Simulizi ya Kijasusi: C.O.D.EX.

Abdallahking

JF-Expert Member
Mar 19, 2018
3,983
10,804
3.jpg


Simulizi : C.O.D.EX. 1
Mwandishi : TARIQ HAJI
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES


C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 1


Allen James ni jina langu, ni dereva wa taxi katika jiji moja maarufu sana duniani Los Angels maarufu kama LA. Kama kawaida mapema vijana tunaingia kazini kutafuta mapeni. Nikiwa nasubiria abiria ghafla aliingia mtu na kunambia niondoe gari. Nami nikifanya hivyo lakini nlipoangalia nyuma niligundua jamaa alikuwa akitoka damu na nlipojaribu kumwambia nimpeleke hospital alikataa na kunambia nimpeleke sehemu ambayo atakua salama. Nilijaribu kufikiria ni sehemu gani hiyo jibu lililokuja kichwani mwangu ilikuwa ni nyumbani kwangu.

Bila kuchelewa niliekea nnapo ishi, nilijaribu kumpatia huduma ya kwanza lakini alikuwa tayari kashapoteza damu nyingi sana hivyo uwezekano wa kuishi ulikuwa mdogo sana. Mwisho kabisa aliniita na kuninong'oneza CODE X, kisha akanipa kitu kama kitambulisho na picha, akanambia nisimtajie mtu yeyote neno lile hadi nitakapomuona mtu alienipa kwenye picha kisha hapo nae akaaga dunia. Nilibakia mdomo wazi nisijue nini cha kufanya kabisa.

Wakati nikiendelea kuwaza hivyo ghafla nikaskia gari zikifunga breki nje ya nyumba yangu. Nilipoangalia kupitia dirisha sikuamini macho yangu baada kuona watu waliovalia suti nyeusi huku wakiwa na silaha nzito. Mshale wa hatari uligonga kichwani mwangu na bila kufikiria nikajikuta nimenyanyuka na kuelekea ulipo mwili wa yule mtu. Nilichomoa bastola yake kwa ajili ya kujihami na haraka haraka nikapitia mlango wa nyuma..

Hata sijui ni kitu gani kilinipata lakini akili yangu iliniambia nielekee moja kwa moja New York City. Na bila kuchelewa niliingia kwenye gari yangu na safari ikaanza. Kwa bahati mbaya sana mmoja wao aliiona gari yangu na kuwashtua wenzake. Kivumbi kakaanza hapo, nilijitahidi kuwakimbia lakini wapi gari zao aina AUDI zilikuwa na uwezo mkubwa sana, hivyo walinifikia na kuanza kunigonga. Nlipoona mambo yanazidi kuwa magumu niliamua kuwapatisha ajali tu, nilifanikiw kwa gari kadhaa lakini bila mategemeo nilipgwa mzinga na gari yangu ikapinduka.

Niliwahi kutoka kabla hawajanifikia na nikaanza kujibizana nao kwa risasi. Mwenyewe nilikuwa najishangaa maana sijawahi kuenda hata polisi lakini kwa jinsi nilivyokuwa nashambuliana nao ni kama nilikuwa nimebobea kwenye utumiaji wa silaha. Nilipohakikisha nimewamaliza nilichukua gari yao moja na safari ya kuekea New York ikaanza.

Safari ya kuelekea New York ikaanza, huku njia nzima nlikuwa nawaza uwezo ule wa kupigana nimetoa wapi maana tokea nipate fahamu zangu sikuwahi kujifunza ngumi. Lakini niliona bora niachane na mawazo hayo. Usiku ulinikuta njiani hivyo nikaona bora nitafute Motel nilale. Siku ya pili mapema niliendelea na safari yangu yenye sintofahamu nyingi, niliwasili New York mnamo saa nne na kidogo.

Niliacha gari sehemu ya maegesho na kuanza kutembea kwa miguu lakini kwa umakini sana. Nilitembea mpaka kwenye hotel moja hivi na kuingia, maajabu nilioyakuta mapokezi yalizidi kunichanganya maana yule mschana aliekuwepo pale alinichamgamkia utasema labda tunajuana kwa muda mrefu sana. Bila hata kuongea kitu alinipa funguo ya chumba. Nilimshukuru na kuondoka huku moyoni nikijaimbia lazima nitafute muda niongee nae kwani anaonekana kujua mengi kuhusu mimi.
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 2


Nilifika chumbani kwangu kitu cha kwanza niliingia bafuni nikaoga maana uchovu ulikuwa ukinitafuna. Nilirudi ndani na kufungua kabati, macho yangu yalikutana na suti za bei mbaya tu. Nilichagua moja na kuvaa baada kuona nishapendeza nilikaa kitandani nikifiria mambo mengi yaliotokea siku ya nyuma. Wakati nikiwa mbali kwenye mawazo ghafla niliskia simu ikiita, niliangaza wapi ilipo na kwenda kuichukua. Nilipoipokea ukaingia ujumbe uliosema "kaa tayari ukisubiria maelekezo mengine". Ukaingia ujumbe mwengine "katika kabati kuna begi, litoe na fuata maelekezo utakayoyakuta".
Nilifungua kabati na kutoa begi nikalifungua, nilikuta picha ya mzee mmoja nyuma ikiwa na ujumbe "chukua sniper iliokuwepo humu na uhakikishe huyu mtu anakwenda kuzimu". Niliiangalia ile sniper nikajikuta natabasamu, nilibeba lile begi na kuchukua ile simu kisha nikatoka. Nilipofika nje uliingia ujumbe mwengine "huyo mtu anapatiakana mji wa Alexandria na kazi ikamilike ndani ya masaa kumi na sita, chukua hiyo gari nyekundu mbele yako". Niliingia kwenye ile gari na safari ya kuelekea Alexandria ikaanza. .
Nilipofika tu uliingia ujumbe ulionielekeza alipo, nilifika sehemu ya tukio na kupanda katika jengo moja refu kidogo lilikuwepo pembeni ya jumba alilokuepo huyo mlengwa. Nilipofika juu nilitoa sniper na kuiunga baada kukamilisha zoezi hilo nilijweka sehemu nzuri na kuanza kumtunga. Kwa msaada darubini ya sniper nilimuona vizuri na hapo nikafyetua risasi ilioingia kichwani na kusambaratisha ubongo. Sikuwa na haja ya kuichukua ile sniper, nilitoa bomu dogo na kulitega pale kisha nikaondoka. Iliripuka na Ushahidi ukapotea, nilipofika tu chini nilikaribishwa na risasi kadhaa hapo nikajuwa nimeshtukiwa.
Nilitoa bastola mbili ndogo na kuanza kujibu mashambulizi huku nikikoswa na risasi kadhaa. Kutoka kwa mlango huo ilikuwa haiwezekani nilirudi ndani na kuanza kutafuta mbinu za kutoka humo maana hata risasi zilikuwa zimeniishia. Mara walianza kuingia ndani,nilijibanza sehemu nikajisemea atakaepita kwanza ni halali yangu. Mara mmoja akapita nilimvuta ndani na kumvunja shingo, nikachukua bastola yake na kukimbia. Wakati nikiwa katika mapambano hayo uliingia ujumbe mwengine ukinitaka niondoke nchini marekani nielekee shanghai china. Nilifanikiwa kutoka nje na kuelekea ilipogari yangu na kutokomea, nilifanikiwa kuwatoroka. Moja kwa moja nilielekea uwanja wa ndege na kukata tiket ya ndege inayofuata kuelekea zangu Shanghai China. Muda wa kupanda ulifika na safari ya Shanghai ilianza na kwa jinsi nilivyokuwa nimechoka usungizi ulinichukua, usingizi uliombatana na ndoto mbaya za mateso ya hali ya juu sana.
*****
"jina lako nani" aliendelea kuniuliza uku akinipiga mgumi kadhaa za tumbo "Allen James" nilijibu lakini bado hakukubali. Mara nikamsikia akisema leteni mashine ya shot, haukupita muda ililetwa mashine hiyo. Aliiwasha na kutaka kunipiga shoti, ghafla nilishtuka kutoka usingizini huku jasho likinitoka, nilimuita muhudumu nikamwambia anipe kinywaji cha baridi baada hapo nilitulia nikiwaza ile ndoto. Kwa sababu ilikuwa ni ndoto tu nikaona bora niipoteze.
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 3

Ndege iligusa ardhi ya Shanghai, nilishuka na kuelekea nje na nlipofika tu nje uliingia ujumbe "kuna macedes benz nyeupe kwenye maegesho, chukua hiyo gari na fuata maelekezo utakayoyakuta" niliangaza huku na huko mpaka nilipoiona na kuifuata. Niliingia kwenye gari hiyo, nilipowasha tu nikaskia sauti ya kike "karibu Shanghai Allen, fuata raman katika computer ya gari hii kufika katika hoteli uliopangiwa" baada hapo ile computer iliionyesha ramani na bila kupoteza muda nilianza safari ya kuelekea katika hiyo hoteli, ilinichukua dakika kumi kufika huko hotelini. Nilifika mapokezi nikataja jina, nikipewa funguo na kuelekezwa kilipokuwa chumba changu. Nilipofika chumbani niliingia chooni nikajimwagia maji na kubadilisha nguo. Wakati nikiwa nimepumzika ukaingia ujumbe "kwenye meza kuna picha na kisu, muue huyo mtu kwenye picha" nilsogea mezani na kuichukua picha. Dah macho yalinitoka kwasababu mlengwa wakati huu ni mwanamke. Nikajisemea moyono huyu mschana anabahati mbaya kweli na uzuri wote huu alokuwa nao leo anakwenda kuzimu. Nilishtuka kidogo na kujishangaa roho ile ya kikatili nimeitoa wapi. .
Nilisubiri hadi usiku nikatoka kuelekea alipo huyo mschana na kwa msaada computer sikupata tabu sana kuijua nyumba yake. Basi nilifika lakini yeye hakuwepo hivyo niliingia ndani na kumsubiria, nusu saa baadae mlango ulifunguliwa, nilijibanza ukutani ili asije akaniona. "umekuja kuniua" aliongea yule mwanamke, nilijikuta nikimuuliza amejuaje kama nipo alkanijibu kuwa mambo yote ninayo yafanya yeye anajua. Nikamuuliza sasa alikuwa anajua kwanini aliamua kurudi, akaniambia kuwa anataka kunisaidia tu ili nitoke kwenye kifungo hicho cha utumwa.
Kidogo nilipowa baada kumsikia anataka kunisaidia maana hata mimi Mwenyewe nilikuwa sijijui tena. Aliniambia kuna kifaa nimewekewa kinachonindesha katika kufanya maamuzi na ndio maana kuuwa naona ni jambo sahihi kwangu. Nilimuuliza kama anaweza kukitoa akanijibu ndio lakini si wakati huo kwa sababu muda si mrefu tutavamiwa. Na kweli hatujakaa sawa tukaskia gari zikifunga breki. Aliniambia nimfate nami nikafanya hivyo, tulifanikiwa kutoka nje bila tabu na kwa kutumia usafiri wake tuliweza kuwaponyoka maadui zetu.
Kwa sababu yeye alikuwa mwenyeji nilimuachia awe kiongozi. Aliendesha gari kwa muda wa saa nzima, tulitoka nje ya mji wa Shanghai. Tulifika katika nyumba moja, hapo ndio ikawa mwisho wa safari yetu. Tulingia ndani, akasema tutapumzika usiku huo na siku itakayo fuata atanitoa hicho kitu.
Mapema siku iliyofuata alinifanyia operesheni ndogo na kukitoa. Alipokitoa tu nikapoteza fahamu. Nilikuja kushtuka nimo ndani ya chumba chenye kiza sana nilipojaribu kuinuka nilishindwa na nilipoangalia vizuri mikono yangu pamoja na miguu ilikuwa imefumgwa na ghafla taa zikawaka.
Dah nilijiona bwege kweli kudanganyika kirahisi kiasi kile, kwa mbali niliona watu wakija na nilipoangaza vizuri miongoni mwao ni yule mwanamke. Alipofika akaniuliza kama nimefurahia usingizi mzito, "kwani nimelala kwa muda gani?" nilimuuliza kwa shauku, akanijibu kuwa nimelala kwa muda wa masaa 72 kwa maneno mwengine nimelala kwa siku tatu.
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 4


Baada maongezi hayo aliingia mtu wa makamo hivi, kwa kumkadiria ni kati ya miaka sabini au sabini na tano.
"kijana mimi sitak tusumbuwane" aliongea, "tusisumbuwane kivipi" ,nilihoji kwa sauti iliojaa hasira. Akanambia kuwa anahitaji password ya kufungua computer yenye siri za Project CODE X. Nikamwambia kuwa mimi sifahamu chochote kuhusu jambo analoliongea, ghafla nilishtukia konde zito la tumbo lililonifanya nikohoe damu. Akarudia tena kuniambia jambo lile lile na mimi jibu langu lilikuwa lile kuwa sifaamu kitu chichite anachokiongea.
"inavoonekana kupata ukweli nitahitaji nitumie nguvu kidogo" aliongea yule mzee na kutoa ishara. Hapo waliingia jamaa watatu miraba minne na walionekana wapo kikazi zaidi. "Pigeni mpaka atakapo tupa kodi" aliongea yule mzee na kutoka. Basi wale washkaji walinisogelea na kunipa kipondo, nilijiapiza nikifanikiwa kutoka hai basi kila mmoja ataambulia kifo kibaya sana ambacho hajawahi kufikiria. Sikumbuki hata muda gani waliacha kunipiga lakini nilikuja kushtuka nimefungiwa chumbani. Kosa walilofanya ni kuamini kuwa mlango utanizuia kutoka na ndio maana hawakunifunga kama mwanzo.

.
Nilikagua mule chumbani nikaona kuna kamera, nikajisemea subiri niwaonyeshe mwanaume wa kweli anavofanya maamuzi magumu. Haraka haraka nilichukua shuka na kulichana, nilifanya nikijuwa kabisa watakuwa wananiona. Kwa ufahamu niliokuwa nao binadamu anaweza kubana pumzi kwa dakika tano bila kupata madhara yoyote yale. Kwa kasi ya ajabu nililifunga lileshuka kwenye dari na kujinyonga, kama hesabu zangu zilivokwenda. Walinzi walikuja mbio kuniokoa, nilitulia vilevile mpaka waliponivua kile kitanzi ndipo nilipoamuwa kuwatenda.
Nilimpiga ngumi ya koromeo yule aliekuwa ameinama na kulivunja na kabla yule mwengine hajafkiria nini cha kufanya nilimpiga teke zito kwenye goti na kumfanya aanguke kama mzigo. Hapo nilikimbilia shingo na kuivunja, kisha nikachukua redio call moja pamoja na bastola zao na kutoka kwenye chumba hicho.
Tayaria wengine walishashituka na kubonyeza alarm, wala sikujali hilo nilitoka humo chumbani na kitu cha kwanza kufanya ni kuzipasua kamera ili tucheze kombolela bila wizi. Nilfanya hivo kila nilipokutana na kamera huku nikiwapunguza mmoja mmoja, wakati nikiendelea na zoezi hilo si nikakutana na mmoja kati ya wale washkaji walonipa kipigo cha mbwa mwizi. Ila alikuwa bastola basi nikatumia tu akili ya kisungura na kumwabia kuwa wanaume hawaneshani kwa silaha kama vipi tuweke moto chini twende mtu kavu tu, nae akakubali bila kinyongo. Nikajisemea unadhani kuwa utaokota hata moja, basi jamaa akaja kichwa kichwa nilimkwepa na kumtegeshea mguu, basi nalo likaanguka kama ngurue alopigwa gongo la kichwa.
Wakati wa kuinuka si ainuke hovyo, hapo sikuchelewa nilimpiga ngumi nzito ya uso na kumfanya aweweseke kama mlevi na kabla hajakaa sawa nilimsindikiza na teke la kifua na kumpeleka chini. Tayari mchuzi ulikuwa ushaachemka na kumwagika. Nikamwambia nitamvunja kiungo kimoja kimoja mpaka vimalizike mwili mzima, aliinuka na kurusha ngumi wala sikuikwepa bali niliidaka na kuviminya vidole katika shemu inayojulikana kama pressure point na kuvivunja.
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 5

Sikumuwacha augulie vizuri, nilimvuta na kumkandamiza teke kwenye goti na kulivunja, niliendelea na shughuli hio mpaka nilipohaikisha hakuna cha kuvunja tena zaidi ya shingo. Nikaona haina haja ya kumvunja shingo kwani angekufa mapema, nilichokifanya nilitafuta msumari na kusindika kwenye chemba ya kifua kisha nikamuacha na kuendelea na safari. .
Nilifanikiwa kuwapunguza kwa kiasi kikubwa kutokana na kuwa nilijuwa kila kitu kilichoendelea kupitia redio call niliochokuwa. Nilifanikiwa kufika mpaka katika mlango uloandikwa EXIT, niliufunguwa kwa furaha lakini nilipigwa na bumbuwazi na pia nilichoka na kukosa la kuongea wala kufanya nikabaki nashangaa tu.
Nilihisi kuishiwa nguvu maana sikutegemea kama nitakutana hali hiyo kabisa maana baada ya kufungua mlango niligundua kuwa nipo jangwani. Nikajisemea ina maana juhudi zangu za kujiokoa ndio ziishie hapa, hata haiwezekani lazima nitafute njia ya kutoroka tu katika jangwa hili. Nilijua ikiwa nitaamua kuingia jangwani basi kuna mawili aidha ningekufa au ningepona lakini la asilimia kubwa ilikuwa ni kufa maana hata hilo jangwa lenyewe nilikua sijui ni la wapi.
Wakati nikiendelea kuwaza nifanye nini lilinijia wazo la kuirudia ile simu yangu labda yule mtu aliekuwa ananitumia ujumbe angenisaidia kutoroka. Lakini pia niliwaza eti nirudi ndani kisa simu, dah lakini kuna wakati inabidi mtu ufanye maamuzi magumu sana.
Basi mwisho niliamua kurudi ndani, huku nikiwaza njia ya kuipata simu hiyo ambayo hata sikujua iko wapi. Lakini nikaona njia pekee ya kujua ilipo ni kujikamatisha kwa sababu katika wakati kama huo hata maadui zangu wakinikamata watanipeleka kwa mkubwa wao. Basi nilirudi kizembembe makusudi, na mpango wangu ulifanikiwa. Walinikamata na kunipeleka kwa mkubwa wao, na kwa kweli bahati ilikuwa kwangu maana vitu vyangu vyote ikiwemo ile simu vilikuwa katika meza ile aliokaa yule kiongozi wao. Alitabasamu kwa kejeli baada ya kuniona, kisha akasema kuwa ndege mjanja hunaswa na tundu bovu. "hivi ulidhani utaweza kutoroka humu" aliuliza kwa hasira, wala sikumjibu kitu maana akili yangu yote ilikuwa ni kwenye ile simu tu. Nilikuwa nikipiga hesabu nitaipaje na kuwatoroka.
Kwa hesabu za haraka niligundua kuwa walikuwepo watu kama kumi ndani ya chumba kile, kwa kujiamini nilisimama kwa kasi ya hali ya juu na kujirusha kwenye ile meza na niakfanikiwa kuichukua simu pamoja funguo mbili za gari na passport yangu. Na pia nilifanikiwa kuwapeleka chini watu watatu na kufanikiwa kufika mlangoni lakini kabla sijatoka nilihisi kitu cha moto kikipenya kwenye mguu wangu wa kulia. Lakini kama unavyojua wakati wa hatari binadamu anaweza kufanya jambo lolote lile, sikuyajali maumivu niliendelea kukimbia mpaka nje na kutoa zile funguo kisha nikabonyeza funguo moja, kwa mbali nikaskia gari ikilia. Nilielekea kule ilipo na kuingia kisha safari ikaanza nikiwa hata sijui naelekea wapi maana sikuweza kuona hata mji. Wakati huo naendesha nilitoa ile simu na kuiwasha, na papo hapo ukaingia ujumbe uliosema ni bonyeze nyota kwenye simu kisha nipige.

ITAENDELEA
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 6

Nilifanya hivyo kisha nikapiga, ilipokea upande wa pili na kunambia kuwa nisiiache hewani kwani walikuwa wanataka kuitrack ili wajue niko wapi. Dakika mbili baadae computer iliokuwepo kwenye gari hiyo iliwaka na kuingia ujmbe, nilipoufungua ilikuwa ni ramani..

Kisha ukaingia ujumbe kwenye simu ukinambia kuwa nipo katika jangwa moja lilokuwepo nchini Afghanisatan, na kutoka nilipo mpaka kwenye makazi ya watu ni kama kilometa 300. Dah ukizingatia na jeraha la mguu nililopata nilijua uwezo wa kutoboa ni mdogo sana, kwasababu nilishapoteza damu nyingi sana. Nilisimamisha gari baada kukumbuka kuwa gari nnayo endesha ni Jeep ya kijeshi na mara nyingi huwa zina kuwa kile kibox cha huduma ya kwanza.

Basi nilishuka na kuikagua na kwa bahati nzuri nilikiona, wala sikutaka kuitoa risasi bai nilichoma sindano ya ganzi ili kupunguza maumivi na kupaka dawa ya kuzuia kutoka damu baada ya hapo nilijifunga bendeg na kurudi siti ya dereva na safari ikaendelea. Nilihakikisha nakwenda kasi kadri gari hyo ilivokubali, na kweli gari hizo maalum kwa kutembelea jangwani na misituni basi haikufanya ajizi kila nilikanyaga mafuta iliitika na kutimua vumbi kiasi kwamba mpaka nikahisi kama nikikanyaga kijwe au kigogo basi itakuwa ndio mwisho wa safari yamgu.

Masaa mawili baadae nilifika mjini na moja kwa moja nilikwenda hospitali iliokuwa karibu kwa ajili ya matibabu zaidi. Walifanikiwa kuitoa risasi na kunambia kuwa haikupiga katika mfupa zilizoathirika zilikuwa ni nyama tu za paja. Baada kutoka hospitali nilirudi kwenye gari na kuifungua ile simu na kupiga nyota. ILipokewa upande wa pili, "hebu nambieni mimi hasa ni nani" hilo niswali la kwanza kuuliza punde ilipopokewa, maana mnajua maisha yanavokuwa magumu kujikuta unawindwa na kila mtu bila kutambua hasa wanachokitak nini. "tukionana utajua kila kitu lakini kwa sasa unatakiwa ufanye haraka uondoke nchini Afghanistan, maana tayari CIA ya Marekani imeshatoa picha zako kuwa unatafutwa iwe umekufa au mzima" upande wa pili ulinijibu kisha ukaendelea "na kwa sasa hatuwezi kukutrack maana GPS device tuliokuekea imetolewa na wale wakidhani ndio protocol CODE X, lakini ukweli wewe unayo hio katika jicho lako la kushoto na itabidi tuiwashe hio ili tuweze kuwasiliana kirahisi zaidi. Dah nilichoka kabisa " wangeipata hiyo ingekuwa balaa na ndio maana sisi tukawa tunakupa kazi ya kuuwa kwa sababu ikiwa hao watu wataendelea kuwa hai basi hawataacha kukufatilia", "sasa cha kufanya nenda bank iliokaribu nawe na onyesha passport yako" alimaliza kuongea na simu ikakatika.

Nilifanya kama alivonambia, niliielekea bank na kuwaonyesha passport yangu. Basi aliitwa mtu na kunipeleka katika makabati fulani hivi na kunambia ningize neno la siri nami ikafanya hivo. Lilifunguka na kuchuka begi na kurudi kwenye gari,
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 7

kisha nikapiga tena simu " sasa tafuta sehemu ambayo unahisi utakaa kwa masaa matatu bila kusumbuliwa kwaajili ya kuiwasha protocol CODE X" nilingalia ramani yangu kwenye gari na kutafuta hoteli moja ya kisasa sana baada kuridhika na maelezo nilioyapata kupitia computer ile nilielekea kwenye hiyo hoteli na kuchukua chumba. Niliingia chooni kwa ajili ya kujisafaisha, nlipotoka nikapiga simu mapokezi kwa ajili ya kunitafutia suti na niipate baada masaa matatu.

Niliekea kitandani na ile simu kisha nikapiga tena, "uko tayari" nilijibu ndio, "tutakapoiwasha tu, utapoteza fahamu maana itaachia kemikal inayoitwa CINDREX OLTIVIASO DECA ENDROLINE X (C.O.D.E.X), na ili iweze kuenea vizuri katika mwili ni lazima uwe umerelax na njiapekee ya kuhaikikisha hilo ni kulala usingizi wa kifo maana maumivu yake huwezi kusatahamili". nilikubali tu maana sasa sikuwa na jinsi kwa sababu kila mtu alikuwa anataka kunikamata au kuniua na sasa nishakuwa WANTED serekali ya Marekani. Baada kukata simu niliwasha AC na kujifunika shuka. Sekunde kadhaa tu nilipoteza fahamu.

****.

"Baba umeniletea zawadi yangu" mtoto mdogo wa kike aliniuliza, "ndio nimekuletea princess wangu" nilimjibu huku nikimbeba. "Pole kwa kazi mume wangu" aliingia mwanamke na kunambia maneno hayo. Nilibaki nimeshangaa maana mimi nilikuwa hata siwajui lakini yule mtoto kaniita baba na yule mwanamke kaniita mumewe. "baba zawadi yangu iko wapi, nataka zawadi yangu, baba zawadi zawad izawadi. nilikurupika kutoka usingizini huku kijasho chembachemba kikinitoka kumbe nilikuwa naota tu, nilipoangalia saa yangu niligumdua tayar masaa matatu yashatimia na mara nikaskia mlango unagongwa. Nilikwenda kufungua nikamkuta muhudumu akiwa na suti, niliichukua na kurudi ndani, nilivaa vizuri kabisa na kuwa kama mtu wa ofisini, simu yangu iliita ,nilipoipokea tu " Habari yako na unajiskiaje, tulia hivo hivo tunakukagua kama hujapata madhara yoyote yale, kila kitu kipo sawa na baada kukata, simu hii itaungua na kuanzia sasa tutakuwa tunakutumia ujumbe moja kwa moja kwenye ubongo wako na chukua tahadhari" ilikatika na hapo ikaanza kutoa moshi kumaanisha kuwa ilikuwa inaungua.

" kuna ndege inaondoka masaa mawili kutoka sasa, inaelekea Korea ya kusini panda hiyo ndege" uliingia ujumbe huo kama mawazo kichwani mwangu na bila kuchelewa niliishuka chini na kuchukua taxi kuelekea uwanja wa ndege. Nilipofika nilikata ticket na kukamilisha tarabi zote na muda ulifika tulipanda abiria wote na safari ikaanza.







NIlitulia nikiitafakari ile ndoto kwa muda bila kupata jibu lolote basi nikaamua kuachana nayo. Kwa vile nilitoka kulala basi sikuwa na usigizi hata kidogo mpaka ndege ilipogusa ardhi ya korea. Nilishuka na wakati naelekea mlango wa kutokea uliingia ujumbe mwengine " kata ticket ya kuelekeea Doha Qatar" ,nilifanya hivyo na baada masaa matatu niliingia kwenye ndege na safar ya Qatar ikaanza, kutokana na uchovu wa safar ya mwnzo usingizi mzito ulinichukua na haukupita muda mrefu nilianza kuota tena ndoto ile ile lakini wakati huu yule mtot alikuwa anaungua moto. Nilishtuka kutoka usingizini baada ya kuguswa bega na mhudumu mmoja wa ndege mwenye asili ya kiarabu akaniuliza kuna tatizo gani, nilimjibu kuwa ni ndoto tu alitabasamua na kuurudi katika siti yake.
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 8


Na mimi nikaamua kubadilisha upande, ili niendelee kulala na kile kitendo cha kufunga macho tu basi ile ndoto ikajirudia tena, nilishtuka tena baada ya kuguswa tena kwenye bega na yule yule mhudumu akaniambia nimfuate. Mtu hakatai wito niliinuka na kumfata nyuma kabisa kwenye kama kijichumba kidogo, akaniuliza tena kama nina tatizo, nikaona bora nimwambie tu basi nikamuelekza kila kitu kuhusu ile ndoto na kuwa ni mara ya tatu naiota. Akanambia mara nyingi hizo huwa si ndoto bali nikumbukumbu kisha akaniuliza kama nishawahi kupata amnesia, Nilimjibu kuwa sikuwahi kupata ugonjwa huo, basi alinipa kikombe cha kahawa. Nilikunywa huku nikiutathminia uzuri wake, nilimaliza kumshukuru na kurudi kwenye siti yangu. Kwa vile nilikunywa kahawa basi usingizi uliruka wote na macho yalikuwa makavu. Hatimae ndege iligusa ardhi ya Doha.

Nilishuka kwa lengo la kutoka nje, nilihisi kama mtu ananiita na nilipogeuka nilimuona yule mhdumu akija upande wangu. Nilisimama mpaka alipofika pale na kuniuliza kuwa kama ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kufika katika jiji hilo. Nilimjibu ndio basi akaomba kuwa mwenyeji wangu, nilikubali lakini pia nilihofia yasije yakawa kama yalonikuta mjini Shanghai, lakini nikajisema mazari kama haya huwa yanakuja mara chache sana hivyo nisiache amba chao kwa msala upitao. Tulitoka uwanja wa ndege na kuelekea hotelini, haikuwa mbali na uwanja wa ndege. Kila mtu alichukua chumba chake na tukakubaliana tukutane mapokezi baada ya saa moja.

Nilipoingia chumbani, nilifanya mambo yangu yote na nlipomaliza nilishuka chini kama tulivyokubaliana ila mimi niliwahi dakika tano nyuma kabla ya muda wa ahadi. Kwa mbali nilimuona mschana akiteremka kwenye ngazi, macho yalinitoka na kujikuta mapigo ya moyo yanakwenda mbio baada kugundua kuwa ni yule mhudumu wa ndege. Mpaka ananikaribia sikushtuka kabisa, alinigusa mkono ndipo akili ilirudi. Nilijikuta nikisema tu umependeza sana alijibu asante na kunambia nimfate, tulitoka nje na kuchukua taxi. Mimi nilikuwa kama bendera nafuata upepo hasa ukizingatia mji wenyewe nlikuwa siujui. Tulifika kwenye mgahawa mmoja ulotulia sana na kuchukua meza, alikuja mhudumu nikamuachia yeye aagize chakula. Baada mhudumu kuondoka "mimi naitwa Tania" alijitambulisha, "Allen James ndio jina langu" nilimjibu. "nashkuru kukufahamu" aliongea huku akitabasamu na kunifanya nijiulize " hivi Mungu alimuumba huyu mschana akamchivya kwenye maji ya uzuri na kumwabia nenda duniani ukawachanganye wanaume au". Maana kwa kweli sijawahi kuona mschana mrembo kama huyo. Basi tuliongea mengi pale mpaka chakula kilipo kuja na kula, baada ya hapo tulizunguka sehemu mbalimbali za starehe na kujikuta nasahau hasaa kama nawindwa kama pesa. .

Ni kwa mara ya kwanza nilikunywa pombe mpaka nikahisi mawenge, baada ya kuzunguka sana mrembo huyo tulirudi hotelini lakini akaniambia nimpe kampany chumbani kwake maana alikuwa hana usingizi pamoja na kuwa amelewa. Basi niliingia katika chumba chake kilichofukizwa kisawa sawiya, harufu nzuri nilioikuta humo ilikuwa balaa.
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 9





“Hamna shida Timasi. Nimemuelewa.” Akajibu kilijari.

Baada ya kauli hizo za kufarijiana, walianza kuongea haya na yale kuhusu biashara na maisha mengine kwa ujumla huku wakiwa wamesahau kabisa kuhusu Limasi na mtindo wake wa kucheza kimahaba.

Wakiwa wamezama kimaongezi, mara kelele zinasikika ukumbini. Vijana wanakuwa kama wamepagawa ndani ya ukumbi. Walipotazama, walishuhudia Limasi akiwa kazunukwa na vijana wapatao kumi na wote walionekana wapo katika kulewa. Limasi alikuwa katika hali ya uoga na wale vijana ambao wengine walikuwa vifua wazi, walionekana wanataka kufanya naye jambo.

“Kaa hapahapa Timasi.” Akaongea Iris na kusimama tayari kwa kwenda pale alipo mrembo Limasi.

ENDELEA.

“Hapana Iris, hao ni wakorofi wa Arusha. Usiende, watakuumiza bila sababu.” Alibwata kwa woga Timasi huku anajaribu kumvuta Iris asiende kwenye lile tukio.

“Kwa hiyo tuache dada yako anafanyiwe upuuzi?” Akauliza swali hilo ambalo lilimfanya Timasi amuachie mkono wake yule mwanaume aende kufanya alichokusudia.

Iris akaenda hadi katikati ya ukumbi ule ambapo Limasi alikuwa kazungukwa na vijana wa Kiarusha wengine wakiwa wamekamata chupa za vilevi vyao.

“Kila kitu kipo sawa vijana?” Iris akaongea kiuungwana ambapo wale vijana wa kiume waligeuka na kumuangalia aliyeongea hayo.

“Hayakuhusu braza. Kaa mbali na hii kitu.” Kijana mmoja mwembamba na mdogo kiumbo, akiwa kavalia kata mikono kama la wacheza kikapu, alibwatuka kwa lafudhi ya Kiarusha.

“Mnataka shilingi ngapi ili mumuache dada yangu.” Iris aliongea tena safari hii akiingiza mkono wake kwenye suruali yake ya kitambaa na kutoa kiasi kadhaa cha fedha na kuanza kuhesabu.

“Tunataka zote hizo, pamoja na huyu kuku tumbambie mpaka turidhike.” Kijana mwingine aliongea huku akipora kiasi kile cha fedha na kukifutika mbele ya sehemu zake za siri.

“Okay. Kwa upendo tu, chukueni hizo fedha na kumuacha huyo dada aendelee kucheza muziki peke yake.” Akashauri Iris.

“Unasemaje wewe bwege?” Kijana mwingine aliyekuwa kifua wazi na kakamata chupa kubwa ya mvinyo, alijitunisha huku anamfata Iris ambaye alitabasamu bila kupenda. “Hivi wewe unazijua charii za ara ama huzijui wewe.” Aliendelea yule kijana mwenye chupa ya mvinyo huku anazidi kutuna kila anapopiga hatua. Alivutia kwa kumuangalia na mwili wake mdogo lakini anajaribu kuutunisha.

“Dogo, bora ukalale kama umelewa na kuchoka.” Maneno yakamtoka Iris na bila kuuliza, yule kijana wa Arusha aliruka kwa haraka na kutaka kumpiga chupa ya kichwani Iris, lakini mwanaume yule alisogea pembeni kidogo tu, na kijana wa watu akapitiliza. Iris hakufanya makosa, akamsukuma kwa mguu kijana yule na kumfanya aende mbele kichwa kichwa na kwa kasi ya ajabu.

“Limasi. Toka hapo njoo huku kama hutaki kuchezewa na hawa madogo.” Iris aliongea lakini pale Limasi alipotaka kutoka katikati ya kundi la wahuni wa Arusha, akajikuta hapati njia ya kutokea na wakati huo, ukumbi mzima ulikuwa kimya na milango yote ikafungwa ili asitoke wala kuingia mtu. “Yoyote atakayejaribu kukugusa, namtengua mkono. Nadhani kila kijana kaelewa nachomaanisha.” Maneno hayo yakampa ujasiri Limasi na kuamua kuanza kutoka katikati ya kundi lile. Alipomfikia kijana mmoja, kijana yule akajaa mbele yake na kumzinga ili aispite. Iris akaenda hadi pale kijana alipozinga na kumshika bega kijana yule. “Muache apite.” Akaongea kwa utaratibu Iris.

“Huyu ni wetu braza. Huwa hatuogopi kitu sisi.” Aliongea kijana yule na kumshika mkono Limasi, lakini alichokutana nacho, nadhani hadi leo anakihadithia kwa wajukuu.

Iris alimtoa mkono wa yule kijana kwenye mwili wa Limasi, na kisha akaunyanyua juu kama refa wa ubondia akitangaza mshindi. Baada ya hapo, akamtwanga ngumi kali ya kwapa yule kijana. Alilia kwa sauti ya juu lakini haikumfanya Iris ashindwe kurudisha mkono wa kijana kwa kasi na kuuzungusha nyuma ya mgongo wake na kuubana vema.

“Nilikwambiaje dogo?” Akaulizwa kijana wa Arusha.

“Niache. Nasema niachee. Kaka ananiumiza huku.” Kijana yule alipiga ukelele mzito na sijui kaka yake alikuwa nani, lakini mara alitokea jamaa mmoja mrefu na mwenye mwili kiasi na kuruka teke la juu lililomkuta Iris kifuani na kumfannya amuachie yule dogo na kurudi nyuma kidogo.

Idris akakaa sawa na kumtazama yule kaka mtu ambaye alikuwa kavaa kapero na mdomoni mwake akiwa anatafuna bazuka.

“Kaeni mbali madogo. Muone nachomfanya huyu bwege.” Aliongea yule aliyeitwa kaka na wale vijana walisogea pembeni huku wakinong’onezana maneno ya kumsifu kaka mtu kuwa anapiga ngumi kama Donnie Yen.

Macho ya Iris yakawa makini zaidi kwa Donnie Yen wa Arusha ambaye naye bila uoga, alifyatuka kama risasi na kuruka teke la juu ambalo Iris alilikwepa lakini kijana yule ni kama alijua kuwa litakwepeka teke lake, akawa karusha ngumi ya haraka ambayo ilimkuta Iris kwenye shavu la kulia. Donnie Yen akatua chini kwa sarakasi ndogo lakini haikuwa kama alivyofikiria, Iris alikuwa amekwishafika nyuma yake na akamnyanyua jamaa yule kwa roba kali. Jamaa akawa ananing’inia juu kwa roba ya mkono mmoja. Lakini katika hali ya kushangaza, yule dogo mwenye chupa ya mvinyo alitokea kwa nyuma yake na kumtwanga Iris chupa ile ya mvinyo hadi ikapasuka.

Iris akamuacha Donnie Yen na kumtazama aliyemtwanga na chupa. Akamuona dogo yule na kipande cha chupa ambacho alitaka kukitumia kama silaha. Iris akamuwahi na kumshika mkono wenye chupa kisha akauminya hadi dogo akaiachia chupa ile, kisha akampa kofi zito lililomfanya apige kelele kama kafiwa.

Kelele hiyo ikawafanya wale vijana wengine wasogee na kuanza kufanya vurugu lakini Iris aliweza kuwamudu kwa kuwakamata na kuwatengua mikono yao. Ilikuwa ni kimuhe muhe ndani ya ukumbi ule wa starehe. Aliyejaribu kumpiga ngwara, Iris alimkanyaga hukohuko chini na kusababisha maumivu makali katika miili yao.

Dakika tano zilitosha kwa Iris kuwafanya wale vijana wawe wamekamata mikono yao kwa maumivu makali sana. Akamuendea yule kijana aliyechukua pesa zake na kuzitoa kule alipoziweka.

“Nilikwambia, chukua na ondoka, ukajifanya unajua. Sasa umekosa vyote.” Akamaliza kwa kumtisha kama anampiga ngumi ya uso, kijana yule akaziba uso na Iris hakupiga usoni bali kwenye mkono alioutengua. Kilio kikamzidi kijana aliyechukua hela.

Akamfata Donnie Yen ambaye alikuwa kakamata shingo yake na anagugumia kwa maumivu makali ya roba mbaya ya kijeshi.

“Wafundishe vijana wako tabia njema badala ya huu upuuzi.” Akamaliza kwa kumpiga kofi zito Donie Yen. Akasimama na kuanza kuondoka eneo lile akiacha ukumbi mzima unampigia makofi.

“Kapiga wababe wa Arusha leo.” Sauti za baadhi ya watu zilisikika lakini Iris hakuzifatilia na badala yake akaenda hadi kwa Limasi.

“Upo salama Limasi?” Akamuuliza, na mwanadada yule badala ya kujibu, alimkumbatia Iris.

“Nipo salama Iris.” Akajibu kwa sauti ya chini na wakati huo, Timasi alisogea hadi eneo la tukio na kuwataka waondoke haraka kabla ukumbi hujajaa wahuni wengine.

Safari ya watatu wale iligotea nyumbani kwa Idris ambapo Timasi na Limasi walianza kuongea haya na yale hasa kuhusu vurugu ambazo zilitokea kwenye ukumbi. Maongezi yalikuwa ya huruma na saa nyingine ya kufurahisha hasa kwa sababu hakuna aliyedhurika sana.

“Idris, niliona yule dogo alikupiga kwa chupa, vipi kakupa jeraha?” Akauliza Timasi huku anaenda pale alipokuwepo Idris na kutaka kumtazama kama alipatwa na jeraha lolote lakini Idris alikataa sana kuonesha sehemu ambapo alipigwa kwa chupa kwa sababu palishajirudisha katika hali yake muda mrefu sana.

“Hapana Timasi, nipo salama tu! Kuwa na amani.” Idris aliongea hayo kwa haraka huku anaelekea lilipo jokofu la vinywaji na kutoa kinywaji chake. “Mtatumia vinywaji gani jamani?” Akauliza Idris.

“Hatuna hata hamu ya vinywaji, tunaomba kwanza twende nyumbani tu! Siku nyingine tutakuja kukutembelea.” Akajibu Timasi.

“Basi hamna shida. Na ni tayari usiku sana. Ngoja niwapeleke.”

“Sawa Idris.” Majibu hayo yakawafanya vijana wale watoke ndani ya jengo mwanana na la kifahari la Idris na kwenda kwenye gari ambalo liliwapeleka nyumbani wanapoishi Timasi na Limasi.

“Usiku mwema Idris.” Akaaga Timasi huku anashuka ndani ya gari la Idris huku akimuacha dada yake akiwa bado kakaa ndani, sehemu ya mbele ya gari lile.

“Nawe pia Timasi.” Akajibu Idris na Timasi akawaacha wawili ndani ya gari.

“Idris…” Akaita kwa kusua kidogo Limasi lakini aliendelea na kilichombakiza ndani ya gari la Idris. “Kwanza naomba unisa….” Kabla hajasema maneno hayo, Idris alimuwahi na kumuwekea mkono wake mdomoni akikamkataza asiseme neno alilokusudia.

Limasi akamuangalia Idris kwa macho ya aibu na wakati huo taratibu Idris alitoa mkono wake na kisha kwa pamoja wakabaki wanaangaliana kwa macho fulani ambayo yalielezea ni nini kinachotaka kutokea.

Taratibu Iris alianza kusogeza kichwa chake kwenye kichwa cha Limasi. Limasi bado alikuwa hajafanya maamuzi sahihi ya kwamba naye asogee au abaki palepale. Mawazo hayo ndiyo yaliyomfaya ajikute kaganda hapohapo hadi kichwa cha Iris kikamfikia na kujikuta analambwa midomo yake na ulimi wa Iris. Hapo ndipo alishtuka na kutoka kwenye mawazo yake ya nini afanye na kisha akatanua midomo yake mitamu hata kwa kuiangalia, na kuruhusu ulimi wa Iris uzame ndani zaidi ya midomo yake. Wakajikuta wameingia kwenye dunia nyingine tofauti sana. Dunia ambayo iliwasisimua kuanzia nywele hadi kucha, visogo hadi visigino.

Ndimi zao ziliendelea kubadilishana nafasi kwenye vinywa vyao na wakati huo Iris alikuwa akijaribu kupapasa pia mapaja ya moto ya mwanadada Limasi. Limasi pia hakuwa nyuma, alikuwa akiingiza vidole vyake kwenye masikio ya Iris na kufanya tendo lile liende kwa utamu wa kipekee. Hadi dakika tatu zinatimia, ndipo waliamua kuachana kugandana midomo yao na kubaki wakiangaliana.

“We’ ni mtamu sana.” Ikabidi Iris ndiye atoe ukimya uliotawala kwa sekunde kadhaa na maneno hayo yalimfanya Limasi aone aibu na kutazama pembeni.

“Id, naomba niende kwanza nyumbani maana hapa naweza kuondoka na wewe nisipoangalia.” Akaongea Limasi akiwa bado na aibu.

“Kwani mimi kuondoka na wewe ni tatizo, Lim?” Naye Idris alifupisha jina la Limasi kama Limasi naye alivyofupisha lake kwa kumuita Id.

“Hapana. Ila kwa leo naweza kugombana na Dada kwa kuondoka wakati tulishafika hadi nyumbani.” Maneno hayo hayakuwa sahihi kwenye kichwa cha Idris, lakini mwanaume yule alielewa kuwa kwa mila za Kitanzania, hamna msichana ambaye huweza kukubali kirahisi siku hiyohiyo akalale na mwanaume, labda iwe biashara yake. Ila unaweza kulala naye au kushinda naye ndani, baada ya siku moja.

“Sawa Lim.” Akakubali Idris. “Kwa hiyo nikufuate lini uje ukae kwangu siku nzima.” Akatupa kete nyingine muhimu.

“Nitakupa taarifa kwenye simu, siwezi kukujibu hapa.” Limasi akaivunja ile kete iliyotupwa na Idris kwa jibu hilo.

“Sawa. Nasubiri mlio wako wa simu.” Idris akakubali huku anampatia kadi yake ya biashara Limasi ambaye aliipokea na kabla hajatoka garini, Idris alimvuta tena na kumuingizia tena ulimi wake kinywani. Wakabadilishana tena ndimi zao na ndipo Limasi aliposhuka garini na kwenda ndani ya nyumba anayoishi.
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 10

“Sawa Lim.” Akakubali Idris. “Kwa hiyo nikufuate lini uje ukae kwangu siku nzima.” Akatupa kete nyingine muhimu.

“Nitakupa taarifa kwenye simu, siwezi kukujibu hapa.” Limasi akaivunja ile kete iliyotupwa na Idris kwa jibu hilo.

“Sawa. Nasubiri mlio wako wa simu.” Idris akakubali huku anampatia kadi yake ya biashara Limasi ambaye aliipokea na kabla hajatoka garini, Idris alimvuta tena na kumuingizia tena ulimi wake kinywani. Wakabadilishana tena ndimi zao na ndipo Limasi aliposhuka garini na kwenda ndani ya nyuba anayoishi.

ENDELEA.

Akiwa na dada yake, Limasi alikuwa haamini kama aliweza kuingia mkenge kirahisi namna ile na kujikuta anachukua busu laini na nyevu la Idris.

“Yaani Tim mimi hata sijui nilikuwaje. Akili yote ilinihama.” Akawa anamuhadithia dada yake huku yupo kitandani kakamata mto wake na Timasi alikuwa akimtazama huku tabasamu hafifu likiupamba uso wake. “Nilikuwa napata msisimko wa ajabu ambao hadi sasa kama siiuelewi vile. Sijui kanipa nini yule mwanaume.” Maneno hayo yakamfanya Timasi naye akae kwenye kitanda cha Limasi na kuzishika nywele za dada yake kwa kuzilaza kwa nyuma.

“Lim. Hayo ndio mapenzi. Ndivyo yalivyo. Uhamisha akili na hupoteza kabisa kujiamini. Na saa nyingine, hata ngvu za mwili. Damu yote hujaa msisimko, unaopoteza nguvu kilaini. Kwa hiyo, usijali sana, ndivyo yalivyo na nafurahi kwa wewe kuingia huko tena. Naimani Idris ni mtu sahihi kwako.” Limasi alimuangalia dada yake kwa macho ya huruma, au tuseme macho ya kudeka.

“Dada naogopa kuumia mimi. Tayari waliniumiza hawa watu, na huyu akiniumiza mimi nitaishi kweli?” Safari hii aliongea huku akitamani kutoa machozi.

“Idris, ndilo chaguo sahihi. Wale wengine kumbuka niliwahi kukuonya. Ila huyu, nakuhakikishia, upo sehemu sahihi na utafurahia mapenzi.” Akajibiwa Limasi.

“Kaniomba niende kwake. Sijui niende lini.”Akachomekea na suala la kwenda kwa Idris.

“Sema anakuja keshokutwa. Ndio anatoka huko Afrika Kusini. Akija na ukasalimiana naye, unaweza kwenda hata mwezi mzima.” Timasi akamuelezea kuhusu kuja kwa mume wake ambaye yupo Afrika Kusini. Na maneno hayo yakampa faraja Limasi kwani alianza kujihisi hali ya kumpenda Idris kwa siku hiyohiyo moja. Hapo ndipo ule usemi wa mapenzi ni kama magugu maji, unapanda asubuhi, saa sita unakuta yametapakaa kiwanja kizima. Unatimia.

“Mwezi nzima. Sasa si bora nihamie.” Akaongea huku anacheka Limasi ambaye kwa muda mfupi tu! Ule ukanjanja wake ulipotea na alikuwa msichana mwenye hekima.

“Kuwa huru Lim. Wala usiogope, Namuamini sana Idris, yaani namuamini kuliko wale wengine. Jitahidi kumtunza awe wako pekee.” Akaongeza maneno mengine ambayo yalikuwa kama msumali wa mwisho kwenye kugongelea hisia za mapenzi kwenye moyo wa Limasi.

Hadithi ikawa hiyohiyo usiku huo hadi wakapitiwa na usingizi wakiwa hapohapo kwenye kitanda cha Limasi.

*****

HUKO Marekani, hali ilizidi kuwawia ugumu baada ya kutompata Idris Iris ambaye alikuwa Tanzania. Walipeleleza kila mahali lakini hawakupata jibu la alipokuwepo Idris. Waliweza kuchukua kamera za barabarani pamoja na za uwanja wa ndege ambao Iris alikwenda, lakini hamna walichoshuhudia. Waliangalia hadi pass za wasafiri wa wiki nzima ndani ya Marekani, lakini hawakumuona Idris wala jina ambalo walihisi ndilo analotumia.

“Mmefikia wapi Ally?” Alifoka kwenye simu Uzo baada ya mkuu wa CIA kupokea simu yake.

“Hamna kitu Uzo. Naomba unipe muda wa kuendelea kumtazama. Na pia kama unavideo za Dokta Ice, naomba uzilete hapa ili tuchunguze mambo kadhaa.” Akaongea Ally.

“Video zipo hadi za siku yake ya kufa. Hilo halina tatizo. Baada ya nusu saa, zitakuja hapo kwa ndege maalumu.” Maneno hayo yalienda sambamba na Uzo kukata simu na kumfanya Ally atoke ofisini kwake na kwenda kusimama kwenye kioo kikubwa ambacho kiliungwa kwenye kompyuta na kuonesha nchi nzima ya Marekani. Wafanyakazi wengi walikuwa wanaendelea kucharaza kompyuta zao, yote ni katika utendaji wao wa kazi.

Wakati hayo yanaendelea kujiri ndani ya Jiji la New York huko Marekani, ndani ya Jiji la Arusha, Tanzania, Idris alikuwa anapapasa kiuno hadhimu cha mwanadada Limasi ambaye alikuwa bado kalala na kajifunika shuka jeupe lililotandikwa kwenye kitanda cha Idris. Usiku mmoja uliopita, ni kelele na lugha za mapenzi ndizo zilizuka kwenye nyumba kubwa ya Idris. Idris aliendelea kuchezea kiuno cha Limasi ambacho kilikuwa kimefunikwa kwa shuka.

“Bwana niache nilalee.” Sauti ya puani ilimtoka Limasi baada ya kuona kashikashi za Idris zinazidi kwenye kiuno chake.

“Kwani nimekukataza jamani.” Naye Idris akajibu.

“Sasa ndio nini hivyo?” Akaendelea kuuliza kwa sauti yake ya puani.

“Basi tu, napenda hivi.” Akajibu tena Idris.

“Je nikifanya hivi.” Limasi akakatika kwa minato na kuzidi kumfanya Idris ahisi yupo dunia nyingine ya kisasa kuliko ile ya sasa hivi ambayo maisha magumu kuliko chuma.

“Ndio maana napapasa hapo kwa sababu jana mambo yaliyokuwa yanatokea, sikuyaelewa kabisa ni kwa sababu gani. Ni hichi ndio kilikuwa kinahusika?” Akafunguka yake Idris.

“Unaonaje kwani?” Safari hii Limasi alinyanyuka kabisa na kufunua shuka walilokuwa wamejifunika. Miili yao ambayo ilikuwa inangozi pekee, ikaonekana na macho yao kwa pamoja walikuwa wanaona jinsi ngozi zao zilivyobarikiwa.

“We’ ni mzuri Lim.” Maneno hayo yakamfanya Limasi asogee kwa Idris na kumlaza kifudifudi, kisha akampandia kwa juu kama farasi na kusogeza kinywa chake hadi kwenye kinywa cha Idris. Tendo la kuchukuliana mate, likapamba moto.

“Id, nimekuheshimu hadi hapa nipo katika kifua chako. Sipo hivi, ila unastahili zawadi hii. Lakini sijui mimi nastahili zawadi gani toka kwako.” Akaongea baada ya kunyonyana ndimi kwa dakika kadhaa huku bado akiwa kamdandia kama farasi.

“Huna unachostahili zaidi ya hicho kidoleni.” Maneno yalimtoka Idris na kumfanya Limasi atazame kwenye kidole chake. Hapo alikutana na pete ndogo lakini imenakwishiwa na jiwe la almasi inayopendeza sana.

“Id?” Akauliza huku katanua midomo yake. “Hii umeweka saa ngapi.” Bado alikuwa haamini. “Na kwa nini……” Akashindwa kumaliza kauli yake baada ya Idris kumvuta kwake na kuanza kunywa kinywaji cha mapenzi. Na mwisho wa yote, walijikuta wakilia kilio cha utamu, utamu ambao uliwafanya waahidiane mambo kibao ambayo sidhani kama wangekuwa hawapo katika dunia hiyo, wangepeana kizembe hivyo.

****

Baada ya mwezi mmoja. Si CIA, FBI wala C.O.D.EX waliokuwa wanataarifa za mwanajeshi aliyepotea (A missing Soldier). Wote walishindwa kutambua ni wapi alipokuwepo Idris Iris. Walichoka na kushindwa kabisa kuendelea kumtafuta mwanaume yule ambaye kwa wakati huo, alikuwa amefanya harusi kubwa sana na kumuoa rasmi Limasi.

Harusi ilikuwa kubwa sana Jijini Arusha. Kila ambaye aliweza kuhudhuria, alikubali harusi ile licha ya upande wa Idris kuwakilishwa na watu wachache sana akiwepo dereva wake pamoja na marafiki wa dereva huyo ambao walisimama kama ndugu wa Idris.

Kwa upande wa Limasi, alikuwa ni mwenye furaha kila mara. Familia za wazazi wake, zilifika katika harusi ile. Na ndugu wa mume wa Timasi nao walifika kunogesha harusi ile iliyokuwa babu kubwa jijini.

“Kwanza napenda kumshukuru MUNGU kwa kunipa pumzi leo, hadi nimesimama hapa kwenu. Bila yeye, mimi si kitu,” Sauti ya Limasi ilipaa baada ya kupewa wasaha wa kuongea. “Pili nimshukuru dada yangu Timasi, yeye ndiye kila kitu kwangu hasa baada ya wazazi wetu kuondoka duniani. Yeye na mumewe, wamekuwa bega kwa bega hadi nikafika hapa leo. Mume wangu Idris, umekuja kuwa wa muhimu sana kwangu. Nakuahidi nitakuheshimu na kukutunza daima. Hilo ndilo kubwa. Wazazi wangu popote walipo, juweni kuwa nawapenda sana na nimewakumbuka sana.” Kimya kikatawala wakati wa maneno hayo machache. “Pia ndugu wa baba na mama na wageni wote mliofika, sina cha kuwapa zaidi ya upendo wangu kwenu. Nawapenda sana jamani.” Watu wote ndani ya ukumbi wakanyanyuka na kupiga makofi kwa maneno hayo machache aliyoyaongea Limasi.

Upande wa mwanaume, pia Idris aliongea na kuhadithia historia ya uongo kuhusu wazazi wake. Wapo walioguswa na wapo waliosikitika sana na kuamua kumpa pole. Hivyo ndivyo harusi ya Idris na Limasi ilivyochukua nafasi katika Jiji la Arusha na wakati huo, mashirika ya kipelelezi na kijasusi, yakiwa yanamtafuta kwa udi na uvumba.

****

“Uzo, umeona hii video?” Ally Ahmed Ally, Mkuu wa CIA, alikuwa anacheza video ambayo ilikuwa inaonesha jinsi Uzo alivyokuwa anamlazimisha Dokta Ice ataje mambo aliyoyafanya. Video hiyo ndio ilionesha kifo cha Dokta Ice pia.

Walikuwa wamekutana kwa mara nyingine ili kupata muelekeo sahihi wa kumsaka Idris na siku hiyo, Ally alikuwa ana ahueni juu ya majibu ya kile wanachokitafuta.

“Hiyo video, mimi nilikuwepo, halafu unaniuliza kama nimeiona tena? We’ vipi bwana?” Alibwata Uzo.

“Yawezekana ukaigiza filamu lakini ukuwahi kuiangalia, ndio maana nimekuuliza.” Akaongea Ally.

“Nenda kwenye mada husika Ally.” Waziri wa Ulinzi ambaye alikuwepo wakati anatoa majukumu ya kumsaka Idris, aliongea na kumfanya Ally asimame na kwenda pale kwenye video.

“Sikilezeni hapa kwa makini alichokiongea Dokta Ice.” Akacheza video ile baada ya kuongea maneno hayo.

“Unajidanganya. Mimi ndiye alpha na omega kwenye kutengeneza hiyo kemikali na kuifanya iwe bora zaidi. Nilioshirikiana nao, wote mliwaua. Bado mimi ni jiwe la pembeni.” Maneno hayo ya kwanza yakasikika toka kwenye video, Wote waliokuwepo kwenye mkutano wakawa kimya zaidi.

“Una uhakika Ice?” Swali la Uzo pia likasika

“Unauliza maembe Tanzania mwezi wa kumi mbili?” Jibu hilo likamfanya Bastian, Mkuu wa FBI kurudisha mgongo wake kwenye kiti.

“Inaonekana unapajua sana Tanzania. Hamna kitu wale, tukiamua kuiangamiza ni dakika tano tu.” Ally hakutaka kuendelea kucheza video ile hadi mwisho bali kuirudisha tena nyuma hadi kwenye maneno aliyoona ni picha ya kuanzia kwenye upelelezi wake.

“Unauliza maembe Tanzania mwezi wa kumi mbili?” Akacheza sehemu hiyo kama mara saba kwa kuirudisha rudisha nyuma. Waliokuwepo kwenye kikao wote wakawa wameelewa anachomaanisha Ally.

“Unataka kusema Soldier yupo Tanzania?” Akauliza Uzo na wakati huohuo, Ally alirudi kwenye kiti chake na kukaa kabla hajajibu.

“Hapana. Nachotaka kukwambia, hivi sasa kaoa pia, huko Tanzania. Na hamna mpango wa yeye kurudi huku.” Akajibu Ally.

“Kwa hiyo unaushauri nini Ally?” Akauliza Waziri wa Ulinzi.

“Tanzania ni marafiki zetu sana. Na hawana uwezo wowote wa kutupiga wala kutengeneza silaha kama ile. Kwa nini tusimuache tu?”

“Yule ni zao letu bwana.” Akawaka Uzo. “Tukimuacha halafu akitoka kwenda nchi nyingine je?” Akazidi kupayuka.

“Kwa hiyo tufanyaje Uzo?” Akauliza Bastian, mkuu wa FBI.

“Tukachukue kilicho chetu.” Akajibu kifupi.

“Kwa sasa anauraia wa Tanzania. Anajulikana ni Mtanzania aliyeishi Marekani. Ni ngumu kumrudisha.” Akatiririka Ally.

“Wapelelezi wa kule wanasemaje kuhusu huyu mwanajeshi wetu?” Akauliza Waziri wa Ulinzi.

“Niliongea na Shirika la Siri la Kipelelezi la kule, wakaniambia wao hawawezi kumkamata mtu wa aina ile kabla ya kupata ruhusa toka kwa Rais wao. Tuliwatumia na video za jinsi mwanajeshi yule anavyofanya kazi. Wakasema watamuangalia asifanye ujinga wowote na yaonekana anatabia njema tu.” Akajibu Ally.

“Hamna tabia njema, yule arudishwe tu huku.” Akabwabwaja tena Uzo.

“Walipoongea na Rais, wakaambiwa kuwa jamaa anatakiwa arudishwe Marekani, kweli. Lakini hawataki waajeshi wetu waende kule kumkamata, wakasema watamkamata wenyewe.” Akaongeza Ally.

“Wataweza. Kuna mtu anaweza kumkamata yule Tanzania?” Akauliza Bastian kwa mshangao.

“Ndio. Rais wao alisema anamtu wake anamuamini sana katika hilo.” Akajibu Ally.

“Mh! Ni nani huyo?” Waziri wa Ulinzi akakaa kitako kusikia mtu ambaye hadi Rais wa nchi anamuamini.

“Wanamuita ‘The Undercover Agent’ au Agent Zero.” Akajibu Ally na kuendelea. “Wanasema huyo ndiye tegemeo la nchi ya Tanzania…” Hakumaliza, Waziri wa Ulinzi akamsitisha maelezo yake.

“Basi, namjua huyo. Hamna kitakachoshindikana.” Waziri akaongea.
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 11


“Wataweza. Kuna mtu anaweza kumkamata yule Tanzania?” Akauliza Bastian kwa mshangao.

“Ndio. Rais wao alisema anamtu wake anamuamini sana katika hilo.” Akajibu Ally.

“Mh! Ni nani huyo?” Waziri wa Ulinzi akakaa kitako kusikia mtu ambaye hadi Rais wa nchi anamuamini.

“Wanamuita ‘The Undercover Agent’ au Agent Zero.” Akajibu Ally na kuendelea. “Wanasema huyo ndiye tegemeo la nchi ya Tanzania…” Hakumaliza, Waziri wa Ulinzi akamsitisha maelezo yake.

“Basi, namjua huyo. Hamna kitakachoshindikana.” Waziri akaongea.

ENDELEA.

IKULU, TANZANIA.

Kijana mwenye mwili mdogo lakini uliyokaa kimazoezi, alikuwepo ndani ya chumba cha mazoezi kwenye Ikulu tukufu ya Tanzania. Alinyanyua vyuma vidogo na vikubwa kwa nyakati tofauti na aliweza kwenda kwenye mashine ya kutafutia pumzi ambayo alikuwa anakimbia juu yake. Jasho lililowanisha fulana yake ya mikono mirefu na rangi ya kijivu lakini hakuonekana kukoma kufanya mazoezi hayo licha ya kuchoka kwake hata kwa kumuangalia.

Alipomaliza mazoezi hayo ya pumzi pamoja na kunyanyua vyuma, alienda kwenye ‘punching bag’ na kuanza kulipiga ngumi pamoja na mateke makali ambayo yalikuwa yanaenda kwa mitindo mbalimbali anayoijua yeye ni wapi alijifunzia.

“Agent.” Ndilo jina ambalo mwanadada wa Ikulu alimuita. Naye bwana yule mfanya mazoezi aliacha kulitwanga lile dubwasha na kumfuata yule kimwana.

“Ndio mrembo.” Akanguruma huku anamtazama yule mwanadada ambaye si haba pia ukimuita mrembo.

“Rais anataka kukutana na wewe.” Akampa ujumbe wake huku bado kasimama mbele ya Agent.

“Wewe hutaki kukutana na mimi?” Agent akamuuliza huku tabasamu lake la kichokozi likipamba uso wake. Yule mwanadada akatazama eneo moja la pembeni na lililojuu ya paa ya Ikulu ile. Naye Agent akatabasamu bila kuangalia eneo lile ambalo lilikuwa nyuma yake. “Huwa sifanyi mazoezi yangu huku kamera zinanitazama. Hiyo kamera nimeshaizima zamani sana. Hapo waliokuwa wananitazama, wanaona napiga ‘push up’ bila kuchoka. Kwa hiyo ondoa shaka mrembo.” Akaongeza Agent safari hii akishika kidevu cha yule mwanadada.

“Bwana wewe, siyo hivyo, mi nimeolewa.” Dada yule aliongea kwa sauti ya chini na ya kuogopa kidogo.

“Sawa, kwani kuolewa kunakataza mimi nisikushike kidevu au kuku…” Agent aliongea hayo huku anasogeza midomo yake na kugusanisha na midomo ya mwanadada yule ambaye naye bila aibu, alianza kutanua midomo yake mwanana kama pipi.

“Agent.” Sauti kali ilisikika kabla hawajafanya kitendo kile cha aibu kwa Mwafrika. Agent akaangalia alipoitwa na wakati huo mwanadada mrembo alipatwa na mshtuko na kuondoka haraka eneo lile. “Wanawake utawaacha lini wewe?” Akauliza tena bwana aliyemuita. Agent akawa anakuna nywele zake za kisogoni bila kujibu lolote.

“Nasikia umeniita mkuu.” Akajitutumua kujibu asichoambiwa.

“Ndiyo. Na nimemtuma huyu mwanadada aje akuite lakini naona ulianza kutumbua mali zisizo zako. Acha ujinga huo Agent, ni wake za watu hawa na wanajiheshimu. Uwe unajiheshimu hata mara moja moja. Siyo kwa kuwa wadhaifu kwa mwili kama wako, basi ndio uwatese kwa tabia zako.” Rais wa Tanzania alionesha wazi kukasirishwa na tabia za Agent.

“Bahati mbaya mkuu.” Alijitetea Agent.

“Nyamaza.” Lakini alikatishwa na sauti kali ya Rais na kumfanya Agent yule anywee kama mchicha ndani ya sufuria lenye maji ya moto. “Twende huku.” Akaongeza Rais akimtaka waongozane hadi ofisini kwake.

“Sijaoga bado.” Akaongea Agent huku anaangalia kilipo chumba cha kujisafi.

“Kwa hiyo ulikuwa unataka uogeshwe na huyu mwanamke?” Akamjibu Rais na Agent hakuwa na jinsi zaidi ya kwenda pale mlangoni aliposimama Rais wake. Akamuona yule mwanadada aliyetaka kumbusu busu nyevu akiwa ndani ya aibu nzito. Akashusha pumzi ya nguvu. “Ni sekretali wangu. Muheshimu kama dada yako au mama yako mdogo, kama unataka, kachukue wapishi huko nje. Huyu sitaki hata umguse.” Akaongeza Rais huku anamtazama Agent.

“Kwa nini sasa Mkuu.” Agent aliongea huku akiwa anataka kucheka kwa sababu ya mkwara wa Rais wake ambao ulionekana kama unambania kuwa na yule mwanadada.

“Kaolewa na mtoto wa kaka yangu. Na hii kazi kaombewa na kaka yangu. Na pia, akiwa na mahusiano na jitu kama wewe, atatoa baadhi ya siri ambazo hupaswi kuzitambua. Umenielewa?” Akajibu Rais na kumfanya Agent anywee hasa kwa ule uhusiano wa Rais na yule mwanadada.

“Samahani dada eeh.” Agent alimuomba msamaha bila kuficha.

“Hilo ndilo la msingi. Sasa nisikie tena hata umemuita lodge zenu za shilingi elfu kumi na tano.” Akaongea tena Rais huku anaingia kwenye ofisi yake.

Agent wakati naye anaingia ofisini, akamtazama tena yule mwanadada, wakakutanisha macho yao na Agent akamkonyeza na kumfanya mwanadada yule atabasamu na kuendelea kucharaza kiparaza cha kompyuta yake.

*****

“Nimekuita hapa kwa jambo moja Agent.” Rais alianza kuongea mbele ya kijana aliyemuita ofisini kwake na wakati huo, ofisi nzima ilikuwa imefungwa na baadhi ya mitambo ya kutotoa sauti nje ilifunguliwa ili kile kinachoongelewa kiwe siri ya wawili tu.

“Ndio mkuu wangu.” Akakaa kitako tayari kwa kumsikiliza mkuu wa Nchi yake.

“Kuna mwanajeshi mpotevu, wao wanamuita ‘a missing soldier’. Lakini wamempatia Tanzania na anaonekana anakula raha zake huko Arusha.” Akaanza maelezo hayo na Agent alionekana akiwa makini kumsikiliza.

“Ni mwanajeshi wa wapi na kwa nini usitume wanajeshi wakamkamata?” Akauliza Agent kabla ya kumuacha Rais kuendelea.

“Ni Mmarekani, na kuhusu swali la pili, ndio nilikuwa nakuja huko.” Akajibu kifupi Rais na kuendelea. “Kwanza kabisa, ni mwanajeshi ambaye aliwahi kufa. Na baada ya kufa, ndipo Dokta mmoja ambaye naye ni marehemu, aliweza kumfufua kwa kumuingizia kemikali za C.O.D.EX.” Akakatishwa maelezo yake na Agent.

“Hizo kemikali si ndizo zile zilifungiwa miaka kumi iliyopita kwa sababu ya kuwaathiri sana Alex na Alex Junior ambao walikuwa wanajeshi tishio sana duniani.” Akaongea Agent.

“Wewe hayo umeyajuaje wakati yalikuwa ni ya siri kubwa?” Akauliza Rais.

“Kuna vitabu, kaviandika Tariq Haji na kaviita C.O.D.EX, vipo vitatu. Vinaelezea kinagha ubagha yote hayo. Ni kama riwaya, lakini nilipofuatilia, haya mambo ni kweli yalitokea.” Akajibu Agent.

“Okay. Ni kweli ulichoongea. Lakini CIA na FBI pamoja na serikali nzima ya Marekani, walifungua tena ile maabara na safari hii walikuwa wanachukua watu waliokwisha kufa hasa wanajeshi wa Kimarekani ambao walifia vitani au wananchi wenye IQ kubwa ili wawasaidie katika kutengeneza silaha.”

“Kwa hiyo huyo mwanajeshi yupo vipi?” Rais akavuta bahasha fulani na kutupa mezani ambapo Agent aliifungua na kuanza kuangalia baadhi ya picha ambazo zilionesha wanajeshi wa C.O.D.EX wakiwa katika mazoezi yao. Walikuwa wanatisha sana kwa wanachokifanya lakini walionekana kutojali wala kuhisi maumivu.

Baada ya picha hizo, Rais pia akampa kijana anayemuamini simu matata sana na kumchezeshea video ambayo ilionesha wale wanajeshi wakiungua na baadae kurudi katika hali yao ya kawaida. Na picha kadhaa za video zile, zilionesha ukatili na silaha zao hatari wanazotumia. Mwili ukamsisimka Agent.

“Hapa kuna kazi kubwa Mkuu.” Akaongea Agent huku anarudisha vile vitu alivyopewa.

“Ndio maana wanajeshi wetu hawawezi. Anahitajika mtu mjanja na mwenye uelewa wa kuwazuia hata kwa sayansi zake. Naye ni wewe.” Rais akatoa jukumu zito.

“Nahitaji kusoma kwanza na sehemu ambapo nitatengeneza baadhi ya silaha zangu.” Akaongea Agent na Rais akamuelekeza kwenye maabara fulani iliyopo ndani ya Ikulu yake. Kisha akamtolea mafaili baadhi ambayo alitumiwa na CIA kwa ajili ya kumtambulisha mtu wanayetakiwa kukamata. Baada ya hapo, akaanza kumuelekeza mambo mengine mengi ambayo alipewa na CIA. Hadi nusu saa inakatika, Agent alikuwa kashiba maneno mengi ambayo yangemuongoza kwenye msako wake.

****

Ndani ya maabara ambayo ilikuwa ndani ya Ikulu, Agent alikuwa kavaa mawani kubwa myeusi na alikuwa anachanganya vitu kadhaa kwenye chungu cha chuma na ambacho kilikuwa kimepata joto kali na kuwa chekundu sana. Kila alipotupia baadhi ya vitu alivyovijua yeye, moto mkali ulifumuaka na kuzidisha joto ndani ya maabara ile ya Kisayansi.

Baada ya kuridhika, alimwagia mchanganyiko ule kwenye sahani moja kubwa na ya bati. Pini ndo go ndogo nyingi sana zikaonekana ndani ya sahani, naye Agent akatabasamu baada ya kufanikisha zoezi lake la kwanza lakini hakuishia hapo, alizimwagia kemikali fulani ambazo zilifanya pini zile zisimame kwenye sahani na kuchongoka zaidi.

Akabofya kiparaza cha kompyuta yake ambayo alikuwa anatembea nayo, na ile sahani ikaanza kuzunguka taratibu kisha kuhama na kwenda sehemu moja ambayo kulikuwa na kijumba kidogo alichokibuni Agent kwa ajili ya shughuli zake za Kisayansi. Kijumba hicho yeye mwenyewe alikiita UHAI. Akimaanisha ni kijumba kinachoweza kuvipa uhai vitu ambavyo havina uhai.

****

Asubuhi iliyofuata, Agent alionana na Rais na kumuelezea kazi yake ilivyokwenda na alimwambia yupo tayari kwa kazi ambayo kamtuma.

“Sawa kijana wangu. Nakuamini.” Rais aliongea kwa tabasamu na kisha akampa simu yake ambayo safari hii, alimtaka aende kuitazamia chumbani kwake kwa sababu yeye hakai tena ofisi sababu ziara ya siku hiyo ya kwenda Tabora kufungua miradi ya treni za angani. “Humo utaona ni wapi mtuhumiwa wako unatakiwa kumpata. Fanya yako leo hii, apatikane. Nishawaambia kuwa kazi ni leo.” Akaongea Rais baada ya kumkabidhi ile simu.

“Sawa Mkuu.” Agent alikubali na kusimama tayari kwa kuondoka ofisini.

“Agent Zero.” Kijana wa Rais akageuka na kumtazama Rais wake. “Kuna zawadi pia kwa ajili yako ukifanikisha hilo, Dola Milioni Moja inakusubiri na yawezekana ikapanda hadi hamsini.” Akampa taarifa mwanana kijana wake na kumfanya Agent atabasamu na kupiga saluti ya kikakamavu. “Nikutakie kheri katika kazi yako.” Akamaliza na Agent Zero kama alivyomuita, akatoka nje ya ofisi.

****

Furaha kubwa ilikuwa imemtawala Idris ambaye kila wakati alijiona mwenye bahati kukutana na Limasi ambaye kama mapenzi alimpa yote mwanaume yule aliyeficha siri nyingi juu yake. Idris akiwa anarudi nyumbani na zawadi kadhaa alizomnunulia mke wake, alisimama njia panda moja ambayo ilikuwa ina mataa ya usalama barabarani. Ilikuwa yapata saa tatu na robo usiku wakati mataa hayo ya usalama yaliposimamisha gari lake.

Aliamua kutumia muda ule mdogo kupekua zawadi kadhaa alizokuwa amemnunulia mpenzi wake. Wakati anafanya hayo akiwa ndani ya gari lake lingine la gharama, kuna gari moja kubwa aina ya scania lilikuwa linatokea upande wa kushoto kwa kasi ya ajabu na ghafla lilikumba gari la Idris na kulipasua katikati kisha ile sehemu inapokaa injini, ililipuka na kusababisha taflani eneo zima la barabara.



ITAENDELEA KESHO
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 12

Kwa kweli niliingia hasira sana maana nilipanga nimmalize pale pale lakini walinzi wake wameleta shobo, nilichomoka nilipo kwa kasi ya hali ya juu sana huku nikifyatua risasi lakini kwa vile wale walinzi hawakuwa miongoni mwa nnaotaka kuwaua basi niliwapiga risasi za miguu tu na kukimbilia ilipo gari yangu na kuondoka kwa kasi.

Niliwasha computer na kuitrack gari ya Jones kwa sababu nilikuwa nimeiwekea GPS tracker hivyo nilijua imeelekea wapi na mimi bila kupoteza muda niliifata, kwa mwendo wa kasi nilifanikiwa kuwa fikia karibu. Nilishusha kioo na kulipiga tairi la gari ya Jones risasi hivyo likapoteza muelekeo na kupinduka, nilishuka kwenye gari yangu na kuelekea ilipo gari hiyo na kumtoa Jones kwa bahati nzuri alikuwa hai. Nimuingiza kwenye gari yangu naa kuondoka nae, nilitafuta sehemu nzuri ya kujificha ili nipate muda mzuri wa kupata majibu yangu. "David hivi imekuaje ukawa hai leo" aliuliza baada kuzinduka, "Jina langu ni Allen James" nilongea kwa hasira, "ah kumbe wewe mwenyewe hukumbuki kitu" aliongea huku akitabasamu, "na ndio maana uko hai mpaka sasa kwa sababu nataka kujua ukweli kwanini mnasema nimekufa" nilimjibu.



"Na unadhani nitakwambia chochote" alinijbu na kunitemea mate usoni, "nadhani unafahamu kuwa ninapo taka kujua kitu chochote kutoka kwa mtu ni lazima nikijua kwa hali yeyote ile" niliongea huku nikijifuta yale mate. Nilifungua begi langu na kutoa kisu chembamba kisha nikavuta kiti na kuka mbele yake. "naona kwa njia ya kiungwana umeshindwa kutoa ushirikiano sasa itabidi niukwangue ukweli kupitia maumivu" niliongeaa hilo na kwa nguvu zote nilimkita kisu cha paja na kufanya kama nachokonowa hivi. Alipiga kelele lakini ni kama alikuwa ananihamasisha niendelee kumtoboa toboa."nambie ukweli", "sahau" alinijibu, nilitoa pini ngumu na nyemba zenye urefu sentimita saba. "sawa basi tuendelee na mchezo wetu, mimi ntaendelea kukutesa na wewe goma hivo mpaka mmoja wetu atakaposarenda amri". Nilitoa sindano ya ganzi na kumchoma ili asisikie maumivu wakati naziiningiza pini hizo kwenye mwili wake.

Taratibu nilianza kuingiza pini kwenye kidole cha kati cha mkono wa kulia, niliendelea na zoezi hilo mpaka nilipohakikisha hakuna kidole nilicho sahau kunazia vya mikono mpaka vya miguu. "najua saa hivi huhisi kitu lakini baada ya dakika mbili hivi utaona kilichomtoa nyoka pangoni kama ni sauti nzuri ya mrembo au maji ya moto" niliongea kisha nikakaa kimya nikisubiria kazi iyanze. Naam baada dakika mbili alianza kukunja uso na machozi yalianza kumtoka bila kupenda, alianza kutetemeka na kijasho chembamba kilianza kumchuruzika katika paji la uso. Alianza kupiga kelele, "hazitakusaidia hizo" nilimjibu huku nikicheka. Hata sikujua ukatili ule na adhabu za aina ile nimejifunza wapi. "sawa nitatoa ushirikiano, naapa naomba unitoe hizi pini" alilalamika kwa nguvu, "namna hiyo ungekubali mapema yasingekufika haya" nilimchoma tena sindano ya ganzi kukata maumivu..
 
C.O.D.EX. 1 ................... SEHEMU YA 13

Alianza kuongea kwa kusema "wewe ulikuwa ni mmoja kati ya watu hatari sana ambao walipata mafunzo kupitia serekali ya USA, katika kitengo cha siri ndani ya C.I.A. Lengo la kupewa mafunzo hayo ilikuwa ni kuwaondoa katika ramani wale ambao walioonekana kumuandama raisi na hiyo ndio ilikuwa kazi yako. Ulifika wakati mpaka raisi akawa anakuogopa kutokana kujua mambo mengi ya siri hivyo akatoa amri na wewe pia upotezwe katika ramani. Mimi ndie niliepewa jukumu hilo na nilihakikisha natimiza wajibu wangu kama mtumishi wa serekali kwa kukuuwa na nilifankiwa lakini nashangaa leo kuona uko hai" alimalza kuongea na kuniangalia. Wakati huo nilikuwa nimevimba kama mbogo aliejeruhiwa, nilisimama "asante kwa ushirikiano wako" nilitowa bastola ndogo na kuweka saini katika paji lake la uso kisha nikatokomea zangu.

Nikiwa natembea uliingia ujumbe "tunajua kwa sasa una maswali mengi hayana majibu, lakini kila kitu kitu kitakaa sawa baada kupata kumbukumbu zako zote, Panda ndege uje Miami". Bila kupoteza muda nilielekea uwanja wa ndege na kukata ticket ya miami, baada masaa mawili niliingia kwenye ndege na safari ya kuelekea Miami ikaanza. Baada muda mrefu wa kukaa angani hatimae ndege ilitua mjini Miami na nilipotoka tu uwanja wa ndege ukaingia ujumbe. "Katika maegesho ya gari kuna gari aina ya Macerati nyekundu, chukua na ufate ramani" nilekea kwenye maegesho na kuchukua gari hiyo na kuondoka, Nilifata ramani mpaka nilipofika kwenye nyumba ambapo ndipo ilipokoma ramani hiyo. Mlango ulikuwa umefungwa lakini haukutiwa loki, niliingia ndani na kushangaa maana kulikuwa hakuna kitu. Uliingia ujumbe mwengine "sogea mpaka ilipo alama nyekudu kweny ukuta na uweke kiganya chako" nilisogea kama nilivoelekezwa na kuweka kiganja katika alama hio. Ghafla ukuta ulisogea na lifti ikafunguka, niliingia na lifti ikajifunga na kuanza kuteremka chini kwa kasi ya hali ya hali ya juu sana.

Ghafla ilisimama na mlango ukafunguka, mwangaza mkali uliokuwemo ndani ya chumba hicho uliniumiza macho kwa dakika kadhaa kabla kuzoea hali ile. "karibu Mr Allen James" niliskia sauti ikinikaribisha, "jina langu ni Albiana Master Computer" iliendelea, nilijiuliza sauti hiyo inatokea wapi maana sijaona mtu humo ndani. "mimi ni compter na ndie niliekuwa nawasiliana na wewe muda wote" nilichoka baada kusikia hivo. "sawa mimi nimeshafika na nataka unieleze kila kitu kinacho nihusu" niliongea kwa kujiamini. "sina haja ya kukuelelza kwani muda mfupi tu utajua kila kitu" ilinijibu computer hiyo, "hatua kadhaa mbele yako kuna mlango umeandikwa PROJECT CODE X, ingia ndani ya chumba hicho". Nilisogea mpaka kwenye mlango huo na kuufungua kisha nikaingia. "vua nguo zako zote na ulale kwenye hicho kitanda" iliniabia na mimi nikafanya hivo. Baada ya kulala tu taa zote humo ndani zikazimika na ghafla ikatoka mikanda na kunizunguka kuotoka upande wa kulia wa kitanda kuelekea kushoto na kisha kitanda kikaingia kwenye mashine fulani hivi.
 
2.

Nilifika chumbani kwangu kitu cha kwanza niliingia bafuni nikaoga maana uchovu ulikuwa ukinitafuna. Nilirudi ndani na kufungua kabati, macho yangu yalikutana na suti za bei mbaya tu. Nilichagua moja na kuvaa baada kuona nishapendeza nilikaa kitandani nikifiria mambo mengi yaliotokea siku ya nyuma. Wakati nikiwa mbali kwenye mawazo ghafla niliskia simu ikiita, niliangaza wapi ilipo na kwenda kuichukua. Nilipoipokea ukaingia ujumbe uliosema "kaa tayari ukisubiria maelekezo mengine". Ukaingia ujumbe mwengine "katika kabati kuna begi, litoe na fuata maelekezo utakayoyakuta".
Nilifungua kabati na kutoa begi nikalifungua, nilikuta picha ya mzee mmoja nyuma ikiwa na ujumbe "chukua sniper iliokuwepo humu na uhakikishe huyu mtu anakwenda kuzimu". Niliiangalia ile sniper nikajikuta natabasamu, nilibeba lile begi na kuchukua ile simu kisha nikatoka. Nilipofika nje uliingia ujumbe mwengine "huyo mtu anapatiakana mji wa Alexandria na kazi ikamilike ndani ya masaa kumi na sita, chukua hiyo gari nyekundu mbele yako". Niliingia kwenye ile gari na safari ya kuelekea Alexandria ikaanza. .
Nilipofika tu uliingia ujumbe ulionielekeza alipo, nilifika sehemu ya tukio na kupanda katika jengo moja refu kidogo lilikuwepo pembeni ya jumba alilokuepo huyo mlengwa. Nilipofika juu nilitoa sniper na kuiunga baada kukamilisha zoezi hilo nilijweka sehemu nzuri na kuanza kumtunga. Kwa msaada darubini ya sniper nilimuona vizuri na hapo nikafyetua risasi ilioingia kichwani na kusambaratisha ubongo. Sikuwa na haja ya kuichukua ile sniper, nilitoa bomu dogo na kulitega pale kisha nikaondoka. Iliripuka na Ushahidi ukapotea, nilipofika tu chini nilikaribishwa na risasi kadhaa hapo nikajuwa nimeshtukiwa.
Nilitoa bastola mbili ndogo na kuanza kujibu mashambulizi huku nikikoswa na risasi kadhaa. Kutoka kwa mlango huo ilikuwa haiwezekani nilirudi ndani na kuanza kutafuta mbinu za kutoka humo maana hata risasi zilikuwa zimeniishia. Mara walianza kuingia ndani,nilijibanza sehemu nikajisemea atakaepita kwanza ni halali yangu. Mara mmoja akapita nilimvuta ndani na kumvunja shingo, nikachukua bastola yake na kukimbia. Wakati nikiwa katika mapambano hayo uliingia ujumbe mwengine ukinitaka niondoke nchini marekani nielekee shanghai china. Nilifanikiwa kutoka nje na kuelekea ilipogari yangu na kutokomea, nilifanikiwa kuwatoroka. Moja kwa moja nilielekea uwanja wa ndege na kukata tiket ya ndege inayofuata kuelekea zangu Shanghai China. Muda wa kupanda ulifika na safari ya Shanghai ilianza na kwa jinsi nilivyokuwa nimechoka usungizi ulinichukua, usingizi uliombatana na ndoto mbaya za mateso ya hali ya juu sana.
*****
"jina lako nani" aliendelea kuniuliza uku akinipiga mgumi kadhaa za tumbo "Allen James" nilijibu lakini bado hakukubali. Mara nikamsikia akisema leteni mashine ya shot, haukupita muda ililetwa mashine hiyo. Aliiwasha na kutaka kunipiga shoti, ghafla nilishtuka kutoka usingizini huku jasho likinitoka, nilimuita muhudumu nikamwambia anipe kinywaji cha baridi baada hapo nilitulia nikiwaza ile ndoto. Kwa sababu ilikuwa ni ndoto tu nikaona bora niipoteze.
kwakwel acha tu iwe ndoto maana daah
 
Nzuri sana ila muwe unakuja pia na simulizi za kijeshi sio kila siku za kipolisi na kijasusi tuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom