. Niliziondoa kitandani nikatandika zingine kisha nikaenda kuoga. Licha ya kujisugua kwa sabauni zaidi ya mara moja, ile harufu bado nilikuwa nikiisikia mwilini mwangu.
Nilikwenda mkahawani nikanywa chai kisha nikapanda pikipiki yangu na kuelekea Chuda kwa kaka yangu.
Nilipofika nilimueleza nilivyoshughulikiwa na yule mganga na alivyonieleza kuwa niende tena siku ile.
“Jana usiku yule mwanamke hakukufuata?” akaniuliza.
“Sikumuona lakini nadhani kama nisingekwenda kwa yule mganga wa Amboni, angenifuata. Naamini zile dawa ndizo zilizomzuia”
“Sasa leo utaakwenda na mama au utakwenda peke yako?”
“Nitakwenda kumsikiliza mama, kama atasema twende tutakwenda”
“Hata kama atakwambia uende peke yako wewe nenda tu, ukirudi utakuja kunieleza”
“Sawa kaka”
SASA ENDELEA
Nyumbani kwa mama nilimkuta mama akinisubiri. Nilipomuuliza kuhusu safari ya Amboni akaniambia tutakwenda sote. Mama yangu alikuwa na huruma sana. Nikampakia kwenye pikipiki tukaenda Amboni.
Tulipofika tulimkuta mganga akiwa kwenye chumba chake cha uganga akishughulika. Tulisalimiana naye akatuambia tumsubiri nje. Baada ya muda kidogo alitoka nje. Uso wake ulikuwa umefadhaika sana. Akatuambia.
“Jana niliwambia mje lakini usiku nilipolala yule jini wako alinifuata na kuniletea vitisho vikali sana. Aliniambia kuwa kama nitaendelea kukushughulikia kitanikuta kile kilichomkuta mganga wa Mnyanjani. Kwa kweli nilipata hofu sana”
“Lakini jana si ulituambia kuwa huyo jini unaweza hata kumpiga makofi?”
“Baba! Ni kweli nilisema lakini sikujua kama jini mwenyewe ni yule aliyenifuata. Yule jini ni mkali. Alipokuja, majini yangu yalinywea”
Maneno ya mganga huyo yalinifanya nimtazame mama. Mama naye akanitazama kwa mshangao.
Kama ambaye aligundua kuwa maneno yake yalikuwa yamemdhalilisha mwenyewe mganga huyo aliendelea kutuambia.
“Sidhani kama utaweza kuepukana na jini yule. Ameniambia kuwa hakuna atakayeweza kuwatenganisha, atakuwa na wewe mpaka kufa”
“Yaani ameshajihakikishia ushindi?” Mama akamuuliza kwa mshangao.
“Yeye mwenzetu ni jini, sisi ni binaadamu. Anatuona lakini sisi hatumuoni mpaka anapotaka mwenyewe” Mganga akasema.
“Sasa unatushauri nini?”
“Lakini huyu jini hana matatizo kama mnavyomdhania, tena ni jini tajiri na kisha ni mganga, kwanini hutaki kuwa naye?” Mganga akaniuliza.
“Siwezi kuwa na mke jini wakati mimi mwenyewe ni binaadamu. Nitaishi naye vipi?” Nikamuuliza mganga.
“Sasa utafanyaje wakati ameshakuchunuka?”
“Nitajitahidi kuhangaika kwa waganga wengine”
“Ukibahatika kwenda Pemba naamini unaweza kupata waganga ambao wataweza kukusaidia. Wapemba ni hodari sana kwa majini”
“Kama hakuna budi nitafika hata huko Pemba”
“Kama utaweza kwenda naamini utafanikiwa”
Tuliondoka kwa yule mganga tukiwa tumenywea. Mategemeo yangu yote yalififia ghafla. Suala lile sasa lilianza kunipa changamoto kali.
“Maneno ya yule mganga yamenitisha sana” Nilimwambia mama wakati namuendesha.
“Hakuna lisilo na mwisho, jini si Mungu, usitishike mwanangu. Endelea kumuamini Mungu. Jini ni kiumbe kama wewe naye ameumbwa na Mungu. Mungu ndiye wa kumuogopa”
Maneno ya mama yalinipa matumaini kidogo. Nilipomfikisha nyumbani kwake aliendelea kuniambia.
“Makosa yetu ndiyo yanayotuponza. Imani za watu zimekuwa ndogo sana katika dini. Watu wanapenda dunia zaidi. Sasa vile vitu ambavyo vilipaswa kuwa chini yetu vinakuwa juu yetu. Mwanaadamu ndiye aliyetakiwa kutawala dunia hii lakini baada ya watu kupunguza kumcha Mungu, sasa majini yanataka kututawala sisi”
“Leo mama umeniambia maneno ya akili na ya kufikirisha sana” nikamwambia mama.
“Rudi nyumbani na muamini Mungu wako, jini hatakufuata”
“Asante mama”
Nikaondoka na pikipiki yangu kurudi nyumbani nikiwa na imani tele. Nilijiambia kama mimi ndiye niliyepaswa kuwa mtawala wa dunia hii sitakubali jini anitawale wala kunitia hofu.
Ni kweli imani ina nguvu, nilikaa wiki nzima bila kuona kitisho chochote. Nikaona kama vile tatizo langu lilikuwa limekwisha.
Wiki iliyofuata nikiwa kazini kwangu, tuliendelea kufanya biashara hadi saa kumi jioni, yaani siku ile kulitokea biashara ya ajabu. Tulipata wateja wengi kutoka vijijini kwa vile ulikuwa msimu wa kuuza mazao.
Nikajikuta nilikuwa na pesa nyingi kwenye dawati langu. Muda huo sikuweza kuzifikisha pesa hizo benki kwa sababu benki zilikuwa zimeshafungwa.
Nilizihesabu pesa hizo, zilikuwa shilingi milioni kumi. Hizo zilikuwa za mauzo ya jioni tu, za mauzo ya asubuhi na mchana zilishapelekwa benki.
Nikaamua kuziacha pesa hizo kwenye dawati langu kwa vile nilifunga kitasa kwa funguo. Tukafunga duka na kuondoka.
Asubuhi ya siku ya pili yake nilikwenda kazini kama kawaida. Nilipofika kitu cha kwanza nilitaka nizitoe zile pesa ili zipelekwe benki. Nilipofungua dawati sikuona kitu.
Nikashituka na kutumbua macho yangu. Sikutosheka kutazama kwa macho, nilitia mkono wangu na kupapasa. Hakukuwa na kitu. Dawati lilikuwa tupu kama mkono uliorambwa!
“Pesa za watu zimewenda wapi jamani?” nikajiuliza kwa fadhaa.
Meza yangu ilikuwa na madawati matatu. Pesa niliziweka katika dawati la juu. Baada ya kuzikosa pesa katika dawati hilo nilianza kuzitafuta katika madawati ya chini yake japouwa nilikuwa na hakika kuwa pesa hizo niliziweka katika dawati la juu.
Nilikuwa kama niliyerukwa na akili. Licha ya kupekua kwenye madawati yote matatu, pesa sikuziona. Akili yangu ilikuwa haiamini kama pesa hizo hazikuwemo kwa sababu niliziweka mwenyewe na dawati nililifunga kwa funguo.
Nikarudi tena kwenye dawati la juu kutazama tena. Nikaja kwenye dawati la pili na la tatu. Lakini hakukuwa na pesa.
Ule mchezo wangu wa kufungua madawati kuanzia la juu hadi la chini na kisha kurudia tena, uliwashitua wafanyakazi wenzangu wakaanza kuniuliza ninachotafuta.
“Amour mbona umeshughulika sana, unatafuta nini?” Mfanyakazi mmoja akaniuliza.
“Natafuta pesa. Jana tulipoondoka niliacha shilingi milioni kumi katika dawati hili la juu, sasa sizioni!” nikamwambia.
“Zimekwenda wapi?”
“Sijui!”
“Kwani ulipoondoka hukulifunga?”
“Nililifunga na funguo niliondoka nazo, sasa nashangaa pesa sizioni!”
“Haiwezekani! Hebu tazama vizuri”
“Nimetafuta sana, pesa hazimo. Sijui nani amezichukua!”
“Na haiwezeani zichuuliwe na mtu wa sababu funguo uliondoka nazo mwenyewe”
Nikanyamaza kimya huku macho yangu yakitanga tanga kwenye meza.
Wafanyakazi wengine waliposikia mazungumzo yetu wakasogea karibu.
“Umepoteza nini, pesa?” mfanyakazi mmoja akaniuliza.
“Ndio pesa”
“Uliziweka wapi?”
“Nilizizifungia kwenye dawati hili hapa jana jioni tulipotoka kazini, sasa nashangaa pesa sizioni”
PESA ZA WATU ZIMEKWENDA WAPI JAMANI? HII IMESHAKUWA BALAA SASA!
ITAENDELEA...
 
SEHEMU YA 24


ILIPOISHIA
Ule mchezo wangu wa kufungua madawati kuanzia la juu hadi la chini na kisha kurudia tena, uliwashitua wafanyakazi wenzangu wakaanza kuniuliza ninachotafuta.
“Amour mbona umeshughulika sana, unatafuta nini?” Mfanyakazi mmoja akaniuliza.
“Natafuta pesa. Jana tulipoondoka niliacha shilingi milioni kumi katika dawati hili la juu, sasa sizioni!” nikamwambia.
“Zimekwenda wapi?”
“Sijui!”
“Kwani ulipoondoka hukulifunga?”
“Nililifunga na funguo niliondoka nazo, sasa nashangaa pesa sizioni!”
“Haiwezekani! Hebu tazama vizuri”
“Nimetafuta sana, pesa hazimo. Sijui nani amezichukua!”
“Na haiwezeani zichuuliwe na mtu wa sababu funguo uliondoka nazo mwenyewe”
Nikanyamaza kimya huku macho yangu yakitanga tanga kwenye meza.
Wafanyakazi wengine waliposikia mazungumzo yetu wakasogea karibu.
“Umepoteza nini, pesa?” mfanyakazi mmoja akaniuliza.
“Ndio pesa”
“Uliziweka wapi?”
“Nilizizifungia kwenye dawati hili hapa jana jioni tulipotoka kazini, sasa nashangaa pesa sizioni”
SASA ENDELEA
“Ulifunga kwa funguo?” Mhasibu aliniuliza.
“Nilifunga kwa funguo na funguo niliondoka nazo”
“Sasa nani atazichukua kama dawati ulilifunga?”
Katika maswali yote niliyokuwa nikiulizwa, swali hilo ndilo lililonikera kwa sababu sikuwa na jibu nalo na lilinifanya nionekane mzushi na mpumbavu.
“Hilo ndilo jambo la ajabu” nilijikuta ninatoa jibu hilo.
Baada ya muda mfupi nikawa nimezungukwa na wafanyakazi wenzangu waliokuwa wakilishangaa tukio hilo.
“Hebu jaribu kukumbuka kama uliziweka sehemu nyingine” Mhasibu akaniambia.
“Sikuweka sehemu nyingine, niliziweka kwenye dawati hili hapa” nilimuonesha lile dawati la kwanza.
“Sasa zitakuwa zimekwenda wapi?”
“Sijui bosi”
“Na ni kwanini hizo pesa hazikupelewa benki tangu jana ?”
“Ni pesa za mauzo ya jioni, benki zilikuwa zimeshafungwa bosi”
“Mara ngapi umeshalaza pesa kwenye droo lako?”
“Mara nyingi tu lakini leo ndio nimekomolewa”
“Sasa umekomolewa na nani? Mhasibu akaniuliza.
“Siwezi kujua”
“Bado sikuelewi Amour, pesa uliziweka mwenyewe na hakuna aliyejua isipokuwa wewe mwenyewe. Sasa utasema umekomolewa, umekomolewa na nani?”
Nikabaki kimya. Sikuwa na jibu
Msibu akanitazama.
“Umehakikisha kuwa hizo pesa hazipo?” akaniuliza.
“Sizioni” nikamjibu kwa sauti iliyonywea
“Sasa njoo ofisini kwangu”
Moyo wangu ukashituka lakini nilijikaza kiume. Nikamfuata mhasibu ofisini kwake. Kwa pembeni mwa macho yangu niiwaona wafanyakazi wenzangu wakinitazama. Kuna niliowaona wakinihurumia na kuna waliokuwa wakiona nilikuwa nimefanya ulaghai wa kuiba pesa za shirika.
Nilipoingia ofisini mwa mhasibu, mhasibu aliniambia.
“Kaa hapa” alinionesha kiti.
Yeye mwenyewe alizunguka nyuma ya meza yake, naye akaketi.
“Nataka nikwambie kitu” akaniambia. Sauti yake na uso wake haukuonesha urafiki hata chembe.
“Ndiyo” nikamuitikia nikiwa sijui anataka kuniambia nini.
“Umekuwa mfanya kazi muaminifu kwa muda mrefu sana lakini hii haitufanyi tusikuchukulie hatua kutokana na wizi huu wa pesa za shirika. Ninachokuomba ni kuwa nakupa siku mbili tu utupatie zile pesa” Alipofika hapo alinikazia macho kisha akaniuliza.
“Sijui umenielewa?”
“Nimekuelewa” Sikuwa na jibu jingine zaidi ya hilo.
“Sasa nenda katuletee zile pesa”
“Si kwamba hizo pesa ninazo, pesa zimeibiwa”
“Sasa nenda katutafutie pesa za watu uzilete”
“Nitakwenda kuzitafuta wapi bosi?”
Nilijua kwamba niliuliza swali la kipumbavu lakini lilitokana na hoja ya kipumbavu.
“Popote utakapojua utazipata, sisi shida yetu ni pesa tu”
Nikageuza uso wangu pembeni kutafakari.
“Nimekupa siku mbili uje na hizo pesa, vinginevyo itabidi suala hilo nilifikishe polisi”
Nilihisi kijasho chembamba kikinitiririka kwenye mfereji wa uti wa mgongo wangu.
“Tumeelewana?” Bosi akaniuliza alipoona nipo kimya.
“Sawa bosi” nikamjibu kisha nikainuka kwenye kiti.
Nilikwenda kwenye mlango. Wakati naufungua mlango huo nikaisikia sauti ya mhasibu akiniambia.
“Kumbuka kwamba nimekupa siku mbili”
Nikageuza uso na kumtazama.
“Nimekuelewa” nikamjibu kisha nikafungua mlango na kutoka.
Wakati natoka, macho ya wafanyakazi wenzangu yaligeuka kwangu. Sikuwapatiliza wala kuwajali. Nilihisi walikuwa miongoni mwa walionikomoa. Mimi nimeshapewa onyo la kusulubiwa, wao wanafurahia milioni kumi za bure.
Nilitoka nje ya duka letu bila kuzungumza na mfanyakazi yeyote. Nilikuwa nimefadhaika kweli. Nilipanda pikipiki yangu nikaiwasha na kuondoka.
Sikujua nilikuwa naenda wapi, nikaona niende kwa mama nikamueleza kuwa nimefikwa na mitihani. Wakati naendesha nilikuwa najiuliza nitazipata wapi shilingi milioni kumi ili nirudishe pesa za watu.
Pale nilipomkubalia bosi, aliponiambia niende nikazitafute pesa hizo nilimkubalia tu ili niweze kuondoka kwani nilijua kuwa sitazipata.
Nilipofika kwa mama yangu nilimueleza mkasa ulionitokea, mama alitaharuki sana.
“Imekuwaje tena mwanangu?” akaniuliza.
“Kwa kweli sielewi kitu mama. Huyo mtu aliyenichezea mchezo huu amenikomoa kweli”
“hilo dawati ulikuta limevunjwa?”
“Halikuvunjwa. Watu wana mbinu nyingi za wizi. Inawezekana kuna ufunguo mwingine uliotumika”
“Kwanini usiwaeleze hivyo wakubwa wako wa kazi?”
“Nani atanisikiliza. Unapotoa malalamiko unatakiwa utoe na ushahidi, ushahidi uko wapi kwamba kuna mfanyakazi mwenzagu amefungua dawati langu kwa ufunguo mwingine na kuiba hizo pesa!”
“Sasa wewe utazipata wapi milioni kumi?”
“Hiki ni kifungo mama!”
“Umekwenda kumueleza kaka yako?”
“Sijakwenda bado”
“Hebu nenda kamueleze usikie atakupa ushauri gani?”
“Sawa. Acha niende nikamsikilize”
Nilipofika nyumbani kwa kaka Chuda, ilikuwa ikikaribia kuwa saa sita mchana.
“Leo hukwenda kazini?” kaka akaniuliza.
“Nimekwenda lakini kumetokea matatizo”
“Matatizo gani?”
“Kuna pesa zimeibiwa kwenye dawati langu”
“Lini?”
“Leo hii”
“Kiasi gani?”
“Shilingi milioni kumi”
Kaka akashituka. Enzi hizo pesa hizo zilikuwa nyingi sana.
“Zimeibiwaje?”
Nikamueleza kaka jinsi wizi huo ulivyotokea.
“Inawezekana huyo jamaa alikuwa na ufunguo mwingine ambao aliutumia kufungua dawati lako akaiba hizo pesa”
“Ndio hivyo lakini sasa dhima imeniangukia mimi”
“Kwa hiyo umeambiwa nini”
Nitoke nikatafute pesa za shirika nizirudishe, nimepewa siku mbii tu”
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 25


Nilipofika nyumbani kwa kaka Chuda, ilikuwa ikikaribia kuwa saa sita mchana.
“Leo hukwenda kazini?” kaka akaniuliza.
“Nimekwenda lakini kumetokea matatizo”
“Matatizo gani?”
“Kuna pesa zimeibiwa kwenye dawati langu”
“Lini?”
“Leo hii”
“Kiasi gani?”
“Shilingi milioni kumi”
Kaka akashituka. Enzi hizo pesa hizo zilikuwa nyingi sana.
“Zimeibiwaje?”
Nikamueleza kaka jinsi wizi huo ulivyotokea.
“Inawezekana huyo jamaa alikuwa na ufunguo mwingine ambao aliutumia kufungua dawati lako akaiba hizo pesa”
“Ndio hivyo lakini sasa dhima imeniangukia mimi”
“Kwa hiyo umeambiwa nini”
Nitoke nikatafute pesa za shirika nizirudishe, nimepewa siku mbii tu”
SASA SONGA NAYO…
“Kama hukuzipata itakuwaje?”Kaka akaniuliza.
“Suala hilo litapelekwa polisi”
“Ukisikia balaa ndio hilo, wadhani utazipata wapi milioni kumi?”
“Hiki ni kifungo kinaningoja”
Kaka akatikisa kichwa kusikitika.
“Nakuhurumia sana mdogo wangu sijui nitakusaidiaje?”
“Msaada ni kupata hizo pesa na pesa hazipo”
“Umekwenda kumueleza mama?”
“Nimekwenda, nimemueleza”
“Amesemaje?”
“Hakuwa na usemi, amesikitika tu”
Wakati ninasema hivyo nilimuona kaka amezama katika fikira. Nikajua lile tatizo lilikuwa limeugusa moyo wake.
“Sasa itabidi tusubiri tuone uamuzi wa wakuu wako” Kaka akaniambia baada ya kimya kifupi.
“Uamuzi! Kuna uamuzi gani tena kaka zaidi ya kufunguliwa kesi ya wizi. Kwani si nimeshaambiwa kama pesa hazitapatikana baada ya siku mbili, hili suala linafikishwa polisi!” Nikamwambia kaka.
Kaka alikuwa amejishika kichwa akisikitika.
“Kilichobaki sasa ni kuomba Mungu hizo pesa zipatikane”
Wakati kaka akisema hivyo mimi nilikuwa kimya.
“Mungu amtie imani huyo aliyeziiba azirudishe kabla ya hizo siku mbili” Kaka aliendelea kuniombea.
Hakuna mwizi au jambazi anayerudisha kile alichokiiba lakini kwa vile kaka yangu alikuwa akiniombea ilibidi nimsikilize.
Siku ile nilishinda bila furaha na kusema kweli nilishindwa hata kula chakula. Nilikwenda nyumbani kulala tu.
Siku ya pili yake nilikwenda kazini. Mhasibu aliponiona akaniita ofisini kwake. Nilipokwenda aliniuliza kama nimefanikiwa kupata zile pesa.
“Sijazipata bosi” nikamwambia.
Uso wa mhasibu ukaonesha kuhamaki.
“Unajua kuwa zile ni pesa za shirika?” akaniuliza kwa ukali kidogo.
“Ninajua bosi”
“Na unajua kuwa nilikupa siku mbili urudishe zile pesa?”
“Ninajua”
“Kama unajua hivyo sawa. Kesho uje na hizo pesa vinginevyo sitakuelewa”
Sikuwa na jingine la kumjibu zaidi ya kumuitikia. Nilishajua kuwa nisipokuja na pesa hizo atanifikisha polisi. Na mimi nilikuwa nimeshajitolea kwenda jela.
Siku ile nilishinda kazini hadi muda wa kutoka kazini nikatoka na wenzangu. Tulipokuwa nje baadhi ya wafanyakazi wenzangu waliniuliza kuhusu upotevu wa zile pesa. Kila mtu alionekana kushangaa jinsi pesa hizo zilivyoibiwa.
“Nimepewa siku mbili nizirudishe hizo pesa vinginevyo suala litafikishwa polisi kwa hatua zaidi” nikawambia.
Kila mtu aling’aka na kunihurumia.
“Sasa ni nani aliyefanya mchezo huo. Hapa kazini kweli hakuna mchezo wa kuibiana pesa” Mfanyakazi mmoja akaniambia.
“Hata mimi nashindwa kuelewa”
Baadhi ya wafanyakazi wenzangu walikuwa wamenizunguka wakinisikiliza na kunihoji. Baadaye tulichangukana tukarudi majumbani.
Lakini mimi sikurudi nyumbani. Nilikwenda nyumbani kwa mama. Ukiwa na mama, hata ukiwa mtu mzima utamdekea tu. Pale kwa mama ndipo nilipopaona mahali muafaka wa kupeleka kilio changu ingawa hakuwa na uwezo wowote lakini alikuwa ni mama.
Nikamueleza mama yaliyojiri huko kazini kwangu. Nikamwambia kwamba kesho ndio natakiwa kupeleka hizo pesa vinginevyo ninafikishwa polisi.
“Itabidi hapo kesho uende kazini na kaka yako ili litakalotokea aweze kulijua” Mama akaniambia.
Jioni ile ile nilikwenda kwa kaka nikamueleza na tukakubaliana kwamba nimpitie asuhuhi anisindikize kazini.
Siku ile nilipanga vizuri vitu vya nyumbani nikijua kwamba kesho yake ninakwenda jela. Usiku wake sikupata usingizi kwa mawazo.
Nakumbuka nilipata usingizi majira ya saa kumi alfajiri nikaota ndoto ya kutisha. Niliota nimesimamishwa kizimbani nikihukumiwa kwa kosa la wazi wa fedha za shirika.
Hakimu aliniambia. “Ushahidi uliotolewa hapa mahakamani umeonesha na kuthibitisha bila shaka yoyote kwamba umeiba shilingi milioni kumi fedha za shirika ukiwa mfanyakazi wa shirika hilo. Hivyo mahakama hii imekutia hatiani”
Hakimu akainua uso wake na kunitazama kisha akaniuliza.
“Una lolote la kuiambia mahakama hii kwanini isikupe adhabu kali?”
“Mheshimiwa hakimu ninaiomba mahakama yako tukufu isinipe adhabu kali kwa kuzingatia kuwa fedha zenyewe sikuziiba mimi na kwa kweli sijui zimeibiwa na nani” nikasema.
Hakimu akaandika maelezo yangu kisha akainua tena uso wake na kuniambia.
“Maelezo yako hayawezi kuizuia mahakama hii isikupe adhabu kali. Ninakuhukumu kifungo cha miaka thelathini jela ili iwe fundisho kwa wengine”
Hapo hapo nikaacha mdomo wazi kwa mshangao kama ambaye sikuamini kuwa nilihukumiwa kifungo hicho. Uso wangu ukiwa umenywea nilimtazama mama yangu na kaka yangu waliokuwa wamekaa katika safu za mbele.
Nikamuona mama yangu anaangua kilio akinililia…
Sauti yake ya kizee ndio iliyoniamsha usingizi. Wakati nazinduka moyo ulikuwa ukinienda mbio na mwili wote ulikuwa umenitota jasho. Nilijiinua kitandani nikaketi.
Nikajiuliza, je ndoto ile ndio inanitabiria hatima yangu, kwamba nitahukumiwa kifungo cha miaka thelathini kama jambazi?
Kama ni hivyo, niliendelea kujiambia, nitafia jela. Sitamuona tena mama yangu, sitamuona tena kaka yangu.
Wazo la kufungwa miaka thelathini lilinifanya nitaharuki. Nikajiambia “…sijui nikimbie nisiende tena kazini…”
Lakini nikajiuliza nitakimbilia wapi katika Tanzania hii ambapo mkono wa serikali hautakuwepo?
Kukimbia ni kama kujidanganya na kuonesha kuwa zile pesa niliiba mimi wakati sivyo, nikajiambia, la msingi ni kwenda kazini, litakalotokea na litokee. Kama ni kufungwa au kuachiwa, ingawa tegemeo la kuachiwa sikuwa nalo.
Mpaka inafika saa moja kamili asubuhi nilikuwa nimeshafika nyumbani kwa kaka. Nilitangulia kwenda kwa mama nikaagana naye. Mama aliniombea Mungu kile ‘kikombe’ kiniepuke.
Nilisubiri kaka ajitayarishe hadi saa moja na nusu ndipo tulipoondoka.
Tulifika kazini saa mbili kama na robo hivi nikaingia ndani na kaka. Tulikwenda katika ofisi ya mhasibu. Mhasibu aliponiona tu akaniuliza.
“Umekuja na pesa?”
Nikatikisa kichwa taratibu.
“Sikufanikiwa bosi”
“Mimi ni kaka yake” Kaka yangu akajitambulisha na kumuuliza mhasibu.
“Mheshimiwa kwani hiwezekani kumkata katika mshahara wake wa kila mwezi hadi hizo pesa zikaisha?”
Mhasibu akakasirika.
“Nyinyi mnaleta utani na kazi. Huu ni wizi, huyu hakukopa pesa hapa hadi tumkate kila mwezi. Shilingi milioni kumi tutamkata kwa miaka mingapi wakati pesa za shirika zinahitajika? Nimeshamwambia kama hakuja na pesa leo atakwenda kujieleza polisi” Mhasibu alifoka na kuinuka kwenye kiti, akaniambia.
“Twende!”
Tukatoka mle ofisini na akawaambia wafanyakazi wengine kuwa tunakwenda kituo cha polisi. Tulikuwa tuna magari mawili ya shirika yenye madereva wake. Tukapanda kwenye gari mojawapo. Kaka yangu tulimuacha pale pale.
Wakati napelekwa polisi na nikijua kuwa ninakwenda kufungwa nilimlaani sana yule aliyeiba zile pesa. Nilipata uchungu nilipowaza kwamba mimi ninakwenda kufungwa, yeye yuko ofisini akiwa ameficha shilingi milioni kumi nyumbani kwake.
Tulikwenda kituo cha polisi cha Chumbageni. Tulipoingia katika kituo hicho mhasibu akatoa maelezo yote kuhusiana na wizi huo.
DUH! JAMAA ANATIA HURUMA KWELI! SI ATAFUNGWA TU HUYU?
ITAENDELEA...
 
SEHEMU YA 26


ILIPOISHIA
Nikajiuliza, je ndoto ile ndio inanitabiria hatima yangu, kwamba nitahukumiwa kifungo cha miaka thelathini kama jambazi?
Kama ni hivyo, niliendelea kujiambia, nitafia jela. Sitamuona tena mama yangu, sitamuona tena kaka yangu.
Wazo la kufungwa miaka thelathini lilinifanya nitaharuki. Nikajiambia “…sijui nikimbie nisiende tena kazini…”
Lakini nikajiuliza nitakimbilia wapi katika Tanzania hii ambapo mkono wa serikali hautakuwepo?
Kukimbia ni kama kujidanganya na kuonesha kuwa zile pesa niliiba mimi wakati sivyo, nikajiambia, la msingi ni kwenda kazini, litakalotokea na litokee. Kama ni kufungwa au kuachiwa, ingawa tegemeo la kuachiwa sikuwa nalo.
Mpaka inafika saa moja kamili asubuhi nilikuwa nimeshafika nyumbani kwa kaka. Nilitangulia kwenda kwa mama nikaagana naye. Mama aliniombea Mungu kile ‘kikombe’ kiniepuke.
Nilisubiri kaka ajitayarishe hadi saa moja na nusu ndipo tulipoondoka.
Tulifika kazini saa mbili kama na robo hivi nikaingia ndani na kaka. Tulikwenda katika ofisi ya mhasibu. Mhasibu aliponiona tu akaniuliza.
“Umekuja na pesa?”
Nikatikisa kichwa taratibu.
“Sikufanikiwa bosi”
“Mimi ni kaka yake” Kaka yangu akajitambulisha na kumuuliza mhasibu.
“Mheshimiwa kwani hiwezekani kumkata katika mshahara wake wa kila mwezi hadi hizo pesa zikaisha?”
Mhasibu akakasirika.
“Nyinyi mnaleta utani na kazi. Huu ni wizi, huyu hakukopa pesa hapa hadi tumkate kila mwezi. Shilingi milioni kumi tutamkata kwa miaka mingapi wakati pesa za shirika zinahitajika? Nimeshamwambia kama hakuja na pesa leo atakwenda kujieleza polisi” Mhasibu alifoka na kuinuka kwenye kiti, akaniambia.
“Twende!”
Tukatoka mle ofisini na akawaambia wafanyakazi wengine kuwa tunakwenda kituo cha polisi. Tulikuwa tuna magari mawili ya shirika yenye madereva wake. Tukapanda kwenye gari mojawapo. Kaka yangu tulimuacha pale pale.
Wakati napelekwa polisi na nikijua kuwa ninakwenda kufungwa nilimlaani sana yule aliyeiba zile pesa. Nilipata uchungu nilipowaza kwamba mimi ninakwenda kufungwa, yeye yuko ofisini akiwa ameficha shilingi milioni kumi nyumbani kwake.
Tulikwenda kituo cha polisi cha Chumbageni. Tulipoingia katika kituo hicho mhasibu akatoa maelezo yote kuhusiana na wizi huo.
SASA ENDELEA
Baada ya kumaliza kutoa maelezo yake na mimi nikatakiwa nijieleze.
Nikaeleze hali iliyotokea ambapo fedha hizo zilichukuliwa ndani ya ndroo yangu wakati ndroo hiyo niliifunga kwa funguo.
Baada ya maelezo yangu nikaanza kukabiliwa na maswali ya polisi.
“Baada ya kufungia hizo pesa kwenye droo yako, asubuhi ulipokwenda kazini kwako ulikuta droo imevunjwa?”
“Ndroo haikuvunjwa”
“Untaka utuambie huyo aliyeziiba pesa hizo alizichukuaje bila kuvunja droo?”
“Pengine alikuwa na ufunguo mwingine”
“Funguo za droo yako ziko ngapi?”
“Ni mbili na zote ninazo mimi”
“Unaona sasa unajiingiza mwenyewe, huo ufunguo wa tatu alioutumia huyo mtu umetokea wapi wakati funguo ni mbili na unazo mwenyewe?”
“Unaweza kuwa ufunguo wa kuchongesha. Kuna mafundi wa kuchonga funguo”
“Tunajua kuwa wapo lakini hata wao ni mpaka uwapelekee ufunguo wa sampuli ndio wanaweza kukuchongea”
“Wezi wana mbinu nyingi. Kama mtu alishapanga kufanya uwizi anaweza kuvizia hizi funguo ninapoziacha juu ya meza yangu wakati sipo, akaukandamiza ufunguo mmoja kwenye sabuni ili kupata meno yake halafu sabuni ile anaipeleka kwa fundi. Fundi anaweza kuchonga ufunguo kama ule”
“Unaweza kuzungumza mengi lakini hayana ushahidi. Hebu twendeni tukaione hiyo droo yako”
Huo ndio ukawa mwisho wa maswali.
Tulitoka na polisi. Mimi nilipakiwa kwenye gari la polisi, mhasibu akaondoka na gari la shirika.
Wakati tunaondoka ndio kaka yangu alikuwa anafika pale kituoni. Akatuona tunaondoka. Siku ile nilimsumbua sana kaka kwa sababu alikuwa akitembea kwa miguu.
Tulipofika kazini kwetu tuliingia ndani, mhasibu akawapeleka polisi kwenye meza yangu.
“Pesa ziliibiwa kwenye meza hii” Mhasibu aliwambia polisi.
“Hebu toa hizo funguo tuzione” Polisi mmoja akaniambia.
Nikazitoa funguo zangu kutoka mfukoni na kuwaonesha
Polisi walizitazama kisha polisi mmoja akaniambia nifungue ile droo. Nikaifungua.
Sote tuliokuwa tunashuhudia, mimi mhasibu na wale polisi pamoja na baadhi ya wafanyakazi, tuling'aka baada ya kuziona zile pesa zilizokuwa zimetoweka zikiwa ndani ya droo.
“Na hizo ni pesa zipi?” Polisi mmoja akaniuliza kwa mshangao.
“Sijui, ndio naziona sasa. Zilikuwa hazimo” nikamjibu.
“Hapo mwanzzo mlihakikisha kwa makini kuwa hizo pesa hazikuwemo?”
“Mimi nilihakikisha na mhasibu pia alihakikisha”
“Hebu zitoe”
“Nikazitoa na kuziweka juu ya meza
“Ni kiasi gani?” Mhasibu akaniuliza
Nikazihesabu na kuona zilikuwa shilingi milioni kumi.
“Sasa nani amezitia hizo pesa?” Mhasibu akauliza kwa mshangao.
Hakukuwa na jibu
“Asubuhi uliangalia kwenye hii droo?” akaniuliza tena
“Sikuangalia”
Mhasibu alipowauliza wafanya kazi wenzangu kuhusu zile pesa hakukuwa na yeyote aliyeeleza kuwa alijua chochote kuhusu pesa hizo.
“Mimi naamini kuwa hizi pesa zimerudishwa kwa sababu mimi mwenyewe niliangalia kwenye hii droo juzi, sikukuta kitu” Mhasibu akatuambia.
“Hapa pana mchezo umepita, mimi nimechezewa na wenzangu” nikasema kwa hasira. Sasa nilikuwa na nguvu baada ya zile pesa kuonekana.
“Sasa ni nani aliyefanya mchezo huu? Tunataka tumjue” Mhasibu akauliza.
“Huu ni wizi ulikuwa umefanyika. Huyo aliyeiba alipoona suala hili limefika polisi ndio aliamua kuzirudisha pesa hizi” Polisi mmoja akasema.
“Tunashukuru kwa vile amezirudisha lakini tunaomba mchezo huu usirudiwe tena” Mhasibu akaonya
“Basi sisi tunakwenda zetu” polisi wakatuambia.
“Mimi naona mwende kwa sababu tatizo lilikuwa ni kwenye hizi pesa ambazo zimeshaonekana” Mhasibu akawambia polisi
Polisi hao wakatuaga na kuondoka.
Mhasibu akachukua zile pesa na kuniambia nimfuate ofisini kwake.
Tulipokuwa ofisini aliniambia.
“Usirudie tena kuacha pesa kwenye droo, sasa hivi sina imani tena na wafanyakazi wa shirika hili”
“Kutokana na msukosuko huu ulionipata, sitarajii kulaza pesa tena kwenye droo yangu”
“Shukuru kwamba hizi pesa zimepatikana, vinginevyo ungelala ndani leo”
“Ni kweli. Hilo nilikwishalijua”
“Kuwa makini sana na wenzako”
“Nitakuwa makini”
Mhasibu akawa anahesabu zile pesa. Alipohakikisha kuwa zilikuwa shilingi milioni kumi taslim nilimuomba anipe mapumziko ya siku moja ili niende nikatulize presha yangu nyumbani.
Mhasibu akaniruhusu, nikaondoka. Wakati natoka mlangoni nikakutana na kaka akitokea kituo cha polisi. Alikuwa amechoka kwa mwendo.
“Imekuwaje?” akaniuliza huku akinitazama kwa uso wa sintofaham.
“Twenzetu” nikamwambia
Akanifuata. Tukashuka baraza.
“Tunakwenda wapi?” akaniuliza akionesha kuwa na wasiwasi
“Nyumbani”
Nikaona uso wake unachanua tabasamu.
“Kwani imekuwaje?”
“Zile pesa zimeonekana”
Kaka akashituka.
“Zimeonekana wapi?”
“Kwenye droo”
“Droo ya nani?”
“Droo yangu”
“Zimeonekana kivipi?”
“Ni tukio la ajabu sana” nikamwambia kisha nikamueleza jinsi tulivyozikuta pesa hizo kwenye droo yangu.
“Una maana huyo aliyeiba ameamua kuzirudisha?”
“Itakuwa ndio hivyo”
“Kwa hiyo zile pesa alikuwa amezificha sehemu nyingine, alipoona unapelekwa polisi akaamua kuzirudisha”
“Bila shaka. Lakini sasa nimepata fundisho sitaacha pesa tena kwenye droo yangu kwa maana wanataka kunitoa kafara”
“Ni tukio ambalo sikulitarajia”
“Naona dua za mama zinafanya kazi. Mama aliniombea sana”
“Wakati tunavuka barabara tukapishana na msichana mmoja ambaye naye alikuwa anavuka kutoka upande ule tuliokuwa tunakwenda sisi. Alinitupia jicho mara moja ili kujua kama nimemuona.
Nukta ile ile nikamtambua.
Alikuwa Zena!
DUH! Huyu ZENA JINI? AMETOKEA WAPI TENA?
ITAENDELEA..
 
SEHEMU YA 27

ILIPOISHIA
Kaka akashituka.
“Zimeonekana wapi?”
“Kwenye droo”
“Droo ya nani?”
“Droo yangu”
“Zimeonekana kivipi?”
“Ni tukio la ajabu sana” nikamwambia kisha nikamueleza jinsi tulivyozikuta pesa hizo kwenye droo yangu.
“Una maana huyo aliyeiba ameamua kuzirudisha?”
“Itakuwa ndio hivyo”
“Kwa hiyo zile pesa alikuwa amezificha sehemu nyingine, alipoona unapelekwa polisi akaamua kuzirudisha”
“Bila shaka. Lakini sasa nimepata fundisho sitaacha pesa tena kwenye droo yangu kwa maana wanataka kunitoa kafara”
“Ni tukio ambalo sikulitarajia”
“Naona dua za mama zinafanya kazi. Mama aliniombea sana”
“Wakati tunavuka barabara tukapishana na msichana mmoja ambaye naye alikuwa anavuka kutoka upande ule tuliokuwa tunakwenda sisi. Alinitupia jicho mara moja ili kujua kama nimemuona.
Nukta ile ile nikamtambua.
Alikuwa Zena!
SASA ENDELEA
Niliendelea kuvuka barabara huku uso wangu nimeugeuza nyuma nikimtazama yule msichana.
Baada ya yeye kunitupia macho mara moja tu, aliugeuza mbele uso wake akaendelea na safari yake. Mimi ndiye niliyekuwa nikiendelea kumtazama.
Kaka yangu alikuwa akinisemesha bila kujua kwamba akili yangu ilikuwa imeshughulishwa na kitu kingine.
Tulipomaliza kuvuka barabara nilimuona Zena akikata kona kwenye jengo lililokuwa na ofisi yetu na kupotea
Hapo ndipo nilipomshitua kaka.
“Nimemuona zena!” nikamwambia.
“Zena….Zena yupi?” akaniuliza.
“Yule msichana wa kijini”
Kaka akageuka kwa hamaki.
“Yuko wapi?”
“Wakati sisi tunavuka barabara na yeye alikuwa anavuka kutoka huku kwenda kule upande wa pili. Tulipishana katikati ya barabara. Nimemuona na yeye ameniona lakini hakunisemesha kitu”
Kaka alikuwa akigeuza uso huku na huku kumtafuta.
“Yuko wapi sasa?”
“Ameshakata kona kwenye hili jengo, hebu njoo tumuangalie”
Tukasogea kwenye ile barabara aliyoelekea Zena na kumchungulia.
Hatukumuona tena.
“Ameshapotea”
“Ungenishitua pale pale ulipomuona” Kaka akaniambia
“Sijui anatoka wapi na anakwenda wapi?”
“Labda ana safari zake mwenyewe”
“Unajua tangu nilipokwenda kwa mganga wa Amboni sjakutana naye hadi hii leo!”
“Lakini yule mganga si alisema asingeweza kumuondoa”
“Alituambia hivyo lakini mama alinipa moyo. Niliamini Mungu”
Baada ya kutomuona yule msichana tukawa tunatembea kurudi nyumbani.
“Sasa ni kwanini unarudi nyumbani?” Kaka akaniuliza.
“Nimeomba mapumziko ya siku moja, unajua ule msukosuko ulikuwa mkubwa”
“Ni kweli inabidi upumzike”
Tulitangulia kwenda kwa mama. Aliponiona nikiwa na uso wa tabasamu alishangaa.
“Imekuwaje wanangu?” akatuuliza.
“Kesi imekwisha mama, dua zako zimesaidia” nikamwambia huku nikiendelea kutabasamu
“Imekwisha kivipi?”
“Zile pesa zimeonekana” Kaka ndiye aliyejibu.
“Zimeonekana!” mama akauliza kwa mshangao.
“Kuna mchezo walinichezea pale kazini” nikamwambia mama.
“Hebu nielezeni vizuri Nataka kujua hizo pesa zimeonekana wapi?”
Nikamueleza tukio lilivyotokea.
“Wenzako unaofanya kazi nao si wazuri” mama akaniambia na kuongeza.
“Jihadhari nao”
“Nimemwambia hivyo hivyo, kesho na kesho kutwa wanaweza kukufanyia tena” Kaka akasema.
“Nimepata fundisho. Sitaacha tena pesa kwenye droo, hata iweje”
“Usiache mwanangu, utajitafutia matatizo ya bure”
Tuliongea mengi na kaka yangu pamoja na mama yangu. Baadaye mimi na kaka tukaondoka kwa mama. Nilimpeleka kaka Chuda kisha nikarudi nyumbani kwangu.
Nilipofika nilipanda kitandani nikajilaza. Wakati nawaza hili na hili usingizi ukanipitia nikalala. Wakati niko usingizini nikaota ilikuwa ni siku ile niliyoweka pesa kwenye droo yangu. Usiku wake Zena akafika kwenye mlango wa duka letu.
Alisimama mbele ya mlango wa duka hilo, milango ukafunguka yenyewe. Akaingia ndani.
Alikwenda hadi ilipokuwa meza yangu akavuta ndroo ambayo ilifunguka. Akachukua zile pesa nilizokuwa nimeziweka akazitia kwenye pochi yake. Wakati akifanya hivyo nilimsikia akisema. “Akijifanya anajua vile na mimi najua hivi, atakoma!”
Alipozitia zile pesa kwenye mkoba wake akatoka. Alipotoka ile milango ya duka ikajifunga yenyewe.
Wakati ule nahangaika kutafuta zile pesa Zena alikuwa yuko mle ofisini lakini alikuwa haonekani. Mpaka siku ile ambayo nilipelekwa polisi alikuwa amekwenda tena usiku kwenye duka letu akazirudisha zile pesa alizokuwa amezichukua kwenye droo yangu kisha akafunga ndroo na kutoka.
Vile nilivyokuwa napelekwa polisi Zena alikuwa ameketi kando yangu kwenye gari lakini tulikuwa hatumuoni. Wakati ule nahojiwa na polisi na yeye alikuwa akisikiliza.
Niliporupi ofisini na polisi Zena alikuwa yuko sambamba na mimi hadi zile pesa zipoonekana.
Sasa wakati ule navuka barabara nikiwa na kaka alijipitisha kusudi ili nimuone kisha akapotea.
Nikazinduka usingizini. Wakati nazinduka niliisikia sauti ya Zena ikiniambia.
“Hilo ni onyo!”
Nikadhani kwamba zena alikuwa mule chumbani. Nilipofumbua macho nikainuka na kuketi, nikaanza kutazama huku na huku kwa hofu kwamba ningemuona Zena mle chumbani. Lakini sikumuona.
Nikashuka kitandani na kutoka sebuleni ambako nilikaa kwenye kochi na kuifikiria ile ndoto.
Hapo ndipo nilipoanza kufahamu kuwa zile pesa zilikuwa zimechukuliwa na Zena ili kunikomoa. Nikajiambia kama asingezirudisha ndio ningekiona cha moto.
“Huyu msichana ataendelea kuniamndama hadi lini?” nikajiuliza.
Nilihisi kwamba kama sitachukua hatua thabiti za kuhakikisha kwamba ninaepukana naye, mwisho wake anaweza kunitia katika matatizo makubwa.
Baada ya kufikiri sana nilitoa pikipiki yangu nikaenda kumueleza mama kuhusu ile ndoto. Mama naye alistaajabu.
“Kumbe bado anakufuatilia!” akaniambia
“Huyu jini atakuja kunitia kwenye matatizo makubwa hapo baadaye” nikamwambia mama.
“Sasa fanya mpango wa kwenda huko Pemba”
“Inabidi nipate mwenyeji au mtu wa kufuatana naye ndio nitaweza kufika”
YAAP! Je jamaa huyo atakwenda pemba na nini kitatokEa?
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 28


ILIPOISHIA
Niliporudi ofisini na polisi Zena alikuwa yuko sambamba na mimi hadi zile pesa zipoonekana.
Sasa wakati ule navuka barabara nikiwa na kaka alijipitisha kusudi ili nimuone kisha akapotea.
Nikazinduka usingizini. Wakati nazinduka niliisikia sauti ya Zena ikiniambia.
“Hilo ni onyo!”
Nikadhani kwamba zena alikuwa mule chumbani. Nilipofumbua macho nikainuka na kuketi, nikaanza kutazama huku na huku kwa hofu kwamba ningemuona Zena mle chumbani. Lakini sikumuona.
Nikashuka kitandani na kutoka sebuleni ambako nilikaa kwenye kochi na kuifikiria ile ndoto.
Hapo ndipo nilipoanza kufahamu kuwa zile pesa zilikuwa zimechukuliwa na Zena ili kunikomoa. Nikajiambia kama asingezirudisha ndio ningekiona cha moto.
“Huyu msichana ataendelea kuniamndama hadi lini?” nikajiuliza.
Nilihisi kwamba kama sitachukua hatua thabiti za kuhakikisha kwamba ninaepukana naye, mwisho wake anaweza kunitia katika matatizo makubwa.
Baada ya kufkiri sana nilitoa pikipiki yangu nikaenda kumueleza mama kuhusu ile ndoto. Mama naye alistaajabu.
“Kumbe bado anakufuatilia!” akaniambia
“Huyu jini atakuja kunitia kwenye matatizo makubwa hapo baadaye” nikamwambia mama.
“Sasa fanya mpango wa kwenda huko pemba”
“Inabidi nipate mwenyeji au mtu wa kufuatana naye ndio nitaweza kufika”
SASA ENDELEA
“Ulizia kwa marafiki zako unaweza kupata mtu anayekwenda. Hapa Tanga watu wa Pemba wako wengi” Mama akaniambia.
“Nitaanza kuuliza uliza kwa watu. Nikipata mwenyeji au mtu anayekwenda huko itabidi niende”
Baadaya kuzungumza na mama nilikwenda kwa kaka, naye nikamueleza kuhusu ile ndoto.
“Mimi naamini majini wana matatizo sana na huyo jini hawezi kukuachia kirahisi lakini kwa vile humuhitaji nitakusaidia kukuulizia waganga kwa wenyeji wa Pemba” Kaka akaniambia.
“Na mimi mwenyewe pia nitakuwa naulizia ulizia kwa jamaa”
Ikapita wiki moja. Siku moja ya jumapili kaka yangu akaja nyumbani. Hakuwa na kawaida ya kufika kwangu, hivyo nilipomuona nilishituka.
Akaniambia kulikuwa na mganga aliyetoka Pemba amefikia katika gesti moja pale Chuda. Katika matangazo yake ameeleza pia kuwa anafukuza majini wabaya.
“Nataka twende umueleze matatizo yako anaweza kukusaidia” Kaka akaniambia.
Nilipopata habari zile nilimwambia kaka anisubiri. Baada ya dakika chache tukawa njiani tukielekea Chuda. Nilikuwa nimempakia nyuma ya pikipiki yangu.
Tulipofika Chuda alinipeleka katika gesti alikofikia huyo mganga aliyeniambia. Ilikuwa mtaa wa pili na ule aliokuwa akiishi yeye.
Wale watu niliowakuta hapo nje wakisubiri zamu ya kuingia kwa mganga huyo walinipa matumaini kwamba huyo mganga alikuwa mganga kweli.
Alikuwa ameweka tangazo lake mbele ya gesti lililoandikwa matatizo aliyokuwa akiyashughulikia likiwemo tatizo la majini.
“Ninafukuza majini mabaya katika mwili au nyumba. Pia ninatuliza wale majini wa kichwa wanoleta maradhi na matatizo mengine” Ilisema sehemu ya tangazo hilo.
Mwisho wa tangazo lake aliandika.
“Njoo ujaribu kwani wengi wamefanikiwa. Nitakuwa Tanga kwa siku tatu”
Kutokana na wale watu niliowakuta kuwa wengi nilitaka kumwambia kaka turudi baadaye, watu watakuwa wamepungua lakini nilivyoona pameandikwa kuwa mganga atakuwa Tanga kwa siku tatu nikaamua nisubri hapo hapo.
Siku tatu ni chache sana. Kama ningemkosa siku ile na pengine siku inayofuata, uwezekano wa kumpata tena ungekuwa mdogo sana. Nilijiambia.
Watu tuliowakuta walifikia arobaini. Nilimwambia kaka kama hatakuwa na muda wa kusubiri hapo aende zake.
“Niache niendelee kusubiri hata kama itafika jioni” nilimwambia.
“Sawa, basi wewe subiri ikifika zamu yako utaingia na utamueleza tatizo lako. Ukitoka hapa utakuja nyumbani kuniambia”
Tulipokubaliana na kaka aliondoka akaniacha pale. Mpaka inafika saa nane mchana walikuwa wamebaki watu kumi nikiwemo mimi. Nikaendelea kusubiri hadi saa kumi jioni ndio ikafika zamu yangu.
Nikaingia.
Chumba cha mganga kilikuwa cha kwanza cha mkono wa kushoto. Niliingia katika chumba hicho nikamkuta mganga aliyekuwa amekaa chini kwenye mswala. Kando yake alikuwa amechoma udi wa kijiti uliokuwa unafuka moshi.
Mbele yake kulikuwa na vitabu kadhaa vya kiarabu pamoja na chupa za dawa za kiasili.
Alikuwa amevaa kofia ya darize aliyoiweka katika muundo wa jahazi. Pia alikuwa amevaa shati jeupe na shuka nyeupe. Hakuwa amevaa suruali.
“Karibu” akaniambia alipoona nimesita baada ya kuingia humo chumbani.
“Asante” nikamjibu.
“Kaa kwenye kiti”
Kulikuwa na kiti kilichokuwa kando ya ukuta kushotoni kwake. Nikaenda kuketi.
“Niambie shida yako” akaniambia.
Nikamueleza matatizo yangu mwanzo hadi mwisho.
“Umepata bahati sana. Kule kwetu ukiwa na jini kama huyo tayari unajihesabu kuwa ni tajiri” Mganga akaniambia baada ya kunisikiliza.
“Huko kwenu kuna watu waliooa majini”
“Enhe! Wapo”
“Mimi simuhitaji huyu jini”
“kama wewe umuhitaji ndipo anapokutia kwenye matatizo”
“Ndio nimekuja kwako unisaidie”
“Unataka nikusaidieje?”
“Umuondoe”
“Una uhakika kuwa umuhitaji kabisa, usije ukajuta baadaye”
“Hapana, siwezi kujuta”
“Kwangu mimi si kazi kubwa kama utanipatia vitu ninavyotaka”
“Unataka vitu gani?”
“Ninahitaji kucha zako na kucha za maiti aliyezikwa. Unaweza kuzipata kucha za maiti?”
“Mh! Itakuwa ngumu!”
“Bila kupata kucha za maiti kazi itakuwa ngumu. Nenda kanitafutie kucha za maiti. Ukizipata niletee nitamuondoa huyo jini siku hiyo hiyo. Mimi nikalipo (nitakuwepo) hadi kesho kutwa. Ukiniletea kesho itakuwa bora”
“Bila hizo kucha haitawekana?” nikamuuliza”
Mganga akatikisa kichwa.
“Itakuwa vigumu”
Nikawaza kidogo kisha nikamwambia.
“Basi acha niende nikafikirie nitakavyoweza kuzipata hizo kucha halafu nitakuja hapo kesho”
“Sikiliza. Kucha zenyewe ni lazima ziwe za maiti aliyezikwa si za maiti ambaye hajazikwa”
“Sasa maiti ambaye amezikwa nitampata wapi?”
“Kaburini”
“Yaani nikafukue kaburi?’
“Ndio”
“Si nitaonekana na watu”
“Huendi mchana, unakwenda usiku”
“Mh!” nikaguna nilipofikiria kwenda usiku makaburini na kufukua kaburi.
“kama hutaweza basi, tutakuwa tumeshindwa”
“Nitakupa jibu hapo kesho kama nitaweza au la”
“Kumbuka kwamba nitakuwa hapa Tanga kwa siku tatu. Nikitoka hapa ninakwenda Arusha”
“Nimekuelewa, acha niende. Nitakuja tena kesho”
Nikaagana na yule mganga na kutoka, Nilipanda pikipiki yangu nikaenda nyumani kwa kaka. Kaka mwenyewe sikumkuta, mke wake aliniambia kaka aliondoka tangu saa tisa na hakumwambia anakwenda wapi.
Nikaona niende kwa mama. Nilipofika nilimueleza kwamba kaka alinipeleka kwa mganga aliyetoka Pemba na mganga akanieleza kwamba nimpelekee kucha za maiti.
“Kucha za maiti utazipata wapi?” mama akaniuliza kwa mshangao.
“Tena anataka maiti aliyekwishazikwa”
“Sasa utampataje huyo maiti aliyezikwa ukate kucha zake?”
“Sijui”
“Mh! Hayo ni makubwa”
“Maana yake niende nikafukue kaburi”
“Kaburi gani utakalokwenda kulifukua?”
“Kaburi lolote tu”
“Mh! Si utaonekana ni mchawi!”
“Labda niende usiku”
MAKUBWA! MAMBO SASA NI YA KUFUKUA ,MAKABURI! MMH! KAZI IPO JAMANI!
INAENDELEA..
 
SEHEMU YA 29


“Yaani nikafukue kaburi?’
“Ndio”
“Si nitaonekana na watu”
“Huendi mchana, unakwenda usiku”
“Mh!” nikaguna nilipofikiria kwenda usiku makaburini na kufukua kaburi.
“kama hutaweza basi, tutakuwa tumeshindwa”
“Nitakupa jibu hapo kesho kama nitaweza au la”
“Kumbuka kwamba nitakuwa hapa Tanga kwa siku tatu. Nikitoka hapa ninakwenda Arusha”
“Nimekuelewa, acha niende. Nitakuja tena kesho”
Nikaagana na yule mganga na kutoka, Nilipanda pikipiki yangu nikaenda nyumani kwa kaka. Kaka mwenyewe sikumkuta, mke wake aliniambia kaka aliondoka tangu saa tisa na hakumwambia anakwenda wapi.
Nikaona niende kwa mama. Nilipofika nilimueleza kwamba kaka alinipeleka kwa mganga aliyetoka Pemba na mganga akanieleza kwamba nimpelekee kucha za maiti.
“Kucha za maiti utazipata wapi?” mama akaniuliza kwa mshangao.
“Tena anataka maiti aliyekwishazikwa”
“Sasa utampataje huyo maiti aliyezikwa ukate kucha zake?”
“Sijui”
“Mh! Hayo ni makubwa”
“Maana yake niende nikafukue kaburi”
“Kaburi gani utakalokwenda kulifukua?”
“Kaburi lolote tu”
“Mh! Si utaonekana ni mchawi!”
“Labda niende usiku”
SASA ENDELEA
“Utaweza kufukua kaburi mpaka uipate maiti kisha uikate kucha?” Mama aliniuliza kwa mshangao.
“Nitajaribu, nikishindwa nitaacha”
“Mh!”
“Sasa nitafanyaje mama?”
“Najua kuwa huna la kufanya”
“Basi ngoja nijaribu”
Nilipoondoka kwa mama nikaanza zoezi la kuzungukia makaburi niliyokuwa nayafahamu. Pale jirani na nyumba niliyokuwa nikiishi paliwa na makaburi lakini yalikuwa karibu na makazi ya watu, ningeweza kuonekana.
Nilikwenda katika eneo la Usagara ambako pia kulikuwa na makaburi. Nikaangalia angalia kisha niliondoka tena nikaenda Gofu. Kulikuwa na makaburi yaliyokuwa kando ya barabara. Mahali hapo ndipo paliponiridhisha.
Laiti ningejua ni balaa gani ambalo ningekutana nalo usiku kwenye makaburi hayo, nisingekwenda na mpango huo ningeuacha kabisa!
Baada ya kupata uamuzi kuwa niende katika makaburi yale wakati wa usiku, nilikwenda katika duka moja la vifaa vya ujenzi nikanunua shepe, viatu vya mvua na mipira ya kuvaa mikononi. Nikavifunga nyuma ya pikipiki yangu kisha nikarudi nyumbani kwangu.
Nilikuwa nimepanga nitoke saa nane usiku ambapo hakutakuwa na watu mitaani na hivyo nisingeweza kuonekana na mtu.
Wakati nimekaa sebuleni nikiwaza nikasikia mlango wa mbele ukigongwa.
Nilisubiri, ulipogongwa tena ndipo nilipoinuka na kwenda kunako mlango huo.
“Nani?” nikauliza.
“Ni mimi Marijani”Sauti ya kaka yangu ikajibu kutoka nje.
Nikafungua mlango.
“Karibu kaka” nikamkaribisha ndani huku nikimpisha kwenye mlango.
Kaka aliingia ndani, nikafunga mlango.
“Umenishitua kidogo” nikamwambia.
“Kwanini?”
“Nilivyokuona umekuja kwangu huu usiku moyo wangu umeshituka”
“Nimekuja na wazo”
“Kaa kwenye sofa” nikamwambia kwa shauku ya kutaka kulisikia wazo alilokuwa amekuja nalo.
“Sitakaa. Nimekuja mara moja tu. Nataka niwahi kurudi”
“Pikipiki ipo nitakurudisha kaka”
“Usijali Amour tunaweza kuzungumza tukiwa tumesimama, sisi bado ni vijana. Tusiogope kusimama”
“Sawa kaka, nieleze hilo wazo ulilokuja nalo”
“Kwanza nilipata salamu kutoka kwa mke wangu kwamba ulikuja nyumbani ulipotoka kwa yule mganga”
“Ndio nilikuja lakini nikaambiwa na shemeji kuwa ulitoka”
“Ni kweli nilitoka, niliporudi ndio nilipata hizo salamu. Nikaenda kumuuliza mama kama ulifika kwake akaniambia ulifika na akanieleza ulivyoelezwa na yule mganga”
“Umeona kuwa mganga wako amenipa mtihani mkubwa”
“Ni mtihani mkubwa. Mama ameniambia ametaka umpelekee kucha za maiti”
“Tena maiti aliyezikwa, yaani niende nikafukue kaburi”
“Sasa mimi nilikuwa na wazo”
“Ndio”
“Kwanini usiwatumie vijana?’
“Kuwatumia kivipi?”
“Yaani unamtafuta kijana wa maskani unampa pesa kisha unamtuma hiyo kazi na unamuahidi kuwa akikuletea hizo kucha za maiti utampa pesa nyingine”
“Ni wazo zuri, sikuwahi kulifikiria wazo hilo”
“Yaani badala ya wewe kupata kazi ya kufukua kaburi, kazi hiyo unampa yeye. Hawa vijana ukiwapa elfu ishirini tu ya kunywea gongo na bangi wanaweza kukupatia hizo kucha”
“Ni kweli. Nitawatafuta huu usiku”
“Tena makaburi yako pale karibu tu. Kuna vijana wanaovutavuta bangi pale”
“Nashukuru kaka kwa wazo lako, umenisaidia sana”
Baada ya kunipa wazo lake hilo nilimrudisha kaka nyumbani kwake kwa pikipiki yangu.
Wakati narudi nyumbani nikawa nalitafakari lile wazo alilonipa kuona kama lilikuwa la busara.
Kwa upande mmoja wa akili yangu niliona lilikuwa wazo la busara kwa sababu lingenigharimu pesa lakini lingenirahisishia kazi. Badala ya mimi kwenda kufukua kaburi, ningempa pesa mtu mwinginne akanifanyie kazi hiyo.
Wahuni walikuwa wengi tu katika mtaa niliokuwa nikiishi, ningeweza kumtuma mmojawapo na akanifanyia kazi hiyo bila wasiwasi.
Lakini kwa upande mwingine niliona halikuwa wazo zuri. Halikuwa wazo zuri kwa sababu huyo mtu nitakayemtuma hiyo kazi nitamuaminije. Atakaponiletea hizo kucha akaniambia kuwa ni za maiti, nitaaminije kuwa ni kucha za maiti kweli?
Je kama atakwenda kukata kucha zake mwenyewe na kuniletea, nitajuaje?
Muhuni ni muhuni tu, anaweza kuona kazi ya kufukua kaburi ni ngumu na pesa haiachiki hivyo akaenda kujikata kucha zake mwenyewe na kuniletea. Sitaweza kujua kama kucha hizo si za maiti au ni zake mwenyewe.
Hivyo nikajiambia, si vizuri kufanya jambo la kubahatisha. Ni vizuri nifanye jambo la uhakika. Na nitakuwa na uhakika wa kucha hizo endapo nitakwenda mimi mwenyewe kufukua hilo kaburi na kukata kucha hizo.
Nilipofika nyumbani niliingiza pikipiki yangu nikasubiri saa nane ifike. Wakati nimeketi sebuleni nikiendelea kusubiri muda, nikapitiwa na usingizi.
Katika usingizi huo eti nikaota nimekwenda kufukua kaburi. Nikakuta mtoto mchanga aliyezikwa, hana hata kucha, Nikalifukia na kufukua kaburi jingine, hilo nalo nilikuta mtu aliyekuwa amekatwa mikono na miguu. Alikuwa amefariki kwenye ajali ya gari.
Nikalifukia tena na kutafuta kaburi jingine ambalo nilianza kulifukua. Wakati nakaribia kulifikia sanduku mvua ikanyesha kwa kishindo. Kaburi likawa linajaa maji. Kazi ikanishinda! Kutahamaki kulikuwa kunaanza kupambazuka.
Ikabidi niondoke nikiwa nimechukia. Hapo hapo nikazinduka.
Nilitazama saa yangu na kuona ilikuwa saa saba ikielekea kuwa na nusu. Nikaona wakati huo pia ulikuwa muafaka kuondoka. Nikaenda kunawa uso kisha nikarudi sebuleni na kuvaa vile viatu vya mvua kwa ajili ya kujikinga na tope wakati wa kufukua kaburi.
Ile mipira ya mikononi sikuivaa kabisa. Nikatoa pikipiki yangu. Lile shepe nilikuwa nimeshalifunga katika siti ya nyuma ya pikipiki.
Kifaa cha kukatia kucha nilikuwa nimeshakitayarisha. Ulikuwa wembe mpya.
Nikaondoka.
Niliendesha piki piki yangu taratibu hadi nikafika Gofu. Usiku huo kulikuwa kimya. Hakukuwa na gari wala watu waliokuwa wakipita. Nilikuwa na hakika kwamba hakukuwa na mtu yeyote ambaye angeniona.
Nilifika katika lile eneo la makaburi. Nikaiingiza pikipiki yangu ndani ya eneo hilo lililokuwa na mti pamoja na vichaka vidogo vidogo.
Nikaiegesha pikipiki chini ya mti huku nikiangaza macho huku na huku. Mbalamwezi ililiangaza vizuri eneo hilo kiasi kwamba sikupata taabu kuyaona makaburi hayo.
Nilianza kuvaa mipira ya mikononi kisha nikalifungua lile shepe. Nililishika mkononi nikaanza kutafuta kaburi la kuchimba.
Makaburi mengi yalikuwa yamewekewa zege, nikaenda mbele zaidi. Nikakuta kaburi moja ambalo halikuwa limewekewa zege na lilionesha lilikuwa jipya. Huenda kulikuwa na mtu aliyekuwa
amezikwa siku iliyopita.
Nikaanza kulichimba. Kwa vile mchnaga wake ulikuwa laini nililichimba haraka harka huku nikirundika mchanga upande mmoja juu ya kaburi hilo. Shimo lilipokuwa kubwa niliweza kuingia ndani nikaendelea kuchimba.
Baada ya kama nusu saa tu nikawa nimelifikia sanduku lililokuwemo ndani. Nilipofanikiwa kuuondoa mchanga wote uliokuwa juu ya sanduku hilo nikaufungua mlango wa sanduku na kuuacha wazi. Ndani ya sanduku hilo niliona maiti ya mwanamke.
Nikatia mkono mfukoni mwangu na kutoa ule wembe. Niliufungua kwenye karatasi yake nikaushika kisha nikaushika mkono wa ile maiti ya mwanamke. Hapo hapo nikaona mwanga wa tochi unanimulika kutoka juu ya kaburi kisha sauti nzito ikaniuliza.
“Wewe nani na unafanya nini hapa?”
Kwa kweli nilishituka sana. Wembe uliniponyoka. Miguu ikanitepeta. Nikainua uso wangu haraka na kutazama juu ya kaburi hilo.
Nilijuta!
DUH! JAMAA KAFUMWA NA NANI TENA? HAYA ITKUWAJE JAMANI! HUU NI MKASA MWINGINE TENA!
 
SEHEMU YA 30


ILIPOISHIA
Nilitazama saa yangu na kuona ilikuwa saa saba ikielekea kuwa na nusu. Nikaona wakati huo pia ulikuwa muafaka kuondoka. Nikaenda kunawa uso kisha nikarudi sebuleni na kuvaa vile viatu vya mvua kwa ajili ya kujikinga na tope wakati wa kufukua kaburi.
Ile mipira ya mikononi sikuivaa kabisa. Nikatoa pikipiki yangu. Lile shepe nilikuwa nimeshalifunga katika siti ya nyuma ya pikipiki.
Kifaa cha kukatia kucha nilikuwa nimeshakitayarisha. Ulikuwa wembe mpya.
Nikaondoka.
Niliendesha piki piki yangu taratibu hadi nikafika Gofu. Usiku huo kulikuwa kimya. Hakukuwa na gari wala watu waliokuwa wakipita. Nilikuwa na hakika kwamba hakukuwa na mtu yeyote ambaye angeniona.
Nilifika katika lile eneo la makaburi. Nikaiingiza pikipiki yangu ndani ya eneo hilo lililokuwa na mti pamoja na vichaka vidogo vidogo.
Nikaiegesha pikipiki chini ya mti huku nikiangaza macho huku na huku. Mbalamwezi ililiangaza vizuri eneo hilo kiasi kwamba sikupata taabu kuyaona makaburi hayo.
Nilianza kuvaa mipira ya mikononi kisha nikalifungua lile shepe. Nililishika mkononi nikaanza kutafuta kaburi la kuchimba.
Makaburi mengi yalikuwa yamewekewa zege, nikaenda mbele zaidi. Nikakuta kaburi moja ambalo halikuwa limewekewa zege na lilionesha lilikuwa jipya. Huenda kulikuwa na mtu aliyekuwa
amezikwa siku iliyopita.
Nikaanza kulichimba. Kwa vile mchaga wake ulikuwa laini nililichimba haraka haraka huku nikirundika mchanga upande mmoja juu ya kaburi hilo. Shimo lilipokuwa kubwa niliweza kuingia ndani nikaendelea kuchimba.
Baada ya kama nusu saa tu nikawa nimelifikia sanduku lililokuwemo ndani. Nilipofanikiwa kuuondoa mchanga wote uliokuwa juu ya sanduku hilo nikaufungua mlango wa sanduku na kuuacha wazi. Ndani ya sanduku hilo niliona maiti ya mwanamke.
Nikatia mkono mfukoni mwangu na kutoa ule wembe. Niliufungua kwenye karatasi yake nikaushika kisha nikaushika mkono wa ile maiti ya mwanamke. Hapo hapo nikaona mwanga wa tochi unanimulika kutoka juu ya kaburi kisha sauti nzito ikaniuliza.
“Wewe nani na unafanya nini hapa?”
Kwa kweli nilishituka sana. Wembe uliniponyoka. Miguu ikanitepeta. Nikainua uso wangu haraka na kutazama juu ya kaburi hilo.
Nilijuta!
SASA ENDELEA
Nilimuona mtu aliyekuwa akinimulika tochi akiwa juu ya kaburi lakini sikuweza kumuona vizuri kwa sababu ule mwanga wa tochi ulikuwa unapiga kwenye macho yangu.
“Ulikuwa unafanya nini?’ Mtu huyo aliendelea kuniuliza kwa ukali.
Sikumjibu. Yeye alikuwa amesimama upande mmoja wa kaburi. Na mimi nilikurupuka kuelekea upande mwingine wa kaburi nikapanda juu haraka.
Wakati ninainuka ili nikimbie, alinirushia rungu. Nikainama na kulikwepa. Wakati nainama niliona kitu kikiruka kutoka mfuko wa shati langu na kuanguka chini. Sikujua kilikuwa kitu gani. Na sikuwa na muda wa kukitazama vizuri.
Yule mtu nilimuona. Kwa jinsi alivyovaa niligundua alikuwa mlinzi. Nikahisi alikuwa mlinzi wa eneo lile.
Nikatimua mbio kuelekea nilikoiacha pikipiki yangu. Wakati nakimbia nilijiuliza kama kulikuwa na mlinzi, alikuwa wapi wakati nafika na kufukua lile kaburi?
Nilitazama nyuma na kumuona alikuwa ananikimbiza.
“Simama wewe, utakufa!” aliniambia.
Lakini sikugeuka wala sikusimama. Niliendelea kukimbia hadi nikaifikia pikipiki yangu, yeye bado akiwa mbali. Niliiwasha haraka haraka. Pikipiki ilikubali mara moja. Nikaipanda na kuondoka kwa kasi.
“Wewe…bahati yako!” aliniambia baada ya kunikosa.
Alikuwa amesimama akinielekeza rungu lake. Niligeuza uso mara moja tu nikamtazama.
Alipoona namtazama aliniambia kwa hasira.
“Usije tena hapa mchawi mkubwa. Ningekuua leo!”
Niligeuza uso wangu nikatazama mbele ninakoelekea. Kimoyomoyo nilikuwa nikijiambia.
“Ningekufa leo!”
Nilikuwa nimekaa kwenye pikipiki huku nikijihisi wazi kuwa nilikuwa natetemeka. Sikuwa nimezoea mapambano hivyo tukio lile la kufumwa na kutimuliwa kwa sime lilitosha kunifanya nitetemeke.
Nilikuwa nikijiambia laiti yule mtu angenishika angeniua kwa vile mwenzngu alikuwa na silaha, mimi niko mikono mitupu.
Nilirudi nyumbani nikiwa nimeacha shepe langu ndani ya lile kaburi.
Lakini halikuwa mali kuliko uhai wangu. Kucha za maiti zilitaka kunitoa roho yangu!
Nilipofika nyumbani nillikuwa nahema kama vile nilikimbia njia nzima kurudi nyumbani. Niliingiza pikipiki yangu. Nikavua vile viatu nilivyovaa kuzuia tope pamoja na mipira ya mikononi kisha nikaingia bafuni kuoga.
Nilipotoka bafuni niliona afadhali kidogo. Nikaenda kulala. Hata usingizi wenyewe sikuupata. Nilianndamwa na njozi za ajabu ajabu hadi kunakucha. Moja ya ndoto iliyonitisha ilikuwa ile maiti niliyoifukua imegeuka mzuka na kunifuata nyumbani ikiwa imetoka kucha ndefu vidoleni.
Kucha hizo ndizo zilizokuwa zinatoboa mlango wa chumbani kwangu. Wakati nashituka mlango wa chumbani kwangu ulikuwa umeshafunguka.
Laiti nisingewahi kuamka sijui ingekuwaje?
Ilikuwa miujiza mitupu!
Baada ya kuoga na kuvaa nilitoa pikipiki yangu. Hapo ndipo nilipogundua kuwa leseni yangu sikuwa nayo mfukoni. Usiku uliopita niliiweka kwenye mfuko wa shati langu na kwa muda ule sikuwa nayo.
Nikahisi ndio iliyonianguka kule makaburini usiku wakati yule mlinzi akinikurupusha.
Nikawa nimegwaya. Nilijiambia kama yule mlinzi ataiona ile leseni yangu ambayo ilikuwa na picha yangu anaweza kuipeleka polisi. Kwa vile tayari nilikuwa na rikodi mbaya polisi, kugunduliwa kwangu kungekuwa rahisi sana.
Polisi watakapoiona picha yangu watanifuata kazini kwangu na kunikamata.
Imeshakuwa balaa!
Licha ya kupatwa na fadhaa kiasi hicho nilipanda pikipiki yangu. Kwanza nilikwenda Chuda kumueleza kaka yangu mkasa mzima.
“Amour umefanya uzembe mwenyewe!” kaka akaniambia baada ya kunisikiliza.
Uso wake ulionesha wazi kuwa hakufurahishwa na kitendo changu.
“Nimefanya uzembe kivipi kaka?” nikamuuliza.
“Jana nilikwambia nini?”
“Hebu nikumbushe pengine nimesahau”
“Si nilikwambia kwamba tuma mtu”
“Kaka kutuma mtu kunaweza kuleta matatizo”
“Matatizo gani?’
“Sitakuwa na uhakika kama hizo kucha atakazoniletea ni za maiti kweli. Anaweza kwenda kujikata kucha zake mwenyewe akaniletea”
“Ungetafuta mtu unayemuamini”
“Wahuni hawaaminiki kaka. Wangechukua pesa zangu halafu wakaniletea kucha zao wenyewe”
Kaka yangu akanywea.
“Saasa umeshajitia kwenye balaa jingine!”
“Kwa kweli ni balaa, sasa sijui itakuwaje!”
“Kwani hivi sasa unakwenda wapi?”
“Ninakwenda kazini”
“Ukitoka kazini nenda ukamueleze yule mganga”
“Nitakwenda”
“Basi wewe nenda kazini kwako, punguza wasiwasi”
Nikaondoka kwa kaka na kwenda kazini. Lakini njia nzima nilikuwa nawaza tu.
Nilipofika niliingia kazini kama kawaida. Baadaye kidogo mhasibu alifika na kuingia ofisini kwake. Haukupita muda mrefu mhasibu alitufuata akatueleza kisa kilichonishitua.
“Jana tulikwenda kuzika kule Gofu, shemeji yangu alikuwa amefariki. Hivi sasa napigiwa simu naelezwa kwamba kuna mtu alikwenda kulifukua lile kaburi usiku. Sijui alitaka kuichukua ile maiti?”
“Labda ni wachawi, lakini hakuwahi kuichukua?” Mfanya kazi mmoja akamuuliza.
“Hakuwahi, alikurupushwa na mlinzi. Lile eneo linalindwa kwa ajili yakuzuia watu kama hao”
“Angemkamata ingekuwa vizuri kwa sababu angefahamika” Mfanyakazi mwingine alidakia.
“Alikimbia na pikipiki. Mlinzi amesema huyo mtu alikuja na pikipiki”
Niliposikia hivyo moyo wangu ulishituka. Kama namba za pikipiki yangu nazo zimeonekana nimekwisha!
Sikujua kama ile maiti ilikuwa ni ya shemeji yake mhasibu wetu. Nikaona nimejiingiza katika matatizo mengine ambayo sikuyatarajia.
“Hivi sasa nimeitwa polisi nikatoe maelezo, ile maiti imepelekwa hospitali kufanyiwa uchunguzi kujua kama ilibakwa. Kuna watu wanabaka maiti” Mhasibu aliendelea kutueleza.
“Inawezekana. Ni vizuri kama amepelekwa hospitali kufanyiwa uchunguzi. Binaadamu hivi sasa hawaaminiki kabisa” nikajidai kusema ili nisionekane nimefadhaika.
“Kumbe yule mlinzi alikwenda kuripoti polisi” Mwenzetu mwingine akauliza.
“Alikwenda polisi asubuhi. Ndio maana ninaitwa polisi” Mhasibu akamjibu kisha akatuaga na kuondoka.
Niliwaza kwamba kama mlinzi alikwenda kuripoti polisi, ile leseni yangu pia aliipeleka baada ya kuiokota pale ilipoanguka. Polisi watakuwa wameshaiona picha yangu. Bila shaka mhasibu wetu ameitwa ili kuoneshwa ile leseni ili athibitishe kama ndiye mimi.
Sasa sijui nikimbie kuepusha aibu, au niwangoje polisi waje wanikamate hapa hapa?
Kwa kweli nilikuwa nimechanganyikiwa.
KWA KWELI JINSI JAMAA ALIVYOANDAMWA NA MIKASA, ANATIA HURUMA. LIKITOKA HILI LINAKUJA HILI. DUH! SASA SIJUI ITAKUWAJE? Jamaa ataumbuka huyu!
INAENDELEA...
 
SEHEMU YA 31


ILIPOISHIA
Niliposikia hivyo moyo wangu ulishituka. Kama namba za pikipiki yangu nazo zimeonekana nimekwisha!
Sikujua kama ile maiti ilikuwa ni ya shemeji yake mhasibu wetu. Nikaona nimejiingiza katika matatizo mengine ambayo sikuyatarajia.
“Hivi sasa nimeitwa polisi nikatoe maelezo, ile maiti imepelekwa hospitali kufanyiwa uchunguzi kujua kama ilibakwa. Kuna watu wanabaka maiti” Mhasibu aliendelea kutueleza.
“Inawezekana. Ni vizuri kama amepelekwa hospitali kufanyiwa uchunguzi. Binaadamu hivi sasa hawaaminiki kabisa” nikajidai kusema ili nisionekane nimefadhaika.
“Kumbe yule mlinzi alikwenda kuripoti polisi” Mwenzetu mwingine akauliza.
“Alikwenda polisi asubuhi. Ndio maana ninaitwa polisi” Mhasibu akamjibu kisha akatuaga na kuondoka.
Niliwaza kwamba kama mlinzi alikwenda kuripoti polisi, ile leseni yangu pia aliipeleka baada ya kuiokota pale ilipoanguka. Polisi watakuwa wameshaiona picha yangu. Bila shaka mhasibu wetu ameitwa ili kuoneshwa ile leseni ili athibitishe kama ndiye mimi.
Sasa sijui nikimbie kuepusha aibu, au niwangoje polisi waje wanikamate hapa hapa?
Kwa kweli nilikuwa nimechanganyikiwa.
SASA ENDELEA
Kwa dakika kadhaa sikuweza kujua nifanye nini. Wafanyakazi wenzangu walikuwa wakilizungumzia lile tukio la kufukuliwa kaburi, mimi nilikuwa kimya. Moyo wangu ulikuwa ukihangaika. Lakini hakukuwa na yeyote aliyeweza kunigundua.
Wasiwasi uliponizidi nilitoka nje ya duka letu. Kilichonitoa ni ule wasiwasi kwamba polisi wakitokea niweze kuwaona mapema. Nilikuwa nimeshapanga kuwakimbia.
Ilikuwa bora kupotea kuliko kupatwa na fedheha kama ile mbele ya wafanyakazi wenzangu.
Nilisimama nje ya duka letu kwa karibu nusu saa, nilipoona hakukuwa na polisi wowote waliokuwa wanakuja nikarudi ndani. Baadaye nikatoka tena. Nikaangalia pande zote za barabara kisha nikarudi.
Wakati nimekaa nikiendelea na mawazo yangu nilishituka nilipomuona mhasibu akiingia. Nilijua kuwa alikuwa amefuatana na polisi waliokuja kunikamata.
Lakini sikuona polisi. Alikuwa peke yake. Nikamkodolea macho ya tashiwishi. Nilikuwa na hisia kwamba alikuwa ameoneshwa leseni yangu na kunitambua.
Mfanyakazi mwenzetu mmoja akamuuliza kilichotokea huko polisi alikokwenda.
“Nimekwenda kutoa maelezo yangu” akasema na kuongeza.
“Ule mwili bado uko hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi”
“Huyo mtu aliyefukua hilo kaburi hakufahamika?’ nikauliza ili kuondoa dukuduku nililokuwa nalo.
“Si rahisi kufahamika. Mtu mwenyewe alikimbia na pikipiki” Mhasibu akanijibu.
Hapo wasiwasi ukanipungua kidogo.
Baada ya mhasibu kuzungumza na sisi kwa dakika chache akaingia ofisini kwake.
Haukupita muda mrefu, simu tuliyokuwa tunaitumia ikaita. Ilikuwa inapokelewa na mtu yeyote aliye karibu nayo. Akaipokea mfanyakazi mmoja akasikiliza kisha akaniita.
“Amour ni simu yako”
Moyo ukanipasuka.
Ni nani tena?
Nikaenda na kukipokea chombo cha kuzungumzia. Nikakiweka sikioni na kusema.
“Hello!”
“Naongea na bwana Amour?” Sauti nzito tena inayokwaruza ikauliza kutoka simu ya upande wa pili.
Moyoni mwangu nilikuwa nikijiuliza ni nani mwenye sauti hii? Akilini mwangu sikuweza kukumbuka mtu yeyote ninayemfahamu mwenye sauti inayolingana na ile.
Nikashuku kwamba anaweza kuwa afisa wa polisi ananipigia kuniita kituo cha olisi.
“Ndio. Wewe nani?”
“Hebu njoo hapa Tropicana, utanijua tu”
Tropicana ulikuwa mkahawa uliokuwa mtaa wa pili ambao wafanyakai wengi hupenda kunywa chai wakati wa saa nne na hata kula chakula cha mchana.
“Ni vizuri unifahamishe wewe nani?”
“Usiwe na wasiwasi. Ukifika hapa utaniona na utanijua”
Nikaurudisha mkono wa simu kisha nikatoka. Niliwaaga wenzangu kuwa ninakwenda kunywa chai.
Nilipotoka nje ya duka letu nilizunguka mtaa wa pili ambako kulikuwa na huo mkahawa wa Tropicana. Wakati natembea nilikuwa nikiwaza huyo mtu aliyeniita atakuwa nani kama si afisa wa polisi.
Nilikuwa na hakika kwamba sikuwa nikifahamiana na mtu aliyekuwa na sauti kavu kama ile.
Nilipofika kwenye mkahawa huo nikaingia. Nilisita kidogo kando ya mlango nikawatupia macho watu waliokuwamo ndani. Nikaona mtu mmoja aliyekuwa amekaa katika meza ya pembeni akinipungia mkono kuniita.
Sikuweza kumfahamu mpaka nilipofika karibu yake.
“Ah Mgosingwa!” nikasema mara tu sura yake iliponijia akilini mwangu.
Alikuwa mlinzi wetu ambaye alifukuzwa kazi kwa tabia yake ya ulevi wa kupita kiasi. Tulikuwa tunamuita Mgosingwa, neno la kabila la kizigua linalotokana na neno mgosi, yaani mwanamme.
Kwa vile yeye mwenyewe alikuwa mzigua, alikuwa akimuita kila mtu “mgosingwa” hasa pale anapotaka kumkopa mtu pesa ya kwenda kulewea. Na sisi tukampa jina hilo la mgosingwa. Nilizoea kumuita hivyo na jina lake halisi nilikuwa silijui.
“Vipi Mgosingwa?” akaniambia huku akinipa mkono kunisalimia.
“Salama tu Mgosingwa. Wewe ndio uliyenipigia simu kuniita?’
“Ndiye mimi Mgosingwa. Karibu ukae”
Nikakaa kwenye kiti.
“Ulikuwa unasemaje Mgosingwa?” nikamuuliza nikiwa na shauku ya kutaka kujua alichoniitia.
“Mgosingwa unatakiwa polisi!”
Kusema kweli nilishituka aliponiambia hivyo. Moyo wangu ukawa unadunda pu!pu!pu!
Nikajidai natabasamu.
“Nimefanya kosa gani Mgosingwa?”
Mgosingwa alitia mkono kwenye mfuko wa shati lake akatoa ganda kama la kitambulisho akaniwekea mezani.
“hii si leseni yako Mgosingwa?’ akaniuliza.
Nikalichukua lile ganda na kulifungua. Naam. Ilikuwa ni leseni yangu niliyokuwa nimeitupa kule makaburini. Pale pale uso wangu ulibadilika rangi kwa hofu iliyochanganyika na fadhaa. Nikamtazama mgosingwa huku nikijiuliza ameipata wapi leseni yangu.
“Huku nikiendelea na tabasamu langu la kulazimisha nilimuuliza.
“Mgosingwa umeipata wapi hii leseni yangu?’
“Si nimekwambia unatakiwa polisi?”
Jibu lake hilo lilizidi kunichanganya na kunifadhaisha. Midomo yangu niliyokuwa ninailazimisha kutabasamu huku nikiwa na fadhaa ilianza kutatizika na kutetemeka. Sasa haikuweza tena kutabasamu.
“Mgosingwa unanichanganya. Sasa nani kakupa hii leseni na kakupa kwa madhumuni gani?” nikamuuliza huku nikiizuia modomo yangu isitetemeke wakati nikimuuliza hivyo.
Mgosingwa aligundua kuwa nilikuwa nimetaharuki. Akacheka. Hata hivyo kwa vile uso wake ulikuwa umekunjana kutokana na kuendeleza kilevi, kicheko chake hakikuufanya uso wake upendeze, bali ulionekana kama anataka kulia.
“Mgosingwa hukumbuki uliiacha wapi leseni yako?” akaniuliza.
Nikatikisa kichwa.
“Sikumbuki” Nilimjibu hivyo ili nijue ataniambia nini.
“Mgosingwa jana usiku si ulikuja kule makaburi ukafukua lile kaburi nikakukurupusha”
JE NINI KITATOKEA?
ENDELEA KUFWATILIA MKASA HUU
 
SEHEMU YA 32


ILIPOISHIA
Mgosingwa alitia mkono kwenye mfuko wa shati lake akatoa ganda kama la kitambulisho akaniwekea mezani.
“hii si leseni yako Mgosingwa?’ akaniuliza.
Nikalichukua lile ganda na kulifungua. Naam. Ilikuwa ni leseni yangu niliyokuwa nimeitupa kule makaburini. Pale pale uso wangu ulibadilika rangi kwa hofu iliyochanganyika na fadhaa. Nikamtazama mgosingwa huku nikijiuliza ameipata wapi leseni yangu.
“Huku nikiendelea na tabasamu langu la kulazimisha nilimuuliza.
“Mgosingwa umeipata wapi hii leseni yangu?’
“Si nimekwambia unatakiwa polisi?”
Jibu lake hilo lilizidi kunichanganya na kunifadhaisha. Midomo yangu niliyokuwa ninailazimisha kutabasamu huku nikiwa na fadhaa ilianza kutatizika na kutetemeka. Sasa haikuweza tena kutabasamu.
“Mgosingwa unanichanganya. Sasa nani kakupa hii leseni na kakupa kwa madhumuni gani?” nikamuuliza huku nikiizuia modomo yangu isitetemeke wakati nikimuuliza hivyo.
Mgosingwa aligundua kuwa nilikuwa nimetaharuki. Akacheka. Hata hivyo kwa vile uso wake ulikuwa umekunjana kutokana na kuendeleza kilevi, kicheko chake hakikuufanya uso wake upendeze, bali ulionekana kama anataka kulia.
“Mgosingwa hukumbuki uliiacha wapi leseni yako?” akaniuliza.
Nikatikisa kichwa.
“Sikumbuki” Nilimjibu hivyo ili nijue ataniambia nini.
“Mgosingwa jana usiku si ulikuja kule makaburi ukafukua lile kaburi nikakukurupusha”
SASA ENDELEA
Aliponiambia hivyo nikanywea na kumtazama. Alipoona nipo kimya aliendelea kunieleza.
“Wakati unakimbia mgosingwa uliiangusha hii leseni yako”
“Kumbe wewe ndiye unayelinda pale?” nikamuuliza.
“Nilipoacha kazi STC niliajiriwa na kanisa kulinda yale makaburi. Sasa jana usiku niliondoka kidogo kwenda kupata ulabu (kilevi), niliporudi nikakuta mtu amechimba kaburi na kuingia ndani. Hii leseni niliiokota asubuhi ndio nikagundua kuwa ulikuwa wewe”
“Sasa Mgosingwa umeshakwenda kutoa ripoti polisi?”
Polisi nimeshakwenda lakini nilipoona hii leseni yako sikuwapa. Niliwambia huyo mtu sikumuona vizuri”
Hapo hapo nilitia mkono mfukoni nakutoa pochi yangu. Niliifungua na kuchomoa noti za shilingi elfu ishirini, nikampa.
“Asante sana Mgosingwa, umenisaidia sana”
SASA ENDELEA
“Tunajuana Mgosingwa , hatuwezi kusalitiana” Mgosingwa aliniambia wakati akipokea zile pesa.
“Unajua lile kaburi ni la shemeji yake mhasibu wetu. Mimi sikujua kabisa”
“Kwani ulikuwa unataka nini Mgosingwa?”
“Kuna kitu nilikuwa nataka”
“Kitu gani?”
Kwanza nilisita kumwambia nilikuwa nataka nini lakini nikaona ni vizuri nimwambie.
“Nilikuwa nataka kucha za maiti”
“Mgosingwa unataka kwenda kuroga au kuua mtu?”
“Hapana. Ni kwa mambo yangu binafsi”
“Mgosingwa ungeniambia, ningekupatia. Mimi Ndio nalinda yale makaburi”
“Bado ninazihitaji Mgosingwa, nifanyie huo mpango”
“Utanipa shilingi ngapi?”
“Ukiniletea hizo kucha nitakuongezea kumi nyingine”
“Fanya ishirini Mgosingwa, kumi ndogo sana”
“Si kitu, nitakupa hizo ishirini”
“Sasa Mgosingwa nitafutie shepe na kiwembe. Niletee pale saa nne usiku. Mimi nitafukua kaburi, asubuhi nitakuletea hizo kucha nyumbani kwako”
“Hakuna tatizo. Nitakuletea hilo shepe. Kiwembe utanunua mwenyewe”
“Sasa Mgosingwa fanya kitu kimoja, nipatie kianzio cha shilingi elfu kumi, hiyo kumi nyingine utanipa asubuhi”
Nilitaka kucheka lakini nilisita kwa sababu tulikuwa katika suala nyeti sana kwa upande wangu.
“Kwanini usisubiri hadi hiyo asubuhi nikupe zote?” nikamuuliza.
“Ninahitaji hiyo pesa kwa sasa”
“Mgosingwa si nimekupa elfu ishirini za bure?”
“Mgosingwa si za bure, polisi ungetoa ngapi ili wakuachie”
“Sawa. Sasa si hizo nimekupa”
“Hazitoshi Mgosingwa”
“Wewe unataka kwenda kulewa tu” nikamwambia huku nikitia mkono kwenye mfuko wa suruali yangu.
Nilitoa pochi yangu nikaifungua na kumpa shilingi elfu kumi alizotaka.
“Umeridhika?” nikamuuliza.
“Hapa Mgosingwa umeniokoa sana”
“Utapata chupa ngapi”
“Acha mzaha Mgosingwa. Mimi siendi kulewa. Mke wangu amekwenda kwao kujifungua. Nilitaka kumtumia hzi pesa”
“Sawa Mgosingwa mtumie, nilikutania tu”
“Sasa Mgosingwa niletee shepe saa nne usiku pale pale”
“Sawa, nitakuletea”
Nikaagana na Mgosingwa na kuondoka.
Nilipotoka kazini jioni nilikwenda kununua shepe jingine nikaenda nalo nyumbani. Nikawa nasubiri saa nne usiku ifike nimpelekee Mgosingwa.
Kwa mara ya kwanza niligundua hata mlevi anaweza kuwa na manufaa yake. Sikutarajia kuwa Mgosingwa mlevu wa gongo na pombe ya mnazi angeweza kunisaidia. Licha ya msaada wa kucha za maiti alioniahidi, kile kitendo chake cha kuiokota leseni yangu na kuja kunipa mwenyewe bila kuipeleka polisi ulikuwa msaada mkubwa kwangu.
Nilimshukuru sana nikijua kama si yeye ningeumbuka. Pengine muda ule ningekuwa niko mahabusi.
Ilipofika saa nne usiku nililifunga lile shepe sehemu ya nyuma ya siti ya pikipiki yangu nikatoka.
Nilikwenda katika lile eneo la makaburi analolinda Mgosingwa. Niliposimamisha tu pikipiki, Mgosingwa akajitokeza. Alitazama kila upande, alipoona kuko kimya akasogea kwenye pikipiki yangu na kunisaidia kulifungua lile shepe.
Ile hewa yake ya mwilini tu ingetosha kumlewesha mtu. Alikuwa akinuka pombe aina ya gongo kama vile alikuwa mtambo wa kuitengenezea. Muda ule tayari alikuwa ameshalewa.
Sikumlaumu. Kulinda makaburi wakati wa usiku ilikuwa kazi ya kutisha. Alihitaji kupata kitu cha kutuliza akili yake, vinginevyo anaweza kuota ndoto za maiti waliozikwa usiku kucha.
Hatukuungumza chochote. Alipochukua lile shepe, alinionesha ishara kuwa tukutane asubuhi akatokomea makaburini.
Nikapanda pikipiki yangu na kuondoka. Nilipofika nyumbani nilifikia kuoga na kulala.
Kulikuwa kunaanza kupambazuka nilipoamshwa usingizini kwa kishindo cha mlango wa mbele uliokuwa unabishwa. Nikatazama saa yangu na kuona ilikuwa saa kumi na mbili kasorobo. Nikajiuliza ni nani abishae mlango? Sikupata jibu.
Nikashuka kitandani na kuvaa suruali yangu kisha nikafungua mlango wa chumbani mwangu na kutoka ukumbini. Nilikwenda kwenye mlango wa mbele na kuuliza.
“Nani abishaye?”
“Ni mimi Mgosingwa!” nikaisikia sauti ya Mgosingwa ikisikika kwa nje.
“Ahaa ni wewe!” nikasema huku nikifungua mlango.
JE MGOSINGWA AMEPATA HIZO KUCHA? JIBU UTALIPATA KESHO
 
SEHEMU YA 32


ILIPOISHIA
Mgosingwa alitia mkono kwenye mfuko wa shati lake akatoa ganda kama la kitambulisho akaniwekea mezani.
“hii si leseni yako Mgosingwa?’ akaniuliza.
Nikalichukua lile ganda na kulifungua. Naam. Ilikuwa ni leseni yangu niliyokuwa nimeitupa kule makaburini. Pale pale uso wangu ulibadilika rangi kwa hofu iliyochanganyika na fadhaa. Nikamtazama mgosingwa huku nikijiuliza ameipata wapi leseni yangu.
“Huku nikiendelea na tabasamu langu la kulazimisha nilimuuliza.
“Mgosingwa umeipata wapi hii leseni yangu?’
“Si nimekwambia unatakiwa polisi?”
Jibu lake hilo lilizidi kunichanganya na kunifadhaisha. Midomo yangu niliyokuwa ninailazimisha kutabasamu huku nikiwa na fadhaa ilianza kutatizika na kutetemeka. Sasa haikuweza tena kutabasamu.
“Mgosingwa unanichanganya. Sasa nani kakupa hii leseni na kakupa kwa madhumuni gani?” nikamuuliza huku nikiizuia modomo yangu isitetemeke wakati nikimuuliza hivyo.
Mgosingwa aligundua kuwa nilikuwa nimetaharuki. Akacheka. Hata hivyo kwa vile uso wake ulikuwa umekunjana kutokana na kuendeleza kilevi, kicheko chake hakikuufanya uso wake upendeze, bali ulionekana kama anataka kulia.
“Mgosingwa hukumbuki uliiacha wapi leseni yako?” akaniuliza.
Nikatikisa kichwa.
“Sikumbuki” Nilimjibu hivyo ili nijue ataniambia nini.
“Mgosingwa jana usiku si ulikuja kule makaburi ukafukua lile kaburi nikakukurupusha”
SASA ENDELEA
Aliponiambia hivyo nikanywea na kumtazama. Alipoona nipo kimya aliendelea kunieleza.
“Wakati unakimbia mgosingwa uliiangusha hii leseni yako”
“Kumbe wewe ndiye unayelinda pale?” nikamuuliza.
“Nilipoacha kazi STC niliajiriwa na kanisa kulinda yale makaburi. Sasa jana usiku niliondoka kidogo kwenda kupata ulabu (kilevi), niliporudi nikakuta mtu amechimba kaburi na kuingia ndani. Hii leseni niliiokota asubuhi ndio nikagundua kuwa ulikuwa wewe”
“Sasa Mgosingwa umeshakwenda kutoa ripoti polisi?”
Polisi nimeshakwenda lakini nilipoona hii leseni yako sikuwapa. Niliwambia huyo mtu sikumuona vizuri”
Hapo hapo nilitia mkono mfukoni nakutoa pochi yangu. Niliifungua na kuchomoa noti za shilingi elfu ishirini, nikampa.
“Asante sana Mgosingwa, umenisaidia sana”
SASA ENDELEA
“Tunajuana Mgosingwa , hatuwezi kusalitiana” Mgosingwa aliniambia wakati akipokea zile pesa.
“Unajua lile kaburi ni la shemeji yake mhasibu wetu. Mimi sikujua kabisa”
“Kwani ulikuwa unataka nini Mgosingwa?”
“Kuna kitu nilikuwa nataka”
“Kitu gani?”
Kwanza nilisita kumwambia nilikuwa nataka nini lakini nikaona ni vizuri nimwambie.
“Nilikuwa nataka kucha za maiti”
“Mgosingwa unataka kwenda kuroga au kuua mtu?”
“Hapana. Ni kwa mambo yangu binafsi”
“Mgosingwa ungeniambia, ningekupatia. Mimi Ndio nalinda yale makaburi”
“Bado ninazihitaji Mgosingwa, nifanyie huo mpango”
“Utanipa shilingi ngapi?”
“Ukiniletea hizo kucha nitakuongezea kumi nyingine”
“Fanya ishirini Mgosingwa, kumi ndogo sana”
“Si kitu, nitakupa hizo ishirini”
“Sasa Mgosingwa nitafutie shepe na kiwembe. Niletee pale saa nne usiku. Mimi nitafukua kaburi, asubuhi nitakuletea hizo kucha nyumbani kwako”
“Hakuna tatizo. Nitakuletea hilo shepe. Kiwembe utanunua mwenyewe”
“Sasa Mgosingwa fanya kitu kimoja, nipatie kianzio cha shilingi elfu kumi, hiyo kumi nyingine utanipa asubuhi”
Nilitaka kucheka lakini nilisita kwa sababu tulikuwa katika suala nyeti sana kwa upande wangu.
“Kwanini usisubiri hadi hiyo asubuhi nikupe zote?” nikamuuliza.
“Ninahitaji hiyo pesa kwa sasa”
“Mgosingwa si nimekupa elfu ishirini za bure?”
“Mgosingwa si za bure, polisi ungetoa ngapi ili wakuachie”
“Sawa. Sasa si hizo nimekupa”
“Hazitoshi Mgosingwa”
“Wewe unataka kwenda kulewa tu” nikamwambia huku nikitia mkono kwenye mfuko wa suruali yangu.
Nilitoa pochi yangu nikaifungua na kumpa shilingi elfu kumi alizotaka.
“Umeridhika?” nikamuuliza.
“Hapa Mgosingwa umeniokoa sana”
“Utapata chupa ngapi”
“Acha mzaha Mgosingwa. Mimi siendi kulewa. Mke wangu amekwenda kwao kujifungua. Nilitaka kumtumia hzi pesa”
“Sawa Mgosingwa mtumie, nilikutania tu”
“Sasa Mgosingwa niletee shepe saa nne usiku pale pale”
“Sawa, nitakuletea”
Nikaagana na Mgosingwa na kuondoka.
Nilipotoka kazini jioni nilikwenda kununua shepe jingine nikaenda nalo nyumbani. Nikawa nasubiri saa nne usiku ifike nimpelekee Mgosingwa.
Kwa mara ya kwanza niligundua hata mlevi anaweza kuwa na manufaa yake. Sikutarajia kuwa Mgosingwa mlevu wa gongo na pombe ya mnazi angeweza kunisaidia. Licha ya msaada wa kucha za maiti alioniahidi, kile kitendo chake cha kuiokota leseni yangu na kuja kunipa mwenyewe bila kuipeleka polisi ulikuwa msaada mkubwa kwangu.
Nilimshukuru sana nikijua kama si yeye ningeumbuka. Pengine muda ule ningekuwa niko mahabusi.
Ilipofika saa nne usiku nililifunga lile shepe sehemu ya nyuma ya siti ya pikipiki yangu nikatoka.
Nilikwenda katika lile eneo la makaburi analolinda Mgosingwa. Niliposimamisha tu pikipiki, Mgosingwa akajitokeza. Alitazama kila upande, alipoona kuko kimya akasogea kwenye pikipiki yangu na kunisaidia kulifungua lile shepe.
Ile hewa yake ya mwilini tu ingetosha kumlewesha mtu. Alikuwa akinuka pombe aina ya gongo kama vile alikuwa mtambo wa kuitengenezea. Muda ule tayari alikuwa ameshalewa.
Sikumlaumu. Kulinda makaburi wakati wa usiku ilikuwa kazi ya kutisha. Alihitaji kupata kitu cha kutuliza akili yake, vinginevyo anaweza kuota ndoto za maiti waliozikwa usiku kucha.
Hatukuungumza chochote. Alipochukua lile shepe, alinionesha ishara kuwa tukutane asubuhi akatokomea makaburini.
Nikapanda pikipiki yangu na kuondoka. Nilipofika nyumbani nilifikia kuoga na kulala.
Kulikuwa kunaanza kupambazuka nilipoamshwa usingizini kwa kishindo cha mlango wa mbele uliokuwa unabishwa. Nikatazama saa yangu na kuona ilikuwa saa kumi na mbili kasorobo. Nikajiuliza ni nani abishae mlango? Sikupata jibu.
Nikashuka kitandani na kuvaa suruali yangu kisha nikafungua mlango wa chumbani mwangu na kutoka ukumbini. Nilikwenda kwenye mlango wa mbele na kuuliza.
“Nani abishaye?”
“Ni mimi Mgosingwa!” nikaisikia sauti ya Mgosingwa ikisikika kwa nje.
“Ahaa ni wewe!” nikasema huku nikifungua mlango.
JE MGOSINGWA AMEPATA HIZO KUCHA? JIBU UTALIPATA KESHO
Endelea mkuu
 
SEHEMU YA 32


ILIPOISHIA
Mgosingwa alitia mkono kwenye mfuko wa shati lake akatoa ganda kama la kitambulisho akaniwekea mezani.
“hii si leseni yako Mgosingwa?’ akaniuliza.
Nikalichukua lile ganda na kulifungua. Naam. Ilikuwa ni leseni yangu niliyokuwa nimeitupa kule makaburini. Pale pale uso wangu ulibadilika rangi kwa hofu iliyochanganyika na fadhaa. Nikamtazama mgosingwa huku nikijiuliza ameipata wapi leseni yangu.
“Huku nikiendelea na tabasamu langu la kulazimisha nilimuuliza.
“Mgosingwa umeipata wapi hii leseni yangu?’
“Si nimekwambia unatakiwa polisi?”
Jibu lake hilo lilizidi kunichanganya na kunifadhaisha. Midomo yangu niliyokuwa ninailazimisha kutabasamu huku nikiwa na fadhaa ilianza kutatizika na kutetemeka. Sasa haikuweza tena kutabasamu.
“Mgosingwa unanichanganya. Sasa nani kakupa hii leseni na kakupa kwa madhumuni gani?” nikamuuliza huku nikiizuia modomo yangu isitetemeke wakati nikimuuliza hivyo.
Mgosingwa aligundua kuwa nilikuwa nimetaharuki. Akacheka. Hata hivyo kwa vile uso wake ulikuwa umekunjana kutokana na kuendeleza kilevi, kicheko chake hakikuufanya uso wake upendeze, bali ulionekana kama anataka kulia.
“Mgosingwa hukumbuki uliiacha wapi leseni yako?” akaniuliza.
Nikatikisa kichwa.
“Sikumbuki” Nilimjibu hivyo ili nijue ataniambia nini.
“Mgosingwa jana usiku si ulikuja kule makaburi ukafukua lile kaburi nikakukurupusha”
SASA ENDELEA
Aliponiambia hivyo nikanywea na kumtazama. Alipoona nipo kimya aliendelea kunieleza.
“Wakati unakimbia mgosingwa uliiangusha hii leseni yako”
“Kumbe wewe ndiye unayelinda pale?” nikamuuliza.
“Nilipoacha kazi STC niliajiriwa na kanisa kulinda yale makaburi. Sasa jana usiku niliondoka kidogo kwenda kupata ulabu (kilevi), niliporudi nikakuta mtu amechimba kaburi na kuingia ndani. Hii leseni niliiokota asubuhi ndio nikagundua kuwa ulikuwa wewe”
“Sasa Mgosingwa umeshakwenda kutoa ripoti polisi?”
Polisi nimeshakwenda lakini nilipoona hii leseni yako sikuwapa. Niliwambia huyo mtu sikumuona vizuri”
Hapo hapo nilitia mkono mfukoni nakutoa pochi yangu. Niliifungua na kuchomoa noti za shilingi elfu ishirini, nikampa.
“Asante sana Mgosingwa, umenisaidia sana”
SASA ENDELEA
“Tunajuana Mgosingwa , hatuwezi kusalitiana” Mgosingwa aliniambia wakati akipokea zile pesa.
“Unajua lile kaburi ni la shemeji yake mhasibu wetu. Mimi sikujua kabisa”
“Kwani ulikuwa unataka nini Mgosingwa?”
“Kuna kitu nilikuwa nataka”
“Kitu gani?”
Kwanza nilisita kumwambia nilikuwa nataka nini lakini nikaona ni vizuri nimwambie.
“Nilikuwa nataka kucha za maiti”
“Mgosingwa unataka kwenda kuroga au kuua mtu?”
“Hapana. Ni kwa mambo yangu binafsi”
“Mgosingwa ungeniambia, ningekupatia. Mimi Ndio nalinda yale makaburi”
“Bado ninazihitaji Mgosingwa, nifanyie huo mpango”
“Utanipa shilingi ngapi?”
“Ukiniletea hizo kucha nitakuongezea kumi nyingine”
“Fanya ishirini Mgosingwa, kumi ndogo sana”
“Si kitu, nitakupa hizo ishirini”
“Sasa Mgosingwa nitafutie shepe na kiwembe. Niletee pale saa nne usiku. Mimi nitafukua kaburi, asubuhi nitakuletea hizo kucha nyumbani kwako”
“Hakuna tatizo. Nitakuletea hilo shepe. Kiwembe utanunua mwenyewe”
“Sasa Mgosingwa fanya kitu kimoja, nipatie kianzio cha shilingi elfu kumi, hiyo kumi nyingine utanipa asubuhi”
Nilitaka kucheka lakini nilisita kwa sababu tulikuwa katika suala nyeti sana kwa upande wangu.
“Kwanini usisubiri hadi hiyo asubuhi nikupe zote?” nikamuuliza.
“Ninahitaji hiyo pesa kwa sasa”
“Mgosingwa si nimekupa elfu ishirini za bure?”
“Mgosingwa si za bure, polisi ungetoa ngapi ili wakuachie”
“Sawa. Sasa si hizo nimekupa”
“Hazitoshi Mgosingwa”
“Wewe unataka kwenda kulewa tu” nikamwambia huku nikitia mkono kwenye mfuko wa suruali yangu.
Nilitoa pochi yangu nikaifungua na kumpa shilingi elfu kumi alizotaka.
“Umeridhika?” nikamuuliza.
“Hapa Mgosingwa umeniokoa sana”
“Utapata chupa ngapi”
“Acha mzaha Mgosingwa. Mimi siendi kulewa. Mke wangu amekwenda kwao kujifungua. Nilitaka kumtumia hzi pesa”
“Sawa Mgosingwa mtumie, nilikutania tu”
“Sasa Mgosingwa niletee shepe saa nne usiku pale pale”
“Sawa, nitakuletea”
Nikaagana na Mgosingwa na kuondoka.
Nilipotoka kazini jioni nilikwenda kununua shepe jingine nikaenda nalo nyumbani. Nikawa nasubiri saa nne usiku ifike nimpelekee Mgosingwa.
Kwa mara ya kwanza niligundua hata mlevi anaweza kuwa na manufaa yake. Sikutarajia kuwa Mgosingwa mlevu wa gongo na pombe ya mnazi angeweza kunisaidia. Licha ya msaada wa kucha za maiti alioniahidi, kile kitendo chake cha kuiokota leseni yangu na kuja kunipa mwenyewe bila kuipeleka polisi ulikuwa msaada mkubwa kwangu.
Nilimshukuru sana nikijua kama si yeye ningeumbuka. Pengine muda ule ningekuwa niko mahabusi.
Ilipofika saa nne usiku nililifunga lile shepe sehemu ya nyuma ya siti ya pikipiki yangu nikatoka.
Nilikwenda katika lile eneo la makaburi analolinda Mgosingwa. Niliposimamisha tu pikipiki, Mgosingwa akajitokeza. Alitazama kila upande, alipoona kuko kimya akasogea kwenye pikipiki yangu na kunisaidia kulifungua lile shepe.
Ile hewa yake ya mwilini tu ingetosha kumlewesha mtu. Alikuwa akinuka pombe aina ya gongo kama vile alikuwa mtambo wa kuitengenezea. Muda ule tayari alikuwa ameshalewa.
Sikumlaumu. Kulinda makaburi wakati wa usiku ilikuwa kazi ya kutisha. Alihitaji kupata kitu cha kutuliza akili yake, vinginevyo anaweza kuota ndoto za maiti waliozikwa usiku kucha.
Hatukuungumza chochote. Alipochukua lile shepe, alinionesha ishara kuwa tukutane asubuhi akatokomea makaburini.
Nikapanda pikipiki yangu na kuondoka. Nilipofika nyumbani nilifikia kuoga na kulala.
Kulikuwa kunaanza kupambazuka nilipoamshwa usingizini kwa kishindo cha mlango wa mbele uliokuwa unabishwa. Nikatazama saa yangu na kuona ilikuwa saa kumi na mbili kasorobo. Nikajiuliza ni nani abishae mlango? Sikupata jibu.
Nikashuka kitandani na kuvaa suruali yangu kisha nikafungua mlango wa chumbani mwangu na kutoka ukumbini. Nilikwenda kwenye mlango wa mbele na kuuliza.
“Nani abishaye?”
“Ni mimi Mgosingwa!” nikaisikia sauti ya Mgosingwa ikisikika kwa nje.
“Ahaa ni wewe!” nikasema huku nikifungua mlango.
JE MGOSINGWA AMEPATA HIZO KUCHA? JIBU UTALIPATA KESHO
Endelea mkuuu
 
SEHEMU YA 33


ILIPOISHIA
Kwa mara ya kwanza niligundua hata mlevi anaweza kuwa na manufaa yake. Sikutarajia kuwa Mgosingwa mlevu wa gongo na pombe ya mnazi angeweza kunisaidia. Licha ya msaada wa kucha za maiti alioniahidi, kile kitendo chake cha kuiokota leseni yangu na kuja kunipa mwenyewe bila kuipeleka polisi ulikuwa msaada mkubwa kwangu.
Nilimshukuru sana nikijua kama si yeye ningeumbuka. Pengine muda ule ningekuwa niko mahabusi.
Ilipofika saa nne usiku nililifunga lile shepe sehemu ya nyuma ya siti ya pikipiki yangu nikatoka.
Nilikwenda katika lile eneo la makaburi analolinda Mgosingwa. Niliposimamisha tu pikipiki, Mgosingwa akajitokeza. Alitazama kila upande, alipoona kuko kimya akasogea kwenye pikipiki yangu na kunisaidia kulifungua lile shepe.
Ile hewa yake ya mwilini tu ingetosha kumlewesha mtu. Alikuwa akinuka pombe aina ya gongo kama vile alikuwa mtambo wa kuitengenezea. Muda ule tayari alikuwa ameshalewa.
Sikumlaumu. Kulinda makaburi wakati wa usiku ilikuwa kazi ya kutisha. Alihitaji kupata kitu cha kutuliza akili yake, vinginevyo anaweza kuota ndoto za maiti waliozikwa usiku kucha.
Hatukuungumza chochote. Alipochukua lile shepe, alinionesha ishara kuwa tukutane asubuhi akatokomea makaburini.
Nikapanda pikipiki yangu na kuondoka. Nilipofika nyumbani nilifikia kuoga na kulala.
Kulikuwa kunaanza kupambazuka nilipoamshwa usingizini kwa kishindo cha mlango wa mbele uliokuwa unabishwa. Nikatazama saa yangu na kuona ilikuwa saa kumi na mbili kasorobo. Nikajiuliza ni nani abishae mlango? Sikupata jibu.
Nikashuka kitandani na kuvaa suruali yangu kisha nikafungua mlango wa chumbani mwangu na kutoka ukumbini. Nilikwenda kwenye mlango wa mbele na kuuliza.
“Nani abishaye?”
“Ni mimi Mgosingwa!” nikaisikia sauti ya Mgosingwa ikisikika kwa nje.
“Ahaa ni wewe!” nikasema huku nikifungua mlango.
SASA ENDELEA
Nikamuona mgosingwa amesimama mbele ya mlango. Kando ya baraza ya nyumba niliyokuwa naishi kulikuwa na baskeli iliyoegeshwa. Katika kiti chake cha nyuma ilikuwa imefungwa shepe.
“Kumekucha mgosingwa. Habari ya leo?” Mgosingwa akaniambia kwa uchangamfu.
“Nzuri Mgosingwa, je umefanikiwa?”
“Nisifanikiwe kwanini?” akaniuliza huku akitia mkono kwenye mfuko wa shati lake na kutoa kibiriti.
Nilidhani alikuwa anataka kuwasha sigara lakini alipokifungua alikielekeza mbele ya macho yangu. Nikaona alikuwa ameweka kucha nyeupe.
“Ndio hizo Mgosingwa?” nikamuuliza.
“Si ulitaka kucha za maiti?”
“Ndiyo”
“Ndio hizo nimekuletea”
“Ulifukua kaburi?”
“Kulikuwa na kaburi moja la maiti iliyozikwa jana, nililifukua usiku nikaikata kucha ile maiti kisha nikalifukia kama nilivyolikuta. Kucha zenyewe ndio hizo”
Nilizitazama vizuri zile kucha alizoziweka ndani ya kibiriti kisha nikakifunga.
“Asante sana Mgosingwa” nikamwambia Mgosingwa kisha nikamtazama.
“Mgosingwa fanya basi hayo makwarukwaru” Mgosingwa akaniambia huku akinitazama kwa jicho la tamaa.
Makwarukwaru ni lugha ya mitaani. Mgosingwa alikuwa akimaanisha nimpe pesa.
“Makwarukwaru yapi Mgosingwa?”
“Si tuliongea jana, nikikuletea hizo kucha utanipa shilingi elfu ishirini”
“Mgosingwa si nilikupa kumi?’
“Ndio, ikabaki kumi”
Nikatia mkono kwenye mfuko wa suruali yangu na kutoa noti za shilingi elfu kumi nikampa.
“Asante Mgosingwa, wewe hata kama utataka mguu wa maiti niambie nitakupatia”
“Sawa bwana”
Mgosingwa akachukua baskeli yake na kuniaga. Na mimi nikarudi ndani.
Nilipoingia ndani nilikwenda kuoga nikavaa na kutoka na pikipiki yangu. Nikaenda kwa yule mganga wa kipemba. Kwa vile ilikuwa bado mapema nilisubiri nje ya gesti hadi mlango wa gesti ulipofunguliwa, nikaingia.
Nilibisha mlango wa chumba cha mganga. Baada ya muda kidogo mlango ulifunguliwa. Mganga aliponiona tu akanikumbuka.
“Oh karibu, wewe si ndiye yule jamaa uliyekuja juzi?” akaniuliza.
“Ndiye mimi”
“Karibu ndani”
Alinipisha kwenye mlango nikaingia mle chumbani.
“Kaa kwenye kiti” akaniambia na kuongeza.
“Bahati yako umenikuta, leo ndio siku yangu ya kuondoka. Naenda Arusha. Nilikutazamia jana sikukuona”
“Jana sikufanikia kupata zile kucha”
“Sasa leo umezipata?”
“Nimezipata”
“Ni kucha za maiti khaswa?”
“Ni kucha za maiti. Kuna mtu alifukua kaburi jana usiku akamkata kucha maiti”
Nilitia mkono kwenye mfuko wangu wa shati nilikoweka kile kibiriti alichonipa mgosingwa.
“Kama umezipata hizo kucha nitaahirisha safari yangu ili nikufanyie kazi yako” Mganga alinaimbia.
Nilikitoa kile kibiriti.
“Ni hizi hapa” nikamwambia na kukifungua kile kibiriti na kumuonesha.
“Ziko wapi. Mbona sioni kitu” Mganga akaniuliza.
Nikashituka na kuangalia ndani ya kile kibiriti.
Hamkuwa na kitu. Kibiriti kilikuwa kitupu kama mkono uliorambwa!
Mbali ya kukichomoa kabisa kwenye ganda lake sikuona chochote.
“Jamani zile kucha zimekwenda wapi?” nikajiuliza kwa mshangao.
“Ulikuwa umezitia humu?” Mganga akaniuliza.
“Ndio, nilizitia humu. Wakati naondoka nyumbani zilikuwamo!”
“Sasa zimekwenda wapi?”
“Sijui”
“Au umezimwaga bila kujua?’
“Sijazimwaga. Nilipoondoka nyumbani kucha zilikuwemo. Nikakitia hiki kibiriti mfukoni na sijakitoa mpaka muda huu”
“Basi itakuwa ni miujiza”
“Sasa miujiza hii inatokea wapi?”
Mganga akawa anafungasha vitu vyake kwenye begi lake alilokuwa ameliweka kitandani. Niliona kama amenipuuza.
“Sasa miujiza hii imetokea wapi?’ nikamuuliza tena.
“Hilo jini limekutawala sana, itakuwa vigumu kuliepuka” Mganga akaniambia huku akiendelea kupanga nguo zake.
“Limenitawala kivipi?’
“Wauliza jibu, wewe huoni mambo yako yanakwenda ovyo unadhani ni kwa sababu ya nini?’
Sikumpinga, mambo yangu yanaenda ovyo kweli.
“Ndio sababu hizi kucha zimepotea?” nikamuuliza.
Mganga hakunijibu. Badala yake aliniambia.
“Kazi kama hizo sizitaki kabisa, zitaniletea nuksi bure”
“Wewe ndiye mtaalamu nilitegemea kuwa utanisaidia”
“Sitaweza kukusaidia, naomba uende zako. Nina safari ya arusha nisije nikachelewa gari” Mganga aliniambia akionesha wazi kukasirika.
Sikuwa na jingine isipokuwa kuinuka kwenye kiti. Nikamuga na kuondoka zangu. Nilivyomuaga hata hakunijibu kitu. Sijui nilimkosea nini. Alikuwa amehamaki mara moja.
Wakati natoka mle chumbani yale maneno yake kwamba hilo jini limenitawala sana na kwamba itakuwa vigumu kuliepuka, yalikuwa yakinirudia akilini mwangu.
Kusema kweli niliondoka pale gesti nikiwa na fadhaa sana. Nilipanda pikipiki yangu. Sikutaka kwenda kwa kaka ingawa hapakuwa mbali na pale gesti, nikaenda kazini kwangu.
Nilifanya kazi huku nikiwaza jinsi zile kucha zilivyopotea kwenye kibiriti. Kwa kuzingatia maneno ya yule mganga iliwezekana kwamba zile kucha zilipotezwa na Zainush.
Lakini kubwa ambalo lilinitia fadhaa ni yale maneno ya yule mganga kwamba hilo jini limenitawala sana na itakuwa vigumu kuliepuka.
Kama mganga wa majini amesema hivyo, je juhudi zangu za kumuondoa zainush zitafanikiwa kweli, nikajiuliza kwa fadhaa.
Mganga mwenyewe amenifukuza, nikaendelea kuwaza, bila shaka na yeye alikuwa amepata hofu baada ya kuona jinsi zile kucha zilivyotoweka kwenye kibiriti.
“Una nini leo Amour?” Wafanya kai wenzangu walikuwa wakiniuliza.
“Nikoje?’
ENDELEA KUFWATILIA MKASA HUU
 
SEHEMU YA 34


ILIPOISHIA
Wakati natoka mle chumbani yale maneno yake kwamba hilo jini limenitawala sana na kwamba itakuwa vigumu kuliepuka, yalikuwa yakinirudia akilini mwangu.
Kusema kweli niliondoka pale gesti nikiwa na fadhaa sana. Nilipanda pikipiki yangu. Sikutaka kwenda kwa kaka ingawa hapakuwa mbali na pale gesti, nikaenda kazini kwangu.
Nilifanya kazi huku nikiwaza jinsi zile kucha zilivyopotea kwenye kibiriti. Kwa kuzingatia maneno ya yule mganga iliwezekana kwamba zile kucha zilipotezwa na Zainush.
Lakini kubwa ambalo lilinitia fadhaa ni yale maneno ya yule mganga kwamba hilo jini limenitawala sana na itakuwa vigumu kuliepuka.
Kama mganga wa majini amesema hivyo, je juhudi zangu za kumuondoa zainush zitafanikiwa kweli, nikajiuliza kwa fadhaa.
Mganga mwenyewe amenifukuza, nikaendelea kuwaza, bila shaka na yeye alikuwa amepata hofu baada ya kuona jinsi zile kucha zilivyotoweka kwenye kibiriti.
“Una nini leo Amour?” Wafanya kai wenzangu walikuwa wakiniuliza.
“Nikoje?’
SASA ENDELE
“Leo unaonekana una mawazo sana” Mfanyakazi mmoja akaniambia.
“Kawaida tu”
“Tuambie kama kuna kitu kimekukwaza”
“Kwa hapa kazini?”
“Popote tu”
“Hakuna kitu. Binaadamu kuwaza ni kawaida”
“Mwenzetu leo umezidi sana”
“Basi nitapunguza” nikasema kwa utani kisha nikacheka ili kukatisha yale mazungumzo yake.
Nilipomwambia hivyo naye akacheka, akaniambia.
“Sawa bwana”
Maneno yakaishia hapo hapo. Sikujua kama wafanyakazi wenzangu walikuwa wananiona nilikuwa na mawazo. Baada ya hapo nikajitia kufanya kazi ili nionekane wa kawaida. Sikutaka mtu yeyote ajue lililokuwa moyoni mwangu.
Jioni nilipotoka kazini nikaenda Chuda kwa kaka. Nilimueleza juhudi nilizozifanya jana yake hadi nikafanikiwa kupata zile kucha na hatimaye zikatoweka zikiwa ndani ya kibiriti wakati nikiwa kwa yule mganga.
“Mganga alipata hasira akanifukuza. Aliniambia niondoke na kwamba yule jini ameshanitawala, itakuwa vigumu kumuondoa” nikamwambia.
“Sasa kwanini alikufukuza?’
“Sijui”
“Na hizo kucha zilitoweka vipi?’
“Sijui. Mgosingwa aliniletea asubuhi zikiwa ndani ya kibiriti. Sasa nafika kwa mganga nafungua kibiriti, kucha hazimo!”
“Na wewe ulihakikisha ulipopewa hicho kibiriti kucha zilikuwemo?”
“Ndio. Mgosingwa aliponipa hicho kibiriti alinifungulia akanionesha. Kucha zilikuwemo”
“Mganga alikwambia hizo kucha zimnmekwenda wapi?’
“Aliniambia huyo jini ndiye anayeniharibia mambo yangu”
“Kwa hiyo huyo jini ndiye aliyezipoteza?’
“Itakuwa ni yeye”
Kaka alifikiri kisha akaniuliza.
“Hizo kucha zilikuwa ndogo sana?”
“Ndio zilikuwa ndogo”
“Inawezekana zilichomoka moja moja kwenye kibiriti bila wewe kujua. Siamini kwamba huyo jini amezichukua yeye”
“Unafikiria hivyo?’
“Acha wasiwasi. Kwanza huyo jini kuna muda mrefu hajakutokea. Mimi nafikiri ameshakata tamaa”
“Sawa kaka, nimekuelewa”
Sikuwa na uhakika kwamba kaka alikuwa akiniambia ukweli kutoka ndani ya moyo wake au alikuwa akinituliza tu.
Baada ya mazungumzo yetu mafupi nikamuaga na kuondoka.
Baada ya wiki moja kaka yangu aliniita na kunishauri nioe.
“Umeshakuwa mkubwa sasa, unatakiwa uwe na mke wako” aliniambia.
“Ni kweli kaka. Haya mambo ya huyu jini aliyekuwa akiniandama ndio yaliyonizubaisha”
“Mimi naamini akikuona una mke hatakufuata tena. Atakwenda kutafuta mtu mwingine. Kama atakubali, awe mke mwenza” Kaka akanichekesha.
Tukacheka sote.
“Nadhani hawezi kukubali kuwa mke mwenza” nikamwambia.
“Ndio atakuacha sasa”
“Ni kweli kaka, ni bora niwe na mke”
“Sasa unaye msichana unayemfikiria kwamba anafaa kuwa mke wako ili tukakuposee”
“Nitakujibu”
“Lini?”
“Nipe siku mbili tu”
“Sawa”
Lile wazo la kuoa alilonipa kaka nilikwenda kulitafakari nyumbani na kuona lilikuwa wazo la busara sana. Mbali ya kwamba nilishafikia umriwa kuwa na mke pia niliona nitakuwa na mwenzangu wa kunifariji kutokana na matatizo yaliyokuwa yananikabili.
Pia nilizingatia kauli ya kaka kwamba nikioa, huenda yule jini akaacha kuniandama.
Kulikuwa na msichana mmoja aliyekuwa akiishi mtaa wa pili na ule niliokuwa nikiishi mimi. Alikuwa akiitwa Salma.
Salama nilikuwa nikimfahamu tangu alipokuwa anasoma shule ya sekondari ya Usagara. Alipomaliza kidato cha nne niliwahi kumtamkia kuwa ninampenda.
Akaniuliza. “Unanipenda kweli au unanidanganya?’
“Ninakupenda kweli” nikamjibu.
“Sasa kama unanipenda kweli, waone wazazi wangu. Mimi nimeshakukubalia”
Kwa vile muda ule sikuwa na mawazo ya kuoa, sikumpatiliza tena ila kila tulipoonana nilimtania kwa kumwambia, “Nitakuja kwa wazazi wako”
Na yeye hucheka na kunijibu. “Njoo tu, njia nyeupe”
Alikuwa mzuri mwenye heshima na alikuwa na sifa zote zinazostahili kuwa mke wangu.
Yeye ndiye niliyemfikiria.
Hata hivyo wakati ule wazazi wake walikuwa wameshahama katika mtaa waliokuwa wakiishi. Mwenyewe aliniambia walihamia Chumbageni.
Kwa wakati ule Salama alikuwa akifanya kazi Shirika la Posta. Nikapanga nimfuate nizungumze naye ili nimueleze nia yangu ya kupeleka posa yangu kwa wazazi wake.
Siku iliyofuata nikaenda kazini. Saa nne wakati wa kwenda kunywa chai nikaenda posta. Nikamkuta.
Nilisubiri watu wawili aliokuwa akiwahudumia walipoondoka nikamsalimia.
“Hujambo mrembo?”
“Sijambo, sijui wewe”
“Mimi ni mzima tu kama unavyoniona, hivi kule Chumbageni unaishi mtaa gani?” nikamuuliza.
Salama akanielekeza mtaa anaoishi. Kwa vile na mimi nilikuwa mwenyeji wa mitaa ya Chumbageni niliifahamu mpaka nyumba waliyokuwa wanaishi.
“Si ile inayotazamana na Cumbageni Guest House?” nikamuuliza.
“Ndiyo hiyo hiyo”
“Natarajia kutuma mshenga kwenu” nikamdokeza.
Salama hakunijibu kitu. Nikaridhika. Kuwa kimya inachukuliwa na masheikh wa kiislamu kuwa ni ishara ya kukubali, kwa vile suala hilo tulishalizungumza.
Nilipotoka kazini jioni nilikwenda kwa kaka nikamueleza kuhusu msichana huyo.
“Umeshazungumza naye” akaniuliza.
“Niliwahi kuzungumza naye siku nyingi lakini ilikuwa kama mzaha, leo ndio nilimfuta kazini kwake nikamwambia kuwa nitatuma mshenga kwao akanyamaza. Nimechukulia ishara kwamba amekubali”
“Sasa tujaribu kupeleka ujumbe kwao?”
“Ndio hivyo”
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 35

ILIPOISHIA
Kwa wakati ule Salama alikuwa akifanya kazi Shirika la Posta. Nikapanga nimfuate nizungumze naye ili nimueleze nia yangu ya kupeleka posa yangu kwa wazazi wake.
Siku iliyofuata nikaenda kazini. Saa nne wakati wa kwenda kunywa chai nikaenda posta. Nikamkuta.
Nilisubiri watu wawili aliokuwa akiwahudumia walipoondoka nikamsalimia.
“Hujambo mrembo?”
“Sijambo, sijui wewe”
“Mimi ni mzima tu kama unavyoniona, hivi kule Chumbageni unaishi mtaa gani?” nikamuuliza.
Salama akanielekeza mtaa anaoishi. Kwa vile na mimi nilikuwa mwenyeji wa mitaa ya Chumbageni niliifahamu mpaka nyumba waliyokuwa wanaishi.
“Si ile inayotazamana na Cumbageni Guest House?” nikamuuliza.
“Ndiyo hiyo hiyo”
“Natarajia kutuma mshenga kwenu” nikamdokeza.
Salama hakunijibu kitu. Nikaridhika. Kuwa kimya inachukuliwa na masheikh wa kiislamu kuwa ni ishara ya kukubali, kwa vile suala hilo tulishalizungumza.
Nilipotoka kazini jioni nilikwenda kwa kaka nikamueleza kuhusu msichana huyo.
“Umeshazungumza naye” akaniuliza.
“Niliwahi kuzungumza naye siku nyingi lakini ilikuwa kama mzaha, leo ndio nilimfuta kazini kwake nikamwambia kuwa nitatuma mshenga kwao akanyamaza. Nimechukulia ishara kwamba amekubali”
“Sasa tujaribu kupeleka ujumbe kwao?”
“Ndio hivyo”
SASA ENDELEA
“Kwa hiyo utaandika barua utaniletea hapa, halafu mimi nitatafuta mzee mmoja niende naye. Unasema anaishi wapi?’
“Anaishi chumbageni lakini usiku tutakwenda kama tunapita njia ili nikuoneshe nyumba yao”
“Sawa, utanifuata saa ngapi?’
“Saa mbili usiku”
“Nitakusubiri”
Baada ya mazungumzo yetu na kaka nikarudi nyumbani. Saa mbili usiku nikamfuata tena na pikipiki yangu. Nilimpakia na kwenda kumuonesha ile nyumba aliyonielekeza Salama. Nilipata uhakika kwamba sikuikosea kwani tulimkuta baba yake ambaye namfahamu, ameketi barazani kwenye kiti cha uvivu akivuta mtemba wake.
Tukapita na pikipiki yetu.
Wakati tunarudi kaka alinaimabia.
“Kama nyumba ni ile nimeshaiona”
“Na yule mtu uliyemuona ameketi barazani kwenye kiti cha uvivu ni baba yake”
“Kumbe baba yake ni yule mzee?”
“Ndio yule”
“Basi tutamuona hapo kesho”
Nikamrudisha kaka nyumbani kwake, akanisisitizia tu nisisahau kuandika barua ya posa.
Nilipofika nyumbani niliiandika barua hiyo usiku ule ule nikaitia ndani ya bahasha. Kwa kawaida barua za posa kama zile huwekwa kitu kidogo. Nikatia shilingi elfu hamsini.
Asubuhi wakati naenda kazini nikaipeleka ile barua kwa kaka. Kaka aliifungua kwa vile sikuwa nimeifunga kabisa. Aliisoma kisha akaniambia.
“Umeiandika vizuri”
“Nimeweka na shilingi elfu hamsini, sijui zinatosha”
“Zinatosha, hizi huwekwa kama ada tu”
“Sawa, sasa mimi naenda kazini utatafuta mtu wa kwenda naye”
“Barua yako itafika leo leo”
Nikaenda zangu kazini.
Saa nne nikaenda posta kwa Salama. Baada ya kusalimiana naye nilimwambia.
“Ujumbe wangu utaupata leo”
Salama akatabasamu.
“Naungojea” akaniambia. Nilikuwa na hakika kwamba alijua ni mzaha wangu.
Jioni nilipotoka kazini nilikwenda kwa kaka. Akaniambia.
“Barua yako imefika”
“Umeshaipeleka?” nikamuuliza kwa tashiwishi.
“Tuliipeleka mchana. Mzee ameniambia nifuatie majibu kesho”
“Hakukuwa na maswali yoyote aliyokuuliza?”
“Kuuliza ni lazima. Aliniuliza ile posa ilikuwa ni ya nani wangu. Nikamjibu ni ya mdogo wangu. Akaniuliza anafanya kazi wapi nikamueleza. Akataka pia kujua unaishi wapi nikamueleza”
“Yule mzee hatufahamiani isipokuwa nafahamiana na binti yake”
“Aliuliza pia kama wewe ulishamueleza binti yake kuhusu nia yako”
“Ukamjibu nini?”
“Nilimwambia mlishazungumza na mlikubaliana. Akaniambia kwamba atazungumza naye na kwamba nifuatie majibu kesho”
“Kwa hiyo mtaenda tena hapo kesho?”
“Tutakwenda”
“Sawa kaka”
Jioni yake niliporudi kazini nikapitia kwa kaka kupata majibu.
Akaniambia. “Kazi imekamilika”
“Kivipi?” nikamuuliza.
“Posa yetu imekubaliwa. Mzee ameniambia wanataka mahari ya shilingi laki tano”
“Mahari yake ni shilingi laki tano?” nikamuuliza kwa mkazo.
“Inaelekea yule mzee msomi. Amesemi yeye hana mambo ya Kiswahili. Hakutaka kututajia gharama kubwa. Mimi naona laki tano si nyingi”
“Sawa”
“Mimi mchango wangu nitakusaidia shilingi laki moja”
“Mimi mwenyewe nitatoa laki nne”
“Lini zitapatikana hizo laki nne”
“Hata kesho zinaweza kupatikana”
“Utaniletea asubuhi?”
“Nitakuletea jioni, wewe utazipeleka kesho kutwa”
“Sasa tupange harusi, sipendi uchumba wenu uchukue muda mrefu sana”
“Tukishalipa hizo pesa tutakaa na mama tupange harusi itakavyokuwa”
“Sawa jitahidi upate jiko lako”
“Nitajitahidi kaka”
Nikaagana na kaka na kwenda nyumbani kwa mama. Nilimueleza ile habari. Akaniambia ameshaelezwa na mwanawe, yaani kaka yangu.
“Ni jambo zuri” akasema.
“Kesho kutwa tutakuja kufanya kikao cha harusi hapa kwako”
“Kwani mambo tayari?’
“kaka atapeleka mahari kesho kutwa”
“Hizo shilingi laki tano?”
“Ndio”
“Umeshampa?”
“Nimemwambia nitampa kesho”
“Yeye atakusaidia shilingi ngapi?’
“Ameniambia atanitolea shilingi laki moja, mimi mwenyewe nitatoa laki nne”
“Kwa hiyo mnasubiri mmpeleke mahari ndio tufanye kikao”
“Ndiyo”
“Mimi nawaunga mkono. Nilitaka sana wewe uwe na mke. Hilo wazo nililitoa mimi”
“Lilikuwa wazo zuri na natumaini nikiwa na mke matatizo yangu yatapungua’
“Utakuwa vizuri mwanangu”
“Sawa mama, basi mimi narudi nyumbani”
Nikaagana na mama na kuondoka.
ITAENDELEA...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom