Xav Emmanuel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2018
- 214
- 315
MATUNI
“NAFSI MOJA SEHEMU TATU TOFAUTI”
By Author Xav
Simulizi; “MATUNI” (01)
Mtunzi; Author Xav
#StarXavEntertainment
====================
-UTANGULIZI-
NI Tumaini, binti ambaye anarithishwa uchawi akina na lika la miaka kumi na sita tu. Licha ya kuhusishwa na mambo ya kishirikina na Bibi yake Bi Sembe toka kuzaliwa kwake.
TUNI ni uchawi ambao unaabudiwa na watu waliopo duniani… wananguvu ya kutenga na kutengua kauli yoyote ya binadamu. Kuishi kwao kunategemea na chakula ambacho ni mwili wa Binadamu…
Swali ni Je; Kwanini MATUNI??
NA HII NI SEHEMU YA KWANZA!..
“Mjukuu wangu Tumaini bin Makungu, Leo ni siku pekee kabisa ambayo maelfu ya dakika yalisubiri kwa hamu kubwa. Tumaini nataka nikufanye moja kati ya nguzo kuu ya ‘TUNI’, najua hunielewi maana yake, ila usiache kunisikiliza.
Nilikua nimeishi maisha ya utwa wa kufa na kupona na wewe Tumaini.., sikuwa na nidhamu hii ya dunia ambayo wengi hujisifia kuwa wao ni wa muhimu sana kuliko sisi.
Mjukuu wangu, ‘Tuni’ ni moja ya dunia ambayo wachache wanaishi kwa ajili ya wengi. Dunia ambayo maamuzi kuchukuliwa mkononi ni moja kati ya sheria, kuua na kumbadilisha mtu ni jambo ambalo lipo na limewekwa katika sheria ya Tuni, mjukuu wangu, tuni ina katiba ambayo huongoza watu wa huko wasivuke mipaka ya dhehebu lao. Nashukuru Mungu tuni imenisaidia kusuluhisha matatizo yangu mbalimbali na kunifanya niishi kwa faraja hadi leo.
Natamani nikwambie mengi sana lakini leo nitajibu tu maswali macheche ambayo ulikuwa ukiniuliza kila siku, maswali yako yalinifanya nikasilike kwa mda, nicheke kwa mda, na kuna kipindi vyote vinatokea kwa pamoja, yaani sikitiko na furaha vinakuja kwa pamoja.
Mjukuu wangu, naomba nikupe kwanza ghadhabu ya muda mfupi kwa kukuambia ukweli kuusu uzao wako, yaani baba na mama yako mzazi. Najua hujawahi kuwaona.. Nataka nikuambie mjuu wangu.
Mwanangu, hapa nilicheka sana ulipokuwa unaniuliza mara kwa mara, “Yupi Baba…? Wapi Mama….?”, hasa pale ambapo kuna mda ulisahau kabisa na kuniita mimi mama yako.
“Hahahahahaha”, nacheka ya mwisho kwani ukweli wa maisha ya wazazi wako yako katika kifua chako Tumaini. Labda tu niseme kuwa, hukufanikiwa kukutana na wazazi wako toka umeeanza kujielewa sababu kubwa ni TUNI. Si kila fumbo nikufumbulie, mengine kazana mwanangu... Moyo wako utakufafanulia jinsi ambavyo maisha yanaenda. polepole tu utaju.
Tuma Mwanangu!!, Tuni ilinifanya nianze kumpoteza Baba yako pindi tu mama yako alipopokea mimba yako, nakumbuka katika Tuni ilikuwa ni zamu yangu kutoa mtu kwa ajili ya watu wengine, yaani niue mtu ambaye yu na muunganiko na familia yangu.
Basi nikaamuliwa nimtoe mama yako!, Lakini kwa kuwa na mimi nina nguvu nikageuza mambo na kushawishi kutolewa kwa baba yako. yaani baadaya kumtoa mama yako, nikaamua kumtoa baba yako mzazi, mda ukafika baba yako akapotea duniani, tukazika, tukasahau.
Hmmm!!!, Tumaini Usitikise kichwa mwanangu, utaelewa tu. Hiyo ndio Tuni. Basi tukaishi weee!, hadi mwaka ukafika ambapo nawe mjukuu wangu kipenzi Tumaini ulikuwa umeshazaliwa. Ikawa tena zamu yangu ya kutoa mtu katika familia, kila nikiangalia hivi sioni watu wengine wa kuwatoa zaidi ya Mama yako na wewe mjukuu wangu Tumaini ambaye bado moyo wangu ulikuwako upande wako. nilikuwa na nafasi mbili tu sasa. ufe wewe au mama yako.. Tumaini.!!.
Kwa safari hii, mbio zangu za kukutetea zikagonga mwamba. “Bi Ndaku” ambaye ni mkuu wa matuni hadi sasa alitoa oda ya kutolewa wewe. Nikagoma katakata lakini sikuweza kutengua.
Basi ukaletwa mbele ya Tuni, sadaka ikaanza lakini mtoa tuni akasema haikua sawa kutolewa mtoto ambaye bado hajajielewa vizuri na inaashiria kuwa mtoto huyo ananguvu kubwa ya kuiongoza Tuni, kwa maana ukitunzwa vizuri waweza kuwa kiongozi wa Tuni, yaani wewe Tumaini.
Basi ukaondolewa pale na zoezi la sadaka likaamia kwa mama yako. Lakini pia mama yako naye hakutolewa sadaka badala yake akatolewa mtu mwingine ambaye alifanya kosa lisilovumilika. Mama yako akauzwa koo nyingine.
Tulikuwa na tamaduni ya kubadilishana watumwa ambao wamenusulika kifo. mama yako akapelekwa koo nyingine ambayo kwa sasa ni mahasimu mno na koo yetu ya Tuni. Lakini duniani tulishamzika mama yako, hayupo!. Duniani Tumemzika na Tuni hayupo.. yu koo nyingine.
Ukawa mwisho wa wewe kuwaona wazazi wako, ulikuwa bado kachanga sana. Hakuna unachokielewa.
Toka hapo umeishi maisha ya kutomjua mama yako wala baba yako, wewe na bibi, bibi na wewe. Umekula vyakula vingi usivyovifahamu, vingi sana matuni….” BIBI Tumaini akaacha kuongea na akainamisha kichwa chini kwa aibu, akafungua sehemu ya kanga katika mwili wake na kufuta machozi, baadae akainuka na kuendelea na maongezi. aliendelea kuongea na mjukuu wake.
“TUMAINI umekula vingi bila kufahamu, siwezi taja vyote ila vingi ni mchanganyiko wa Damu za watu, nyama za watu, makohozi na hata vinyesi vya binadamu na hiyo ndio dawa ya Tuni mwanangu, uoni ulivyo imara sasa. Kila mtu anakushangaa, hehehehehe malezi ya bibi hayo...” BIBI Tumaini aliachia cheko fupi kabla ya kuendelea. Bibi Tumaini alibobea katika mambo ya furaha na huzuni kwa pamoja. alivichanganya vyote viwili bila wasiwasi. Alicheka tu.
“Sitaki mengi niongee mwanangu, ninachotaka ni kuwa nimekupa tu mwanga wa sehemu ya kuanzia, nakuacha mwanangu, yote utayajua kwa uwezo wako, wewe ni mtu mkubwa sana, hata mimi ni mdogo kwako ndio maana naamua kupotea ili nikupishe katika majukumu yako ya kuendeleza Tuni. Mimi ninapotea Tuma..
Labda niishie hapo kwa kukupa maneno machache kabla ya kukukaribisha kwenye TUNI. Mwanangu, Tuni ni Uchawi, tena uchawi ambao umeshindikana, haupo katika dunia hii ya karaha na shida nyingi.
Ukiwa huko ni raha tu mwanangu, hakuna kero wala nini, utacheza, utakula, utafanya kila kitu bure, sadaka ni kitu cha kawaida tu. Hakuna haja ya shule ukiwa TUNI, hakuna haja ya KANISA ukiwa Tuni, hakuna haja ya kubishana na mtu anaekukwaza; wote unawapoteza tu.
Sasa mwanangu naona koo langu lauma sasa kutokana na umri wa maneno mengi yaliyonitoka kwa pupa bila komo. Naomba niishie hapo kwa kukuambia jambo la mwisho na la uhakika zaidi. Mwanangu kuanzia leo mwanangu, jina lako ambalo litakujulisha uko uendako ni MATUNI, futa kabisa neno Tumaini ukiwa huko.....!. ukiwa Tuni wewe ni Matuni!.
ITAENDELEA..
Sent using Jamii Forums mobile app
“NAFSI MOJA SEHEMU TATU TOFAUTI”
By Author Xav
Simulizi; “MATUNI” (01)
Mtunzi; Author Xav
#StarXavEntertainment
====================
-UTANGULIZI-
NI Tumaini, binti ambaye anarithishwa uchawi akina na lika la miaka kumi na sita tu. Licha ya kuhusishwa na mambo ya kishirikina na Bibi yake Bi Sembe toka kuzaliwa kwake.
TUNI ni uchawi ambao unaabudiwa na watu waliopo duniani… wananguvu ya kutenga na kutengua kauli yoyote ya binadamu. Kuishi kwao kunategemea na chakula ambacho ni mwili wa Binadamu…
Swali ni Je; Kwanini MATUNI??
NA HII NI SEHEMU YA KWANZA!..
“Mjukuu wangu Tumaini bin Makungu, Leo ni siku pekee kabisa ambayo maelfu ya dakika yalisubiri kwa hamu kubwa. Tumaini nataka nikufanye moja kati ya nguzo kuu ya ‘TUNI’, najua hunielewi maana yake, ila usiache kunisikiliza.
Nilikua nimeishi maisha ya utwa wa kufa na kupona na wewe Tumaini.., sikuwa na nidhamu hii ya dunia ambayo wengi hujisifia kuwa wao ni wa muhimu sana kuliko sisi.
Mjukuu wangu, ‘Tuni’ ni moja ya dunia ambayo wachache wanaishi kwa ajili ya wengi. Dunia ambayo maamuzi kuchukuliwa mkononi ni moja kati ya sheria, kuua na kumbadilisha mtu ni jambo ambalo lipo na limewekwa katika sheria ya Tuni, mjukuu wangu, tuni ina katiba ambayo huongoza watu wa huko wasivuke mipaka ya dhehebu lao. Nashukuru Mungu tuni imenisaidia kusuluhisha matatizo yangu mbalimbali na kunifanya niishi kwa faraja hadi leo.
Natamani nikwambie mengi sana lakini leo nitajibu tu maswali macheche ambayo ulikuwa ukiniuliza kila siku, maswali yako yalinifanya nikasilike kwa mda, nicheke kwa mda, na kuna kipindi vyote vinatokea kwa pamoja, yaani sikitiko na furaha vinakuja kwa pamoja.
Mjukuu wangu, naomba nikupe kwanza ghadhabu ya muda mfupi kwa kukuambia ukweli kuusu uzao wako, yaani baba na mama yako mzazi. Najua hujawahi kuwaona.. Nataka nikuambie mjuu wangu.
Mwanangu, hapa nilicheka sana ulipokuwa unaniuliza mara kwa mara, “Yupi Baba…? Wapi Mama….?”, hasa pale ambapo kuna mda ulisahau kabisa na kuniita mimi mama yako.
“Hahahahahaha”, nacheka ya mwisho kwani ukweli wa maisha ya wazazi wako yako katika kifua chako Tumaini. Labda tu niseme kuwa, hukufanikiwa kukutana na wazazi wako toka umeeanza kujielewa sababu kubwa ni TUNI. Si kila fumbo nikufumbulie, mengine kazana mwanangu... Moyo wako utakufafanulia jinsi ambavyo maisha yanaenda. polepole tu utaju.
Tuma Mwanangu!!, Tuni ilinifanya nianze kumpoteza Baba yako pindi tu mama yako alipopokea mimba yako, nakumbuka katika Tuni ilikuwa ni zamu yangu kutoa mtu kwa ajili ya watu wengine, yaani niue mtu ambaye yu na muunganiko na familia yangu.
Basi nikaamuliwa nimtoe mama yako!, Lakini kwa kuwa na mimi nina nguvu nikageuza mambo na kushawishi kutolewa kwa baba yako. yaani baadaya kumtoa mama yako, nikaamua kumtoa baba yako mzazi, mda ukafika baba yako akapotea duniani, tukazika, tukasahau.
Hmmm!!!, Tumaini Usitikise kichwa mwanangu, utaelewa tu. Hiyo ndio Tuni. Basi tukaishi weee!, hadi mwaka ukafika ambapo nawe mjukuu wangu kipenzi Tumaini ulikuwa umeshazaliwa. Ikawa tena zamu yangu ya kutoa mtu katika familia, kila nikiangalia hivi sioni watu wengine wa kuwatoa zaidi ya Mama yako na wewe mjukuu wangu Tumaini ambaye bado moyo wangu ulikuwako upande wako. nilikuwa na nafasi mbili tu sasa. ufe wewe au mama yako.. Tumaini.!!.
Kwa safari hii, mbio zangu za kukutetea zikagonga mwamba. “Bi Ndaku” ambaye ni mkuu wa matuni hadi sasa alitoa oda ya kutolewa wewe. Nikagoma katakata lakini sikuweza kutengua.
Basi ukaletwa mbele ya Tuni, sadaka ikaanza lakini mtoa tuni akasema haikua sawa kutolewa mtoto ambaye bado hajajielewa vizuri na inaashiria kuwa mtoto huyo ananguvu kubwa ya kuiongoza Tuni, kwa maana ukitunzwa vizuri waweza kuwa kiongozi wa Tuni, yaani wewe Tumaini.
Basi ukaondolewa pale na zoezi la sadaka likaamia kwa mama yako. Lakini pia mama yako naye hakutolewa sadaka badala yake akatolewa mtu mwingine ambaye alifanya kosa lisilovumilika. Mama yako akauzwa koo nyingine.
Tulikuwa na tamaduni ya kubadilishana watumwa ambao wamenusulika kifo. mama yako akapelekwa koo nyingine ambayo kwa sasa ni mahasimu mno na koo yetu ya Tuni. Lakini duniani tulishamzika mama yako, hayupo!. Duniani Tumemzika na Tuni hayupo.. yu koo nyingine.
Ukawa mwisho wa wewe kuwaona wazazi wako, ulikuwa bado kachanga sana. Hakuna unachokielewa.
Toka hapo umeishi maisha ya kutomjua mama yako wala baba yako, wewe na bibi, bibi na wewe. Umekula vyakula vingi usivyovifahamu, vingi sana matuni….” BIBI Tumaini akaacha kuongea na akainamisha kichwa chini kwa aibu, akafungua sehemu ya kanga katika mwili wake na kufuta machozi, baadae akainuka na kuendelea na maongezi. aliendelea kuongea na mjukuu wake.
“TUMAINI umekula vingi bila kufahamu, siwezi taja vyote ila vingi ni mchanganyiko wa Damu za watu, nyama za watu, makohozi na hata vinyesi vya binadamu na hiyo ndio dawa ya Tuni mwanangu, uoni ulivyo imara sasa. Kila mtu anakushangaa, hehehehehe malezi ya bibi hayo...” BIBI Tumaini aliachia cheko fupi kabla ya kuendelea. Bibi Tumaini alibobea katika mambo ya furaha na huzuni kwa pamoja. alivichanganya vyote viwili bila wasiwasi. Alicheka tu.
“Sitaki mengi niongee mwanangu, ninachotaka ni kuwa nimekupa tu mwanga wa sehemu ya kuanzia, nakuacha mwanangu, yote utayajua kwa uwezo wako, wewe ni mtu mkubwa sana, hata mimi ni mdogo kwako ndio maana naamua kupotea ili nikupishe katika majukumu yako ya kuendeleza Tuni. Mimi ninapotea Tuma..
Labda niishie hapo kwa kukupa maneno machache kabla ya kukukaribisha kwenye TUNI. Mwanangu, Tuni ni Uchawi, tena uchawi ambao umeshindikana, haupo katika dunia hii ya karaha na shida nyingi.
Ukiwa huko ni raha tu mwanangu, hakuna kero wala nini, utacheza, utakula, utafanya kila kitu bure, sadaka ni kitu cha kawaida tu. Hakuna haja ya shule ukiwa TUNI, hakuna haja ya KANISA ukiwa Tuni, hakuna haja ya kubishana na mtu anaekukwaza; wote unawapoteza tu.
Sasa mwanangu naona koo langu lauma sasa kutokana na umri wa maneno mengi yaliyonitoka kwa pupa bila komo. Naomba niishie hapo kwa kukuambia jambo la mwisho na la uhakika zaidi. Mwanangu kuanzia leo mwanangu, jina lako ambalo litakujulisha uko uendako ni MATUNI, futa kabisa neno Tumaini ukiwa huko.....!. ukiwa Tuni wewe ni Matuni!.
ITAENDELEA..
Sent using Jamii Forums mobile app