Jamwambo
Member
- May 21, 2020
- 6
- 10
Uzuri akileta mzigo unakuwa wa maana lazima usome siku tatu na zaidiNa alituahidi itaisha siku ya Eid Al fitri
Uzuri akileta mzigo unakuwa wa maana lazima usome siku tatu na zaidiNa alituahidi itaisha siku ya Eid Al fitri
Roma alikuwa ashahisi akisogelewa kwa muda mrefu lakini hakutegemea kama jini huyo angemuamrisha kusimama tena kwa sauti kubwa , mara baada ya kugeuka aliweza kuona jini mzee ambaye amevalia joho la rangi nyeusi akiwa na nywele ndefu za rangi nyeupe.>>>>>>
Kutokana na jeuri yenu ya kumhukum kwa sababu ya kutaja siku sasa hajaweka siku tukose pa kumshikiaStory tamu sana lini tena bosi
nihatari sana hi.Kutokana na jeuri yenu ya kumhukum kwa sababu ya kutaja siku sasa hajaweka siku tukose pa kumshikia
nihatari sana hi.
Du!. Kumbe??.Hii DUNIA inawatumia makatili aisee
Kumbe sio roma Romani pekeake wengine hawana majina ila wapo
Shukran sanaNILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA.
Mono no aware
SEASON 25
SEHEMU YA 721.
Kama Roma angeweza kufananisha uwezo wa Jini Anjiu na Bi Tigola basi uwezo wa Tigola ungekuwa ni kama maji yaliojazwa nusu kipimo kwenye glass huku Jini Anjiu uwezo wake ni glass iliojaa maji mpaka pomoni na kuanza kumwagika, ni uwezo ambao ulikuwa nje ya matarajio yake.
Kwa haraka haraka Roma alijua pengine Anjiu ni jini pekee ambaye anaweza kuingia katika mzunguko tisa ya awamu ya mapigo tisa ya radi.
Anjiu dakika ileile aliangalia mavazi ya Roma na kumfanya amwangalie kwa macho yaliojaa kejeli.
“Ni ujasiri wa namna gani uliokuwa nao , nadhani tayari umemuua Laofi”Aliongea.
Kauli yake ile ilimshangaza Roma ambaye alianza kuhisi hisia zisizokuwa za kawaida.
“Ulijua tokea muda mrefu?”Aliuliza Roma.
“Unanichukulia mwepesi , unadhani nitaacha kuwa makini baada ya kile ulichokifanya katika miliki ya Kekexil , unadhani naweza kufeli kulinda miliki yangu?”Aliongea
Dakika ileile ma elfu ya majini yalitokeza kila pande katika makao makuu hayo ya miliki na Roma aliweza kuhisi uwepo wao kutokana na msuguano wa nguvu za kijini .
Kufumba na kufumbua majini wenye vyeo vya juu katika miliki hio walikusanyika nyuma ya mkuu wa majini Anjiu. Huku walinzi kutoka katika kila familia wakimzingira Roma na Rufi.
Zianji , Leiana , XiaoXiao na Lahani na wengine wote walikuwepo , dakika ambayo Lahani alimuona Rufi na Roma hasira zilijidhihirisha kwenye macho yake.
Upande wa XiaoXiao aliishia kuziba mdomo wake kwa mshangao akiwa haamini kile anachokiona.
Kwa kutumia mkono tu Jini Anjiu alianza kusambaza sauti yake katika makazi yote ya majini katika eneo hilo la makao makuu.
“Kila mmoja na anisikilize , huyu ni mwizi ambae amemuua Guru mkuu Tigola wa Kekexil, jina lake ni Roma Ramoni kutoka dunia ya binadamu na Rufi ni mpenzi wake , alitumia hila na kumuua mtumishi Lao na mzee wetu mkuu Laofi mapema ya leo , hajaishia hapo tu bali pia ameiba hazina zetu ndani ya jengo la kutengenezea vidonge na kuuwa majini wenzetu zaidi ya kumi na mbili na sasa anajaribu kumtorosha mfungwa wetu Rufi kutoka hapa”
Maneno ya mkuu huyo wa majini yalifanya kila jini alieweza kusikia katika ngome hio kushikwa na mshituko.
Hakuna ambaye aliamini Laofi alikuwa ameuliwa na Roma , mzee ambaye alikuwa akiheshimika kwa uwezo wake wa levo ya maji ya kiroho.
Mara baada ya Zianji kusikia kauli hio alijikuta akipauka mwili , na alijikuta akiangalia mavazi ya Roma.
“Huyu binadamu anao uwezo mkubwa wa nguvu za mbingu na ardhi na anamiliki Dhana ya hatari ya Chungu cha maafa , haina haja ya kujitoa kafara bila maana yoyote na mimi kama mkuu wa miliki hii nitamuadhibu”
Maneno ya jini mkuu Zianji yalifamfanya kila jini aliemsikia kuwa na heshima juu yake.
Malezo yake ya kuchukua hatua zidi ya mwizi yalikuwa yamemjengea heshima kati ya majini hao kwa kuwazuia kutotoa kafara maisha yao , kwani kama mtu huyo alikuwa na uwezo wa kumuua Laofi ilimaanisha kwamba wao hawakuwa na uwezo wa kudili nae hata kwa kuunganisha nguvu.
Upande wa Roma alikuwa na hasira kwa kuona kila alichokuwa akifanya alikuwa akijiingiza ndani ya mtego aliowekewa na Anjiu.
Laofi alikuwa ni gugu katika utawala wa jini Anjiu na kutokana na kukosa sababu ya kuweza kudili nae basi aliacha Roma amsaidie kufanya kazi hio na mara baada ya hapo alijitokeza baada ya Roma kuiba ndani ya jengo la kutengenezea vidonge ili amkamate akiwa na ushahidi na baada ya hapo amshughulikie ili ajichukulie umaarufu na heshima.
Roma aliishia kutoa kicheko kutokana na maneno yale licha ya kwamba alikuwa na hasira kwa kuingia mtegoni.
“Hakika uvumilivu wako sio wa kawaida , kwasababu ulishajua tokea muda mrefu nilichomfanyia mtumishi Lao lakini pia ukajua lazima nitamshambulia Laofi basi lazima utakuwa pia unajua uhusiano wa kimapenzi uliopo kati ya mke wako na Lao ,Zianji na Laofi , umesalitiwa kwa zaidi ya miaka na sasa unajaribu kunichokoza waziwazi hahaha…huna aibu”
“Whoaa…!!!”
Kila jini ambaye amesikia maneno hayo alijikuta akitoa mshangao kutokana na kile Roma alichosema.
“Acha kutafuta namna ya kujiokoa kwa kuongea upumbavu , umemuua Lao na Laofi na sasa hivi unamsingizia mke wangu na Zianji , unafikiri unaweza kuondoka hapa kwa kuongea huo ujinga?”
Baada ya kuongea maneno wale wazee na raia wa miliki hio waliona lazima Roma anadanganya hivyo walimuamini mkuu wao na kumwangalia Roma kwa macho ya kimauaji.
Zianji alikuwa akitoa kindoo cha jasho na kutokana na mambo kufikia hatua kama hio alijua lazima kaka yake alikuwa akijifanyisha hajui kinachoendelea na kumtetea kwasababu Roma hakuwa na ushahidi kwa wakati huo.
Lahani na Xiao walikuwa na muonekano tata katika nyuso zao mara baada ya mama yao kuhusishwa kufanya Dhambi na mmoja ya wanafamilia.
Roma alishangaa kwa namna ambavyo Anjiu alipotezea swala hilo bila ya kuonyesha hali ya kukasirika na alijikuta akikosa usemu na alijuliza ulikuwa ni uungwana au ndio kwamba anafurahia kusalitiwa.
Ghafla tu muda uleule Anjiu alitumia uwezo wake wa kijini kuongea na Roma bila ya wengine kusikia.
“Wewe mtukutu umenidharau sana , hivi unafikiria Leiana ataniathiri kwa matendo yake , ngoja nikuambie ana cheo cha kuwa mke wangu tu lakini sijawahi kumchukulia kama mwanamke wangu hivyo kwanini nijali kama ananisaliti , kama unataka nikupunguzie adhabu rudisha mbinu ya Andiko la Urejesho wa azimio maana hapa huwezi toka kwani upo kwenye miliki yangu”
Hakuna jini ambalo lilikuwa likisikia kutokana na kwamba wote uwezo wao ulikuwa wa chini sana.
Roma alishangazwa na kauli yake mara baada ya kuona sasa hajamuathiri kwa namna yoyote Anjiu, alikuwa akiongea ukweli kabisa hakuwa akimchukulia Leiana kama mke wake hivyo hakujali kupigwa mtungo na mdogo wake na majini wengine katika miliki , ndoa yao ilikuwa ni ya maneno tu , Roma alijiona ni mjinga na alipaswa kujua jini mwenye nguvu kama huyo asingeshindwa kuona kile kinachoendelea.
“Si nilishakupatia andiko , au ndio umeshindwa kujua kama ni halisi au ni feki?”Aliongea Roma akimjibu.
“Tunazo mbinu nyingi za mafunzo ya kijini katika miliki yetu kuliko hata miliki zote katika ulimwengu huu , ulichonipatia licha ya kutokukamilika ni mbinu tunayoita hatua tisa za Andiko la Ahadi, unaniona mimi ni mjinga”
Roma alishangazwa na kauli yake , Hatua tisa ya Andiko la Ahadi ni kitu gani au ni kama vilevile ilivyo kwa miliki ya Kekexil kuwa na andiko lake lakini hawajui maana yake.
Roma alishangaa na kujiuliza kwanini mbinu yake ya Andiko la urejesho kila mahali inaitwa majina tofauti tofauti au ni kwamba kuna maana ambayo hajawahi kuijua iliopo nyuma ya andiko hilo , je kama ni hivyo Andiko lilitokea wapi?.
Roma mara baada ya kuona Anjiu hakuwa akiamini maneno yake hakuona haja ya kumuaminisha kwani kama ni andiko ni kweli alimpatia lakini ilionekana lilifanana na hatua tisa za mbinu ya ahadi kama alivyosema.
Muda uleule Roma macho yake yalikwenda kutua kwa jini Lahani aliekuwa nyuma ya baba yake.
Ijapokuwa hajawahi kumuona ana kwa naa lakini aliweza kumfahamu kutokana na chuki iliokuwa imepamba uso wake.
Muda huo Roma alimuona Lahani kama mfu kwa kile alichomfanyia mpenzi wake Rufi.
Kutokana na kuwa na uwezo mkubwa wa utambuzi palepale jini Anjiu alijua nini ambacho Roma anaangalia.
“Lahani ondoka hapa”
Aliamuamrisha mtoto wake na kumfanya kushangaa huku akijiuliza baba yake anamaanisha nini kumpa agizo hilo.
“Haha… una uhakika anaweza kunitoroka?”
Sekunde ambayo Roma anatamka kauli hio alikuwa ashachomoka alipokuwa amesimama na kumsogelea Lahani kwa spidi.
Ndio muda ambao Lahani alipatwa na kiwewe na mshangao kwa kujiuliza inakuwaje anataka kumuua mbele ya baba yake na majini wote hao, haogopi kifo.
Lakini ukiachana na mawazo yake aliweza kugundua mkandamizo wa nguvu za kijini kutoka kwa Roma ulikuwa ni mkubwa mno na kumuogofya na kujiuliza ilikuwaje Rufi akaja kukutana na huyo kichaa , alijiambia amewezaje kufikia hatua hio ya nguvu za kijini kwani anaonekana kuwa katika umri sawa na yeye.
Lahani alikuwa katika hali ya woga mkubwa mno na akili yake ilikuwa ni kama imeshikiliwa na Roma kwani alishindwa kuchuukua maamuzi ya kukimbia kama alivyoamrishwa na baba yake.
Lakini Anjiu alikuwa ashaliona hilo hivyo alimzingira Lahani na ngao ya kijini na kufanya majini waliokuwa wakiangalia tukio hilo kupatwa na ahueni.
“Unathubutu vipi kwenda kinyume na maneno yangu , unadhani utaweza kushindana na mimi kwasabbau ya hicho chungu chako cha maafa?”Aliongea Anjiu na palepale aliinua mkono wake juu kama vile anapokea kitu hewani na kitenesi cha mwanga kama wa moto wa Zambarau kilitokea na sekunde ileile kitenesi kile kibadilika umbo na kumsogelea Roma kama vile ni boriti ya mwanga wa Laser.
“Pumbavu nani kasema nitatumia Cauldron?”
Roma na yeye alijibu kijeuri wakati akishuhudia nguvu ya shoti ile iliokuwa kama vile ni radi na Roma hakutaka kujaribu bahati yake kuacha imguse katika mwili wake kwani hakujua nguvu yake ikoje na palepale na yeye alitoa moto wa mchanganyiko wa rangi nyeupe na elementi za radi ya zambarau na kurushia lile shambulizi na sekunde ambayo shambulio la Anjiu linakutana na siraha ya Roma ya kijini palepale boriti yake ya moto ilipanguliwa na kusambaratishwa bila hata ya kumfikia.
Mng’ao wa rangi nyekundu na zambarau ulimulika eneo lote huku nguvu yake ya kijini ikiwaogofta majini waliokuwa karibu na kuwafanya wakimbie kwenda mbali.
Roma mpango wake ni kupigana na Anjiu kwa kutumia chungu lakini alikipa maagizo ya kumlinda Rufi kwani hakutaka majini wengine kumshambulia wakati akiwa bize katika kupambana na Anjiu.
Sasa mara baada ya Roma kuona Lahani alikuwa mbele yake , hakutaka kupoteza fursa hio kumshikisha adabu kwa kile alichomfanyia Rufi kwani anaweza asimpate tena kama akimuacha.
Kwa mzunguko mmoja tu wa mashambulizi sasa Roma aliweza kujua uwezo halisi wa Jini Anjjiu, kimahesabbu Roma alikuwa katika levo ya mapigo tisini na tisa ya radi ya Zambarau na Anjiu yeye alikuwa mwishoni mwa levo ya maji ya upako hivyo kwa haraka haraka ni kwamba hamuwezi Roma, lakini licha ya hivyo nguvu zake za kijini zilikuwa kubwa mno kuliko jini yoyote ambaye yupo katika levo ya majji ya upako.
Moto wa rangi ya zambarau wa Roma licha ya kwamba ulikuwa na nguvu kuliko moto wa radi ya Zambarau wa jini Anjiu, haukumpa nafasi ya juu katika kushinda.
“Usije kujaribu”Aliongea Roma kwa nguvu mara baada ya kuona Lahani anataka kukimbia.
Na Roma alizunguka kama vile ni mwanariadha na kurusha moto wa rangi ya bluu uliiokuwa katika maumbo ya nyoka kumfukuzia Lahani.
Lahani hakuwa na uwezo wa kumshinda Roma katika spidi ya mashambulizi yake na ni sekunde tu aliweza kuhisi nguvu ya ajabu ukimsogelea kwa nyuma na alijikuta akipagawa lakini baba yake alikuwa na spidi sana kwani palepale alitupia boriti za moto wa kimaajabu na kwenda kuzuia mashambulizi ya Roma
Kilichosikika hapo ni ngurumo tu kama vile anga linataka kudondoka huku nguvu ya moto ule wa vinyoka ulififia.
Jambo lile lilimtia hasira Roma , ijapokuwa moto wa Anjiu haukuwa na nguvu lakini ulikuwa na masafa ya maajabu ambayo yalikuwa yakiingiliana na moto wake wa rangi ya bluu.
“Mshindani wako ni mimi”
Aliongea Anjiu mara baada ya kutokea mbele ya Roma huku akimrushia mashambulizi ya nguvu za kijini yalioambaana na moto wa radi ya zambarau akimlenga Roma kichwani.
Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Roma kukutana na mshindani mwenye spidi namna hio na kama sio wepesi wake wa kuzuia na kukwepa pengine mashambulizi yale yangemfikia , lakini tofauti na kuwa na wasiwasi Roma alifurahi.
“Nice , wewe ndio umejileta mbele yangu”
Aliongea Roma na palepale madonge ya maji ya upako yaliokuwa kama vile ni mapovu yalianza kumtoka Roma na kwenda kumshambulia Anjiu na Lahani kwa wakati mmoja.
“Maji ya upako!!”
Kutokana na umbali wao kuwa karibu sana ilikuwa ngumu kwa Anjiu kukwepa maji hayo ya kiroho kutokana na athari zake lakini alikuwa mepesi sana kwani aliruka na kwenda kutua upande mwingine.
Miondoko yake ilikuwa rahisi mno kama vile ni spidi ya shoti za umeme na aliruka na wakati uleule kuachia moto wa radi ya zambarau kwenda kwa Roma na kumpiga kwa pembeni.
Roma mara baada ya kupigwa na ule moto wa radi palepale alisogea mita hamsini hivi kurudi nyuma huku maji yake ya upako yakisambaratishwa.
Upande wa Lahani mara baada kwa shida sana kukwepa mashambulizi ya Roma alijikuta akishikwa na woga usiokuwa na kifani , kama angeguswa hata na tone moja tu la maji hayo basi angepotezwa mazima.
“Pumbavu!”
Roma alitingishika kwa hasira kwani hakutegemea mashambulizi ya Anjiu ya radi ya zambarau kuwa na aina flani hivi ya masafa(freuency) ya ajabu lakini pia spidi yake kuwa kubwa mno na kujiongeza yenyewe , yaani shambbulizi lake lilikuwa na spidi ndogo kuliko moto huo na kumfanya shambulizi lake kumkosa Lahani na wakati huo kupokea shambulizi kutoka kwa Anjiu.
Ngozi yake iliwasha kila mahali na sehemu ya shati lake lilikuwa limechanika lakini kwa bahati nzuri utimamu wa mwili wake ulikuwa sio wa kibinadamu hivyo hakuumia.
Roma mara baada ya kugeuka aligundua Lahani amefanikiwa kukimbia na ilikuwa ngumu kumfikia tena.
“Pumbavu nimremruhusu yule msheni kuniponyoka”Aliongea Roma huku aking’ata meno yake kwa hasira na msisimko wa nguvu ya kimauaji ulianza kumvaa palepale.
Majini wa miliki hio walikuwa wakiangalia kwa hofu kutoka kwa mbali na mara baada ya kuona shambulizi la mkuu wao limempiga Roma wote kwa pamoja walishangilia.
Kuhusu XiaoXiao aliishia kutoa pumzi ya ahueni mara baada ya kaka yake kukimbia na sekunde iliofuata wasiwasi wake aliuelekezea kwa Roma na kisha akageuza uso wake kwa baba yake na katika hali hio hakuwa na chakufanya , ilionyesha dhahiri hakutaka baba yake kushindwa na pia hakutaka Roma kushindwa na kufa mbele yake,mwenye alishangazwa na hisia hizo.
“Nini tena , hicho ndio kitu pekee unachoweza kufanya lakini bado unajaribub kumua mwanangu huku huwezi hata kutoroka hapa”Aliongea Jini Anjiu kwa kejeli.
“Hakuna shida , nitakuua wewe kwanza na baada ya hapo nitamuua yule mshenzi”Aliongea Roma na sekunde hio hio alimsogelea Jini Anjiu kwa spidi huku mkono wa kulia akiwa na shambulizi la moto wa bluu na upande mwingine akiwa na shambulizi la moto wa zambarau.
Anjiu hakutaka kuzembea na kutokana na kumiliki radi ya rangi nyekundu iliokuwa imemzingira kama ngao aliamua kukumbana na mashambulizi ya Roma ya moto huku akitaka kutumia fursa hio kumpiga Roma na shambulizi la kushitukiza.
Mapema tu muunganiko wa moto na radi ulionekana angani na wimbi la nguvu za kijinni ulipasuka kwa wakati mmoja na kusababisha majini ambao walikuwa na uwezo mdogo kukimbilia mbali zaidi.
Wote waliishia kujiondolea ule woga kwa kile kinachoendelea kwani kila mmoja alikuwa na hamu ya kuona mapigano kati ya washindani wawili ambao wote wapo katika levo zinazokaribiana.
Ijapokuwa Roma moto wake wa bluu na Zambarau ulikuwa na nguvu lakini ulikingwa na mashambulizi ya shoti za mwanga wa zambarau na kuzimshwa na kwa kuangalia tu aliona hana uwezo wa kushinda kwa mbinu hio.
Rufi ambaye alikuwa akiangalia kila kitu alijihisi moyo wake kuuma na dakika ileile alikuja kupata uelewa wa jambo.
“Hubby kuwa makini hio ni mbinu ya juu ya kijini ya Xia ifahamikao kwa jina la Radi mshale wa zambarau uvukao anga , ni muunganniko wa atomu za madini na moto na uwezo wake ni kusambaratisha kila aina ya shambulizi , mbinu pekee yenye safu ya juu ndio inayoweza kupita”
Roma mara baada ya kusikia maelezo hayo palepale sasa alishaelewa na kujua kumbe huo ndio mtego wa huyu jini mzee ngoja sasa amuonyeshe.
SEHEMU YA 722.
Roma mpango wake ilikuwa ni kutumia uwezo wake wa kijini ili kumshinda Anjiu lakini hakuweza kuelewa, ijapokuwa mashambulizi yake ya radi yalikuwa na ukubwa kiwango flani basi kama atamshambulia kwa pande zote Anjiu hatokuwa na uwezo wa kuzimisha mapigo yake yote.
Kwa wakati mmoja hakuamini kama Anjiu alikuwa na uwezo wa kuhimili maji yake ya upako kama yatamgusa.
“Haha.. unaonekana kujua vitu vingi”Aliongea Anjiu huku akimwangalia Rufi.
“Zianji hebu leta hao majini wote waliopo levo ya maji ya barafu wavunje ulinzi wa nguvu ya Chungu”
Zianji ambaye alikuwa amesimama kwa mbali palepale alielewa uhalisia ulivyo , mwanzoni alitaka kushikirikiana na Laofi katika kumshambulia Anjiu kaka yake lakini wakati huo Laofi alikuwa amekwisha kufa hivyo alipaswa kusikiliza maagizo ya Anjiu kama anataka kuendelea kuishi kwa amani.
Baada ya macho yake kutua katika sura ya Rufi ambaye alikuwa chini ya ulinzi wa nguvu ya chungu cha maafa , alitoa taasamu la kejeli na aliongoza dazeni ya majini ambao wapo katika levo ya maji ya barafu kwa ajili ya kukishambulia.
Miliki hio ilionekana kuwa na mbinu nyingi za mafunzo ya kijini na mashambulizi mbalimbali yalirushwa kuelewa eneo ambalo Rufi alikuwa amesimama akipewa ulinzi na Caudron.
Chnngu kile kiliweza kumeza kila aina ya mashambulizi lakini sio yote na kilianza kupata athari na nguvu yake ilianza kufifia.
Roma alikunja ndita na alikumbuka kama chungu hicho kikiendelea kuwa katika hali ya ki ulinzi kitakuwa na uwezo wa kuhimili kwa muda mrefu kidogo hivyo hana haja ya kuwa na wasiwasi.
Baada ya kupatwa na wazo hilo palepale alikusanya nguvu kubwa ya andiko la urejesho na kuunganisha na nishati ya mbingu na ardhi na kuanza kumzingira kwa ukubwa.
Na palepale aliamua kupambana na moto wa radi ambao unamshambulia bila ya kukoma , muda huo huo Roma alitengeneza donge kuubwa la maji ya kiroho ambalo lilikuwa likipanuka kwa spidi kubwa mno kiasi cha kufikia saizi ya futi kumi.
Lilikuwa kama puto kubwa ambalo linanesa nesa hewani na halikuweza kupasuka kila baada ya kukutana na mashambulizi ya radi.
Dakika ileile majini wote walianza kupatwa na hofu na ilikuwa ni kama vile kitu cha ajabu kina wavamia kutoka juu mbinguni.
Jini Anjiu palepale alijikuta akisawajika uso kwa kushindwa kuamini Roma alikuwa na uwezo wa kukusanya kiasi kikubwa hivyo cha maji ya kiroho kwani ilihitaji nguvu kubwa mno za kijini.
Chini yake kile chungu cha chuma kilikuwa kikitoa mng’ao kila mara baada ya kumeza mashambuizi na kuendelea kumlinda Rufi na mfululizo wa milipuko ya Dhana haikuonekana kuwa na mwisho na kumfanya Rufi kujihisi anakwenda kua majivu muda wowote , lakini kwa wakati huo hakuwa na jinsi zaidi ya kusimama chini ya chungu hicho huku akiwa amafumba midomo yake asipige yowe.
Kwa bahati nzuri ni kwamba kadri walivyokuwa wakikishambulia ndio kilivyokuwa kikiongezeka nguvu kwani kilikuwa kikinyonya nishati yao na sasa kilianza kunesa nesa hewanni na nguvu yake kupanuka zaidi na kuwafanya wale majini kushindwa kuvunja fensi yake ya ulinzi.
Anjiu alikuwa makini mno huku akiendelea kushambulia lile donge la maji ambalo Roma ametengeneza na moto wake wa shoti za radi ya Zambarau huku akijiuliza ni kitu gani ambacho Roma anapanga kufanya muda huo na maji yote hayo.
Lakini dakika hio hio Roma sasa alijua hatimae muda umewadia na palepale alilirusha lile donge la maji kwenda juu zaidi ya angani huku akipiga kelelele ya ‘Nendaa’
Baada ya kufika angani palepale alilipiga na mshale wa nguvu y a kijini na likapasuka kama vile ni puto ambalo lina maji ndani yake na mvua ya maji ya kiroho ilianza kunyesha katika mzingo wa kilomita mia moja.
Mpasuko ule ulisababisha matone mengi kudondoka na kusafiri kwa kutumia nguvu ya kijini na hakukuwa na uwezekano kwa majini wa levo za maji ya barafu kuweza kukwepa matone yale kwani ilikuwa ni sawa na kukwepa mvua bila ya mwamvuli.
“Arghhhh…!!!”
Vilio viliweza kusikika mara baada ya matone yale kugusana na miili ya majini waliopo katika levo ya maji ya barafu na kuanza kuwayeyusha.
Dakika ileile Chungu chenyewe hakikukaa kizembe kwani kilitumia kama fursa na kuanza kunyonya nguvu zao za kijini kwa spidi kubwa mno huku kikizungukwa hewani kama pia.
Muda huo huo Roma na yeye aliweza kupokea shambulizi la radi ya zambarau kutoka kwa Anjiu lakini shambulizi hilo halikumuua kama ambavyo shambulzi lake limewamaliza majini wale wa levo ya maji ya barafu.
Zianji ndio peke yake ambaye aliweza kuepuka kwani uwezo wake ulikuwa wa juu hivyo alijitengenezea ngao kama mwamvuli na kisha kukimbia na muda huo Anjiu na yeye aliweza kupokea matone mengi ya maji ya kiroho lakini hakuathirika kwani nguvu zake za kijini zilikuwa zimenzingira kwa kumtengenezea ngao.
Lakini muda huo mashambulizi yake yalikoma kwani utimamu wake wa mwili haukufnana na wa Roma hivyo alianza kupambana na maji yale yasimdhuru.
Roma pia hakuwa na mpango wa maji yake ya kiroho kumuua na alichokuwa amepanga ni kuondoa hao majini wasumbufu wa Xia ili kuwaelimisha kwamba hayo sio mapigano ya levo zao.
Mara baada ya kuona Anjiu ameacha kushambulia alichukulia fursha hio na kuanza kumshambbulia kwa kasi na maji ya upako Anjiu.
Jini Anjiu aliona kukaa sehemu moja na kuangalia namna ambavyo ngao yake inayeyushwa taratibu taratibu na maji ya upako aliona ingekuwa ni chaguzi mbaya sana.
Hasira ilimshika palepale katika macho yake sio kwasababu ya hila za Roma lakini vilevile kutokana na kuua majini wengi kwa wakati mmoja.
“Unathubutu vipi , unakitafuta kifo”
Kwa wakati huo alikuwa na hasira mno kiasi cha kutokujali mbinu ya Andiko la Urejesho tena na alichotaka nikumuua Roma tu.
“Pata kionjo cha moto wangu wa ndege wa miguu mitatu , Moto wa ukweli, Ndege wa Dhahabu”
Palepale moto ambao ulikuwa ukifanana na mwanga wa jua ulionekana mbele yake na kutengeneza umbo la ndege wa miguu mitatu(Three Legged Golden Crow) , miguu yake ilikuwa mirefu saizi ya futi tatu huku mabawa yake yakiwa pia katika umbo kubwa la kimaajabu.
Na mwanga kama wa jua ulianza kuwaka kwa kuongezeka katika eneo hilo na kumeza giza lote na ndani ya sekunde tu yale maji yake ya upako yalikaushwa palepale.
Muda huo Jinni Ajiu alikuwa amebadilika kabisa na kuonekana kama vile ametengenezwa kwa moto wa jua.
Roma alikuwa ashasikia hio mbinu kutoka kwa Rufi hivyo alishaielewa kwa kiasi lakini kwa wakait huo hakuweza kuamini ilikuwa ikiogopesha kiasi hicho.
Aina ya moto huo wa kimaajabu ulikuwa ukikaribiana na nguvu halisi ya moto wa jua.
Sasa Roma hatimae alijua ni kwanini Rufi alisema ni Jini huyo pekee ambaye aliweza kumaster mbinu hio.
Lakini kitu kingine ambacho Roma aliweza kujua ni kwamba licha ya kwamba ni mbinu yenye nguvu lakini ukali wake unategemeana na nguvu ya nishati ya mbingu na ardhi na kwa jini kama Anjiu ambaye ndio kwanza yupo mwishoni mwa levo ya maji ya upako hakuwa na uwezo wa kutoa nguvu yake yote.
Ndege yule ambaye alikuwa katika umbo la moto alianza kupiga piga mabawa yake , ijapokuwa ni ndege ambaye yupo katika umbo la moto lakini msuguano wa moto ule na elementi za hewa ulifanya eneo lote kusikika vilio ambavyo havikueleweka.
Roma alijaribu kumkwepa yule ndege kwa spidi lakini licha ya hivyo alijikuta akiunguzwa na yale mabawa yake na palepale alijikuta akitoa mguno wa maumivu na kuhisi ni kama vile mwili wake unachemshwa katika pipa la mafuta.
Lakini hata hivyo mafuta ya kawaida hayawezi kumpa madhara makubwa lakini maumivu alioweza kuyapata kusikia hapo yalikuwa sio ya kawaida kabisa.
Ilikuwa ni bahati kwamba uwezo wake wa Andiko la urejesho ulifanya kazi na kumponyesha ndani ya sekunde na kuondoa seli ambazo zimeunguzwa.
“Sidhani kama nitaendelea kuhimili kama nitaendelea kupokea mashambbulizi ya aina hii”Aliwaza Roma.
Kwa mara nyingine anakutana na jini ambaye yupo vizuri kuliko yeye kutokana na kutokuogopa moto wa anga wala moto wa rangi nyeupe na wa bluu, ukweli ni kwamba Roma hakuwa na uelewa wa kutosha na moto huo wa kimaajabu na hivyo aliona anaweza kuzidiwa.
Hali ya mshangao iliweza kumkumba jini Anjiu mara baada ya kuojna Roma alivyoweza kupona kwa spidi kubwa lakini haikumrudisha nyuma katika kufanya shambulizi lingine.
“Ndege wa Dhahabu wa miguu mitatu,Yang’wi katika umbo halisi , kusanyiko la ndege elfu moja!!!”
Aliongea jini Anjiu kwa sauti kama vile anaita viumbe hao na ndani ya sekunde tu kundi la ndege wengi sana ambao wapo katika maumbo ya moto walionekana wakija katika eneo hilo kwa spidi kubwa na walionekana kwa dhahiri ya macho kutokana na giza.
Majini wote wa miliki hio walijikuta wakipatwa na woga usio na kifani akiwemo Zianji mwenyewe kasoro Xiao tu ambaye aikuwa na hali ya wasiwasi mkubwa mno.
Kutokana na miliki yao kutokumbwa na adui mwenye uwezo mkubwa kwa kipindi kirefu hawakuwahi kuona uwezo halisi wa mbinu hio ya ndege wa miguu mitatu.
Roma hakuweza kupata hata muda wa kufikiria ni hatua gani afanye kukabiliana na hao ndege na palepale alijitengenezea ngao ya maji ya barafu kuzingira mwili wake kwa kujua kabisa asingeweza kuwamaliza hao ndege kwa shambulizi moja.
Lakini sasa mara baada ya wale ndege wa moto kugusana na ngao yake ya barafu iliyeyushwa palepale , licha ya kwamba baadhi yao waliweza kuzimishwa lakini ilikuwa ngumu kuzuia shambulizi hilo.
Roma alishikwa na mshangao na hakuwa na namna zaidi ya kukimbia ili kuepuka moto wao usigusane na mwili wake lakini hata hivyo spidi yao ilikuwa kubwa mno na alijua asingeweza kuwahimili kuwakwepa wote na wangemuweka kati.
Chini ardhini Chungu kilipo, Rufi alikuwa kwenye woga mkubwa mno na uso wake ulipuaka.
“Hubby chukua chungu , huna haja ya kunilinda”Aliongea kwa nguvu huku akitamani kulia.
Alijua kama Roma angekuwa akitumia chungu hicho cha maafa basi uwezo wa Jini Anjjiu ungepungua mpaka nusu yake kwasababu kilikuwa na uwezo wa kuhimili mashambulizi mengi kwa wakait mmoja.
Lakini Roma hakuwa na mpango wa kutumia chungu hicho kwani hakutaka kumuweka katika hatari licha ya kwamba alijua angekuwa na nafasi kubwa ya kushinda kama angekitumia.
Sababu nyingine ya kutotumia chungu hicho ni kwamba Anjiu bado hakuwa ametumia Dhana yoyote katika mashambulizi na alijua kama angeshindana nae kwa kutegemea chungu hicho basi anaweza kushindwa kirahisi.
Ki ufupi ni kwamba Roma hakutaka kushindana na Anjiu kwa kutumia chungu kwasababu hata yeye hatumii Dhana bali uwezo wake tu wa kijini , hivyo alitaka kama ni kumshinda basi amshinde kwa uwezo wake na sio kwa Dhana.
Sababu pia ya kutotaka kutumia chungu ni kutokana na kwamba mpango wake ni kuja kupitia mapigo mia tisa tisini na tisa ya radi hapo baadae ili kuweza kuimarika zaidi na zaidi na hilo ili litokee basi anahitaji kupambana na jini mwenye uwezo mkubwa zaidi na utalaamu wa hali ya juu ili aaweze kujifunza.
Wale ndege wa miguu mitatu ambao majini huwaita kwa jina la Yang’wi baadhi yao walikuwa wakigongana wao kwa wao na kusababisha mlipiko na wengine kumpiga na kumfanya Roma kutetemeka kutokana na ukali wa moto ambao unamtengenezea majeraha.
Lakini Roma hakutaka kukata tamaa zaidi ya kutumia moto wa bluu na wa zambarau kuendelea kushambulia kwa spidi kubwa.
Roma alijua kwasababu Anjiu hakuwa na uwezo wa kumuua basi nafasi ya kupambaana nae ipo tu isitoshe hao ndege wasingeweza kuhimili nguvu yake ya mapigo tisini na tisa ya radi ya Zambarau
Lakini alipatwa na kiwewe kwasababu hakuwa na uwezo wa kujitoa katika mtego wa hao ndege kwani alikuwa akijilinda zaidi ya kufanya mashambulizi.
Walikuwa ni wengi sana na akishambulia huyu alikuwa akishambuliwa na huyu zaidi sana ni kwamba nguvu ya kiijini ya moto huo kutoka kwa Anjjiu ilionekana haina kikomo.
“Huyu mtukutu anajifanya mwamba kutotaka kutumia Dhana yake, Mkuu wetu lazima atafanikisha kumdhibiti”
“Kama tulivyoratarjia kwa jini wa kwanza kuweza kubobea katika mbinu ya Yang’wi kwa zaidi ya miaka elfu moja , kumbe hii ndio nguvu yake halisi tunayoiona, ni hivyo tu hautotoweza kufanikisha kuijua”
“Haha….huyo binadamu ni mshenzi sana ameua majini wetu wengi , anapasswa kuwa kaa la moto”
Majini hao wa miliki ya Xia walikuwa washamuona Roma kama mfu tayari , walijua kila ukinzani ambao angeweka ungekuwa ni bure tu na hakutofautiana na mnyama ambaye yupo kwenye zizi.
XiaoXiao aliishia kuweka mkono wake mdomoni bila ya kujielewa akiendelea kung’ata kucha zake kwa wasiwasi na alijiuliza huyu mwanaume mbaya ashamuumiza mara kibao kwanini bado anaonyesha kumjali.
Muda huo katika hali hio hatarishi Roma bado alikuwa na utulivu huku akifikria namna ya kudili na hao ndege wa moto.
“Sina namna nyingine lakini kwasasa napaswa kutumia ile mbinu, ijapokuwa bado haijaimarika lakini nadhani inaweza kufanya kazi”Aliwaza Roma bila ya kuelewrka ni mbinu ipi , lakini ilionyesha ni dhahiri ile siku ambayo alikuwa akifanya mazoezi aligundua mbinu hio
SEHEMU YA 723
Roma mara baada ya kuamua kutumia mbinu ya ufunuo ambayo aliweza kugundua hakuwa na haja tena ya kujizuia na palepale mkono wa kulia alitengeneza moto wa kiroho wa rangi nyeupe na kishoto kwake alitengeneza maji ya kiroho na baada ya palepale kama vile anapiga makofi aliunganisha moto ule wa kiroho na maji yale ya kiroho.
Fission(mgawanyiko) wa nguvu ya maji ya kiroho na moto wa kiroho ulikuwa ni wa hatari mno kwani ni kama vile ni rutubisho la atomu na atomu na kutengeneza nguvu ya kinyuklia lakini sasa nguvu hio kuwa kubwa zaidi ya mara kumi ya nyuklia na kutengenza mionzi ya hatari ya uyeyushaji.
Roma alipokuwa katika mafunzo alijaribu kuunganisha moto wa rangi ya bluu na maji ya upako na jaribio lake lilikubali lakini alikuja kugundua maji ya upako na moto wa upako vilikataa kuunganishika na kutengeneza kitu kama bomu.
Upotofu wa kimwili aliokuwa nao Roma haukuwa wa kawaida kwani kitendo kile cha kuunganisha nguvu mbili ambazo zinakataana zilimsababisha athari kubwa katika roho yake na kumtengenezea maumivu.
Ukweli ni kwamba licha ya kwamba mwanzoni aliona mbinu hio ilikuwa ikikataana haikumaanisha kwamba haikuwa ikifanya kazi , kilichokuwa kikimchanganya ni kwamba kuna kitu ambacho alikuwa akishindwa kuelewa kuhusu nguvu hio.
Katika spidi ya kupepesa macho , ngurumo kubwa ilisikika mara pamoja na wimbi kubwa la nguvu za kijini, palepale alifanikisha kuunganisha elementi za maji ya kiroho na moto wa kiroho na kutokea ktiu cha ajabu mbele yake.
Ilikuwa ni kama donge la moto wa rangi ya samawati na moto ule ulikuwa ni kama vile unaunguza anga na kutengeneza nguzo ya moto ambayo ilienda moja kwa moja mpaka mawinguni.
Tukio lile lilimfanya Jini Anjiu ambaye amesimama karibu kuanza kuhishi hisia za kifo kwani roho yake ilikuwa ikifurukuta na mshituko ulimshika palepale.
Wale ndege wake mfano wa kungnru waliendelea kumshambulia Roma bila kukoma na kuacha majeraha ya vidonda katika mwili wake, maumivu yale makali ya ule moto ndio ambayo yalimpatia ufunuo wa ajabu Roma , ilikuwa ni kama vile mtu anavyoamua kujinyonga na kabla ya kukata Roho anaona Jehanamu ilivyo na kutaka kughairi kufa.
Palepale alijikuta msisimko wa mwili ukiongezeka na kupitia mawazo yake tu ule moto wa rangi ya samawati uligawanyika na kuwa kama vile ni vinyoka nyoka vingi sana vyenye mabawa na kuanza kupambana na wale ndege kwa spidi kubwa mno na wale ndege walianza kukosa nguvu na kupotea mmoja mmoja.
Upande wa mita kadhaa mbali na Roma jini Anjiu alionyesha hali ya maumivu kwani yeye ndio ambaye alikuwa akiwadhibiti ndege hao kutumia nguvu zake za kijini hivyo mashambulizi ambayo ndege wake walikuwa wakipokea maumivu aliyasikia yeye.
“Inawezekana vipi!!”
Alijikuta akipatwa na mshituko usiokuwa na kifani na kukunja ngumi yake huku uso wake ukipatwa na kiwewe.
Anjiu macho yalimtoka na kuwa mekundu mara baada ya kuelewa sasa moto ambao Roma ametengeneza ulikuwa ukiharibu ndege wake na kumtengenezea kupatwa na athari kubwa katika nafsi yake.
Aliona kabisa kama mashambulizi hayo ya moto wa Roma wa ajabu ukiendelea kumshambulia basi anaweza kupoteza roho yake kabla hajamuua.
Roma ambaye alikuwa akishambiliwa na ndege wale sasa alijua walikuwa wakiathirika na wengine walikuwa wakikwepa ule moto hivyo alijikuta akiachia kicheko cha furaha.
Hakuamini angeweza kutengeneza siraha ya ajabu katikati ya maumivu ambayo ilikuwa na uwezo wa kuzima mashambulizi ya moto wa majabu uliokuwa ukizaliwashwa na dnege hao wa miiguu mitatu.
Ndege wale sio kwamba walikuwa wakijitegemea uwezo wao ulikuwa umeunganishwa na uwezo wa Anjiu , hivyo alijua fika kila kinachowapata wale ndege kina mpata na Anjiu na sio kwa namna ya kimwili bali kiroho zaidi.
Kwahio kama angeendelea kuwatumia katika mashambulizi basi atashindwa kuwadhibiti na ataishia kutumia mashambulizi ya radi wa Zambarau.
Dakika chache baadae wale ndege walianza kupoteza nguvu na kuanza kupoteza maumbo yao na kuanza kusambaa kama majivu angani na kuacha cheche pekee.
Roma alijikuta sasa akivuta pumzi ya ahueni na mara baada ya kumuangalia Anjiu sasa ule muonekano wake kama wa jua ulikuwa umepungua kabisa.
Maelfu ya majini wa miliki hio walijikuta wakishangazwa na jambo lile na kuogopa kwa wakati mmoja , hawakuamini ule moto wa ajabu uliotokea umeweza kudhibiti nguvu ya moto wa Yang’wi.
Mara sasa baada ya kuona Roma kapindua meza hakuna jini hata mmoja ambaye alikuwa na ujasiri kwenda kumsaidia mkuu wao , kwani waliona kabisa pambano hilo sio levo zao hivyo waliishia kuangalia tu bila ya kutoa msaada.
Muda uleule Roma alitumia nguvu ya andiko kuponyesha majeraha yake ya moto na mudi yake ilikuwa imeimarika huku akiwa ameshikilia moto wake wa rangi ya samawati ambao haukuwa na mng’ao wowote , yaani ilikuwa ni kama vile ni donge la moshi na hakuamini kama ameweza kupata ufunuo huo katika hali hatarishi kama hio na alijiambia mambo kama hayo hayatokei kwa bahati mbaya.
Mara baada ya kuona Rufi alikuwa salama nguvu yake ya kimauaji iliongezeka kwa kasi na sasa dhamiri yake ilikuwa ni kumuua Anjiu kwa kutumia ule moto ambao bado hakuwa akijua hata aupe jina gani na baada ya hapo amuue na Lahani.
Lakini sasa wakati akitaka kufanya hivyo alikuja kuona Anjiu hali yake ilikuwa ya ajabu kidogo , alikuwa ameshika kichwa chake huku mwili wake ukiwa umejikunja na meridiani zake za mwili zilikuwa zikipanuka kama vile ni vidonda vyenye usaha na alikuwa akitoa kilio cha ajanbu kama vile ameshikwa na ukichaa , ilionekana wazi alikuwa katika hali ya maumivu makali.
Dakika ileile michirizi ya rangi nyeusi ilianza kujitokeza katika sura yake huku nguvu ya giza ya ajabu ikianza kumtoka na kucha zake zilikuwa zikirefuka na kurudi katika hali ya kawaida.
“Baba..!!!”
Xiao ambaye alikuwa mbali alijikuta akipiga ukulele mara baada ya kumuona baba yake kuwa katika hali ile.
Wazee wengine wa miliki hio walikuwa katika hali ya mshangao pia kutokana na kile kinachoendelea na waliishia kuongea wenyewe kwa kumung’unya maneno.
Hata Roma mwenyewe alikuwa katika hali ya kuchanganyikiwa , bado hakuwa amedili nae lakini amebadilika na kuwa hivyo na palepale msisimko wa nguvu za giza uliokuwa ukimtoka ulimfanya kuhisi ni kama vile kuna mahali aliweza kuhisia nguvu hio.
“Devil beast blood!!”
Roma aliongea mara baada ya akili yake kufanya kazi na kukumbuka damu iliofahamika kwa jina la Damu ya mnyama wa kishetani.
Alikumbuka kutokana na msisimko wake wa giza mara baada ya kuona ile chupa ambayo alikuwa ameipata katika hifadhi ya pete ya mtumishi Lao, lakini pia aliweza pia kusikia kuhusu hio damu ilivyokuwa ikitumika kama sumu kwa Anjiu.
Ilionekana sasa damu hio ya kishetani ya mnyama ndio ilikuwa imeanza kufanya kazi , lakini Roma alijiuliza si Laofi na wenzake walisema ingechukua miezi kadhaa mpaka kuonyesha athari zake.
Roma aliishia kumwangalia Jini Anjiu kwa mbali ambavyo alikuwa na muonekano wa ajabu, ulikuwa ni muonekano wa mshangao na sio wa wasiwasi lakini uliojaa utata ndani yake na mchanganyiko wa furaha na ufumbuzi.
Roma alijiuliza kwanini yupo vile , au na yeye pia hajui kwanini sumu hio imefanya kazi mapema.
Ukweli hapo enzi za kale katika hadithi za majini aliwahi kuwepo jini hatari sana ambaye alikuwa katika umbo la mnyama ambaye alibatizwa jina laTaowu.
Inasemekana mnyama huyu mara baada ya kuzidiwa na mashambulizi kutoka ulimwengu wa kijini alikimbilia katika ulimwengu wa kawaida katika bara la Asia
Kabla ya jiniTouwu kutorokea katika ulimwengu wa kawaida alikuwa amejeruhiwa sana na inasemekana ndio wakati ambao majini waliweza kukinga damu yake kutoka katika majeraha.
Sasa haikueleweka Taowu alikufa vipi lakini mababu wa kijini katika miliki ya Kekexil ndio ambao walikuwa na damu hio ya Taowu na ilikuwa ikirithishwa katika kila kizazi.
Ni damu ambayo ina elementi za ajabu na sumu kali sana baada ya kuingunanisha na baadhi ya elementi nyingine za sumu.
Kwa majini wenye nguvu kama Anjiu ilikuwa ngumu sana kumuwekea sumu kwani anao uwezo wa kuhisi kila aina ya nguvu ya ziada inayoongezeka katika mwili wak.
Lakini sasa likija swala la hio damu ya kishetani ya mnyama ilikuwa imetengenezwa kwa namna ambayo ni ngumu sana kwa jini yoyote kuweza kuigundua pale inapoingia mwilini.
Hivyo mara baada ya Laofi kuingia dili na jini Mohi kutoka Kekexili walimpatia mtumishi wa karibu wa Anjiu ambaye ni Lao kwa ajili ya kumuwekea katika kifaa maalumu cha kuchomea ubani.
Kwahio moja kwa moja wakati Anjiu alipokuwa akivuna nishati alikuwa akivuta hio sumu taratibu bila ya kujua kwa miaka miwili mfululizo.
Sumu hio mara nyingi inafanya kazi taratibu na kadri ambavyo alikuwa akiinusa ilikuwa ikimuathiri nafsi yake na kumfanya kuwa na hali ya ukichaa na mwishowe kwenda kinyume na masharti ya nguvu za kijini za kawaida na moja kwa moja angekosa uhalali wa kuendelea kubakia katika ulimwengu huo , kwani watu ambao wana nguvu ya giza ya ukichaa moja kwa moja walistahiri kwenda kuishi katika ulimwengu wa majini pepo au majini wakuu wa ulimwengu huo kumuua kutokana na kumuepusha kuua watu kutokana na ukichaa.
Jini Mohi alikuwa tayari kufanya dili kutoa damu hio kutoka Kekexil licha ya uadimu wake kwasababu alijua masharti yake ya matumzii yalikuwa magumu sana kwani inahitajika muda mrefu mpaka athari zake kuonekana , pili Kekexil siku zote walitaka kuona kifo cha Anjiu ili kupunaguza nguvu ya miliki hio.
Laofi na Zianji licha ya kiujua hilo hawakujali sana kwani matamanio yao ni kuwa na madaraka tu maswala ya kuwa na nguvu wangefikiria baada ya kufika katika nafasi ya juu.
Lakini ndio hivyo katika hali ya kutokutegemewa Laofi na Lao wameshakufa , hivyo ilimaanisha wasingeendelea kumuwekea Anjiu damu hio.
Lakini kwa bahati mbaya sasa Roma aliweza kuiamsha athari ya sumu hio kwa kutumia moto wake mpya wa rangi ya samawati kabla ya muda muafaka.
Roma hakutaka kuonyesha huruma kutokana na muonekano wa jini Anjiu , kwani miliki hio ilikuwa imemtesa sana Rufi na kumchukulia kama mnyama.
Katika ulingo wa kupambania uhai na kifo huruma ni sawasawa na kujishambulia mwenyewe.
Hivyo Roma hakutaka kujizuia na palepale alitengeneza moto mwingine akiwa tayari kumshambulia jini Anjiu.
“Usije kumuumiza baba yangu!!”
Ghafla tu mwanamke alievalia mavazi ya pinki aliweza kuja kutoka mbali na kusimama mbele ya jini Anjiu huku akimkodolea macho Roma.
Hakuwa mwingine bali ni Xiao ambaye alikuwa akijaribu kumzuia Roma kutokumshambulia Anjiu.
Kulikuwa na maelfu ya majini hapo ndani akiwemo Zianji lakini hakuna hata mmoja ambaye alipata ujasiri na kumzuia Roma na kumsaidia Anjiu , ni Xiao peke yake ambaye yupo katika levo ya nafsi aliepata ujasiri wa kusimama mbele ya Roma na kumzuia.
Roma alijikuta akisimama palepale na kumwangalia msichana huyo ambaye machozi yashaanza kujitengeneza katika macho yake.
Kulingana na sheria zake mtu yoyote ambaye atamzuia kumuua adui yake basi anapaswa kufa wa kwanza lakini Xiao alikuwa tofauti kwasababu alikuwa amemkosea.
Tokea mwanzo alikuwa amemdhania vibaya na kumuumiza lakini pia Rufi alikuwa na deni kwa Xiao.
Roma muda ule baada ya kugeuza macho yake na kumwangalia Rufi aliona alikuwa akitingisha kichwa akimwashiria asifanye chochote kumuumiza Xiao.
“Toka mbele yangu sitaki kukuumiza”Aliongea Roma huku akiwa amekunja ndita.
“Kuniumiza? Kuniumiza mara ngapi wakati ushafanya hivyo mara kibao, lakini bado unataka kumuua baba yangu , wewe ni mtu mbaya sana kama unataka kumuua baba yangu nitapigana na wewe kwani sikuogopi”Aliongea Xiao.
Roma aliishia kupanua mdomo wake akitaka kuongea lakini maneno yalishhindwa kumtoka , kama asingekuwa na kiburi cha kuzaliwa basi angemuomba msamaha lakini hali aliokuwa nayo wakati huo ilikuwa ni ya kifo na uhai.
Ghafla tu Anjiu ambaye alikuwa ameinama hatimae aliweza kusimama wima kwa kujikaza sana , uovu ulikuwa ukioneakana kwenye macho yake ambayo ni kama yamegeuka na kuwa ya mnyama.
Ilionekana bado alikuwa akipambana na nguvu ya ushetani wa mnyama Taowu kwa kutumia utayari wa ufahamu wake,kilichokuwa kikimtokea ni kama Roma alivyokuwa akipambana na uchizi wake.
Dakika hio hio Anjiu aliweza kuzuia ule ukichaa kutokana na uwezo wake mkubwa wa kijini na aliinua uso wake na kumwangalia binti yake ambaye hakuwa na woga kusimama mbele ya Roma.
Ijapokuwa Anjiu alisifika kwa na ukiburi lakini matendo ya Xiao ni kama yalimgusa na kujiuliza huyu ni binti yake kweli ambaye anafanya vitu vya kijinga kwa kutaka kushindana na mtu ambaye yupo juu ki uwezo.
Licha ya kujiuliza maswali hayo hakuweza kujizuia kujisikia vizuri kwa kile mtoto wake ambacho alikuwa akitakakufanya.
Hakuwa na uelewa ni wapi anaelekea tokea muda ambao aliamini ufunuo mkubwa aliokuwa nao ulikuwa sio juu ya huruma na aliamini mtu mwenye nguvu ndio anaeweza kuongoza dunia.
Kwake kinachojulikana kama ujamaa, urafiki na upendo si chochote bali mawazo potofu yasioendeshwa na akili na ndio chanzo cha udhaifu.
Kidonge kimoja tu cha daraja la juu kinaweza kumgeuza rafiki kuwa adui, uongozi unaweza kugeuza ndugu kuuana lakini mara baada ya kupanda juu zaidi kilevo kila kitu kilionekana kuwa si kitu mbele yake.
Alitafuta ufunuo bila kujali chochote anachokiona kama kizuizi na akapambana wazi na kwa siri kwa njia yoyote ile inayohitajika ili kuvunja vifungo vyote vya mafanikio.
Na ni katika wakati huo hatimae kile alichokuwa akikitafuta kilikuwa wazi.
Ghafla alihisi hali ya akili ya ajabu ambayo haijawahi kumtokea hapo awali ,maumivu yalioigusa roho yake yalioletwa na nguvu ya damu ya mnyama wa kishetani yalikuwa makali mno kiasi cha kushindwa kuvumilia
Miridi za mwili wake zilikuwa zikiuma kama vile alikuwa akichemshwa katika sufuria.
Katika hali hio ya maumivu hatimae mawazo mbalimbali yalianza kupita moja baada ya jingine ndani ya sekunde moja tu.
“Xiao ondoka nenda mbali…”Aliongea Anjiu katika sauti hafifu.
“Baba!?”
Xiao aligeuka na kumwangalia baba yake katika hali ya tahamaki na akajaribu kumpa baba yake mkono lakini aliishia kusukumiwa mbali.
“Nimesema ondoka”
Kutokana na kusukumwa na nguvu iliokuwa kubwa kiasi ilimfanya kwenda mbali lakini kutokana na hofu Xiao hakutaka kusogea mbele tena.
Hatimae Anjiu alisimama katika urefu wake tena na kumwangalia Roma kwa hali ya tabasamu la ajabu.
Roma palepale alihisi kuna kitu hakipo sawa ,Jini ambalo lipo mbele yake halikuonekana kama limepatwa na ukichaa kutokana na damu bali uwezo wake umeongezeka zaidi na zaidi ndani ya sekunde tu.
“Kumbe ndio ilivyo … hatimae nime elimika”
Tabasamu hafifu lilimtoka akionyesha hali ya kuridhika , tofauti na kumshambulia Roma alinyanyua kichwa chake juu na kunyooosha mikono yake yote angani kama vile mtu anaepokea baraka kutoka kwa Mungu au mtu aneonyesha ishara ya shukrani.
Mkondo wa nishati giza palepale ulianza kujikusanya katika mwili wake lakini haikumsababishia madhara kama ilivyokuwa ikitegemewa bali muda huo ilikuwa ni kama nguvu ya kijini.
Isitoshe damu ya mnyama wa kishetani ilitoka kwa jini wa kishetani afahamikae kwa jina la Taowu , ijapokuwa ni kiasi kidogo tu lakini ni cha thamani kutokana na uhalisi wake.
Muda huo ni kama sasa ile damu ambayo ilikuwa ndani ya mwili wake imeungana na mwili wake na kuwa sehemu moja ya kimwili.,
Unachopaswa kuelewa ni kwamba katika ulimwengu wa kiroho damu ina nguvu sana kuliko kitu chochote na ndio uhai wenyewe , hivyo ni sawa na kusema damu ina unganiko la nafsi ndio maana damu hio malengo yake ilikuwa ni kumfanya Anjiu kuchanganyikiwa kwa kuvamiwa na pepo kichaa.
Lakini sasa tofauti na mategemeo ni kwamba ile roho chafu ambayo ilikusudiwa kumuumiza hatimae imepatana na roho yake.
Roma sasa aliweza kuona nguvu ambayo ilikuwa ikimtoka Anjiu katika mwili wake ilikuwa ni kubwa sana kuliko mwanzo
Roma hakutaka kumpa nafasi kuendelea kupona na kutoboa na palepale alimshambulia Anjiu na ule moto mweusi
Lakini sasa Anjiu hakuonyesha kukwepa kabisa shambulizi lake na palepale alianza kumung’unya maneno kama anasali.
“Askari wa kiroho pepo wa ndani!”
Mara baada ya kuongea ile kauli Roma aliweza kuona Anjiu ni kama vile kivuli cheusi kinamtoka , Roma mara baada ya kuangalia kwa umakini aliona ni kivuli cha Jini Anjiu mwenyewe.
Ilikuwa ni kama vile amejigawa kati na kubadilika na kuwa jini katika umbo la roho.
“Boom!!!”
Dakika ileile ule moto wake ulivyokwenda kukutana na askari pepo ,shambulizi la Roma lilipotea palepale bila ya kuleta madhara.
“What the hell!!”
Roma alijikuta akitamka kauli hio mara baada ya kushangazwa na jambo lile lakini jini Anjiu hakuonyesha kabisa kushangaa.
“Miaka nane iliopita uwezo wangu uliweza kufika katika mwishonni mwa levo ya maji ya kiroho lakini nilishindwa kuingia katika Dhiki tisa za mapigo ya radi , sikuweza kwasababu mwili wangu haukuwa na uwezo wa kuhimili mapigo, ili kuzuia athari katika mwili wangu nilihamisha uwezo wangu wa ziada na kulipa nguvu pepo la ndani ili kuendelea kutafuta njia , baadae wakati nikiendelea kutengeneza Dhana nilikuja kutengeneza nafsi yangu ya pili inayofanana na mimi na kuipa jina la Askari wa ndani wa kipepo ambaye umemuona , hio ni Dhana yangu ya kijini , ijapokuwa ni ya daraja la juu ila kadri uwezo wangu unavyoongezeka itaweza kubadilika kutoka kuwa nguvu ya kipepo na kuwa nguvu ya nishati ya mbingu na ardhi”
Maneno yake hayakumshangaza Roma tu bali yalishangaza majini wote ambao walikuwa katika eneo hilo mara baada ya kuona mkuu wao alikuwa amefikia kiwango hicho cha uelewa .
Alichokifanya Anjiu ni kulipa nguvu pepo la ndani ya mwili wake na kisha akaligeuza kuwa Dhana na hapo ndipo alipotoa uwezo wake wa kijini kwenda katika hilo pepo.
Alifanya hivyo kutokana na kwamba mwili wake ulikuwa Dhaifu kuhimili mapigo tisa ya radi , hivyo ili kuepuka adhabu ya mbingu ndio akaamua kutumia njia hio ili kuendelea kutafuta suluhisho la kuimarisha mwili wake.
Sasa uelewa huo wa kugeuza pepo la ndani kama Dhana ni uwezo wa hali ya juu sana katika ulimwengu wa watu na majini ambao wanavuna nishati za mbingu na ardhi na ili kufikia hapo inamaana kwamba uwezo wako haupo tena katika levo ya maji ya kirho bali ni zaidi ya hapo.
Boom .. Boom.. Boom !!!”
Wakati kila mmoja akiwa katika hali ya mshangao anga lilifunikwa na wingu kubwa ambalo lilikuwa likizungukwa kwa kasi kubwa mno na kusababisha ngurumo za radi , ilikuwa ni kama vile ni ngurumo za wanyama wengi wakitoa sauti kwa pamoja.
SEHEMIU YA 724.
Radi ya mbingu hatimae inapiga tena , Roma ambaye ashawahi kupitia steji hio alikuwa na uelewa na tukio hilo.
“Haiwezekani kwanini ndio anaingia katika levo ya mapigo tisa ya radi wakati huo wakati yeye tayari ashapitia mapigo tisini na tisa lakini akawa na uwezo wa kumpa ushindani mkubwa?”
Ki ufupi ni kwamba Anjiu hakuwa amepitia mapigo ya radi bado licha ya kwamba uwezo wake ni wa juu , alikuwa katika levo ya kuiepuka Dhiki katika levo ya maji ya kiroho hivyo uwezo wake ulikuwa ni kama unalingana na Roma.
Hakuweza kupitia Dhiki kwasababu hakuwa na njia ya kuweza kuhimili mapigo ya radi hivyo kutengeneza kwake Dhana inayofanana na yeye ni kwamba angeruhusu yule askari wake wa kipepo kupokea mapigo kwa niaba yake na nguvu ya radi ile ingemuingia yeye.
Sasa Roma wazo ambalo alikuwa nalo ni kwamba kama alikuwa hajapitia mapigo ya radi na alikuwa na uwezo huo , inamaanisha kwamba kama atafanikiwa kupita inamaana atakuwa na uwezo mkubwa kuliko wa kwake.
Pengine kuna mambo mengi ambayo hakuwa akiyaelewa kuhusu nguvu za kijini na levo ya Dhiki ndio maana Anjiu alikuwa na nguvu kubwa kuliko yeye licha ya kwamba alikuwa amepitia mapigo ya radi tisini na tisa.
Ndani ya dakika moja tu wingu ambalo lilikuwa likizunguka lilitengeneza kitu kama vortex hivi na radi na mawaingu yalianza kupiga shoti za radi huku kasi ya mawingu kuzunguka ikiongezeka maradufu.
Majjini wote ambao walikwua katika eneo hilo walikuwa katika hali ya mshangao kwani ndio wanaanza kuona kwa mara ya kwanza Dhiki ya radi tisa.
Anjiu ambaye ndio alichokoza anga na kutengeneza radi hio hakutaka kujifcha tena na alisimama katika eneo lileile huku juu yake mawingu yakiendelea kutengeneza msuguano.
Majengo hayo ya madini ya Jade kama radi itapiga hapo ilimaanisha kwamba yangegeuzwa na kuwa majivu lakini hakutaka kujali tena kuhusu majengo ambayo yapo chini yake.
“Baada ya mapigo ya radi kunishukia ndio nafasi pekee ya kuweza kunishinda , chukulia kama hutofanya shambulzi wakati huo na kuendelea kuangalia na nikafanikiwa kupita hutokuwa na uwezo tena wa kunishinda”Aliongea huku akiwa amefumba macho yake katika utulivu kabisa akisubiria mapigo ya radi.
Roma alijihisi ni kama vile anadhalilishwa na kauli yake na kujiambia ana uhakika gani atashindwa hata kama akipitia hio dhiki au ni kwamba haogopi kuuliwa na nguvu hio ya radi.
Ijapokuwa alikuwa na Dhana yake ya askari wa kipepo ilikuwa ngumu kuhimili mapigo hayo na ilimfanya Roma kuwa katika maswali.
Dakika hio Roma alihisi kuongezeka kwa mchecheto wa chungu chake chini.
Ndio muda ambao Roma alianza kukumbuka wakati anapita katika mnara akitokea ulimwengu wa majini pepo ni chungu hicho hicho ambacho kilipitia mapigo tisini na tisa ya radi na kuigeuza ile radi kuwa nishati yake sasa alijiuliza vipi kama atakipatia nafasi ya kupitia mapigo tisa ya radi si inamaana kitakuwa na uwezo wa kusharabu nguvu hio ya radi na kumuongezea nguvu maradufu.
Roma wazo palepale lilimwingia na kujiambia au azuiemapigo hayo ya radi yasimfikie kwa kutumia chungu chake , alijiambia pia inaweza kumuwezesha kupata uzoefu utakaomsaidia akija kupitia mapigo mia tisa tisini na tisa ya radi.
“Nitamziuia”Aliongea
Roma mara baada ya kujua hio ni nafasi adhimu sana kutumia , hakutaka kuchelewa na alikiita chungu kutoka chini pamoja na Rufi.
Baada ya kumshikilia Rufi vizuri katika kiuno chake ili kumlinda kwa ukaribu hatimae alikisukumiza chungu chake kwenda juu zaidi angani ili kikapitie mapigo ya radi.
Anjiu na majini wengine walishangazwa na jambo hilo na kujuliza Roma anajaribbu kufanya nini.
“Unataka kuharibu mpango wangu sio?”Anjiu aliongea kama vile hakuwa ametegemea Roma kuchukua maamuzi hayo hivyo alikuwa akitegemea labda Roma alikuwa akipanga kumshambulia lakini alionekana kutaka kuzuia mapigo yale ya radi yasimfikie.
Anjiu alionekana kuwa na hasira mara baada ya kuona chungu kile kipo juu yake.
“Huwezi kufanikiwa, Askari wa kipepo nenda!!”Aliongea na palepale askari wake wa kipepo alimsogelea Roma kwa ajili ya kumshambulai.
“Yang’wi na moto wa Dhahabu!”
Sauti ilitoka katika lile pepo na palepale liligeuka na kuwa moto na kuanza kumfukuza Roma.
“Shit… hili pepo lake lina mbinu kama zake tu”Aliongea Roma huku aking’ata meno yake kwa hasira
“Kuwa makini mpenzi, kwasababu akili yake imegawanyika na nafsi yake,Anjiu anao uwezo wa kuliendesha na akili yake tu , hivyo kama utatumia moto wa samawati kulipiga hakutakuwa na mafanikio,utafanikiwa kuliweza kwa kutumia moto wa kiroho”Aliongea Rufi ambae alikuwa akijitahidi kutokuona hofu.
Ijapokuwa haikuwa vizuri kupambana akiwa na mwanamke pembeni yake lakini alishukuru kwmaba pepo hilo halikuwa na nguvu kama alivyokuwa jini Anjiu mwenyewe .
Ndio hivyo tu kanuni za anga hazikufanya kazi vizuri katika ulimwengu huo na kama angezitumia ingekuwa rahisi kulishinda.
Roma mara baada ya kuona Rufi alikuwa na pointi hakutaka kuzembea tena na palepale alitengeneza moto wa rangi nyeupe na wa zambarau na kwenda kulishambulia.
Muda uleule hatimae anga lilianza kuangaa mara baada ya awamu ya kwanza ya radi kupiga.
“Boom!!”
Radi ambayo ilikuwa kama mti wenye matawi iliweza kushuka chini katika ulimwengu huo wa kijini na kupiga kwa sauti ya kuumiza masikio.
Ijapokuwa pigo hilo halikuwa kali kama lile ambalo alishawahi kupokea lakini ilimpelekea Roma kuhisi kiwewe kutokana na maumivu.
Alijua kabisa licha ya kwamba alikuwa akielewa nguvu huo ya radi tisa lakini bado haikumaanisha kwamba anaweza kupokea mapigo yake kila anapotaka.
Dakika ambayo chungu kile kilifikiwa na ile radi ile roho ya mnyama ilikuwa ndani yake ilitoa ngurumo kubwa mno ambayo iliweza kusikika katika akili ya Roma.
Nusu ya radi hio ilimezwa na chungu cha maafa na palepale ilibadilishwa na kuwa nishati ya mbingu na ardhi na kusababisha kile chungu kutoa mng’ao kama vile kimetengenezwa kwa madini ya almasi.
Nguvu za Roma palepale zilianza kuongezeka kwa kasi kubwa mno mara baada ya nguvu ya nishati ile ya radi kumuingia.
Upande wa Jini Anjjiu alipokea kiasi kidogo tu cha ile radi na kama utajumlisha na uwezo wake basi alichopokea ni kidogo sana na hakina faida.
Akiwa katika hali ya kuchukia lile pepo lake lilianza kumshambulia Roma na moto wa randi ya zambarau lakini mashambulizi hayo kwa Roma hayakuwa kitu kabisa na aliweza kuyazuia.
Muda huo Roma hakutaka kumshambulia Anjiu kwani alijua kama atamuua basi na Adhabu hio ya Dhiki ingeacha mara moja na asingeweza kufaidika nayo.
Yaani kwasababu radi alieisababisha ni Anjiu basi kama angekufa na radi hio ingeacha na Roma asingeweza kunufaika , kwani alikuwa akitaka kutumia radi hio kujiongezea nguvu yaani tofauti na Anjiu kupokea mashambulizi ya radi yeye ndio alikuwa akiyapokea.
Dakika ileile mara baada ya wingu kuzunguka kwa kasi radi nyingine iliokuwa katika rangi ya Zambarau na bluu ilishuka, awamu hio ilikuwa pana mno na yenye nguvu kuliko ya mwanzo.
Kama awali mara baada ya kufikia chungu iliweza kumezwa kiasi na nyingi ilimshukia Anjiu.
Roho ya mnayama ilifurahia kwa mara ya pili na kujikusanyia nguvu kubwa zaidi na kuisafirisha kwenda kwa Roma na nusu kujinufaisa yeye , Roho yake ambayo ilikuwa imepunguzwa nguvu na Roma mwanzoni sasa ilionekana kuamka tena baada ya kurutubishwa na radi..
Roma aliweza kuhisi uwezo wake kuongezeka kwa asilimia tisa hivi , mwanzoni uwezo wake ulikuwa mdogo kiasi kufikia radi ya mapigo mengi lakini kwa nguvu yake iliovyongezeka aliona anakaribia.
Uelewa huo ulimfanya kuwa na furaha kwakuwa tu na Dhana ya chungu pamoja na mapigo ya radi hio hakuwa na haja ya kuwa na wasiwasi tena kwa uwezo wake kuongezeka taratibu taratibu.,
Ambacho majini walikuwa wakitumia miongo kufikia yeye alikuwa anakikamilisha ndani ya siku chache tu.
Lakini muda uleule jini Anjiu alianza kutoa kicheko cha juu ambacho kilikuwa kikiumiza masikio na kisha kumwangalia Roma kwa kejeli.
“Hahah.. Chaos!!, Roma Ramoni napaswa kukushukuru kwa kunisaidia kuizuia radi hii vinginevyo ningekuwa nusu mfu hata kama ningekuwakama wewe ambaye mwili wako umeimarishwa na mwanga wa kiuungu , kwangu kiasi hichi kidogo cha radi nilichokipata kinanitosha kabisa”
Roma palepale alishikwa na mshangao na hasira kwa wakati mmoja na kujua kumbe alikuwa akijifanyisha kukasirika ili tu yeye atumia chungu chake kumsaidia kupita dhiki ya mapigo ya radi hio.
Ni ngumu sana kwa majini kupita levo ya mapigo ya radi bila ya kuwa na Dhana, kitendo cha Roma kuwa na Dhana ambayo ina uwezo wa kuhimili mapigo ya radi kama hio ilikuwa ni fursa kwa Anjiu kuweza kuitumia.
Aliamua kumtega Roma kwa kujifanyisha amekasirika ili tu Roma atumie chungu chake kukinga radi ili yeye asiathirike kimwili.
Majini walichokuwa wakikitafuta katika mapigo ya radi sio kupigwa na radi yote bali ni kutumia radi kuweza kupanua uwezo wa wa kufikiria na hatimae kuufikia ufunuo katika mbingu za juu.
Unapaswa kuelewa nguvu za kijini hazipo katika mkusanyiko wa nguvu za kijini bali ni ile uwezo wa akili ya ufumbuzi inavyopanda viwango kwenda mbingu za juu zaidi na kadri ambavyo unapata ufumbuzi ndio namna ambavyo uwezo wako moja kwa moja unapanda na hicho ndio ambacho alikwua akilenga Anjiu , yaani wakati Roma akilenga kufyonza nishati ya radi upande wa Anjiu yeye alikuwa akilenga kufumbua fumbo.
Lakini swali lingine likaibuka katika kichwa cha Roma na kujiuliza yalikuwa ni mapigo mawili tu ya radi ambayo yameshuka kwanini afichue mpango wake mapema kabla ya awamu zote?.
Roma alijikuta akiwa kwenye tafakari kutaka kujua Anjiu alikuwa akifikiria nini lakini alikuwa akipoteza muda na bado alishindwa kujua ni kipi ambacho anafikiria.
“Hubby fuata moyo wako usifuate maneno yake ya upotofu”Aliongea Rufi mara baada ya kuona Roma anashindwa kuchukua maamuzi.
Lakini sasa Roma alishindwa hata kumsikiliza kabisa Rufi na kuendelea kuwa katika tafakari nzito na ni sekunde ileile awamu nyingine ya mapigo ya radi ilishuka na awamu hio chungu hakikuweza kuimeza yote kutokana na ukubwa wake na kiwango kikubwa kilimshukia Anjiu.
“Haha…nimefanikiwa!!”
Aliongea Anjiu mara baada ya kupona maumivu ya radi na katika hali ya kushangaza wimbi kubwa la nguvu za kijini lilimtoka na akawa ni kama vile amebadilika kabisa na kuwa mwingine.
Nguvu ya kijini ambayo ilikuwa imenzingira iliongezeka maradufu na kusababisha upepo mkali ndani ya hilo eneo na mchanga kuamka kutoka ardhini.
Majini ambao walikuwa wamesimama mbali kuangalia kile kinachoendelea waliishia kushikwa na mshangao mara baada ya kuhisi mkandamizio usiokuwa wa kawaida ukimtoka mkuu wao.
Zianji alijikuta aking’ata meno kwa hasira huku akimuonea wivu kaka yake kwa wivu na kujiambia ni kwa mara nyingine kaka yake anapanda levo mbele ya macho yake.
Roma aliemshikilia Rufi aliinua sura yake juu na kumwangalia Anjiu ambaye alikuwa amebadilika kabisa katika uwezo wake wa nguvu za kijini, kutokana na kusita sita hatimae ameweza kumfanya Anjiu kufaidika na uwepo wa Dhana yake na kupanda levo maradufu.
Licha ya kwamba Anjiu alikuwa amepitia mapigo machache tu ya radi uwezo wake uliongezeka na kuwa mkubwa mno na kulingana kikamilifu na uwezo wa Roma.
Yaani kwa lugha nyepesi ni kwamba Anjiu hakuwa na haja ya kupitia mapigo tisini na tisa ya radi ili kufikia levo za Roma bali alihitaji ufumbuzi wa nguvu ya radi ili kuweza kupanda levo.
Yaliwezekana yote hayo kutokana na maarifa mengi aliokuwa nayo juu ya nguvu za mbingu na ardhi kuliko Roma ambaye ndio ana miaka michache tu tokea anze kujifunza.
“Umenishindwa , Roma Ramoni wewe ni mtoto na hujui mambo mengi kuhusu nishati za mbingu na ardhi , wazo moja tu linaweza kuamua nani ni mshindi na nani amepoteza pambano kati ya watu wawili wenye nguvu sawa , uliweza kudanganyika na maneno yangu na imekupelekea kushindwa , mwanzoni ulikuwa na uwezo mkubwa kuliko mimi katika vitu vingi lakini sasa hivi uwezo wako hauna utofauti mkubwa na wangu na nguvu zangu za kijini ni kubwa kuliko zako hivyo huniwezi tena na nitakumaliza hapa hapa”
ITAENDELEA.
0687151346 WATSAPP ONLY
NaaaaamNILIMDHANIA KAHABA KUMBE BIKRA
MTUNZI: SINGANOJR
Mono no aware
SEHEMU YA 701.
Ni dakika chache tu mara baada ya mlinzi aliefahamika kwa jina la Quif kutoka ndani ya eneo hilo aliweza kurudi akiwa ametangulizana na mwanaume ambaye alionekana amechanganya rangi , alikuwa na rangi ya kiafrika kwa mbali na ya kiarabu na jambo hilo lilimshangaza Roma kidogo.
Upande wa Zomu na Zato walikuwa na shukrani sana juu ya Roma kwa kile ambacho ameamua kukifanya, maana hawakumsaidia kwa chochote lakini kaamua kupambana na jini ambaye yupo mwishoni mwa levo ya nafsi.
Katika maisha yao kwenye ulimwengu huo Roma alikuwa mtu adimu sana ambaye ameamua kuwasaidia bila mawaa.
Kwa jini ambalo lipo kwenye levo mwishoni mwa levo ya nafsi na jini ambalo lipo mwanzo mwa levo ya nafsi utofauti wao ni ile presha wanayotoa pamoja na ukali wa mapigo.
Mwanaume ambaye alifahamika kwa jina la Feilo alikuwa kweli katika levo ya nafsi na alionekana muda wowote anaweza kuvunja kwenda levo ya dhiki.
“Feilo tofauti na kutotumia siraha zako za kimaajabu usijizuie kwenye matumizi ya nguvu, tumia asilimia mia moja ya nguvu zako za kijini kumshambulia Xiao Cheni”Aliongea Mohi.
Yuile bwana alimwangalia Roma kwa macho ya mshangao kama vile ilikuwa jambo la ajabu sana kutumia nguvu zake zote kwa mtu ambaye yupo na uwezo wa chini.
Lakini kwasababu alikuwa ni jini mwenye uwezo ambaye yupo chini ya miliki ya Kekexil hakuwa na namna ya kukataa maagizo ya mkuu wake
“Kwasababu Mkubwa namba tatu amenipa ruhusa sitokuwa na huruma , kama ukiona umeshindwa usijilazimishe kuvumilia”Aliongea Feilo akimwangalia Roma usoni.
Muda uleule wote walisongea kwenye uwanja wa mapambano Roma akiwa upande wa kulia na Feilo akiwa upande wa mashariki na upande kushoto kwao ndio jukwaa lilipo Mohi na ndugu zake wakiwa wanaangalia kinachokwenda kutokea.
Feilo paleplae hakujizuia na mwili wake ulizingirwa na nguvu za kijini na alimsogelea Roma kwa nguvu na kumpiga ngumi.
Mapambano ya aina hio mara nyingi ni adimu sana kuyaona , kwani mapambano ya majini yanakuwa ni yale ya kutumia kila Dhana walizokuwa nazo , lakini Feilo hapo hakuwa akituia siraha zake za maajabu zaidi ya kutumia mwili wake kupambana..
Kwa jinsi ambavyo Feilo alikuwa akishambulia kwa haraka haraka Roma alijua lazima atakuwa na mafunzo ya Kishaolini , kwani alikuwa akitumia mbinu maarufu ya kimapambano ya Shaolini Luohan na jambo hili lilimshangza na kujiuliza au Feilo sio jini.
Ngumi za Feilo zilikuwa ni kama nyundo na kama sio kwa Roma kuwa na mbinu za kuzuia mgongano usiwe mkubwa basi pengine kwa mtu wa kawaida ingekuwa kifo palepale maana aliunganisha nguvu zake za kijini na ngumi yake.
Roma hakutaka kutumia mfumo rasmi wa kimapambano kama Kung Fu hivyo alichanganya changanya na yote hio ni kumzuia Feilo asijue ni mbinu gani atatumia kumshambulia.
Feilo alirusha teke kupangua ngumi ya Roma na palepale alijizungusha kama ufito na kumpiga Roma kifuani na teke kwa nguvu sana na kumpelekea Roma kurushwa hewani kama mpira.
Ilikuwa ni kama vile amepatwa na presha ya bomu kutokana na namna alivyorushwa na teke la Feilo.
“Teke moja tu la kushitukiza tayari amefyatuka namna ile , huyu ni takataka”Aliongea jini Manyani lakini dakika ileile alijikuta akipatwa na mshangao huku akimwangalia Roma.
“Inawezekana vipi hii?”Aliongea akiwa na mshangao mkubwa
Kitendo cha Roma kupigwa teke na kupaishwa hewani kwa kuchora Parabola kabla hata hajatua chini Roma alijizungusha kistadi kabisa na kutua chini na miguu yake yote na sehemu ambayo amepigwa na Feilo hapakuwa na ishara yoyote ya kuumia.
Mohi na Lilsi wote walionyesha hali ya mshangao , wote walitegemea pigo lile lingemharibu kabisa Roma lakini ajabu alionekana hajaumia kabisa na walijikuta wakishangaa , walikuwa ni majini ambao wameishi muda mrefu lakini hawajawahi kuona mtu ambaye ana mwili mgumu kama Roma.
“Inaonekana angalau atakuwa na faida”Aliongea jini Mohi huku akiangalia kwa umakini kiachokwenda kutokea.
Muda huo Feilo na yeye alishaona hali ambayo sio ya kawaida kutoka kwa Roma lakini kwa wakati huo hakutaka kujali , alichokuwa akiwaza ni kushinda kwani hakutaka kuabika kwa kupoteza pambano kwa binadamu ambaye ndio kwanza ameingia katika levo ya Nafsi hivyo palepale alimsogelea Roma na uanza kumshambulia kwa kasi.
Upande wa Roma bado hakuona njia nzuri ya kumdhibiti Feilo bila ya kushitukiwa , hivyo aliishia kukubali kupokea mapigo kutoka kwake , mbinu ya kishaolini ya Luohan huwa faida yake ni kwamba pigo lake moja linalenga kulegeza mwili hivyo Roma alipokea mapigo mengi makubwa ya tumbo na kifuani,
Lakini hata hivyo Roma licha ya kupigika hakutema damu wala kutapika wala hakuna mfupa au viungio vya mifupa ambavyo vilipatwa na shida.
Mpaka mwishoni Feilo alikuwa ametumia mapigo ishirini na tatu kjaribu kumshambulia Roma lakini hakukuwa na dalili ya kumshinda na mapigo saba pekee ndio ambayo yalikuwa yamebaki..
Kwa dili ambalo Roma aliingia na mkuu namba tatu wa majini ni kuhimili kupigwa mapigo therathini lakini mpaka hapo alikuwa amepokea mapigo ishirini na tatu tayari hivyo yalikuwa yamebakia mapigo saba tu.
Roma nguo zake zilikuwa zishaharibika kabisa lakini hakuonekana kuwa na jeraha la aina yoyote na alisimama kwenye uwanja akiwa na tabasamu akisubiria kupigwa mapigo ya mwisho.
“Mbinu zako za kuvumilia mapigo ni nzuri mno lakini unapaswa kuwa makini kwani awamu hii mapigo ninayokwenda kukushambulia nayo hayatakuwa butu”Aliongea Feilo
Na palepale Roma aliweza kumuona Feilo uso wake kubadilika na kuwa na sura ya Simba huku akiongea maneno ya ajabu kama vile mtu anaenena kwa lugha.
“Om!woll!oh!bahi bahi!mi Hum!!!”
Roma palepale alijua nini ambacho anafanya Feilo , alikuwa akimtupia laana , Roma alijua ni laana kwani alishawahi kupambana na Monk na kuongea kauli hio hio.
“Sijategemea Feilo kuwa na huo ujuzi , kwa ninavyojua huo ni uchawi wa kishaolini wa ngurumo ya Simba”Aliongea Jini Mohi akimwambia Lilsi.
“Inawezekana , hii nguvu ya uchawi inaonekana kuwa na nguvu,ongezeko la nguvu ya kijini ni kama wimbi la bahari ambalo halina mwisho , kama Feilo ataingia levo ya kuipita dhiki , itakuwa ni laana yenye nguvu mno kuwahi kuwepo katika ulimwengu wetu”Aliongea Lilsi.
Upande wa Roma hakujali maoni yao kabisa , kwake hapo anaigiza na kama akitaka kumuua Feilo ni kwa kuchezesha kidole tu lakini kwa muda huo alikuwa akijifanyisha mdhaifu mbele ya Feilo ili malengo yake kutimia.
Upande wa Feilo alikuwa siriasi mno na mara baada ya kubwabwaja kwa muda mrefu nguvu yake ya kijini iliongezeka maradufu na palepale aliachama kwa nguvu na kuanza kunguruma na sauti iliomtoka hapo ni kama vile ni Simba wa Nyika.
Lakini ukubwa wa sauti hio ulikuwa ni mkubwa mno na ilimfanya kuona hio kweli ni nguvu ya kichawi kwani ni kama sauti inatokea angani na sio kwenye mdomo wa Feilo.
Haikuwa sauti tu bali iliambatana na wimbi la upepo mkali mno na ilifanya hata waliokuwa wakiangalia kutumia nguvu za kijini kuhimili wimbi la upepo.
Upande wa Roma alijifanyisha hata yeye alikuwa akifurukuta kutokana na nguvu ya upepo ule na alijikuta akielea bila kupenda na alihisi maumivu makali kutokana na kwamba hakutumia nguvu ya kijini kujilinda kwa kuogopa kugundulika.
Feilo aliendelea kunguruma kama simba kwa zaidi ya dakika tatu huku akimpa tabu Roma kutokana na mwili wake kunyongwa nyongwa na wimbi la nguvu za kijini , mpaka anakuja kumaliza Roma alidondoka chini akiwa hoi na damu zilimtoka kwenye mdomo wake huku akijitahidi kusimama akitetemeka.
Mchezo huo ulipaswa kumalizka kwa namna hio , Roma alijiambia isingekuwa uhalisia kama angeshinda bila hata ya kutoka damu.
Licha ya Roma kutoka damu kitendo cha kuweza kuhimili nguvu ya kichawi ya ngurumo ya Simba iliwashangaza kila mmoja na kukubali utimamu wake wa kimwili.
“Hii inawezekana vipi…”Feilo alijikuta akishangaa mno na alijikuta akikosa ile hali ya kujiamini aliokuwa nayo na alionekana kabisa amekata tamaa ya kuendelea kumshambulia Roma.
Jini mkuu namba tatu na wengine wote walikuwa kwenye mshangao na furaha kwa wakati mmoja , ilikuwa ni kama wameokota Hazina na wote waliona Roma angekuwa na msaada mkubwa mbeleni kama wangemfua vizuri kimapambano.
Zato na Zomu wote walikuwa na furaha , ilionekana Roma kweli ni kama alivyosema anaweza kuhimili mapigo therathini na mpaka hapo waliamini wanaweza sasa kupata vidonge kama walivyoahidiwa.
“Mkuu namba tatu , siwezi kuendelea zaidi , hata kama naweza kumalizia mapigo yangu matatu yaliobakia lakini siwezi kumshinda Xiao Cheni”Aliongea Feilo.
Upande wa Roma alimwangalia Feilo na kujiambia huyu bwana inaonekana ni mtu mwenye busara mno , mwanzoni alijiambia anapaswa kuwa makini lakini bwana huyo aliamua kuishia katikati pasipo kumalizia mapigo , kama angeendelea Roma alikuwa na hofu angetumia uwezo wake wa kijini wa zaidi ya levo ya nafsi kujilinda na ingemfanya kugundulika.
“Feilo wewe ni bindamu wa kwanza wa kizazi cha ujana uliefanikisha kuingia katika levo ya nafsi mapema , hakika upo vizuri nje na nilivyofkiria , umefanya kazi nzuri na nitatuma mtu kukuletea kidonge kingine kwa ajili ya kukusaidia”Aliongea Mohi na palepale Roma sasa alielewa hisia zake zilikuwa sawa Feloi hakuwa jamii ya kijini bali alikuwa ni binadamu aliengia ujinini , Roma alijulza Feilo ana stori gani, ila kwa muda huo hakuweza kupata majibu.
Upande wa Feloi mara baada ya kuambiwa angepatiwa kidonge cha kijini alijikuta akiwa na furaha , vidonge ni kitu cha thamni kubwa na watu waliokuwa wakipewa mara nyingi ni wanafamilia.
“Asante sana Master , nitajitahidi kwa uwezo wangu wote na kungia kwenye levo ya Dhiki ndani ya muda mfupi”Aliongea na Mohi alimpa ishara ya kuridhika na jibu lake.
“Xiao Cheni umefanya vizuri pia , miliki yetu ya Kekexil inajali vipaji bila ya kujali wewe ni binadamu au Jini , ninamuagiza sasa hivi mkuu wa Chemba, Mkuu Ganyo kukuandalia nafasi ya kuishi na kuendelea kujifunza na utapewa vidonge vitatu vya Poya kwa ajili ya kukusaidia”
“Asante sana Mkuu namba tatu , lakini vipi kuhusu Zomu na Zato kupata vidonge?”
“Vidonge vya daraja la wingu bado vipo katika utengenezaji na itachukua kama mwezi mpaka kukamilika”Aliongea na kuwafanya Zato na Zomu kunyongea, pengine waliona Mohi anaenda kinyume na ahadi yake.
“Mnadhani baba anawadanganya?, ijapokuwa ni kweli vidonge vya wingu vina thamani kubwa lakini hatuwezi kuwa na uchoyo navyo”Aliuliza yule jini ambaye alikuwa amevalia suti na buti
“Zilha yupo sahihi , mimi Mohi mkuu namba tatu wa ukoo siwezi kwenda kinyume na ahadi yangu”
“Mkuu namba tatu usituelewe vibaya , tupo tayari kusubiri”Aliongea Zomu na kumfanya Zilha macho yake kuonyesha furaha.
“Zomu na Zato mnaonaje mkifanya hivi , kwasababu itachukua mwezi mpaka vidonge kukamilika , mtapatiwa sehemu ya kuishi hapa makao makuu pamoja na familia yetu”
“Huo utakuwa ni usumbuvu kwa familia”
“Nimeongea hivyo ili kuwapa fursa , ili kuweza kuvuna nishati ya mbingu na ardhi kwa haraka mnapaswa pia kuwa vizuri katika mapambano ya kutumia siraha , Master Shagoni muda si mrefu atafika hapa kwa ajili ya kufundisha namna ya kutumia siraha kwa majini ambao watatuwailisha , je nyie hamtaki pia kujifunza kutoka kwa Master Shagoni?”
Zomu na Zato walijikuta wakijawa na furaha mara baada ya kusikia kauli hio kutoka kwa Zilha , kama wangepata mafunzo kutoka kwa Master Shagoni ingekuwa ni fursa kwao kwani ndani ya miliki hio Master Shagoni aliaminika kwa kuwa na mafunzo ya juu sana ambayo husaidia majini wengi katika kupanda levo.
Upande wa Lilsi na Manyani walimwangalia Zilha kwa macho yasiokuwa ya kawaida , lakini hata hivyo hawakumzuia kwa kile ambacho ameongea na anapanga.
Baada ya kila kitu kumalizika hatimae Roma alipokelewa rasmi na kwenda kutafutiwa eneo la kuishi na sehemu ambayo pia angetumia kwa ajili ya kujifunzia mafunzo ya kijini.
Hakuna aliekuwa akijua yupo hapo kwa misheni maalumu ya kumtafuta mpenzi wake Rufi na hakuna aliemjua kutokana na kwamba alikuwa akitumia sura ambayo ni feki.
Eneo hilo lilikuwa ni kubwa mno na kulikuwa na familia kadhaa za majini lakini Roma mazingira haya aliyaona kidogo yalikuwa na utofauti sana na ulimwengu wa majini pepo.
Majini hao wote walionekana kama binadamu lakini katika kila jini ambalo ameona hakubahatika kuona jini mdogo yaani mtoto wala jini ambalo lina umri kuanzia miaka mitano kushuka chini , asilimia kubwa ya majini ambao ameona wanajifunza mbinu za anga wengi wao wapo na umri wa miaka kumi hivi kuendelea alijikuta akiwa na maswali mengi watoto wako wapi au ndio kwamba majini hawazai.
Sehemu ambayo Roma alionyeshwa pa kuishi ilikuwa ni karibu na sehemu ambayo Zato na Zomu wamepatiwa pia kukaa kwa muda hivyo ilikuwa rahisi kwa Roma kuongea neo.
Muda huo Roma aliamua kuwapa vidonge vya daraja la kati ambavyo vimetengenezwa kwa moto wa njano ambavyo amepewa na Mohi kama zawadi , Zato na Zomu walikataa vidonge vile lakini Roma aliwalazimisha na kuwaambia wasipopokea itamaanisha sio marafiki na hapo ndio walipokea.
Majini hawakupenda kuishi na deni ndio maana walisita kupokea lakini kwasabau Roma aliwapa kama ishara ya urafiiki wao walipokea.
Kitendo kile cha kuwapatia vidonge kilimfanya Zato kumwangalia Roma kwa macho ya kimahaba mno na kumfanya hata Roma mwenyewe kushangaa.
Asilimia kubwa ya majini wa kike katika ulimwengu huo wanaguswa sana na vitendo vya upendo , ukiwaonyesha ukarimu kidogo tu basi ndio tiketi ya kukupenda tena haswa ambaye anaonyesha huo ukarimu awe ni binadamu mwenye uwezo wa kijini.
Ukweli ni kwamba wanapenda pia kuzaa na binadamu kuliko na majini wenzao kwasababu wanapata nafasi ya kuwapakata watoto wao, lakini kisheria majini wa kike hawakuruhusiwa kutembea na binadamu labda kwa misheni maalumu ya kikoo.
Roma aliwapa vidonge hivyo kwa ajili ya kutaka kuwauliza maswali na sio vinginevyo na baada ya kukaa nao na kuongea alikuja kugundua vitu vingi sana lakini katika maelezo yao hakuweza kupata taarifa yoyote inayohusiana na Rufi.
Roma alijiambia ni muda sasa wa kuanza kumtafuta ndani ya makazi hayo lakini alijiuliza ni kwa namna gani ambayo anaweza kutembea bila kushitukiwa
Kingine ambacho kilimpa maswali ni kwamba hakuweza kukutana na majini ambao Rufi alisema wanacheo cha Super Master katika ulimwengu huo na kutokuwaona kwao kulimfanya kupatwa na wasiwasi.
Wakati Roma akiwa amekaa peke yake akiwaza cha kufanya hatimae Feilo bwana aliepigana nae alikuja alipo.
SEHEMU YA 702.
“Bro vipi mazingira , umeridhika na hapa unapoishi?”Aliuliza Feilo akiwa na tabasamu usoni
Roma kwa kumwangalia tu huyo bwana alijiua tayari alishapotezea yale ambayo yametokea na kutoa tabasamu la kirafiki.
“Bwana Feilo , kuna kitu unataka nikusaidie?”
“Hapana, ni kwamba nimekuja kukupa taarifa kwamba kila jini au biadamu anaekaribishwa katika miliki ya Kekexil anapata fursa ya kuingia kwenye Jumba jeupe la fahari ya milki kwa mwaka mara moja na kuchagua mbinu mbalimbali za kijini ambazo unataka kujifunza , huu mwaka ni mara yangu ya tatu kuingia na ndio najiandaa kwenda kuchangua mbinu nyingine ya kujifunza, naamini Bro Cheni na wewe utapenda kwenda ndio maana nimekuja”
Roma mara baada ya kuskia kauli hio palepale alipatwa na wazo , alikuwa na wazo la kuingia kwenye hili Jumba Jeupe mara baada ya kuambiwa na Zomu kwamba jengo hilo ukiachana na kuhifadhia vitabu na vidonge lakini pia kuna gereza la wafungwa, Sasa Roma alijiuliza kama Rufi ameletwa kwenye ukoo huo si inamaanisha atakuwa ndani ya hilo jengo.
“Asante sana Bro Feilo, hata mimi pia napenda kwenda”Aliongea Roma na kisha akasimama na kuongozana nae kuelekea huko.
“Bro mbinu yako ya mafunzo inashangaza sana , je unaweza kunishirikisha na mimi nijifunze?”Aliuliza.
“Unaonekana kuvutiwa na mbinu yangu sio?”
“Kuna jambo ambalo hulijui kuhuu mimi bro , ukweli ni kwamba kabla ya kuja huku nilikuwa mwanajeshi Komandoo kutoka jeshi la Vietnam , baada ya kukutana na Master na kunileta huku aliniambia kwamba sitokuwa na uwezo wa kutosha kupanda levo kwasababu mwili wangu ni mchafu, lakini sikutaka kukatishwa tamaa na maneno yake na kwanzia hapo nilijifua kwenye mafunzo na kila kilichokuwa mbele yangu nilijifunza na hatimae nimefikia hatua hii ya leo lakini bado nina shauku na mbinu nyingi”
“Ukweli ni kwamba nina uwezo ambao sio wa kwaida bila hata ya kuwa na nguvu za kijini , na sijui hata huu mwili imekuwaje nikawa nao”Aliongea Roma.
Alikuwa akidanganya hakuwa tayari kumwambia kwamba alikuwa amemulikwa na mwanga wa kiuungu.
Walitembea wakiongea na kupita kwenye uwanja mkubwa ambao kuna watu wengi waliokuwa wakijifunza mbinu za kijini na shauku ya Roma kutaka kujua kwanini haoni watoto ilimvaa palepale.
“Feilo kwanini kwenye huu ulimwengu sioni majini watoto wadogo?”Aliuliza Roma.
“Bro inaonekana bado hujajua mambo mengi , hata mimi nilishangaa hivyo hivyo wakati naanza kuja , majini wao uzao wao ni tofauti na binadamu , wao wanazaa roho kwanza kabla ya mwili”
“Unamaanisha nini wanazaa roho kwanza kabla ya mwili?”
“Ipo hivi bro majini wanabeba ujauzito kama kawaida lakini kinachotokea ni kwamba mtoto anaezaliwa anakuwa hana nguvu zozote za kijjini hivyo moja kwa moja anakuwa kama roho , yaani kama unavyoona pepo lilivyo ndio wanavyozaliwa , kwa maneno marahisi wanakuwa ni majini bila miili ya kibinadamu”Aliongea na kumfanya Roma kushangaa na kumwambia aendelee kumwelezea.
Kwa maelezo yake ni kwamba majini wakishajifungua watoto wao wanakuwa ni majini kamili , yaani majini ambao hawana miili ya kibinadamu na wanakuwa kama roho , sasa ikishatokea mama wa kijini amejifungua mtoto huchukuliwa na kupelekwa sehemu iliopewa jina kama Palaoni, hio ni sehemu ambayo ni kama hospitali ya majini vichanga na kazi yake kubwa huko Palaoni ni hutunza majini wachanga ambao hawana miili mpaka pale watakapopata miili yao ndio hutolewa na kwenda kuungana na familia.
Feilo anasema inaweza kuchukua mwaka mmoja mpaka miaka kumi jini kutoka Palao baada ya kupata miili na hili hutokea kutokana na kufundishwa namna ya kuvuna nishati za mbinu na ardhi na kadri jini linavyokuwa na uwezo wa kunyonya nishati kwa haraka ndio ambavyo linapanda levo kwa haraka na kufanikiwa kupata mwili na mara nyingi miili yao wanaipata ikiwa ni mikubwa kabisa kama binadamu wa miaka kumi na tano na kuendelea.
“Kwahio ikitokea kama jini halijapata mwili inakuwaje?”
“Mara nyingi hatua ya kwanza jini kupata mwili ni kupitia hatua ya kuishinda laana ya kipepo ndani yake na ndio hufanikiwa kupanda levo na kupata miili yao , lakini kama ikitokea jini halijaweza kufanikiwa kupata miili ya kibinadamu kwa kutokushinda Laana hugeuzwa nyoka au kiumbe chochote na kisha hupelekwa kwenye mnara na kusafirishwa kwenye ulimwengu mwingine”Aliongea na kumfanya Roma kushangazwa na kauli ile
“Unamaanisha ulimwengu wa majini pepo?”
“Bro ushawahi kusikia huo ulimwengu?”
“Ndio nishawahi kusiia sikia kuhusu habari zake”
“Mimi sina habari za kutosha lakini inasemekeana huko pia baada ya majini kujifunza namna ya kulipa pepo nguvu wanaweza kufanikiwa kupata miili ya kibinadamu”Aliongea na kumfanya Roma kuelewa sasa inavyokuwa.
Ilionekana na ulimwengu huo ulikuwa na mnara vilevile wa kuelekea ulimwengu wa majini pepo , lakini aliona inaleta maana maana Roma alikumbuka Zimo alimwambia kabisa kuna watu mbalimbali wanaofka katika uliwmengu huo kwa njia mbalimbali.
“Ikitokea roho ikigoma kupatiwa mwili wowote hata wa mnayama nini kinatokea?”
‘”Bro hapo sijajua lakini nilichoweza kusikia ni kwamba kuna majini ambao wanabakia bila miili maisha yao yote , wanakuwa kama roho na hawana uwezo wa kujionyesha kwa binadamu bali wanao uwezo wa kumwingia binadamu na kumtawala, lakni mara nyingi inatokea mara baada ya jini huyo kutoroka Palao”Aliongea na hapo Roma alikuwa sasa ameelewa kitu muhimu sana.
Pengine wale wanaomiliki majini ndio hawa ambao walikosa miili na kutoroka na kwenda kumiliki nafsi za binadamu au kumilikiwa na binadamu.
“Inaonekana binadamu tumependelewa muonekano ambao unapendwa na kila kiumbe”Aliongea Roma.
“Upo sahihi lakini licha ya hivyo majini wanaamini binadamu bila nguvu za kijini atakuwa ni dhaifu tu, lakini wanapenda sana kuonekana kama binadamu , kwani kuwa na mwili wa kibinadamu inamaanisha kuishinda laana waliopewa na Mungu”
“Unataka kusema majini nao wanaamini uwepo wa Mungu…?.”Aliuliza lakini palepale Feilo alishindwa kumjibu kwani ndio walikuwa wapo nje ya geti.
Ukweli kuna mambo mengi sana Roma alijifunza na maneno ya Feilo yalikuwa sahihi , katika majini wote ambao amepishana nao wote wapo levo ya nafsi , aidha mwanzoni mwa levo ya nafsi au mwishoni mwa levo ya nafsi hakuona jini ambalo lipo kwenye levo ya mzunguko kamili wala nusu mzunguko , pengine aliamini labda hao ambao wapo katika nusu mzunguko na mzunguko kamili ndio ambao wapo huko Palao wanalelewa mpaka watakapopata miili na kurudi kwenye familia zao.
Roma pia aliweza kuona majini wengi ambao wamepita Dhiki na ambao pia wameiepuka dhiki na kuweza kufanya maajabu ya juu kabisa.
Ilionekana Dhana ndio ambazo ziliwafanya kuwa na uwezo wa kuipita dhiki lakini kitu ambacho pia Roma aliona ni kwamba asilimia kubwa ya wengi ambao wameipita dhiki nguvu yao ilikuwa ndogo mno na alijua pengine wamepitia mapigo machache ya radi maana alishawahi kusikia majini wana Dhana ambazo huwasaidia kuepuka radi awamu zote.
Lakini hata hao ambao wamepitia pigo moja moja la radi au mawili walikuwa na uwezo ambao sio wa kawaida na Roma alijiambia kwa nguvu yao kama watakusanyika kama mia hivi na kumshambulia kwa wakati mmoja atakachokifanya ni kukimbia tu maana hakuna namna.
Au vinginevyo apitie tena mapigo mia tisa tisini na tisa ya radi nyeupe ndio ambapo angekuwa na uwezo wa kupambana na makundi makubwa ya majini waliovuka Dhiki.
Kilichomfanya Roma na Fileo kutoendelea kuongea ni mara baada ya kufika getini , kulikuwa na geti ambalo lilijengwa kwa muonekano ambao sio wa kawaida , chuma chake cha rangi nyeusi kilionekana kuwa kizito mno kwa kuangalia tu kwa nje , halikuwa geti kama ya binadamu wanayojenga.
Sasa katika geti hilo la kuingilia kulikuwa na Ajuza alievalia gauni la hariri rangi ya gray, alikuwa ni mzee sana kutokana na mikunjo mingi katika uso wake na alikuwa amefumba macho.
Ilionekana alikuwa akilinda hilo geti kwa muda mrefu sana hila kusogea hata hatua kwani mavazi yake yalikuwa na vumbi jingi mno, yaani alionekana kama vile ni Ajuza lakini pia kwa namna abavyo Roma alimuona ni kama vile ni sanamu alikuwa amekaa bila kusogea na ilionekana alikaa hapo bila kuondoka kwa muda mrefu sana pengine mwaka.
“Mimi Feilo na Xiao Cheni tunaomba kwako Bibi kufungua mlango wa geti”Aliongea Feilo kwa sauti.
Roma ambaye alikuwa pembeni yake mwanzoni hakutaka sana kujali muonekano wa huyo jini Ajuza lakini baada ya kumchunguza kwa umakini aliwez kuona kitu ambacho hakipo sawa.
Roma hakuweza kuona yule bibi yupo katika levo gani ya nguvu za kijini, kumbuka alikuwa na mwili wa kibinadamu hivyo alipaswa kuwa na nguvu ya kijini lakini Roma alishindwa kuona alikuwa levo ipi.
Jawabu pekee ambalo Roma alifikiria ni kwamba pengine alishindwa kuona uwezo wake kutokana na levo yake kuwa kubwa mno , kwani kadri jini linavyopanda levo ndio uwezo wake unavyozidi kujificha ndani kabisa.
Roma palepale akili yake ilicheza , alijiuliza au hawa ndio Masters waliojificha ambao Rufi alizungumzia kwamba walikuwa levo za juu kabisa katika kuipita dhiki.
Roma hakutaka kujaribu hata kuonyesha mshangao na kushitukiwa maana hakujua hata muda huo kama tayari ashagundulika ameficha uwezo wake na sura yake au Lah, ukweli huyo ajuza alimtia Roma wasiwasi.
Kwa maelezo ya Fileo eneo hilo la ghorofa ndio sehemu ya thamani zaidi katika ulimwengu hio , hivyo ilileta maana jini mwenye nguvu kubwa kuwa mlinzi.
Yule bibi hakujihangaisha hata kufumbua macho yake na kuwaangalia na palepale nguvu ya kijini ilimtoka na kwenda kuvamia lile geti la chuma kiguumu sana na palepale kama vile ni maporomoko ya mawe geti lile lilifunguka taratibu na kuacha uwazi.
“Asante sana bibi”
Aliongea Feilo kwa shauku kubwa na kumpa ishara Roma waingie ndani.
Dakika hio hio mara baada ya kuingia waliweza kukutana na korido ndefu mbele yao ambayo pembeni yake kulikuwa kumesimikwa mawe makubwa mno ya rangi nyeupe.
Jumba hilo tofauti na geti pekee kila kitu kilionekana kuwa rangi nyeupe tupu.
“Bro yule bibi ndio nani?”Aliuliza Roma na Feilo hakuelewa kwanini Roma kauliza swali hilo na aliishia kujikuna kichwa.
“Sijui sana kuhusu yeye lakini jina lake halisi ni Tigola ambaye ni sehemu ya familia ya Kekexil ambaye anahusika na ulinzi wa hili jengo ,kila mtu anamwita Bibi tu , sio mimi tu ambaye simjui lakini pia wakubwa wote ambao wapo hapa kwa miongo mingi hawajui chochote kuhusu yeye na haijulikani kama ashawahi kutoka ile sehemu aliokaa au lah lakini uje usiku au mchana utamkuta pale nje ya geti akilinda, inasemekeana kwamba nguvu zake za kijini ni kubwa mno lakini ni makisio tu kwani haijawahi tokea akapigana na mtu au jini yoyote yule”aliongea
Roma alijiambia huenda ni kama alivohisia , inaonekana huyo bibi yupo levo ya kudhibiti maji ndio maana hakuna ambaye ameweza kujua ni levo ipi amefikia.
Kwa alichosema Rufi ni kwamba wapo Master wakubwa katika ulimwegu huo wa kijini ambao kazi yao kubwa ni kuhakikisha usalama wa ulimwengu huo lakini hakna ambaye alishawahi kuwaona hao Master kwa macho zaidi ya kusikia habari zao tu.
Kwa kifupi hata majini wenyewe wa kizazi cha kati hawajui kama wapo au hawapo.
“Xiao Cheni unaweza usijue hili , ila hili jengo lilijengwa zamani sana na falme ya kijini iliofahamika kama Falme ya majini wa kijani , asili ya Kekexil ni miti na mimea ndio maana unaona hata nyumba zao nyingi zimejengwa kwa kutumia miti, kila mwanafamilia katika jumba la kifalme hupata nafasi ya kujifunza mbinu ya kijini ambayo hufahamika kwa jina la Aoki , hii mbinu ni siri yao na wanajifunza wao tu na ndio namna ambavyo wanalinda nguvu yao na ukuu wao ndani ya miliki , hili jengo lote lina floor mia moja na nane kwenda juu na kila floor ina kazi yake,mbiu ya Aoki pekee ndio haihifadhiwi ndani ya hili jengo , juu kabisa katika floor za mwisho mwisho ni sehem ya kutengenezea vidonge na huko dio Master wenye nguvu ndio wanapoishi na floor ya mwisho kabisa ndio sehemu ambapo kuna gereza la kuwafungia majini”Aliongea na kumfanya Roma kushanga.
“Unafahamu kila mfungwa ambaye yupo katika hilo gereza”
“Sijui na sijawahi kufika pia , ninachojua ni kwamba wafungwa wao ni wale ambao wanaenda kinyume na miliki ya Kekexil , wengine ni wasaliti na wengine wamefanya makosa kulingana na sheria , mara nyingi kama wana nguvu za kijini hawawekwi gerezani zaidi ya kuuliwa kabisa au kutupiwa mnarani lakini baadhi yao makosa yao ni madogo hivyo wanawekwa kizuizini kutumikia adhabu, mara ya mwisho kuona mfungwa anaingizwa ni kipindi cha vita ya kijini kati ya miliki tatu, sisi wa levo za chini tunaishia maktaba tu, upande wa juu kabisa huko wanaoruhusiwa kuingia ni familia ya Wakuu wa milki na kuna ulinzi mkali mno”
Roma alijiuliza atawezaje kwenda huko juu , hisia zake zilimwambia pengine Rufi atakuwa amefungiwa huko lakini kulikuwa na walinzi ambao wanalinda vidonge hivyo ilikuwa ngumu kufika.
Roma na Feilo waliendelea kupanda ngazi kwenda juu , jengo hilo halikuwa pana sana na hata ngazi zake zilikuwa sio pana lakini kwa namna moja kwa namna ambavyo limejengwa ungejiuliza ni teknolojia gani imetunika kukamilisha ujenzi wake kwani angle zake zilikuwa zimekaa kimaajabu ajab na ni refu mno na hakuna uhakika wa matumizi ya Cranes za kujengea.
Roma aligundua jengo hili pia lilikuwa na ulinzi wa nguvu za kijini na kila ukifika katika floor unatakiwa kuvunja kizuizi na kupita na kama nguvu zako ni ndogo basi uwezekano wa kupita unakuwa mdogo kwani uzio hautokuruhusu kupita.
Jengo hilo pia lilikuwa kama la majaribio , kwa mfano jini ambalo lipo katika levo ya nafsi ambalo linataka kwenda katika floor za juu zaidi kuona mbinu mpya za mafunzo itashindikana kwani nguvu zake ni ndogo, kila ngazi ilikuwa ikipitwa na jinni kulingana na uwezo wake.
Kwa maelezo ya Feilo ni kwamba kuna baadhi ya majini wanalazimisha kwenda floor za juu lakini waangalizi wa jengo hiloo wanawakataa pale wanapolazimisha kuvunja uzio na hio ilifanyika katika hio miliki ili kuwapa majini motisha ya kujifunza zaidi na zaidi.
Lakini kwa wakuu wa familia wao ni tofauti, kwa mfano msichana aliefahamika kwa jina la Manyani na Zilha hawa wanaingia ndani ya jengo hilo bila kuzuiwa kwani ndio wamiliki wa ukoo mzima na ndio viongozi.
Baada ya Roma na Feilo kupaa na kwenda kutua katika floor ya tano waliona ingekuwa ngumu kwenda zaidi floor za juu kabisa , sio kwamba Roma hakuwa na uwezo wa kwenda lakini kila alichokifanya alihakikisha kinakuwa ndani ya levo ya nafsi ili asingundulike mapema kabla ya misheni yake.
“Xiao Cheni hii ni floor ya tano , yenyewe sio mbaya sana mara ya mwisho nilivyofika niliingia floor ya tatu , ngoja tuone kilichomo ndani ya floor ya tano”Aliongea Feilo na wote kwa pamoja waliingia katika floor hio ya tano.
Roma alitamani kwenda juu zaidi lakini kwasababu Feilo alimchukulia kama rafiki aliona akae nae kwenye hio floor ya tano.
Feilo alionekana kuwa binadamu ambaye ana shauku ya kupanda levo mno kiasi cha kumfanya Roma kumuonea huruma na kujiambia kama isingekuwa misheni yake ndani ya ulimwengu huo wa kijini basi angempatia vidonge v ya kumuwezesha kupanda levo kwa haraka..
Baada ya kuingia kwenye Floor hio kulikuwa na mikusayansiko ya vitabu vingi pamoja na ‘scrolls’ na maandishi yaliokuwa kwenye miti , vitabu vingi vilionekana kuchakaa chakaa , ilikuwa ni maktaba ya kale sana lakini ilikuwa safi.
Roma alianza kukagua huku Feilo yeye akiwa bize kuchngua mbinu za kichawi kwa ajili ya kujifunza.
Mbinu za kichawi zipo kabisa katika maandishi , nguvu za kijini zenyewe sio uchawi kwasababu ukishaingia katika levo ya nafsi moja kwa moja unapata ufunuo wa namna ya kutumia elementi za dunia kutengeneza maajabu , lakini sasa majini wengine ili kujiongezea nguvu wanajifunza na mbinu za kichawi.
Kwa mfano Feilo mbinu yake ya kichwi ya ngurumo ya simba alijfunza hapo hapo kutumia vitabu ambavo vinapatikana katika jumba hilo jeupe .
Upande wa Roma alitemebea upande ambao aliona vitabu ambavyo kwa kiasi flani viliandikwa kwa mfumo mzuri wa karatasi na baada ya kukagua Roma macho yake yalichaua mara baada ya kuona vitabu vya dini vingi ndani ya eneo hilo.
Moja wapo ya vitabu vya kidini alivyoona ni Biblia na Quran tena zile ambazo zimeandikwa katika lugha ya kiarabu cha kidini na kiebrania kabisa.
Roma palepale alikumbuka swali ambalo alimuuliza Feilo juu ya majini kuamini katika Mungu na baada ya kuona vitabu hivyo aliona pengine swali lake limejibiwa nusu , kama hawaamini uwepo wa Mungu kwanini wamehifadhi vitabu vya kidini ndani ya hilo eneo.
“Nilikuuliza kuhusu majini kuamini Mungu kama binadamu , naona hapa kuna kitabu cha Enock kilichoandikwa kwa Kieabrania na Quran”Aliongea Roma.
“Broo majini hawachukulii biblia au Quran kama imani bali wanachukulia hivyo vitabu kama mbinu ya kuwasiadia kupanda levo”
“Unamaanisha nini kusema hivyo?”
“Binadamu ambao wanaamini katika uwepo wa Mungu wanatumia Biblia na Quran kama msingi wa sala na mafundisho , upande wa majini wao wanatumia maneno ndani ya vitabu vya dini kama msaada wa kuzitoa akili zao katika mazingira ya kawaida, kwa mfano kuna majini wanatumia mistari ya biblia na Quran katika kuvuna nishati na wanafanikiwa , ni maswala ya kimbinu tu hapo tofauti na kiimani , kama mimi nimejikita katika kutumia maandishi ya vitabu vya Budha katika kujifunza ipo hivyo kwa kila jini , kuhusu majini kuamini uwepo wa Mungu au kutokuwepo kwa Mungu ni swali gumu kulijibu moja kwa moja kwani imani kwao inaendana na matokeo”
“Unamaanisha kile ambacho kinawasaidia ndio huweka imani yao hapo”
“Umenielewa vizuri hapo, Bro chagua na wewe mbinu yako hapo , kama unachagua mbinu ya mistari ya kibiblia au Quran kuna muongozo wake upo chini hapo”
“Muongozo gani?”
“Sio biblia au Quran yote hutumika katika mafunzo ni baadhi ya maandiko tu ndio wanatumia”Aliongea na kumfanya Roma kuelewa lakini kwake hakuwa akitafuta mbinu ya kujifunza bali alikuwa akishangaa vitu ambavyo vinapatikana hapo ndani.
Ukweli kulikuwa na vitabu vingi sana ambavyo vilikuwa katika lugha mbalimbali, vingine vilikuwa katika ‘Code’ maalumu na vingine viliandikwa kwa michoro ya nyota nyota na viumbe wasioelezeka.
Roma alishangaa na kujiambia kama hii floor tu ina vitabu vngi hivi na kuna zaidi ya floor mia moja je vitabu hivyo vingine vinashikiria siri gani.
Roma alikuja kupata kitabu kingine kikubwa mno na juu kilikuwa na maandishi ya Great Ancient practice Codes, Roma mwanzoni hakujua kinahusiana na nini lakini mara baada ya kukifungua ndani na kuanza kusoma alijikuta akishangaa kwani ni kitabu ambacho kilikuwa kikielezea mafunzo yote ya kuvuna nishati na utofauti wa kila levo na maajabu yake , ilikuwa ni kama Enclopedia.
Roma alikaa chini na kuanza kujifunza kuhusu kile kitabu maandishi yake , kilikuwa kizito mno kama vile ni ndoo ya maji hivyo alifanya kukibwaga chini na kufundua karatasi moja moja.
“Bro hicho ndio kitabu cha muongozo nilichokuambia , ukiendelea kusoma kwenda mbele ndio utaona ni maandiko yapi katika biblia na Quran hutumiwa na majini kama mbinu za kujifunzia mafunzo ya kuvuna nishati za mbingu na ardhi , kila floor kuna hicho kitabu” Aliongea Feilo na kumfanya Roma kutingisha kichwa na kuendelea kupitia, shauku yake ilikuwa ni kutaka kujua nini kitatokea mara baada ya kuipita dhiki
Jambo moja ambalo Roma alipata kuelewa ni kwamba kuna Dhiki nyingi sana ambazo zinahusiana na mafunzo ya kijini lakini ambazo zilimshangaza ni Dhiki ya awamu sita ya barafu na Dhiki ya mapigo ya radi , Dhiki humjengea mtu msingi tu wa kuelewa nini kipo mbele yake na kama ukishafanikiwa kudhibiti elementi za anga na kutengeneza aina zote tano za moto basi moja kwa moja unakuwa umefaulu kuingia katika levo ya Tuzo , hii ni levo ambayo Roma hakuelewa sana inazungumzia nini lakini alichoweza kufahamu ni kwamba kuna zaidi ya levo ya kupigwa na mapigo ya radi na kilichomfurahisha zaidi sio lazima kupitia mapigo yote ya radi ndio upande levo au kuwa na nguvu kubwa bali ni namna ambavyo unapitia changamoto na kuzitatua.
Roma alipitia haraka haraka kitabu hicho na akaacha na kisha akaanza kutafuta kitu kingine cha kusoma , vitabu vipo vingi hivyo alichagua kutokana na hisia zake zinavyomtuma.
Roma alivutiwa na Scroll moja iliofunikwa na ngozi ya Simba , Scroll ni karatasi ambalo limekunjwa kunjwa na katika hio shelf Scroll hio ilikuwapeke yake kabisa tofauti na eneo lingine.
“ Bro hio karatasi hata mimi nimekwisha isoma , haieleweki kabisa na imetengwa kutokana na ugumu wake , inasemekeana majini ambao wametumia mbinu inayopatikana katika hio karatasi waliweza kufikia levo ya tano tu na hawakufanikiwa hata kupata miili ya kibinadamu”Aliongea Feilo.
Roma alijiuliza kwanini imewekewa ngozi tofauti na karatasi nyingine , ilionekana ni kitu chenye thamani ndio maana namna kilivyotunzwa ni tofauti na karatasi nyingine.
Yaani karatasi lake limebandikwa kwenye ngozi na ndio ikakunjwa kunjwa, ilimaanisha kwamba imeongezea ulinzi wa kutokuharibika.
Dakika ile ambayo Roma anafungua alijikuta akishagnaaa mno , huku akiwa haamini macho yake.
“Maandiko ya urejesho wa Azimio usiokoma”
Roma alisoma kwa mashaka kidogo huku akificha mshangao wake licha ya kwamba alikuwa ameshangaa kuona kitu hicho ndani ya eneo hilo.
SEHEMU YA 703.
Dakika ileile Roma alijiambia au kitendo cha kutoa andiko lile kule China kwa mtu mwenye Mask ndio ameleta andiko hilo ndani ya hili eneo, lakini kwa haraka sana aliona haiwezekani , kama kweli mtu angechukua mbinu yake lazima angeficha na asingeweka eneo la wazi hivyo kwa kila jini kuona.
Andiko hilo lilikuwa likifanana na mbnu yake kabisa ya mafunzo aliofundishwa na Master Tang chi , utofauti ni kwamba mwishoni kuna maandishi yameandikwa kwamba ni andiko ambalo halijatimia.
Roma alikagua na aligundua kuna utofauti wa kimatamshi tu lakini kila kitu kipo vilevile.
Roma alijiuliza kwanini miliki ya Kekexil ina mbinu yake , au ni mbinu ambayo pia ilimilikiwa na majini na wakashindwa kujifunza.
Kwa haraka haraka alianza kusoma maandiko yale na kutumia mbinu yake kuyakagua na palepale ni kama akili yake inampotea hivi na alishindwa kuona nguvu yake kabisa na aliamua kuacha.
Wakati wakiendelea kuwa bize ndani ya floor hio hatimae aliongezeka mtu mwingine na Roma palepale alimjua alikuwa ni binamu yake Rufi , bwana aliefahamika kwa jina la Zilha , alikuwa ni bwana ambaye mavazi yake ni kama vile sio jini kabisa hakuwa akivalia kitamaduni kama maijini wengine.
“Feilo wewe unaweza kwenda lakini Xio Cheni yeye atabaki nina mauzngumzo nae”Aliongea Zilha na kumfanya Feilo kushangaa Zilha anataka kuongea nini na Roma.
Baada ya Feilo kutoka na kubakia Roma jini Zilha alitoa tabasamu la kihuni mbele ya Roma.
“Xiao Cheni , nipo hapa na vidonge vya daraja la kwanza , je utapenda kutumia?”Aliongea na kumfanya Roma ashindwe kusoma mawazo yake kwani hakujua hata anafikiria nini, ila kitu kimoja tokea mwanzo alishajua huyo bwana ni muhuni.
“Nitashukuru sana kama utanipatia kaka mkubwa”aliongea Roma kwa upole na kumfanya Zilha kutabasamu.
“Nitakupatia vyote lakini unapaswa na mimi kunisaidia jambo moja”
“Chochote utakachotaka nitakusaidia Master”Aliongea Roma.
“Ni rahisi sana , wewe si una ukaribu na Zomu na Zato , saa nne ya leo usiku tafuta namna yoyote ya kuhakikisha unamtenganisha Zomu na dada yake , mbali kabisa itakuwa vizuri zaidi , kwa mfano unaweza kumpeleka Zomu kwenye uwanja wa mazoezi kule , yaani hakikisha tu hakai karibu na Zato…”
Roma palepale alijua nia ya Zilha kutokana na namna ambavyo alionekana kuwa na tamaa.
Ijapokuwa majini wengi walikuwa wakipambana kupanda levo lakini kuna wengine ambao wanajua kabisa hata kama wajitahidi vipi hawawezi kupanda levo hivyo wanachokifanya ni maisha ya starehe tu na moja wapo ni Zilha yeye hakujali maswala ya mafunzo bali alijali starehe ya kujivinjali na warembo wa kijini.
“Mimi Xiao Chen lazima nihakikishe natimiza agizo lako”Aliongea Roma
“Vizuri kama mpango ukienda vizuri nitahakikisha familia ya Zaola haikuletei shida”Aliongea na Roma aliishia kutabasamu na kujiambia huyu kajileta mwenyewe, baada ya usiku itajulikana.
Roma mara baada ya kushuka ghorofani alikutana na Feilo nje na kuanza safari , Feiloi alimuuliza Roma Zilha alikuwa na habari gani na Roma aliwambia tu kwamba alikuwa akiulizia kuhusu mbinu yake ya mafunzo kiasi cha kuwa na uwezo wa kuhimili mapigo mengi.
Kabla ya Roma kuachana na Feiloi alipendekeza usiku ajifunze mafunzo ya kuvuna nishati na mtu ambaye yupo levo ya juu zaidi yake na Roma alimwambia itakuwa vizuri kama wataungana na Zomu usiku kujifunza na Feiloi alifurahi na kumwambia yupo tayari kujifunza na jini ambalo lipo levo ya juu kuliko ya kwake na hapo ndio Roma alimwambia muda mzuri itakuwa ni saa nne usiku.
Roma hakuelekea moja kwa moja sehemu anapoishi maana hakuwa bize kama majini wengine ambao mara zote wanajifunza kuvuna nishati za mbingu.
Roma aliweza kumkuta Zomu akiwa bize anafanya tahajudi kama kawaida.
“Xiao Cheni unadhurula sana na sio vizuri kwa mafunzo yako”Aliongea mara baada ya kumuona.
“Ndio tuseme kwamba hutaki nikikaribia”Aliongea Roma hku akimwangalia jini huyo alivyokuwa ametokwa na jasho kwa kujifunza , walionekana walikuwa wakitumia juhudi kubwa sana katika mafunzo kuliko hata wanawake wake wanavyojifunza na alijiambia nadiko wanalo lakini hawajifunzi.
“Muda wowote na sehemu yoyote tunakukaribisha , umekuwa msaada kwa familia yetu na tutakumbuka wema wako milele, hata hivyo naamini ndani ya mwaka mmoja utaweza kuingia katika levo ya kuipita dhiki wakati huo utasimama kwa kujiamini kati ya majini wote wa koo hii na kupewa majukumu, pengine utashiriki katika mashindano”
Roma wakati alipokuwa akipiga stori na Zomu aliweza kumwambia kuhusu mashindano ambayo yanafanyikka ndani ya ulimwengu huo wa kijini kila baada ya miaka mia moja.
Mashindanno hayo yalikuwa yakihusisha majini ambayo yapo katika umri chini ya miaka hamsini kujumuisha koo zote kubwa za kijini zenye nguvu , ni mashindao ambayo yanafanyika kila baada ya miaka mia moja na ndio maana kaka yake Lilsi afahamikae kwa jina la Master Shagoni aliitwa kwa ajili ya kutoa mafunzo.
Sababu ya mashindano hayo ilikuwa ni kam ulimwengu wa majini pepo , ila hapo kuna utofauti ni kwamba wao wanashindana kwa ajili ya kuingia kwenye jicho la Anga.
Katika ulimwengu huo wa kijini kuna kaburi kubwa ambalo limejengwa katika upande wa kusini mwa miliki hizo , inasemekana kabuli hilo lipo kama fremu ya mlango mkubwa sana ambao upo ishara ya alama ni kama mfano wa ile fremu pale Dubai ya mlango.
Sasa inasemekana mahali hapo ndio kuna jicho la Anga , yaani kwao jicho la anga inamaanisha ni kama mlango wa kuingia ulimwengu mwingine kabisa wa kijini pepo.
Wanasema kwamba ukishangia kwenye hilo jicho la Anga ni kama umeingia kwenye ulimwengu mwingine wa majini pepo ambao ni wakali sana ambao hawapatani kabisa na majini wa kawaida na binadamu.
Yaani ni kama ulimwengu wa majini pepo lakini upande huo ni tofauti kidogo na ulimwengu wa majini pepo.
Sasa jicho hilo hufunguka kila baada ya miaka mia moja katika hesabu za ulimwengu wa kijini na huruhusu majini wa kawaida kungia katika jicho hilo ili kufika katika ulimwengu mwingine na kujikusanyia hazina.
Inasemekeana ulimwengu huo una vitu vingi vya thamani kwa ajili ya majini kama vile siraha za maajabu na vidonge.
Sasa unaambiwa tabia kubwa ya ulimwengu huo walioupwa jina la jicho la Anga ni kunyonya nguvu za majini wanaotembelea kila baada ya kufunguka kwake , hivyo mashindano yalikuwa yakifanyika ili kuruhusu majini wachache kuingia kwani kama wakiruhusu majini wengi kuingia jicho hilo hujifunga lenyewe kutokana na kunyonya nguvu nyingi ya kijini na likishajifunga inamaana kwamba ni zaidi ya miaka mia moja mingine katika kusubiria mpaka kufunguka tena.
Viumbe ambao wanaishi huko inasemekana ni roho za majini mara baada ya kufariki kwao.
“Kwahio hilo jicho likifunguka roho ambao wapo ndani ya ulimwengu huo hawarudi kwenye ulimwengu huu?”
“Huko pepo hao hawana miili , asilimia kubwa wote wapo katika mfumo wa pepo na sheria za jicho la Anga linaruhusu pepo kuingia na sio kutoka , hivyo mara nyingi majini wanapoingia katika ulimwengu huo pepo hao wanawashambulia sana ili kuiba miili yao na kurudi katika huu ulimwengu”
Roma alisikiliza Stori hizo za kustaajabisha , ijapokuwa maelezo ya Zomu hayakumwingia akilini vizuri lakini alitamani kwenda kujionea mwenyewe kama angepatta hio nafasi.
Alitaka kujua nini kinapatikana katika huo ulimwengu ambao mlango wake ni kama jicho.
TO BE CONTINUED.