Abou Shaymaa
JF-Expert Member
- Oct 19, 2022
- 2,117
- 5,240
- Thread starter
- #81
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA KUMI NA SABA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA KUMI NA SITA : wakina Higgno wakaendelea kumtazamia Hilda, hata giza lilipoingia na kwenda kulala bila kumuona mschana huyu, mpaka siku ya nne mida ya saa tano za usiku, wasi wasi ukiwa umetanda moyoni kwa Higgno na wazazi wake, wakihofia kupata kesi endapo kuna jambo baya lita kuwa lime mpata Hilda, Higgno akiwa chumbani kwake na mtoto wa hilda, kwenye mabanda ya uwani, na wazazi wake wakiwa chumbani kwao ndani ya nyumba kubwa, mara wakasikia muungurumo wa gari nje ya nyumba yao, hapo hofu zika zidi kuwa shika, wakidhania kuwa ni gari la polisi limekuja kuleta taarifa ya Hilda, kama sio kuwasomba, wakiwa wanaendelea kujiuliza ndipo wakaanza kusikia milio mikali mfululizo ya honi za gari ikilindima nje ya nyumba yao ………. ENDELEA NAYO
Nakufanya kuwa kero kwa kina Higgno ambao walishindwa kutoka kwa hofu, mara zile honi zika gota, “hebu nikawagongee, watakuwa wanashangaa tu! maana halijawahi kuja gari hapa nyumbani kwao” ilikuwa ni sauti ya kike iliyojaa ulevi wa kupindukia, “Hilda” jina hilo lilitajwa karibia na wote walioisikia, kuanzia baba na mama walioko nyumba kubwa, mpaka Higgno aliekuwepo kwenye chumba chake, sio yeye peke yake tu ambae aliinuka kitandani na kujiandaa kufungua mlango, hata wazazi wake pia, waliinuka kitandani na kuanza kujiandaa, kutoka nje wakashuhudie kinachoendelea huko nje.
Lakini kabla Higgno hajaufikia mlango akasikia mlango ukigongwa kwa fujo, tena ilionyesha kuwa mgongaji alitumia jiwe kugongea mlango, “fungua bwana usijifanye umelala, unawezaje kupata usingizi kwenye kibanda kama hiki?” ilikuwa ni sauti ya kilevi ya Hilda iliyojaa dharau na kebehi, maneno ambayo hata mzee Frank na mke wake waliyasikia, nao wakafungua mlango na kutoka nje, ambako waliweza kumuona Hilda akiwa amesimama Mbele ya mlango wa chumba cha Higgno, ameshika jiwe mkononi, lakini hakuwa peke yake alikuwa wanaume watatu nyuma yake, huku wote pamoja na Hilda mwenyewe wakipepesuka kwa ulevi.
Baba na mama Higno wakamuona Hilda akiugonga tena mlango wa chumba cha Higno, “fungua bwana wenzako tuna chelewa” alisema tena Hilda akiwa ana ugonga lango ule kwa fujo, “hivi huyu binti mbona amekuwa shetani hivi jamani” aliuliza mama Higgno kwa sauti ya chini, huku wakiendelea kuwatazama wakina Hilda pale mlangoni kwa Higgno, na wakaona mlango unafunguliwa, na kabla aHiggno haja toka nje, wakamuona Hilda ana ingia ndani kwa kumsukuma Higgno pale mlangoni, akifuatiwa na wale vijana watatu, “njoo baby umuone mwanao” alisikika Hilda, na hapo wakamuona Higgno anatoka nje ya chumba kile na kusimama mita kadhaa pembeni ya nyumba ile ndogo.
Naam sauti za vicheko na furaha vilivyo ambatana na sifa na hongera vilisikika toka kwenye ile nyumba ya Higno, “mwanangu hii ni chata yako kabisa” alisikika mmoja kati ya wale wanaume kwa sauti ya kilevi pia, ambae Higgno alimtambua kama Vitus, “nimemtolea kitu” alisikika Hilda, “siku moja inabidi nikamuonyeshe shangazi” alisema mmoja wao, ambae mimi na wewe msomaji tuna mfahamu kuwa ni Talib, “yaani mwanangu hili ni bonge la chata” alisifia tena mwingine, ambae japo alikuwa ndani lakini Higgno aliposikia alijua kuwa alikuwa ni yule mwingine ambae alimkumbuka kuwa ni yule aliemuona na Vitus siku ile wakiwa ndani ya gari wanawasubiri wale vijana wawili waliomvamia mzee Mahamud, “poa wana, tumwache dogo alale, twenzetu tukale bata” alisema Talib, na hapo wakatoka zao na kuelekea kwenye gari, “kesho inabidi nimpige shoping ya nguvu sana” alisikika Talib akiongea kwa kujigamba akiwa anaingia ndani ya gari, wote wakionyesha kuwa wamelewa sana na wenye furaha tele.
Higgno na wazazi wake waliwatazama wakina Hilda mpaka walipotoweka na gari lao, ndipo mama Higgno, alipomgeukia mume wake, “baba Higgno, haya mambo mwisho wake lini?” aliuliza mama Higgno kwa sauti iliyojawa na machungu yaliyotokana na dharau ya hilda ambayo sio kwamba ilifika kwa Higgno peke yake ila kwa familia nzima, “mpaka lini wakati leo ndiyo mwisho” alisema baba Higgno kwasauti iliyojaa hasira kali.
Usiku ule wakina Hilda hawakuishia kwa akina Higgno peke yake, ila walipotoka kwa Higno wakaenda nyumbani kwa kina Hilda, ysani kwa mzee Komba, ambako pia waliwakuta wamesha lala, nako wakapiga honi za fujo mpaka mzee Komba na mke wake ambao ni siku ya tatu sasa hawakuwa wameonja ulanzi, kutokana na kutoweka kwa binti yao Hilda ambae ndie mfadhiri wao wa ulanzi.
Huwezi amini japo walikuwa wamesha lala fofo, lakini ile kusikia honi za gari walikurupuka mara moja na kutoka nje, mzee Komba akiwa amejifunga shuka na mke wake akiwa amejifunga kitenge chakavu, hakika walistaajabika mara baada ya kuliona gari dogo likiwa lime simama mbele ya nyumba yao likiwamulika kwa mwanga mkali wa taa, ambapo kwa heshima ya kawaida, ni kwamba dereva anapofika sehemu kama hii hupunguza mwanga wa taa za gari au kuzima kabisa, maana haikuwa heshima kuwamulika wenyeji tena ukizingatia ni wazazi wa rafiki yao, kwao haikuwa kitu, walizidi kulishangaa lile gari maana haikuwahi kutokea gari kusimama nyumbani pao, toka nyumba ile imejengwa, zaidi ya kuyaona yakipita na njia, “nani hawa au wanaleta taarifa mbaya ya Hilda?” aliuliza mama Hilda huku mapigo ya moyo yakimuenda mbio, “mh! ndio usiku huu, si wangesubiri asubuhi” alisema mzee Komba, huku wakilikodolea macho gari lile, ambalo licha ya kuwa na muungurumo mbaya kutokana na kukosa huduma muhimu, kama kubarishwa oli za engine na gear box, lakini sauti kubwa ya music ilisikika kwafujo, mioyo yao iliongeza kasi ya kudunda mara walipo uona mlango wa mbele wa gari upande wa kushoto ukifunguliwa, “hoooo! kumbe ni Hilda mwanangu” alipiga kelele mama Hilda, huku akimkimbilia Hilda aliekuwa anashuka toka kwenye gari, mkononi ameshka chupa mbili kubwa za pombe kari, ile ambayo ina picha ya mtunisha misuri, huku Hilda mwenyewe anayumba yumba kama nyasi ndefu wakati wa upepo mkali wa masika, “ni mimi mwanao mama, nimeona nikuletee na wewe ujichane” alisema Hilda kwa sauti ya kilevi kweli kweli, hapo mzee Komba akatoka mbio akishikilia shuka lililotaka kumvuka na kuzidaka zile chupa za pombe, “hapo umefanya jambo la mbolea” alisema mzee Komba huku anavuja mate kama mama mjamzito alieona chachandu ya limao au embe bichi, maana kiukweli pombe hizi za kizungu aliwahi kunywa mara nne, mara ya kwanza kwenye harusi ya bwana Frank na mke wake mama Higgno, miaka zaid ya ishirini iliyo
pita, na mara moja ni miaka minne iliyopita yaani mwaka 2000, kipindi cha uchaguzi wakati wa kikao na mbunge wa kipindi hicho ambae kwa sasa ni marehemu, “baba we jiandae kufaidi, mkweo amesema atahakikisha kila siku unapata mizinga miwili” alisema Hilda kwa sauti ile ile ya kilevi, “yupo wapi huyo mkwe mbona ashuki kwenye gari?” aliuliza mama Hilda huku akisogea kwenye gari, “hooo! kumbe wewe baba, umemkumbuka mwenzio” alipaza sauti mama Hilda mara baada ya kumuona Talib, akiwa ametulia kwenye kiti cha dereva,
Kwa akili ya kawaida ungesema mara baaada ya mama huyu kumuona Talib pengine angemtimua na kumrudishia zile chupa za pombe, “ndio mama, mpotevu amerudi nyumbani” alisema Talib huku akicheka cheka kilevi, huwezi amini ndio kwanza mama huyu alipiga magoti na kusema, “asante baba yangu karibu sana, hapa ni kwako, karibu sana” alisema mama Hilda huku akiwa bado amepiga magoti, na wakati huo mzee Komba nae akasogea kumuona mkwe wake, nae kama mke wake, japo hakupiga magoti lakini alipomuona mkwewe na kumkumbuka, akamsalimia kwa furaha zote, “karibu sana baba, maana walikuwa wanatusema vibaya, eti umemkataa mwenzio na kwamba umetelekeza na mtoto” alisemelea mzee Komba, “mzee utawaziba mdomo, maana tarajia mambo makubwa zaidi” alisema Talib, kwa sauti ile ile ya kilevi.
Naam baada ya maongezi na ahadi nyingi, Hilda akaingia kwenye gari kisha wakaondoka zao, kwa ahadi ya kwamba kesho Hilda angekuja kuwaletea fedha na pombe, huku nyuma mzee Komba na mke wake, wakaanza kunywa konyagi zao, wakianza na chupa ya kwanza ambayo mpaka wanaimaliza ilishatimia saa tisa za usiku, wakashauriana ya kwamba ile iliyobakia wainywe kesho.*******
Naam Kitu ambacho ambacho Talib hakuwa amekijua usiku ule ni kwamba wakati yeye anaendelea kutumia fedha zake zinazotokana na biashara ya samaki na dagaa wa ziwa Nyasa, huku kiasi kikubwa cha fedha hizo zikiwa ni mtaji, na sio faida kama wengine wanavyo fanya, Huku mzee Mahamud alikuwa anaingia na msafara wa mabasi mapya kabisa, ambayo alihitaji kuyapangia safari za mikoani, ikiwa na kuajiri wafanya kazi wapya, ambao watachanganyika na wale wa zamani ili kuyatumia magari hayo, ndio alikuwa anaingia mkoani Ruvuma, na sasa ni mjini songea na kwenda kuyaegensha kwenye gereji yake kubwa iliyopo pembezoni mwa ghara kuu la mkoa wa Ruvuma, ambako alipokelewa na mke wake na bint binti yake Soraya, “mwanangu nimekukosa siku tano tu, nakuona umezidi kuwa mkubwa na mng’aavu, bila shaka kuna ujumbe mzito nitaukuta kwa mama yako” alitania mzee Mahamud, wakiwa njiani wanaelekea nyumbani, ambae kiukweli hilo ndilo lilikuwa tarajio lake kwa umri wa Soraya, mschana ambae hajawahi kumletea aibu, Soraya aliekuwa anaendesha gari alicheka kidogo, “mh! ujumbe gani, unadhani soraya anapango wa kuolewa, angekuwa mkristu tungesema anataka kuwa sister, sijui sasa anataka kuwa nani?” alisema mama Soraya, aliekuwa amekaa seat ya nyuma pembeni ya Soraya aliekuwa dereva, “lakini mama si nimesha kuambia kuwa nikimuona mwanaume mwenye sifa nzuri nitakuambia?” alisema Soraya kwa sauti ya kulalamika, kwamba mama yake anashindwa kumuelewa, ni kama jibu la soraya lilimuingia mzee Mahamud, japo alikaa kimya mpaka walipofika nyumbani na kuingia chumbani kwao, “lakini ni kweli mama Soraya, unajua vijana wengi watakuwa wanahitaji kuwa na Soraya kutokana na sababu nyingine na sio upendo wa kweli, wengi watakuwa na tamaa ya kuwa ni mtoto wa tajiri” alisema mzee Mahamud kwa sauti ya upole, wakati akipembua nguo zake tayari kuingia bafuni, “lakini kumbuka kuwa Soraya pia ni mzuri na mrembo, hivyo sio ajabu kupendwa na mvulana yoyote” alisema mama Soraya, aliekuwa anaweka vizuri begi alilokuja nalo mume wake, “umeongea vyema mke wangu, hapo unaweza kuona ugumu alionao Soraya katika kujua yupi anampenda kweli na yupi anamtamani yeye au utajiri wake” alisema mzee Mahmudu kabla hajaonekana kukumbuka jambo, “hivi sijamuona Talib akija kunipokea, au amkumjulisha kama narudi” aliuliza mzee Mahamud ambae kiukweli alitokea kumuamini, sana Talib kuwa amebadilika kwa tabia, “mh! ukweli ni siku ya nne hatuja muona Talib, pengine amesafiri kwenda Nyasa” alisema mama Soraya.********
Ilikuwa hivi usiku ule ule, mara baada ya bwana Mahamud kupita kwenye lango la jumba lake, mlinzi akarudishia gate na kumpigia Talib, ambae hakupokea simu, akaamua kutuma ujumbe ili muda wowote akishika simu yake auone, “Boss amesharudi” hayo ndio yalikuwa makubaliano ya Talib na mlinzi huyo, ambae ndie alikuwa mshirika wake kwa hapa nyumbani, maana hata anapotoka au kurudi usiku sana, akiwa peke yake au na mwanamke yeyote, yeye ndie anae mfungulia lango, na pengine kumsaidia kuwatoa asubuhi sana wakati wa swala ya Alfajiri.
Ujumbe ule ulimfikia Talib saa moja za asubuhi, akiwa ndani ya chumba cha guest moja bubu ya uswahilini kweli kweli, ni mara baada kukurupuka toka kitandani akiwa amesha jikojolea, ni baada ya kushindwa kuamka akipitiwa na usingizi mzito, kutokana na pombe alizo kunywa jana usiku, na alipousoma ule ujumbe toka kwa mlinzi akainuka haraka na kuokota nguo zake zilizokuwa chini sakafuni, akaziokota na kuzipachika mwilini mwake na kujikagua mfukoni kwa kile alichobakia nacho, alikuwa na shilingi elfu tano tu! akairudisha mfukoni akachukuwa simu yake na funguo za gari akatoka mbio mbio kuelekea nje akimuacha Hilda bado amelala anakoroma kwa usingizi wa pombe, Talib alipitia sokoni akanunua dagaa nyasa wa elfu mbili na samaki wa elfu tatu, kisha akaelekea nyumbani, ambako aliwakuta wanafamilia wakiwa wameshaenda kwenye mihangaiko yao, akakabidhi wale dagaa na samaki, ikiwa ni alama ya kuwa ametokea Nyasa, kisha akamueleza mlinzi kuwa akija mwanamke yeyote kumuulizia amwambie kuwa hayupo, kisha kusema hivyo, Talib akaingia ndani kwake na kwenda kujilaza kwa lengo la kufidia usingizi wa siku nne akiwa na Hilda.
lakini ukweli ni kwamba Talib hakupata hata tone moja la usingizi, sio kwamba aliwaza kuhusu Hilda aliemuacha guest bubu, hakuwaza kuhusu mwanae na ahadi aliyoitoa ya kumfanyia shoping leo hii, hakuwaza kuhusu wakwe zake ambao jana usiku walipiga magoti mbele yake na alijua fika kuwa, mpaka sasa watakuwa wanasubiri chupa za pombe ili waendelee kulewa, ukweli Talib aliwaza juu ya kupata fedha ambayo itarudisha mtaji wa biashara yake, ambayo leo asubuhi ndiyo amemalizia elfu tano ya mwisho kwa kununua dagaa na samaki za kuwadanganyia mjomba na shangazi yake, “lazima mpango wangu ufanikiwe, siwezi kuishi kindezi, mjomba mwenyewe haeleweki, yeye anampa ulaji Soraya wakati mimi kidume nipo” aliwaza Talib, akisahau kuwa Soraya ndie mwenye haki zote za kuwa katika nafasi aliyopo, kwasababu ni mtoto wa Mahamud.******
Huku Luhuila seko nako, asubuhi hii tayari taarifa za Hilda kurudiana na Talib zilisha anza kuzagaa, huku bwana Komba ambae ni kama aliamka na pombe kichwani akitambaza taarifa hizo, ambazo baadhi ya watu walishindwa kuzielewa, maana walichojua wao ni kwamba, Hilda anaishi na Higgno kijana wa mzee Frank.
Mzee Komba alienda kwa mzee Nganyanyuka na kukopa lita ishirini za ulanzi kwa ahadi ya kulipa jioni akiamini kuwa mwanae Hilda atamletea shilingi elfu tatu ya kulipia pombe hiyo, ambayo aliipeleka pale kwake na kuwaita rafiki zake wakina Nyoni, Njogopa, Ngonyani, na wengine kibao, hasa wale waliokuwepo siku ile ya ndoa ya mkeka kwa mzee Frank, na kuanza kunywa pombe hiyo wakishushia supu ya mboga za majani ya maboga, wenyewe wanaita pitiku, na kuendelea kunywa ulanzi wakichangia konyagi, huku wakiamini kuwa kuna nyingine zinakuja baadae.*****
Mida hii mschana mrembo Soraya, alikuwa njiani na dereva wake wanatoka SeedFarm ya Lumecha, kilomita kama ishirini toka songea mjini, ambako alienda kuweka oda ya mbegu za miti ya matunda kwaajili ya kupanda shambani kwake sehemu ambayo alikuwa na malengo nayo makubwa sana, sio shamba pekee ila alikuwa na mpango wa kutengeneza hotel kubwa sana sehemu hiyo na kuanza kutangaza utalii wa kusini mwa tanzania hasa upande wa nyuma ya mji wa songea, ambako kulikuwa na vivutio vingi vya utalii, “da Laylah, unamkumbuka yule kijana alienisaidiaga siku ile nilivyo kamatwa na wanafunzi wa songea boys?” aliuliza Soraya wakati safari inaendelea, “na mkumbuka sana da Soraya inaonyesha unampenda sana yule kaka, yani bado unamkumbuka mpaka leo?” aliuliza Laylah huku anacheka cheka, “mh! sijui kama nampenda, lakini…. lakini… nataka tu nimuone nimuabie asante, kwasababu bila yeye ningesha poteza uschana wangu kwa aibu kubwa sana, tena sio kwangu tu! hata kwa wazazi wangu” alisema Soraya huku safari inaendelea, “halafu kwanini hatukuwahi kurudi kule matogoro kumtafuta tena?” aliuliza Laylah, akionyesha kujishangaa, “kweli bwana, hivi kwanini hatukuwahi kumtafuta kwenye ile barabara, hata hivyo mbona tumepita sana ile barabara lakini hatuja muona, kila ijumaa tunaenda shambani na tunapita kule kule?” aliuliza Soraya, “usikute alikuwa ni mwanachuo na alitokea mkoa mwingine” alisema Laylah, “mh! kwa umri wake yule kama alikuwa anasoma basi ni form one au two” alijibu Soraya, “kama ni hivyo basi sasa hivi atakuwa na mke na watoto kabisa” alisema Laylah, na kauli hiyo ilionekana kummaliza nguvu Soraya, ambae hakujibu kitu zaidi ya kukaa kimya mpaka walipoingia mjini.*******
Wakati mzee Komba akiwa ana fanya yake, hakujuwa kuwa mwanae Hilda ndio kwanza alikuwa anagongewa mlango na muhudumu wa Guest bubu hii, ambayo haitambuliki na msajili wa nyumba za wageni na kushtuliwa toka usingizini, akatazama pembeni yake pale alipolala Talib jana usiku hakuona mtu, na alipo tazama vizuri hakuoan dalili ya uwepo wa mtu huyu, kwa maana ya kwamba hakukuwa na nguo wala viatu vya Talib, zaidi ya mkojo alioumwaga kitandani, “we dada si ufungue mlango lisaa limepita toka saa nne” ilisikika sauti ya mhudumu wa kike toka nje ya mlango, “nilikuwa navaa dada yangu” alisema Hilda huku anafungua mlango ambao haukuwa umefungwa na funguo zaidi ya kuegeshwa na kitasa(kubugazwa), “yaani mwenzio ameondoka mapema tu, wewe unalala mpaka saa tano, unadhani usafi nitafanya saangapi, halafu akikukuta boss si atasema nimechukua hela yako ya leo” alisema yule mhudumu huku anaingia mule chumbani na kuanza kupembua mashuka, “nisamehe dada yangu nilipitiwa na usingiz..” kabla hajamaliza kuongea akakatishwa na yule mhudumu, “usinitanie wewe dada ndio maana ulikuwa umejifungia humu chumbani, kumbe umemwaga mkojo” alisema yule mhudumu, huku ameshika yale mashuka………haya sasa mambo yanazidi kuwa pambe, baba Higgno kawaka kwa dharau walizofanyiwa na hilda, mzee komba ndio huyooo na marafiki zake wana matumain makuuuuubwa huku hilda kakimbiwa gesti na talibu, soraya nae anamtaka kijana mpole amshukuru kwa kumuokoa miaka mingi iliyopita nini kitaendeleaaaa.... Usikose sehemu inayofuata.
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA KUMI NA NANE
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA KUMI NA SABA : “yaani mwenzio ameondoka mapema tu wewe una lala mpaka saa tano, unadhani usafi nitafanya saangapi, halafu akikukuta boss si atasema nimechukuwa hela yako ya leo” alisema yule mhudumu huku anaingia mule chumbani na kuanza kupembue mashuka, “nisamehe dada yangu, nilipitiwa na usingiz..” kabla hajamaliza kuongea akakatishwa na yule muhudumu, “usinitanie wewe dada ndio maana ulikuwa umejifungia humu chumbani, kumbe umemwaga mkojo” alisema yule muhudumu, huku ameshika yale mashuka……ENDELEA SASA
“mkojo?, labda Talib ndie alielala upande huo” alijitetea Hilda ambae mpaka hapo hakujuwa ni kwanini Talib aliondoka na kumuacha hapo guest, “usinitanie we dada nenda kafue uchafu sijui wa bwana wako, sasa unataka akufulie nani?” ndivyo ilivyo kuwa kwa Hilda, kabla hajaondoka hapo Guest alikabidhiwa mashuka na kuyafua kwanza, nae alifanya hivyo huku akiwaza kwanini Talib aliondoka kimya kimya, “labda alipigiwa simu anaitwa haraka, maana anaonyesha kuwa bado ananipenda, si unaona ameahidi kunipa hela za kumnunulia mtoto nguo, halafu aliwaambia wakina mama kuwa atawaletea pombe nyingine” alijipa moyo Hilda, ambae mwisho akapanga kuwa akimaliza kufua aende nyumbani kwa akina Talib akachukue fedha za matumizi kisha aende nyumbani, na kama Talib atapata nafasi atamfuata huko huko kwao.*****
Wakati huo pia mzee Frank, aliondoka nyumbani kwake yeye na mwanae Higgno na mke wake, wakiwa wame mbeba mtoto wa Hilda mpaka kwa mwenyekiti, ambae walimueleza kilichotokea jana usiku nyumbani kwao, nae mwenyekiti, akawaita wajumbe wawili wa nyumba kumi na kuelekea nyumbani kwa mzee Komba, ambako walifika pale saa tano za asubuhi na kukuta watu kibao wakiendelea na sherehe ya pombe, huku wakiongea na kucheka kwa furaha, wakionekana wameshaanza kulewa ulanzi, “hooo! mwenyekiti samahani bwana nilisahau kukualika” alisema mzee Komba huku anainuka na kuwasogelea wageni hawa, ambao hata alipowaona akushukuru kwa ujio wao, “usijali bwana Komba tume jialika wenyewe” alisema mwenyekiti, nao wakapewa viti, sehemu za kukalia ambazo zilikuwa ni matofari kutokana na uhaba wa viti, “hapana bwana Komba hatuwezi kunywa pombe mapema hii, labda tukueleze kilicho tuleta hapa kwako” alisema mwenyekiti baada ya kuona wana letewa vikombe vilivyo jazwa ulanzi, “lakini musituharibie sherehe yetu tafadhari” alisema mzee Njogopa kwa sauti ya kilevi, tena imekuwa vyema tume wakuta nyie ambao mulikuwepo usiku ule ambao tulimkuta Hilda kwa huyu kijana na kumkabidhi kuwa mke wake” alisema mwenye kiti akimuonyesha Higno, “mwenyekiti unazunguka sana, nenda kwenye point” alisisitiza Ngonyani.
Hapo mwenyekiti akaanza kueleza kilicho waleta pale nyumbani kwa mzee Komba, “bwana Komba nadhani unakumbuka siku ile ambayo tulimfumania binti yako nyumbani kwa bwana Frank, akiwa na huyu kijana wa bwana Frank yaani Higgno?” aliuliza mwenyekiti huku akimtazama mzee Komba, “hakuna asiekumbuka mwenyekiti hata sisi tulikuwepo, si ndio tukawapiga gundi kwa mkeka?” alisema Njogopa, kwa sauti ya kilevi, “haswaaaa, najua mulikuwepo, lakini itapendeza kama akijibu bwana Komba” alisema mwenyekiti kwa msisitizo, “ndio nakumbuka bwana mwenyekiti” alijibu mzee Komba yaani baba yake Hilda kwa sauti ya kilevi, “sawa sawa bwana Komba, sasa kuhusiana na hilo, kuna jambo limetokea jana usiku” alisema mwenyekiti, “nilijua tu, yaan tayari imesha kuwa nongwa” alisema mama Hilda kwa sauti ya chini chini, huku anatazama pembeni na kubetua midomo ya kubeza.
Mwenyekiti akamtaka mzee Frank, aeleze kilicho tokea mwanzo mpaka mwisho, na nia ya kuja pale kwa mzee Komba.*******
Naam baada ya kumaliza kufua mashuka ya mikojo, akaruhusiwa kutoka, nae akatoka zake akiwa amevalia nguo zile zile alizotoka nazo nyumbani kwa Higgno siku tano zilizopita, huku njaa ikiwa ina mchamanda kweli kweli, moja kwa moja akaelekea upande wa mjini, alitumia nusu saa kufika kwenye lango la nyumba ya mzee Mahamud akagonga na kufunguliwa mlango mdogo, “habari yako binti, nikusaidie nini?” aliuliza mlinzi huku anamtazama kwa umakini sana Hilda, “nashida na Talib” alisema Hilda kwa sauti ya tahadhari, “mh! we binti bado tu unamganda Talib, wewe si ndie yule uliekuja na wale wazee ulikuwa na mimba?” aliuliza mlinzi kwa sauti ya kutia shaka, “ndio lakini siku hizi ni mpenzi wangu” alisema Hilda kwa sauti fulani hivi ya kujiamini, “yeye anajua kama unakuja sasa hivi, maana mademu wake huwa hawaji mchana, na ameniambia kuwa akija mtu kumuulizia nimwambie hayupo” alisema mlinzi ambae alionekana kumtazama hilda kama mschana alie danganyika kabisa, “we mwambie tu Hilda anakuhitaji hapo nje” alisema Hilda kwa sauti ile ile ya kujiamini, ambae muda huo ukimsogelea ungeweza kuisikia harufu kali ya pombe, na ukizubaa unaweza kulewa kwa harufu hiyo iliyo changanyika na kutokupiga mswaki, “sawa lakini utakubaliana na majibu yatakayo toka, maana mi navyomjuwa Talib huwa hapendi kufuatwa na wanawake hapa nyumbani” alisema yule mlinzi huku anaingia ndani na kufunga lile geti dogo.
Hilda alisimama pale getini kwa dakika tano nzima, njaa ikizidi kumuuma, akimsubiri Talib ambae aliamini kuwa angetoka, mara hilda akasikia gate likianza kufunguliwa, akatabasamu kwa furaha, gate likafunguliwa na akatokea Talib akiwa amekunja uso kwa hasira na chuki, “we! mpumbavu umefuata nini hapa, au unataka kuni haribia kwa mjomba?” aliuliza Talib kwa sauti ya chini, lakini yenye ukali na hasira, “lakini Talib, si ulisema utanipa hela ya kumnunulia nguo mtoto” alisema Hilda kwa sauti ya mshangao, “hivi wewe unaniona mimi fala, yaani mtoto wa mtu mwingine halafu mimi nikamnunulie nguo?” aliuliza Talib, na kumshangaza Hilda ambae alimtazama Talib kama vile ndio anamuona leo kwa mara ya kwanza, “Talib jamani si ulimuona alivyofanana na wewe, usifanye hivyo Talib, mtoto ni wa kwako” alisema Hilda kwa sauti ya kuhuzunisha iliyokaribia kuangua kilio, “anafanana na nani, unadhani angekuwa wangu Higgno angekubali kuishi na wewe na mtoto, yaani wewe unakaa huku siku nne, yeye akae na mtoto ambae sio wa kwake, inawezekana vipi, kama unampenda huyo mwanao si ungeacha kunywa pombe halafu hela ungenunua nguo, hebu ondoka tena usiridi hapa” aliongea kwa harisa na sauti iliyojaa ghadhabu, kama uliwaona jana hakika leo ungeshangaa ni kwanini leo hii Talib yupo hivi.
Ukweli ni kwamba Talib sio tu hakuwa na mapenzi na Hilda, zaidi ya kumchezea na kukata kiu yake, pia alimchukia na kumuona kuwa ndie aliemsababishia akamaliza fedha za biashara yake ya samaki, “basi sawa naomba hata mia mbili ya nauuli” alisema Hilda ambae kiukweli hakuwa na hata shilingi moja, maana hata fedha aliyokuja nayo mjini siku ile alishaitumia siku nyingi, “acha useng.. wewe hela itoke wapi, hebu jikatae haraka usije kunijazia nzi hapa” alisema talib na kufunga gate, akibakia ndani huku Hilda akiwa nje, “jamani Talib, nimekukosea nini lakini? umeshaniharibia kwa Higgno na leo unanifanyia hivi” alilalamika Hilda kwa sauti ambayo ilishindwa kuficha kilio chake.******
“kwahiyo unataka kusemaje, unataka Hilda arudi kwa Higgno au?” aliuliza mzee Komba kwa sauti ya dharau na kebehi na kuwafanya wenzake wakina Nyoni wacheke kwa dharau, ilikuwa ni mara baada ya mzee Frank, kumaliza kuelezea jinsi ilivyokuwa toka siku Hilda alipotoweka, mpaka jana usiku alipoletwa na gari, akiwa pamoja na Talib wakija kumtazama mtoto wao, kisha kuondoka pamoja wakiacha maneno ya kashfa, “unadhani hata Hilda mwenyewe atakubali ujinga kama huo” alijibu bwana Ngonyani, huku wakiendelea kucheka, “bwana Komba, nikiwa kama mwenyekiti ambae nilifungisha ile ndoa ya mkeka ya Higgno na Hilda, leo hii naitengua rasmi” alisema mwenyekiti na hapo kikafuata kicheko cha kejeri, toka kwa mzee Komba na rafiki zake, “yaani mwenyekiti kama ungechelewa nilipanga nije kwako kukueleza swala hilo hilo, unajua huyu kijana sio wa hadhi ya mwanangu, ni kama alikuwa anamfuja tu! subiri sasa uone atakavyo nawiri, na kwa taarifa fupi ni kwamba yule kijana amesema tuandae makoo yetu, kila siku itakuwa ni pombe za kizungu tu!” alisema mzee komba kwa sauti ambayo kama ungeisikia kwa jinsi ilivyojawa na dharau, pengine ungerusha ngumi, kwa hasira, Naaam huyo ndio mzee komba hajui lolote linaloendelea kuhusu Hilda, nini kitajiriiiii? ITAENDELEA.
SEHEMU YA KUMI NA SABA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA KUMI NA SITA : wakina Higgno wakaendelea kumtazamia Hilda, hata giza lilipoingia na kwenda kulala bila kumuona mschana huyu, mpaka siku ya nne mida ya saa tano za usiku, wasi wasi ukiwa umetanda moyoni kwa Higgno na wazazi wake, wakihofia kupata kesi endapo kuna jambo baya lita kuwa lime mpata Hilda, Higgno akiwa chumbani kwake na mtoto wa hilda, kwenye mabanda ya uwani, na wazazi wake wakiwa chumbani kwao ndani ya nyumba kubwa, mara wakasikia muungurumo wa gari nje ya nyumba yao, hapo hofu zika zidi kuwa shika, wakidhania kuwa ni gari la polisi limekuja kuleta taarifa ya Hilda, kama sio kuwasomba, wakiwa wanaendelea kujiuliza ndipo wakaanza kusikia milio mikali mfululizo ya honi za gari ikilindima nje ya nyumba yao ………. ENDELEA NAYO
Nakufanya kuwa kero kwa kina Higgno ambao walishindwa kutoka kwa hofu, mara zile honi zika gota, “hebu nikawagongee, watakuwa wanashangaa tu! maana halijawahi kuja gari hapa nyumbani kwao” ilikuwa ni sauti ya kike iliyojaa ulevi wa kupindukia, “Hilda” jina hilo lilitajwa karibia na wote walioisikia, kuanzia baba na mama walioko nyumba kubwa, mpaka Higgno aliekuwepo kwenye chumba chake, sio yeye peke yake tu ambae aliinuka kitandani na kujiandaa kufungua mlango, hata wazazi wake pia, waliinuka kitandani na kuanza kujiandaa, kutoka nje wakashuhudie kinachoendelea huko nje.
Lakini kabla Higgno hajaufikia mlango akasikia mlango ukigongwa kwa fujo, tena ilionyesha kuwa mgongaji alitumia jiwe kugongea mlango, “fungua bwana usijifanye umelala, unawezaje kupata usingizi kwenye kibanda kama hiki?” ilikuwa ni sauti ya kilevi ya Hilda iliyojaa dharau na kebehi, maneno ambayo hata mzee Frank na mke wake waliyasikia, nao wakafungua mlango na kutoka nje, ambako waliweza kumuona Hilda akiwa amesimama Mbele ya mlango wa chumba cha Higgno, ameshika jiwe mkononi, lakini hakuwa peke yake alikuwa wanaume watatu nyuma yake, huku wote pamoja na Hilda mwenyewe wakipepesuka kwa ulevi.
Baba na mama Higno wakamuona Hilda akiugonga tena mlango wa chumba cha Higno, “fungua bwana wenzako tuna chelewa” alisema tena Hilda akiwa ana ugonga lango ule kwa fujo, “hivi huyu binti mbona amekuwa shetani hivi jamani” aliuliza mama Higgno kwa sauti ya chini, huku wakiendelea kuwatazama wakina Hilda pale mlangoni kwa Higgno, na wakaona mlango unafunguliwa, na kabla aHiggno haja toka nje, wakamuona Hilda ana ingia ndani kwa kumsukuma Higgno pale mlangoni, akifuatiwa na wale vijana watatu, “njoo baby umuone mwanao” alisikika Hilda, na hapo wakamuona Higgno anatoka nje ya chumba kile na kusimama mita kadhaa pembeni ya nyumba ile ndogo.
Naam sauti za vicheko na furaha vilivyo ambatana na sifa na hongera vilisikika toka kwenye ile nyumba ya Higno, “mwanangu hii ni chata yako kabisa” alisikika mmoja kati ya wale wanaume kwa sauti ya kilevi pia, ambae Higgno alimtambua kama Vitus, “nimemtolea kitu” alisikika Hilda, “siku moja inabidi nikamuonyeshe shangazi” alisema mmoja wao, ambae mimi na wewe msomaji tuna mfahamu kuwa ni Talib, “yaani mwanangu hili ni bonge la chata” alisifia tena mwingine, ambae japo alikuwa ndani lakini Higgno aliposikia alijua kuwa alikuwa ni yule mwingine ambae alimkumbuka kuwa ni yule aliemuona na Vitus siku ile wakiwa ndani ya gari wanawasubiri wale vijana wawili waliomvamia mzee Mahamud, “poa wana, tumwache dogo alale, twenzetu tukale bata” alisema Talib, na hapo wakatoka zao na kuelekea kwenye gari, “kesho inabidi nimpige shoping ya nguvu sana” alisikika Talib akiongea kwa kujigamba akiwa anaingia ndani ya gari, wote wakionyesha kuwa wamelewa sana na wenye furaha tele.
Higgno na wazazi wake waliwatazama wakina Hilda mpaka walipotoweka na gari lao, ndipo mama Higgno, alipomgeukia mume wake, “baba Higgno, haya mambo mwisho wake lini?” aliuliza mama Higgno kwa sauti iliyojawa na machungu yaliyotokana na dharau ya hilda ambayo sio kwamba ilifika kwa Higgno peke yake ila kwa familia nzima, “mpaka lini wakati leo ndiyo mwisho” alisema baba Higgno kwasauti iliyojaa hasira kali.
Usiku ule wakina Hilda hawakuishia kwa akina Higgno peke yake, ila walipotoka kwa Higno wakaenda nyumbani kwa kina Hilda, ysani kwa mzee Komba, ambako pia waliwakuta wamesha lala, nako wakapiga honi za fujo mpaka mzee Komba na mke wake ambao ni siku ya tatu sasa hawakuwa wameonja ulanzi, kutokana na kutoweka kwa binti yao Hilda ambae ndie mfadhiri wao wa ulanzi.
Huwezi amini japo walikuwa wamesha lala fofo, lakini ile kusikia honi za gari walikurupuka mara moja na kutoka nje, mzee Komba akiwa amejifunga shuka na mke wake akiwa amejifunga kitenge chakavu, hakika walistaajabika mara baada ya kuliona gari dogo likiwa lime simama mbele ya nyumba yao likiwamulika kwa mwanga mkali wa taa, ambapo kwa heshima ya kawaida, ni kwamba dereva anapofika sehemu kama hii hupunguza mwanga wa taa za gari au kuzima kabisa, maana haikuwa heshima kuwamulika wenyeji tena ukizingatia ni wazazi wa rafiki yao, kwao haikuwa kitu, walizidi kulishangaa lile gari maana haikuwahi kutokea gari kusimama nyumbani pao, toka nyumba ile imejengwa, zaidi ya kuyaona yakipita na njia, “nani hawa au wanaleta taarifa mbaya ya Hilda?” aliuliza mama Hilda huku mapigo ya moyo yakimuenda mbio, “mh! ndio usiku huu, si wangesubiri asubuhi” alisema mzee Komba, huku wakilikodolea macho gari lile, ambalo licha ya kuwa na muungurumo mbaya kutokana na kukosa huduma muhimu, kama kubarishwa oli za engine na gear box, lakini sauti kubwa ya music ilisikika kwafujo, mioyo yao iliongeza kasi ya kudunda mara walipo uona mlango wa mbele wa gari upande wa kushoto ukifunguliwa, “hoooo! kumbe ni Hilda mwanangu” alipiga kelele mama Hilda, huku akimkimbilia Hilda aliekuwa anashuka toka kwenye gari, mkononi ameshka chupa mbili kubwa za pombe kari, ile ambayo ina picha ya mtunisha misuri, huku Hilda mwenyewe anayumba yumba kama nyasi ndefu wakati wa upepo mkali wa masika, “ni mimi mwanao mama, nimeona nikuletee na wewe ujichane” alisema Hilda kwa sauti ya kilevi kweli kweli, hapo mzee Komba akatoka mbio akishikilia shuka lililotaka kumvuka na kuzidaka zile chupa za pombe, “hapo umefanya jambo la mbolea” alisema mzee Komba huku anavuja mate kama mama mjamzito alieona chachandu ya limao au embe bichi, maana kiukweli pombe hizi za kizungu aliwahi kunywa mara nne, mara ya kwanza kwenye harusi ya bwana Frank na mke wake mama Higgno, miaka zaid ya ishirini iliyo
pita, na mara moja ni miaka minne iliyopita yaani mwaka 2000, kipindi cha uchaguzi wakati wa kikao na mbunge wa kipindi hicho ambae kwa sasa ni marehemu, “baba we jiandae kufaidi, mkweo amesema atahakikisha kila siku unapata mizinga miwili” alisema Hilda kwa sauti ile ile ya kilevi, “yupo wapi huyo mkwe mbona ashuki kwenye gari?” aliuliza mama Hilda huku akisogea kwenye gari, “hooo! kumbe wewe baba, umemkumbuka mwenzio” alipaza sauti mama Hilda mara baada ya kumuona Talib, akiwa ametulia kwenye kiti cha dereva,
Kwa akili ya kawaida ungesema mara baaada ya mama huyu kumuona Talib pengine angemtimua na kumrudishia zile chupa za pombe, “ndio mama, mpotevu amerudi nyumbani” alisema Talib huku akicheka cheka kilevi, huwezi amini ndio kwanza mama huyu alipiga magoti na kusema, “asante baba yangu karibu sana, hapa ni kwako, karibu sana” alisema mama Hilda huku akiwa bado amepiga magoti, na wakati huo mzee Komba nae akasogea kumuona mkwe wake, nae kama mke wake, japo hakupiga magoti lakini alipomuona mkwewe na kumkumbuka, akamsalimia kwa furaha zote, “karibu sana baba, maana walikuwa wanatusema vibaya, eti umemkataa mwenzio na kwamba umetelekeza na mtoto” alisemelea mzee Komba, “mzee utawaziba mdomo, maana tarajia mambo makubwa zaidi” alisema Talib, kwa sauti ile ile ya kilevi.
Naam baada ya maongezi na ahadi nyingi, Hilda akaingia kwenye gari kisha wakaondoka zao, kwa ahadi ya kwamba kesho Hilda angekuja kuwaletea fedha na pombe, huku nyuma mzee Komba na mke wake, wakaanza kunywa konyagi zao, wakianza na chupa ya kwanza ambayo mpaka wanaimaliza ilishatimia saa tisa za usiku, wakashauriana ya kwamba ile iliyobakia wainywe kesho.*******
Naam Kitu ambacho ambacho Talib hakuwa amekijua usiku ule ni kwamba wakati yeye anaendelea kutumia fedha zake zinazotokana na biashara ya samaki na dagaa wa ziwa Nyasa, huku kiasi kikubwa cha fedha hizo zikiwa ni mtaji, na sio faida kama wengine wanavyo fanya, Huku mzee Mahamud alikuwa anaingia na msafara wa mabasi mapya kabisa, ambayo alihitaji kuyapangia safari za mikoani, ikiwa na kuajiri wafanya kazi wapya, ambao watachanganyika na wale wa zamani ili kuyatumia magari hayo, ndio alikuwa anaingia mkoani Ruvuma, na sasa ni mjini songea na kwenda kuyaegensha kwenye gereji yake kubwa iliyopo pembezoni mwa ghara kuu la mkoa wa Ruvuma, ambako alipokelewa na mke wake na bint binti yake Soraya, “mwanangu nimekukosa siku tano tu, nakuona umezidi kuwa mkubwa na mng’aavu, bila shaka kuna ujumbe mzito nitaukuta kwa mama yako” alitania mzee Mahamud, wakiwa njiani wanaelekea nyumbani, ambae kiukweli hilo ndilo lilikuwa tarajio lake kwa umri wa Soraya, mschana ambae hajawahi kumletea aibu, Soraya aliekuwa anaendesha gari alicheka kidogo, “mh! ujumbe gani, unadhani soraya anapango wa kuolewa, angekuwa mkristu tungesema anataka kuwa sister, sijui sasa anataka kuwa nani?” alisema mama Soraya, aliekuwa amekaa seat ya nyuma pembeni ya Soraya aliekuwa dereva, “lakini mama si nimesha kuambia kuwa nikimuona mwanaume mwenye sifa nzuri nitakuambia?” alisema Soraya kwa sauti ya kulalamika, kwamba mama yake anashindwa kumuelewa, ni kama jibu la soraya lilimuingia mzee Mahamud, japo alikaa kimya mpaka walipofika nyumbani na kuingia chumbani kwao, “lakini ni kweli mama Soraya, unajua vijana wengi watakuwa wanahitaji kuwa na Soraya kutokana na sababu nyingine na sio upendo wa kweli, wengi watakuwa na tamaa ya kuwa ni mtoto wa tajiri” alisema mzee Mahamud kwa sauti ya upole, wakati akipembua nguo zake tayari kuingia bafuni, “lakini kumbuka kuwa Soraya pia ni mzuri na mrembo, hivyo sio ajabu kupendwa na mvulana yoyote” alisema mama Soraya, aliekuwa anaweka vizuri begi alilokuja nalo mume wake, “umeongea vyema mke wangu, hapo unaweza kuona ugumu alionao Soraya katika kujua yupi anampenda kweli na yupi anamtamani yeye au utajiri wake” alisema mzee Mahmudu kabla hajaonekana kukumbuka jambo, “hivi sijamuona Talib akija kunipokea, au amkumjulisha kama narudi” aliuliza mzee Mahamud ambae kiukweli alitokea kumuamini, sana Talib kuwa amebadilika kwa tabia, “mh! ukweli ni siku ya nne hatuja muona Talib, pengine amesafiri kwenda Nyasa” alisema mama Soraya.********
Ilikuwa hivi usiku ule ule, mara baada ya bwana Mahamud kupita kwenye lango la jumba lake, mlinzi akarudishia gate na kumpigia Talib, ambae hakupokea simu, akaamua kutuma ujumbe ili muda wowote akishika simu yake auone, “Boss amesharudi” hayo ndio yalikuwa makubaliano ya Talib na mlinzi huyo, ambae ndie alikuwa mshirika wake kwa hapa nyumbani, maana hata anapotoka au kurudi usiku sana, akiwa peke yake au na mwanamke yeyote, yeye ndie anae mfungulia lango, na pengine kumsaidia kuwatoa asubuhi sana wakati wa swala ya Alfajiri.
Ujumbe ule ulimfikia Talib saa moja za asubuhi, akiwa ndani ya chumba cha guest moja bubu ya uswahilini kweli kweli, ni mara baada kukurupuka toka kitandani akiwa amesha jikojolea, ni baada ya kushindwa kuamka akipitiwa na usingizi mzito, kutokana na pombe alizo kunywa jana usiku, na alipousoma ule ujumbe toka kwa mlinzi akainuka haraka na kuokota nguo zake zilizokuwa chini sakafuni, akaziokota na kuzipachika mwilini mwake na kujikagua mfukoni kwa kile alichobakia nacho, alikuwa na shilingi elfu tano tu! akairudisha mfukoni akachukuwa simu yake na funguo za gari akatoka mbio mbio kuelekea nje akimuacha Hilda bado amelala anakoroma kwa usingizi wa pombe, Talib alipitia sokoni akanunua dagaa nyasa wa elfu mbili na samaki wa elfu tatu, kisha akaelekea nyumbani, ambako aliwakuta wanafamilia wakiwa wameshaenda kwenye mihangaiko yao, akakabidhi wale dagaa na samaki, ikiwa ni alama ya kuwa ametokea Nyasa, kisha akamueleza mlinzi kuwa akija mwanamke yeyote kumuulizia amwambie kuwa hayupo, kisha kusema hivyo, Talib akaingia ndani kwake na kwenda kujilaza kwa lengo la kufidia usingizi wa siku nne akiwa na Hilda.
lakini ukweli ni kwamba Talib hakupata hata tone moja la usingizi, sio kwamba aliwaza kuhusu Hilda aliemuacha guest bubu, hakuwaza kuhusu mwanae na ahadi aliyoitoa ya kumfanyia shoping leo hii, hakuwaza kuhusu wakwe zake ambao jana usiku walipiga magoti mbele yake na alijua fika kuwa, mpaka sasa watakuwa wanasubiri chupa za pombe ili waendelee kulewa, ukweli Talib aliwaza juu ya kupata fedha ambayo itarudisha mtaji wa biashara yake, ambayo leo asubuhi ndiyo amemalizia elfu tano ya mwisho kwa kununua dagaa na samaki za kuwadanganyia mjomba na shangazi yake, “lazima mpango wangu ufanikiwe, siwezi kuishi kindezi, mjomba mwenyewe haeleweki, yeye anampa ulaji Soraya wakati mimi kidume nipo” aliwaza Talib, akisahau kuwa Soraya ndie mwenye haki zote za kuwa katika nafasi aliyopo, kwasababu ni mtoto wa Mahamud.******
Huku Luhuila seko nako, asubuhi hii tayari taarifa za Hilda kurudiana na Talib zilisha anza kuzagaa, huku bwana Komba ambae ni kama aliamka na pombe kichwani akitambaza taarifa hizo, ambazo baadhi ya watu walishindwa kuzielewa, maana walichojua wao ni kwamba, Hilda anaishi na Higgno kijana wa mzee Frank.
Mzee Komba alienda kwa mzee Nganyanyuka na kukopa lita ishirini za ulanzi kwa ahadi ya kulipa jioni akiamini kuwa mwanae Hilda atamletea shilingi elfu tatu ya kulipia pombe hiyo, ambayo aliipeleka pale kwake na kuwaita rafiki zake wakina Nyoni, Njogopa, Ngonyani, na wengine kibao, hasa wale waliokuwepo siku ile ya ndoa ya mkeka kwa mzee Frank, na kuanza kunywa pombe hiyo wakishushia supu ya mboga za majani ya maboga, wenyewe wanaita pitiku, na kuendelea kunywa ulanzi wakichangia konyagi, huku wakiamini kuwa kuna nyingine zinakuja baadae.*****
Mida hii mschana mrembo Soraya, alikuwa njiani na dereva wake wanatoka SeedFarm ya Lumecha, kilomita kama ishirini toka songea mjini, ambako alienda kuweka oda ya mbegu za miti ya matunda kwaajili ya kupanda shambani kwake sehemu ambayo alikuwa na malengo nayo makubwa sana, sio shamba pekee ila alikuwa na mpango wa kutengeneza hotel kubwa sana sehemu hiyo na kuanza kutangaza utalii wa kusini mwa tanzania hasa upande wa nyuma ya mji wa songea, ambako kulikuwa na vivutio vingi vya utalii, “da Laylah, unamkumbuka yule kijana alienisaidiaga siku ile nilivyo kamatwa na wanafunzi wa songea boys?” aliuliza Soraya wakati safari inaendelea, “na mkumbuka sana da Soraya inaonyesha unampenda sana yule kaka, yani bado unamkumbuka mpaka leo?” aliuliza Laylah huku anacheka cheka, “mh! sijui kama nampenda, lakini…. lakini… nataka tu nimuone nimuabie asante, kwasababu bila yeye ningesha poteza uschana wangu kwa aibu kubwa sana, tena sio kwangu tu! hata kwa wazazi wangu” alisema Soraya huku safari inaendelea, “halafu kwanini hatukuwahi kurudi kule matogoro kumtafuta tena?” aliuliza Laylah, akionyesha kujishangaa, “kweli bwana, hivi kwanini hatukuwahi kumtafuta kwenye ile barabara, hata hivyo mbona tumepita sana ile barabara lakini hatuja muona, kila ijumaa tunaenda shambani na tunapita kule kule?” aliuliza Soraya, “usikute alikuwa ni mwanachuo na alitokea mkoa mwingine” alisema Laylah, “mh! kwa umri wake yule kama alikuwa anasoma basi ni form one au two” alijibu Soraya, “kama ni hivyo basi sasa hivi atakuwa na mke na watoto kabisa” alisema Laylah, na kauli hiyo ilionekana kummaliza nguvu Soraya, ambae hakujibu kitu zaidi ya kukaa kimya mpaka walipoingia mjini.*******
Wakati mzee Komba akiwa ana fanya yake, hakujuwa kuwa mwanae Hilda ndio kwanza alikuwa anagongewa mlango na muhudumu wa Guest bubu hii, ambayo haitambuliki na msajili wa nyumba za wageni na kushtuliwa toka usingizini, akatazama pembeni yake pale alipolala Talib jana usiku hakuona mtu, na alipo tazama vizuri hakuoan dalili ya uwepo wa mtu huyu, kwa maana ya kwamba hakukuwa na nguo wala viatu vya Talib, zaidi ya mkojo alioumwaga kitandani, “we dada si ufungue mlango lisaa limepita toka saa nne” ilisikika sauti ya mhudumu wa kike toka nje ya mlango, “nilikuwa navaa dada yangu” alisema Hilda huku anafungua mlango ambao haukuwa umefungwa na funguo zaidi ya kuegeshwa na kitasa(kubugazwa), “yaani mwenzio ameondoka mapema tu, wewe unalala mpaka saa tano, unadhani usafi nitafanya saangapi, halafu akikukuta boss si atasema nimechukua hela yako ya leo” alisema yule mhudumu huku anaingia mule chumbani na kuanza kupembua mashuka, “nisamehe dada yangu nilipitiwa na usingiz..” kabla hajamaliza kuongea akakatishwa na yule mhudumu, “usinitanie wewe dada ndio maana ulikuwa umejifungia humu chumbani, kumbe umemwaga mkojo” alisema yule mhudumu, huku ameshika yale mashuka………haya sasa mambo yanazidi kuwa pambe, baba Higgno kawaka kwa dharau walizofanyiwa na hilda, mzee komba ndio huyooo na marafiki zake wana matumain makuuuuubwa huku hilda kakimbiwa gesti na talibu, soraya nae anamtaka kijana mpole amshukuru kwa kumuokoa miaka mingi iliyopita nini kitaendeleaaaa.... Usikose sehemu inayofuata.
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA KUMI NA NANE
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA KUMI NA SABA : “yaani mwenzio ameondoka mapema tu wewe una lala mpaka saa tano, unadhani usafi nitafanya saangapi, halafu akikukuta boss si atasema nimechukuwa hela yako ya leo” alisema yule mhudumu huku anaingia mule chumbani na kuanza kupembue mashuka, “nisamehe dada yangu, nilipitiwa na usingiz..” kabla hajamaliza kuongea akakatishwa na yule muhudumu, “usinitanie wewe dada ndio maana ulikuwa umejifungia humu chumbani, kumbe umemwaga mkojo” alisema yule muhudumu, huku ameshika yale mashuka……ENDELEA SASA
“mkojo?, labda Talib ndie alielala upande huo” alijitetea Hilda ambae mpaka hapo hakujuwa ni kwanini Talib aliondoka na kumuacha hapo guest, “usinitanie we dada nenda kafue uchafu sijui wa bwana wako, sasa unataka akufulie nani?” ndivyo ilivyo kuwa kwa Hilda, kabla hajaondoka hapo Guest alikabidhiwa mashuka na kuyafua kwanza, nae alifanya hivyo huku akiwaza kwanini Talib aliondoka kimya kimya, “labda alipigiwa simu anaitwa haraka, maana anaonyesha kuwa bado ananipenda, si unaona ameahidi kunipa hela za kumnunulia mtoto nguo, halafu aliwaambia wakina mama kuwa atawaletea pombe nyingine” alijipa moyo Hilda, ambae mwisho akapanga kuwa akimaliza kufua aende nyumbani kwa akina Talib akachukue fedha za matumizi kisha aende nyumbani, na kama Talib atapata nafasi atamfuata huko huko kwao.*****
Wakati huo pia mzee Frank, aliondoka nyumbani kwake yeye na mwanae Higgno na mke wake, wakiwa wame mbeba mtoto wa Hilda mpaka kwa mwenyekiti, ambae walimueleza kilichotokea jana usiku nyumbani kwao, nae mwenyekiti, akawaita wajumbe wawili wa nyumba kumi na kuelekea nyumbani kwa mzee Komba, ambako walifika pale saa tano za asubuhi na kukuta watu kibao wakiendelea na sherehe ya pombe, huku wakiongea na kucheka kwa furaha, wakionekana wameshaanza kulewa ulanzi, “hooo! mwenyekiti samahani bwana nilisahau kukualika” alisema mzee Komba huku anainuka na kuwasogelea wageni hawa, ambao hata alipowaona akushukuru kwa ujio wao, “usijali bwana Komba tume jialika wenyewe” alisema mwenyekiti, nao wakapewa viti, sehemu za kukalia ambazo zilikuwa ni matofari kutokana na uhaba wa viti, “hapana bwana Komba hatuwezi kunywa pombe mapema hii, labda tukueleze kilicho tuleta hapa kwako” alisema mwenyekiti baada ya kuona wana letewa vikombe vilivyo jazwa ulanzi, “lakini musituharibie sherehe yetu tafadhari” alisema mzee Njogopa kwa sauti ya kilevi, tena imekuwa vyema tume wakuta nyie ambao mulikuwepo usiku ule ambao tulimkuta Hilda kwa huyu kijana na kumkabidhi kuwa mke wake” alisema mwenye kiti akimuonyesha Higno, “mwenyekiti unazunguka sana, nenda kwenye point” alisisitiza Ngonyani.
Hapo mwenyekiti akaanza kueleza kilicho waleta pale nyumbani kwa mzee Komba, “bwana Komba nadhani unakumbuka siku ile ambayo tulimfumania binti yako nyumbani kwa bwana Frank, akiwa na huyu kijana wa bwana Frank yaani Higgno?” aliuliza mwenyekiti huku akimtazama mzee Komba, “hakuna asiekumbuka mwenyekiti hata sisi tulikuwepo, si ndio tukawapiga gundi kwa mkeka?” alisema Njogopa, kwa sauti ya kilevi, “haswaaaa, najua mulikuwepo, lakini itapendeza kama akijibu bwana Komba” alisema mwenyekiti kwa msisitizo, “ndio nakumbuka bwana mwenyekiti” alijibu mzee Komba yaani baba yake Hilda kwa sauti ya kilevi, “sawa sawa bwana Komba, sasa kuhusiana na hilo, kuna jambo limetokea jana usiku” alisema mwenyekiti, “nilijua tu, yaan tayari imesha kuwa nongwa” alisema mama Hilda kwa sauti ya chini chini, huku anatazama pembeni na kubetua midomo ya kubeza.
Mwenyekiti akamtaka mzee Frank, aeleze kilicho tokea mwanzo mpaka mwisho, na nia ya kuja pale kwa mzee Komba.*******
Naam baada ya kumaliza kufua mashuka ya mikojo, akaruhusiwa kutoka, nae akatoka zake akiwa amevalia nguo zile zile alizotoka nazo nyumbani kwa Higgno siku tano zilizopita, huku njaa ikiwa ina mchamanda kweli kweli, moja kwa moja akaelekea upande wa mjini, alitumia nusu saa kufika kwenye lango la nyumba ya mzee Mahamud akagonga na kufunguliwa mlango mdogo, “habari yako binti, nikusaidie nini?” aliuliza mlinzi huku anamtazama kwa umakini sana Hilda, “nashida na Talib” alisema Hilda kwa sauti ya tahadhari, “mh! we binti bado tu unamganda Talib, wewe si ndie yule uliekuja na wale wazee ulikuwa na mimba?” aliuliza mlinzi kwa sauti ya kutia shaka, “ndio lakini siku hizi ni mpenzi wangu” alisema Hilda kwa sauti fulani hivi ya kujiamini, “yeye anajua kama unakuja sasa hivi, maana mademu wake huwa hawaji mchana, na ameniambia kuwa akija mtu kumuulizia nimwambie hayupo” alisema mlinzi ambae alionekana kumtazama hilda kama mschana alie danganyika kabisa, “we mwambie tu Hilda anakuhitaji hapo nje” alisema Hilda kwa sauti ile ile ya kujiamini, ambae muda huo ukimsogelea ungeweza kuisikia harufu kali ya pombe, na ukizubaa unaweza kulewa kwa harufu hiyo iliyo changanyika na kutokupiga mswaki, “sawa lakini utakubaliana na majibu yatakayo toka, maana mi navyomjuwa Talib huwa hapendi kufuatwa na wanawake hapa nyumbani” alisema yule mlinzi huku anaingia ndani na kufunga lile geti dogo.
Hilda alisimama pale getini kwa dakika tano nzima, njaa ikizidi kumuuma, akimsubiri Talib ambae aliamini kuwa angetoka, mara hilda akasikia gate likianza kufunguliwa, akatabasamu kwa furaha, gate likafunguliwa na akatokea Talib akiwa amekunja uso kwa hasira na chuki, “we! mpumbavu umefuata nini hapa, au unataka kuni haribia kwa mjomba?” aliuliza Talib kwa sauti ya chini, lakini yenye ukali na hasira, “lakini Talib, si ulisema utanipa hela ya kumnunulia nguo mtoto” alisema Hilda kwa sauti ya mshangao, “hivi wewe unaniona mimi fala, yaani mtoto wa mtu mwingine halafu mimi nikamnunulie nguo?” aliuliza Talib, na kumshangaza Hilda ambae alimtazama Talib kama vile ndio anamuona leo kwa mara ya kwanza, “Talib jamani si ulimuona alivyofanana na wewe, usifanye hivyo Talib, mtoto ni wa kwako” alisema Hilda kwa sauti ya kuhuzunisha iliyokaribia kuangua kilio, “anafanana na nani, unadhani angekuwa wangu Higgno angekubali kuishi na wewe na mtoto, yaani wewe unakaa huku siku nne, yeye akae na mtoto ambae sio wa kwake, inawezekana vipi, kama unampenda huyo mwanao si ungeacha kunywa pombe halafu hela ungenunua nguo, hebu ondoka tena usiridi hapa” aliongea kwa harisa na sauti iliyojaa ghadhabu, kama uliwaona jana hakika leo ungeshangaa ni kwanini leo hii Talib yupo hivi.
Ukweli ni kwamba Talib sio tu hakuwa na mapenzi na Hilda, zaidi ya kumchezea na kukata kiu yake, pia alimchukia na kumuona kuwa ndie aliemsababishia akamaliza fedha za biashara yake ya samaki, “basi sawa naomba hata mia mbili ya nauuli” alisema Hilda ambae kiukweli hakuwa na hata shilingi moja, maana hata fedha aliyokuja nayo mjini siku ile alishaitumia siku nyingi, “acha useng.. wewe hela itoke wapi, hebu jikatae haraka usije kunijazia nzi hapa” alisema talib na kufunga gate, akibakia ndani huku Hilda akiwa nje, “jamani Talib, nimekukosea nini lakini? umeshaniharibia kwa Higgno na leo unanifanyia hivi” alilalamika Hilda kwa sauti ambayo ilishindwa kuficha kilio chake.******
“kwahiyo unataka kusemaje, unataka Hilda arudi kwa Higgno au?” aliuliza mzee Komba kwa sauti ya dharau na kebehi na kuwafanya wenzake wakina Nyoni wacheke kwa dharau, ilikuwa ni mara baada ya mzee Frank, kumaliza kuelezea jinsi ilivyokuwa toka siku Hilda alipotoweka, mpaka jana usiku alipoletwa na gari, akiwa pamoja na Talib wakija kumtazama mtoto wao, kisha kuondoka pamoja wakiacha maneno ya kashfa, “unadhani hata Hilda mwenyewe atakubali ujinga kama huo” alijibu bwana Ngonyani, huku wakiendelea kucheka, “bwana Komba, nikiwa kama mwenyekiti ambae nilifungisha ile ndoa ya mkeka ya Higgno na Hilda, leo hii naitengua rasmi” alisema mwenyekiti na hapo kikafuata kicheko cha kejeri, toka kwa mzee Komba na rafiki zake, “yaani mwenyekiti kama ungechelewa nilipanga nije kwako kukueleza swala hilo hilo, unajua huyu kijana sio wa hadhi ya mwanangu, ni kama alikuwa anamfuja tu! subiri sasa uone atakavyo nawiri, na kwa taarifa fupi ni kwamba yule kijana amesema tuandae makoo yetu, kila siku itakuwa ni pombe za kizungu tu!” alisema mzee komba kwa sauti ambayo kama ungeisikia kwa jinsi ilivyojawa na dharau, pengine ungerusha ngumi, kwa hasira, Naaam huyo ndio mzee komba hajui lolote linaloendelea kuhusu Hilda, nini kitajiriiiii? ITAENDELEA.