Mkushi w jani
JF-Expert Member
- Oct 2, 2021
- 1,576
- 1,302
Kaka ungetupa ata kdgo kumalizia boxing day
Kaka ungetupa ata kdgo kumalizia boxing day
Ila uhalisia huyu mwana inaonekana akikueeka kwenye 18 zake wewe ni kuitikia ndio ndio Hadi mwisho.Mwamba anajua kutunga aisee
Na siku achanyikiwe awaue wanawake wa Roma wote, wananiudhi mie
Hiyo ndio imetuchanganya zaidi 783
Hii 783 imenichanganya sana,lini tena muendelezo kwenye group?Hiyo ndio imetuchanganya zaidi 783
Wacha nifungue code tu kwa msio kwenye group,kumbe Edna ndio athena!lini tena mkuu umeishia patamu saaaanaHii 783 imenichanganya sana,lini tena muendelezo kwenye group?
NomaSEHEMU YA 589.
Wanajeshi wote hakuna ambaye aliamini kama Kamanda wao ndio amekufa hivyo ,ilikuwa ni kama vile wapo ndotoni na muda wowote wangeamka na kuona sio kweli.
Kamanda mwenye cheo cha ubrigedia jenerali alikuwa amekufa kiwepesi kwa namna hio .
Matendo ya Roma yaliwaambia kabisa hawakuwa wakiota bali walichokuwa wakiona ni uhalisia mara baada ya kurushiwa mwili wa Kamanda wao uliolegea shingo.
“Baba kamuua Brigedia Makwera haitaleta shida zaidi?”Aliuliza Damasi ambaye alikuwa kwenye taharuki kwa kila ambacho ameshuhudia.
Ni moja wapo ya watu waliokuwa na woga zaidi ya wengine wote na alimuogopa Roma maradufu , ijapokuwa mwanzoni alikua akijua ana uwezo mkubwa na ni mkatili wa hali ya juu lakini kwa matendo ambayo ameyaona kwa macho yake alijihisi kabisa huenda Roma sio mtoto wa Raisi Senga na alisingiziwa mahali.
“Kuna kipi cha kufanya wakati tayari unaona ashakufa”Aliongea Kamanda Mstaafu ,Mzee Kweka huku akionyesa hana wasiwasi wowote , ilikuwa ni kama vile hata yeye angechukua maamuzi yaleyale.
Lakini huo ndio ukweli inawezekana Roma alitengenezwa kisayansi na akawa na ukatili wa hali ya juu na kuua kwake ikawa ni kitu kidogo lakini ukweli ni kwamba Afande Kweka ni moja wapo ya watu wakatili sana sana ambao washawahi kuwepo ndani ya Taifa la Tanzania , watu wengi ambao walimpinga ndani na nje ya jeshi aliwaua kwa siri sana kwa mbinu tofauti tofauti , hivyo anachokifanya Roma ni kama karithi tu na utofauti wake na Roma ni staili zao tu za kuua , yeye alikuwa akiagiza watu wake kutekeleza vifo lakini upande wa Roma alikuwa akiwa hadharani bila hofu yoyote.
Damasi aliekuwa akitaka kutokwa na machozi alitaka kuongea lakini Afande Kweka alonyesha kwamba hakuwa na mpango wowote wa kumsikiliza na palepale aliwapa ishara walinzi wake wamsogelee na kisha akatoa maagizo ambayo waliyafanyia kazi kwa haraka haraka.
Upande wa Denisi lisha ya kuonyesha mwonekano usiokuwa wa kawaida kama wa kukata tamaa lakini yeye hakuona shida kwa watu waliokufa.
“Kamanda wenu ndio huyo amekufa , je bado mnataka kuendelea kumuonyeshea utii muungane nae au utii wenu mtauojesha kwa taifa?”Aliuliza Roma huku akitoa tabasamu lake lilelile la kuogopesha na kuwafanya wale wanajeshi kushikwa na baridi ya woga
“Master Roma , tulilazimishwa kufanya hivi tu , kwanzia leo tupo tayari kukutambua kama Kamanda wetu mpya”Aliongea mmoja ya mwanajeshi mwenye jino la mbele lililokatika.
“Upo sahihi Kamanda Makwera alitumia madaraka yake vibaya kwa faida zake mwenywe , alistahili kufa , nipo tayari kufanya chochote ambacho Master Roma ataniambia”Mwingine aliunga hoja juu kwa juu lakini kauli zao hazikumfurahisha Roma hata kidogo na palepale alichukua bunduki kutoka kwa mwanajeshi aliekuwa karibu yake na ilikua kwa spidi sana wale wanajeshi wote wawili waliokuwa wakimpamba walipasuliwa kichwani palepale na kudondoka chini.
Kila mmoja alimwangalia kwa mshituko mara baada ya tukio hilo na walishindwa kujua anataka kufanya nini.
Roma hakujali mshangao wao kwani alitupa siraha pembeni huku akiwa na uso wa kutokuathirika na kile alichokifanya.
“Bado hamjaelewa tu , nimesema onyesheni utii wenu kwa Taifa sio mimi , au mnanniona mimi ni Makwera wenu kudhania mimi ni mhaini ambaye muda wowote naweza kuanzisha vita?”Aliongea Roma na wale wanajeshi wote waliangaliana huku sura zao zikipauka kwa wasiwasi
Mpaka hapo walijua Roma ni mtu ambaye hatabiriki ndio maana moja kwa moja walikosa ujasiri wa kuongea tena kwa kugopa kusema kimakosa.
“Master Roma tafadhari punguza jazba , tupo tayari kupigana kwa ajili ya taifa letu tutapigana zidi ya wahaini wote wa nchi mpaka mwisho wa maisha yetu “Aliongea mmoja wapo alieonekana kumuelewa Roma na wengine wote walionekana kuelewa na waliongea kwa sauti kwamba wanakwenda kupigana na kuonyesha utii kwa manufaa ya taifa na sio kwa ajili ya mtu mmoja mmoja.na hata wale waliojificha waliweza sasa kutokea misituni na kuungana na wengine.
Ni kama vile dakika hio ilikuwa ikisubiriwa kwani muda uleule waliingia wanajeshi makomandoo kwa spidi zote na kuimarisha ulinzi huku wale waliokuja na Marehemu Afande Makwela wakiponywa siraha zote na kukalishwa chini ya ulinzi.
Dakika hio hio Brigedia Jenerali wa jeshi mkoa waSongea , Afande Murasa aliiweza kufika akiwa na kombati za jeshi.
Na mara baada ya kutoka tu kwenye gari alimsogelea Afande Kweka na kumpigia saluti ya heshima na kugeukia wanajeshi aliokuja nao na kuwapa maelekezo huku yeye akiongozana na Afande Kweka mpaka kwenye ofisi yake ndogo kuanza mazungumzo.
Kila kitu kilitokea kwa kasi sana , ni swala la dakika kama ishirini tokea kuanza kwake na kumalizika .
Afande Tobwe alimwangalia Roma bila kuongea chochote , ijapokuwa walikuwa ni Wakwe lakini alimuogopa.
Kila mwanajeshi aliekuwa njiani alimpishaRoma kwa woga sana na yeye hakujali na muda huo alikuwa amechafuka mwili mzima kwa damu na alitembea kuelekea upande wa nyuma alikomuona Denisi.
“Kaka niseme ujasiri wako umetuokoa , kwa staili hii nadhani kwanzia leo hii kila mtu ndani ya jeshi atatuogopa”Aliongea Denisi mara baada ya kusogelewa na Roma.
“Ndio unavyoona?”Aliongea Roma kwa sauti kali na ghafla tu huyu hapa ashaishika shingo ya Denisi na kuining’iniza hewani.
Kitendo kile kilishangazaza watu sana akiwemo Damasi mwenyewe na hata afande Kweka ambaye alishatoka nje akiambatana na Afande Murasa.
“Master Roma tafadhari punguza hasira?”Walinzi waliongea kwa hofu.
“Ndio, Denisi ni mdogo wako”Wasaidizi na walinzi walijaribu kubembeleza
“Roma tafadhari naomba usimuumize mdogo wako”Sauti ya Damasi iliweza kusikikika kwa nyuma huku akisukuma watu kupita kusogea mbele.
Damasi hakujali tena kule kumuogopa Roma bali alimsogelea na kumshika mkono wake wa kushoto akimbembeleza.
“Roma mwanangu nakuomba , mdogo wako najua amefanya makosa mengi nyuma lakini sasa hivi amebadilika , unatakiwa kumpa na yeye nafasi ya kijirekebisha , huwezi kumshambulia tu bila sababu”Aliongea huku akianza kutoa machozi ya kiutu uzima.
“Roma umesema unaamini Denisi ndio anakufanyia njama lakini huwezi kumshambulia bila ushahidi”Aliingilia Afande Kweka.
Ijapokuwa alikuwa akisita kumuachia Denisi lakini kutokana na mbinu nzuri aliokuwa nayo Denisi kujificha hakuwa na uwezo wa kumuua bila kuwa na ushahidi wa kueleka.
Roma alimwangalia Denisi kwa macho ya kumpa tahadhari na kisha akamsukumia mbali.
Damasi alijikuta akihema kwa ahueni huku akimwangalia Roma kwa macho ya shukrani.
“Brigedia Murasa amenipa taarifa hapa ya kinachoendelea na Afande Tozo yupo Dar es salaam na uchunguzi unakaribia kumalizika na wote waliohusika watakamatwa na kupelekwa mbele ya sheria na hali ya hewa ikitulia watatuutaarifu”Aliongea Afande Kweka.
“Nadhani wanajua kabisa kilichoendelea hapa na wanaangalia tu namna ya kulimaliza hili swala”
“Haijalishi makusudio yao ni nini , walionekana wapo tayari kutumia hela zao kutaka kutuyumbisha lakini sasa yameisha na hili watalimaliza kwa njia zao za kisiasa”
“Vyovyote vile ni sawa tu , hata hivyo sitaki kuuwa viumbe dhaifu tena”Aliongea Roma na kisha aliondoka.
Wakati tukio lote hilo linatokea Edna alikuwa yupo upande wa nyuma.
Muda ambao Roma alifika upande wa nyuma kuingia kwenye Korido ya chumba chao aliweza kumuona Edna ambaye alikua akitembea kurudi nyuma na mbele akionekana kama mtu mwenye kuchanganyikiwa.
Lakini alijikuta akisimama mara baada ya kumuona Roma akiwa kama mwenye hali ya furaha lakini alijikuta akishituka mara baada ya kuona damu katika mwili wake.
Roma aliweza kujua mshangao wa Edna ulikuwa ukihusiana na nini na alijikuta akinusa shati lake lwenye damu na kutoa tabasamu la kifedhuli.
“Mh .. damu zinanuka vibaya hizi , Edna mke wangu usiwe na wasiwasi nitaenda kuoga kwenye chumba kingine”Aliongea Roma huku akitaka kugeuka kuelekea upande mwingine wa vyumba lakini Edna alimkimbilia na kumshika mkono.
“Unaongea kuhusu nini wewe , kwanini ukaoge kwenye chumba kingine , unataka watu wanifikirie vibaya, tumekuwa pamoja kwa muda mrefu hivyo nishazoea , ni damu tu na vinyama nyama kwanini unataka kuyakuza, hebu nifuate huko”Aliongea huku akitangulia kuingia ndani.
Roma moyo wake uliridhika mara baada ya kusikia meneno hayo kutoka kwa mke wake na alishukuru kumuona Lanlan hayupo.
Edna alimwingiza Roma mpaka kwenye bafu lao na baada ya kufika alifungua vifungo vya shati lake pamoja na suruali na kutupia pembeni na baada ya hapo alifungulia bomba la maji ya mvua na kuacha yamwagikie Roma huku yeye akitoka tena na kuchukua sabuni maalumu ya kuogea ya marashi na kurudi nayo akiwa ameshikilia taulo.
Roma alishangazwa na namna Edna ambavyo hakuzingatia mwili wake uliokuwa hauna nguo .
“Mke wangu ni lini umebadilika , nakumbuka mara ya mwisho ulikuwa na aibu hata ya kuingia kwenye chumba changu”Aliongea Roma na kumfanya Edna kushituka kwani akili yake haikuwa ikizingatia mwili wa Roma bali damu zilizokuwa kwenye mwili wake.
“Nini?”
“Ndio maana wahenga wanasema ndoa ni kaburi la mapenzi , nadhani kuanzia sasa inabidi nikuite Mama Lanlan”Aliongea Roma kwa kumtania.
“You Suck , nilikuwa nikijaribu kukusaidia kukusafisha na sasa unaanza kunichokoza , nitaenda kulala na Lanlan mimi wewe endelea”
“Edna my Darling , nilikuwa nikitania , usichukulie siriasi , ukiachana na hayo Lanlan yuko wapi?”
“Karudi kulala tena kwenye chumba cha babu yake , inanifanya niwe na wasiwasi maana kila akishiba tu anakimbilia kulala”
“Huna haja ya kuwa na wasiwasi , bado ni mdogo na kuvuna nishati za mbingu ni kuumiza ubongo hivyo ni kawaida, kipindi hicho mimi sikuweza hata kuuruhusu usingizi unichukue ili kuweza kuishi , nilihitajika kuvuna nishati kadri niwezavyo ndani ya muda mfupi kabla ya maadui zangu hawajanipata .. lakini kwa yeye kila kitu anacho na hana haja ya kuhofia usalama wa maisha yake , hivyo naweza kusema amebarikiwa kuliko nilivyokuwa mimi , tena hili jambo linanijia akilini sasa hivi , tokea nije Tanzania nilikuwa nikijiwazia mimi mwenyewe lakini siku hizi kila ninachofanya ni kwa ajili yako na yeye.”Aliongea Roma huku akiendelea kuwa bize na kujisafisha.
Na kukabidhiwa Taulo na mke wake kujifuta maji tayari nguo Edna ashaziandaa na kumsaidia kuvaa naRoma mara baada ya kukaa chini picha ya Denisi ilimjia akilini mwake na kumfanya kuanza kuwa na wasiwasi usioelezeka.
Roma alisita sita kumfanya Denisi chochote kutokana na kujali uwepo wa Damasi tu.
“Nitatafuta namna ya kumuua kwa siri”Alijiwazia Roma.
“Unafikiria nini tena?”
“Sio jambo kubwa , nawaza ni kwa namna gani huyu mzee ataweza kulimazliza hili swala”
“Najua sikupaswa kuuliza kilichotokea , lakini nataka kusikia ukweli wote kutoka kwako”
“Nini unataka kujua?”
“Kama bado tupo hatarini?”Aliongea Edna akiwa na wasiwasi.
“Bado nipo na hivyo usiwe na wasiwasi”
“Kama ni hivyo basi niahidi kitu kimoja , kama kitu chochote kitatokea niambie , unanijua mwenyewe mimi sio mwanamke ambaye ni mjinga , nina uwezo wa kuchanganua mambo pia”Aliongea kwa upole na kumanya Roma kumuona mke wake amegeuka na kuwa mke mtiiifu mbele yake na kuonekana kama mtoto.
Roma palepale alinyanyua mkono wake kutaka kushika shavu lake lakini mara baada ya kufikiria kitendo alichokifanya dakika kadhaa zilizopita alijikuta akiishia njiani na kuurudisha , ni kama akili yake ilikuwa ikihofia kumchafua mke wake.
Edna aliona kitendo kile na palepale alichuhukua mkono wake na kuuweka kwenye shavu lake.
“Kwanini hujafanya ulichodhamiria wakati sijakuambia uache , au unaniona mimi mchafu?”
“Hapana mikono yangu ndio nahisi bado inanuka damu na hata kucha zangu sijazisafisha vizuri”
“Nimeongea lolote kuhusu hilo ?”Aliuliza Edna huku macho yakianza kuwa mekundu.
“Mhmh..”Roma alishindwa kuendelea kuongea zaidi ya kuguna na Edna alimsogelea karibu zaidi.
“Hivi unajua kwamba hata mikono yako ichafuke vipi na damu au ni maiti ngapi umweza kushika kwangu ni mikono hii hii ambayo ilinisaidia kipindi nilichokuwa kwenye matatizo , ni mikono hii ambayo ilinikumbaita na kunifanya nilale na ni hiii ambayo ilimshikilia binti yangu .. haitotokea nikaiona ni mikono michafu kwasababu hii ni mikono ya mume wangu , mikono ya mtu ninaempenda”
Roma aliguswa na maneno yake na hakuamini kama ni Edna ambaye anaongea.
“Edna mke wangu nani kakuandikia Script au ni zile roboti za mtandaoni”Alitania Roma.
“Mimi nipo siriasi”Aliongea na kumfanya Roma kumeza utani wake na palepale alisimama na kumbeba juu juu na kumrushia katikati ya kitanda na Edna ashajua nini kinakwenda kutokea.
“Tiusifanye sasa hivi bado ni mapema na sijaoga bado”Alilalamika .
“Mke wangu wewe hujali kama mikono yangu ni michafu kwanini nikuache uoge , isitoshe My darling wife unanukia vizuri muda wote”Aliongea na baada ya pale alijichimbia kwenye kifua cha mkewe na kuanza kazi na ndani ya madakika kadhaatu Edna hakuweza kumpinga tena na kumuacha afanye atakavyo lakini ghafla tu Roma aliacha anachokifanya na kusimama huku akiangalia mlangoni.
Edna alishangaa mara baada ya Roma kuacha lakini alielewa mara baada ya kuona mlango ukifunguliwa.
“Mommy, mommy! Is dady back”(Mama , mama , je baba amerudi)
Lanlan mara baada ya mwili wake wote kuingia ndani alianza kukagua mazingira , mashavu yake yalitingishika mara baada ya kuwaona wazazi wake na alianza kuonyesha hali ya kutoelewa hali inayoendelea.
“Dady ,mommy what kind of game are you playing?”Aliuliza Lanlan akisema ni mchezo gani wanacheza.
Edna alijikuta akibadilika rangi na kuwa mwekundu , alitamani aingie uvunguni , ilikuwa ni afadhari nguo zake bado hazikutolewa mwilini.
“Baba na mama yako tunachukua mazoezi sawa chubby”Aliongea Roma
“Mazoezi!! , Lanlan anataka pia kuchukua mazoez na nyie”
“Lanlan utachukua mazozi kama haya ukishakuwa mkubwa… sasa hivi nenda kacheze na babu yako , usije huku ndani mpaka tutakapotoka”Aliongea Roma lakini Lanlan alionyesha hakufurahishwa na kauli ya baba yake na aliendelea kumwangalia Roma kwa kutia huruma kwani aliona ni kama vile baba yake anamfukuza.
Roma suruali yake ilikuwa ikishituka shituka kama ina uhai na akili yake ni kama anaelekea kuupata uchizi.
SEHEMU YA 590.
Hali aliokuwa nayo Roma ilimfanya Edna kutamani kucheka huku akisahau aibu yake.
“Lanlan kuwa mtoto mzuri na utoke , Lanlan ushawahi kuonja nyama ya Kondoo wa kukaanga?”
“Kondoo ndio wanyama gani baba?”
“Ni wanyama wenye tabia ya kulia, ‘Baa .. baaa’ , ni nyama nzuri sana ikikaangwa, nitahakikisha unaonja kitu kipya kama utaenda kuendelea kucheza na babu yako”
“Daddy you have to keep your promise , I’ll go to play wirh great grandfather”Aliongea akimaanisha kwamba Roma anapaswa kutii ahadi yake na yeye anaenda kucheza na babu yake mkubwa na akakimbilia nje huku akisahau kufunga mlango tena na kumfanya Roma kung’ata meno yake kwa hasira lakini hata hivyo alimuona Lanlan ni mwepesi kudanganyika kila nyama inapotajwa na alishuka kwa hasira na kuubamiza mlango.
“Huyu litoto tundu napaswa kulifundisha , anaachaje mlango wazi kwa mfano” Aliongea na kama chui alimrukia Edna kitandani na namna suruali yake ilivyomtoka kiunoni huenda ni rekodi mpya ya dunia.
Dakika chache mbele chumba chote kilijaa sauti za mguno wa kimahaba kutoka kwa Edna.
*******
Upande mwingine jijini Dar es salaam wakati Roma yeye akijipongeza baada ya kuua ilikuwa ni zamu ya Raisi Senga kukamilisha kile alichopanga.
Hakuamini kila kitu kilienda kama alivyopanga , ijapokuwa namna ambayo Roma ametatua tatzio ilikuwa ndio kama alivyotarajia lakini ukweli ni kwamba aligundua alikuwa na mtoto ni katili mno na kuzidi kumugoopa mara mbilimbili.
Katika jengo la ikulu chumba cha mikutano kulikuwa na kikao kizito ambacho kilikuwa kimeitishwa tokea jana yake na hakikuhusisha wale watu tu ambao walikuwa wamehusika katika mpango wa kumtengenezea Roma matukio.
Raisi wa Visiwani pia alikuwepo katika kikao hicho na baadhi ya wanasiasa wakubwa ambao Raisi Senga alikuwa akijua kabisa utulivu uliokosekana nchini ulianzishwa na wao.
Muda huo mara baada ya kuingia katika chumba hicho na kunagalia sura za kila mtu alietii wito alijikuta akitabasamu ndani kwa ndani na kujiambia yes huo ndio muda wa kukamilisha ndoto yake ya siku nyingi.
Wakati kikao hicho kikiwa kinaendelea ndani ya ikulu, upande wa mitandaonni wananchi walikuwa wamecharuka mara baada ya sauti zinazosemekena kuwa za Waziri wa nishati , Waziri wa ulinzi, Afande Makwera na Mke wa raisi Kigombola kusambaa kwa kasi.
Maudhui yaliokuwa kwenye sauti hio ndio kitu kilichowafanya wananchi kuweza kusikia kila kitu kilichokuwa kikiendelea kwani mipango yote ya Afande Makwera kushawishiwa kumshambulia Afande Kweka na mjukuu wake ziliweza kusikika , ijapokuwa hakukuwa na uthibitisho wa moja kwa moja wa kusema sauti hizo zilikuwa za watu hao lakini zilifanya kila mtu kuwa katika Dilema na kubwa zaidi ni kwamba mtu alieanza kuzisambaza alisifika kuwa kinara kwa kumkosoa Raisi Senga mtandaoni.
Ni dakika chache tu mara baada ya Sauti hizo kusambaa ndipo taarifa ya kifo cha Afande Makwera kilipoweza kutangazwa kwa kuthibitishwa na mkuu wa majeshi wakati alipokuwa akiongea na waandishi wa habari jijinni Dar es salaam , huku sababu halisi kuwekwa wazi , uthibtishwaji wa kifo hicho na namna kilivyotokea haikuhitaji elimu ya kuthibitisha yale maongezi ya sauti yaliokuwa yakisambaa mtandaoni kuwa kweli.
Lakini swali moja tu liliibuka nani ambaye aliwarekodi wenzake kwani vikao hivyo ni vya siri,lakini ilibakia kuwa habari ilioibua mjadala na kumshuku huyu na huyu .
Wakati hayo yanaendelea upande wa Mheshimiwa raisi wa visiwani alikuwa amenywea sana kiasi cha kushindwa hata kumwangalia Raisi Senga usoni , ile hali yake ya kujiamini aliokuwa nayo siku kadhaa zilizopita ilikuwa imemshuka sana na hakuwa yeye tu bali pia kwa baadhi ya wanasiasa wengine.
Hali ya woga ilianza kuwatawala kila mmoja huku wakiwa kama watu ambao wanasubiri hukumu yao kutolewa na Senga, lakini kwa wakati mmoja na wao walikuwa na maswali lukuki imekuwaje mipango yao ikawa inajulikana kwa uwazi namna hio na walianza kuangaliana kwa hasira.
Wakati ambao walikuwa wakijiuliza maswali hayo , upande wa Raisi Senga na yeye alikuwa akijiuliza swali ni nani ambaye yupo nyuma yao , kwani hata kabla ya kufanya kikao hicho alikuwa na mazungumzo ya siri na Raisi wa Visiwani na kujaribu kumhoji lakini mwisho wa siku na yeye hakuwa na jina la mtu ambaye yupo nyuma yao zaidi ya kumjua akiitwa The Don.
Raisi Senga ijapokuwa kila kitu kilienda upande wake , lakini kile ambacho siku zote alikuwa na wasiwasi nacho ni kama kimefufuka upya.
“The Doni amerudi tena?”Ndio kauli aliojiambia.
Raisi Senga ni kwa muda mrefu sana ambao alikuwa akihitaji kumjua The Doni , mtu ambaye alikuwa nyuma ya hayati Raisi mstaafu Kigombola lakini mpaka siku hio hakuwahi kumjua wala kumuotea ni nani , mwanzoni hisia zake zilimwambia ni Roma lakini hakuweza kuthibtisha hilo na kwa yalitokea ni kama yamemthibtishia kabisa kwamba Roma hakuwa The Doni.
Hivyo licha ya kushinda mpango wake lakini bado moyo wake ulikuwa mzito juu ya huyu mtu aliejiita The Doni na kuna hisia pia zilimwambia huenda Denisi ana ukaribu na The Doni kwasababu Yan Buwen alikuwa na ukaribu na The Doni kwa maelezo ya hayati Kigombola, lakini licha ya kuwaza sana hakutaka kusumbua kichwa chake kwanza na kuanza kufikiria namna ya kumaliza swala lililokuwa mbele yake.
Kikao hicho kilijumuisha na Katibu mkuu wa Chana cha Maendeleo na waliweza kujadiliana kwa zaidi ya masaa manne huku mwishoni wakikubaliana vitu vingi.
Lakini matokeo ya kikao hicho yalijumuisha kwa kukamatwa kwa baadhi ya watu ambao sauti zao zilisikika na jeshi la polisi kwa ajili ya uchunguzi huku mheshimiwa Raisi wa Visiwani akipewa nafasi ya mwisho ya kwenda kutuliza wananchi wake ndani ya masaa mawili tu.
Wakati kila kitu kikienda kila alivyopanga hatimae Raisi Wa Visiwani mheshimiwa Huseni Husani alitoa hutuba fupi akiwa ikulu na mbele ya jopo la waandishi wa habari na viongozi wenzake kuwaasa wananchi kuwa na utulivu huku akienda mbali kukanusha Roma kuhusika katika mauaji ya Kamanda Razaq na kusema yote hio ilikuwa ni mipango ya adui kutaka kuigawanya nchi na uchunguzi yakinifu unaendelea kumbaini.
Baada ya hotuba ya Raisi wa Zanzibar , Muongeaji mkuu wa Serikali alitoa Tangazo kwamba siku inayofuata Mheshmiwa Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania atalihutubia taifa kupitia ikulu ya makao makuu ya nchi mkoani Dodoma.
Kutarajiwa kwa hotuba yake hio iliwafanya wananchi wa Tanzania kuwa na shauku ya kutaka kujua kile ambacho Raisi anakwenda kuhutubia.
*********
Kabla hayo yote hayajatokea upande mwingine mwanadada Suzzane ni moja ya watu ambao walikuwa kwenye tafakari nzito sana kuhusu bosi wake Edna kwa kauli yake ya mara mwisho ambayo alimpatia siku moja kabla ya kustaafu kuwa CEO wa kampuni.
“Suzzane kwanzia sasa nataka uachane na uchunguzi wote wa maswala yanayohusiana na mama yangu , najua kila kitu kwa sasa na nawaza namna ya kukabiliana na kilichopo mbele yangu , sitokuambia ni lakini taarifa hii ni siri kwako na asitokee mtu yoyote ukamwambia”
Kauli hio ya Edna ilimchanganya sana mwanadada Suzzane , sababu kubwa ya kumchanganya ni kutokana na namna ambavyo aliitamka , lakini pia kukosa maelezo sahihi ya kile kilichotokea siku kadhaa zilizopita katika hoteli ya Peacock.
Suzzane alikuwa ni tofauti na Edna katika siku ile , alikua kwenye mshangao na maswali mengi kwa kile kitu kilichotokuwa kimetokea , alijiuliza Edna alitoa wapi ile pete na swali hili hakujiuliza yeye mwenyewe bali aliulizwa na wanachama ambao walikuwa ni wa taasisi ambayo ni kama mara ya pili anaisikia jina, jumuia ya siri ya kitaasisi iliojiia Ant- illuminat.
Kitu pekee ambacho kilimfanya Suuzzane kutaka sana kujua kuhusu mama yake Edna ni kutokana na kifo cha mpenzi wake Dr Elvice Daniel , siku zote alitamani kulipa kisasi ka wale waliomuua mpenzi ake kabla hata hawajafunga ndoa lakini mpaka wakati huo hakuwa amepata mwanga namna ya kulipiza kisasi.
Sasa ni masiku tokea mrembo Suzzane akiwa katika mawazo , siku ambayo nchini Tanznia kukiwa na mambo makubwa yanayoendelea , Suzzane yeye alikuwa ndani ya jiji la Doha nchini Qatar.
“Karibu sana Suzzane kwenye umoja wetu wa siri , umefanya maamuzi sahihi sana”Sauti ya mrembo Nadia Alfonso iliweza kusikika ndani ya gari la kifahari refu aina ya Limuosine , gari yenye ufahari wa kila aina ndani yake na kumfanya Suzzane kuwa mara yake ya kwanza kupanda gari aina hio.
“Asante Nadia lakini bado ni mwenye wasiwasi?”Aliongea Suzzane na kumfanya Nadia kutabasamu kidogo.
“Wasiwasi wako ni wa muda , ukishajua nini maaana halisi ya umoja wetu basi hofu yako yote itaisha , kwasasa uvae ujasiri unapokwenda kutamblishwa kwa mara ya kwanza na kupewa nafasi ya awali ya uanachama na kupokea misheni yako ya kwanza ya kujithibitisha”
“Misheni ya kwanza ya kujithibitisha!!!?”Aliuliza Suzzane na kumfanya Malkia wa sheria , mrembo Nadia kutoa abasamu na kuangalia nje.
“Tushafika Suzzane”Aliongea Nadia na kumfanya Suzzane kuangalia mazingira ya nje na kuweza sasa kuelewa kwamba akili yake ilikuwa mbali sana kwnai hakujua hata ni namna gani waliweza kuingia ndani ya ukuta mrefu huku mbele yao kukiwa na jengo kubwa kama hoteli.
*******
Muda wa mchana Roma aliweza kutoka chumbani bila wasiwasi , lakini upande wa Edna alikuwa na aibu kwani ni kama vile kila mtu ndani ya nyumba hio alikuwa akijua kile kilichokuwa kikiendelea na aliishia kuangalia chini huku akitembea kwa mwendo wa kujilaizmisha kwani miguu yake ilikuwa haipo vizuri.
Roma mara baada ya kutokezea kwenye bustani mahali ambapo Afande Kweka hukaa na kuota moto, aliweza kumuona mzee wake akiwa na Lanlan wakiwa katika umakini mkubwa wa kimaongezi.
“Nyie watu mnaongea nini mpaka kuwa na umakini hivyo?”Aliuliza Roma kwa kiswahili
“Daddy , babu alikuwa ananihadithia stori namna alivyoweza kuwashinda watu wabaya”Aliongea .
“Babu yako huyo anajua kujisifia tu kama utaendelea kumsikiliza”
“Ukorofi huo”Aliongea huku akimpotezea na kujivuta mwili na muda uleule kijakazi aliweza kuwasogelea.
“Master mtu wa hoteli ametupigia simu na kuuliza kama kuna kingine zaidi tunatakakuagiza”
“Waambie waandae tulichowaagiza kama kuna cha kuongezea wanaona inafaa basi wafanye hivyo”Aliongea na yule mfanyakazi wa kiume aliitikia na kuondoka.
“Mnazungumzia nini mambo ya hoteli hoteli?”
“”Unapata wapi ujasiri wa kuniuliza wakati ni wewe mwenyewe ulioemwambia binti yako utampa nyama ya mnyama anaelia ‘Baa.. baa ‘wa kukaanga, mimi hao kondoo nawatolewa wapi muda huu , nimeamua kupitia hoteli maarufu hapa Iringa wanaopika nyama ya Kondoo watuandalie”
“Asiee wewe mzee upo makini , wakati naongea hata sikuwa siriasi , angalau umefanya mambo kua mepesi hehe..”Aliongea Roma na kumfanya Afande Kweka kutoa tabasamu la kifedhuli ambalo linafanana kabisa na la Roma licha ya uzee wake.
“Lanlan leo usiku ukalale na wazazi wako na umwambie baba yako akuhadithie stori , anazo stori za kimapigano nzuri zaidi kuliko za kwangu”Aliongea na kumfanya Lanlan kumgeukia baba yake kwa shauku aone anasema nini.
Roma alijikuta midomo yake ikicheza alijua tu huyo babu yake anamfanyia makusudi, alikuwa akimzuia kutofanya mazoezi na mke wake.
Edna hakuwa mbali na aliweza kusikia kila kitu lakini hata hivyo alikuwa na shauku na yeye ya kusikia stori ambayo Roma atamwambia Lanlan.
“Kijana najua una Stamina nzuri lakini ni kheri kujizuia muda mwingine..”Aliongea huku akipotezea muonekano wake
*****
Upande mwingine nje ya chumba cha Damasi alionekan Denisi ambaye ni kama vile alikuwa akijishauri lakini dakika ileile aligonga mlango na ukafunguliwa na mama yake ambaye alishangaa kumuona Denisi.
“Vipi Denisi uliesema unaenda kumsaidia baba yako baadih ya majukumu kwanini upo hapa?”
“Kila kitu kinaonekana kumalizika hivyo hakuna kingine ambacho ninaweza kufanya”
“Kama ni hivyo , mbona unaonekana kama una kitu unataka kuongea na mimi?”
“Ndio mama , lakini sio kitu kikubwa sana, nilitaka kuona unaendeleaje , lazima utakuwa kwenye mshituko mkubwa kwa kilichomtokea Binamu Aloni na tukio la leo pia”Aliongea na kumfanya Damasi kutabasamu kwa mbali na kisha akamshika mtoto wake mkono.
“Denisi najua unanijali sana kama mama yako ila nipo sawa , ninajisikia vizuri kwa kupumzika kwa muda mrefu kidogo , kaka yako ndio ambaye anannigopesha , ni mtu mwepesi sana na hasira zake”Aliongea na kumfanya Denisi kumwangalia Damasi kwa macho ya huruma.
“Mama , kwanzia sasa jitahidi kujali afya yako , usiwe na wasiwasi sana na siku zote kumbuka afya yako ni muhimu”Aliongea na kumfanya Madam Damasi kuwa na mshangao kidogo na kumwangalia Denisi kwa wasiwasi.
“Kwanini unaongea maneno hayo ghafla tu , ni kama vile hayapo sawa”
“Mama ni kwasababu binadamu tunabadilika muda mwingine hata kama hatutaki kubadilika , siku zote tunalazimika kufanya maamuzi na kubadili maisha yetu kwa sababu ya watu na matukio “
“Unazidi kunitia wasiwasi na maneno yako Densi kuna kitu chochote kinakusumbua , niambie mimi mama yako na kama sitoweza kukusadia nitakuombea kwa baba yako akusaidie yeye”
“Hapana sina tatizo , nimefurahi kwamba upo sawa , ninatoka sasa kwenda kambini kwani kuna mambo nataka kudili nayo na naweza nisirudi kwa muda”
“Sawa nenda mwanangu huna haja ya kuwa na wasiwasi na mimi”Aliongea Damasi bila ya kufikiria mara mbili mbili na baada ya Denisi kutembea mita kadhaa aligeuka na kumwangalia mama yake aliekuwa akimwangalia.
“Kwaheri ya kuonana mama”Aliongea ndani ya nafsi yake na Damasi ambaye hakujua nini kipo kichwani mwa Denisi aliinua mkono wake kwa tabasamu na kumpiugnia mkono wa kwaheri bila kujua hio ndio kwaheri ya moja kwa moja kuiona sura ya mwanae wa kiume katika uhalisia.
Na mara baada ya kuingia kwenye gari lake palepale macho yake yalibadilika rangi na kiini cha macho kupotea na kuwa kama vile ni sananmu la rangi ya Silver.
ITAENDELEA.
BurudanNILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI: SINGANO JR
SEASON 21
SEHEMU YA 601.
Moli alijitahidi kupotezea hofu ya kumuogopa Roma na kisha akaanza kuwaelezea kuhusu eneo hilo lilivyo.
Kwa maelezo yake ni kwamba eneo hilo lilikuwa likiiitwa ulimwengu wa mapepo kutokana na kwamba viumbe ambao walikuwa wakipatikana hapo ni wale majini ambao walikuwa wakijifunza mbinu za kuvuna nishati ya mbingu na ardhi ili kulipa nguvu pepo la ndani(inner demon) kutawala mwili.
Inaaminika kwamba kila binadamu au kila kiumbe ana pepo lililo ndani yake na ndio pepo hio ambalo huibua hisia hasi katika roho ya kiumbe , kwa mfano wa hisia hasi ni kama chuki husda na wivu na mengineyo ya mfano huo.
Sasa kuna aina mbili za kuvuna nishati za mbingu na ardhi aina ya kwanza ni ile ya kulishinda pepo la ndani na hatimae kuweza kupata ufunuo wa siri za ulimwengu na aina ya pili ni kwenda kinyume chake yaani kulipa nguvu pepo la ndani ili kukutawala na kukufunulia siriza ulimwengu.
Aina hizi mbili za uvunaji wa nishati ndio ambazo zinatofautisha majini, kuna majini ambao wanawachukia binadamu na kuwaona ni viumbe dhaifu na kuna wale ambao wanaheshimu binadamu , asilimia kubwa ya majini wabaya wanaochukia binadamu ndio ambao wanajifunza mbinu za nishiti za kuamsha pepo la ndani(inner demon).
Sasa hapo zama za kale baada ya majini wanaojifunza mbinu za kuamsha pepo kuonekana ni hatari kwa binadamu walitokea kutenganishwa kwa kutolewa katika ulimwengu wa majini wa kawaida na kutengwa katika ulimwengu mwingine ambao haukuwa wa kawaida , ulimwengu ambao ilikuwa ni ngumu kuweza kuwasiliana na binadamu tofauti na majini ambayo yanavuna nishati kwa ajili ya kushinda pepo la ndani.
Yaani kwa maneno marahisi wale majini wazuri kama wa Hongmeng , Panas na Kekexil hawa wanavuna nishati kwa staili ambayo ni kwa ajili ya kushinda hisia zao hasi na hatimae kufunuliwa wasio yajua, ni kama mtu anavyosali au kuswali na Mungu wake ndio kinachotokea.
Ulimwengu huo sasa wa majini yanayoenda kinyumena njia za kawaida ndio ukapewa jina la Demonic Realm, yaani ulimwengu wa majini mapepo.
Njia pekee ambayo iliwekwa kwa ajili ya kusafiri kuingia katika ulimwengu huo ni kupitia minara au majengo maalumu ambayo kazi yake ni kuvuta kila aina ya nguvu kubwa ya kipepo katika dunia ambayo binadamu hawezi kuhimili.
Moli anasema katika watu ambao waliweza kuingia katika ulimwengu huo kila mtu aliingia kwa staili yake , kuna ambao waliingia kupitia minara iliokaa kimajengo na kuna wengine ambao waliingia kwa njia ambazo hazikuwa zikieleweka na kushindwa kupata majibu.
Mnara inayozungumziwa hapa ni mfano wa ile ya kuongozea meli au ndege sio minara ya simu, mara nyingi inajengwa kama nyumba flani hivi kwenda juu na hata ule wa Shushani ulikuwa hivyo hivyo ila tu ni kwamba ulitofautiana na minara mingine ya kichina ya kitamaduni.
Kwa duniani kuna uwezekano wa kuwa na njia nyingi za kuingia katika ulimwengu huo lakini ukiwa ndani ya ulimwengu huo wa Kidemonic njia ya kutoka nje ni moja tu ambayo ni Mnara wa Mbingu.
Hivyo ilikuwa ni rahisi kusema ulimwengu huo ni wa viumbe hatari visivyokuwa na huruma kutokana na namna yao ya kujifunza mbinu ya kuvuna nishati ilikuwa ikiendana kinyume na ile ya kawaida na kuwapelekea kupandwa na mashetani .
Sasa Moli anamwambia Roma kwamba ili aweze kutoka hapo ndani lazima autafute huo mnara wa mbingu ambao upo katikati ya ziwa na aweze kupitia mapigo tisini na tisa ya radi rangi ya zambarau na bluu ndio aweze kutoka.
Inaaminika kwamba mapigo hayo ya Radi tisini na tisa hayakufanana na yale mapigo tisa ya duniani , mapigo hayo katika ulimwengu huo huwa yana athari za kipekee sana ya nguvu za giza kama vile nishati za giza na nguvu ya kiroho ya giza.
Anasema imepita zaidi ya miaka elfu kumi na haijawahi kutokea jini lolote ambalo liliweza kufaulu kupigwa na mapigo tisini na tisa ya radi na kuweza kutoka katika ulimwengu huo au kupona.
Hivyo kutokana na hilo kila kiumbe kilichoingia katika ulimwengu huo pamoja na majini yenyewe ya pepo yaliokuwepo yalikubali kwamba hakuna namna ya kuweza kutoka katika ulimwengu huo kupitia huo mnara labda kwa njia nyingine ambayo bado haijagunduliwa.
“Hii sehemu ambayo tupo sasa ni Msitu Giza aneo ambalo linamilikiwa na Mbweha wa Jade, ukienda kaskazini mbali huko kuna koo nne za kimajini katika msitu wa Mianzi Zambarau , ukienda mbali mashariki huko unakutana na ukoo wa Mazimwi hatari, eneo ambalo linafahamika kama Bonde Joka ambao ukoo wenyewe unafahamika kwa jina la koo ya Joka kuu.
“Bro mimi nina miaka mia tatu hivyo inanifanya kuwa mkubwa kwako, hivyo mimi kama kaka yako ninakushauri kwamba ijapokuwa una nguvu kubwa za kimaajabu kuliko mimi haziwezi kuwa kubwa kuliko wakuu wa koo husika”Aliongea Moli akimpa Roma tahadhari.
Sophia alionekana kuogopa sana kutokana na maelezo hayo na mbaya zaidi aliposikia kuhusu uwepo wa majini wenye nguvu zaidi ya Roma.
“Je unajua miliki za kijini nje ya hapa kama vile Hongmeng , Kekexil na Panas?”Aliuliza Roma ambaye hakuwa katika hali ya woga hata kidogo.
“Nishawahi kusikia kuhusu Hongmeng na inasemekeana ni miliki ya majini wadhaifu tu wa kawaida kuhusu sehemu zingine sijapata maarifa huenda ni kutokana na nguvu yao kuwa ndogo”
“Kwahio unasema kwamba ulimwengu huu ndio wenye nguvu zaidi kuliko wa majini ya maeneo mengine”
“Inaweza kuwa kweli au isiwe kweli , lakini unapaswa kuelewa kwamba hii sehemu ilikuwepo miaka zaidi ya elfu hamsini iliopita kabla hata kwa ujio wa wale viumbe kutoka sayari nyingine waliojiita miugnu miaka elfu ishirini iliopita, kuna sehemu nyingine ambazo zimetengenezwa kwa ajili ya kuwafanya binadamu kuwa salama, sisi tunaamini kwamba roho ya kiumbe chochote haipotei hivyo kama kweli miaka iliopita kabla ya ujio wa binadamu kulikuwa na wanyama wakubwa na wakali kama inavyohadithiwa basi roho zao zitakuwa zimeshikiliwa katika upenyo maalumu kama hili eneo?”
Roma alielewa baadhi ya maneno ya Moli , ilikuwa ni kweli kabisa miugu walikuja miaka elfu ishirini iliopita na katika kipindi hicho binadamu walikuwa wakiishi kawaida na hakukuwa na majini katika uso wa dunia hivyo moja kwa moja ni kwamba ulimwengu wa majini kama huo ulikuwepo kabla yao.
Kuhusu roho za wanyama wakubwa wakali waliokuwepo alijikuta akianza kuhishi huenda ni kweli kutokana na kumiliki Cauldron ambayo ndani yake ilikuwa na roho ya mnyama mwenye nguvu.
Roma alimuonea huruma Sophia kwa kuja nae katika eneo hilo la hatari , kuhusu Lekcha alijiambia ni haki yake kukamatwa katika ulimwengu huu kwasababu nguvu ya nishati ya ant-matter ilikuwa ni tishio sana lakini huku akiomba isitokee Lekcha kuweza kupata namna ya kujiongezea nguvu akiwa katika eneo hili kwani anaweza kumpa changamoto kutokana na kwamba hakuwa na uwezo wake kamili.
Baada ya maongezi ya muda, Moli aliangalia anga na kuona tayari lishakuwa jeusi na hakutaka kuulizwa maswali mengine .
“Bro Roma nimekuja katika huu msitu kwa ajili ya kutafuta mmea adimu , hapa ni eneo la mpakani na sikutegemea kukutana na yale majitu , ila kwa kunisaidia kwako lazima kutakuwa kumewaamsha wamiliki wa hili eneo , hivyo angalau unapaswa kuwa makini katika eneo hilo lote la Mbweha wa Jade, najua mpango wako ni kutaka kwenda kuona mnara lakini nakushauri kama mnataka kuwa salama tafuteni uelekeo wa Ziwa la mbingu”
“Kwa maelezo ambayo umenipatia haiwezi kunisumbua kwenye kutafuta uelekeo na safari ikawa ndefu?”
“Ni kheri safari yenu iwe ndefu kuliko kukamatwa na walinzi wa jumba la Mbweha wa Jade , mkuu wao anafahamika kwa jina la Mbweha wa anga wa mikia tisa na ndio ambaye ana uwezo mkubwa sana katika hili eneo kimapambano , yupo juu katika daraja la tisa huku akilindwa na mapepo wa anga therathini na sita na majitu kama mlioyaona hapa 72 hivyo fikirieni mara mbilimbili”
Roma aliweza kuelewa uvunaji wa nishati katika huo ulimwengu ulikuwa umegawanyika katika madaraja tisa na kila baada ya kupita madaraja matatu ilimaanisha nguvu na zenyewe zinaongezeka.
Kwasababu wote walikuwa na muonekano mbaya basi wanapofikia katika levo ya tatu tu ndio huweza kupata maumbo ya kibinadamu.
Unapaswa kuelewa katika ulimwengu binadamu ndio kiumbe ambaye ana muonekano mzuri kuliko aina yoyote ile ya kiumbe na asilimia kubwa ya hawa viumbe wasioonekana wenye miili mibaya ndoto yao ni kuwa na miili ya kibinadamu na hata hapo mwanzo ilisemekana majini yalikuwa yakiwaonea wivu binadamu kwa kuwa na maumbo mazuri ya kuvutia ndio maana majini mabaya wakawa wanawaingia binadamu na kuwatawala kiroho.
Katika mafunzo ya kawaida ya kijini ili kuweza kuwa na uwezo wa kujitengenezea mwili wa kibinadamu sharti ni kuingia katika levo ya Nafsi.
Kwa maelezo ya Moli alielewa kwamba katika hilo eneo hakukuwa na levo ya kuipita dhiki kutokana na kukosekana kwa radi za mapigo tisa.
Kundi la kwanza la majini ambalo uwezo wao ni wa kawaida ni kuanzia daraja la kwanza mpaka la tatu , kundi la kati ni kwanzia daraja la nne mpaka la sita , kundi hili lilikuwa la watu wachache zaidi, kundi la mwisho ni kuanzia saba ndio waliitwa majini pepo ya anga au mashetani pepo wa anga”
Roma hakutaka sana kujali kuhusu uwepo wa Mbweha wa anga wa mikia tisa na isitoshe kwa maelezo ya Moli hakuna ambaye alikuwa akimfahamu vizuri na kingine inasemekana alikuwa tofauti sana na majini na hakuwa ni mwenye kujali sana , wasiwasi wa Roma muda huo ni namna ya kutoka katika ulimwengu huo tu kwa namna yoyote ile.
Roma aliagana na Moli kisha yeye na Sophia walianza kutembea kuelekea upande wa Kaskazini , kulingana na maelezo ya Moli mji wa kwanza watakao kutana nao ni Mji wa Wingu Jeupe , ambao ndio mji mkubwa zaidi ndani ya miliki ya Mbweha wa Jade na itawachukua siku tatu katika kutembea.
Walipewa taarifa nyingine ya kutafuta mawe maalumu ndani ya mji huo ambayo yanaitwa kama mawe ya kiroho ambayo hutumika kama hela au njia ya kibiashara.
Roma hakutaka kutumia njia ya pemeni kama ambavyo ameelekeza Moli maana kutokana na maelekezo yake njia rahisi kufikia ziwa la mbingu ambapo kuna mnara ni kupitia ndani ya jiji la Wingu jeupe.
*******
Siku tatu ziliweza kupita na taratibu za maombolezo ya kifo cha Denisi ziliweza kufanyika ndani ya Iringa, haikuwa na maana ya kwenda Songea kwa ajili ya kuomboleza msiba kutokana na kwamba hakukuwa na mwili wa kuzika , hivyo kilichofanyika ni ibada ya kawaida tu kupitia kanisa la kikatoliki na kuruhusu jamaa na marafiki kutoa salamu za pole.
Licha ya maombolezo hayo, wanafamilia hao walikuwa katika hali ya wasiwasi kuhusu Roma , katika siku hizo tatu waliweza kupewa taarifa zote kutokea China kuhusu kupotea kwa Roma na Sophia kupitia mnara.
Ilikuwa ngumu kuamini kwa tukio hilo lakini kutokana na maajabu aliokuwa akifanya Roma iliwafanya kuamini kwamba ni kweli wameweza kupotea.
Asilimua kubwa ya wana ukoo waliogopa zaidi kupotea kwa Roma kwani alikuwa ni kama ashakuwa mhimili kwa ukoo wao kwa yale ambayo yametokea hivi karibuni , waliogopa maadui zao kuwachukulia hatua na kujaribu kuwayumbisha kwani kupotea kwa Roma ilimaanisha uwiano wa kinguvu kubadilika , hatua za awali walizochukua ni kufanya jambo hilo kuwa siri ya familia.
Afande Kweka alionekana kuchoka kweli kutokana na kutopata usingizi kwa zaidi ya siku tatu mfululizo , katika eneo la sebuleni alikuwa amekaa pembeni ya raisi Senga pamoja na Damasi ambaye macho yake yalikuwa yamevimba na mbele kabisa alikuwa amekaa Blandina mama yake Roma pamoja na Edna aliempakata Lanlan.
Kushoto kwao kulikuwa na mgeni ambaye ni mchina alievalia mavazi ya kitamaduni , alifahamika kwa jina la Abbess Yumiao na ndio aliekuwa ni mkuu wa Dhehebu la Shushani na ndio aliefika hapo kutoa taarifa.
Wageni wengine walikuwa ni wazazi wa Sophia , Balozi Athumani pamoja na mke wake.
“Tuliweza kutafuta kuzunguka eneo lote la Shushani lakini hatukuweza kupata chochote , tunaomba radhi kwa hilo “Aliongea yule Master.
“Na amini mmefanya kazi kwa jitihada kubwa , hata hivyo unaonekana ulikuwa ukimpenda Sophia hivyo haiwezekani ukakubali apotee kirahisi”Aliongea Afande Kweka kwa kingereza.
“Jamani Sophia wangu mimi,……”
Mama yake Sophia alikuwa akitoa machozi na kuwafanya watu wote waliokuwa hapo ndani kumuonea huruma.
“Sophia atakuwa sawa naamini yupo na Roma na mimi namwamini atamrudisha akiwa salama, huna haja ya kuendelea kulia, Roma ni mwanangu na imani yangu inaniambia atarudi salama”Aliongea Blandina akijaribu kumpoza Mama Sophia lakini wakati huo huo na yeye akitoa machozi , ilikuwa ni kama alikuwa akijifariji.
“Blandina haina haja ya kuendelea kulia , hatujapokea taarifa mbaya, naamini ataweza kurudi muda si mrefu”Aliongea Raisi Senga huku akimwangalia Damasi ambaye muda wote alikuwa ameinamisha kichwa chake chini.
“Upo sahihi mwanangu Roma atakuwa sawa ,naamini hilo..”Aliongea huku akifuta machozi.
“Okey kwasasa tutaliacha hili kwa jeshi letu kitengo cha wachawi , Master Yumiao na kitengo cha jeshi la Wachawi kutoka china cha Yellow Flame iron Brigade na wao ndio watatupa taarifa ya kile kinachoendelea, Senga umefanya vizuri kwa kuongea na uongozi wa serikali ya china kwa kuruhusu wanajeshi wetu kuweka kambi katika dhehebu la Shushani naamini muda wowote wataweza kupata fununu”Aliongea Afande Kweka na Raisi Senga alitingisha kichwa.
SEHEMU YA 602.
Siku tatu ziliweza kuwawezesha kutoka katika Msitu wa Giza , ijapokuwa ulimwengu huo ulikuwa ni ardhi ambayo haijagawanyika lakini eneo lilikuwa kubwa mno.
Roma kadri ambavo alikuwa akitembea ndio uvumilivu wake ulizidi kupungua na ili kurahisisha safari aliweza kutumia nguvu yake ya kijini kujaribu kupaa kwa kuruka ruka ruka kama chumba ili kufupisha safari.
Inasemekena mwishoni mwa eneo hilo kulikuwepo na bahari isio na mwisho ambayo mito yote katika eneo hilo humwaga maji yake na kwa maelezo ya Moli ni kwamba wasafiri washawahi kusafiri lakini hawakuwahi kufika mwisho na kuona ardhi ndio maana wakaipa jina la Bahari sio na mwisho.
Mto ambao ulikuwa ukipita katika jiji la Wingu jeupe ulikuwa na upana wa kilomita moja au zaidi na kwasababu ya mvuke uliokuwa ukitoka pamoja na Ukungu ilifanya jiji hilo kuitwa Jiji la wingu Jeupe kutokana na kwa mbali liliweza kuonekana nyumba zilizofunikwa na wingu.
Kilichomshangaza Roma na Sophia ni kwamba licha ya eneo hili kuwa la majini lakini miundo mbinu yao ilikuwa ni ya kawaida kabisa kama ya binadamu, kulikuwa na kila aina ya staili ya usanifu wa nyumba karibia tamaduni zote na mpangilio wake ulikuwa ni wa kueleweka kwani kulia na kushoto kulikuwa na nyumba huku katikati kukiwa na barabara,
Halikuwa aneo kama ulimwengu wa kawaida kutokana na kukosa ule ukisasa, lakini hata hivyo haikushangaza sana kwani kuna watu wengi ambao walikuwa wakiingia katika ulimwengu huo kutoka dunia ya kawaida na kuleta ustaarabu wa aina tofauto tofauti.
Kwa muonekano wa eneo hilo ni kama vile majini hao hawakuwa na tamaa ya kuujenga mji kuwa wa kisasa zaidi na sababu ya moja kwa moja haikueleweka na isitoshe Roma hakuwa na taarifa za kutosha.
Tokea kuumbwa kwa binadamu aliweza kupewa mamlaka ya kutawala viumbe vyote hata wale wasiokuwa wakionekana huenda ndio maana kila kitu majini yalichofanya kilikuwa kikiendana na binadamu wa kawaida.
“Bro tunaingia hivi hivi tu bila tahadhari , vipi kama wakitushambulia?”Aliuliza Sophia aliekuwa akiangalia jiji hilo kwa wasiwasi kupitia mlimani.
“Tunapaswa kuingia ndio hata kama watakuwa ni wakali zidi yetu , kwanza kabisa bado siamini maneno yote alioongea Moli hivyo lazima nifike katika mnara huo na kujionea mwenyewe kwani ndio njia pekee ya sisi kutoka huku, pili kama alivyotuambia lazima tutafute mawe ya kiroho ili kuweza kununua wanyama wa kijini ili tuweze kusafiri kwa urahisi na kutoka katika hilo eneo”
Kwa maelezo ya Moli ili kuishi katika eneo hilo hakuhitajika pesa bali mawe ya kiroho ndio hutumika kama njia ya biashara.
“Bora uwezo wangu ungekuwa mkubwa , kwa staili hii ninakwenda kuwa mzigo tu kwako”
“Hivi unajua siku zote sisi wanaume hatupendi wanawake wenye nguvu , tunapenda mwanamke ambae ni tegemezi, hakuna mwanaume ambaye atakupenda kaa una nguvu kumzidi na huna unachomtegemea”
“Sidhani ni kweli, kama ni hivyo kwanini mpaka leo hii hujaweza kuzikubali hisia zangu”Aliongea na kumfanya Roma kuvuta hewa kwa nguvu.
“Hilo limetokea wapi katika muda kama huu? , aisee naona unazidi kuwa mwanamke jasiri”
“Unataka niwe muoga , nishakaa chini na kufikiria tayari , kama kweli hatuwezi kutoka huku , hakuna wa kujali maswala ya kimaadili, hivyo matatizo yetu yote yatatatulika kirahisi”Aliongea akimaanisha kwamba kama hawawezi kutoka inamaana yeye na Roma wanaweza kuwa wapenzi.
Roma hakuteka kuendelea kusikiliza maneno ya Sophia na aliishia kumwambia waanze safari ya kuingia ndani ya jiji hilo na Sophia hakutaka kuendelea kuongea kwani aliogopa kumkasirisha.
Haikuwachukua dakika nyingi hatimae waliweza kuingia katika mji huo huku wakiangaliwa na majini hao kwa macho yasiokuwa ya kawaida .
Katika ulimwengu huo elimu haikupewa kipaumbele , kinachopewa kipaumbele ni mafunzo ya uvunaji wa nisahti pekee na kufika katike levo ya kuweza kuwa na mwili wa kibinadamu.
Jini ambalo halina mwili wa binadamu mara nyingi huonekana dhaifu sana na hufanya kazi za kitumwa.
Cha kuwashangaza zaidi ni kwamba ndani ya eneo hilo kulikuwa na wanyama wa ajabu sana ambao walikuwa wakitumika kama vile ni farasi , hakukuonekana magari na vifaa vingine , maisha yao yalikuwa ni yale ya kikale zaidi.
Kila kitu kilionekana kuwa kipya kwa Sophia , lakini kwa namna moja ni kama anafanya utalii.
Ni muda huo huo wakati wakipita katika jengo ambalo lilikuwa limefunikwa na ngozi nyingi kwa nje alionekana mwanamke jini aliekuwa katika mwili wa kibinadamu akiwaangalia , alikuwa ni mwanamke ambaye alikuwa na mwonekano wa kiarabu.
Alikuwa amevaa gauni refu ambalo lilikuwa na mkato wa kuacha shingo wazi huku akiwa amevaa cheni kubwa za madini ya dhahabu tupu ambazo zilikuwa ni za kuwaka waka.
“Wewe mwanaume wa kibinadamu nadhani wewe ni mgeni”Aliongea yule mwanamke kwa lugha ya kingereza lakini rafudhi yake haikuwa ni ya kunyooka , Roma aliamini huenda alikuwa akizungumza lugha nyingine tofauti na kingereza.
“Nimekuja huku bila ya kujielewa , nadhani unaweza kuniona mgeni”
“Unaonekana sio wa kawaida , karibia ya wote walioweza kukamatwa na mnara ni kwasababu ya aina moja”
“Inaonekana watu wengi wamekuja huku kabla yangu , tumeingia hapa lakini hakuna ambaye ametuongelesha zaidi ya kuangaliwa tu, ni kama jambbo ambalo limezoeleka”
“Upo sahihi , siwezi kusema kuna binadamu wengi lakini binadamu wanakuja mara kwa mara , nyie mnaweza kuwa binadamu lakini hapa hamchukuliwi kama alien , jina langu naitwa Mei , je tunakuitaje”
“Niite Roma Ramoni”
“Oh.. Braza Romaa,,!!!”
Aliongea huku akimsogelea Roma karibu kabisa huku akisuguanisha manyonyo yake na kifua cha Roma kwa staili ya kumtega.
“Braza Roma kwasababu ushakuja huku unapaswa kuyachukulia maisha kawaida , unaonaje ukiingia ndani na kuungana na wengine kula raha”Aliongea na kumfanya Roma kuangalia jengo hilo na kuweza kugundua nini kinafanyika huko ndani.
“Kwahio hata huku mna madanguro?”Aliuliza wakati huo Sophia alionekana kuwa na aibu kwa namna ambavyo Mei alikuwa akijigusanisha manyonyo yake na Roma.
“Kuna tatizo gani juu ya hilo , majini pia yana hisia , unadhani ni binadamu tu ambao wanapaswa kuuza miili yao na sisi majini hatuwezi?”Aliuliza lakiini Roma alipotezea.
“Nimeambiwa kwamba hela katika ulimwengu huu ni mawe ya kiroho kutoka bahari isio na mwisho , sina hayo mawe hivyo siwezi kutoa malipo hata kama nikiingia”
“Roma..!!”Aliita Sophia kwa hasira na kumfanya Roma amwangalie.
“Huwezi kuingia nae huyo , kwanini unataka kufanya hivyo wakati una mke anakusubiria?”Aliongea na kumfanya Roma kumwangalia na kutabasamu kwa uchungu , hakuelewa ni kwanini sasa hivi ndio anaanza kuwaza kuondoka katika hilo eneo.
“Lakini si ndio maana nimesema sina mawe ya kiroho”
“Wewe…:!!”
“Hakuna shida , unaweza kupata hayo mawe hata baadae , unachotakiwa unaweza kujiandikisha na kupata huduma na kisha utalipia baadae”
“Ah.. kwahio hamuogopi kwamba naweza kukimbia bila kuwalipa”Aliuliza Roma.
“Haishangazi ndio maana nasema wewe ni mgeni hapa , hili ni jiji la Wingu Jeupe na Bwana Mkuu Baiju ni sehemu ya majini pepo 36 ambaye anapendelewa sana na jenerali mkuu wa Jade, hivyo yoyote ambaye atashindwa kulipia deni lake atakutana na kifo cha maumivu”Aliongea Mei na kumfanya Roma kuelewa na sasa kusita sita.
“Basi nitapita, sijui namna ya kutengeneza hela hapa , sitaki kufa kifo cha maumivu kwa kushindwa kulipa deni , unaonaje ukiniambia sehemu ambayo naweza kupata hayo mawe pamoja na majini wanyama wa kusafiria?”Aliongea na kumfanya jini pepo Mei kufikiria kidogo.
“Braza Roma kama unahitaji hayo mawe unaonaje tukifanya biashara?”
“Niambie hio biashara”
“Huyu mwanamke hawezi kuishi kwa muda mrefu ndani ya ulimwengu huu na jini pepo lolote lenye mwili wa kibinadamu linaweza kumuua , huwezi kumlinda hivyo unaonaje tukibadilishana, mimi nitakupa mawe na yeye atabakia hapa katika Danguro langu na kutoa huduma kwa wateja , anaweza pia kuweza kulipwa bonasi ya Mawe na kuendelea kuishi”
Roma mara baada ya kusikia biashara hio alielewa ndio maana mwanamke huyo aliwasogelea , kumbe alikuwa na lake jambo la kutaka kumchukua Sophia kwa ajili ya biashara, alijiambia hauzwi mwtu hapa.
Sophia mara baada ya kusikia anataka kuuzwa alimsogelea Roma na kujibana kwake kwa hofu.
Roma alijaribu kumtuliza Sophia na kumwambia hakuna kibaya ambacho kinaweza kumpata.
Roma hakuwa tayari kumuuza Sophia kwa ajili ya kujipatia mawe, hivyo alimwambia Mei kwamba wanaondokana watajua mbele kwa mbele.
Upande wa yule jini pepo wa kike baada ya kuagana nao aliwaangalia na kutoa tabasabasamu lisilokuwa la kawaida na palepale baada ya kuwaona wametokomea upande wa mbele alibadilika na kuwa mwewe na kisha akapaa na kuondoka.
Roma baada ya kuelewa baadhi ya mitaa hio walipita pamoja na kuja kutokezea katika soko na hapo ndipo aliposhangaa kuona watu mbalimbali wakiongea lugha wanazozijua , ilikuwa rahisi kwake kuwasiliana kutokana na kujua lugha nyingii.
Roma aliulizia bei ya wanyama wa kusafiria na alipotajiwa ndio alipogundua wale wanaosafiri kwa kasi tena kwa kupaa walikuwa ghali sana na wale wa chini wanaofananana na nguruwe au Kenge walikuwa ndio wa bei rahisi.,
Hivyo ilikuweza kuwapata hao wanyama alipaswa kukusanya mawe mengi ya kiroho.
Inasemekana mawe hayo hupatikana katika bahari isio na mwisho na wale ambao wanaoenda kuyatafuta huwa ni kama wanaenda vitani kwani kuna viumbe wakali sana chini bahari ambao wanapaswa kupigana nao na kisha kuweza kuchukua mawe hayo.
Hivyo upatikanaji wake ulikuwani mdogo sana ndani ya hilo eneo na ndio maana yalikuwa ni adimu na thamani kubwa.
Roma alitamani kuwa kibaka na kuibia baadhi ya majini ndani ya hilo eneo lakini alijizuia kwa kuamini huenda angeweza kukasirisha mamlaka na kujiingiza katika matatizo.
Jiji la Wingu jeupe halikuwa na vurugu kama alivyodhania , ilikuwa ni sehemu iliokuwa na utulivu na kila mtu alikuwa na mambo yake , ijapokuwa walikuwa wakikodolewa macho lakini hawakujali na kuendelea na safari.
Baada ya kutoka nje ya jiji hilo waliweza kufikia kijimlima ambacho kilikuwa kikiwapa uwezo wa kuona upande wa chini wa bonde , ilikuwa ni eneo ambalo lilikuwa na mwonekano mzuri mno.
Roma paepale alitaka kumshika Sophia ili apae nae mpaka upande wa chini wa bonde hilo lakini aliweza kuhisi kundi la watu wakija upande wao.
Dakika chache tu ilikuwa ni kama hisia zilivyomwambia kwani waliweza kusogelewa na watu ambao walikuwa wamepanda juu ya wanyama kama Kenge(Thunder Lizard) na kuwazuia kwa mbele.
Wanyama hao walikuwa ni warefu mno na wanene waliokuwa wamepakwa rangi ya dhahabu kwa juu huku wakiwa na mapembe makubwa , walikuwa wakitisha lakini walikuwa ni wapole mno kutokna na uwezo wao mdogo wa akili , walikuwa wakishambulia na mapembo yao tu hivyo ndio maana mara nyingi yalipendelewa kutumiwa kama nyenzo ya usafiri.
“Mnaonekana wageni ,Je nyie ni wapya katika hili eneo?”Aliuliza mmoja wapo , walikuwa wakiwaangalia kwa ujeuri wa hali ya juu.
Aliekuwa akiwaongoza alikuwa amevalia Vest ya ngozi ya chui na uso wake ulikuwa mpana na umekaa kama chapati huku mdono ukiwa kama kijishimo, licha ya kubahatka kuwa na mwili wa kibinadamu lakini alikuwa mbaya wa sura mno na Roma alijiambia huenda hio ndio sura mbaya ya kibinadamu alioweza kuona katika maisha yake.
“Sisi ni wageni ndio , je kuna kitu chochote mnataka kutoka kwetu?”Alijibu Roma akiwa mpole maana alishagundua walikuwa na uwezo mkubwa kama Moli.
“Mnaweza kupita katika hili eneo lakini kabla ya hapo mnapaswa kulipia ushuru”Aliongea huku akitoa tabasamu.
Roma alijikuta akiwaza , hakuamini mpango wake wa mwanzo wa kutaka kuiba sasa umegeuka na yeye ndio anataka kuibiwa , alitamani kupaa na Sophia katika hilo eneo na kuwakwepa lakini aliona hilo sio chaguo bora.
“Jamani kama kweli mnatuona sisi ni wapya na tumewajibu hivyo mnawezaje kutaka ushuru ilihali hatuna mawe ya kiroho , kwanini msitusamehe kwa leo”
“Binadamu siku zote hamkosagi maneno nyie , kama tusipokusanya ushuru tunawezaje kupata hela , kama huna unaweza kulipia kwa kumtoa huyo mwanamke na wewe kuondoka , isitoshe hana nguvu zozote za ziada na atakuwa mzigo kwako”
“Nilijua ni Madanguro pekee ndio ambayo yanaweza kufanya biashara waziwazi , nadhani mambo ni ya kimkanganyiko sana ndani ya hili eneo”
“Madanguro gani, mimi ndio mkuu wa hili eneo kwenda kule chini na kila mtu ananijua jina langu mimi Baba Huja , unatakiwa kujifikiria mara mbilimbili la sivyo nitaruhusu hawa Kenge wetu kuwala nyama”Roma alijikuta akikunja sura lakini hata hivyo hakutaka kuogopeshwa na maneno yake maana aliona kama ni kupambana nao angeweza kuwaua wote.
“Hamtaki kutupisha ilihali tunaomba kwa upole , basi sawa hata hivyo nilikuwa nikitafuta mtu wakumuibia ,Shukeni kutoka kwenye hao wanyama wenu na mtoe mawe yenu yote ya kiroho na nitawatunuku kifo cha kistaarabu”
“Hahahaa… mmemsikia ? Binadamu mgeni anapanga kutuibia sisi , hivi hata unajua nani mkuu wa hili eneo lote”
Roma hakutaka kupoteza muda palepale alisogelea jini lililokuwa karibu yake kwa kasi kubwa na kulipiga ngumi na kusababisha liteme damu kutokana na baadhi ya viungo vyake kuharibika.
Baada ya kulishambulia na ngumi ile palepale liligeuka na kuwa kama kifaru huku ikionekana ameacha shimo katika ngozi yake.
Wale hawakutajarajia kama Roma anaweza kupigana , kwanza alikuwa na spidi kubwa kiasi cha kuwashangaza , yule jini aliegeuka kifaru alidondoka chini palepale na kufariki.
“Muueni”Aliongea kwa nguvu yule bwana Huji akiwaamrisha aliokuja nao na wote kwa pamoja walimwangalia Roma kwa macho makali.
SawaSEHEMU YA 603.
Wale majini walionyesha hasira za hali ya juu kutokana na kushuhudia mwenzao akipoteza maisha na palepale waliruka kutoka kwenye wale wanyama na kumsogelea Roma kwa spidi na kuanza kumshambulia.
Uwezo wao wa kimapigano mara nyingi ulitegemea zaidi kipaji na ulijumuisha upepo , mawe ,moto na barafu, mbinu zao hazikuwa chini na zile za majini ya kawaida pamoja na binadamu wanaojifunza mbinu za mbingu na ardhi
Roma hakuweza kukwepa mapigo yao kwani alijua akijiwekea ngao ndio ambavyo atazidi kupoteza nguvu zake kwa kiwango kikubwa hivyo alichokifanya ni kuita moto wa rangi nyeipe kujaribu kuwaunguza lakini ni kama walionekana walikuwa na mbinu za kuhimili moto huo sababu walianza kuongezeka ukubwa na kubadilika miili yao
Roma mara baada ya kuona mbinu hio haiwezi kufanya kazi palepale alifungua anga ya Sumeru na kuvuta Dagger ya damu ya Dragoni alioiiba kwa majini ya Hongmeng na kushambulia nayo.
Yale majini mara baada ya kuona kile kisu waliweza kukifahamu na walionyesha hofu lakini Roma hakujali kwani ndani ya dakika chache alikuwa ameshawafyeka, kisu hicho kilikuwa na tabia kwamba jeraha lake ilikuwa ni ngumu kupona lenyewe kwa haraka hivyo iliwapelekea kupoteza damu kwa haraka sana na kupoteza nguvu.
Jini pepo pekee ambalo lilikuwa limebakia ni yule kiongizi wao na baada ya kuona wenzake wote wamekufa alijikuta akipandwa na hasira maradufu.
“Nitakuuua !”Aliongea na palepale mkononni kwake kiliokana kisu cha kumeta meta na kumsogelea nacho Roma kwa kasi kwa ajili ya kumchoma , lakini Roma alionekana kuwa mwepesi kwani alimkwepa na akachukulia faida wepesi wake na kupeleka kisu chake nyuma lakini Huja alionekana kuwa na hisia kali kwani kwa wepesi aliosogea pembeni na kikapita.
Baada ya kuona hakuwa na uwezo wa kumshinda Roma alimwangalia kwa wasiwasi.
“Una bahati sana..”Aliongea akitaka kukimbia lakini Roma hakutaka kumruhusu aondoke na akaite wengine, palepale alimsogelea kwa kasi na kumchoma na kisu eneo la bega na muda huo huo akaita moto wa rangi nyeupe na kuanza kumuunguza lakini alionekana kuwa mjanja kwani palepale alipotea mbele ya Roma kwa kukimbia kwa spidi kubwa na kumfanya Roma ashindwe kumfukuzia kwa kuhofia kumuacha Sophia.
Baada ya kuwadhibiti wote kulibakia wale wanyama ambao walikuwa wamebeba mizigo aina ya viroba na Roma alimwambia Sophia aache woga na aanze kukagua kutafuta vitu ambavyo vinaweza kwuasaidia mbele ya safari.
Baada ya kukagua kwa dakika kadhaa Roma aliweza kukuta mawe ya kiroho yaliokuwa yakizungumziwa , yalikuwa ni mawe ya aina yake yalikuwa meupe sana huku ndani yake kukiwa na kitu cha rangi nyekundu kilichokuwa kikionekana, ni kama vile madini ya Almasi kwa nje na kwa ndani wekundu wake ni kama wa madini ya Rubi laini kitu pekee cha tofauti kuhusu mawe hayo yalikuwa yakipiga shoti ukishika mkononi.
Roma alijaribu kuyachunguza na kugundua kile kiini cha ndani kilikuwa ndio nguvu ya kiroho yenyewe kwani alijaribu kutumia uwezo wake kunyonya nguvu yake na kweli ndani ya dakika alihisi msisimko wa aina yake ukimwingia mwilini kama vile alikuwa akivuna nishati za mbinu na ardhi na ndani ya dakika chache tu kile kiini kilipotea.
Sasa wakati akiwa anaendelea kusachi Kenge wa mwisho aliekuwa na mzigo mkubwa ndipo alipoweza kugundua ndani yake kulikuwa na msichana mdogo aliekuwa amebebwa na alikurupuka palepale mara baada ya kiroba kile kufunguliwa.
“Naombeni msiniue waliniteka”Aliongea kwa kupiga kelele na kumfanya Sophia amsogelee kwa haraka.
“Hatuwezi kukuua usigope”Aliongea Sophia akijaribu kumtuliza , alikuwa na mwonekano wa kirembo mno na kwa haraka haraka sura yake ni kama vile ni mhindu.
“Nadhani ndio kwa mara ya kwanza ameweza kuupata huu mwili wake , nguvu zake ni za chini mno kuliko wengine”Aliongea Roma mara baada ya kumchunguza.
“Ndio nimeingia daraja la tatu la kupata mwili”Aliongea lakini upande wa Roma kuna kitu ambacho sio cha kawaida ambacho alikuwa akikiona kwa msichana huyo lakini hakutaka kujifanya mjuaji sana kwani hata hivyo mbinu hizo zilikuwa zikifanyika kinyume tofauti na yeye.
Majini ili kuweza kuishi walihitajika sana kuwa na nguvu kuliko hata wanavyokula chakula ili tu kuendeleza kudumisha miili yao.
Inasemekana wale ambao wanakaribia kuingia katika levo ya Nafsi hutengwa mahali palipotulia sehemu maalumu na hupewa jiwe la ndoto linalofanana na yai na kisha hulikalia na kulipa joto huku wakiendelea kutahajudi kwa muda mrefu na wakati wakianza kupokea miili yao huwa sio kwa chaguzi zao , kinachoanza kuonekana kwao ni kama ndoto wanaona sura ya mtu mbele yao na huyo mtu ndio mwili wao na kinachofanyika ni kuhakikisha wanapandisha nguvu zao mpaka kuweza kuumiliki .
“Unaitwa nani?”Aliuliza Sophia , alionekana kupata furaha mara baada ya kupata msichana mpole ambaye anaweza kumuuliza maswali.
“Naitwa Aoli, nilikuwa nikielekea katika mji wa Mto Wa Anga karibu na ziwa la mbingu ninakoishi lakini nikaja kukutana na hawa majini pepo wa gredi ya juu na kunikamata”
Maelezo yake yaliwafahamisha kabisa ni dhahiri walikuwa wamemteka kwa ajili ya kwenda kumuuza kwenye Danguro
“Unaonda karibu na Ziwa la Mbingu ?!!”Aliuliza Sophia huku akiwa na furaha kwani hata wao ndio walikuwa wanaelekea.
“Nina uhakika utakuwa unaijua njia ya mkato ,unaonaje tukiongozana pamoja kuelekea huko?”
“Sophia itakuwa hatari kama tukimruhusu akaungana na sisi , nitapaswa kulinda watu wawili kwa wakati mmoja”Aliongea Roma , alimuona msichana huyo wa kijini kuwa mrembo lakini uwezo wake wa kijini ulikuwa wa chini sana na hata yeye mwanzoni alishangaa kwani hakutegemea jini kuwa na mwili na nguvu zake kuwa za chini.
“Sio kweli, huyu yupo kwenye daraja la tatu ambalo ni sawa na levo ya Nafsi hivyo uwezo wake ni mkubwa kuliko wa kwangu na anaweza kujilinda , isitoshe kama tukimuacha hapa si wale watu watarudi na kumchukua tena na kuingia hatarini”Aliongea na kumfanya Roma kukosa neno alikuwa sahihi anaweza kuwa katika hatari lakini alihofia kuongozana na mtu asiemjua.
“Master mimi ni jini wa kawaida tu nisie na uwezo mkubwa , kama tutakuwa katika hatari unapaswa kumlinda mwenzako , sitokuwa na makasiriko zidi yako kwa kutokunilinda , ninajua njia ya karibu kuelekea Ziwa la Mbingu na itawachukua muda mchache kufika mkiwa chini ya uongozi wangu , nyie si wageni nitaendelea pia kuwaelezea baadhi ya mambo msio ya jua”
Roma alijiambia alikuwa na akili , kwani maneno yake yalikuwa yakivutia, ni kweli hawakuwa wakijua njia na mambo mengi pia kuhusu huo ulimwengu hawakuwa wakifahamu.
Sophia mara baada ya kuona Roma anawaza sana alimsogelea na kumwambia kwa taratibu kwamba hakuna ambaye ataweza kumshinda huko njiani hivyo waondoke nae kwani anatia huruma na Roma alitingisha kichwa kukubal.
******
Katika ulimwengu huo huo upande mwingine kando ya ziwa ambalo limezungukwa na msitu wa Mianzi Zambarau alionekana mwanaume ambaye alikuwa na nywele za rangi nyeupe kama mvi hivi , alikuwa amevaa kanzu ya Rangi ya Zambarau huku akiwa na ushanga mkubwa kwenye shingo yake kama Rozari iliotengenezwa na madini ya Jade, alikuwa ni bwana ambaye alikuwa na mwonekano wa kichina na muda huo alikuwa ameegamia kwenye jiwe huku akiwa ameshikilia ufito wa muanzi uliokuwa na kamba ambayo iimeingia majini , alionekana alikuwa akivua samaki.
Nyuma yake kulikuwa na nyumba ambayo ilikuwa imejengwa na Mianzi tupu iliokuwa ikifuka moshi.
Mtu huyo alionekana kuwa katika hali ya raha akifurahia kile alichokuwa akifanya, huku mkono wake wa kulia akiwa ameshikilia kifaa kama kikombe kilichotengenezwa kwa mianzi , ilionekana ni kifaa ambacho kilikuwa na kinywaji ndani yake kwani alikuwa akipeleka mdomoni na kunywa kwa kila baada ya dakika tatu huku akipiga mluzi akionekana kama anaimba.
Dakika hio hio pua yake ilicheza akiwa kama mtu ambaye alikuwa amenusaharufu nzuri na palepale alttupia pembeni ile fimbo na kukimbia kuelekea upande wa kwenye kile kijumba lakini kabla hata hajafika mwanaume mwingine alionekana akitoka katika hicho kijumba akiwa mkononi ameshikilia kibuyu cha mvinyo kama chungu vile , mwanaume huyo pia alikuwa ni mchina ila yeye akiwani mwenye nywele nyeusi.
“Inanukia vizuri “Aliongea yule bwana mwenye nywele nyeupe huku akipeleka pua yake kwenye kile chungu na kunusa huku akionyesha hali ya kufurahi.
“Braza Chi kama nilivyotegemea , inaonekana uwezo wako wa kutengeneza mvinyo ni wa hali ya juu sana , uko vizuri sana katika utengenezaji wa pombe , hii ndio uliniambia unatengeneza kabla ya mvinyo eh?”Yule bwana mwenye nywele nyeusi alishika udevu wake kama vile anautelezesha na mkono na kisha akamwangalia yule mwanaume mwenye udevu wa mvi kwa tabasamu.
“Wang Han Manasaba wa enzi ya Tang hapo zama za kale kama alivyoimba katika ushairi wa Liangzhou, ndipo vikombe vya Jade vilipojaa Divai, sauti ya mtirriko wa pipa ikawaambia na ondokeni…. nimekuandalia huu mvinyo kwa ajili yako, je Braza Zao umeandaa vikombe vya Jade?”Aliongea na kumfanya yule bwana kuanza kuwaza kuhusu Shairi hilo , walionekana ni kama vile walikuwa wakiongea kimafumbo kukumbushiana mambo ya kale hata hivyo alikumbushia ushairi wa Wang Han kuoka enzi ya Tang.
“Braza Chi nimejaribu kuvitafuta vikombe hivyo ila sijavipata , niliwaagiza ndugu zangu Mao Tai na Du Kang kwenda kutafuta katika milima ya Qillian lakini hawakuweza kupata , walivyoleta ni kutoka mlima ya Kunlun , je tunaweza kutumia hata hivyo?”
Mwanaume alieitwa kwa jina la Braza Chi alivuta pumzi na kuzishusha huku akimwangalia Braza Zao..
“Inasikitisha sana lakini sio mbaya tutatumia hivyo hivyo”
Yule mzee Zao mwenye nywele nyeupe alitoa tabasamu pana la furaha huku macho yake yote yakiangalia chungu kilichojaa mvinyo.
Na dakika ileile alionekana ameshikilia vikombe viwili vya Jade ambavyo haikueleweka amevitolea wapi na kuviweka katika meza ya jiwe lililochongwa.
Dakika hio hio wakati akitaka kuchota mvinyo kwa ajili ya kujaza kikombe kingine aliweza kutokeza mbele yao mtu mwingine aliekuwa amevalia kanzu na mwenye nywele za Zambarau, alikuwa ni Moli.
“Kaka Zao je umemuomba Master Chi kukutengenezea kilevi , nimeweza kunusa harufu yake hata nilipokuwa mbali”Moli aliangalia kwa macho ya tamaa chungu kilichokuwa kimejaa mvinyo.
“Bro umekuja muda muafaka , Master Chi ndio amenitengenezea huu mvinyo na sasa upo tayari , njoo ukae na wewe uionje radha yake lakini Du Kang yule mtukutu ameniletea vikombe viwili tu vya Jade kutoka milima ya Kunlun hivyo itakubidi utumie kikombe cha Muanzi.
Walikuwa wakifuata tamaduni za kichina , wenyewe wanaamini utamu wa mvinyo hutofautiana na kikombe ambacho huandaliwa , kikombe cha Jade ndio kinachofanya Mvinyo kuwa mtamu zaidi.
Upande wa Moli alionekana kuwaelewa vizuri kwani hata yeye alikuwa akizungumza lugha ya kichina tena kile cha kale.
Baada ya kuwekewa mvinyo kwenye kikombe chake cha mti na kuonja alijikuta macho yake yakichanua kwa utamu.
“Master Chi wewe ni kaka yangu wa ukweli kuanzia sasa , licha ya kuwa mgeni kwenye huu ulimwengu lakini umeweza kumfanya kaka yangu Zao kulia mara kibao kupitia mvinyo wako”Aliongea na Master Chi alijikuta akicheka.
“Braza Moli ni mara chache sana kukutana na marafiki wazuri kwenye maisha yetu , sikuweza kudhania ninaweza kukutana na mtu ambaye tunafanana kwenye vitu vingi , mwanzoni nilikuwa nishaachana kabisa na mambo ya pombe lakini baada ya kukutana na nyie mabraza nimekosa uvumilivu”
“Eh..!!”
“Braza Chi kabla yako nilikuwa na Moli tu kama ndugu yangu lakini hajui chochote kuhusu maswala ya kutengeneza pombe na anajali sana kukusanya mimea , waliochini yangu wengine wanachojua ni kuvuna nishaiti za mbingu na ardhi , nilikuwa nimeboreka sana kabla haujaja”
“Bwana wetu mkuu wa majini ya kishetani na mmiliki wa Msitu wa Mianzi Zambarau , wewe ndio kiongozi wa majini ya kishetani na unasifika kwa uwezo wako mkuu ndani ya ulimwengu huu lakini ajabu ukaagiza majini ya Gredi ya chini kukutafutia vikombe vya Jade , naamini ni kwasabbau tu wanakuheshimu ndio maana hawakuwa na jinsi , wenzetu wakisikia ulichokifanya wataishia kucheka”
“Hata sijali , yule Mbweha kutoka Jumba la Jade mwenyewe ana mambo ya kipuuzi tu kama mimi , ni mkubwa kuliko mimi na pia ni mzuri zaidi ya wale minyoo katoka Korongo la Joka ,lakini akili yao muda wote ni kuwaza namna ya kutoka ndani ya huu ulimwengu na wasivyojua wanapoteza nguvu na hela zao kwa ajili ya mambo ya kipuuzi”Aliongea huku akitingisha mabega.
“Tuachane nao na tufurahie maisha yetu kwa kunywa mvinyo , Braza Zao unaonaje?”Aliongea Master Chi huku akiinua kikombe chake cha Jade.
“Vizuri sana , sijawahi kukutana na mtu kama wewe unaefurahia sana pombe”Aliongea na palepale alijaza na cha kwake na wakagongesheana na kuendelea kunywa kwa furaha.
“Braza Zao nimetoka Msitu wa Giza na kidogo tu niingie matatizoni lakini kwa bahati nzuri kuna mgeni ambaye ni binadamu alienisaidia”
“Eh… kuna mtu mwingine amefika tena? , haukutumia kadi yangu? , ila sidhani kama wale watu wa miliki ya Mbweha wa Jade wanaweza kukudhuru ilihali wanakujua upo chini yangu “
“Nilitaka kupambana nao lakini wakati nataka kuitoa ndio walitokea hao binadamu na kunisaidia”Aliongea na kisha akamgeukia Master Chi.
“Master Chi sidhani kama ushawahi kusikia binadamu anaevuna nishati za mbingu na ardhi katika ulimwengu wa nje … jina lake anaitwa Roma Ramoni”Aliongea na palepale macho ya Master Chi yalibadilika na kuwa makali
SEHEMU YA 604.
Moli mara baada ya kuona mshangao wa Master Chi palepale alikumbuka namna ambavyo Roma aliweza kutengeneza vinyoka nyoka vya moto.
“Nilijua tu , alikuwa akitumia mbinu za moto katika kushambulia lakini sijawahi kusikia mtu yoyte ambaye ashawahi kufanya hibyo , Roma alikuwa a uwezo wa kuwasha Dragoni za moto bila tabu yoyote na palepale nilikumbuka mbinu zako Master unazotumia zinafanana”
Bwana Zao alijikuta akishangazwa na jambo hilo baada ya kusikia maelezo yote ya Moli.
“Master Chi je huyo ni mwanafunzi wako?”Aliuliza na kumfanya Master Chi kutoa pumzi nyingi huku uso wake ukiwa ni ngumu kuusoma na kisha akapeleka kikombe chake cha mvinyo mdomoni na kunywa pafu moja.
“Huyu mtu siwezi kusema alikuwa ni mwanafunzi wangu bali tulishawahi kukutana na kufahamiana, naamini hili limepangwa kutokea .. nililazmishwa kuja huku kwasababu nilikuwa nikitaka kuuliwa , je na yeye ndio kilichomtokea kama mimi?”Aliuliz lakini swali lake lilimlenga yeye mwenyewe.
“Moli kama wewe ulikuwa ushaona ana tumia mbinu sawa na za Braza Chi kwanini usingekuja nae hapa?”Aliuliza Bwana Zao huku akionyesha kutopenda.
“Sikuwa nikijua kama anafahamiana na Master Chi , isitoshe mpaka sasa una mtegemea zaidi Master Chi kwa ajili ya Mashindano ya Mbingu, sikutaka kuvujisha taarifa za uwepo wake ila nilimshawishi kuja na mimi katika msitu wa Mianzi Zambarau kwa zaidi ya mara mbili lakini alikataa na kusema yeye safari yake ni kuelekea katika Ziwa La Mbingu hivyo nilimuacha kwani sikutaka kuingilia mambo yake”
“Kama hivyo ni kweli basi sasa hivi naweza kukisia atakuwa kwenye miliki ya Mbweha wa Jade , Braza Chi ninaweza kukusindikiza kwenda katika jumba la Mbweha wa anga mikia tisa kama unataka kumfuata”Aliongea Mzee Zao na kumfanya Master Chi kuwaza kwa dakika kadhaa.
“Yupo imara sana na sidhani kama uwezo wake ni wa chini kuliko wa kwangu kulingana na maneno ya Zimo , Majini hata hivyo hayawezi kuonyesha nguvu zao zote , naamini atakuwa sawa . isitoshe hawezi kufika katika mnara wa Mbingu kabla mashindano ya Mbingu kumalizika , tutakuwa na uwezo wa kukutana nae tukielekea katika Ziwa la mbingu”Aliongea Master Chi na kumfanya Zao kutoa kicheko hafifu.
“Unaonekana upo makini kweli , kama ni hivyo kwanini tusipige mkupuo mwingine wa kinywaji chetu , bado ipo ya kutosha , tunaweza kuongezea maana kilevi chake sio kikali sana”
‘Tutakynywa kutosheka leo hakuna namna”Aliongea huku akijiambia atajua mwenyewe huyo mtukutu wa maka mingi iliopita , hakutaka kujishughulisha na kile ambacho kitamtokea na pia hakuwa na nguvu ya kumjali katika mazingira kama hayo , hivyo anapaswa kunywa kujigalagaza.
Moli ambaye hakuwa mnywaji sana aliishia kutingisha kichwa chake huku akiwa ni kama anawaonea huruma kwa ulevi wao.
******
Roma alikuwa na uhukika yule jini Huja angekwenda kuleta wenzake hivyo alichokifanya ni kumbeba Aoli pamoja na Sophia na kisha akapaa nao ili kwenda umbali mrefu kutoka katika eneo hilo.
Roma hakutaka kumuacha nyuma ilihali alikuwa ashakubali kuongozana nae na isitoshe pia uwezo wake ulionekana kuwa mdogo.
Roma licha ya roho yake kujiambia muda wowote watakamatwa lakini hakutaka kujisumbua kuhusu hilo , alijiambia atapambana na kila ambalo litakuwa mbele yake.
Baada ya kuweza kupita kilima hatimae waliweza kufika sasa katika ardhi ya tambarare , katika eneo hilo kitu pekee ambacho aliona atumie kuweza kurahishisha safari ni mbinu nyingine ambayo alijifunzaga iliokuwa ikitofautiana na mbinu za kijini , ilikuwa ni Qinggong .
Roma hakuwa akitembea bali alikuwa akikimbia huku akiruka ruka kwenda mbele kama vile ni chui anaejaribu kufukuzia swala, kuhusu Aoli alikuwa akipambana kuweza kumfukuzia Roma bila kuchoka asiachwe mbali.
Baada ya kupumzika walianza kutembea taratibu taratibu na Sophia alimuuliza Aoli mwonekano wake wa mwazno kabla ya kuwa na mwili wa kibinadamu ulikuwa vipi lakini Aoli alionekna kuona aibu.
Majini ni viumbe ambao wanachukia sana miili yao wanayo zaliwa nayo na ndio maana mara nyingi hata kama wakipambana na adui wakiona ni mkubwa kiliko wao wanaacha na kukimbia.
Mbinu pekee ya kuweza kutumia nguvu zao zote ni lazima wabadilike maumbo yao.
Roma yeye hakufuatilia mazungumzo yao na aliuliza mara chache kuhusu taarifa ambazo alikuwa akihitaji tu kwa ajili ya kumsaidia kufika mwisho wa safari yake.
“Mister Roma je unapanga kutoka kwenye huu ulimwengu kupitia Manara?”Aliuliza Aoli lakini Roma aliona mrembo huyo wa kijini anauliza swali ambalo lipo wazi.
“Nadhani siendi huko kucheza eti, nasikia lakini radi inayotokea katika huo mnara ni ngumu sana kuhimili?”Aliuliza Roma na Aoli alionekana kushangaa kidogo.
“Mr Roma utanisamehe kwa uongeaji wangu wa moja kwa moja , licha ya kwamba uwezo wako unakaribiana na majini pepo ya anga na Majini Shetani ya anga haiwezekani kabisa kuweza kuhimili mapigo tisini na tisa ya mpangilio wa radi”
“Kila mtu ananiambia haiwezekani , ninapaswa kuondoka katika huu ulimwengu , nitafanya lisilowezekana kuwezekana”
“Hakika unaonekana ni jasiri mno , lakini nakuasa kuwa makini usijjilazimishe sana kama utaweza kupata nafasiya kuingia katika huo mnara la sivyo utakufa”
“Unamaanisha nini kupata nafasi , huo mnara sio kila mtu ambaye anaweza kuufikia?”
“Ndio , Mnara wa mbingu haupo wazi kwa kila mtu , mara nyingi unakuwa umezigingwa na radi ya zambarau, ukiwa umefungwa haitokuwa rahisi kuweza kuufikia na kuupanda isitoshe sehemu ya kuingilia kwenye mnara inafunguka mara moja tu kila baada ya miaka sitini”
“Miaka sitini!!?”Roma alitoa mshangao huku akipandisha sauti yake wakati akiuliza.
“Kwahio unamaanisha napaswa nisubiri kwa miaka sitini mpaka niweze kutoka?”Aliuliza na kumfanya Aoli kutoa tabasamu.
“Una bahati kubwa mnara huo mwaka huu unatimiza miaka sitini tokea kufunguka kwake maara ya mwisho , hivyo ndani ya mwezi ujao utafnguka kwa mara nyingine”Aliongea na kumfanya Roma macho yake kuchanua kwa furaha.
“Kama ni hivyo basi naweza kusema nimekuja huku ndani ya muda muafaka”
“Ndio lakini ..”Aoli alionekana kupumua kwanza.
“Lakini nini?”
“Unapaswa kukidhi vigezo kama unataka kuingia ndani ya mnara huo , vigezo ni mpaka ushinde Mashindano ya Vita ya mbingu”
“Mashindano ya Vita ya Mbingu unamaanisha nini?”Aliuliza Sophia akionekana kushangaa.
“Ili kukuelewesha vizuri napaswa kukuelezea stori ilivyo tokea mwanzo , ukiachana na mawe ya kiroho ambayo yanachimbwa chini ya bahari , sehemu nyingine ambayo ina nguvu za kiroho ni ndani ya mnara huo ambao upo juu ya Ziwa , nishati hio inatokana na Radi inayopiga ndani ya hilo eneo , floor ya kwanza ya mnara huo haina radi lakini kwasababu ya uwepo wa kiwango cha juu cha nishati ya kiroho kuna mimea adimu sana inakuwa hapo ndani , ni mimea amayo inatafutwa sana na wakuu wote wa huu ulimwengu , kuna pia hazina za kiroho ambazo hupatikana katika hilo eneo , hizo hazina pamoja na mimea husaidia sana katika kupanda levo kwenye uvunaji wa nishati ya mbingu na ardhi , lakini kutokana na hilo katika Floor hio mara nyingi inageuka kama eneo la machinjio.
Miaka elfu kumi iliopita wakuu wote wa majini waliweza kuona kwamba wanazidi kupungua siku hadi siku kama wataendelea kuchinjana kila baada ya mnara huo kufunguka ili tu kuingia , hawakutaka mbinu zao za kuvuna nishati kupotea hivyo ili kurudisha tumaini kwa ulimwengu huu yakawekwa makubaliano kwa kila upande kutuma wawakilishi kila baada ya miaka sitini kushindania nafasi ya kuingia katika mnara huo na kuweza kupata hio mimea na baadhi ya hazina hizo , kupitia mashindano hayo hakukuwa na haja ya watu kufa kwani anaeshinda ndio anaeingia , ni shindano pia ambalo limeandaliwa kwa ajili ya kuongeza spidi ya watu kujifunza mbinu za kijini ili kila miaka sitini inapokaribia waweze kupata nafasi ya kushindana , kwa mwaka huu lazima shindano hili lifanyike
Huu ulimwengu umegawanyika katika miliki kubwa tatu ambazo zilijigawa miaka mingi iliopita, kuna miliki ya Mbweha wa Jade , Miliki ya msitu wa Mianzi zambarau na Bonde la Joka”
Roma mara baada ya kusikia maelezo hayo alijiambia kweli hawa majini sio wa kuchezea, wanaonekana kuwaza mbali sana mpaka kuandaa mashindano hayo.
“Kwahio unamaanisha kama nitalazimisha kuingia ndani ya huo mnara nitashambuliwa na hizo nguvu tatu si ndio?”
“Hilo sio tatizo , kuna baadhi ya majini wengine wanajitegemea lakini kutokana na koo tatu kuwa na washindani wenye nguvu sana , basi mara nyingi wale wanaopenda kushindana kwa kujitemgea wanakosa ujasiri”
“Bro Roma kama kweli wapo levo ya daraja la tisa si inamaanisha uwezo wao ni mkubwa kuliko wa kwako?”Aliuliza Sophia.
“Kama hao viongozi watatu wa juu kila koo wapo kwanini wasipigane wao kwa wao mpaka kutuma wawakilishi?”
“Hao watatu waliweza kupata umaarufu wao miaka mingi iliopita na wanajua fika , kama watapambana wenyewe kwa wenyewe inaweza ikachukua hata mwaka na asipatikane mshindi hivyo mnara utafunga ndio maana wanatuma wawakilishi , sheria ya mashindano ni kwa wale tu ambao hawakuwahi kushidana , yaani majini wapya ambao wanataka kupata umaarufu na heshima , mara nyingi wanaonda kupamban ni wale walio katika levo ya Pepo wa anga na shetani wa anga”
Roma mara baada ya kusikiliza maelezo hayo alipata kitu cha kufanya lakini kwa wakati mmoja alikuwa na mgogoro wa nafsi.
Alijiambia anaweza akashinda kama tu ataweza kuwa mwakilishi wa moja wapo ya koo , lakini kama ataingia peke yake nafasi ya kushinda inaweza kua ndogo au isiwezekane kabisa na itambidi kusubiria miaka sitini ijayo kuweza kuingia tena.
Roma tokea aingia katika huo ulimwengu bado hajakutana na jini ambalo lipo levo ya daraja la saba lakini Moli mwenyewe ambaye uwezo wake ulikuwa ni wa chini alionekana kuwa ni hatari, hivyo Roma alikosa kujiamini kama ataweza kushinda hao majini ambao watakuwa katika daraja la saba ,nane na tisa.
“Aoli katika mashindano yaliopita nani alishinda pambano?”
“Ni Majoka mawili kutoka Bonde la Joka na ukiachana na lililopita na la nyuma yake zaidi walishinda hao hao , hao Drago ni majini ambao wapo chini ya mkuu wa majini Majoka na washindi hao wote kwa sasa wana vyeo vikubwa , mmoja ni Joka mjumbe wa shetani , Joka Mjumbe wa upepo na Joka Mjumbe wa ngurumo, ndio watawala ambao hata mkuu wao hawagusi kabisa kutokana na uwezo wao lakini licha ya hivyo bado wanatuogopa sisi majini tuliopo chini ya Bwana wetu mzuri, Mbweha wa mikia tisa”
“Kwa jinsi unavhyoongea ni kama vile umekutana na kiongozi mkuu wa Mbweha wa Jade?”Aliongea Roma huku akicheka.
“Bwana wetu ni jini pekee lenye muonekano mzuri kuliko kitu chochote ndani ya ulimwengu huu , urembo wake hakuna ambaye ashawahi kuufikia wala kuufananisha na kitu”Aliongea akijaribu kumsifia.
Roma hakutaka kupingana nae maana hata hivyo bado hajakutana na huyo mrembo anaeitwa Mbweha wa mikia tisa.
“Hata awe mrembo vipi hawezi kumfikia mke wangu”Aliwaza Roma huku hisia za kumkumbuka mke wake Edna zikimvaa na kuzidi kupatwa na hali ya kutaka kurudi duniani.
Dakika hio hio wakati Roma akimuwazia Edna alijikuta akishituka mara baada ya kuhisi mkandamizo wa hewa wa aina yake unatokea upande wa kusini.
Ilikuwa ni kufumba na kufumbua mwanaume aliweza kuonekana mbele akiwa angani amepanda ndege mkubwa mno wa rangi nyeupe na kwa jinsi ambavyo alikuwa akipepea alifanya upepo kupeperusha majaini.
Ndege huyo alikuwa akifanana sana na Shakwe wa baharini lakini yeye alikuwa mkubwa mno na kwa jinsi ambavyo alikuwa akipaa ilimshangaza sana Roma.
Roma alijiambia kama angekuwa na uwezo wa kupaa ndege mkubwa kama huyo basu ingemrahisishia kuzunguka katika miliki yote ndani ya muda mfupi.
Wakati Roma akimtamani yule ndege upande wa mwanaume huyo alikuwa akimwangalia Roma kwa chuki, na kitendo cha kuona Roma hamwangalii ilimfanya kutoa tabasamu la kifedhuli.
“Nadhani utakuwa ndio wewe binadamu mgeni mwenye uwezo wa kijini?”Aliuliza mwanaume huyo , alikuwa na nywele ndefu mno ambazo zilikuwa zikifika kiunoni za rangi ya kahawia, alikuwa amezifunga na kitambaa chekundu na kufanya mkia wake kupiga piga mgongoni.
Aoli alionyesha hofu na aliweza kujificha nyuma ya Roma kwa Woga ni kama vile mtu anapomuona mtu wa heshima.
“Mister Roma huyo ni Bwana mkuu wa jiji loote la Wingu jeupe , ni moja wapo ya majini therathini na sita ya uwezo wa anga anaitwa Baiju
Ni Roma pekee ambaye alikuwa akiweza kumwangalia moja kwa moja machoni , mkandamizo wake wa hewa ulikuwa mkubwa mno kwa mtu wa kawaida kumwangalia .
“Wewe upo katika daraja la tatu , kwanini umeongozana na hawa binadamu?”Aliuliza akimwangalia Aoli kwa hasira.
Aoli alionekana kutetemeka mno akikosa ujasiri wa kuongea .
“Tushaondoka katika mji wako tayari, je umenifuata mpaka huku ili angalau niongeze muda wangu wa kukaa”Aliongea Roma mara baada ya kumtuliza Aoli.
“Una maneno marahisi mno , umewaua watu wangu na kisha ukamjeruhi generali wangu Huja , nilitaka kupotezea lakini kilichoniuzi ukaamua na kuiba na mawe yao ya kiroho , unanichukuliaje kwa mfano kama unaweza kuondoka kirahisi”Aliongea na Roma kama kawaida alitoa tabasamu la kifedhuli.
“Nilijnua tu, inawezekanaje Huja akateka msichana mdogo na kumbeba kwenye kiroba hivi hivi , kumbe wana sapoti zote kutoka kwako?”
“Kuteka nini , sijui chochote kuhusu hilo , ninachojua ni kwamba nakudai uhai wako”Dakika hio hio alioongea aliruka kutoka kwenye ndege wake na kisha akampiga Roma teka la kifua.
Jini Baiju uwezo wake wa kijini ulikuwa katika daraja la nane ambao ulikuwa ukichukuliwa ni wajuu kati ya majini therathini na sita ya uwezo wa anga , wakati alipokuwa akiita nguvu zake za kijini miti ilianza kuyumba kutokana na upepo mwingi ulikuwa ukijikusanya na haikuwa miti tu hata mawe yalianza kuruka
Roma aliwaambia Sophia na Aoli kukimbia huku akikwepa shambulio la kwamba la wimbi la upepo na palepale aliita moto wa rangi nyeupe na kuungannisha na wa njano kwenye mikono yake.
Baiju uso wake ulibadilika mara baada ya kuona mpira wa moto huo lakini hata hivyo hakuonyesha kuuhofia.
Kwa jini la uwezo wake moto wa rangi nyupe na wa njano haukuwa na uwezo wa kumpa majeraha makubwa , alichopaswa kufanya ni kujikinga tu na nishati ya mbingu na ardhi.
Roma alianza kumrushia mipira ya moto kwa spidi zote lakini Baiju alikuwa mtaalmu mno wa kukwepa na kujikinga kwa wakati mmoja, baada ya kuona amekwepa sana palepale mkono wake uliadilika na kuwa kama mkuki mrefu wenye kumeta meta huku ukiwa na ncha kali isokuwa ya kawaida.
Roma palepale aliweza kukumbuka katika maneno ya Aoli aliomwambia ni kwamba majini yakifikia katika levo flani ya juu yanakuwa na uwezo wa kubadilisha viungo vyao kuwa siraha kutokana na kujiunganisha na vyuma , haijalishi muonekano wao ukoje lakini siraha hizo zilikuwa na urofauti kabisa na viungo vya mwili.
Aoli pia alimwambia kwamba majini ya kipepo hayana uwezo wa kutengeneza Dhana kama majini ya kawaida lakini siraha zao hazikuwa za kupuuzwa hata kidogo na isitoshe hata kama ikiharibika inaweza kurudi katika umbo lake.
“Nguvu yako ya moto haiwezi kuhimili nguvu ya panga zangu za upepo”Aliongea huku akitoa kicheko na alipigisha hewani ile siraha yake na palepale kulidhalishwa visu vya aina nyingi kwa wakati mmoja ambavyo vilikuwa vikiambaa kwa upepo tu kumshambulia Roma.
Roma hakutaka kuleta masikhara kukinga visu hivyo na mwili wake, hivyo palepale aliita nguvu ya kijini na kujaribu kuvizuia huku akivikwepa kwa spidi kubwa kwa sarakasi za kila namna , kuna kingine manusura kimtoboe kichwani lakini aliwahi kukwepesha kichwa na kikaambulia nywele.
Roma wakati huo aliweza kuelewa kitu, kadri visu hivyo vilivyo kuwa vikikata upepo na kutoa ile sauti yake ya Swiii.. vilikuwa vikisababisha mapigo yake ya moyo kwenda mbio mno.
“Pumbavu kabisa , hizi sauti zina matatizo gani”Alilaaani Roma maana ni kama mishipa ya damu inataka kumpasuka.
Roma palepale aliweza kugundua nini tatizo mara baada ya kuona tabasamu la kifedhuli la Baiju.
Tofauti na kuwa na makali hatari kama viwembe , suati zao za mkato wa hewa zilikuwa zikitegneneza mtetemo(vibration) ambazo zilikuwa na madhara kwa nguvu ya kijini iliokuwa ndani ya mtu
Roma kama mwili wake ulikuwa dhaifi angeweza kutema damu palepale.
“Unathubutu vipi kutumia mbinu zako hizo za hila”
Roma alikuwa amekasirika kiwango cha rami , wakati akiwa anasukumia mbali vile visu kwa kutumia nguvu ya mbingu na ardhi , palepale aliiita donge la Maji kubwa kama kitenesi kwenye mkono wake na baada ya kuliachia hewani Donge lile liligeuka barafu na kupasuka pasuka kama cheche na kuanza kumeza sauti ya mawimbi ya visu.
Baiju alionekana kushangazwa na kitendo hicho , hakuamini kama Roma alikuwa na uwezo wa kuita maji ya kiroho na kuyagandisha.
“Huu ni uchawi ,,, hio ni mbinu gani umetumia katika mafunzo yako?”Aliongea kwa kujiwazia na mpaka hapo aliona kabisa hakuna matumaini kwa shambulio lake la visu, hivyo aliamua kutumia mkuki wake kuanza kumsogelea Roma na kumshambulia nao.
Alionekana alikuwa na mpango wa kumuua kabisa Roma na pigo moja lakini upande wa Roma alionekana kutoa tabasamu lakifedhuli.
“Nilikuwa nikisubiri ufanye shambulio la aina hio”Aliongea Roma na palepale alichezesha mikono yake na kulitokea mng’ao kama wa moshi na palepale alimsogelea Baiju kwa spidi kubwa na kushika ncha ya ule mkuki wake na palepale barafu ilianza kusambaa kutoka katika ncha ya mkono wake na kuanza kumsogelea Baiju na kumfunika kwa kasi ya ajuu mno.
Baiju alijikuta akitoa ukulele kutokana na baridi kali aliokuwa akiisikia mwilini na alijitahidi kuvuta ule mkuki kutoka kwa Roma lakini ulikuwa umeshikiliwa vyema.
Sophia aliekuwa akiona mbali alijikuta akiruka ruka kwa kushangilia mara baada ya kuona matumaini ya Roma kushinda.
“Aoli angalia Bro Roma anashinda , Bwana wenu wa mji hana uwezo wa kumshinda , kwa staili hii naamini Bro Roma anaweza kuingia katika mnara , wewe unaonaje?”
Sophia alishindwa kuona mabadiliko ya ghafla ya Aoli huku macho yake yakiangalia namna ambavyo Baiju aligeuka barafu kwa ghafla.
“Huenda anaweza kuwa na kaji uwezo ..”Aliongea huku akitabasamu ki ovu na palepale alisogea kwa spidi kuelekea sehemu ambayo Roma na Baiju wanapambana , Sophia alitaka kumzuia lakini ile anataka kumshika ni hewa tu aliweza kushika kwani Aoli alikuwa na spidi ya hali ya juu na ilimfanya na yeye kuanza kumkimbiza
Baiju alijikuta akianza kutoa matusi kwa kutokuwa makini na kuanza kushindwa pambano kirahisi namna hio , Roma palepale hakutaka kumchelewesha alitaka kuinguza roho yake na moto wa Bluu kwani ulikuwa tayari ushajitengeneza katika mkono.
“Umekuja mwenyewe kwangu na sikuwa na kinyongo chochote na wewe lakini hata hivyo sitaki kusumbuana na mtu kama wewe hivyo nitakupeleka moja kwa moja kuzimu”aliongea Roma
“Huwezi kuniua ,,, Bwana wangu hawezi kukuruhusu uniue na atakuua wewe”Aliongea huku akishindwa kuzungusha chingo yake kutokana na kukabwa na barafu.
Roma hakutaka kusumbuka na maneno yake na ndio alikuwa akianza kutaka kuruhusu mpira ule wa moto wa rangi ya bliuu kuelekea kwake lakini ghafla tu mikono yake iliokuwa imeshikilia ule mpira wa moto ilifungwa fungwa na kamba ndeefu ya nguo ya hariri kwa nguvu kiasi cha kushindwa kudhibiti ule moto na palepale ulizimika.
Alijikuta akishangazwa na kitendo hicho kwani aliamini mtu pekee ambaye anaweza kuuzima moto wake ni mwenye uwezo mkubwa kuliko wa kwake.
Roma alijikuta jasho likimtoka na palepale kwa haraka sana aligeuza shngo yake na kuangalia nani ambaye amemshambulia kwa ghafla sana.
Roma mara baada ya kuangalia alijikuta akishikwa na mshituko mara baada ya kuona aliefanya hivyo ni Aoli na hata kamba ya hariri iliokuwa imemshikilia ilikuwa ikitoka kwake.
“Baiju alijikuta akisogea pembeni haraka sana na kujiifcha mara baada ya mkuki wake kuachiwa., lakini wakati huo huo alijikuta akipauka uso mara baada ya kumuona Aoli.
“Bwana wangu …. Bwana wangu…!!!”
Sophia alijikuta akisimama ghafla mara aada ya kushitukia tukio lile na aliishia kuachama tu.
Upande wa Roma akili yake ni kama ilikosa kufanya kazi kwa muda na hisia zake zilikuwa ni kama mtu ambaye alikuwa akiamini ukweli flani na sasa anaambiwa huo ni uongo.
“Wewe ni nani haswa?”Aliuliza Roma na kumfanya Aoli kumwangalia kwa dharau na palepale kama vile anamulikwa na tochi usoni na haraka sana mwili wa Aoli ulibadilika kabisa na kuwa mwanamke mwingine kabisa aliekuwa ni mrembo wa ajabu.
Mwanamke ambaye alikuwa mbele yake alikuwa amevalia mavazi ya hariri nyeupe huku yakiwa na kamba kamba zilizokuwa zimejiachia kama vile ni Ribon huku zikipepewa na upepo , nywele zake zilikuwa ndefu na nyeusi zikiwa zimefungwa na kitambaa .
Kwa jinsi ambavyo alikuwa akimwangalia Roma ni kama anamtega , ijapokuwa mavazi yae yalikuwa ya kawaida sana lakini uzuri wake haukujificha.
Hakukuwa na maneno sahihi ya kumwelezea kwani alikuwa ni kama uso wake unabadilika badilika na kuzidi kuwa mzuri , mbaya zaidi eneo lote lilijaa marashi ya aina yake ambayo yalitamanisha pua.
“Mister Roma mimi ndio mkuu wa miliki yote ya eneo la Mbweha wa Jade na jumba la kimalkia, naitwa Aoline , Nice to meet you”Aliongea huku akibadilisha muonekano wake na kuweka tabasamu la kiheshima , kwa namna ambavyo alikuwa akimwangalia Roma ni kama vile anamwambia naomba unipende.
ITAENDELEA.
NILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI :SINGANOJR.
WATSAPP: 0687151346.
SEHEMU YA 605.
Baiju miguu yake katika vigoti ililelegea palepale mara baada ya kujua mwanamke ambaye hakuwa amemtambua ni Aoiline mkuu wake.
“Bwana wangu , sikujua kama upo hapa tafadhari naomba unisamehe”Aliongea kwa kutetemeka huku akiwa amemsujudia chini , hakuwa tena yule mwenye kiburi.
Aoiline aliachana na Roma na kisha alimsogelea Baiju kwa hatua hafifu huku uso wake ukiwa ni ule wa kichokozi , hakuonyesha kabisa kuwa na hasira.
“Baiju nimepewa ripoti kwamba unakusanya kiwango kikubwa cha mawe ya kiroho kupitia Madanguro , ukiichukulia faida kwa mimi kutokuwa makini na maswala hayo , inaonekana umeweza kuteka majini wanawake kwa tamaa zako”
“Bwana wangu wananisingizia tu , waliochini yangu ndio ambao wamefanya kosa hilo kwa kunipatia rushwa , nitahakikisha nina wahukumu vifo nikirudi”Aliongea Baiju huku akionekana kutengeneza kisingizio.
“Hata mimi naona , kwa hio unasema mimi ndio mkosaji hapa kwa kusingizia si ndio?”Aliongea huku kitingishcha kichwa chake kama mtu ambaye anajaribu kumwelewa.
Baiju alitaka kutingisha kichwa kujaribu kujitetea kwamba hakupaswa kumbebesha lawama zote lakini hakuweza kufanya chochote wala kukubali kama ana kosa na uso wake ulibadilika rangi na kuwa mwekundu kutokana na presha ambayo ilikuwa ikijiandaa kumkumba.
“Umekuwa na mimi kwa zaidi ya miaka mia mbili , nimekufanya uwe Bwana wa mji wangu wa Wingu Jeupe na ukapokea tani na tani za mawe ya kiroho kutoka katika maghala ya mji na watu wengi wakakuonea wivu lakini bado ukaamua kukusanya zaidi Mawe ya kiroho kupitiia Danguro , Ingekuwa ni sawa kama tu ungekuwa ukidanganya hao ambao walikuwa wakipenda kufanya kazi chini yako lakini ukathubutu kuteka wale ambao wanajaribu kupita katika mji wetu , hivi unadhani mimi siwezi kuishi bila wewe , unafikiri mimi ni mwepesi kudanganywa?”
Jasho la baridi lilimtoka Baiju na kuloanisha nguo zake na aliishia kutingisha kichwa chake akiwa amekiinamisha chini akishindwa hata kumwangalia Aoiline.
“Bwana wangu, Sikuwa nikifikiri sawa sawa , tafadhari naomba unisamehe kwa dhambi nilizoafanya kwa zaidi ya karne moja”
“Sawa”Aliongea huku akikusanya nguo za mkono wake na kutingisha kichwa.
“Itakuwa ni ukatili kama sitoweza kukupa nafasi , nitakusamehe kwa kuwateka wasichana wa kijini nyuma ya mgongo wangu”Aliongea na kumfanya Baiju kufurahiswa na maneno yake huku akitaka kuanza kusujudu kwa mara nyingine lakini Aoiline alimkatisha.
“Lakini hata hivyo napaswa kukuadhibu kwa jambo moja”
“Ah..!”Alitoa sauti huku sura yake akipeleka chini kwa mara nyingine akiwa kama amechanganyikiwa.
“Watu wako hususani Huji wameniteka siku ya leo na wakaniingiza kwenye kiroba ,… ningekuwa mrembo wa kukuingizia hela ndani ya Danguro leo kama sio Mr Roma kunisaidia”
Hio ilikuwa ni taarifa mbaya sana kwa Baiju na sasa aliweza kuelewa kwanini Aoiline alibadilisha mwonekanno wake , kila kitu kilikuwa ni mtego wa kumkamata na ufisadi wake.
Ingekuwa afadhari kama angekamata wanawake wengine lakini sasa alikuwa amemsaliti hata Bwana wake hakukuwa na sababu ya kuachwa hai.
Dakika hio alivyojaribu kuunganisha Dot katika akili yake , Baiju alijiambia hakukuwa na faida yoyote ya yeye kuomba kusamehewa au kujitetea na anapaswa kufanya kitu chochote kile ili kuweza kukimbia na kutoka katika hio miliki, alijiambia kama ataweza kufika katika Korongo la Joka , Mfalme wa Majoka lazima angemlinda kwani alikuwa ni jini mwenye uwezo mkubwa wa kimapambano katika levo ya nane.
Baada ya kupatwa na mawazo hayo hakutaka tena kuchelewa, palepale aliita kwa hisia ndege wake mweupe kwa ajili ya kumshambulia Aioline .
Ndege mweupe na yeye akasikia kuitwa na mkuu wake , na palepale lilitoa kilio kikubwa cha juu huku likipiga piga mabawa yake kumsogelea Aoiline moja kwa moja.
Aoline hakuonakana yule mpole tena kwani alibadilika na alikuwa na uso wa kikauzu usio kuwa wa kawaida na kwa Roma ni kama alikuwa akimuona Edna party two, ilikuwa ni kama vile hewa iliokuwa ikimzunguka imeganda.
“Wewe mjinga , unathubutu vipi kujaribu kunipinga mimi?”Aliongea kwa nguvu na palepale kulitokea mwanga kama nguzo mbili nyuma ya gauni lake na nguo moja ya mwanga ilimshikilia yule ndege kwa kumfunga funga.
Roma aliangalia kwa ukaribu zile nguzo zilizokaa kama kamba kamba na palepale ndipo alipogundua ni mikia na pale ndipo alipojihakikishia kweli huyo ni jini ambaye alikuwa akiitwa Mbweha wa mikia tisa.
Mikia yake ilikuwa ni mirefu mno na haikuwa ya kawaida , ilikuwa ni kama boriti au nguzo.
Yule ndege licha ya Roma kumuona mkubwa lakini mbele ya ile mikia alionekana kuwa mdogo mno kwani alikamatwa na akawa hafurukuti kabisa.
Ndege yule alianza kutapa tapa kama vile kuku ambaye anapoteza uhai na ndani ya dakika tu damu zilionekana kuruka juu , ilionekana alikuwa amekamuliwa kwa kiwango kikubwa kiasi cha viungo vyake kuharibika na hata manyonya yake yalianza kusambaa angani.
Sophia alishindwa kabisa kuangalia kitendo kile lakini kwa Roma alikuwa akiona kitu kile kama hasara kwani yule ndege alimpenda na kujiambia angalau kabla ya kutoka katika ulimwengu huo amwendeshe hata mara moja.
Wakati Aoiline akidili na ndege Baiju alikuwa ashakimbia kwa kupaa umbali mrefu kidogo , lakini bahati mbaya kwake ni kwamba mkia mwingine wa Aoiline ulikuwa ukimfukuzia na ulikuwa ukiongezeka urefu kadri alivyokuwa akikimbia kwenda mbali..
Roma ni jambo lingine ambalo lilimshangaza kwani hakuamini kama mkia huo ungekuwa na uwezo wa kuongezeka urefu na kusafiri umbali mrefu tena kwa haraka sana.
Ni kufumba na kufumbua tu Baiju alipigwa na mkia ule kwa nguvu mara baada ya kusogelewa na alijikuta akitema damu kutokana na kichapo.
“Rudi”
Ule mkia ulimviringa Baiju kufumba na kufumbua tu na kumvuta nyuma na kisha kumrudisha ardhini mbele ya Aoiline na dakika ileile ulipotea katika macho yao , ilikuwa ni kama vile haukuonekana kwani licha ya urefu wake ulirudi ndani ya mwili wa Aoiline kwa spidi kubwa mno.
Roma alijikuta akitengeneza sauti kupitia ulimi wake , Roma alikuwa akijua mwanamke huyo alikuwa na mikia tisa na ameonyesha mwili tu na kilichotokea sio cha kawaida.
Pengine siraha yake kubwa ni hio mikia na kama atapambana nae basi atakuwa ni moja ya washindani hatari ambao ashawahi kukutana nao kwani angekuwa na uwezo wa kujikinga na wakati huo huo akishambulia.
Kwa spidi yake hio na nguvu zake za kijini aliona kabisa hata yeye hakuwa akimuweza kimapambano kabisa, na hakutaka kujiona yeye ni mkubwa zaidi hivyo alikubali Aoiline alikuwa ni levo ya juu kuliko yeye.
Baiju alijikuta amepauka mno kwa woga , alikuwa tyari amekwisha kujikatia tamaa katika kukimbia na aliishia kusujudu kadri awezavyo na kujaribu kuomba kuhurumiwa , lakini licha ya kujitetea huko kulifanya tabasamu la kikatili la Aoiline kuzidi kutisha.
“Bwana nimetenda dhambi zidi yako , unaweza kuondoa nguvu zangu zote za kijini na kunigeuza kuwa mnyama lakini tafadhari naomba usinie , naomba unisamehe”
“Siku zote nilikuwa mpole sana kwa viongozi kama nyie , kwanini nikuondolee nguvu zako za kijini ?,Baiju je utanisaidia jambo moja?”
“I’m willing to redeem myself!”Aliongea
“Great”
Kufumba na kufumbua Aoline alikuwa nyuma ya Baiju na kuishika shingo yake na palepale mkandamizo wa hali ya juu ulianza kumtoka.
“Sophia kuwa makini”
Aliongea Roma na palepale alimsogelea Sophia na kumzingira na nguvu ya kijini kwani tayari ashajua ni nini kinachokwenda kutokea .
Aoiline alikuwa akipanga kumkandamiza na nguvu yake ili kuweza kutawala uwezo wake hivyo kutokana na mkandamizio mkubwa ambao alikuwa akijaribu kutoa Aoiline ilikuwa ngumu kwa Sophia kuweza kuhimili na angetema damu kwani mara nyingi inakuwa kama vile ni mlipoko wa bomu.
Ilikuwa ni kama vile mwanamke huyo mrembo amegeuka na kuwa mungu wa huo ulimwengu kwani macho yake yalikuwa yamebadilika kabisa na kile kiini cheusi kilikuwa kimempotea kwenye macho na jicho likabakia jeupe kama vile ni barafu.
Dakika ileile Aoiline alifumbua mdomo wake na meno yake yaliongezeka urefu kama Vampire na kuyapelekea katika shingo ya Baiju na kumng’ata.
Baiju sura yake mwanzo ilikuwa imepinda kutokana na mkandamizo mkubwa lakini mara baada ya kung’atwa mwili wake ulibonyea palepale .
Sophia aliekuwa nyuma ya Roma hakuweza kupata ujasiri wa kuangalia kile kinachotokea kwani iliogopesha , upande wa Roma alikuwa katika bumbuwazi kwa kile kinachotokea
Alijiambia swala la kunyonya damu ni la kawaida kwani kilichofanyika ni kujaribu kunyonya nguvu za lile jini lakini hakutegemea mwanamke mrembo kama huyo ndio ambaye anafanya kitendo hicho.
Kile kitendo huenda angekuwa ni binadamu wa kawaida ambaye anaangalia angepoteza fahamu palepale , Sophia kwa kiasi hakuwa wa kawaida kwani alikuwa ashaishi na Roma na kuzoea baadhi ya mambo ya ajabu ya namna hio.
Dakika chache tu mwili wa Baiju ulibadilika na Akawa Kunguru mkubwa ambaye ameoza huku mifupa yake ikianza kuonekana na Aoiline alimsukumia mbali maiti ile ya Kunguru na kuanza kuilamba midomo yake kwa damu zilizokuwa pembeni, alikuwa ni kama vile analamba asali kwa jinsi alivyonekana kufurahia.
Baada ya mkandamizo wa hewa kuondoka ndio aligeuza macho yake kwa Roma huku akiachia mkandamizo wa kawaida kama vile alikuwa akijaribu kumuogopesha Roma.
“Mr Roma huna haja ya kuniangalia hivyo na kuniona kama mchawi mnyonya damu , nimefanya hivi kwa zaidi ya miaka elfu moja , hatima yake ilikuwa ni kifo hata hivyo , kwanini nisimtumie kama kirutubisho , Au naongea uongo?”
Roma alikuwa akianza kuwa na wasiwasi juu yake , hata kama alionekana kuwa mrembo wa kuita lakini matendo yake na uwezo wake wa kijini ulimpa mashaka makubwa na kushindwa kuijua nia yake halisi juu yao.
“Nadhani tunapaswa kuendelea na safari yetu maana ushamaliza maswala yako”Aliongea Roma na kisha akamwangaliaSophia akimwambia waanze safari ya kuondoka hapo haraka iwezekanayvyo.
Sophia hakuwa na shida na alikubali kuondoka , yule Aoiline ambaye alitaka kuwa nae karibu hakumtaka tena maana alikuwa akitisha.
Aoiline palepale alitoa tabasamu la kifedhuli na kufumba na kufumbua alikuwa mbele ya Roma na kuwazuia wasiondoke.
“Mr Roma tupo karibu na jumba langu la kimalkia kwanini msiende kupunzima kwa muda”
“Hakuna shida sana juu ya hilo , safari yetu ni kuelekea kando ya ziwa la Mbingu”Aliongea Roma huku akijaribu kutafuta upenyo wa kumpita.
“Hata kama nimekudanganya kuhusu ubini wangu , lakini sikuwa nikidanganya kuhusu mambo mengine , kuna zaidi ya wiki tatu mpaka kwa mnara kufunguka , kwenda huko ni kupoteza muda wako tu”
“Mimi naweza kutokuwa na akili kama wewe lakini siwezi kuwa kichaa kabisa na kuanza kupigana na mtu kama wewe ambaye umeishi maisha marefu , lazima una nia nyingine hivyo acha kuzunguka zunguka”Aliongea Roma mpaka hapo alijua mwanamke huyo hakuwa na nia ya kuwaruhusu waondoke kirahisi.
“Mr Roma sisi majini tunaweza kufikiria pia na sio wanafiki kama binadamu , mosi nimekuja huku kwasababu nimesikia taarifa kutoka kwa watu wangu ndio maana nimekuja kujionea mwenyewekama ni kweli Baiju alikuwa akitenda mambo ya kifisadi, kitu kingine pia waliniambia kwamba kuna binadamu wageni ambao wameweza kufika katika ulimwengu wetu , Watu watatu ambao ulipigana nao katika msitu wamekuongelea vibaya sana lakini sikuwachukulia siriasi na sina nia ya kuwalipizia kisasi kwa uliowafanyia”
“Lakini bado siamini mtu kama wewe unaweza tu kunialika kwako kwa ajili ya kupumzika”Aliongea Roma huku akitoa tabasamu.
“Nimeongea vya kutosha je tunaongozana au hatuongozani”
“Hatuongozani”Aliongea Roma kwa sauti huku akitingisha kichwa chake kukataa kusisitizia msimamo wake.
Aoiline alitoa pumzi ya kukatishwa tamaa huku akimwangalia Roma kwa masikito.
“Kama hutaki kuongozana na mimi basi sina budi kukulazimisha”Baada ya kuongea hivyo msisimko aliokuwa ukitoa ulibadilika kabisa na macho yake hayakuwa mazuri tena kwani yalibadilika na kuwa ya chuki.
Roma alishindwa kuelewa chuki yake inatokana na nini , aliajiambia kwanini kumbadilikia namna hio ndani ya dakika tu wakati hajamchokoza.
Roma palepale alimsukumia mbali Sophia ili tu asije akapata madhara na baada ya kumuona ameenda mbali zaidi aliita nguvu zake za kijini ili kuweza kuhimiri mkandamizio uliokuwa ukitolewa na Aoiline.
Dakika hio hio Aoiline muonekano wake wa kirembo ulikuwa umebadilika na kuwa kama vile ni jitu kubwa la kutawala , macho yake yalikuwa ni kama yale ya kutaka mtu yoyote anaemuona kumsujudia.
Roma hakutaka kumruuhusu msichana kama huyo kuendelea kumkandamiza , hakutaka tena kulinda nguvu yake ya kijini isipotee na alimsogelea Aoiline kwa nguvu zake zote.
Mpira wa moto wa bluu ulionekana katika mkono wake wa kulia na mkono wake wa kushoto ulitegneneza maji ya kiroho ya kuosha uovu.
Aoiline alitoa tabasamu la kejeli kama vile alikuwa akidharau kile anachotaka kufanya.
Awamu hio hakutoa mikia yake bali nguo yake ilianza kutengeneza kamba kama Ribbon kutoka kwenye nguo yake ya hariri akidhamiria kupigana na hio .
Roma hakutaka kujali mbinu yake ambayo anataka kutumia na dhamira yake ilikuwa ni kutaka kumchapa na maji ya kiroho akiamini hata tone lake linaweza kumletea madhara.
Lakini nguo yake ile haikuwa nguo kama nguo kwani ilikuwa ikidhalisha kiwango kikubwa cha nishaiti isiokuwa ya kawaida na kadri ilivyokuwa ikipepea kuelekea upande wa Roma ni kama ilikuwa ikimzuia asimfikie.
Roma alijikuta akishangazwa na uwezo wake , aliweza kujua mtu anaepambana nae ndio yupo katika levo ya juu kabisa ya daraja la tisa la mafunzo ya kijini ya kuita pepo.
Kutokana na mkandamizio wake kuwa mkubwa Roma alijikuta akiamini huenda hata Athena akashindwa kabisa kudili nae.
Kutokana na uwezo mkubwa aliokuwa nao mpizani wake Roma alianza kupoteza pambano mapema kabla hata hajaanza kushambulia kwani alishindwa hata kubadilisha nguvu zake kuleta faida katika kushambulia.
Aoiline hakuonyesha kutumia nguvu yoyote alikuwa ni kama vile anacheza na zile kamba za nguo zake za hariri na alianza kuzifanya zipeperuke hewani na zilikuwa zikitoa nguvu kubwa mno .
Roma palepale aliweza kufikiria huenda mbinu yake haikuwa ikitegemea muundo au nguvu bali alikuwa akitegemea akili yake na ufahamu . mpaka hapo alijua kwamba ulimwengu huo wenyewe ulikuwa kikwazo kwake hivyo hakuwa na namna ya kumshinda.