Simulizi: Tugawane Maumivu

Simulizi: Tugawane Maumivu

Sehemu ya 20.

Nikiwa najizoa zoa kwenda kumsalimia, akili ilikuwa ikiuliza maswali mengi sana.
"Je, ndiye aliyeniita?"

"Kama ni yeye anataka kuniambia nini?"
"Mh! Eliza akijua nilikuwa na mumewe hotelini si patachimbika?"

"Za leo shemeji?" nilimsalimia huku nikikaa kwenye kiti. Alikuwa amekaa peke yake kiasi kwamba nilishangaa kwanini sikumuona nilipoingia.

"Salama tu, karibu sana," aliniambia huku akinisaidia kwa mkono wake mmoja kukiweka kiti vizuri.
"Asante," nilimjibu huku nikimkazia macho ya kumsoma usoni kama ni yeye kweli aliyeniita.

"Vipi kumbe unafikaga mpaka huku?" aliniuliza.
Hata kama ni wewe ungejua si yeye aliyeniita.

"Aah kuna mtu amenipigia simu ameniambia yuko hapa. Sasa nimekuja nashangaa simuoni," nilimjibu.

"Aisee au kaenda chooni, ungemsubiri au umpigie simu umwambie kwamba umeshafika," aliniambia. Kauli yake hiyo ilizidi kunijulisha kuwa si yeye aliyeniita.
Nilichukua simu bila kumwambia kama nimejaribu lakini hapatikani.

"Kha! Mbona sasa hapatikani?" nilisema nikijifanya ndiyo nagundua muda ule.
"Hapatikani sasa itakuwaje? Msubiri lakini. Au akikukuta umekaa na sisi ni soo?" aliuliza.

"Hapana, hakuna tatizo."
"Ni mwanaume au mwanamke?"
"Ni mwanaume," nilimjibu nikiendelea kushikashika simu yangu.

Mara kidogo alikuja mtu mwingine na kukaa kwenye meza aliyokaa mume wa Eliza. Hata mimi nilipofika pale niliona kama kulikuwa na mtu kwani kulikuwa na glasi yenye bia na chupa yenye bia nusu.

Huyo mtu alinisalimia kisha akaendelea kunywa. Mume wa Eliza alinitambulisha kuwa yule mtu ni rafiki yake kipenzi, wamekutana pale kunywa na kwenda kulala.

"Nashukuru kumfahamu," nilisema.
Mhudumu alikuja kunisikiliza, niliagiza bia na kuanza kunywa sambamba na wenyeji wangu.

Kuna wakati nilimuona mume wa Eliza akitoa simu yake mfukoni, nikamuuliza namba yake nikidhani huenda ni yeye aliniita akaizima sasa anaiwasha. Aliponitajia namba zake zilikuwa ni tofauti na zile za aliyeniita, hata mitandao ni tofauti.
Niliisevu namba yake kisha nikai-beep. Ikaita.
"Hiyo yangu," nilimwambia nikiwa nimehakikisha siye mwenyewe.
*
*


Je, nini kitaendelea?
 
Sehemu ya 21.

Kila wakati nilikuwa nikijaribu ile namba lakini wapi. Nikahisi labda yule rafiki wa mume wa Eliza ndiye mwenye namba ile lakini kazima kwani suruali ya jinzi aliyovaa ilionekana kuna simu mfukoni lakini alikuwa hajishughulishi nayo. Lakini naye kama alijua ninachowaza, pale pale akawa kama ameshuka na kuitoa.

Aliangalia kama kuna ujumbe au missed call alipoona hamna akawa anairudisha mfukoni. Nilimwambia naomba kuiona simu yake nimeipenda, akanipa.

Niliingiza namba zangu na kuibeep, namba zilizojionesha kwenye simu yangu sizo. Nikafuta namba nilizoziandika kisha nikampa simu yake.

Mara meseji kwenye simu yangu iliingia, nikaifungua haraka haraka nikijua huyo mtu amepata meseji sasa ananijibu.
"Unajua shemeji we ni mzuri sana...yaani we acha tu!"
Ndivyo ilivyoandikwa hiyo meseji, kuangalia jina la mtumaji.

Zilikuwa za mume wake Eliza. Kwanza nilitabasamu mwenyewe kisha nikainua macho kumwangalia. Sijui na yeye alinitega akijua chupa moja ya bia inatosha kuharibu netiweki yangu kichwani. Kwani kule kumtazama nikajikuta nasisimkwa na damu.
Hilo ndilo tatizo langu kubwa.

Kila ninapokungwa bia, hata kama ni glasi moja, lazima mwili usisimke! Nikaongeza bia ya pili, ya tatu na ya nne ndio kabisa! Hata kichaa akinitaka naweza kumpa 'ofa'.
Niliyarudisha macho kwenye simu yangu ili kuujibu ujumbe wa mume wa Eliza ambaye pia nilizoea kumuita shemeji.

"Naona shemeji unataka siku moja nimwagiwe maji ya moto nini?"
Nilimtumia ujumbe huo huku nikichukua glasi yenye bia na kuipeleka kinywani. Kisha nikajikausha kama sikutuma ujumbe kwa mtu.

Nilimuona shemeji akiusoma ujumbe ule kisha akawa bize kuandika, nikajua anataka kunijibu. Alipoacha na kushika glasi yake, ujumbe wake ukaingia kwenye simu yangu.
"Acha hizo kwani utamwambia?" nilicheka sana lakini chini kwa chini, kwani sikumbuki kusikia kama kuna mtu aliyewahi kumfuata mke wa mtu na kumwambia mimi natembea na mumeo.

Au hata mume wa mtu na kumwambia mimi natembea na mkeo.
Meseji ile sikujibu, ningejibu nini sasa.
Lakini kitu kimoja kiliniuma sana moyoni. Kila nilipofikiria usaliti wa shemeji, mume wa dada Light kwa mwenzake nilijisikia vibaya.
*
*

Itaendelea...
 
Sehemu ya 22.

Kuna wakati nilikuwa namwangalia shemeji huyu kisha navuta picha siku asikie kuwa mpangaji mwenzake, tena waliyeshibana, anakula mali zake itakuwaje?

Basi tuliendelea kula bia, nyama choma, kusoma magazeti na kupiga stori mbalimbali. Pia nilipata nafasi ya kumsoma vizuri shemeji yangu huyu.

Niligundua ni mwanaume mwenye akili nyingi sana. Hana pupa, hapendi kumsengenya, kumdharau mtu kwani wakati wote tukiwa pale sikumsikia akimsema mtu hata nisiyemfahamu.

Nilipofika bia ya tatu, siyo siri netiweki zilikata kabisa. Safari za chooni nazo zikaanza. Siunajua tena, pombe si chai.
Kuna wakati nilikuwa nakwenda chooni, nikirudi kabla ya kukaa nilijisikia haja ndogo tena, nikarudi.

Nilimokuwa nikipita sasa, salamu kibao, vimeseji sasa ndo usiseme. Wanaume wengine waliniangalia nikipita wakaishia kusonya. Na mimi ndiyo nikazidisha kujilegeza wakati wa kutembea. Na hivi nilivaa suruali ya kubana na umbo langu ni namba nane, yaani we acha tu.

Ukitaka kuamini kuwa baadhi ya wanaume ni wakware sana tena wana hatari, kuna wakati mhudumu mmoja alinijia nilipokaa na kuninong'oneza jambo.
"Kuna kaka pale anasema mpe namba yako, atakutafuta."

"Mwambie yeye ndo anipe ya kwake," na mimi nilimjibu kwa kumnong'oneza kama yeye alivyofanya.

Mhudumu alipoondoka, niliokaa nao wakaniuliza nini kinaendelea?
"Aaah, anasema eti kama ananifahamu," niliwadanganya lakini nikahisi wameishtukia picha, kwa vyovyote vile nao wanafahamu michezo kama ile kwenye mabaa.

Nilitamani kumwambia mhudumu asije tena kwani ndo bomu litalipuka, lakini hiyo nafasi ikawa haipatikani.

Nilipobanwa tena na mkojo, nilisimama kwenda chooni. Ile natoka tu chooni, yule mhudumu huyo.

"Namba yake hii hapa," alinipa kwenye kipande cha gazeti. Nilikipokea haraka na kukitia ndani ya kimkoba changu. Si unajua tena sisi wanawake, tukiendaga chooni, mkoba juu....ukiwa na tishu au toiletipepa kwa ajili ya mambo fulani.

Niliporudi nikaendelea kuagiza bia kadri ya hamu yangu.

Yule rafiki yake shemeji yeye alianza dalili za kuangusha gari. Naamini walianzia mbali.
Aibu zilinitoka nikaanza kummiminia bia shemeji. Nilihakikisha kila baada ya muda bia kwenye glasi yake ilipoanza kwisha nammiminia haraka sana...

Nini kitaendelea...
 
Sehemu ya 23.

Na yeye akawa anashukuru.
"Asante shemeji."
"Usijali shemeji," na mimi nilimjibu.
Kuna wakati chupa ya bia yake kwa kuwa ilikuwa ni ya baridi ilisababisha maji maji pale juu ya meza, badala ya kumuita mhudumu afute, mimi nilichukua kitambaa changu na kumfutia.

"Asante kwa kunifutia shemeji," alishukuru.
"Usijali shemeji," nilimjibu.

Sasa macho yetu yalipokutana yaliluwa yakiongea mengi. Mfano, kuna wakati tulikutana macho, ya kwake yakasema, mtoto mzuri nikubalie basi, na mimi ya kwangu yakajibu, usikonde shem, kwanza lazima nimsaliti Eliza maana na yeye anamsaliti dada angu, we hujui tu.

Tulijikuta tunaachia tabasamu, lakini la kwangu liliambatana na aibu kidogo huku nikizungusha macho kuangalia watu wengine.

Hasa hasa nilikuwa nikimtafuta huyo mwanaume aliyenipa namba yake ya simu, kwani nilipokea lakini sikujua ni yupi.
Ilifika mahali shemeji akawa ananitamkia wazi wazi kuwa, anapenda mimi niwe mpenzi wake na kwamba atahakikisha anatunza siri ili dada yangu na mkewe wasijue.

Kabla sijamjibu nilimwangalia yule rafiki yake, nilipogundua hana habari na huenda alikuwa akiota ndoto, nilimgeukia shemeji na kumwambia.
"Unanihakikishiaje kwamba hakuna atakayejua?"

Shemeji alijiinamia kwa muda kisha alipoinua uso wake na kuniangalia, alisema.
"Sina cha kukuhakikishia, lakini we wajua kwamba lazima nitafanya hivyo."
Niliachia tabasamu lakini kisha nikamfinyia jicho moja kama ishara kwamba niko katika mahaba naye.

Lakini aliendelea kunikazia macho kama anayesubiri jibu kutoka kwangu.
"Sawa shemeji lakini tuwe makini mkeo asijue, wala dada yangu asijue. Pia shemeji asijue."

Nilipomaliza kusema hivyo, pale pale shemeji aliamka kutoka kwenye kiti chake na kunisogelea kwa kuuleta uso wake kwangu. Nikajua hakuna lingine, alihitaji busu.
Nilimuwahi na kumbusu la shavuni kisha nikamlamba midomo.

Alirudi kukaa huku akisema.
"Nimefurahi sana kusikia hivyo Maria. Kuanzia sasa ushemeji ndio umekoma, au siyo?"

"Ndiyo shemeji," nilimjibu huku nikiwaangalia watu kama walikuwa wakitukodolea macho.
Giza lilipoanza kuingia shemeji alimwamsha mwenzake ambaye sidhani kama leo hii nikikutana naye atanikumbuka kwa jinsi alivyokuwa amelewa siku hiyo.
*
*
Itaendelea.....
 
Sehemu ya 24.

"Maliza bia yako tuondoke au unaongeza?"
"Noo kama tunaondoka, tuo......iihikii," alitaka kutapika.

Shemeji alisimama huku akinishika mkono. Rafiki yake naye alisimama, tukateremka chini na kutafuta usafiri. Rafiki yake alichukua taksi peke yake na sisi tulichukua taksi.

Tulikaa siti ya nyuma huku nikiwa nimekumbatiana na shemeji. Kila hatua niliyoifanya nilijisikia raha, kwani nilihisi namkomoa Eliza ambaye naye alikuwa anamkomoa dada yangu.

Mwendo mfupi mbele shemeji alinishika mabega na kuniinamishia kwenye flaizi ya suruali yake. Nikawa nimempatapata. Sikufanya ajizi.

Nilipoinua kichwa kuangalia tunakokwenda, nikajua shemeji alipania turudi nyumbani.
"Kwani tunakwenda wapi mpenzi?" nilimuuliza.

"Si home, we utashuka njiani, mi nitakwenda na taksi mpaka nyumbani," alinijibu huku akinipapasa mwilini.
"Hapana bwana mi sitaki kwenda nyumbani," nilimjibu bila aibu.
"Unataka nini sasa?" aliniuliza kwa sauti ya upole.

Badala ya kumjibu kwa kusema, nilimfinya kwenye flaizi.
Mwanaume ni mwanaume tu, alitambua haraka kwanini nilifanya vile na si ajabu alitaka hivyo, lakini akajifanya hataki.
"Dereva hapo nyoosha," shemeji alimwambia dereva akimpa daireksheni nyingine na kuachana n Ile ya kuelekea maeneo ya nyumbani.

"Hapo mbele kula kulia," alizidi kuelekeza. Na dereva alivyoonekana kuwa makini, wala hakuwa akiuliza uliza.
"Kwa wale watu mbele yako utachinja kulia kisha utaona bango la hoteli," alizidi kuelekeza shemeji.
Lakini ghafla moyo wangu ukawa mzito sana.

"Kweli nikalale na huyu mwanaume ambaye najua kabisa mkewe na dada yangu ni mtu na shoga yake, hata kama mkewe anamsaliti dada ni upumbavu wake, lakini je, na mimi nastahili kuwa mpumbavu kama mkewe?" nilijiuliza mwenyewe.

Nikahisi kwamba kwa kukubali kulala na shemeji huyu nitakuwa naudhalilisha uwanamke wangu, halafu isitoshe mimi ni msomi, nina akili za kujitegemea kuliko zile za kushikiwa na mtu.

"Shemeji samahani ni mawazo tofauti kidogo tena yamenijia ghafla," nilimwambia mume wa Eliza.

"Yapi hayo tena?" aliniuliza kwa sauti ya chini ili dereva asisikie.
"Unajua nitakuwa namsaliti sana dada Eliza?"
"Kwa kufanyaje?"
*
*

Itaendelea.
 
Sehemu ya 25.

"Kwa kulala na wewe shemeji yangu. Mkeo na dada yangu ni mtu na rafiki yake. Tena wameshibana sana. Kwa maana hiyo, mkeo mimi namuita dada kama ninavyomuita dada yangu," niliyameza mate kwa mbali kisha nikaendelea.

"Kwa hiyo huoni mimi kutembea na wewe ni sawa sawa na wewe kutembea na mdogo wake Eliza?"

Nilimjibu shemeji lakini wakati huo huo nikamuona kama amebadilika sura.
"Inawezekana ni kweli shemeji, lakini si mimi niliyetaka turudi nyumbani lakini wewe ukanionesha dalili kwamba unataka kufanya mapenzi na mimi?"

Nilijiinamia mwenyewe, kisha nikaacha na kumwegemea yeye mapajani mwake.
"Basi nisamehe shemeji," nilimwambia kwa sauti ya upole na yenye kujaa mahaba, kwani niliitoa nje kwa kuibana ikatengeneza uhondo.

"Sura geuza gari bwana," shemeji alimwambia dereva.
"Wapi sasa," dereva aliuliza kwa sauti isiyokuwa na pupa. Yeye shida yake nini si atalipwa bwana.

Tulipokaribia nyumbani mimi nilishuka na kutembea kwa miguu, shemeji akaenda na gari hadi mlangoni.

Mimi wakati naingia, yeye alishaingia dakika kama kumi na tano nyuma, hivyo haikuwa rahisi kwa mtu kujua kama tulikuja safari moja.

"Dada Eliza huyo shikamoo," nilimsalimia Eliza ambaye alikuwa anapika kwenye korido.

"Marahaba mdogo wangu, karibu tunapika," Eliza alisema kwa furaha na amani wakati mwenzake moyoni nilisema, wewe una bahati kama mtende. Kama si ushujaa wangu mumeo saa hizi ningekuwa namjua kinyumenyume.

"Asante da Eliza ngoja niangalie situation huku," nilimjibu huku nikiwa nafungua mlango kuingia ndani.

Hata kabla sijazama mume wa Eliza alitoka kwake akiwa na bukta tu.
"Shikamoo shemeji," nilimsalimia kwa heshima zote. Si unajua tena kujibalaguza ili dili lisigundulike.

"Marahaba Maria, upo, huonekani?"
Kumbe na yeye mtu wa vimeo, alijifanya hajaniona siku nyingi.
"Nipo shemeji yangu weee ila leo nilikwenda Kariakoo mara moja ndo narudi," nilimjibu nikizama ndani.

Nilimkuta shemeji amekaa sambamba na dada Light. Niliwasalimia wakaitikia wote, huku dada Light akinitania kuwa alitaka kwenda kutoa ripoti kituo cha Polisi Urafiki.
*
*
Itaendelea....
 
Sehemu ya 26.

"Kwamba?" nilimuuliza nikijikaza kwa bia za New Top Land.
Shemeji alicheka kwa utani wa dada, akasema.
"Mi hata akipotea wiki sitoi taarifa polisi , ya kazi gani?"
Kwa nini shemeji?"

"Warembo hawapoteagi bwana, wanapotea manung'ayembe, hata ukimuona mzazi anahaha kumsaka binti yake mkubwa aliyepotea ujue ni nung'ayembe," alisema shemeji na kusababisha kicheko.

Kwa kuwa mlango ulikuwa wazi, kicheko hicho kiliungwa mkono wa Eliza aliyekuwa anapika. Lakini alicheka tu bila kuchangia kitu.

Saa tatu na nusu Eliza na mumewe waliingia kuangalia mchezo mmoja kwenye Tv, walidai Tv yao imeharibika ghafla.

Kwa kuwa mchezo ulishaanza walikaa kochi moja, dada Light na mumewe nao kochi moja. Mimi peke yangu kochi dogo.
Nilikuwa nikijitahidi kumwangalia shemeji na Eliza kwa kuwaibia. Walikuwa wanaangaliana kiaina na kuachiana tabasamu fulani ambapo sikupenda hiyo tabia.

Nikataka kumtumia meseji Eliza kumuonya, lakini nilichokifanya nikawa namtumia mumewe naye akawa ananijibu tena haraka sana.
*


Itaendelea...
 
Sehemu ya 27.

"Shemeji usiwe na wasi wasi iko siku utafurahi," nilimwambia katika meseji.
"Usijali shemeji, hata mi najua," alinijibu. Ilifikia mahali Eliza alimshtukia mumewe.
"Mwenzetu mbona meseji nyingi," aliuliza huku akiangalia saa kama vile alikuwa na maana kwamba haikuwa muda wa meseji.
"Si yeye hata Maria pia," dada alidakia.

"Sasa una maanisha wanatumiana meseji siyo?" shemeji naye alidakia huku akicheka. Wengine nao wakacheka na kuendelea kuangalia runinga.

Moyoni nilimuonea huruma dada Light. Angejua nilikuwa napambana na mbaya wake wala asingesema vile, lakini anyway nilijikaza kuhakikisha hakuna atakayejua kitu.

Wakati mume wa Eliza alibaki amekodolea macho runinga mimi niliendelea kutuma meseji kwa watu wengine ili isijulikane kama tulikuwa tukichati sisi kwa kitendo cha wote kuacha kuchati.

Wao wakawa bize wakisimuliana habari za ule mchezo lakini mimi nikawa najishughulisha na simu yangu. Kuna wakati salio lilikuwa halitoshi, nikaamua kucheza gemu.

Mchezo ulipoisha, Eliza na mumewe waliaga kwamba wanakwenda kulala. Mumewe akatoa mikono kwa wote akianza na mume mwenzake, yaani shemeji, akaja kwa dada Light kisha akamalizia na kwangu, lakini mimi akanifinya kidogo. Nikajikausha kama sikufinywa.

Kisha mkewe Eliza naye akatoa mkono akianza na kwangu kisha akaenda da Light na kumalizia kwa shemeji ambapo nilikazia macho mikono yao, nikaona inaminyana sana. Moyo ukanilipuka puu!
Kumbe kuna wapenzi wanaweza kufanya ufisadi wao hata mbele ya wenye mali, jamani!

Walipoondoka nilitafuta kila nafasi ili niweze kuonana na shemeji ili nimuonye kwa kumwambia kwamba kama ataendelea kuwasilina na Eliza kwa namna zozote zile kama alipofanya pale nitalipua bomu lake kwa dada, lakini nafasi hiyo sikuipata kwa vile wakati wote alikuwa sambamba na mkewe.

Asubuhi wakati Eliza anatoka kwenda kazini alitangulia peke yake, mumewe alibaki nyuma.
"Shikamoo da Eliza," nilimsalimia kwa upendo huku nikijua ni muuaji wa dada yangu.

"Marahaba mdogo wangu, vipi za kuamka?"
"Salama tu, da Eliza nina mazungumzo na wewe. Ikibidi ukisharudi au useme wewe unatakaje?" nilimwambia.
Eliza alionekana kushituka kwa kauli yangu lakini alijikaza kikike tu na kujifanya ngangari.
*
*

Itaendela.....
 
Sehemu ya 28.

"Sema sasa hivi mdogo wangu," alisema Eliza huku akiangalia mlangoni.
Nahisi hakuwa tayari mumewe ajue habari itakayoongelewa.
Na mimi nikaitumia nafasi ile kumchamba.
"Unajua dada Eliza wewe na shemeji mnavyomfanyia da Light sio vizuri."
Mara dada Light na mumewe walitokea, pia mume wa Eliza naye alitokea. Wakawa wote nje wakisalimiana, lakini Eliza alikosa furaha.
"Basi tutaongea baadaye mdogo wangu," Eliza aliniambia.
"Nini tena mwenzetu?" dada Light aliuliza.
*
*

Itaendelea...
 
Sehemu ya 29.

Eliza alipotezea swali hilo kwa kumjibu dada Light kuwa, hakuna kitu chochote kile kisha akaaga na kuondoka zake kuelekea kazini.
Siku hiyo majira ya jioni nilipanga kukutana na mume wa Eliza kwenye ukumbi wa Old Trafford, lakini kitu cha kushangaza wakati nimefika nje ya ukumbi huo nilikutana na Eliza.

"Hee mdogo wangu kumbe unakujaga hadi huku?" aliniuliza.
"Ndiyo mara moja moja lakini," nilimjibu huku moyoni nikijiuliza alifuata nini mahali pale?
Kiukweli sikuweza kupata jibu.

"Ooh halafu imekuwa vizuri kweli njoo huku ukumbini uniambie kile kitu ulichotaka kuniambia asubuhi," alisema Eliza huku akinishika mkono kunivuta nimfuate.
Sikuwa na jinsi, nilimfuata Eliza mpaka ndani ya ukumbi. Alipokaa na mimi nilikaa. Lakini mpaka kufikia hapo hakuna aliyekuwa amemuona mumewe. Si mimi wala yeye.

Sehemu kubwa ya watu walikuwa wamekaa kwenye viti vya jirani na jukwaa la ukumbi huo unaojulikana kwa jina la Old Trafford.
"Haa mume wangu yule pale," alihamaki Eliza huku akisimama na kumfuata.
Aliniacha nimekaa pale pale na wala sikusimama kwenda naye. Moyoni nilikuwa nikisema:

"Ungejua yupo kwa ahadi na mimi, wala usingekubali kuingia."
Baada ya muda Eliza alikuja akiwa ameongozana na mumewe na rafiki wa mumewe, yuleeee...aliyekuwa naye siku ile pale New Top Land Hotel, Magomeni. Moyo wangu ulishtuka na kuzidisha kasi ya mapigo. Nilihisi yule rafiki yake baada ya kuniona angesema, 'aa shemeji za toka siku ile bwana?' ingekuwa soo.
Pangechimbika.

"Vipi shemeji yangu hujambo?" mume wa Eliza alinisalimia kwa furaha na uchangamfu wa hali ya juu akiwa amesimama. Tulishikana mikono lakini akawa ameniminya kiaina.

"Eti anashangaa kutuona tumeingia pamoja humu ndani," Eliza aliniambia.
"Tumekutana hapo nje," na mimi nilimwambia mume wa Eliza ingawa najua alishaambiwa.

Baada ya hapo nilisalimiana na rafiki wa mume wa Eliza ambaye alishakaa na alikuja na glasi yenye bia.

Mume wa Eliza naye alivuta kiti akakaa huku mhudumu akileta chumba mbili zenye bia na glasi moja nayo ilikuwa na bia.

Nimeeleweka!
Ikabidi Eliza na yeye aagize bia yake na kuniruhusu na mimi kuagiza kinywaji changu. Niagize nini, niliagiza bia kama wao.
*
*

Itaendelea.
 
Sehemu ya 30.

Ukitaka kujua uhondo wa ngoma sharti na wewe uingize ucheze.
Eliza na mumewe wakawa bize na maongezi yao huku wakiinamiana. Mimi nilikuwa peke yangu, kwani yule rafiki wa mume wa Eliza alirudia yale yale...alikuwa analala, akiamka anachukua glasi yake yenye bia na kuipeleka kinywani kisha analala tena.

Hana habari na mtu!
Nilikuwa sijamaliza hata bia ya kwanza, getini nikamwona shemeji mume wa dada Light akiingia. Macho yangu na yake yalipokutana akaonekana kushangaa na kulipunja tabasamu.

Najua kwa nini alishangaa badala ya kuchangamka. Kwa sababu alijiuliza nini kilichonipeleka mitaa ile jioni ile.

Alitembeza miguu mpaka pale, lakini kadri alivyokuwa akija ndivyo alivyoonekana akiongeza mshangao zaidi kwani aliweza kubaini kuwa, mbali na mimi alikuwepo mume wa Eliza ambaye kwa sehemu aliyokaa ilikuwa rahisi kwa shemeji kumtambua kuliko Eliza mwenyewe ambaye alimpa mgongo.

Uso wa shemeji ulibadilika tena kama joto la malaria. Sasa alionekana kuhoji moyoni kwanini nilikaa pale na mume wa Eliza. Lakini mimi nilitabasamu kuashiria kuwa, sikuwa na baya pale kwani nilikuwa nimeingia na mke wake Eliza.
"Vipi shemeji," alianza kusalimia kwa mbali akipanda ngazi kuja tulipo.

"Safi tu," nilimjibu nikiinua shingo kumwangalia vizuri na pia ishara ya kumkaribisha kwa upendo.
Kitendo cha mimi kuitikia salamu, kiliwafanya Eliza na mumewe washtuke na kuangalia mbele na nyuma.

"Aa kumbe upo na majirani," alisema shemeji. Hapo alishamuona Eliza pia.
Alitupa mikono wote kisha akavuta kiti na kukaa jirani na mimi. Wakati huo rafiki wa mume wa Eliza hakuwa yeye.
Aliegemea kiti na kuangalia juu! Kiufupi alilala.

"Vipi shem," shemu aliniuliza.
"Poa tu, nilikuwa nakwenda hapo Mikocheni ndiyo nikakutana na da Eliza hapa akanikaribisha humu ndani," nilimjibu shemeji ambaye nilipotaja jina la Eliza tu aligeuza uso na kumwangalia.
Eliza na yeye licha ya kuwa alikuwa akiongea na mumewe aliacha na kumwangalia shemeji.

Jamani watu wapenzi utawajua tu, hata wakiangaliana, sijui kwa nini mume wa Eliza alikuwa hajaligundua hilo, kwani macho ya mkewe yalipokutana na macho ya shemeji, hali ya aibu na tabasamu la huba vilijitokeza usoni pa Eliza.
*
*

Itaendelea.
 
Sehemu ya 31.

Wakati sura ya shemeji ilijaa ujasiri wa kitandani huku akionekana kutamani kumwambia waondoke wote jioni ile.
"Ni mimi ndiye nimemwingiza humu," alisema Eliza akimwambia shemeji.
"Na mimi mwenyewe nilishangaa kuwaona wapo humu ndani," mume wa Eliza naye aliongezea kusema kwa sauti nzito.

Basi ikawa kunywa, kunywa, kunywa, kunywa! Kuja kushtuka saa mbili kasoro robo usiku. Ilibidi nimdanganye Eliza kwamba amenisababishia niliyekuwa namfuata kuondoka. Mumewe kusikia hivyo na vile alikuwa amelewa alinipa simu yake.
"Ee, mpigie mwambie umekutana na shemeji zako. Mtaonana kesho."

Nilipokea huku nikimwangalia shemeji uso wake unasemaje?
Unakubaliana na usamaria ule au la!
"Sawa sawa kabisa mpigie," alisema shemeji. Nikajua hana neno. Kwanza angetia neno gani wakati anajua mimi nafahamu siri yao nzito, hata kama ningeamua pale pale pangechimbika.

Nilichukua simu na kufungua sehemu ya kuandika ujumbe. Lakini nimwandikie nani sasa. Maana hakuna mtu aliyekuwa ananisubiria. Halafu nilimshangaa sana huyo mume wa Eliza. Yeye anajua ishu yote kwamba nilikuwa namfuata yeye, asa kunipa simu yake eti nimpigie huyo mtu alikuwa na maana gani?

Aliyetakiwa kunipa simu ni shemeji, au Eliza ambao walikuwa wameamini kuwa, kuna mtu niliyekuwa namfuata.
Niliinama chini ya meza na kuandika ujumbe mfupi wa maneno hivi;
"Nakupenda, asa dili limeharibika turudi home."

Nilijitahidi sana kumpa simu mume wa Eliza mkono kwa mkono kwani meseji hiyo ilikuwa bado kwenys draft ya kuandikia.
Niliinamisha simu chini nikiipeleka kwake ili aipokee mwenyewe huku nikimshukuru. Naye kama alitambua hilo, kwani alinyoosha mkono kwa kasi na kupokea simu yake. Aliishika na kuiteremsha chini kidogo. Nahisi alijua kwamba nilimuandikia ujumbe mfupi ausome.

Itaendelea...
 
Sehemu ya 32.

"Mbona hukunipigia simu au ulinitumia meseji tu?" Eliza aliuliza alisimama na kuondoka. Sikujua alikuwa anakwenda wapi. Lakini nilipomfuatilia niligundua anakwenda chooni.

Pale pale akili zilinicheza kwamba huenda huko chooni anakokwenda alikuwa ana lengo lake la kwenda kumtumia meseji shemu yaani mume wa dada Light au kumpigia simu kabisa. Lakini kumpigia simu sikuwa nimelifikiria sana zaidi ya kumtumia meseji.

Kabla sijamaliza kuwaza, simu ya shemeji iliita. Wakati anaangalia nilimuona kama kashtuka vile.
Alituangalia kwa zamu wote tuliokaa pale mezani kisha akataka kama kusimama kwenda kuisikilizia kwa mbali, lakini akarudi kitini.

"Enhe niambie," alianza kusema shemeji.
Sijui huko upande wa pili alikuwa akiambiwa nini lakini mimi niligundua kutokana na majibu yake. Nilijua ni Eliza tu huyo aliyempigia simu.

"Saa ngapi?" aliuliza shemeji.
"Wapi?" aliendelea kuuliza.
"Lakini hatukai sana au?"
"Oke, oke!"

Alipokata simu tu, dakika moja nyingi, Eliza alitoka chooni tena huku akiwa ameuchanua uso kama si yeye.
"Jamani twendeni," alituamuru akionekana hatakaa tena licha ya kwamba glasi yake ilikuwa na bia.

Shemeji alikuwa wa kwanza kusimama kama vile aliyetoa kauli hiyo ni mkewe, da Light. Akafuata mumewe huku akimwambia rafiki yake. Lakini mume wa Eliza nilimuona kama vile amekosa raha.

Tulipofika nje Eliza alisema maneno ambayo mimi binafsi sikupenda ayaseme.
"Dear itabidi utangulie nyumbani mi nitapitia saluni pale Shekilango."

Mumewe alimkodolea jicho hilo.
"Kumbe ulikuwa unapitia saluni, kulikuwa kuna haja gani sasa ya kutuondoa wote pale baa. Si ungetangulia peke yako tu," alisema mumewe. Eliza bila hata kusema samahani alileta hoja yake huku ikinikera mimi nisiyeolewa.
"Wanawake wengine bwana," nilijisemea moyoni.

Pale pale nje rafiki wa mume wa Eliza alichukua taksi, tukabaki watatu tunaokwenda sehemu moja, ingawa mwingine alikuwa anapitia saluni.
Mume wa Eliza aliita taksi aina ya baluni akidai kuwa ni kubwa, tutakaa kwa raha mustarehe. Sijui ni pombe sijui ni nini?
Taksi ilipofika, shemeji aliingia nyuma, Eliza naye akajitumbukiza haraka kumfuata huku akisema...
"Acha nikae na shemeji yangu huku nyuma."

Itaendelea.....
 
Sehemu ya 33.

Laiti kama ningekuwa mimi nisingeingia kwa utaratibu huo. Ningefanya hivi....
Ningeacha na mume wangu aingie kisha mimi ningeingia mwisho. Kwa maana hiyo upande mmoja ningepakana na mume wangu upande mwingine ningepakana na mlango. Hasa kwa hali ile ya yeye kuwa na uhusiano wa kimapenzi na shemeji.

Basi, Eliza alipoingia, mimi nikamshika mkono mumewe na kumwambia.
"Shemeji inabidi na wewe uingie nyuma ukae na mamaa, mimi nitakaa mbele."
Lakini mkewe akawahi kusema.

"Acha akae mbele yeye mwanaume bwana."
Eti mumewe akae mbele kwa vile ni mwanaume. Mbona pia shemeji ni mwanaume na aliingia siti ya nyuma?
Sikuona sababu ya msingi ya yeye kusema hivyo. Hata shemeji pia naona alijisikia vibaya.

Basi mimi nikakaa nyuma, nikiwa nimepakana na Eliza, yeye amepakana na shemeji. Au tuseme Eliza alikaa katikati.
Dereva alitoa gari, akakata kona na kuongeza mafuta. Mara tukawa maeneo ya Faya.

Nilianza kuuona mkono wa kulia wa Eliza ukienda kwenye mapaja ya shemeji. Mara shemeji naye akaupeleka mkono wake nyuma ya Eliza na kumshika kiuno.
Najua walitumia kigezo cha giza kufanya hivyo.

Pia waliamini kuwa, bia tulizokunywa zinaweza kutufanya sisi wengine kutowafuatilia.
"Saluni unayokwenda ni ya wapi?" mume wa Eliza aliyekuwa amekaa mbele aliuliza kwa sauti na kukata ukimya uliyokuwepo.

Itaendelea....
 
Sehemu ya 34.

"Pale Tip Top jamani, si nilikwambia dear," alijibu Eliza.
Huu ni unafki katika mapenzi. Eti alijifanya kutumia neno dear kujifanya anampenda sana mumewe wakati ni msaliti mkubwa, tena anayesaliti naye yupo ndani ya gari.

"Oke lakini ujue usiku sasa," mumewe alisema akionekana hakuwa amebariki safari ya mkewe kwenda saluni muda ule.
Halafu kwanini saluni iwe Tip Top wakati yeye anaishi Shekilango?

Ndiyo inawezekana wapo wanawake wanakwenda saluni hata mjini kabisa, lakini muda nao ulikuwa umekwenda.
Kwanini asiende asubuhi? Hayo yalikuwa maswali niliyokuwa nayawaza mimi.
"Lakini kwanini usiende kesho asubuhi?" mumewe alimuuliza.

"Bwana mume wangu acha niende leo," Eliza alijibu kwa sauti ya kudeka. Hana lolote, mtu mzima lakini ovyooo.

Wakati huo mkono wa shemeji ulikuwa bado upo kwenye kiuno cha Eliza ingawa Eliza yeye alishautoa mkono wake kwenye mapaja ya shemeji.

Inaonekana kule kukumbatiwa pia kuliongeza dhamira ya Eliza kwenda saluni usiku ule.

"Tip Top si hapa," shemeji alisema wakati tunapita daraja la Manzese.
"Ee dereva paki hapo mbele kituoni," alisema Eliza huku akiandaa mkoba wake.
Akamwambia mumewe akashuke na mfuko wa rambo aliokuwa nao, una vitu vya nyumbani.

"Poa poa," mumewe alijibu.
Baada ya kushuka, nyuma nilibaki mimi na shemeji, akanisogelea na kuniambia.
"Shemeji mi nitashuka Legho, nipate japo bia mbili kisha nitakuja nyumbani, sawa?"
Sikumjibu, nilimtumbulia macho ya kumsuta. Nadhani alinielewa.

Lakini akili yangu ilifanya kazi haraka sana. Nikagundua huenda Eliza hakuwa anakwenda saluni na wala shemeji hataingia Legho kama alivyodai.

"Hawa kuna sehemu wanakwenda kukutana," nilijisemea moyoni.
Taksi ilipofika Legho ilikata kushoto kuingia nyumbani, shemeji akamuomba dereva amshushe pale.

Itaendelea....
 
Sehemu ya 35.

"Ee, vipi na wewe unakwenda saluni nini?" Mume wa Eliza alimtania shemeji baada ya kumsikia na yeye anashuka.

"Aa, kuna mtu namcheki hapa Legho mara moja, lakini sikai sana," shemeji alimjibu mume mwenzake. Kama binadamu angepewa uwezo wa kuona moyo wa mwenzake kusingekuwa na amani duniani, lakini pia si ajabu ingekuwepo tena ya kudumu.

Baada ya shemeji kushuka, sasa tukawa tumebaki abiria wawili, mimi na mume wa Eliza.

"Na wewe Maria vipi?" aliniuliza mume wa Eliza.
"Kuhusu?"
"Si unaona dili lote limeingiliwa na wahuni hawa, halafu wamekuja kutuacha karibu na home."

"Aa, tena wahuni kweli, utafikiri walijua kwamba sisi tulikuwa tunakutana wakaamua kutuvurugia," nilimjibu mume wa Eliza. Wakati huo taksi ilikuwa imefika nje nyumbani. Ile mume wa Eliza anashuka tu, dada Light akafungua mlango mkubwa wa nje.

Nafikiri alisikia mlio wa gari ndiyo maana akatoka. Alisimama kuangalia gari. Na mimi nikashuka na kukutana na macho ya dada Light.

"Hee! Maria," alihamaki. Sikujua kwanini alihamaki.
Alitangulia ndani bila kuniambia kitu alichohamakia na wala bila kusalimiana na mume wa Eliza wakati si kawaida.

Niliingia ndani nikitegemea kumkuta dada amekaa sebuleni, lakini kumbe alipitiliza hadi chumbani kwangu.
Nilipoingia nilimkuta amekaa kitandani, uso umekunjamana kwa hasira.
"Maria," aliniita.

"Abee."
"Unataka kuleta tabu humu ndani?"
"Tabu gani?"
"Unatoka wapi na mume wa Eliza? Mi mwenyewe sijawahi kuongozana naye kwenda barabarani. Nikijua anakwenda barabarani na mimi na kwenda barabarani nasubiri atangulie, hapa ni mjini hakuishi maneno maneno mdogo wangu."

Itaendelea......
 
Sehemu ya 36.

Aliponiambia hivyo ndipo hapo nikaanza kugundua kumbe ndiyo mama alihamaki pale nje wakati nashuka kwenye taksi. Ikabidi nimpe dada kisa cha mimi na mume wa Eliza kuja wote pale.

"Kwa hiyo Eliza kashuka Tip top saluni, shemeji yako kashuka Legho?"
"Eee!"

"Aa, hapo sawa. Nilifikiria wewe na yeye mmekutana huko mkachukua taksi, usithubutu mdogo wangu. Eliza ni rafiki yangu lakini simwamini sana. Naamini akitokea kukuhisi una ukaribu na mume wake anaweza akakuua, si unajua wapo wanawake wa hivi?"

"Najua dada."
Japokuwa nilikuwa nimelewa lakini dada alimtuma msichana wa kazi akanunue bia nyingine nne, anywe yeye pamoja na mimi. Akasema tukae nje ili tupate upepo mzuri.
Tulitoka nje na kukaa kibarazani. Bia zikaja tukawa tunakunywa huku tunapiga stori. Siku hiyo ilibaki dakika mbili tu nimwambia dada kwamba uchunguzi wangu umegundua kwamba, mume wake, yaani shemeji anatembea na rafiki yake Eliza. Lakini nilijikaza na kuvumilia pia.

Saa tano usiku Eliza anaingia! Nini kutengeneza nywele, hata kutinda nyusi tu hakufanya.
"Vipi mwenzetu, hizo nywele zilizokupeleka saluni ziko wapi?" nilimwambia Eliza bila kuona haya. Aliinama chini kwa aibu kisha akaniambia.

"Mwenzangu umeme umeharibu kila kitu."
Akamsalimia dada na kuingia ndani. Lakini dakika tano baadaye tukasikia kelele, Eliza analia. Wakati tunashangaa, shemeji naye akaingia.

Alipishana na Eliza kama dakika saba tu. Naye akashangaa kusikia vurugu ndani kwa Eliza.
"Huwezi kunidanganya mimi, kama ni umeme ulikatika kwanini usirudi mapema?"

Itaendelea.....
 
Sehemu ya 37.

Dada Light alimshauri mumewe awagongee kuuliza kulikoni kwani kwa jinsi mume wa Eliza alivyokuwa akiongea kwa jazba lolote lingeweza kutokea.

Nilimwangalia shemeji akienda. Alionekana kuwa mtu mwenye wasiwasi kibao, kwani hali halisi alikuwa anaijua. Kwa vyovyote vile, yeye alikuwa na Eliza 'somewhere'. Na ndiyo maana Eliza kashtukiwa na mumewe.
"Kwani Eliza ana mambo ya uhunihuni?" mimi sasa nilimuuliza dada wakati mumewe anakwenda kumgongea mume wa Eliza. Bado tulikuwa nje.

"Aa, mambo yake ya siri siyafahamu. Si unajua urafiki wetu ni kwa sababu tunakaa nyumba moja, halafu wote tunalingana rika," da Light aliniambia akionekana kweli hafahamu undani wa habari za Eliza.

"Angalia da Light, shoga kama huyu kuwa naye mbali, kama mumewe anamwakia hivyo 'oviazi' anahisi kitu fulani. Kama mume hakufikirii vibaya na wewe uko safi, hata siku moja hakuna kelele. Ukisema ulichelewa sehemu anakuelewa."
Nilimuona dada akibadilika sura huku akinikazia macho.

"Sasa niangalie nini, ina maana anaweza kunifundisha tabia mbaya mimi?"
"Sina maana hiyo ila anaweza kuwa kipanga, akamchukua hata shemeji."
Nilimuona dada akicheka sana, akaichukua bia yake na kuinywa. Aliporudisha chupa alisema.

"Hata weza hata siku moja. Namchunga mume wangu."
Moyoni niliumia sana. Nilitamani pale pale nimpasulie bomu lake, lakini nilijisikia huruma kwani ningelipasua amani ingetoweka ndani ya nyumba hiyo pengine kwa muda wa mwaka mzima.

Mtu akuchukulie mumeo halafu umjue ni huyu, mbaya zaidi mnakaa nyumba moja, mbaya kuliko zote ni shoga yako, weee! Sio patachimbika bali patakuwa na mashimo kila siku.

Tulikatishwa na sauti ya shemeji mume wa da Light na shemeji, mume wa Eliza.
"Kama anataka imani irudi aendelee kuwa mke wangu, twende chumbani avue nguo nimkague. Sijawahi kumfanyie hivi bwana mzee, lakini leo imebidi kwani nina uhakika wa asilimia mia kwamba hakwenda saluni, alikuwa na mwanaume," mume wa Eliza alilalama.

Itaendelea....
 
Sehemu ya 38.

Kule nje mimi niliongezea moyoni, 'na mwanaume mwenyewe ni huyo huyo uliyesimama naye hapo. Usifikirie ni hakimu wako, huyo ndiye mshtakiwa.'

Kitu kimoja nilichomsifu Eliza ambacho wanawake wengine wezi hawanacho ni kwamba, mumewe alikuwa akisikika sana kwa maneno lakini yeye kimyaa! Na hata aliposema sisi nje tulitega sikio ili kumpata alichokuwa akikiongea.
Ingekuwa wenzangu na mimi ungesikia kivumbi chake.

"Huyo mwanaume ulinitafutia wewe! Tusibabaishane bwana, mi nimechoka kuchungwachungwa," anajifanya kukasirika huku moyoni, yeye na malaika wake wanajua kwamba kweli ametoka kuiba nje ya ndoa.
Msimamo wa mumewe ulikuwa pale pale. Moja, Eliza aingie chumbani, mbili avue nguo zote, tatu akaguliwe.

Ninavyomjua Eliza kuingia chumbani kwake haikuwa ishu, si kila siku anaingia. Kuvua nguo zote si ishu, tena huenda anavuaga bila kuamrishwa, ila ishu ilikuwa kwenye kukaguliwa.

Kukaguliwa halafu matokeo yake yatatangazwa hadharani au? Hapo!
Tulimuona shemeji akitoka huku akitingisha kichwa kwamba ameshindwa kusababisha suluhu.

Macho yake na yangu yalipogongana alikuwa akikimbiza ya kwake.
"Sasa?" dada Light alimuuliza.
"Sina jinsi," alijibu shemeji.

Zogo liliendelea huko ndani kwa Eliza. Ilikuwa ni kitimtim kutoka kwa mumewe alishikilia msimamo wake wa kumkagua.
Baadaye kidogo Eliza alitoka nje na kuja tulipokuwa tumekaa sisi.

"Pole shoga," da Light alimwambia.
"Asante yote maisha," alijibu Eliza.
"Kwani haukuwa saluni kweli?" mimi nilimuuliza huku nikimkazia macho.
"Si nilikwambia umeme ulikatika mdogo wangu....sasa eti anasema kama ni kweli anikague, maana anaamini nilikuwa na mwanaume."

Pale nje tuliongea mpaka kwenye saa sita usiku. Majirani walikuwa kimya wameshaingia makwao kulala. Da Light naye akapendezwa tuingie ndani.
Kivumbi kwa Eliza sasa.

Alisema anaomba alale sebuleni mpaka asubuhi atakapokwenda kwa mama yake mdogo, Kimara.
Lakini da Light alisita, kwani anajua ni mke wa mtu sasa si kulala tu sebuleni, kuna miiko yake.

"Mwenzangu labda uongee na shemeji yako. Ngoja nikakuitie," alisema dada kisha akasimama.
Mimi na Eliza tulikuwa sebuleni wakati da Light alipoingia chumbani kumwita shemeji.

Itaendelea....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom