Simulizi ya kweli: Mwanamke jini

Simulizi ya kweli: Mwanamke jini

SEHEMU YA 36


ILIPOISHIA
Nikaagana na kaka na kwenda nyumbani kwa mama. Nilimueleza ile habari. Akaniambia ameshaelezwa na mwanawe, yaani kaka yangu.
“Ni jambo zuri” akasema.
“Kesho kutwa tutakuja kufanya kikao cha harusi hapa kwako”
“Kwani mambo tayari?’
“kaka atapeleka mahari kesho kutwa”
“Hizo shilingi laki tano?”
“Ndio”
“Umeshampa?”
“Nimemwambia nitampa kesho”
“Yeye atakusaidia shilingi ngapi?’
“Ameniambia atanitolea shilingi laki moja, mimi mwenyewe nitatoa laki nne”
“Kwa hiyo mnasubiri mmpeleke mahari ndio tufanye kikao”
“Ndiyo”
“Mimi nawaunga mkono. Nilitaka sana wewe uwe na mke. Hilo wazo nililitoa mimi”
“Lilikuwa wazo zuri na natumaini nikiwa na mke matatizo yangu yatapungua’
“Utakuwa vizuri mwanangu”
“Sawa mama, basi mimi narudi nyumbani”
Nikaagana na mama na kuondoka.
SASA ENDELEA
Siku iliyofuata nilikwenda benki, nikatoa shilingi laki tano kutoka katika akaunti yangu. Jioni nilipotoka kazini nikampelekea kaka shilingi laki nne kama tulivyokubaliana.
Nilipotoka kwa kaka nikaenda kwa mama. Nikamueleza kuwa nimeshampa kaka shilingi laki nne.
Mama akafurahi.
“Nawatakia heri na mafanikio” akaniambia na kuniuliza.
“Zitapelekwa kesho?”
“Kaka ameniambia atazipeleka kesho na kesho hiyo hiyo tutakuwa na kikao hapa kwako”
“Saa ngapi?’
“Nadhani itakuwa usiku”
“Sawa wanangu, nawasubiri”
Siku iliyofuata ilikuwa jumapili, sikwenda kazini. Nilibaki nyumbani kufanya usafi na kufua nguo zangu zilizochafuka.
Saa saba ndipo nilipotoka. Nilikwenda kwenye mkahawa mmoja kula chakula. Nilipotoka hapo nikaenda kwa kaka. Aliniambia ndio kwanza amerudi kutoka chumbageni.
“Mzee ameniambia baada ya kupata mahari anachosubiri ni kutajiwa siku ya harusi” kaka akaniambia.
“Sasa tujiandae, tupeleke siku”
“Kwani tutakutana saa ngapi kwa mama?’
“Nimemwambia tutakutana usiku”
“Usiku saa ngapi?’
“Tukutane kuanzia saa moja”
“Sawa”
“Naona mambo yanakwenda vizuri”
“Yanakwenda vizuri sana”
Saa mbili usiku tulikutna nyumbani kwa mama. Mimi nilifika mapema zaidi kabla ya kaka. Ilibidi niwahi kwa sababu mimi ndiye niliyekuwa na shughuli, ilikuwa vyema mwenzangu anikute pale nyumbani na sio nimkute yeye.
Kaka alipofika tukaanza mazungumzo. Mazungumzo yetu yalikuwa marefu na yaliishia saa nne usiku. Tulipanga kila
kitu. Kwa vile mimi nilikuwa na akiba yangu ambayo nilipanga niitumie kwa ajili ya harusi yangu, tulikubaliana kwamba harusi ifanyike haraka, baada ya wiki mbili.
“Hizi wiki mbili ndio za kufanya maandalizi, mnaonaje zinatosha au tuongeze siku?” kaka alituuliza wakati tunaendelea na kikao chetu.
Nikamtazama mama, nikaona mama naye ananitazama mimi.
“Mimi naona zinatosha, hakuna haja ya kuongeza siku zaidi” nikasema.
“Mama unasemaje?” Kaka akamuuliza mama aliyekuwa kimya.
“Mimi sina usemi, nawasikiliza nyinyi”
“Na wewe unaafiki kwamba wiki mbili zinatosha kwa maandalizi?” Kaka akamuuliza.
“Kama Amour mwenyewe amesema zinatosha na mimi nasema hivyo hivyo zinatosha”
“Sawa. Naona tumeafikiana kwa hilo. Sasa tupange siku yenyewe ya kufunga ndoa” kaka akatuambia.
“Tuweke siku ya ijumaa baada ya mshuko. Muda huo ni mzursana kufunga ndoa” nikasema.
“Mimi pia naafikiana na muda huo. Kwa hiyo hatuhitaji kwenda kutazamia siku wala saa?’
“Enzi zetu tulikuwa tunatazamia siku lakini siku hizi mambo yamebadilika” mama akasema.
“Mama unajua kutazamia siku ni kuleta ushirikina. Siku zote zinafaa kuoa na saa zote mtu unaweza kuoa. Mtume ametuambia saa nzuri ni baada ya mshuko wa ijumaa” nikamwambia mama.
“Swadakta Amour, umesema sawa. Umekuwa answar sunna” Kaka akanikubalia.
“Si lazima niwe answaar sunna. Hivi ndivyo tulivyofundishwa na mtume wetu. Kufanya vinginevyo ni ushirikina”
“Wanasema kwamba usipotazamia siku unaweza kuoa siku mbaya na maisha yako ya ndoa yakawa ya mikosi na vifo” kaka akayuambia.
“Uongo mtupu. Ni imani tu za watu” nikasema.
“Sawa. Tumeshakubaliana kwamba ndoa itafanyika baada ya mshuko wa ijumaa. Kutahitajika tende kidogo na kahawa au siyo”
“Ndiyo”
“Ndoa itafanyika wapi?”
“Msikiti wa ijumaa”
“Msikiti ule ni mkubwa, siku za ijumaa unakuwa na watu wengi, haluwa haitatosha. Tuchague msikiti mwingine” kaka akashauri.
“Basi tutatafuta msikiti mwingine kule kule Chumbageni”
“Hilo tumelimaza. Sasa tayarisha kadi mapema uzitoe kwa wafanyakazi na rafiki zako. Na mimi nitachukua kiasi. Baada ya wiki moja tukutane tena tuone tumepata kiasi gain”
“Sawa kaka”
Tulimaliza mazungumzo yetu. Nikampakia kaka kwenye pikipiki yake kumrudisha nyumbani kwake. Na mimi nikarudi nyumbani kwangu.
Usiku wa siku ile ndoto zangu zote zilikuwa za harusi. Niliota ninamuoa Salma aliyekuwa akingara kama mwezi. Ingawa mwenyewe nilipanga kumuoa mchana, niliota ninamuoa usiku wa manane.
Ndoa yenyewe ilifanyika kwenye kisiwa kisicho na watu. Tulikuwa mimi na yeye na muozeshaji wetu..
Baada ya kuota ninaona na salama nikaota Salama amepata mtoto wa kiume, mzuri ajabu.
Nilipoamka asubuhi na kiondoka nyumbani nilikwenda kazini kwangu. Siku ile ile nikashughulikia mpango wa kuchapisha kadi za harusi ambazo nilizipata siku ile ile.
Wakati tunatoka kazini jioni nilimkabidhi kiasi kikubwa cha kadi msichana mmoja ambaye ni mfanya kazi mwenzangu ili anichangie kwa marafiki zake na kwa wafanyakazi wenzetu. Nikawataarifu baadhi ya wafanyakazi wenzangu kuhusu ndoa yangu.
Nilipotoka kazini nilikwenda nyumbani kwa kaka. Naye nikampa kiasi cha kadi ili azigawe kwa marafiki zake.
Mimi mwenyewe nilibaki na kiasi kidogo cha kadi hizo kwa ajili ya kuwagaia marafiki zangu.
Nilishukuru kwa jinsi nilivyoungwa mkono. Kadi zote ziligaiwa kwa watu na kila aliyepewa kadi aliahidi kunichangia baada ya wiki moja.
Kweli, baada ya wiki moja nilipata mchango wa kutosha sana ambao ulinipa matumaini kuwa ndoa yangu itafanikiwa. Ile wiki tuliyopanga nifunge ndoa, kaka alipeleka taarifa ukweni kuwa ndoa itafanyika siku ya ijumaa. Tulikuwa tumewapa siku saba tu za maandalizi lakini walikubaliana na sisi.
Naam siku ikawadia. Niliwekwa ndani kama mwari, nikasingwa kwa msio na mafuta ya nazi. Walionisinga walikuwa ni binamu zangu. Ilikuwa raha asana.
Ndoa ilifungwa katika msikiti mmoja uliokuwa maeneo ya Chumbageni.
Nakumbuka hadi leo jinsi sheikh mmoja alivyonifungisha ile ndoa.
Aliniita jina langu kisha akaniambia nimuitikie “Labaika”
“Labaika” nikamuitikia.
Akaniita tena.
“Amour Amrani”
“Labaika” nikamuitikia.
“Ninakuozesha Salama binti Riyami kwa mahari mliyokubaliana, umekubali?”
“Ndiyo” nikamuitikia huku midomo yangu ikitetemeka. Sikujua ilitetemeka kwa sababu gani.
“Hapana. Hilo silo jibu linalotakiwa ujibu. Unatakiwa useme nimekubali kumuoa Salama binti Riyami kwa mahari tuliyokubaliana”
“Sawa”
“Amour binti Amraani” Sheikh akaniita tena.
“Labaika”
“Ninakuozesha Salama binti Riyami kwa mahari mliyokubaliana, umekubali?”
Nikayakumbuka yale maneno aliyonifundisha.
“Nimekubali kumuoa Salama binti Riyami kwa mahari tuliyokubaliana” nikajibu.
Sheikh alirudia tena kuniambia hivyo mara tatu na mimi nilijibu mara tatu. Baada ya hapo ikasomwa hutuba ya ndoa iliyochukua karibu nusu saa.
JE NINI KITATOKEA?
ENDELEA KUFWATILIA MKASA HUU WA KUSISIMUA
 
SEHEMU YA 37


ILIPOISHIA
Nakumbuka hadi leo jinsi sheikh mmoja alivyonifungisha ile ndoa.
Aliniita jina langu kisha akaniambia nimuitikie “Labaika”
“Labaika” nikamuitikia.
Akaniita tena.
“Amour Amrani”
“Labaika” nikamuitikia.
“Ninakuozesha Salama binti Riyami kwa mahari mliyokubaliana, umekubali?”
“Ndiyo” nikamuitikia huku midomo yangu ikitetemeka. Sikujua ilitetemeka kwa sababu gani.
“Hapana. Hilo silo jibu linalotakiwa ujibu. Unatakiwa useme nimekubali kumuoa Salama binti Riyami kwa mahari tuliyokubaliana”
“Sawa”
“Amour binti Amraani” Sheikh akaniita tena.
“Labaika”
“Ninakuozesha Salama binti Riyami kwa mahari mliyokubaliana, umekubali?”
Nikayakumbuka yale maneno aliyonifundisha.
“Nimekubali kumuoa Salama binti Riyami kwa mahari tuliyokubaliana” nikajibu.
Sheikh alirudia tena kuniambia hivyo mara tatu na mimi nilijibu mara tatu. Baada ya hapo ikasomwa hutuba ya ndoa iliyochukua karibu nusu saa.
SASA ENDELEA
Baada ya ndoa kufungwa nilipewa mawaidha. Niliambiwa siku ile nimeoana na Salama kwa wema, kwa hiyo niishi naye kwa wema na kumpa huduma zote zinazopaswa kutolewa kwa mke.
Sheikh aliendelea kuniambia kuwa kama itabidi kuachana, pia tuachane kwa wema kwani hivyo ndivyo ambavyo tumeusiwa na mtume wetu.
Baada ya hapo halua na tende pamoja na visheti ziikagaiwa. Watu wakala na kufurahi.
Baada ya shughuli kumalizika tukaenda nyumbani kwa mke. Nilikuwa nimekodi magari matano. Tulipofika tulikuta shamra shamra zikiendelea. Tuliingia chumbani kwa mke wangu aliyekuwa amepambwa vilivyo.
Nikampa mkono. Hapo hapo sheikh akatuombea dua na kututakia afya njema na maisha mema ya ndoa. Tulipiga picha za kumbukumbu zikiwemo za mnato na za video.
Ikafuatia pilau. Mimi na mke wangu tuliletewa sahani ya pamoja na jagi la juisi.
Tulishindwa kula sana kwa sababu ya zile hekaheka. Si unajua siku ya ndoa mtu unapata fadhaa kidogo.
Baada ya shughuli zote kumalizika, mtu aliyekuwa amesimamia ndoa upande wangu alitaka tuondoke. Wenyeji wetu wakapinga na kutaka tuendelee kuwepo kwa vile sherehe ilikuwa ikiendelea.
“Hapana, sisi hatukufuata sherehe hapa. Tumekuja kuoa” Msimamizi wangu alisema.
“Na ndoa ni sherehe, kama mtaondoka mapema hakutakuwa na sherehe tena” alijibiwa na msemaji wa upande wa mke wangu.
“Tatizo ni nini? Kama tumeshaoa tunachukua mke wetu tunaondoka” Msimamizi wangu akachachamaa.
“Msiondoke jamani, sherehe bado zinaendelea. Mkiondoka nyinyi mtatukatisha”
Msimamizi wangu akanishika mkono na kuniinua.
“Sisi tunaondoka. Nyinyi endeleeni na sherehe zenu. Na sisi huko tuna sherehe zetu”
Tukatoka.
“Jamani mnaondoka!” Wenyeji wetu wakalalamika.
“Waswahili bwana, wanataka tuendelee kukaa hapa, tufanye nini? Kwani sisi hatuna kwetu?” Msimamizi wangu alisikika akisema peke yake.
Tulitoka nje, gari zilikuwa zikitusubiri. Tukajipakia. Mimi nilipanda gari moja na mke wangu pamoja na wapambe wetu.
Gari nyingine mbili zikapanda watu wengine.
Tukaelekea Msambweni ilikokuwa nyumba yangu.
Nyumbani kwangu pia kulikuwa na sherehe. Tulipokewa kwa vifijo na hoihoi. Tulipoingia chumbani. Wapambe wetu wakatuacha.
Sherehe ziliendelea hadi saa sita usiku. Sisi tulikuwa chumbani tumelala.
Nilikuwa nimeomba ruhusa ya siku tatu kazini kwangu. Kwa hiyo nilikaa siku tatu bila kwenda kazini. Katika siku hizo tatu sikuchezea mbali. Muda wote nilikuwa chumbani na mke wangu Salma. Mara chache nilitoka peke yangu na kukaa sebuleni.
Baada ya siku hizo tatu kwisha nilikwenda kazini. Huko nilipata pongezi nyingi sana kwa kupata jiko (kuoa).
Sasa nikawa nimefungua ukurasa mpya wa maisha yangu. Siku za mwanzo mwanzo nilipotoka kazini tu nilirudi nyumbani haraka. Siku za jumapili sikuondoka nyumbani.
Ile tabia ya kula kwenye mikahawa ikaisha, nikawa nakula nyumbani tena chakula kizuri kilichopikwa na laazizi wangu. Naam. Maisha yalikuwa matamu sana!
Ilikuwa imepita miezi mitatu. Usiku mmoja wakati tumelala na Salma, Salama alianza kuweweseka akiwa
usingizini. Nilimuamsha na kumuuliza alikuwa na nini, akaniambia alikuwa anaota kuna msichana mmoja anamuamrisha aondoke pale nyumbani.
“Ananiambia hapa si kwangu, ni kwake yeye” Salma aliniambia.
Nikashituka na kumuuliza.
“Huyo msichana yukoje?”
“Umbo lake ni kama mimi ila yeye ni mweupe sana na ana sura kama muarabu”
Mara moja nikamkumbuka Zena ambaye nilikuwa nimeshamsahau.
“Anakwambia uondoke hapa nyumbani?”
“Ndio. Tena amenishikia bakora, anataka kunichapa”
Ili kumtoa hofu Salama nikajaribu kuzuga.
“Unajua ulikuwa umelala kichali chali halafu ulishiba sana. Lazima uote ndoto zisizoeleweka”
“Nilaleje sasa?” Salma akaniuliza kwa hofu.
“Lala kiubavu ubavu, elekea huku kwangu” nikamwambia”
Salma alipoelekea upande wangu akaniambia.
“Nikumbatie naogopa”
Nikamkumbatia. Salma hakuchelewa kupata usingizi. Akalala fofo. Mawazo yakabaki kwangu.
Asubuhi tulipoamka nilimuuliza.
“Uliota tena”
“Hapana, sikuota” akaniambia.
Nikashukuru aliponiambia hivyo. Nikajitayarisha kwenda kazini. Muda wangu wa kutoka ulipowadia nikatoka.
Nilichapa kazi hadi saa kumi jioni nikarudi nyumbani. Nilikuta nyumba ilikuwa imefungwa. Funguo nilipewa na mpangaji mwenzangu wa upande wa pili.
“Mke wako aliondoka, akaniachia hizi funguo. Amesema ukija nikupe”
“Amekwambia amekwenda wapi?”
“Hakuniambia”
Nikazichukua zile funguo na kufungua mlango huku nikiwa na mawazo. Nilipoingia chumbani nilikuta karatasi ya barua iliyokuwa imeachwa kitandani. Nikaichukua na kuisoma.
Mwandiko ulikuwa wa mke wangu Salma. Iliandikwa.
“Nimelazimika kuondoka hapa nyumbani ili kuokoa maisha yangu. Ile ndoto ilinijia tena mchana. Nilimuota tena yule msichana. Aliniuliza kwanini sijaondoka. Akaanza kunitandika bakora. Ngozi yangu ya mgongo imeharibika kwa jinsi alivyonichapa. Hali yangu ni mbaya. Ninakwenda hospitali na nikitoka hospitali narudi kwetu. Naomba uniletee talaka yangu. Huyo msichana ninayemuota ameniambia kama nitaendelea kukaa ataniua”
Salama alimaliza barua yake kwa kuweka jina lake.
Kusema kweli maneno ya Salma aliyokuwa ameniandikia yalinishitua sana. Nilipomaliza kusoma barua ile niliona miguu ikininyong’onyea na kuishiwa na nguvu.
UNAJUA BALAA? HILI NI BALAA LINALOMKUTA KIJANA HUYU! HAYA TWENDE NAYE POLE POLE
 
SEHEMU YA 38


ILIPOISHIA
Nikamkumbatia. Salma hakuchelewa kupata usingizi. Akalala fofo. Mawazo yakabaki kwangu.
Asubuhi tulipoamka nilimuuliza.
“Uliota tena”
“Hapana, sikuota” akaniambia.
Nikashukuru aliponiambia hivyo. Nikajitayarisha kwenda kazini. Muda wangu wa kutoka ulipowadia nikatoka.
Nilichapa kazi hadi saa kumi jioni nikarudi nyumbani. Nilikuta nyumba ilikuwa imefungwa. Funguo nilipewa na mpangaji mwenzangu wa upande wa pili.
“Mke wako aliondoka, akaniachia hizi funguo. Amesema ukija nikupe”
“Amekwambia amekwenda wapi?”
“Hakuniambia”
Nikazichukua zile funguo na kufungua mlango huku nikiwa na mawazo. Nilipoingia chumbani nilikuta karatasi ya barua iliyokuwa imeachwa kitandani. Nikaichukua na kuisoma.
Mwandiko ulikuwa wa mke wangu Salma. Iliandikwa.
“Nimelazimika kuondoka hapa nyumbani ili kuokoa maisha yangu. Ile ndoto ilinijia tena mchana. Nilimuota tena yule msichana. Aliniuliza kwanini sijaondoka. Akaanza kunitandika bakora. Ngozi yangu ya mgongo imeharibika kwa jinsi alivyonichapa. Hali yangu ni mbaya. Ninakwenda hospitali na nikitoka hospitali narudi kwetu. Naomba uniletee talaka yangu. Huyo msichana ninayemuota ameniambia kama nitaendelea kukaa ataniua”
Salama alimaliza barua yake kwa kuweka jina lake.
Kusema kweli maneno ya Salma aliyokuwa ameniandikia yalinishitua sana. Nilipomaliza kusoma barua ile niliona miguu ikininyong’onyea na kuishiwa na nguvu.
SASA ENDELEA
Nikakaa kitandani na kuanza kutafakari. Tayari nilihisi presha yangu ikiwa juu na moyo ukienda mbio.
Nilirudia kuisoma tena ile barua. Nikaona kama uso wa Salma umetokeza katikati ya ile karatasi ukitamka yale maneno aliyoandika.
Nikaisikia waziwazi sauti yake ikimalizia kusoma barua hiyo kwa kuniambia.
“Naomba uniletee talaka yangu. Huyo msichana ninayemuota ameniambia kama nitaendelea kukaa ataniua…”
Nilihisi sasa mwili mzima ukipoteza nguvu. Tukio lile lilikuwa limenichoma mithili ya mkuki wa moto moyoni mwangu. Picha ya kuachana na Salama haikukubalika akilini mwangu. Si tu nilikuwa nampenda bali alikuwa ni kila kitu kwangu.
Tukio lile liliniashiria kwamba sitaweza tena kuishi na mke yeyote.
Zena amemtandika bakora Salma kama alivyowatandika wale vijana waliomuibia pochi.
Nilijua kuwa kama Salma asingeondoka na yeye angeuawa. Kuondoka kwake ulikuwa uamuzi wa maana ingawa sikuupenda.
Pia nilijua huo ulikuwa ndio mwisho wangu na Salma. Salama singeweza kurudi tena pale nyumbani na asingetaka tena kuishi na mimi.
Yale mawazo niliyokuwa nayo kwamba nikioa mke zena atakuwa mbali na mimi hayakuwa sahihi. Sikuweza kutambua huyu jini alikuwa na nia gani na mimi.
Kusema kweli nilisikia uchungu sana. Nikatikisa kichwa changu kusikitika. Nilishindwa kuvumilia machungu niliyokuwa nikiyasikia moyoni mwangu, nikaona machozi yakinitiririka.
Wakati nimeinamisha kichwa changu, nilihisi kama Zena amesimama mbele yangu akinicheka. Nikashituka na kudhani alikuwa Zena kweli. Kumbe yalikuwa ni mawazo yangu tu.
Nikajiuliza niende kwa kina salma nizungumze naye, lakini nikajiuliza tena ningekwenda kuzungumza naye nini wakati Salama ameshaamua kuondoka kusalimisha roho yake?
Nikajiambia kuwa si ajabu ameshagundua kuwa nina jini mwanamke ambaye hataki niwe na mke. Kama itakuwa hivyo nikifika kwao Salama anaweza kukataa nisizungumze naye zaidi ya kudai talaka yake kama alivyoniandikia kwenye barua.
Nilijihisi nilikuwa nimekabiliwa na uamuzi mgumu sana. Baada ya kuwaza kwa dakika kadhaa bila kupata ufumbuzi niliamua kutoka na kwenda kumueleza kaka kilichonitokea.
Kaka akapatwa na mshangao hasa nilipomueleza kuwa Salama ametandikwa bakora na Zena na ameshaondoka nyumbani.
“Sasa tufanye nini?” Kaka akaniuliza. Swali lake lilinikatisha tamaa. Nilichotarajia ni kupata ushauri kutoka kwake na sio mimi nimueleze yeye la kufanya.
Ilionesha mpaka kufikia kuniuliza tufanye nini ni kwamba alikuwa amekwama.
“Mimi sijui la kufanya. Nimekuja kwako ili nipate ushauri” nikamwambia.
“Mmh!” kaka aliguna kwanza kabla ya kuniambia.
“Sijui nikupe ushauri gani. Nikikwambia umbembeleze mke wako arudi ni kwamba atatandikwa tena na nikikwambia muache huko huko kwao, unyumba wenu utakuwa haupo tena!”
“Yaani tangu sasa unyumba wetu hauko tena, anadai nimpe talaka yake!”
“Ndio hapo sasa!”
“Mimi siwezi kumpa talaka. Nataka nipambane na hili tatizo kwa nguvu zote”
“Utapambana nalo kivipi?”
Swali hilo likanifanya nihamaki. Niliona kama vile kaka hakuwa pamoja na mimi.
“Kaka kwa mara ya kwanza naona una maswali ya kunikatisha tamaa” nikamwambia huku nikitikisa kichwa kusikitika.
“Hapana Amour, usinifikirie hivyo. Mimi niko pamoja na wewe. Nimekuuliza ili unieleze jinsi tutakavyopambana na hilo tatizo”
Nilikuwa nimeshahamaki. Nikaondoka kwenye kiti.
“Sasa unakwenda wapi?” Kaka akaniuliza.
“Niache kwanza” nilimwambia na kufungua mlango ili nitoke.
Kaka akanyanyuka.
“Hebu subiri Amour…!”
Nikatoka haraka. Nilipanda pikipiki yangu nikaiwasha na kwenda kwa mama.
Mama alivyouona uso wangu alijua kulikuwa na jambo lisilo la kawaida. Akaniuliza.
“Kulikoni?”
“Kuna matatizo yametokea” nikamwambia na kumueleza tatizo la kutandikwa bakora kwa mke wangu na kuondoka nyumbani.
“Nimekwenda kwa kaka, kaka ameshindwa kunisaidia kimawazo. Sasa mimi naondoka nyumbani nitakwenda kokote ambako naona nitapata msaada. Kama itashindikana, basi bora nife huko huko!”
Nilipomwambia hivyo mama nilitoka na kupanda pikipiki yangu. Mama alikuwa ametoka nje akinisemesha lakini sikujua alikuwa akiniambia nini na sikutaka kumsikiliza. Nikaondoka.
Nilirudi nyumbani, nikapanga baadhi ya nguo zangu kwenye begi. Nilikuwa na akiba ya pesa nilizokuwa nimeziweka kwenye kabati. Nikazichukua.
Kwa vile kichwa kilikuwa kimenichafuka, nilimuachia funguo mwenzangu wa upande wa pili nikaenda kulala gesti.
Kitu ambacho kilinikera sana, niliota Zena amesimama kwenye jangwa akinicheka. Alikuwa akinicheka hadi anayumba kama mlevi.
Asubuhi kulipokucha nilitoka nikaenda kituo cha mabasi. Nilipanda basi la kuelekea Dar. Nilifika Dar saa sita mchana nikaenda kutafuta gesti. Nilipopata gesti niliacha begi langu na kwenda kwenye mkahawa uliokuwa karibu kupata chakula kwani sikuwa nimekula chochote tangu subuhi.
Baada ya kula chakula nilirudi pale gesti. Kulikuwa na mgeni mmoja wa kipemba aliyekuwa amepangisha chumba. Tulikutana ukumbini. Nikamsalimia na kumuuliza kama alikuwa anatoka Zanzibar.
“Natoka Mwanza, ndio niko safarini kuelekea Zanzibar” akaniambia.
“Unakwenda Unguja au Pemba?”
“Mimi naenda Pemba”
“Unatarajia kwenda lini?”
“Kesho asubuhi Mungu akipenda”
“Basi tutaondoka sote, nilikuwa na tatizo linalohusu huko Pemba na nitakueleza”
“Ni tatizo gani?”
“Hebu njoo huku chumbani kwangu nikueleze”
Yule mtu alikubali kuingia chumbani kwangu. Nikamueleza yale matatizo yangu.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 39


ILIPOISHIA
Nilirudi nyumbani, nikapanga baadhi ya nguo zangu kwenye begi. Nilikuwa na akiba ya pesa nilizokuwa nimeziweka kwenye kabati. Nikazichukua.
Kwa vile kichwa kilikuwa kimenichafuka, nilimuachia funguo mwenzangu wa upande wa pili nikaenda kulala gesti.
Kitu ambacho kilinikera sana, niliota Zena amesimama kwenye jangwa akinicheka. Alikuwa akinicheka hadi anayumba kama mlevi.
Asubuhi kulipokucha nilitoka nikaenda kituo cha mabasi. Nilipanda basi la kuelekea Dar. Nilifika Dar saa sita mchana nikaenda kutafuta gesti. Nilipopata gesti niliacha begi langu na kwenda kwenye mkahawa uliokuwa karibu kupata chakula kwani sikuwa nimekula chochote tangu subuhi.
Baada ya kula chakula nilirudi pale gesti. Kulikuwa na mgeni mmoja wa kipemba aliyekuwa amepangisha chumba. Tulikutana ukumbini. Nikamsalimia na kumuuliza kama alikuwa anatoka Zanzibar.
“Natoka Mwanza, ndio niko safarini kuelekea Zanzibar” akaniambia.
“Unakwenda Unguja au Pemba?”
“Mimi naenda Pemba”
“Unatarajia kwenda lini?”
“Kesho asubuhi Mungu akipenda”
“Basi tutaondoka sote, nilikuwa na tatizo linalohusu huko Pemba na nitakueleza”
“Ni tatizo gani?”
“Hebu njoo huku chumbani kwangu nikueleze”
Yule mtu alikubali kuingia chumbani kwangu. Nikamueleza yale matatizo yangu.
SASA ENDELEA
“Sasa shida yangu ni kupata mganga ambaye ataliondoa hili tatizo” nikamwambia.
Mpemba alinyamaza kimya akafikiri kisha akaniambia.
“Yuko mama mmoja pale Pemba ni mganga anayetegemewa sana kwa matatizo ya majini. Kama yeye atashindwa ujue hutapata tena mganga ambaye atamuweza huyo jini wako”
“Ningekuomba unipeleke kwa huyo mwanamke”
“Nitakuelekeza na hutapotea”
“Lakini wewe pia si unakwenda huko huko”
“Ndio, mimi nakwenda Pemba lakini ninakokwenda ni kwingine na huyo mganga yuko kwingine. Yaani hata tukienda sote tutaachana bandarini”
“Si kitu, wewe nielekeze tu, nitafika”
Kwa vile mji wenyewe nilikuwa siujui, yule mtu alinichorea ramani ikianzia bandari ya Pemba hadi ulikokuwa mtaa huo. Akaniambia nyumba ya mganga huyo iko kwenye kona. Ni nyumba kubwa lakini ni ya kizamani sana na imepakwa chokaa nyeupe.
“Alama yake ni kuwa mlango wa mbele wa nyumba hiyo umechorwa picha ya nyota na mwezi” akaniambia.
“Nitapaelewa tu” nikamwambia.
Asubuhi ya siku iliyofuata tukasafiri sote kwenye boti. Tulipofika Pemba akanielekeza tena. Nikaenda mwenyewe katika huo mtaa.
Kwa vile nilikwenda kwa miguu ili nisipotee nilitembea sana
Mara kwa mara nilikuw a nawauliza watu niliokutana nao njiani kama wanamfahamu mganga huyo. Baadhi ya watu hao walikuwa wanamfahamu na wakanielekeza zaidi mtaa aliokuwa anaishi.
Baada ya mwendo mrefu nikafika katika mtaa huo, nikawa naitafuta ile nyumba. Baada ya kuhangaika sana nikaiona. Ilikuwa kwenye kona na ilipakwa chokaa nyeupe.
Alama kubwa iliyonipa moyo ni picha ya nyota na mwezi niliyoikuta kwenye mlango.
Kama alivyonieleza yule mtu niliyesafiri naye, nyumba hiyo ilikuwa ya kizamani sana na ilikuwa kwenye hatari ya kuanguka kwani ilikuwa ni nyumba iliyojengwa kwa mawe na udongo ingawa ilipauliwa kwa bati. Bati hilo lilikuwa limeota kutu na kuchakaa.
Nikaenda kwenye mlango na kubisha. Nilibisha mara mbili bila kupata jibu. Nilipobisha mara ya tatu nikajibiwa.
“Karibu” Ilikuwa sauti ya mwanamke. Nilishaambiwa kuwa mgaga mwenyewe ni mwanamke.
Baada ya sekunde chache mlango ukafunguliwa. Ndani kulikuwa kiza. Hata mtu aliyenifungulia mlango sikuweza kumuona vizuri.
“Karibu ndani” Sauti ya mwanamke ikaniambia.
Nikaingia. Kulikuwa na ukumbi mpana uliokuwa umetandikwa jamvi.
“Karibu ukae kwenye jamvi”
Nikakaa. Yule mwanamke naye akakaa kando yangu.
“Pole kwa safari, naona umetoka mbali” akaniambia huku akinitazama. Sasa pale ndipo nilipomuona vizuri. Kumbe alikuwa Zena!
Nilishituka sana nilipogundua kuwa mwanamke mwenyewe alikuwa Zena.
Nilishindwa kuelewa kwanini amekuwa Zena wakati niliambiwa kulikuwa na mwanamke ambaye ni mganga.
“Habari za huko?” Zena aliniuliza alipoona nimepigwa na butwaa.
Niligeza haraka uso wangu nisitazamane naye. Nikawa natazama chini.
“Nzuri” nikamjibu. Sauti yangu ilikuwa nzito ya mtu aliyetahayari.
“Mbona umekuja huku, una shida gani?” akaniuliza huku akinitazama kwa makini. Nilikuwa nimeinamisha uso wangu lakini nilikuwa namuona kwa pembeni mwa macho yangu.
Nilishindwa kujibu Swali lake kwa sababu sikujua ningemjibu nini. Nimjibu kuwa nimekwenda Pemba kufuata mganga na badala yake nakutana na yeye? Hapana.
“Nimekuja kutembea tu” nikamwambia
baada ya kushindwa kumueleza ukweli.
“Umekuja kutembea tu huku Pemba?” Zena akaniuliza kwa sauti iliyoonesha kuwa hakuyaamini maneno yangu.
“Ndio” nikamjibu.
“Sasa umeshatembea na kuuona mji?”
“Ndio”
“Umeuonaje?”
“Ni mji mzuri”
“Kumbe unatembea hadi huku Pemba?’
“Ni leo tu”
“Umepanga kurudi lini?”
“Nitarudi leo”
“Si ulale uondoke kesho?”
Nikatikisa kichwa.
“Nitaondoka leo leo”
“Nisubiri basi tuondoke sote”
Zena akainuka. Aliingia kwenye chumba kimojawapo ambacho mlango wake ulikuwa wazi. Nikamuona anavaa baibui. Akachukua mkoba wake na kutoka.
“Twendezetu” akaniambia kama vile tulikuja safari moja.
Nikainuka na kumfuata. Tulitoka kwenye ile nyumba tukashika njia ya kuelekea bandarini.
Wakati wote nilikuwa nikijiuliza kwanini nilimkuta Zena pale nyumbani. Huyo mganga mwenyewe alikuwa wapi?
Ile ilikuwa ni miujiza ya ajabu ambayo sikuwahi kuiona katika maisha yangu.
Matarajio yangu ya kumpata mganga wa kuliondoa tatizo langu yalififia kabisa moyoni mwangu. Huyu jini alikuwa amenizingira kila pembe.
Tulipofika bandarini Zena alikata tikiti mbili za boti inayokwenda kasi. Boti hiyo ilikuwa inakwenda Dar. Siku ile hakukuwa na chombo chohote kinachokwenda Tanga.
Tulipojipakia kwenye boti nilikaa na Zena siti zilizokuwa zimepakana. Tulisubiri kwa muda wa saa nzima kabla ya safari kuanza.
Kweli kupambana na jini aina ya Zena ni kazi! Sasa alikuwa akinirudisha Dar. Niliamini kuwa alikuwa akijua kilichonipeleka Pemba ingawa hakuniambia. Kitu ambacho nilishindwa kuelewa ni jinsi nilivyomkuta yeye pale nyumbani kama vile ni kwake.
Wakati boti iko katikati ya safari nilimuona Zena amelala usingizi kabisa. Nikawa namtazama. Alikuwa na weupe uliochanganyika na wekundu. Uso wake ulikuwa na pozi la kiarabu ingawa alionekana kuchanganya damu ya Kiafrika. Sikujua kama majini nao wanakuwa machotara kama binaadamu.
Kwa uzuri alikuwa mzuri sana, sikuwahi kuona msichana mwenye mvuto wa sura na umbile kama yeye. Tatizo lake ni kwamba alikuwa jini tena jini mbaya mwenye vituko vilivyoshindikana.
Hadi pale nilikuwa nimesalimu amri. Nilishasema kuwa Zena sitamuweza tena na hakukuwa na mganga yeyote atakayemuweza.
Ghafla tuliona boti ikikata moto. Ikawa inasuasua juu ya bahari. Muda si muda ikapigwa na wimbi kubwa. Sote tulitikiswa. Hapo ndipo watu walipoanza kwenda mbio na kuifanya boti ilale upande mmoja.
Baadhi ya abiria wakaanza kujitosa baharini. Nikaona sasa hali ilikuwa mbaya. Nilijikuta nikimuamsha Zena bila kupenda. Zena akaamka.
“Nini. Mbona kuna hekaheka?” akaniuliza.
“Boti inazama” nikamwambia.
“Boti inazama?” akaniuliza kwa fadhaa.
Kabla sijamjibu, ule upande wa boti uliokuwa unazama ukazidi kulala.
“Duh ni kweli, twende tukaruke, tutakufa humu!” akaniambia huku akiinuka kwenye siti.
Tulikwenda kwenye mlango wa boti tukatoka. Watu walikuwa wakiendelea kuchupa baharini.
“Chupa!” Zena akaniambia.
Laiti angejua jinsi ambavyo sikuwa nikijua kuogelea asingeniambia chupa.
Upande wa pili wa boti nao ikaanza kuzama.
“Chupa, boti inazama!” akaniambia tena.
Sikuthubutu. Nilibaki kuitazama bahari.
“Amour unasubiri kufa humu ndani ya boti?” Zena akaniuliza kwa hasira.
Nikatikisa kichwa.
“Siwezi kuogelea, nikiruka ndio nimekwisha!”
“Mwanaume mzima unasema huwezi kuogelea, mimi mwanamke nisemeje?” akaniuliza.
Sikuwa na jibu. Nikaendelea kutikisa kichwa changu.
Sikujua ilikuwaje. Zena alinishika mkanda wa suruali yangu kwa nyuma kisha akanirusha baharini. Hadi leo nashindwa kujua alinirushaje.
Kabla ya kutumbukia baharini, nilijiambia ule ulikuwa ndio mwisho wangu.
Nilitanguliza mikono na kichwa, Nikazama chini kabisa.
DUH! MASIKINI KIJANA HUYU! JE HUU NDIO MWISHO WA AMOUR?
 
SEHEMU YA 40


ILIPOISHIA
Kabla sijamjibu, ule upande wa boti uliokuwa unazama ukazidi kulala.
“Duh ni kweli, twende tukaruke, tutakufa humu!” akaniambia huku akiinuka kwenye siti.
Tulikwenda kwenye mlango wa boti tukatoka. Watu walikuwa wakiendelea kuchupa baharini.
“Chupa!” Zena akaniambia.
Laiti angejua jinsi ambavyo sikuwa nikijua kuogelea asingeniambia chupa.
Upande wa pili wa boti nao ikaanza kuzama.
“Chupa, boti inazama!” akaniambia tena.
Sikuthubutu. Nilibaki kuitazama bahari.
“Amour unasubiri kufa humu ndani ya boti?” Zena akaniuliza kwa hasira.
Nikatikisa kichwa.
“Siwezi kuogelea, nikiruka ndio nimekwisha!”
“Mwanaume mzima unasema huwezi kuogelea, mimi mwanamke nisemeje?” akaniuliza.
Sikuwa na jibu. Nikaendelea kutikisa kichwa changu.
Sikujua ilikuwaje. Zena alinishika mkanda wa suruali yangu kwa nyuma kisha akanirusha baharini. Hadi leo nashindwa kujua alinirushaje.
Kabla ya kutumbukia baharini, nilijiambia ule ulikuwa ndio mwisho wangu.
Nilitanguliza mikono na kichwa, Nikazama chini kabisa.
SASA ENDELEA
kisha nikarudishwa tena juu. Wakati natokeza juu nilimuona Zena akijirusha baharini. Alichupa kama samaki. Akawahi kunishika kabla sijazama kwa mara ya pili.
Nilivamia mwili wake ili nijiokoe kwani pumzi zilikuwa zimeniishia.
“Usinivamie, tutazama sote. Tuliza akili yako” akaniambia huku akielea juu ya maji.
Niliendelea kumg’ang’ania.
“Usining’ang’anie, tutazama sote. Shika miguu yangu. Usishike mwili wangu!” Zena alinipigia kelele. Sasa nilikuwa kama hayawani nisiyejielewa.
Zena alipoona bado simsikilizi alinipiga ngumi ya shavu, nikamuachia na kuzama chini. Wakati niko ndani ya maji nikipelekwa chini, Zena alipiga mbizi akaniwekea mgongo wake kwenye kifua changu kisha akaibuka na mimi juu ya maji.
”Tulia kwenye mgongo wangu, ukifurukuta nakuacha. Nishike mabega yangu” akaniambia.
Nikafanya vile alivyotaka.
Zena akaanza kuogelea huku nikiwa kwenye mgongo wake. Yule msichana alikuwa hodari sana.
Aliweza kuogelea kwa mwendo mrefu akiwa na mimi bila kunidondosha na bila kuonesha kuchoka.
Ile boti iliyokuwa inazama tuliiacha mbali kabisa.
Zena aliendelea kuogelea tu kama vile alikuwa na mashine iliyokuwa inampa nguvu. Nikakumbuka maneno ya watu wanaosema kwamba majini huzaliwa baharini. Nikahisi kuwa hiyo ndio sababu akawa na uzoevu mkubwa wa kuogelea.
Hatimaye ile boti sikuiona tena. Sasa nikawa najiuliza tunaelekea wapi. Sikupata jibu. Jua lilikuwa linakuchwa kwa haraka upande wa magharibi na tayari lilionekana likitoa mionzi ya kimanjano iliyoashiria kuwa wakati wa magharibi ulikuwa unakaribia.
Mbele yangu nikaona kitu kimejitokeza. Baadaye niligundua kuwa tulikuwa tunatokea kwenye kisiwa. Kilikuwa bado kiko mbali na sisi. Kwanza nilianza kuona majani ya miti yaliounda shada kubwa la rangi ya kijani. Halafu nilianza kuona msitu mkubwa.
Kadiri tulivyokuwa tunakikaribia kisiwa hicho ndivyo nilivyoweza kukiona vizuri. Naam kilikuwa ni kisiwa. Sasa ardhi yake ilionekana waziwazi. Kilikuwa kisiwa kidogo kilichokuwa na msitu mkubwa wa miti.
Tulipofika maji madogo Zena aliniambia niondoke mgongoni kwake.
Sikumsikia vizuri, nilikuwa nimeendelea kumshikilia. Ile harufu ya udi wa mawaridi niliyokuwa nikisikia mgongoni mwake ilikuwa imenilewesha.
“Ondoka bwana, mwenzako nimechoka!” akaniambia kwa sauti ya ukali.
Nikajaribu kuishusha miguu yangu taratibu, taratibu, nikaona ninakanyaga mchanga lakini maji yalikuwa yakinifika kwenye kifua. Nikaanza kutembea kwa miguu nikiwa bado nimemshikilia Zena. Ilibidi nipate kitu cha kushika, vinginevyo maji yangeweza kunikupua.
Niliendelea kutembea hadi maji yaliponifikia kiunoni ndipo nilipomuacha Zena. Sasa tulikuwa tukitembea pamoja. Nguo zetu zilitota chapa. Maji ya chumvi yalikuwa yakitutiririka mwilini.
Tulifika ufukweni mwa kisiwa hicho. Fukwe yake ilikuwa nzuri yenye mchanga mweupe.
“Hapa ni wapi?” nikamuuliza Zena.
Zena aliyeonesha wazi kuwa alikuwa amechoka hakunijibu chochote, aliendelea kwenda hadi tukaingia kwenye ule msitu.
Zena alitafuta sehemu iliyokuwa juu akapanda na kujilaza chini.
“Oh leo nimechoka sana. Sijaogelea mwendo mrefu kama leo” Zena akajisemea peke yake akiwa amejilaza kichali chali.
Baibui alilokuwa amevaa lililoa maji na kuonya kama kioo. Nguo aliokuwa amevaa ndani nayo ilikuwa ikionya kwa sababu ya kutota maji. Ngozi nyeupe ya mwili wa Zena iliyokuwa na malaika marefu ilikuwa ikionekana wazi wazi.
Mimi nilikuwa nimeketi nikihema huku nikiyatembeza macho yangu kila upande wa kile kisiwa. Sikujua tulikuwa katika kisiwa gani na kilikuwa wapi.
Pia sikujua tungeondokaje katika kisiwa hicho ambacho hakikuonesha dalili yoyote ya kuishi watu. Nilikuwa nikijiambia kama kutakuwa na wanayama wakali wanaweza kutudhuru.
“Unangoja hizo nguo zako zikaukie mwilini mwako?” Zena akaniuliza.
“Sasa nizifanye nini?”
“Si uzivue?”
“Nizivue nikae uchi?”
“Kwani huna chupi?”
“Acha tu, zitakauka humu humu”
“Mimi nguo zangu ni nyepezi, zitakauka mara moja”
Niliyapuuza yale maneno ya Zena. Akili yangu ilikuwa kwingine. Nilikuwa nikijiuliza jinsi tutakavyoondoka kwenye kisiwa kile.
“Tutaondokaje hapa?” nikamuuliza Zena.
Kabla ya Zena kunijibu nikaona kitu kikitokeza kwenye miti mbele yetu. Nilishituka nilipogundua kuwa lilikuwa joka kubwa na refu. Lingeweza hata kutumeza mimi na Zena kwa wakati mmoja.
“Zena! Zena!” nikamuita Zena.
Zena akainua kichwa na kunitazama.
“Nini?’ akaniuliza.
“Angalia kule!” nikamwambia huku nikimuonesha lile joka kwa kidole.
Zena akapeleka macho yake na kuliona.
“Sijakwambia lakini sasa nakwambia, hiki kisiwa ni cha majini. Lile si joka kama unavyoliona ni jini limejigeuza joka. Wako wengi tu hapa”
Maneno yake yalizidi kunitisha.
“Sasa kwanini tumekuja hapa?” nikamuuliza kwa taharuki.
“Unawaogopa? Si majini wakubwa kama sisi, ni visubiani vya ovyo ovyo tu. Ngoja nitamfukuza”
Lile joka lilikuwa limetusogelea, likitaka kupandisha kichwa chake juu ya ile sehemu tuliyokuwa.
Zena akaanza kulifokea kwa lugha ya kikwao. Mimi nilisogea nyuma ya Zena kwa hofu. Zena akanyanyuka na kulifuata kabisa huku akiendelea kulifokea.
Lile joka lilibaki pale pale likinitazama mimi.
Zena akavua kiatu chake akakishika na kulipiga kichwani. Joka hilo likatoweka hapo hapo.
“Shika” alinipa kile kiatu. Akaniambia.
“Ukiona joka linakufuata lipige na hiki kiatu changu, litatokomea”
“Halitanimeza?” nikamuuliza huku nikipokea kile kiatu.
“Hapana”
“Kumbe hapa mahali ni pa hatari namna hii?”
“Wewe ndio umetaka tufike hapa”
“Nimetaka mimi?”
“Ndio”
“Nilikwambia kuwa tuje hapa?”
“Kwani wewe siku zote unajua mimi nataka nini kwako?”
Hapo nikagwaya.
Zena akaendelea kuniuliza.
“Ulifuata nini Pemba?”
Sikuwa na la kumjibu.
“Sasa niambie utanioa niwe mke wako au bado hutaki?”
“Nikishakuoa tutakwenda kuishi wapi?’ nikamuuliza.
“Kule kule unakoishi wewe”
“Turudi kule kwanza ndio tupange mipango ya ndoa, si hapa”
“Nataka tukirudi niwe tayari ni mke wako”
“Kwani tutakwenda kuoana wapi?” nikamuuliza Zena.
“Mtu huolewa kwao na mimi utakwenda kunioa kwetu”
“Kwenu wapi?”
“Kwetu hukujui?”
“Sikujui”
“Kwetu ni ujinini”
“Yaani tutakwenda kuoana kwenu ujinini?”
“Ndio”
“Sasa ungeacha kwanza nirudi nyumbani nikajiandae. Hatuwezi kuoana ghafla”
“Wewe umekuwa mkaidi mara nyingi. Siwezi kukupa nafasi hiyo. Madhumuni yangu ya kukuleta hapa ni kuwa twende tukaoane. Muda umeshafika”
Nikanyamaza kimya.
Zena alikuwa akiendelea kuniambia.
“Ile boti niliizamisha mimi kusudi ili nikulete hapa. Ninajua tukiwa hapa hutakuwa na ujanja wowote”
Ndipo nilipogundua kuwa Zena alikuwa amenizunguka! Kumbe ile boti aliizamisha yeye ili anipate mimi…
Kufika Kwetu pale kisiwani nilidhani nilikuwa nimesalimika na kifo, kumbe nilikuwa ninasubiriwa na matatizo mengine.
Kama alivyoniambia Zena, ni kweli pale kisiwani nisingekuwa na ujanja wowote zaidi ya kusalimu amri.
Lakini akili yangu bado ilikuwa haikubaliani na mawazo ya Zena. Kumuoa jini lilikuwa jambo ambalo sikuwa tayari nalo.
“Sikiliza Zena, naona sasa unatumia jazba ambayo si nzuri” nikamwambia Zena. Lakini hataka kabla sijamaliza sentensi yangu au alinikatiza.
“Kumbe ulitaka nifanye nini?”
Sasa sauti yake ilikuwa ya hamaki.
“Nilitaka unisikilize ninachokwambia”
“Kipi?”
“Turudi Tanga ili nijiandae kwa jambo hilo, kwanini wewe unachukulia nguvu?”
“Nachukulia nguvu kwa sababu nimeshaakuona kuwa huko tayari kunioa”
“Niko tayari, nani kakwambia kama siko tayari. Ninachotaka mimi unipe muda tu wa kujiandaa”
“Amour usinidanganye, huko tayari. Kama ungekuwa tayari usingekwenda kumuoa yule mwanamke wako niliyemfukuza pale nyumbani”
“Yule nilimuoa kwa sababu ndugu zangu walimtaka yeye lakini sasa nitawaambia kuwa nataka kuoana na wewe”
“Usiniambie habari ya ndugu zako, nyote nyinyi ni kitu kimoja”
“Mbona hutaki kunisikiliza Zena!”
“Sitakusikiliza. Wewe ni muongo ingawa sipendi kukuita hivyo. Wewe hunitaki mimi wakati mimi nimekusaidia sana. Kwanza niambie ulifuata nini Pemba?”
“Si nimekwambia kwamba nilikwenda kutembea”
“Usinidanganye. Usinifanye mimi sina akili. Wewe ulikwenda Pe,mba baada ya kuambiwa kuna mganga ambaye ataweza kupambana na mimi”
Nikajikuta natikisa kichwa changu kwa fadhaa.
“Si kweli” nikamwambia lakini uso wangu ulikuwa umetahayari.
“Unaona aibu mwenyewe kutokana na hila zako, Unadhani kuna mganga ataniweza mimi?”
Nikabaki kimya. La kusema nilikuwa sina.
“Sasa usinipotezee muda wangu, nataka jibu lako. Tutakwenda ujinini kuoana au hatutakwenda?” Zena akaniuliza.
Nilikuwa nimeinamisha kichwa changu nikiwaza. Sikuwa na jibu la kumpa, nikabaki kutikisa kichwa kuashiria kutokukubaliana naye.
“Amour nakuuliza tena, tutakwenda ujinini tukaoane au hatutakwenda?”
Niliendelea kutikisa kichwa.
“Una maana huko tayari siyo?”
Sikumjibu.
“Sasa mimi nakwenda zangu, nakuacha hapa hapa. Hutaniona tena”
Nikainua uso wangu haraka ili nimwambie asiniache pale lakini Zena alitoweka ghafla kama upepo. Kama alivyoniambia sitamuona tena na kweli sikumuona tena!
Nikatazama huku na huku, Zena hakuweko. Nikabaki peke yangu kwenye kisiwa kile cha majoka!
DUH!
HAYA ATAFANYA NINO HUYU LKIJANA WA WATU MASIKINI!
 
SEHEMU YA 41


ILIPOISHIA
“Usiniambie habari ya ndugu zako, nyote nyinyi ni kitu kimoja”
“Mbona hutaki kunisikiliza Zena!”
“Sitakusikiliza. Wewe ni muongo ingawa sipendi kukuita hivyo. Wewe hunitaki mimi wakati mimi nimekusaidia sana. Kwanza niambie ulifuata nini Pemba?”
“Si nimekwambia kwamba nilikwenda kutembea”
“Usinidanganye. Usinifanye mimi sina akili. Wewe ulikwenda Pemba baada ya kuambiwa kuna mganga ambaye ataweza kupambana na mimi”
Nikajikuta natikisa kichwa changu kwa fadhaa.
“Si kweli” nikamwambia lakini uso wangu ulikuwa umetahayari.
“Unaona aibu mwenyewe kutokana na hila zako, Unadhani kuna mganga ataniweza mimi?”
Nikabaki kimya. La kusema nilikuwa sina.
“Sasa usinipotezee muda wangu, nataka jibu lako. Tutakwenda ujinini kuoana au hatutakwenda?” Zena akaniuliza.
Nilikuwa nimeinamisha kichwa changu nikiwaza. Sikuwa na jibu la kumpa, nikabaki kutikisa kichwa kuashiria kutokukubaliana naye.
“Amour nakuuliza tena, tutakwenda ujinini tukaoane au hatutakwenda?”
Niliendelea kutikisa kichwa.
“Una maana huko tayari siyo?”
Sikumjibu.
“Sasa mimi nakwenda zangu, nakuacha hapa hapa. Hutaniona tena”
Nikainua uso wangu haraka ili nimwambie asiniache pale lakini Zena alitoweka ghafla kama upepo. Kama alivyoniambia sitamuona tena na kweli sikumuona tena!
Nikatazama huku na huku, Zena hakuweko. Nikabaki peke yangu kwenye kisiwa kile cha majoka!
SASA ENDELEA
Kile kiatu chake alichokivua na kulipiga lile joka nikabaki nacho. Mwenyewe amekwenda na kiatu kimoja.
Nilipata hofu kweli kweli.
Jua lilikuwa limeshakuchwa na kiza kilikuwa kinaingia. Nikajiuliza “nitafanyaje Amour?”
Zena alikuwa ameshaniacha peke yangu. Nikawa nahisabu dakika zangu za kufa au kuliwa na majoka.
Nikaondoka mahali pale nilipokuwa nakwenda kupanda juu ya mti nikiwa na kile kiatu. Nilikaa kwenye tawi moja nikawa naitazama bahari. Hakukuwa na mtumbwi wala ngarawa iliyokuwa ikipita. Bahari ilikuwa nyeupe.
Kusema kweli nilijuta kufunga safari ile ya kwenda Pemba kufuata mganga. Na kama niliamua kwenda ningekwenda na ndugu yangu na si peke yangu kama nilivyofanya.
Nilianza kusikia baridi mwilini, sikujua itakapofika usiku ingekuwaje.
Nilitamani Zena anionee huruma aje anichukue. Lakini mawazo yangu yalikuwa sawa na dua la kuku. Hakuna aliyelisikia.
Wakati nimekaa kwenye tawi nikiendelea kuwaza nikasikia majani yakichakachika juu ya ule mti kama vile kulikuwa na kitu kinatambaa.
Nikainua uso wangu juu kutazama kulikuwa na nini.
Nikashituka. Niliona kichwa cha joka kikiwa karibu yangu kabisa. Kumbe katika ule mti niliokuwa nimeupanda kulikuwa na joka ambalo sikuliona.
Kile kiatu cha Zena nilikuwa nacho mkononi, nikakipiga kile kichwa. Nikadhani lile joka lingeniangukia lakini pale pale lilitoweka. Sikuliona tena.
Nikagundua kuwa licha ya Zena kunikimbia alikuwa ameniachia silaha ya maana sana.
Nikaangaza angaza juu ya ule mti kuona kama kulikuwa na joka jingine. Sikuona joka.
Hata hivyo sikuamini. Kila wakati nilikuwa natazama tena.
Kiza kiliendelea kushamiri na baridi ilizidi kuwa kali lakini sikuwa na la kufanya. Nilibaki kutetemeka tu.
Nilijiambia kama nitakufa pale kisiwani maiti yangu haitapatikana. Mama yangu na kaka yangu hawatajua nimepotelea wapi na hawatajua kuwa mwenzao ni marehemu.
Eti wakati nawaza vile nikapitiwa na usingizi ghafla. Nikalala pale pale juu ya mti bila kujitambua.
Nikaota nimelala chumbani kwangu, mara nikaona mwanamke ametokea kwenye dirisha langu lakini alikuwa kama kivuli. Sikuweza kumuona sura yake. Akaniambia.
“Ni mpaka uirithi pete ya Sulaiman Dauud na hutairithi mpaka uishuhudie damu ya kaka yako ikimwagika”
Hapo hapo nikazinduka. Ile ndoto haikuwa ngeni kwangu nakumbuka katika kipindi cha mwaka mmoja nilishaiota zaidi ya mara tatu. Lakini sikujua maana yake.
Wakati nazinduka niliona mawingu yakianza kun’gaa. Kumbe kulikuwa kunanaanza kupambazuka. Nikatambua kuwa nililala usiku kucha pale juu ya mti ingawa niliona nililala kwa muda mfupi.
Wakati naangaza macho baharini nikaona boti moja kubwa inakuja kwa kasi. Nikashukuru ingawa sikujua ilikuwa boti ya kina nani.
Boti ile ilikuja hadi maji madogo ikatia nanga. Nikaona watu watano wanashuka na kutembea kuelekea ufukweni. Walikuwa wamesega suruali zao ili zisitote.
Mmoja wa watu hao alikuwa amebeba tenga kubwa kichwani. Nikasikia sauti kama ya mlio wa mbuzi.
Watu hao walipofika ufukweni walitembea hadi kwenye ule msitu. Yule aliyebeba tenga akalitua chini. Ule mlio wa mbuzi uliendelea kusikika.
Nikaona mbuzi mweusi anatolewa kwenye tenga hilo. Sikuweza kuona vizuri kilichokuwa kinaendelea isipokuwa niliona kama walikuwa wanamchinja yule mbuzi na kumuacha pale chini.
Nikapata hisia kwamba watu hao walikuwa wanafanya kafara lakini ghafla nikaona wanaingia katika ule msitu.
Baada ya muda wa kama nusu saa hivi wakaanza kutoka mmoja mmoja lakini kila aliyetoka alikuwa amebeba pembe nne za ndovu.
Walikwenda nazo kwenye ile boti wakazipakia kisha wakarudia zingine.
Walirudia mara kumi, zilikuwa pembe nyingi sana. Ile mara ya kumi waliobeba pembe walikuwa watu wawili. Nikahisi walikuwa wamemaliza pembe zao na kwamba walikuwa wanakwenda zao.
Nikadhania tu kuwa wale watu walikuwa wafanya magendo na walikuwa wakificha pembe zao katika kisiwa kile.
Nikaona nisiipoteze ile nafasi ingawa sikujua watu wale walikuwa wanaelekea wapi.
Nikashuka haraka kwenye ule mti na kuwakimbilia.
“Jamani naomba mnichukue!” nikawa nawapigia kelele.
Watu hao walipoona ninawafuata huku nikiwaomba msaada wakasimama na kunisubiri.
Nilipowafikia, mtu mmoja mfupi aliyekuwa amevaa pama jeusi akaniuliza.
“Wewe nani na umetokea wapi?”
“Mimi ni mwananchi niliyekuwa natokea Pemba nikielekea Dar kwa boti inayokwenda kasi ambayo ilizama jana” nikamwambia.
“Boti ilizama jana mbona wewe upo hadi leo”
“Nilinusurika baada ya kuogelea….”
Kabla sijamaliza kile nilichotaka kumueleza akanikatiza.
“Ulifuata nini kwenye kisiwa hiki?”
“Niliogelea hadi nikafika hapa”
“Tangu jana ulikuwa unafanya nini hapa?”
“Nilikuwa nimekaa tu nikisubiri msaada”
“Wewe ni muongo sana!”
“Hapana. Ninachokieleza ni ukweli mtupu”
“Wewe ni mpelelezi siyo, umekuja kutupeleleza sisi?”
“Hapana, hapana. Mimi siwajui, nimewaona tu hapa. Ninachoomba ni msaada wenu tu”
“Haya twende tukaingie kwenye boti”
“Asante bwana, nakushukuru sana kwa maana nilikuwa sijui ningefikaje Tanga”
Nilifuatana na wale watu hadi kwenye boti yao nikajipakia. Yule mtu aliyekuwa akinihoji ambaye alionekana kama mwenye mali alikuwa akiamrisha kila kitu ndani ya ile boti.
Safari ikaanza. Nikadhani kwamba nilikuwa nimenusurika. Sikujua tulikuwa tunaelekea wapi na jinsi nilivyowaona watu wenyewe ni wakali nilishindwa kuwauliza.
Nilikuwa nimeshaamua popote watakaponifikisha patatosha. Kama watanirudisha Pemba au kama watakwenda Unguja au Dar itakuwa sawa.
Boti iliendelea na safari kwa kasi. Kitu kilichonishitua ni kwamba baada ya kukiacha kile kisiwa, yule mtu aliyekuwa amevaa pama jeusi alikwenda kukaa peke yake akatoa bangi na kuanza kuvuta.
Moshi wa bangi ulienea kwenye boti ukawa unaniumiza kichwa lakini yule mtu hakujali kabisa. Alikuwa akiendelea kuvuta tu.
Baada ya kwenda mwendo wa karibu kilometa thelathini tukaona boti nyingine inatufuata. Wale watu walipoiona ile boti walishituka.
Yule mtu aliyevaa pama akakitupa kipisi cha bangi baharini kisha akanitazama na kuniambia.
“Polisi wenzako wanatufuata, mimi nilishajua kuwa wewe ni mpelelezi!”
“Polisi gani?” nikamuuliza.
MAMBO YANAZIDI KUPAMBA MOTO! SI MCHEZO!
 
SEHEMU YA 42


ILIPOISHIA
Kabla sijamaliza kile nilichotaka kumueleza akanikatiza.
“Ulifuata nini kwenye kisiwa hiki?”
“Niliogelea hadi nikafika hapa”
“Tangu jana ulikuwa unafanya nini hapa?”
“Nilikuwa nimekaa tu nikisubiri msaada”
“Wewe ni muongo sana!”
“Hapana. Ninachokieleza ni ukweli mtupu”
“Wewe ni mpelelezi siyo, umekuja kutupeleleza sisi?”
“Hapana, hapana. Mimi siwajui, nimewaona tu hapa. Ninachoomba ni msaada wenu tu”
“Haya twende tukaingie kwenye boti”
“Asante bwana, nakushukuru sana kwa maana nilikuwa sijui ningefikaje Tanga”
Nilifuatana na wale watu hadi kwenye boti yao nikajipakia. Yule mtu aliyekuwa akinihoji ambaye alionekana kama mwenye mali alikuwa akiamrisha kila kitu ndani ya ile boti.
Safari ikaanza. Nikadhani kwamba nilikuwa nimenusurika. Sikujua tulikuwa tunaelekea wapi na jinsi nilivyowaona watu wenyewe ni wakali nilishindwa kuwauliza.
Nilikuwa nimeshaamua popote watakaponifikisha patatosha. Kama watanirudisha Pemba au kama watakwenda Unguja au Dar itakuwa sawa.
Boti iliendelea na safari kwa kasi. Kitu kilichonishitua ni kwamba baada ya kukiacha kile kisiwa, yule mtu aliyekuwa amevaa pama jeusi alikwenda kukaa peke yake akatoa bangi na kuanza kuvuta.
Moshi wa bangi ulienea kwenye boti ukawa unaniumiza kichwa lakini yule mtu hakujali kabisa. Alikuwa akiendelea kuvuta tu.
Baada ya kwenda mwendo wa karibu kilometa thelathini tukaona boti nyingine inatufuata. Wale watu walipoiona ile boti walishituka.
Yule mtu aliyevaa pama akakitupa kipisi cha bangi baharini kisha akanitazama na kuniambia.
“Polisi wenzako wanatufuata, mimi nilishajua kuwa wewe ni mpelelezi!”
“Polisi gani?” nikamuuliza.
SASA ENDELEA
“Utawaona sasa hivi”
Mazungumzo ya polisi yakaanza ndani ya boti huku wale watu wakinishutumu mimi kuwa ni mpelelezi niliyekuwa nimetumwa katika kile kisiwa kuwachunguza.
Kumbe ile boti iliyokuwa inatufuata ilikuwa boti ya polisi wanamaji iliyokuwa kwenye doria.
Upande mmoja wa moyo wangu nilipata hofu lakini kwa upande mwingine nilipata matumaini. Nilipata hofu kutokana na zile shutuma nilizokuwa ninazipata kutoka kwa wale watu kuwa mimi ni mpelelezi. Na nilipata matumaini kujua kuwa kulikuwa na polisi wanatufuata.
Sikuwa na hofu na polisi hao kwa sababu sikuhusika na wafanya magendo hao ambao hata sikujua walikuwa wanaelekea wapi.
Kadiri ile boti ilivyokuwa inatukaribia wale watu walikuwa wakihaha huku wakitukana.
Boti ya polisi ilipotufikia polisi wanne waliingia kwenye ile boti. Polisi mmoja alikuwa ameshika bunduki.
“Mnakwenda wapi?” Polisi aliyeshika bunduki akatuuliza.
Polisi hao hawakupata jibu. Jamaa wote walikuwa kimya.
Katika kukagua kagua ndani ya ile boti, polisi hao wakaziona zile pembe za tembo.
“Kuna meno ya tembo mengi sana wanayasafirisha!” Polisi mmoja akawapigia kelele polisi wengine waliokuwa kwenye boti ya pili.
Yule mtu aliyevaa pama aliingia kwenye kijichumba kilichokuwa ndani ya boti hiyo. Muda ule ule alitoka akiwa ameshika kitu kama chupa kubwa iliyokuwa na utambi uliokuwa ikiwaka moto, akairusha ile chupa kuelekea kwenye boti ya polisi. Ile chupa ilipotua chini ililipuaka kama bomu.
Kitendo kile kilinishitua. Mara moja ile boti ya polisi ililipuka moto. Wale polisi walioingia kwenye boti niliyokuwemo walikuwa wameduwaa. Hapo hapo wakavamiwa na wale watu, wakapigwa na kufungwa kamba. Yule polisi aliyekuwa na bunduki alinyanganywa bunduki yake.
Jambo lililonishitua zaidi ni kuwa hata mimi nilikamatwa nikafungwa pamoja na polisi hao.
“Tutakwenda kuwatosa huko mbele ya safari” aliyekuwa amevaa pama akatuambia.
“Lakini mimi ninahusikaje, mimi niliwaomba msaada tu kwanini mnataka kwenda kunitosa?” nikawalalamikia.
“Wewe ndio mpelelezi uliyekuwa ukitoa taarifa kwa wenzako. Pale nilipokuwa nakupakia nilishakupangia kwenda kukutosa” Mwenye pama akaniambia.
“Balaa gani hili jamani linalonikuta. Jana nilikaribia kufa, leo tena balaa jingine linaningoja. Nimekosa nini jamani!” nikalalamika peke yangu.
Wakati huo ile boti ya polisi tulishaiacha mbali ikiendelea kuwaka.
Mpaka jua linafika utosini ikiashiria ilikuwa saa sita mchana, boti ya watu hao ambao sasa niliwahisi walikuwa majambazi ilikuwa ikiendelea kukata maji.
Nilikuwa nimeshafuta mawazo kwamba tulikuwa tunaelekea katika miji iliyokuwa karibu kama Pemba au Unguja. Nilihisi kwamba tulikuwa tunaelekea mahali kwingine kusikojulikana.
Hofu ya kuuawa ilikuwa imenitawala. Wakati wote moyo wangu ulikuwa ukienda mbio. Sikujua kwamba tungeuawa au tungetoswa baharini saa ngapi.
Mara nikamuona yule mtu aliyekuwa amevaa pama akitoka kwenye kile chumba kilichokuwamo ndani ya boti, akawambia wenzake.
“Eneo hili lina papa wengi, tuwatose hapa hapa”
Kauli yake ile ilinishitua. Ilikuwa kama nyundo ya moto iliyopigwa kwenye moyo wangu.
Mapama aliposema hivyo aliwaagiza watu watatu wamuinue polisi mmoja na kumtosa. Polisi huyo alilalamika kuomba asitoswe lakini hakukuwa na aliyekuwa akimsikiza. Jamaa hao walimbeba na kumtosa baharini akiwa amefungwa kamba miguu na mikono.
Mara moja tukaona damu kwenye eneo lile la bahari. Kipande kimoja cha mwili wa polisi huyo kiliibuka juu na kwenda na maji. Bila shaka kipande kingine kilikuwa kimeshamezwa na papa.
Hapo hapo tukamuona papa upanga akibuka kutoka chini ya bahari na kuking’ata kipande kingine cha ule mwili na kuzama nacho baharini.
Tayari jamaa hao walikuwa wameshambeba polisi wa pili ambaye kama mwenzake alikuwa akilalamika bila kusikilizwa, naye akatoswa.
Polisi wa tatu naye akatoswa. Nikabaki mimi na polisi mmoja. Nilikuwa nikiomba toba kimoyomoyo ili nipate msamaha huko ahera ninakokwenda.
Machozi yalikuwa yametosa kifua changu na yalikuwa yakiendelea kunitoka hasa nilivyoona vipande vya miili ya wale polisi ilivyokuwa ikidakwa na papa.
Wale jamaa wakatufuata tena.
Sikujua ilikuwa zamu ya nani, mimi au yule polisi?
Jibu nililipata baada ya nusu dakika. Watu hao wakamshika mwenzangu. Bila shaka mimi waliniweka mwisho. Polisi huyo alibebwa juu juu. Ingawa alikuwa akipiga kelele, hakukuwa na aliyemjali. Kiasi cha kufumba na kufumbua tu akawa ametoswa baharini. Kwa vile alikuwa mnene na mzito kuliko wenzake waliokuwa wametoswa, alisababisha kishindo kukubwa, maji ya bahari yakaruka na kuingia kwenye boti!
Wakati wote nilikuwa na matumaini kuwa wangewatosa wale polisi kwa kuamini kuwa mimi sikuwa mwenzao na ndio maana waliniacha.
Lakini matumaini yangu yaliyayuka mara tu nilipowaona wale watu wakinifuata mimi baada ya kumtosa yule polisi wa mwisho,
Nilipoona wananishika nikawambia.
“Jamani, jamani mimi nina kosa gani. Kuwaomba msaada ndio kosa, mnataka mniue”
Hawakunijibu na hawakuonesha kama walihitaji kunijibu, Walinibeba kama walivyowabeba wenzangu. Vile ambavyo mwili wangu haukuwa mzito walinichota kama takataka. Wakanipeleka kwenye ukingo wa boti.
Kufika hapo waliniinua juu wakahesabu moja...mbili…
Kabla hawajafika tatu, kuliibuka kitu kilichotokea baharini. Kiliibuka kwa nguvu na kwa kishindo huku kikitoa mlio uliofanana na mlio wa fataki iliyorushwa.
Yale maji yaliyorushwa juu na kitu hicho yalitutosa wote. Ghafla kitu hicho kikatuvamia. Mimi niliachiwa nikaangukia ndani ya boti. Wale watu pia walianguka na kulaliwa na kitu hicho kizito kilichotua ndani ya boti.
Nilikuwa nimefungwa kamba mikono na miguu. Nilipoanguka sikuweza kusimama ila niliweza kujigeuza ili nikione kitu hicho kilichoibuka kutoka baharini na kuvamia ndani ya boti ile.
Nilishindwa kuamini macho yangu! Lilikuwa dude kubwa kama joka lililokuwa na mikono yenye vidole vyenye kucha ndefu. Urefu wake ulikuwa kama guzo la umeme. Lilipokuwa ndani ya ile boti lilikuwa limejikunja. Mwili wake ulikuwa na magamba makubwa kama ya samaki.
Kwa kutumia kucha zake lilimvamia mtu mmoja na kuruka naye juu kisha likajitosa baharini likiwa na mtu huyo.
Sote tulikuwa tumetaharuki na hatukujua ni jambo gani lilitaka kutokea. Wakati wale watu wanajiinua pale chini, joka hilo likaibuka tena likiwa halina mtu. Likavamia mtu mwingine na kuruka naye kisha likajitosa baharini.
Watu hao wakawa wanapigana vikumbo ndani ya boti kutafuta pa kujificha. Kutahamaki joka hilo likatokea tena, likamnyakua mtu mwingine na kuzama naye chini ya bahari. Watu wote wakamalizwa nikabaki mimi na Mapama
Mapama alikuwa akihangaika akijua kwamba joka hilo litaibuka tena na kumchukua yeye.lakini dakika zikapita hatukuliona. Kwa sababu ya hofu na kujiona amebaki peke yake mtu huyo alikuja kunifungua zile kamba.
“Njoo huku” akiniambia akitangulia kuingia katika kile kijichumba kilichokuwa ndani ya ile boti.
Nikainuka na kumfuata. Mikono yangu ilikuwa imekufa ganzi kutoka na kufungwa kamba kwa muda mrefu. Nikawa ninainyooshanyoosha.
Ndani ya chumba hicho kulikuwa na kioo cha kutazamia mbele. Pia kulikuwa na sukani na mitambo ya boti.
“Samahani bwana, naona tumebaki sisi wawili tu. Sijui lile lilikuwa joka gani na limetokea wapi?” Mapama akaniambia kwa hofu.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 43


ILIPOISHIA
Nilishindwa kuamini macho yangu! Lilikuwa dude kubwa kama joka lililokuwa na mikono yenye vidole vyenye kucha ndefu. Urefu wake ulikuwa kama guzo la umeme. Lilipokuwa ndani ya ile boti lilikuwa limejikunja. Mwili wake ulikuwa na magamba makubwa kama ya samaki.
Kwa kutumia kucha zake lilimvamia mtu mmoja na kuruka naye juu kisha likajitosa baharini likiwa na mtu huyo.
Sote tulikuwa tumetaharuki na hatukujua ni jambo gani lilitaka kutokea. Wakati wale watu wanajiinua pale chini, joka hilo likaibuka tena likiwa halina mtu. Likavamia mtu mwingine na kuruka naye kisha likajitosa baharini.
Watu hao wakawa wanapigana vikumbo ndani ya boti kutafuta pa kujificha. Kutahamaki joka hilo likatokea tena, likamnyakua mtu mwingine na kuzama naye chini ya bahari. Watu wote wakamalizwa nikabaki mimi na Mapama
Mapama alikuwa akihangaika akijua kwamba joka hilo litaibuka tena na kumchukua yeye.lakini dakika zikapita hatukuliona. Kwa sababu ya hofu na kujiona amebaki peke yake mtu huyo alikuja kunifungua zile kamba.
“Njoo huku” akiniambia akitangulia kuingia katika kile kijichumba kilichokuwa ndani ya ile boti.
Nikainuka na kumfuata. Mikono yangu ilikuwa imekufa ganzi kutoka na kufungwa kamba kwa muda mrefu. Nikawa ninainyooshanyoosha.
Ndani ya chumba hicho kulikuwa na kioo cha kutazamia mbele. Pia kulikuwa na sukani na mitambo ya boti.
“Samahani bwana, naona tumebaki sisi wawili tu. Sijui lile lilikuwa joka gani na limetokea wapi?” Mapama akaniambia kwa hofu.
SASA ENDELEA
“Nadhani limekuja kuwaua kutokana na ule unyama wenu wa kututosa baharini bila hatia”
“Sio mimi, ni wale jamaa. Mimi sikuweza kuwazuia”
Nikaona yule mtu alikuwa akijitetea kwa kusema uongo wakati yeye ndiye aliyeamrisha tutoswe.
Sikutaka kumsuta kwa sababu hata mimi nilikuwa nimepata hofu na sikuwa nikijua hatima yangu.
“Lakini sidhani kama litakuja tena” nikamwambia kumpa moyo. Hata hivyo nilijisemea tu bila kuwa na uhakika.
Mapama alikuwa akiendesha lile boti huku akiwa matu matu. Kila mara alikuwa akitupa macho pande zote za boti. Nilijua alikuwa akihofia lile joka ambalo hata mimi liliniweka katika hali ya wasiwasi.
“Tuombe Mungu. Tukinusurika tutatajirika” Mapama akaniambia.
“Kwani tunaelekea wapi?” nikamuuliza.
“Tunakwenda Somalia”
“Kumbe mlikuwa mnakwenda Somalia?”
“Mnunuzi wa hizi pembe yuko Somalia, ndio tulikuwa tunampelekea”
“Ni mali ya nani?”
“Mwenyewe yuko Dar. Mimi ndiye msimamizi wake na mmiliki wa hii boti. Mara kwa mara ananituma kupeleka pembe zake Somalia”
“Huwa mnazihifadhi kwenye kile kisiwa?”
“Pale ndio tunazificha tunapozikusanya kutoka kwa majangili”
“Mnapokwenda pale mnachinja mbuzi kwa ajili ya nini?’
“Kile kisiwa kinakaa majini. Hivyo tunapofika tunawapa kafara ili wasitudhuru. Na wewe ulifuata nini pale?”
“Pale nilifika jana kwa kogelea. Mimi nilikuwa ninatoka Pemba kwenda Dar. Boti yetu ilizama.”
“Ndiyo nilisikia. Kwa hiyo ulilala pale pale?’
“Ndiyo nililala juu ya mti. Sasa nilipowaona leo asubuhi nikawafuata kuwaomba msaada lakini inaelekea hamkunielewa”
“Unajua hii kazi ni ya siri na ya hatari, wale wenzangu walipokuona walidhani wewe ni mpelelezi ulikwenda pale kufanya uchunguzi”
Jamaa yule alikuwa akiwasingizia wenzake kila kitu wakati yeye ndiye aliyekuwa akinituhumu.
“Sasa ukifika Somalia unarudi lini huku Tanzania”
“Tukifika tu tunapakua huu mzigo na kuupakia kwenye boti nyingine halafu tunarudi”
“Hiyo boti tutaikuta wapi?”
“Tukiingia Somalia tu tunaikuta inatusubiri”
“Halafu hizi pembe zinapelekwa wapi?’
“Zinasafirishwa kwa meli na kupelekwa nchi za kiarabu. Waarabu wanatengezea mipini ya majambia”
Sikuwa nikijua kuwa pembe za ndovu hutengezwa mipini ya majambia. Hata hivyo niliyaacha yale mazungumzo ya pembe. Dukuduku langu lilikuwa ni kurudi nyumbani.
“Tutafika leo huko Somalia?” nikamuuliza.
“Hapa tuko katika bahari ya Mombasa nchini Kenya. Mpaka ikifika saa kumi na moja alfajiri tutaingia Somalia”
“Eh! Kumbe safari bado ni ndefu?”
“lakini tumeshafika nusu ya safari yetu”
“Kama ni kurudi itakuwa kesho”
“Kesho si mbali. Sasa hivi jua litakuchwa, usiku utaingia”
Mapama aliposema hivyo alitoa kicheko cha kujilazimisha akaondoka kwenye sukani baada ya kuitegesha muelekeo aliokuwa anautaka. Akafungua kabati lililokuwa humo ndani na kutoa sufuri iliyokuwa imefunikwa.
Aliiweka kwenye kimeza kisha akafunua ule mfiniko. Ndani ya sufuria hiyo mlikuwa na pilau na vipande vya nyama. Sijui ilikuwa nyama ya nini.
Akapakua ile pilau kwenye sahani na kuniambia.
“Tule”
Kusema kweli nilikuwa na njaa lakini zile nyama ziliniogopesha kwa sababu zilikuwa nyingi na sikujua zilikuwa nyama za mnyama gani kwani zilikuwa na mafuta mengi.
“Hizi ni nyama za nini?” nikamuuliza.
“Nyama ya nyati, ni tamu sana. Hebu onja”
Aliokota kipande cha nyama bila kuosha mkono akanipa.
Alinishangza sana. Mikono yake ilikuwa imeshika kila kitu. Imeshika magwanda ya polisi waliowatosa baharini. Imeshika mapembe ya ndovu. Imeshika sukani ya boti. Imeshika bangi…loh! Hawa watu wachafu kweli!
Alipoona nimesita nikimtazama akagutuka na kuinuka.
“Ngoja nioshe mkono” akaniambia.
Aliosha mkono kwa kutumia maji yaliyokuwa yamewekwa kwenye dumu.
“Na wewe njoo uoshe mikono yako” akaniambia.
Wakati wote nilikuwa nikisema na moyo wangu kuhusu kile chakula. Nilikuwa nikijiuliza nile kile chakula au nisile. Ukweli ni kwamba nilikuwa na njaa na njaa haina ustaarabu. Ikikushika unaweza kula hata kisocholika. Japokuwa kwanza nilisita sita lakini hatimaye niliinuka kwenda kuosha mikono.
Baada ya kuosha mikono tukarudi pale tulipokuwa.
“Kula” Mapama akaniambia.
Tukaanza kula. Pilau ilikuwa ikinuka moshi wa kuni. Nikahisi kwamba waliipika wao wenyewe kwa kutumia kuni walizoziokota fukweni mwa bahari..
Kwa sababu ya njaa niliyokuwa nayo nilikula sana mpaka nikahisi kwammba ningevimbiwa. Pilau ilikuwa nyingi hatukuimaliza.
Nilimuacha Mapama akiendelea kula.
“Ukiwa katika hali ya baridi unatakiwa ule sana” Mapama aliniambia.
Tonge zake zilikuwa kubwa na nilihisi alikuwa akimeza bila kutafuna.
Alipotosheka na yeye aliiacha. Akairudisha sinia kwenye kabati.
Baada ya kuosha mikono Mapama alinipa maji ya kunywa nikayanywa. Na yeye akanywa.
“Sasa baridi hatutaisikia. Tunaweza kuendelea na safari” Mapama akaniambia.
Tukakaa na kuendelea kuzungumza. Mara moja moja alikuwa akitazama mitambo. Nilikuwa nimejifunza kwamba boti haikuwa ikiendeshwa kama gari.
Haihitaji kushikiliwa sukani wakati wa kuendesha. Unaweza kuweka muelekeo wako na ukaiacha iende yenyewe.
Ndivyo Mapama alivyokuwa akifanya. Hatimaye Mapama alianza kusinzia. Alikuwa akisinzia huku akishituka.
“Nikuache uangalie, mimi najinyoosha kidogo” akaniambia.
Nikajua kuwa pilau aliyokuwa ameila kwa wingi ilikuwa imemlewesha.
“Wewe lala, baadaye nitakuamsha” nikamwambia.
Mapama akajitupa chini. Baada ya muda kidogo nilimsikia akikoroma.
Huku boti ilikuwa ikiendelea na safari. Masaa yalipita. Saa yangu ilikuwa imesimama kutokana na kuingia maji ya chumvi, sikuweza kujua ilikuwa saa ngapi.
Je nini kitatokea?
 
SEHEMU YA 44


ILIPOISHIA
Kwa sababu ya njaa niliyokuwa nayo nilikula sana mpaka nikahisi kwammba ningevimbiwa. Pilau ilikuwa nyingi hatukuimaliza.
Nilimuacha Mapama akiendelea kula.
“Ukiwa katika hali ya baridi unatakiwa ule sana” Mapama aliniambia.
Tonge zake zilikuwa kubwa na nilihisi alikuwa akimeza bila kutafuna.
Alipotosheka na yeye aliiacha. Akairudisha sinia kwenye kabati.
Baada ya kuosha mikono Mapama alinipa maji ya kunywa nikayanywa. Na yeye akanywa.
“Sasa baridi hatutaisikia. Tunaweza kuendelea na safari” Mapama akaniambia.
Tukakaa na kuendelea kuzungumza. Mara moja moja alikuwa akitazama mitambo. Nilikuwa nimejifunza kwamba boti haikuwa ikiendeshwa kama gari.
Haihitaji kushikiliwa sukani wakati wa kuendesha. Unaweza kuweka muelekeo wako na ukaiacha iende yenyewe.
Ndivyo Mapama alivyokuwa akifanya. Hatimaye Mapama alianza kusinzia. Alikuwa akisinzia huku akishituka.
“Nikuache uangalie, mimi najinyoosha kidogo” akaniambia.
Nikajua kuwa pilau aliyokuwa ameila kwa wingi ilikuwa imemlewesha.
“Wewe lala, baadaye nitakuamsha” nikamwambia.
Mapama akajitupa chini. Baada ya muda kidogo nilimsikia akikoroma.
Huku boti ilikuwa ikiendelea na safari. Masaa yalipita. Saa yangu ilikuwa imesimama kutokana na kuingia maji ya chumvi, sikuweza kujua ilikuwa saa ngapi.
SASA ENDELEA
Mawazo yangu yalikuwa ni kurudi kwetu salama. Nilijiambia Zena alikuwa amenifikishia mkasa wa kutatanisha sana ambao sikutegemea kama ungenitokea.
Niliamini kuwa siku zangu za kufa bado zilikuwa mbali, vinginevyo ningelikwishakufa.
Kama nisingekufa kwenye ile ajali ya meli, ningekufa wakati Zena ananikokota baharini. Na kama nisingekufa baharini, ningekufa kwenye kile kisiwa chenye majoka na baridi.
Lakini bado, japo nilinusurika kote, wale washenzi wenye ile boti wangeniua kama walivyowaua wale polisi waliowatosa. Na kama hawakuniua ningeuliwa na lile joka lililowaua watu wote na kumbakisha Mapama na mimi. Mpaka muda ule nilishindwa kujua joka lile lilitoka wapi na pia nilishindwa kujua jinsi nilivyonusurika
.
Kusema kweli niliona kunusurika kwangu kulikuwa kwa ajabu sana.
Wakati nikiwa kwenye mchanganyiko huo wa mawazo huku macho yangu yakitazama mbele tunakoelekea, niliona kitu kama kimulimuli kikielekea upande wetu. Nikashituka na kuangaza macho vizuri.
“Nini kile?” nikawa najiuliza kimoyo moyo.
Baadaye kidogo niligundua kuwa ilikuwa boti iliyokuwa na kimuli muli na ilikuwa na maandishi yaliyosomeka POLISI KENYA.
“Mama yangu we!”
Kwa haraka nikamuamsha Mapama.
“Hebu amka uone!”
“Nini?” Mapama aliniuliza akiwa bado amefumba macho.
“Polisi. Kuna boti ya polisi inatuufuata. Amka!” nikamwambia.
“Polisi?”
“Tunafuatwa na boti ya polisi!”
Mapama akainuka.
“Iko wapi?” akaniuliza.
“Inakuja, imewasha kimulimuli. Simama uione”
Mapama akainuka na kuitazama ile boti kwenye kioo. Nilidhani angeanza kubabaika kama nilivyokuwa nikibabaika mimi. Badala yake nilimuona akiizima boti na kujipekua mifukoni. Alitoa burungutu la pesa za Kenya akalishika mkononi.
“Usiogope” akaniambia na kuongeza.
“Watakwenda zao sasa hivi”
Ile boti ya polisi ikatufikia. Ikawa ubavu kwa ubavu na boti yetu. Mapama akalirusha lile burungutu la noti kwenye ile noti. Polisi mmoja akalidaka. Hapo hapo nilimsikia akisema.
“Safari njema”
Mapama akaiwasha boti. Tukaendelea na safari. Ile boti nayo ikaelekea upande mwingine.
“Wale wanataka pesa tu” Mapama akaniambia na kuongeza.
“Kila tunapokuja huku tajiri wetu anatupa pesa maalum kwa ajili ya kuwapa polisi wa Kenya wanaofanya doria baharini. Wao wenyewe wanajua, wakiiona hii boti wanafuata pesa tu. Hawakagui kitu”
“Mimi nilikuwa na wasiwasi sana. Nilijua tutaishia polisi”
“Hapana. Hizi ni kazi zetu za kila siku, lazima tujuane na polisi. Huwezi kuvuka kwenda Somalia bila kukupamba nao”
“Kile kimulimuli kilinitisha kweli”
“Ile ni mikwara tu ya kutaka pesa. Hebu iangalie kama utakiona tena kimulimuli”
Nikatazama upande ule ilikoelekea ile boti. Sikuona kimulimuli wala sikuiona boti yenyewe.
“Boti yenyewe haionekani tena”
“Ni kwa sababu wamekizima kimulimuli”
“Huko Somali itakuwaje sijui?”
“Hakuna tatizo. Huyo tunaempelekea huu mzigo ni mtu mzito sana. Serikali pia inamjua”
Baada ya hapo tukabaki kimya.
Hatimaye aflfajiri ilianza kuchomoza. Sikuona dalili yoyote ya kufika Somalia. Usingizi ukaanza kuniuma.
“Uliniambia tutaingia Somalia wakati wa alfajiri” nikamwambia Mapama.
“Bado kidogo, usiwe na wasiwasi”
“Nasikia usingizi” nikamwambia.
“Lala kidogo”
Nikajilaza pale chini. Usingizi ukanichukua hapo hapo.
Mpaka nakuja kuzinduka lilikuwa jua la utosi. Mapama ndiye aliyeniamsha. Boti ilikuwa imesimama na kulikuwa na boti nyingine kubwa iliyokuwa imesimama kando ya ile boti tuliyokuwamo. Ilikuwa boti kubwa na nzuri.
“Tumeshafika?” nikamuuliza Mapama.
Sikujua kabisa kuwa Mapama angenigeuka na kunisaliti kwa magaidi..
Bila shaka, zile boti ndio zilikuwa zimekutana. Ile boti ya pili ilikuwa ndiyo ile ambayo Mapama aliniambia tutakutana nayo tutakapoingia Somallia ili ifaulishe ule mzigo wa pembe za ndovu.
Wakati ule namuuliza Mapama kama tumeshafika, niliona mtu mmoja akitoka katika boti ile ya pili na kuingia katika boti ya Mapama. Alikuwa kijana. Ingawa alikuwa mwembamba alionekana kunawiri na alivaa mavazi yalliyompendeza japo shati alilovaa lilionekana kubwa kutokana na wembamba wake.
Alikuwa Msomali mweusi mwenye nywele za singa. Mkono mmoja alikuwa ameshika kichanga cha mirungi aliyokuwa akitafuna na mkono mwingine alishika sigara iliyokuwa ikifuka moshi.
Katika kiganja cha mkono wake wa kushoto alivaa pete kubwa iliyokuwa inang’ara.
Niliukadiria umri wake kutozidi miaka thelathini na mitano. Alikuwa amenizidi kiumri kidogo.
Kijana huyo alisalimiana na Mapama aliyekutana naye nje ya kile kijichumba nilichokuwemo. Nilimshangaa Mapama kwa jinsi alivyokuwa ametaharuki kiasi kwamba alipuuza hata kunijibu nilipomuuliza kama tumeshafika. Alikuwa amebadilika kabisa. Niliona kama hakuwa mwenzangu tena.
Aliposalimiana na yule msomali alimuonesha ule mzigo wa Pembe. Msomali huyo aliutazama kisha akamuuliza.
“Wenzako wako wapi?”
“Nilikuja nao lakini tulipata matatizo makubwa”
“Matatizo gain?”
“Nitakueleza. Wambie jamaa wafaulishe huu mzigo”
Msomali huyo alitumia lugha ya kisomali kuwambia wasomali wenzake waliokuwa katika ile boti ya pili waingie katika boti ya Mapama na kufaulisha ule mzigo. Wasomali hao walioonekana kama wapagazi wakaingia na kuanza kazi.
Mapama na yule msomali niliyemdhania kuwa ndiye tajiri wa ule mzigo wakaingia katika ile boti nyingine. Sikujua walikwenda kuzungumza nini. Baada ya muda Mapama alirudi peke yake na kuniambia.
“Yule jamaa anataka kukuona?”
“Jamaa gani?” nikamuuliza.
“Yule msomali niliyekuwa nazungumza naye”
“Kwani mimi nahusikaje?”
“Sasa utakwenda au utaleta ubishi?” Mapama akaniuliza kwa ukali.
Kabla sijamjibu, Msomali mwenyewe akatokeza kwenye ile boti na kuninyooshea mkono kama ishara ya kuniita, nikaenda. Niliingia katika ile boti akanishika mkono na kuniingiza katika chumba kilichokuwa katika boti yake.
Chumba hicho kilikuwa kikubwa kuliko cha boti ya Mapama na kilikuwa kizuri kilichozungukwa na kuta za vioo. Ndani kilikuwa na sehemu ya kulala na makochi ya kukalia.
“Karibu, kaa hapo” Msomali akaniambia akinionesha moja ya makochi yaliyokuwa katika kile chumba.
Nikakaa.
“Asalaam alaykum” Msomali akaniambia huku akiketi upande wa pili wa chumba hicho.
“Waalaika Salaam” nikamjibu kwa sauti iliyonywea huku nikimtazama usoni kwake.
“Nimeelezwa na Nahodha kuhusu wewe na mkasa uliowatokea mlipokuwa mnakuja. Ameniambia kulitokea joka kama nondo na kuwaangamiza wenzake, ni kweli?”
“Ni kweli”
“Kwani walitaka kukufanya nini?”
“Walitaka kuniua”
“Wapumbavu wale, mtu unaomba msaada wanataka kukuua. Sasa hilo joka lilitoka wapi?”
Nikabetua mabega yangu.
“Sijui”
“Bila shaka hilo ndilo lililokuokoa usiuawe, ungekuwa umeshatoswa na kuliwa na papa”
Hapo sikumjibu kitu.
“Wewe unaitwa Umar?” Msomali akaniuliza.
“Hapana”
“Unaitwa Amiri?”
“Hapana”
“Basi utakuwa unaitwa Amour”
Nikamkubalia.
“Ndio naitwa Amour, umejuaje?”
Msomali huyo akacheka. Badala ya kunijibu akaniambia.
“Nataka twende Somali mara moja”
Nikashituka na kumuuliza.
“Kwani hapa tuko wapi?’
MAMBO HAYO! PANA FUMBO GANI HAPA?
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 45


ILIPOISHIA
Chumba hicho kilikuwa kikubwa kuliko cha boti ya Mapama na kilikuwa kizuri kilichozungukwa na kuta za vioo. Ndani kilikuwa na sehemu ya kulala na makochi ya kukalia.
“Karibu, kaa hapo” Msomali akaniambia akinionesha moja ya makochi yaliyokuwa katika kile chumba.
Nikakaa.
“Asalaam alaykum” Msomali akaniambia huku akiketi upande wa pili wa chumba hicho.
“Waalaika Salaam” nikamjibu kwa sauti iliyonywea huku nikimtazama usoni kwake.
“Nimeelezwa na Nahodha kuhusu wewe na mkasa uliowatokea mlipokuwa mnakuja. Ameniambia kulitokea joka kama nondo na kuwaangamiza wenzake, ni kweli?”
“Ni kweli”
“Kwani walitaka kukufanya nini?”
“Walitaka kuniua”
“Wapumbavu wale, mtu unaomba msaada wanataka kukuua. Sasa hilo joka lilitoka wapi?”
Nikabetua mabega yangu.
“Sijui”
“Bila shaka hilo ndilo lililokuokoa usiuawe, ungekuwa umeshatoswa na kuliwa na papa”
Hapo sikumjibu kitu.
“Wewe unaitwa Umar?” Msomali akaniuliza.
“Hapana”
“Unaitwa Amiri?”
“Hapana”
“Basi utakuwa unaitwa Amour”
Nikamkubalia.
“Ndio naitwa Amour, umejuaje?”
Msomali huyo akacheka. Badala ya kunijibu akaniambia.
“Nataka twende Somali mara moja”
Nikashituka na kumuuliza.
“Kwani hapa tuko wapi?’
SASA ENDELEA
“Hapa ni Somalia, nina maana nataka twende Mugadishu”
“Kufanya nini?”
“Nitakuwa na kazi na wewe”
“Mimi nataka kurudi. Nilishamwambia Nahodha akishafaulisha mzigo wake turudi”
“Sasa amri ni yangu mimi si ya Nahodha. Mimi nataka twende Mugadishu”
“Mimi sitakwenda huko”
Msomali huyo hakunisikiliza akainuka na kutoka katika kile chumba. Na mimi nikainuka na kumfuata.
Alipoona nimetoka alihamaki akaniuliza.
“Unataka kuleta ubishi?”
“Hapana”
“Nani amekuamrisha utoke?”
“Nilikwambia sitakwenda Mugadishu, nahitaji kurudi”
Msomali huyo hakusema kitu tena, alitia mkono ndani ya shati lake akatoa bastola na kunielekezea.
“Sasa chagua moja, nikutoe roho au baki kwenye hii boti!” akaniambia kwa hasira.
Nikanywea hapo hapo.
“Nenda kakae”
Ikabidi nirudi kwenye kile chumba. Nilijua kama nitaendelea kubishana naye anaweza kuniramba risasi. Wasomali hawa hawana huruma, kuna wengine hawana utu kabisa.
Nikakaa kinyonge kwenye kohi huku macho yangu yakimtazama yule Msomali kwa macho ya kulaani. Nikamuona mapama akiingia kwenye ile boti.
Akasimama na yule Msomali na kuzungumza naye kwa kirefu. Sikuweza kusikia walichokuwa wanazungumza. Mara moja moja Mapama alikuwa akinitazama. Nilikuwa nikimuonesha ishara ya kumuita ili nimuulize mbona ananigeuka.
Lakini Mapama licha ya kuona kuwa nilikuwa ninaashiria kumuita hakunijali hata chembe.
Pembe za ndovu zilikuwa zikiendelea kingizwa kwenye boti hiyo. Kazi ilipokwisha, Msomali aliingia katika kile chumba akafungua dawati mojawapo na kutoa mfuko ambao alitoka nao.
Ule mfuko ulikuwa na pesa. Sikujua zilikuwa pesa za wapi isipokuwa niliona Msomali akitoa vitita vya noti na kumhesabia Mapama. Mapama naye alizitia pesa hizo kwenye mfuko wa ngozi aliokuwa ameushika kisha nikaona wanaagana kwa furaha.
Hapo ndipo nilipotoa sauti nikamuita.
“Nahodha!”
Nilimuita zaidi ya mara tatu lakini hakunipatiliza akatoka kwenye ile boti na kuingia kwenye boti yake. Yule Msomali akaingia kwenye kile chumba. Bastola yake ilikuwa bado mkononi ingawa aliishika kwenye mtutu.
Boti ya Mapama ikawashwa moto. Nikajua kuwa Mapama alikuwa ameshaniuza kwa wasomali hao. Kwa lugha nyingine ilikuwa sawa na kusema kuwa Nilikuwa nimetekwa nyara na kupelekwa mahali bila hiyari yangu.
Boti ya Mapama ikaondoka, ilikata kona ndefu na kugeuka ilikotoka. Nikaachwa mikononi mwa wasomali.
Nilikuwa nimetaharuki na akili yangu iliniruka. Boti ya wasomali ikawashwa, nayo ikaondoka kuelekea Somalia.
Sikujua Mapama alikuwa amezungumza nini na yule msomali na pia sikujua walikuwa wananipeleka Somalia kwa ajili gani.
Pia nilikuwa nimeshangazwa na jinsi msomali huyo alivyolitambua jina langu ambalo sikuwahi kumtajia hata Mapama.
Kijana huyo wa kiosamali alikuja kukaa kando yangu na kuendelea kutafuna mirungi yake. Bastola yake aliipachika kiunoni. Bila shaka alifanya hivyo mbele yangu ili kunionya nisimletee ukaidi.
Lakini ukiacha muda ule aliponichomolea bastola hiyo ambapo alionesha kukasirika, uso wake ulikuwa wa kirafiki wakati wote.
“Mimi naitwa Abdi” akaniambia wakati akiendelea kutafuna mirungi kisha akaniuliza.
“Unakula mirungi?”
Nikatikisa kichwa. Mdomo ulikuwa mzito kumjibu.
“Najua wewe ni mzaliwa wa Tanga lakini sijui unaishi sehemu gani?” akaniuliza.
Swali lake hilo nalo lilinishangaza. Alijuaje kuwa mimi ni mzaliwa wa Tanga?
“Ninaishi sehemu inayoitwa Msambweni” nikamjibu.
“Wazazi wakao wako wapi?”
“Baba yangu alikwishakufa, mama yangu ndio yupo”
Msomali huyo alinikubalia kwa kichwa.
“Unafanya shughuli gani?”
“Nimeajiriwa katika shirika moja linaloitwa CTC”
“Najisikia ni mwenye furaha sana kukutana na mtu kama wewe”
“Umelitambuaje jina langu pamoja na mahali nilipozaliwa?” nikamuuliza.
Badala ya kunijibu aliangua kicheko.
“Nilikuwa nakisia tu kumbe nilipatia”
“Haiwezekani ukisie halafu iwe sawa”
“Amour sina jibu jingine la kukupa kwa sasa”
“Uliwahi kufika Tanga?”
Abdi akatikisa kichwa.
“Sijawahi”
“Kwanini unalazimisha twende Somalia?”
“Ni kwa sababu za kiudugu na kiurafiki tu. Utakuwa huko kwa muda tu halafu utarudi kwenu na kama utapenda kuendelea kuishi huko huko nitakupatia nyumba, kazi na gari”
“Kwa vyovyote vile itabidi nirudi, mama yangu na ndugu zangu hawajui niko wapi”
“Basi utarudi”
Boti iliendelea kusonga mbele. Baada ya mwendo wa kilometa tano hivi tukakutana na meli iliyokuwa imetia nanga. Boti ilikwenda kusimama ubavuni mwa meli.
Abdi aliniacha akatoka kwenye kile chumba. Kuna ngazi iliyoshushwa kutoka kwenye meli. Abdi alipanda ngazi hiyo akaingia ndani ya meli. Baada ya muda kidogo alishuka akiwa na maafisa wawili wa meli hiyo ambao niliwatambua kutokana na mavazi yao.
Waliyakagua yale meno ya tembo kisha nikaona krini ya meli inashushwa kutoka kwenye meli. Yale meno ya tembo yalikuwa yamepangwa kwenye turubai. Turubai hilo lilikuwa na vipete vinne vilivyowekwa kwenye pembe nne za turubai hilo. Kamba ikapitishwa kwenye vipete hivyo kisha ikapachikwa kwenye mkono wa krini.
Turubai likavutwa juu pamoja na pembe zake. Zilivutwa juu kuupita usawa wa meli kisha zikaingizwa ndani ya meli.
Abdi pamoja na wale maafisa wawili wa meli walirudi melini. Walipoteza muda wa karibu saa nzima kabla ya Abdi kurudi akiwa peke yake.
Aliingia kwenye kile chumba akiwa na mfuko uliotuna ambao aliuweka kwapani. Akafungua dawati mojawapo na kuuweka.
“Hizi ni pesa” akaniambia bila kumuuliza.
Sikumjibu kitu. Akarudi kuketi pale alipokuwa.
“Zile pembe zinakwenda Oman kwa waarabu” akaniambia lakini mimi bado nilikuwa kimya. Kitendo kile cha kunipaleka Mogadishu kwa lazima kilikuwa kimenifadhaisha sana.
Sikuwa nimeamini zile sababu zake kwamba alinipeleka kwa sababu za kiudugu na kiurafiki. Sikuwa na udugu naye wala urafiki naye na hatukuwa tukijuana zaidi ya kukutana siku ile.
Nilihisi kuna kitu ambacho alizungumza na Mapama ndio wakapanga niende Mogadishu. Sasa sikujua kama walikuwa wanakwenda kuniua au kunifanya nini.
Wakati niko katika lindi la mawazo nilianza kuona mataa kwa mbali. Ilikuwa ni bandari ya Mogadishu. Tulifika katika gati moja boti ikasimama.
Abdi akasimama alifungua dawati akauchukua ule mfuko wake wa pesa akaniambia.
“Tushuke”
Tulishukia kwenye gati. Tulikuta gari ndogo ya kifahari ya rangi nyekundu ikitusubiri.
Abdi alifungua mlango wa nyuma wa gari hilo akaniambia nijipakie. Nikajipakia.
Yeye alifungua mlango wa mbele kando ya dereva akajipakia. Gari ikaondoka.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 46


ILIPOISHIA
Abdi alifungua mlango wa nyuma wa gari hilo akaniambia nijipakie. Nikajipakia.
Yeye alifungua mlango wa mbele kando ya dereva akajipakia. Gari ikaondoka.
“Tunakwenda wapi?” Mtu aliyekuwa akiendesha alimuuliza Abdi tulipoingia kwenye mitaa.
“Nipeleke hotelini kwangu nikamuweke mgeni wangu halafu utaniachia gari”
Hapo ndipo nilipoliona na kulijua jiji la Mugadishu. Ilikuwa ni kabla ya serikali ya Somalia ya Rais Siad Barre kupinduliwa na kuanza kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoendelea hadi leo hii na kuzua vikundi vya kigaidi.
Jiji lilikuwa zuri na la kisasa. Nililifananisha sana na jiji la Nairobi ambalo niliwahi kufika.
Baada ya kupita katika barabara kadhaa, gari hilo lilisimama mbele ya hoteli moja iliyokuwa na ghorofa tano.
“Zima gari unipe funguo” Abdi alimwambia dereva wa gari hilo ambaye alilizima gari na kuchomoa funguo akampa Abdi.
“Utatumia ile gari nyingine” Abdi alisema huku akifungua mlango wa gari na kushuka.
“Amour shuka twende nikakupatie chumba”
Abdi aliniambia huku akivuta hatua kuelekea kwenye mlango wa hoteli hiyo.
Nikafungua mlango wa gari hilo na kushuka, nikamfuata Abdi Msomali.
“Hii ni hoteli yangu” akaniambia na kuongeza.
“Inaitwa Handeni Hotel”
Alipotaja jina ‘handeni’ nilishituka kidogo kwa sababu Handeni ni moja ya walaya za mkoa wetu wa Tanga.
“Inaitwa Handeni au sikukusikia vizuri?” nikamuuliza.
“Inaitwa Handeni, pia ndio jina la eneo hili tuliopo”
“Handeni ni moja ya wilaya za mkoa ninaotoka mimi”
“Ninajua. Niliwahi kusikia kuwa Wasomali wanaoishi katika eneo hili wana asili ya kizigua. Ninajua kwamba Wazigua wako Handeni au nimekosa?”
“Ni kweli. Hata mimi ni mzigua”
“Basi hapa utakutana na ndugu zako”
“Lakini ndugu zangu hao ni Wasomali?”
“Ndio ni Wasomali kama mimi lakini babu zao walitokea Handeni miaka mingi iliyopita”
“Nimekuelewa”
SASA ENDELEA
“Kama usingefika hapa ungeijuaje historia?”
“Kwa kweli nisingeijua”
Tulikuwa tumeshaingia ndani ya jingo hilo la hoteli. Tulikwenda mapokezi ambapo niligundua msomali huyo alikuwa akiheshimiwa sana na wafanyakazi wa hapo.
“Nipatieni chumba kimoja” alimwambia mmoja wa wahudumu wa mapokezi huku akiegemea kaunta hiyo.
Mhudumu huyo ambaye alikuwa msichana wa kisomali aliyekuwa amevaa sare ya koti jeusi na sketi alichukua kitabu cha wageni na kukifungua.
“Niandike jina gain bosi?” akamuuliza Abdi kwa nidhamu huku akishika kalamu.
“Niandike mimi mwenyewe” akamwambia.
“Nitumie jina gani?”
“Una maana hujui ninaitwa nani?”
“Samahani bosi, ninalijua jina lako”
Msichana aliandika kwenye kitabu hicho kisha akainua uso wake na kumtazama Abdi.
“Niandike chumba cha daraja gani?”
Abdi akanitazama. Bila shaka alikuwa akinipima kama ninastahili chumba cha daraja gani.
“Mpatie chumba cha daraja la kwanza”
Mhudumu aliandika kisha akanitazama mimi.
“Ungependa ukae ghorofa ya ngapi?”
“Ghorofa ya kwanza au ya pili”
“Nitakupatia ghorofa ya kwanza”
Msichana alijaza kwenye kitabu kisha akamtazama Abdi.
“Mgeni atakaa kwa siku ngapi”
Abdi akanitazama tena kisha akamjibu.
“Hapo paache tu…”
Msichana akageuka na kuchukua funguo.
“Nimekupatia chumba namba 85 ghorofa ya pili” akaniambia.
Sikumjibu kitu kwa sababu hicho chumba sikukitaka mimi.
“Mpeleke” Abdi akamwambia.
“Twende nikakuoneshe chumba chako” Msichana akaniambia.
Alitoka nyuma ya kaunta akaelekea kwenye ngazi.
“Mfuate akakuoneshe chumba utakachokaa” Abdi akaniambia.
Nilimfuata yule msichna. Wakati anapanda ngazi nilikuwa nyuma yake. Niliuona mwili wake. Ulikuwa wa kuvutia. Alikuwa na umbo lililofinyangwa kisomali hasa..
Nilifuatana naye hadi ghorofa ya kwanza. Akanionesha chumba namba 84. Akakifungua na kuingia ndani pamoja na mimi.
Baada ya kukiona chumba hicho msichana alitoka na kuniacha. Kwa vile sikuwa nimepata maelezo yoyote kutoka kwa Abdi na mimi nikatoka. Nilifunga mlango nikashuka ngazi.
Nilimkuta Abdi akinisubiri mapokezi.
“Umekiona chumba?” akaniuliza.
“Nimekiona”
Akamgeukia mhudumu wa mapokezi.
“Mtakuwa mnamuhudumia kwa kila kitu muda wote atakaokuwa hapa. Mtampatia chai ya asubuhi, chakula cha mchana na cha jioni, vinywaji na kila kitu atakachohitaji ikiwa ni pamoja na kufua nguo zake na kuzipiga pasi. Bili itakuwa juu yangu” akamwambia.
“Sawa bosi, tumekuelewa”
Abdi akanitazama.
“Twenzetu” akaniambia.
Sikujua aliniambia twenzetu wapi lakini kwa vile nilishakuwa kama mateka wake sikumuuliza kitu nikamfuata.
Tulitoka nje ya hoteli tukajipakia kwenye gari lake na kuondoka.
Tukiwa ndani ya gari nilitarajia angeweza kuniambia tunakwenda wapi lakini hakuniambia kitu. Nilimuona alikuwa katika lindi la mawazo. Sikujua alichokuwa akiwaza.
Baadaya kukata mitaa miwili mitatu alilisimamisha gari mbele ya jingo moja
la ghorofa lililokuwa na maduka makubwa. Akaniambia tushuke.
Tukashuka na kuingia katika duka mojawapo. Wakati tunaingia aliniambia.
“Hili pia ni duka langu”
“Ahaa…kumbe pia una maduka?” nikamuuliza.
Licha ya kwamba nilikuwa na fadhaa kwa kutojua hatima yangu, nilijaribu kujichangamsha na kuzungumza naye kwa vile alionesha kama ananijali.
“Sina maduka, nina duka moja tu” akaniambia.
Tulipoingia ndani ya duka hilo nililiona lilikuwa duka kubwa la nguo za wanaume. Kulikuwa na suti, mashati, fulana, suruali na aina kadha wa kadha ya nguo za kiume.
“Angalia nguo unazopenda, upate nguo za kubadili” akaniambia.
Ilikuwa kweli nilihitaji kubadili nguo. Licha ya kuwa sikuwa na nguo za kubadili, zile nilizovaa zilikuwa zimechafuka na zilikuwa zinanitia aibu.
Nikachagua nguo. Nilichukua shati moja
na suruali moja pamoja na viatu na soksi.
“Ongeza” Abdi akaniambia.
Nikaongeza shati moja.
Abdi akanichagulia mashati mengine matatu.
“Ongeza suruali tatu” akaniambia.
Nikachagua suruali zingine tatu, nikawa na suruali nne.
Abdi akaniita upande uliokuwa na suti.
Nilipokwenda alinaiambia.
“Mimi napenda sana kuvaa suti na wewe chagua suti moja ya kuvaa”
Nikatabasamu. Ilikuwa ni mara ya kwanza kukunjua uso wangu tangu ile boti tuliyokuwa tukisafiria kutoka Pemba ilipozama.
Abdi alipoona natabasamu akacheka.
“Chagua suti moja au nikuchagulie mimi?” akaniuliza.
Kabla sijamjibu alishachomoa suti moja ya rangi ya kijivu.
“Chukua hii” akaniambia.
MAMBO YANAZIDI KUSONGA. Hebu endelea kufuatilia.....
 
SEHEMU YA 47


ILIPOISHIA
Ilikuwa kweli nilihitaji kubadili nguo. Licha ya kuwa sikuwa na nguo za kubadili, zile nilizovaa zilikuwa zimechafuka na zilikuwa zinanitia aibu.
Nikachagua nguo. Nilichukua shati moja
na suruali moja pamoja na viatu na soksi.
“Ongeza” Abdi akaniambia.
Nikaongeza shati moja.
Abdi akanichagulia mashati mengine matatu.
“Ongeza suruali tatu” akaniambia.
Nikachagua suruali zingine tatu, nikawa na suruali nne.
Abdi akaniita upande uliokuwa na suti.
Nilipokwenda alinaiambia.
“Mimi napenda sana kuvaa suti na wewe chagua suti moja ya kuvaa”
Nikatabasamu. Ilikuwa ni mara ya kwanza kukunjua uso wangu tangu ile boti tuliyokuwa tukisafiria kutoka Pemba ilipozama.
Abdi alipoona natabasamu akacheka.
“Chagua suti moja au nikuchagulie mimi?” akaniuliza.
Kabla sijamjibu alishachomoa suti moja ya rangi ya kijivu.
“Chukua hii” akaniambia.
SASA ENDELEA
Nikaichukua ile suti.
“Nenda kajaribu hizo nguo kwenye kile chumba pale” akaniambia huku akinionesha mlango wa chumba hicho.
Nikaingia kwenye hicho chumba. Unapoingia katika chumba hicho unajiona mwenyewe kwani kilikuwa na vioo vitupu. Nilizijaribu nguo zote na kuona zilikuwa sawa.
Nilipotoka katika chumba hicho nilimwambia Abdi.
“Bado viatu na soksi”
“Kachague jozi mbili za viatu na soksi” akaniambia.
Nikaenda kuchukua jozi mbili za viatu na jozi mbili za soksi.
Abdi alinifuata na kuninong’oneza.
“Chukua na chupi kumi”
Aliponiambia hivyo sote tukacheka.
Baada ya kufanya manunuzi hayo ambayo Abdi aliyalipia kwa dola za Kimarekani tuliondoka kwa gari. Tulirudi kule hoteli ambako Abdi aliniacha.
“Nitakupitia baadaye” aliniambia wakati nikishuka kwenye gari. Alinyamaza kidogo kisha akaongeza.
“Najua utahitaji kujiweka vizuri kidogo na pia kupata chakula kizuri”
“Ndio. Nahitaji vyote hivyo”
“Kwa upande wa chakula nimeshaagiza utakula unachopenda”
“Sawa”
“Mimi naondoka kidogo, nitakupitia baadaye”
Abdi akatia gea gari lake na kuondoka.
Niliingia hotelini nikiwa na begi langu lililokuwa na nguo. Mhudumu mmoja alioniona aliniekea lile begi akapanda ngazi na kwenda kunisubiri kwenye mlango wa chumba changu.
Nilipofika nilifungua mlango nikamwambia.
“Karibu ndani”
Alikuwa msichana mweupe wa kisomali mwenye mwili wa kutamanisha.
Msichana alitabasamu akaliingiza lile begi chumbani kwangu kisha akaniaga
na kutoka.
Sikujua kama wasomali walikuwa wanazungumza Kiswahili. Pale hotelini niligundua baadhi ya wasomali walikuwa wanajua kuzungumza Kiswahili tena Kiswahili cha kipwani kilichonyooka.
Nilipobaki mle chumbani nilivua nguo nikaenda kuoga. Niliotoka bafuni nilivaa ile suti mpya aliyoninunulia Abdi. Nikajitazama kwenye kioo na kuona nilipendeza. Angalau ilinisahaulisha madhila niliyokuwa nayo moyoni.
Baada ya kuvaa nilishuka chini nikaingia katika eneo la mkahawa. Yule mhudumu aliyeniokea begi alinifuata.
Akanisemea kwa kisomali.
“Sijui hiyo lugha labda mnifundishe” nikamwambia.
“Unajua Kiswahili peke yake?” akaniuliza.
“Na kizigua”
“Unatoka Handeni Tanzania?”
“Umejuaje”
“Kule ndio kuna wazigua”
“Nasikia na nyinyi pia mna asili ya huko”
“Babu zetu wametoka huko lakini mimi unaniona mweupe mama yangu ni mbarawa”
“Mmejifundisha Kiswahili?”
“Mimi nilizaliwa Garisa nchini Kenya, kule watu wanazungumza Kiswahili. Wenzangu wengine wametoka Mombasa”
JE NINI KITATOKEA?
 
SEHEMU YA 48


ILIPOISHIA
Nilipobaki mle chumbani nilivua nguo nikaenda kuoga. Niliotoka bafuni nilivaa ile suti mpya aliyoninunulia Abdi. Nikajitazama kwenye kioo na kuona nilipendeza. Angalau ilinisahaulisha madhila niliyokuwa nayo moyoni.
Baada ya kuvaa nilishuka chini nikaingia katika eneo la mgahawa. Yule mhudumu aliyenipokea begi alinifuata.
Akanisemea kwa kisomali.
“Sijui hiyo lugha labda mnifundishe” nikamwambia.
“Unajua Kiswahili peke yake?” akaniuliza.
“Na kizigua”
“Unatoka Handeni Tanzania?”
“Umejuaje”
“Kule ndio kuna wazigua”
“Nasikia na nyinyi pia mna asili ya huko”
“Babu zetu wametoka huko lakini mimi unaniona mweupe mama yangu ni mbarawa”
“Mmejifundisha wapi Kiswahili?”
“Mimi nilizaliwa Garissa nchini Kenya, kule watu wanazungumza Kiswahili. Wenzangu wengine wametoka Mombasa”
SASA ENDELEA
“Nashukuru kwa mazungumzo, ninahitaji chakula”
“Upatiwe menyu?”
“Kwani wewe si ndiye unayehusika”
“Mimi pia nahusika lakini kuna mhudumu maalum wa hapa. Ngoja nimuite”
Shamsa akamuita msichana mmoja na kumwambia.
“Mgeni wa bosi. Bosi ameagiza apatiwe kila atakachohitaji. Bili itakuwa juu yake”
“Sawa” Msichana alimkubalia kisha akaniuliza.
“Nikupatie menyu?”
“Ndio nipatie”
Menyu alikuwa anayo mkononi, akaniwekea juu ya meza.
Nikaishika na kutazama orodha ya vyakula. Nikachagua wali kwa samaki na juisi.
Wasichana wote wawili waliondoka na kuniacha.
Baada ya muda kidogo nililetewa chakula nilichoagiza. Wakati nakula nilianza kujiwazia mustakbali wangu kule Somalia. Nilijiuliza Abdi alikuwa na madhumuni gani kunichukua mimi Somalia, kuniweka hoteli na kunihudumia kama rafiki yake wakati tulikuwa hatujuani.
Pia nilijiuliza ningekaa Somalia hadi lini. Ingawa niliingia kienyeji lakini wakati ule Somalia ilikuwa na serikali. Nilitakiwa kuwa na paspoti. Nilijiambia kama ningekamatwa nitakuwa na kosa la kuingia nchi ya watu bila paspoti.
Nilishindwa kumuuliza Abdi kuwa ningekaa hapo Somali kwa siku ngapi, hasa nikikumbuka muda ule alionitolea bastola kwa kumhoji niende Somalia kufanya nini.
Niliogopa kuwa ningeweza kumkasirisha na hivyo akanipiga risasi na kwenda kuutupa mwili wangu jalalani. Mtu mwenyewe licha ya kuwa mchangafu, mkarimu na anayependa kutabasamu, alionekana kuwa katili na asiyejali kitu.
Mtu wa aina yake kuua ni kazi ndogo tu!
Nilipomaliza kula niliondoka nikarudi ghorofani. Niliingia chumbani nikaenda kusimama kando ya dirisha na kutazama mandhari ya nje.
Niliendelea kusimama hapo nikiangalia magari na watu waliokuwa wakipita barabarani huku akili yangu ikitafuta jibu la kwanini niko pale Somalia lakini sikupata jibu.
Nilipitisha kama nusu saa nikiwa hapo, nikaingia chumbani na kuvua koti kisha nikajilaza kitandani.
Nilikuwa nina uchovu na nilikuwa na usingizi. Kwa vile moyo wangu kidogo ulikuwa umetulia nikaona naweza kulala.
Na nililala. Nilipokuja kuzinduka niliona giza. Ilikuwa ni usiku. Kwa vile sikuwa na saa sikuweza kujua ilikuwa ni usiku wa saa ngapi.
Nikainuka kitandani na kuwasha taa. Pale mchagoni mwa kitanda palikuwa na simu. Nikainua mkono wa simu na kuzungumza na opereta.
“Abdi ameshafika?” nikamuuliza.
“Wewe nani?”
“Mimi ni mgeni wake, niko ghorofa ya kwanza”
“Alifika, akakupigia simu lakini haikupokelewa akajua umelala”
“Sasa yuko wapi?”
“Ameshaondoka, ametuambia tukuambie kuwa mtakutana asubuhi”
“Ni saa ngapi sasa?”
“Saa mbili inakwenda kwenye na nusu”
“Nitashuka sasa hivi kuja kupata chakula”
“Sawa, chakula kipo”
Nikauweka mkono wa simu mahali pake na kuvua nguo. Nilikwenda kuoga tena.
Nilipomaliza nilirudia kuvaa suti yangu kisha nikashuka chini. Niliingia katika ukumbi wa mkahawa wa hoteli hiyo.
Mhudumu aliponiona tu akanifuata na kunipa menyu.
“Nahtaji chai tu” nikamwambia.
“Chai na nini?”
“kama kuna sambusa nipatie tatu”
Mhudumu aliondoka. Baada ya muda kidogo alirudi akiwa na chano kilichokuwa na kisahani kilichokuwa na sambusa tatu, birika ndogo ya maziwa, kipakiti cha majani ya chai, jagi la sukari na kikombe kitupu kikiwa na kisahani chake.
Aliniwekea juu ya meza. Nikachukua birika na kumimina maziwa kwenye kikombe nikatia kijiko kimoja na nusu cha sukari na kukoroga.
Baada ya sukari kukolea, nilitumbukiza kile kipakiti cha majani ya chai ambacho kiliyafanya maziwa kuwa na rangi ya chai.
Nilitumia nusu saa nzima kunywa chai huku nikijiwazia. Mpaka muda ule sikuwa nimeitambua dhamira ya Abdi.
Nikajiambia baada ya siku tatu nitamwambia kuwa nahitaji kuondoka kurudi kwetu kwani sikuwa na sababu yoyote ya kuendelea kukaa Somalia huku ndugu zangu na mama yangu wakiwa hawajui niliko.
Baada ya kumaliza kunywa chai nilikwenda kujipumzisha kwenye eneo la wazi la hoteli ambapo palikuwa na upepo mwanana kutoka Bahari ya Hindi.
Pale nilipoteza dakika kadhaa kabla ya kuamua kurudi chumbani kwangu.
Mawazo ya Zena yalinijia usiku ule. Nikajiambia msichana wa kijini aliamua kunisaliti kwenye kile kisiwa baada ya kukataa kuoana naye.
Kitendo cha kutoonana tena na Zena kilinipa picha kwamba Zena aliamua kuachana na mimi.
Nikajiambia kama kweli alikuwa ameamua hivyo lilikuwa jambo la kushukuru sana kwani msichana yule alikuwa ananisababishia matatizo makubwa.
Baada ya kuwaza sana nilipitiwa na usingizi. Sikujua nililala kwa muda gani lakini nilihisi kama nilishituka katikati ya usiku au nilikuwa katika ndoto. Nikaona kama mlango wa chumba nilichokuwa nimelala unafunguliwa taratibu.
Kitendo hicho kilitokea nikiwa na kumbukumbu kamili kichwani mwangu kwamba mlango wa chumba hicho niliufunga kwa ndani na kuhakikisha kuwa ulikuwa umefungika.
Mlango ulipokuwa wazi nilimuona mtu akiingia. Alikuwa mzee mwembamba na mrefu. Wembamba wake ulichanganyika na kukonda. Alikuwa na nywele ndefu, nyeupe tupu.
Alikuwa amejifunga shuka nyeupe kiunoni na mabegani alijitanda shuka nyingine nyeupe kuziba kifua na tumbo lake. Hata hivyo upande mmoja wa kifua chake ulikuwa ukionekana. Mbavu zake zilikuwa zimetokeza na kuhisabika.
Akaingia mle chumbani kwa kunyata. Wakati akiingia nilikuwa nikijiuliza nilikuwa ninaota au nilichokuwa nakiona kilikuwa ni kweli.
Muda huo niligundua kuwa sikuwa sawa. Nilikuwa kama niliyepatwa na jinamizi. Mwili wangu haukuwa na uwezo wa kufanya chochote hata kupiga kelele.
Kadhalika akili yangu ilikuwa imepoteza uwezo wake na nilikuwa kama taahira au zezeta. Sikuweza kujua ni kwanini nilijihisi kuwa vile.
Yule mzee wa kisomali alikuja hadi karibu na kitanda nilichokuwa nimelala.
Nilimuona vizuri. Alikuwa na pua ndefu na macho makali na madogo. Akasimama na kuniita.
“Amour!”
Nikanyamaza kimya. Nikamuona anasema maneno fulani kwa lugha ya kisomali kisha akanyoosha mkono wake na kupapasa kitanda nilichokuwa nimelalaa akashika mkono wangu na kuubana.
JE NI MZEE GANI TENA HUYO NA AMETOKEA WAPI? HAYA NI MAMBO YA KUTISHA SASA! DUH!
 
SEHEMU YA 49


ILIPOISHIA
Baada ya kuwaza sana nilipitiwa na usingizi. Sikujua nililala kwa muda gani lakini nilihisi kama nilishituka katikati ya usiku au nilikuwa katika ndoto. Nikaona kama mlango wa chumba nilichokuwa nimelala unafunguliwa taratibu.
Kitendo hicho kilitokea nikiwa na kumbukumbu kamili kichwani mwangu kwamba mlango wa chumba hicho niliufunga kwa ndani na kuhakikisha kuwa ulikuwa umefungika.
Mlango ulipokuwa wazi nilimuona mtu akiingia. Alikuwa mzee mwembamba na mrefu. Wembamba wake ulichanganyika na kukonda. Alikuwa na nywele ndefu, nyeupe tupu.
Alikuwa amejifunga shuka nyeupe kiunoni na mabegani alijitanda shuka nyingine nyeupe kuziba kifua na tumbo lake. Hata hivyo upande mmoja wa kifua chake ulikuwa ukionekana. Mbavu zake zilikuwa zimetokeza na kuhisabika.
Akaingia mle chumbani kwa kunyata. Wakati akiingia nilikuwa nikijiuliza nilikuwa ninaota au nilichokuwa kitendo nakiona kilikuwa ni kweli.
Muda huo niligundua kuwa sikuwa sawa. Nilikuwa kama niliyepatwa na jinamizi. Mwili wangu haukuwa na uwezo wa kufanya chochote hata kupiga kelele.
Kadhalika akili yangu ilikuwa imepoteza uwezo wake na nilikuwa kama taahira au zezeta. Sikuweza kujua ni kwanini nilijihisi kuwa vile.
Yule mzee wa kisomali alikuja hadi karibu na kitanda nilichokuwa nimelala.
Nilimuona vizuri. Alikuwa na pua ndefu na macho makali na madogo. Akasimama na kuniita.
“Amour!”
Nikanyamaza kimya. Nikamuona anasema maneno fulani kwa lugha ya kisomali kisha akanyoosha mkono wake na kupapasa kitanda nilichokuwa nimelalaa akashika mkono wangu na kuubana.
SASA ENDELEA
.
Aliubana kwa nguvu nikaona kama nilishikwa kwa koleo.
“Inuka” akaniambia.
Kwa sababu nilikuwa kama taahira nisiyejielewa nikainuka kweli.
“Shuka kwenye kitanda” akaendelea kuniambia.
Nikashuka kwenye kitanda. Nilikuwa nimevaa chupi tu. Akaichukua ile shuka aliyoitanda mabegani mwake akanifunga nayo kiunoni kisha akanishika tena mkono na kuniambia.
“Twende”
Nikatoka naye mle chumbani.
Tulishuka ngazi, akatumia mlango wa nyuma wa hoteli kunitoa. Nilikuta gari limewekwa sambamba na mlango. Nikafunguliwa mlango wa nyuma wa gari, nikajipakia bilakuambiwa.
Mzee naye aliingia katika siti ya nyuma. Kulikuwa na mtu aliyekuwa kwenye siti ya dereva ambaye sikuweza kumuona vizuri. Sikujua alikuwa nani.
Kama ningemchunguza ningeweza kumjua lakini akili yangu haikuona umuhimu wa kutaka kumjua wala kujua nilikuwa napelekwa wapi.
Gari likapigwa moto na kuondoka. Safari ikaanza. Mji ulikuwa kimya na hakukuwa na watu wowote walioonekana barabarani zaidi ya walinzi wa maduka waliokuwa wakisinzia.
Baada ya mwendo wa karibu kilometa tano nilihisi kuwa tulikuwa tumeuacha mji kwani sikuona tena majumba ya ghorofa isipokuwa nyumba ndogo ndogo.
Tulikuwa tumeingia katika maeneo ya ambayo kwa lugha ya kwetu tungeyaita ‘uswahilini’
Mwanga wa gari tulilokuwemo ulimulika mapaka yaliyokuwa yakirandaranda kutafuta vyakula vilivyotupwa kwenye mapipa ya takataka. Ingawa ilikuwa usiku maji taka yalikuwa yakitiririka kutoka kwenye majumba ya watu na kuunda vidimbwi vya maji taka kandokando ya barabara.
Wakati wote nilikuwa nashindana na akili yangu. Nilikuwa naona kichwa kizito kama niliyelemewa na usingizi, wakati huo huo sikutaka usingizi unichukue.
Kila muda nilikuwa najigutuka na kukaza macho yangu ili nisilale. Lakini mwisho wake nilizidiwa nguvu, usingizi wa moja kwa moja ukanichukua ghafla.
Hata sikuweza kujua tena lile gari lilielekea wapi.
Lakini nilipokuja kuzinduka nilijiona mimi na yule mzee tumekaa kando ya shimo lililokuwa mbele yetu. Shimo hilo lilichimbwa usawa wa kaburi kando ya mti mkubwa. Mahali tulipokuwa palikuwa ni porini.
Kulikuwa na taa ya chemli iliyokuwa inawaka pembeni mwa kaburi hilo na kufanya sehemu ile tuliyokuwa iwe na mwanga kwani eneo lote lilikuwa na kiza totoro.
Yule mzee wa kisomali aliingia kwenye lile kaburi akasimama na kuniambia.
“Ingia”
Na mimi nikaingia.
“Kaa hapo chini”
Akanionesha mahali pa kukaa, nikakaa. Nikaona analishika sikio langu la upande wa kulia na kusema maneno kwa lugha ya kisomali kama mtu aliyekuwa anasoma dua kisha akaniinamia na kukigandamiza kichwa chake kwenye komo langu.
Alinishika na kunigandamiza kwa nguvu sana mpaka nikasikia maumivu ya kichwa. Nilitaka kupiga kelele nilipomuona amerushwa na kuanguka chini. Alikuwa kama aliyerushwa na umeme.
Akainuka taratibu na kutoka kwenye lile kaburi. Kilichofuatia baada ya hapo sikukifahamu, nilishitukia tu nikiamka kitandani pale hoteli nilipokodiwa chumba na Abdi.
Nikahisi kwamba labda nilikuwa katika ndoto. Moyo ulikuwa ukinienda mbio. Nikainuka na kwenda kuutazama
mlango wa mle chumbani. Niliukuta umefungwa kwa ndani. Kitu ambacho kiliashiria kuwa hakukuwa na mtu aliyeingia humo chumbani.
Lakini ni ndoto gani ile? Nikajiuliza. Kila kitu nilikiona waziwazi kama vile kinatokea kweli.
Kama ilikuwa ndoto ilikuwa ya ajabu sana, nikajiambia.
Wakati ule nilipoamka kulikuwa kumekucha. Nikaingia maliwatoni. Nilipotoka nikavaa nguo. Nilivaa suti ile ile niliyonunuliwa na Abdi.
Nikashuka chini na kuingia mkahawani. Nilipatiwa kifungua kinywa. Wakati nakunywa chai nikamuona Abdi akiingia.
“Amour salaam alaykum” akanisalimia kwa bashasha huku akinipa mkono.
“Alayka salaam. Habari ya tangu jana?”
“Nzuri bwana, umeamkaje?”
“Nashukuru, nimeamka salama. Sijui wewe”
Na yeye akaagiza kifungua kinywa.
“Kuna sehemu nataka twende” akaniambia.
“Wapi?”
“Mogadishu ni kubwa sana. Kuna sehemu nyingi nataka kukuonesha”
“Sawa”
Tulipomaliza kunywa chai tukatoka.
“Jana nilikufuata usiku nikakuta umelala” Abdi aliniambia wakati tunatoka.
“Nililala mapema kwa sababu ya uchovu”
“Niliwambia wale wasichana wasikuamshe. Nilijua ulikuwa na uchovu mwingi”
Tulitoka nje ya hoteli tukajipakia kwenye gari. Lilikuwa ni gari la aina nyingine sio lile la jana yake.
Baada ya kujipakia tukaondoka.
“Nataka uuone mji wetu vizuri” Abdi alikuwa akinizungumzisha huku gari likiwa katika mwendo wa taratibu au wa kinyonga . Nilikuwa sijui tunakwenda wapi.
“Mji wenu ni mzuri sana. Una majumba makubwa na umejengeka sana” nikamwambia.
“Bado. Kuna maeneo mengi hujayaona”
“Inavyoonekana mmepiga hatua kubwa ya maendeleo”
“Sana”
Baada ya mwendo wa karibu nusu saa tuliingia katika maeneo ya mashamba. Nilikuwa nikijiuliza alikuwa akinipeleka shambani kwake au alitaka kunionesha kitu gani?
Tulitokea katika mtaa mmoja uliokuwa umezagaa uchafu. Tulipishana na mbuzi, kondoo na kuku wa kienyeji. Abdi alikuwa akikata kona ovyo kukwepa mashimo na vidimbwi vya maji machafu.
“Tuache gari hapa” Abdi akaniambia huku akifunga breki pembeni mwa njia. Bila shaka alishindwa kuendesha kutokana na barabara yenyewe kujaa mazagazaga.
Tulishuka tukatembea kwa miguu. Tulizipita nyumba mbili za ghorofa. Zilikuwa nyumba zilizoonekana zimeshapitwa na muda wake wa kuishi watu kwani zilichakaa sana. Huenda zilijengwa miaka mia moja iliyopita. Enzi za utawala wa kikoloni.
Tuliingia mtaa mwingine uliokuwa na tifutifu jingi. Tukapita msikiti. Tulikwenda mbele kidogo, Abdi akasimama mbele ya mlango wa nyumba moja iliyokuwa imepakwa rangi nyeupe.
Mlango wake ulikuwa umechorwa picha ya nyota na mwezi.
Abdi alibisha mlango huo. Baada ya muda kidogo mlango ukafunguliwa.
Mzee mmoja akachungulia nje. Alimtazama Abdi kisha akanitazama mimi.
“Karibuni” akatuambia na kurudi ndani.
Abdi akaingia na kuniambia.
“”Karibu”
Na mimi nikaingia. Tulitokea katika ukumbi mpana kama darasa. Harufu tuliyokutana nayo humo ndani ni ya udi na marashi.
Katikati ya ule ukumbi palitandikwa jamvi. Katika lile jamvi niliona sinia iliyotiwa vitu mbalimbali kama vile ndizi mbivu, vipande vya miwa, mkate wa mchele, tende na vitu vingine ikiwemo chupa kubwa lenye asali.
Katika kila pembe ya lile jamvi kuliwekwa nazi moja. Jumla zilikuwa nazi nne.
Yule mzee wa kisomali alikuwa amesimama nyuma ya mlango.
Alimwambia Abdi maneno kwa lugha ya kisomali. Abdi akaniambia mimi.
“Twende tukakae pale”
Alinionesha lile jamvi.
Tukaenda kukaa. Yule mzee wa kisomali alitoka uani. Baadaye akarudi tena akiwa ameshika kitabu kikubwa cha kiarabu na yeye akakaa kwenye lile jamvi.
Sasa niliweza kumuangalia vizuri. Nikajiuliza mbona amefanana na yule msomali niliyemuota akinichukua kule chumbani? Alikuwa mrefu vile vile na pua yake pia ilikuwa ndefu.
Nikashangaa sana.
KUNA NINI HAPA? HUYU MZEE NI NANI? ANA MIPANGO GANI NA ABDI?
 
SEHEMU YA 50


ILIPOISHIA
Mzee mmoja akachungulia nje. Alimtazama Abdi kisha akanitazama mimi.
“Karibuni” akatuambia na kurudi ndani.
Abdi akaingia na kuniambia.
“”Karibu”
Na mimi nikaingia. Tulitokea katika ukumbi mpana kama darasa. Harufu tuliyokutana nayo humo ndani ni ya udi na marashi.
Katikati ya ule ukumbi palitandikwa jamvi. Katika lile jamvi niliona sinia iliyotiwa vitu mbalimbali kama vile ndizi mbivu, vipande vya miwa, mkate wa mchele, tende na vitu vingine.
Katika kila pembe ya lile jamvi kuliwekwa nazi moja. Jumla zilikuwa nazi nne.
Yule mzee wa kisomali alikuwa amesimama nyuma ya mlango.
Alimwambia Abdi maneno kwa lugha ya kisomali. Abdi akaniambia mimi.
“Twende tukakae pale”
Alinionesha lile jamvi.
Tukaenda kukaa. Yule mzee wa kisomali alitoka uani. Baadaye akarudi tena akiwa ameshika kitabu kikubwa cha kiarabu na yeye akakaa kwenye lile jamvi.
Sasa niliweza kumuangalia vizuri. Nikajiuliza mbona amefanana na yule msomali niliyemuota akinichukua kule chumbani? Alikuwa mrefu vile vile na pua yake pia ilikuwa ndefu.
Nikashangaa sana.
SASA ENDELEA
Mzee huyo wa kisomali akamtazama Abdi kisha akamuuliza maneno na kwa kisomali.
Abdi akanitazama kisha akamwambia.
“Amour”
Nikahisi labda alimuuliza jina langu.
Mzee wa kisomali akanitazama kisha akafungua kitabu chake. Karasa zilikuwa zimegandana akakigusisha kidole chake kwenye ulimi kukitia mate kisha akaufungua ule ukurasa.
Akaanza kusoma maneno ya kiarabu. Sikuwezaa kujua alikuwa anasoma nini lakini nilisikia akitaja jina la Zena Binti Jabal Keysi. Wakati mwingine akitaja jina langu.
Mara kwa mara nilikuwa nikimtazama Abdi kuona kama mwenzangu alikuwa anaelewa chochote. Abdi alikuwa amenyamaza kimya. Alikuwa ametulia kama aliyekuwa anaaguliwa.
Ghafla tukaona nazi iliyokuwa katika pembe moja ya lile jamvi inapasuka yenyewe. Mzee alikuwa akiendelea kusoma tu. Naizi ya pili ikapasuka. Ilipopasuka nazi ya tatu ukuta wa uliokuwa mbele yetu ulifanya ufa akatokea mtu.
Alikuwa mwanamke aliyevaa vizuri. Gauni alilovaa lilikuwa limedariziwa vimemeta vya dhahabu. Alikuwa amevaa mkufu wa dhahabu na bangili za dhahabu. Masikioni alikuwa amevaa vipuli vya dhahabu.
Kichwani kwake nywele zake zilibanwa kwa taji la dhahabu lililomfanya aonekane kama malikia wa visiwa vya Sheba.
Alipotokea sote tulishituka tukamtazama. Ilinichukua sekunde mbili au tatu kutambua kuwa alikuwa Zena!
Zena alikuwa amependeza kuliko siku zote nilizowahi kumuona. Alikuwa aking’ara kama mwezi mpevu! Sikuweza kujua ni kitu gani kilichomleta pale na kwanini alitokea katika hali tofauti na anavyotokea siku zote.
Siku zote nilizokutana naye alinitokea katika hali ya kawaida, si hali kama ile ya kuibuka kutoka kwenye ufa wa ukuta. Ilikuwa hali ambayo si tu ilinitisha mimi, ilimtisha hata Abdi aliyekuwa ameketi karibu yangu. Nilimuona akimtazama kwa shauku iliyochanganyika na hofu.
Mzee wa Kisomali alimtazama kisha alimwambia maneno kwa lugha ya kiarabu.
Zena hakusema chochote. Akiwa miguu pekupeku alikuja taratibu hadi ilipokuwa ile sinia iliyokuwa na vitu akaipindua kwa miguu. Sinia ilipinduka, na vitu vyote vilimwagika chini.
Alipomaliza kuipindua ile sinia alimfuata yule mzee wa kisomali akampiga kibao cha shavu. Mzee alianguka chini. Hakuinuka tena. Sasa akamfuata Abdi. Abdi alipoona anafuatwa aliinuka haraka akatoka mbio. Na mimi nikainuka na kutoka mbio kumfuata Abdi.
Tulitoka kwenye mlango. Abdi kama ambaye alibadili mawazo alirudi kwenye mlango huo na kuchungulia. Na mimi nikarudi kuchungulia.
Zena hatukumuona tena. Tulimuona yule mzee akijiinua na kukaa. Abdi akarudi. Mimi sikurudi.
Nilibaki kwenye mlango nikichungulia.
Nikawasikia Abdi na yule mzee wakizungumza kwa lugha ya kisomali. Mzee alikuwa akifoka na akimuashiria Abdi aondoke.
Abdi akatoka na kuniambia.
“Twenzetu”
Wakati tunatembea kurudi tulikoliacha gari Abdi hakunieleza chochote na mimi sikumuuliza chochote.
Nilibaki kujiuliza mwenyewe ni kitu gani kilichokuwa kimetendeka pale hadi Zena akatokea na kumwaga vile vitu na kisha kumpiga kibao yule mzee? Sikupata jibu.
Nilihisi kuwa jibu alikuwa analo Abdi lakini hakuonesha dalili yoyote ya kutaka kunieleza chochote. Na mimi nikashindwa kumuuliza.
Niliona uso wake ulikuwa umefadhaika na alikosa raha. Hakuwa hata akinitazama.
Tulirudi kwenye gari lake tukajipakia na
kuondoka.
Wakati Abdi akiendesha gari kurudi mjini aliniambia.
“Nina hoteli mbili. Ile unayokaa wewe na nyingine mpya. Nataka uwe mneneja wa ile hoteli yangu mpya”
“Nitawezaje kuwa meneja wa hoteli yako wakati nataka kuondoka?” nikamuuliza.
“Huwezi kuondoka bila paspoti. Subiri nikutengezee paspoti”
“Utanitengezea lini?” nikamuuliza.
“Usiwe na haraka Amour. Ninakuhakikishi
a kuwa nitakutengezea isipokuwa katika kipindi hiki cha kusubiri paspoti yako iwe tayari nataka uwe meneja wa hoteli yangu. Nitakupa nyumba na gari na kama utahitaji mke wa kisomali nitakutafutia msichana mrembo”
Abdi alianza kunitia tamaa ya maisha na kunipa ushawishi wa kubaki Somalia.
Hata hivyo moyo wangu ulikuwa mzito kukubaliana naye. Nilikuwa simuelewi japokuwa mipango aliyonieleza ilikuwa ya maana kwa upande wangu.
“Unataka kurudi Tanga, kuna nini? Kama utakaa hapa kwa muda mfupi tu Amour unaweza kupata maendeleo makubwa na ukarudi kwenu ukiwa tajiri” Abdi aliendelea kunishawishi.
Muda wote nilikuwa nimebaki kimya nikiyatafakari maneno yake. Alipoona nipo kimya na yeye akanyamaza. Sikuweza kujua ni kwanini aliileta ile mada ya hoteli wakati kulikuwa na tukio jingine la kuibuka kwa Zena ambalo ndilo alilopaswa kunieleza.
Kwanza kile kisomo alichokuwa anasoma yule mzee hadi nazi zikapasuka na Zena akatokea, nilijiuliza, kilikuwa kiosomo cha nini. Hapo pia sikupata jibu.
Dakika chache baadaye Abdi alilisimamisha gari mbele ya nyumba moja iliyokuwa katika mtaa mtulivu.
Aliniambia tushuke, tukashuka.
“Nifuate” akaniambia.
Tuliingia katika geti la ile nyumba tukakuta mafundi wakipaka rangi kwenye kuta. Alizungumza nao kwa kiomali kisha tukaingia ndani ya ile nyumba.
Ilikuwa nyumba nzuri na ya kupendeza. Abdi alitazama sehemu zilizokuwa zimeshapigwa rangi, akaniambia.
“Hii ni nyumba yangu. Ninaifanyia ukarabati kwa ajili yako. Wewe utakuja kuishi hapa”
“Wewe mwenyewe unaishi wapi?”
“Nitakupeleka ukapaone nyumbani kwangu”
“Ni lini hii nyumba itakuwa tayari?”
“Leo watamaliza kupiga rangi. Labda keshokutwa unaweza kuhamia. Kesho nitakuwekea fanicha mpya”
Alifungua milango ya vyumba na kunionesha ndani.
“Patakufaa sana hapa” akaniambia.
Sikumjibu kitu. Nilikuwa bado ninajadiliana na moyo wangu kuhusu suala la kubaki pale Somalia.
“Amour unafikiria nini. Unataka kuiacha bahati kama hii?” Abdi aliniambia kisha akacheka peke yake.
“Twenzetu” akaniambia.
Tukatoka tena. Tulijipakia kwenye gari tukaondoka.
Breki ya kwanza ilikuwa mbele ya hoteli moja iliyokuwa katika mtaa mwingine. Ilikuwa hoteli ndogo ya ghorofa moja, Ilikuwa imeandikwa kwa herufi kubwa. AL ASAD.
“Hii ndio hoteli ambayo nitakuachia wewe, itakuwa kama mali yako kwani tutakuwa tunagawana faida kila mwezi na kila mwaka kama utapenda kuendelea kubaki Somalia” Abdi aliniambia tukiwa bado tupo kwenye gari.
Alipoona nilikuwa nikiiangalia angalia ile hoteli, aliniambia.
“Tushuke uione vizuri”
Tukashuka.
Tuliingia ndani ya ile hoteli. Kwa kweli ilikuwa imechangamka.
“Sasa nani anaiendesha kwa hivi sasa?” nikamuuliza.
“Yuko mtu lakini nitamuondoa”
“Sasa ni kwanini umuondoe?”
“Lengo langu ni kukunufaisha wewe rafiki yangu au nimefanya kosa?’
“Hapana. Ni vizuri”
Abdi alinitembeza hoteli nzima kisha tukaingia katika ofisi ya meneja.
Meneja mwenyewe alikuwa mtu mzima. Kichwa chake kilishaanza kutoka mvi.
JE WEWE MSOMAJI UMESHAPATA WAZO GANI KUHUSU HUYU ABDI? MIMI BADO SIMUELEWI! LAKINI HEBU ACHA TUENDELEE TUTAMGUNDUA TU. KWA LEO NAKOMEA HAPA.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom