SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

Hapo tunawakana kama mzee kipanta wa KITUMBUA CHA BUKU
Mtakanaje na namba ya simu iko kula na msg ya ya kuchukua funguo mmetuma? mtasema namba sio yenu? au ndo mtasema mlikuwa mnawasiliana na Higgno, na ile simu Soraya alimuona aliyekuwa anatumia siku ile mnatokaje hapo
 
Mtakanaje na namba ya simu iko kula na msg ya ya kuchukua funguo mmetuma? mtasema namba sio yenu? au ndo mtasema mlikuwa mnawasiliana na Higgno, na ile simu Soraya alimuona aliyekuwa anatumia siku ile mnatokaje hapo
Subiri utaona mwenyewe
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA SABINI NA TATU
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA SABINI NA MBILI: “sito kula mpaka unitajie mshenga wako” alisema Soraya kwa sauti ya utani, lakini wenye ukweli ndani yake, “hoooo! nikikutajia hauto amini” alisema Higgno kwa kujisifu, “mh! amekuwa nani huyo mpaka nisiamini” alisema Soraya akionyesha tabasamu la furaha, huku anaptiliza ndani kuweka begi lake, kisha akatoka na kukaa kwenye kigoda, “haya niambie sasa, mshenga atakuwa nani na atakuja lini? Hakutaka kumueleza kuhusu shuku la wazazi wake, “ni yule mzee mwarabu Mahamud, nimekutana nae leo nimeongea nae sana, akasema atakuwa mshenga wangu, kuhusu kuja kwenu kuleta barua amesema nije nikuulize wewe ni moto wa nani…” alisema Higgno ambae alikatizwa na sauti ya mshtuko...….. ENDELEA NAYO……..
Na mshangao toka kwa Soraya, “unasema!!! nani atakuwa mshenga wako?” aliuliza Soraya kwa mshangao na pasipo kuamini alicho kisikia, sio kwamba alishangaa kuwa Higgno ana fahamiana na Mahamud ambae ni baba yake, ukweli Soraya alikuwa anafahamu fika kuwa Higgno, anafahamiana na baba yake, tena baba yake alikuwa anamuamini na kumkubali sana mchumba wake huyu, ila kitendo alichosema Higgno na kumsimulia Soraya jinsi ilivyokuwa mpaka wakakutana na maongezi yao yote hata lile ombi la kumchumbia binti yake na vitu ambavyo angemfanyia endapo angekubali kufanya hivyo, “nikamuambia kuwa tayari nina mchumba” alisema Higgno wakiwa wamekaa nje ya kibanda chake, Soraya akatabasamu kidogo, “mh! kwanini ulikataa mali zote?” aliuliza Soraya, ambae sasa ni kama alikuwa anamtega Higgno na kutafuta majibu sahihi ya kuwaeleza wazazi wake, “Soraya sijawahi kumpenda mtu nisiemjuwa, halafu utajiri sio chanzo cha mimi kupenda” alisema Higgno, kwa kujiamini, “Higgno, unamfahamu huyo mtoto mwenyewe wa Mahamud?” aliuliza Soraya ambae swali la hili jibu alikuwa nalo na alikuwa anahitaji uthibitisho wa moja kwa moja toka kwa Higgno, “mimi simjuwi, ila nadhani anafahamiana na wazazi wangu, kwasababu baba ameniambia kuwa anamsaidia kufufua duka lake lililoungua mtoto” alisema Higgno pasipo kujuwa anachoongea ni marudio kwa Soraya, “kwanini hukuniambia kuwa duka la baba yako limeungua moto?” aliuliza Soraya, akijifanya kuhuzunika, ungesema ndio kwanza anaisikia taarifa hiyo, “mh! samahani Soraya, lakini niliona kama ni mapema sana kukueleza kuhusu matizo ya huko nyumbani, ila hakuna tatizo mambo yanaenda vizuri, na huyo mschana mwema anamsaidia baba kurudisha duka lake” alisema Higgno kwa sauti ya upole, “ilikuwaje mpaka duka likachomwa moto au kuna watu amegombana nao” aliuliza Soraya ambae tayari alisha dokezwa sababu, ni kama alikuwa anampima Higgno, “baba anasema kuwa kuna jamaa alikuja pale dukani akaagiza sigara, lakini hakulipa baada yake akaniulizia, na baba alipomjibu kuwa siku hizi sipo pale nyumbani akasema kuwa ananitafuta kwasababu nime ingilia na kuharibu mipango yake, lazima atafanya kitu kunikomesha kama alivyonifanyia miaka iliyopita, usiku wa juzi ndio duka lika chomwa moto, baba anahisi ni huyo huyo” alieleza Higgno kwa sauti ya upole, “kwani wewe una ugomvi na nani, au uliingilia mipango ya nani na ni mipango gani?” aliuliza Soraya huku anasogeza kigoda chake karibu na alipokaa Higgno kisha akaegemeza mikono yake kwenye mapaja ya Higgno, ambae sasa alimtazama usoni, “kwa kweli mimi sikumbuki kuingilia mpango wowote, pengine ni ule wa kukusaidia wewe usitekwe, na kwa upande mwingine mtu ambae aliwahi kunipiga miaka mingi iliyopita ni Talib yule mtoto wa Mahamud, nadhani nilisha kusimulia kilichotokea kati yetu” alisema Higgno, ambae alikuwa ni kama anasisimkwa kwa kitendo cha Soraya kukaa mkao ule kwenye mapaja yake.
Kusikia hivyo Soraya akatulia kidogo kama anawaza jambo fulani, kisha akauliza, “kwanini usimuambie mzee Mahamud kama Talib alikufanyia fujo nyumbani kwenu” aliuliza Soraya akimaanisha siku ile alipokuja na Hilda kumuona mtoto wake, “Soraya siwezi kufanya hivyo, kwanza nasikia Talib sio mtoto wa Mahamud, tumezoea tu kumuita hivyo, sasa nikisema hivyo si nitaonekana nina mgombanisha na mjomba wake?” alisema Higgno, na hapo Soraya akatabasamu kidogo, “Higgno jamani unawezaje kuthamini maisha ya mtu mwingine kuliko ya kwako, yaani mtu ambae pengine ndie ana hatarisha maisha yako wewe unawaza kuhusu, maisha yake?” aliuliza Soraya kwa mshangao, na mastaajabu “huwa sipendi kutengeneza maadui, hasa ambao chanzo cha ugomvi sijui” alisema Higgno kwa sauti ya upole iliyojaa busara.
Mpaka hapo ni kama Soraya alikuwa ameshaanza kuhisi kuwa Talib anahusika na uchomaji wa duka la baba yake Higgno, sasa akaanza kutafuta njia sahihi ya kuthibitisha kuwa Higgno siyo mtu mbaya kama wazazi wake wanavyo hisi, “kwahiyo baba yako akimuona huyo Talib anaweza kumkumbuka?” aliuliza Soraya akiwa bado ameegemeza mikono yake kwenye mapaja ya Higgno, “sijajuwa labda nikamuulize, ila tuyaache hayo ngoja niandae chakula tule ni saa tatu kasoro sasa” alisema Higgno huku anajiinua pale alipokaa na kufanya Soraya atoke mapajani mwake, na wakati huo simu ya Higgno ikaanza kuita, “atakuwa baba huyo” alisema Higgno na kuitoa simu mfukoni, “mbona unajiami kwani hakuna mwingine wakukupiga hebu nione” alisema Soraya huku anakwapua simu toka mkononi kwa Higgno, lakini Higgno hakuonyesha wasi wasi wowote, “hoo kweli ni baba yako, halafu nime kumbuka nipe kwanza ile simu ya wale walioniteka” alisema Soraya huku anampatia Higgno simu yake ambayo aliinunua yeye mwenyewe, ni mara baada ya kuona aliempigia ni baba yake na sio mtu mwingine.*******
Yap Baada ya Talib kuingia ndani ya kijumba chake kizuri kidogo, akawasha udi na kuwasha bangi yake, kisha akaanza kuivuta taratibu, “sasa mambo yanaanza kukaa poa” aliwaza Tarib huku anatoa funguo na kuitazama, “yaani nikiukamata ule mkwanja, sijui itakuwaje?” alijisema Talib, huku anarudisha funguo mfukoni na kutoa simu nakufungua upande wa messeji, kisha akaanza kutafuta namba fulani aliyowahi kuitumia sms.
Talib alifanya hivyo kwa sekunde kadhaa mpaka alipo pata namba ya Zido, “yaani kesho ndio mwisho wa umasikini” alijisemea Talib, huku anaandika ujumbe kwenda kwa Zido, “funguo nimeshaupata nawaletea kesho mapema, jitahidini musifanye makosa kama kule shamba” kisha akaituma kwenye namba hiyo ya zido, alipo maliza akaiona sms nyingine aliyowahi kuituma kwa Zido, hapo akajisonya kidogo maana sio kwamba sms hii ilimuuzi, hapana sms hii aliyomtumiaga Zido siku ile ya jumapili iliyosema kuwa, “mjomba anataka kuwaambia polisi, hebu mtishieni” ni sms iliyomkumbusha “khaaa! hii simu si ameipoteza” alijisemea Talib huku ana anza kuandika tena ujumbe na wakati huo huo ikaja stutas report ikionyesha kuwa messeji deriverd, lakini hakujali, sijui ni kutokana na mibangi aliyo kuwa anaivuta au vipi, aliandika ujumbe mwingine na kuutuma kwa Vitus, nayo ikarudisha taarifa kuwa imepokelewa na jibu likaja baada ya dakika mbili, “poa hakikisha mambo yamekaa fresh” lilikuwa jibu la Vitus.*******
“hallow baba” alisikika Higgno mara baada ya kupokea simu huku anaelekea ndani, Soraya aliweza kufuatilia mazungumzo ya Higgno na baba yake, “kweli baba…… kwani anajuwa kama una mtoto mkubwa kama mimi….. hooo! lakini hajui kama mimi na fahamiana na baba yake sio?........ sawa …….. itakuwa saa ngapi?” alisikika Higgno akiuliza huku anatoka nje ya kibanda na simu nyingine mkononi, “sawa lakini nitamuambia na mchumba wangu afahamu asije akanifikiria vibaya” alisema Higgno, huku anampatia Soraya ile simu ya mkononi mwake Soraya, nae akaipokea huku anamtazama usoni kwa macho ya tabasamu la kumsuta, kwamba anamtaja mbele ya baba yake, “ndiyo nilimemsimulia….. si unajuwa na yeye lazima ajuwe kuhusu mshenga wetu” alisema Higgno kisha akakata simu na kumtazama Soraya ambae bado alikuwa anamtazama kwa macho ya tabasamu, “kwahiyo ulisha muambia baba yako kuwa mimi ni mchumba wako?” aliuliza Soraya huku anacheka kwa furaha, “mhhh!!!.... ndiyo ……. ndiyo nilimuambia, kwani wewe bado hujawaambia wazazi wako?” aliuliza Higgno huku anasogeza ndoo yake anayoifanya kama kiti akionyesha kuwa alikuwa anamkwepa Soraya, “ho! bado sijawaambia, inabidi mpaka mukija kuleta barua ya posa” alisema Soraya huku anavuta ndoo kuirudisha pale pale ilipokuwa, yaani karibu yake, “hooo! nimesahau kuchukuwa chakula……” alisema Higgno huku anandoka kurudi ndani, akimuacha Soraya anamtazama kwa macho ya kumcheka, maana Higgno alionyesha wazi bado hajiamini anapokuwa mbele yake, “kweli huyu ajawahi kuwa na mwanamke” aliwaza Soraya huku anatabasamu, na wakati huo huo akaona ujumbe unaingia kwenye ile simu aliyopewa na Higgno, akatazama jina la mtumaji wa ujumbe liliandikwa Talib mwarabu, “mh!” Soraya aliguna mwenyewe kwa mshtuko, huku anafungua ile sms ambako alikuta sms nyingi zimeongozana, yeye akafungua ile ya mwisho, “funguo nimeshaupata nawaletea kesho mapema, jitahidini musifanye makosa kama kule shamba” ndivyo ulivyo someka ujumbe ule uliotoka kwa Talib mwarabu, “mama yangu, Talib !!!!!” alijiuliza Soraya kwa sauti ya chini iliyojaa mshangao.
Naam wakati Higgno anaendelea kuandaa chakula, yaani anaingia na kutoka ndani, Soraya alikuwa kimya akifungua sms ya pili iliyotumwa na Talib Mwarabu kwa mmiliki wa simu ile ambayo yeye Soraya alimuona nayo mmoja kati ya watu sita waliomteka, “mjomba anataka kuwaambia polisi, hebu mtishieni” ndivyo ilivyosomeka sms ya pili, ukweli Soraya akazidi kushangazwa na jambo lile, hapo Soraya akaona bora aanze kusoma sms za mwanzo na ile kuifungua moja alijikuta anahisi kuzimia, maana hakuamini alicho kiona na kukisoma, kwamba kilikuwa ni kwaajili yake, endelea kufuatilia mkasa huu wa TEMBELE LA UWANI hapa hapa jamii forums
Mkuu hichi ndio cha kulalia?
 
Back
Top Bottom