TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA
MTUNZI
Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA ISHIRINI: Baada ya kughala ghala kwa dakika kadhaa huku anapiga kelele za mayowe, mama Hilda akatulia ghafla, na kusimama, akawatazama watu waliokuwepo mwanzo wamejaa eneo wakinywa pombe, sasa aliwaona wachache wanaume wawili na wanawake watatu, ambao pia walikuwa wanamalizia ulanzi uliobakia, wengine walishaondoka, hata mzee Njogopa na Nyoni na Ngonyani pia walisha ondoka, “nime lsema hawaniwezi, wanadhania sijajuwa walicho kifanya, dawa ya mchawi ni kumfanyia uchawi, lazima watakuwa wameenda kwa mganga ili kumuharibia mwanangu” alisema mama Hilda yaani mke wa mzee Komba kwa sauti ya hasira, iliyo maanisha kuwa anaamini alicho kisema……. ENDELEA NAYO
Sidhani kama kuna mtu alimsikiliza zaidi ya mwanae Hilda aliekuwa bado analia chini chini, “kweli mama, yaani yule mwana mama anaonekana ni mchawi kabisa, hata jana tulipoenda kule kwao, alikuwa ananitazama kwa jicho baya sana” alisema Hilda, kwa sauti iliyo ambatana na kiashilio cha kunyamaza kilio, hakuna mwingine aliewaunga mkono katika maongezi yao, zaidi ya kuendelea kunywa pombe ya mkopo ambayo kiukweli mpaka sasa mzee Komba uko chumbani kwake, alikuwa amekaa kwenye kingo ya kitanda chake ameinamisha kichwa, mikono shavuni, anajiuliza ata lipaje madumu kumi ya ulanzi, hakika hata ile aliyokunywa toka asubuhi alihisi inayeyula na kumletea kizungu zungu.
Mzee Komba, zaidi ya kuwaza deni la pombe, pia aliwaza mambo mengi sana, aliwaza jinsi alivyo waletea kashfa wakina Frank na mwenyekiti, aliwaza jinsi alivyojitangazia ufalme, na kueneza kashfa kwa familia ya mzee Frank, “yule kijana mshenzi sana, yaani amenitia aibu kiasi hiki” aliwaza kwa machungu mzee Komba. ******
Yap, maisha yakaendelea week ilikatika Higgno akiwa kule porini kwenye makazi mapya, makazi ambayo mzee Frank aliyaona kuwa yalikuwa yana faida kwake na kwa maendeleo ya familia nzima, maana Higgno alijituma na kufanya ubunifu mkubwa kule shambani, akiongeza kilimo cha mboga mboga na kupanda miti mingine ya matunda, huku kila jioni kijana huyu akifanya zoezi ya karate kwa juhudi kubwa.
kingine bwana Frank, aliona jinsi bwana Komba ambae amekuwa adui yake, jinsi alivyoishi kwa kujificha ficha kukwepa aibu, huku akitoa kipande cha shamba lake kulipia ulanzi alioukopa kwaajili ya kusherehekea mwanae kupatana na kijana mtoto wa tajiri, taarifa zilizoanza kusambaa ni kwamba mschana Hilda, yaani binti wa mzee Komba, sasa amepewa jina la
TEMBELE LA UWANI kwa maana alikuwa chumba cha nadharia, kwav maana ya kwamba, mwanaume yoyote ambae angehitaji kujifundisha jambo lolote kwenye ngono, angeenda kujifunzia kwa Hilda, ambae hakuchagua mwanaume wala umri wa mwanaume ambae anaenda kumpa kitumbua, ilimradi angenunuliwa pombe au kupewa kete ya bangi, kilevi ambacho hata wazazi wake walikuwa wanajuwa kuwa binti yao alikuwa anakitumia, na kuzidi kuleta minong’ono kwa wananchi na wakazi wa Luhuila, ambao mwanzo walimuona Higgno ni mjinga na ndie anaefanya fitina ya kumkosanisha Hilda na Talib, na sasa walijuwa tabia halisi za binti huyu, ambae kwa jina la utani aliitwa
TEMBELE LA UWANI,
Tembele la uwani ndiyo mboga ambayo hutumika kwa haraka na kuokoa wakati wa njaa na dhiki, bila kujari maji yanayotumika kumwagia na kustawisha mboga hiyo, ambayo mara nyingi, hukatizwa na kijifereji cha bafuni, mboga ambayo muda wowote unaweza kuichuma na kuitumia kwa uharaka pasipo usumbufu wakuitafuta au kuifuata mbali, japo haipewi heshima inayostaili.
Sifa hizo mpya za hilda, zilishamfikia hata Higgno aliekuwa shambani, ameshaanza kuzoea maisha ya huko shambani, japo siku moja ya juma tano week ya pili, baba yake alimtembelea Higgno kule shambani, “mwanangu kuna jambo nahitaji tuliongee” aliongea baba Higgy wakiwa wamekaa nje ya kibanda cha Higgno pale shambani, hapo kengele ya tahadhari ikagonga kichwani mwake, maana baba yake alionekana anajambo muhimu kweli kweli, “Higgno umekuwa kijana mkubwa sana, sawa sihitaji uoe kwasababu bado hujapata kazi ya kukusaidia, pengine una ndoto ya aina ya maisha unayohitaji kuishi, lakini inakuwaje sija kuona hata siku moja ukiwa hata na rafiki wakike ambae mnacheza cheza kidogo zaidi ya huyu mshenzi ambae sasa hivi wanamwita nani sijui, nae ulikataa kuwa haujawahi kushiriki nae tendo” aliongea bwana Frank, akishindwa kueleza moja kwa moja, na kumfanya higgno acheke kidogo, “baba unahaja ya kujiuliza sana, mimi nipo vizuri tu, lakini ukweli nimejikuta nikiwa busy na mzoezi, na mambo yangu, isitoshe baba toka Hilda aliponigeuka mara ya kwanza tukiwa form one, ukweli sijawahi kufikiria kama kuna mwanamke ambae atakuwa mkweli” alisema Higgno kwa sauti ya kujiamini, “kama swala ni hilo Higgno, basi niachie nikutafutie mschana ambae atakuwa rafiki yako na pengine baadae muoane, maana hivyo ndivyo walivyofanya wazee wetu hapo zamani” alishauri baba Higgno, yaani bwana Frank wakati wanamaongezi yao, “mh! sasa baba kama nisipo mpenda itakuwaje?” aliuliza Higgno, “kama hautompenda sawa tunatafuta mwingine, naimani atakuwa mzuri au kama kuna unaempenda sema tukaongee na wazazi wake, na pengine yeye mwenyewe” alisema mzee Frank, ambae licha ya kuongea vizuri na mwanae siku zote, lakini hakuwahi kuongea nae juu ya swala hili la mausiano.
Mwisho wa maongezi walikubaliana kuwa Higgno atafutiwe mwanamke ili awe rafiki yake kwa maana ya uchumba, na mwisho wa siku aje kuwa mke wake.*****
Siku ya moja, mida ya saa nne za asubuhi, mzee Mahmud, alikuwa ndani ya ofisi ya pale nyumbani kwake, yeye na mwanae Soraya, wakijiribu kupitia majina ya watu walioomba nafasi za kazi, ambazo, walizitangaza, kutokana na kuongeza magari mapya, ambayo ni mabasi makubwa ambayo walipanga kuyapa safari za mikoa ya mbali, kama vile dar es salaam , Dodoma, arusha na sehemu nyingine nchini, “naona atuta hangaika sana kupata madereva na mafundi wenye uzoefu, mfano huyu, aliwahi kufanya kazi kwa…” alisema baba Soraya, akitaja jina la kampuni mmoja ya zamani ya usafirishaji, “ni kweli hata mafundi naona wengi wametokea kwenye ule mradi wa barabara wa mtwara kolido” alisema Soraya, “ila kuna kama huyu hapa, yeye amemaliza chuo cha ufundi pale jimboni, wale jamaa wanafundisha vizuri sana, halafu wana nidhamu sana wanafunzi wa pale” alisema baba Soraya, huku wakizitenga barua kwa makundi, “hao wanafunzi usiwape kipaumbele sana wengine huwa wanategeaga kwenye masomo yao, bora hawa wenye uzoefu kwanza” alisema Soraya, huku akiichukuwa ile barua toka kwa baba yake na kuiweka pembeni, huku macho yake yakipita juu ya ile barua na kuona jina la Higgno Frank, “ila ni kweli, unajua wapo wanaochukuwa hata vyeti vya wenzao kwaajili ya kuombea kazi, hao tutawafanyia interview ya vitendo, endapo hawa hawatatoshea” alisisitiza baba Soraya yaani tajiri mwarabu, Mahmud.
Naam wakati wanaendelea kuchambua barua na majina, ni kama kuna kitu Mahmud alikumbuka, “hivi Talib yupo wapi?” aliuliza bwana Mahamud, “mh! sijuwi labda chumbani kwake, alijibu Soraya, hapo kikapita kimya kifupi, huku wanaendelea kusoma maelezo ya waombaji wa kazi, kabla Mahamud hajaongea tena, “nafirikiria kumpatia nafasi ya usimamizi wa mabasi ya zamani, yale ambayo tutayaondoa kwenye safari za mbali, tuyapeleke safari za karibu kama mbinga, njombe masasi, newala na tunduru” alisema bwana Mahamud, “ni vizuri ukimpa nafasi hiyo, lakini ulishawahi kumchunguza kama anafaa kusimamia hayo magari?” aliuliza Soraya, akiwa anafahamu baadhi ya maovu ya binamu yake, hapo baba yake alitulia kidogo, kama anawaza jambo, kabla hajamtazam mwanae, “kwanini unauliza hivyo Soraya, inamaana bado unamashaka na binamu yako?” aliuliza baba yake, yaani mzee Mahamud kwa sauti ya mashaka, “kwani baba wewe unaweza kumjaji mtu kwa kumtazama tu! mi naona kabla hujampa hiyo kazi, jaribu kwanza kumchunguza” alisema Soraya, na wakati huo mlango wa chumba cha ofisi iliyopo hapo nyumbani kwao ukagongwa na alieenda kufungua mlango alikuwa ni Soraya, “asalam aleykum” alisalimia Soraya kwa sauti iliyojaa heshima na adabu, na kumfanya baba yake atazame mlangoni, kuona mtu aliesalimiwa, akawaona watu wawili na sio mmoja wakiingia mule ofisini, “aleykum salaam” alikuwa ni mzee wa makamo mwenye asili ya kiafrika halisi, maana hakuchanganya rangi hata kidogo, alieongozana na kijana mwenye kati ya umri wa miaka ishirini na saba, mpaka ishirini na tisa, wote wawili wakiwa wamevalia kanzu yeupe na baragashia zao vichwani mwao, “asalam aleykum” alisalimia tena Soraya kwa yule kijana ambae walikutanisha macho yao, na yule kijana akaitikia huku anaachia tabasamu pana, “aleykum salam”, Soraya akashindwa kumtazama kijana huyu usoni, na kujikuta akitazama chini, huku kikimponyoka kitabasamu cha aibu.
Naam wale wageni walipita ndani, “karibu bwana Mahadhi bin Salum, toka nirudi dar salaam atujaonana” alisema bwana Mahamud, akionyesha kuwa, alikuwa anamfahamu vyema huyu mzee mwenzie, ambae hata kwa umri ni kama walikuwa wanalingana na bwana Mahamud, “asante bwana Mahamud, tulipishana kidogo, nilisafiri kwenda mtwara kupokea mizigo toka South afrika, huyu kijana wangu alituma kwenye meli” alisema yule mzee Mahadhi Salum, huku akimuonyeshea yule kijana aliekuja nae, ambao sasa walikuwa wanakaa kwenye viti vya mule ndani ya ofisi ya nyumbani, Soraya akimtazama kijana huyu mtanashati akijaribu kumtathimini kama angefaa kuwa mume wake, hakujiuliza kama atakuwa ameshaoa au laa, “kwani huyu ni nani?” aliuliza Mahamud, huku akimtazama yule kijana, ambae kwa muonekano alikuwa ni kijana mtanashati, mwenye harufu ya maisha mazuri, ung’aavu wa ngozi yake na muonekano wa sura yake, viliashiria kuwa, alikuwa ni kijana mwenye mafanikio, kama sio kutoka kwenye familia yenye mafanikio, “huyu ni Idd, yule kijana wangu wa pili” alisema mzee Mahadhi, kwa sauti ya kujipata na kujigamba, “hooo Idd, aliadimika sana miaka ya hivi karibu” alisema mzee Mahamud, akionyesha anamkumbuka kijana huyu, ambae binti yake, licha ya kumuona kuwa ni kijana mwenye sifa za wazi, ambazo yeye anazihitaji, lakini pia alihitaji kujuwa sifa za kijana huyu za ndani, “alikuwa south afrika, amerudi siku tatu zilizopita, hivyo akaniambia twende kwa mzee Mahamud, nikamsalimie” alisema mzee Mahadhi Salum, kwa sauti ya kujinasib, huku Idd mwenyewe mara kwa mara akitabasamu, na kujichekelesha, huku akimtazama Soraya kwa macho ya kuibia, hata yalipo kutana macho yao, walitabasamiana na Soraya kutazama chini kwa aibu.
Sio kwamba wawili hawa hawafahamiani, wana fahamiana toka miaka mingi nyuma, walikuwa wanakutana mara kwa mara msikitini hasa siku za ijumaa kipindi kile wanasoma, walikuwa wana salimiana vizuri na kuoemeshana mawili matatu, hata akitokea Soraya akawa amevaa ile nikab ya kujiziba mdomo na pua, basi yeye mwenyewe ange muita na kumsalimia Idd, lakini walikosana mara baada ya Idd, kujaribu bahati yake kwa kuomba penzi la Soraya ambae hakumjadili hata mara moja, alimkatalia bila kumzungusha, na huo ndio ulikuwa mwisho wa ukaribu wao, japo wazazi wao walikuwa wanafahamiana vizuri, na marafiki, hawakuweza kuona wala kuwa karibu mpaka leo wakina Idd na baba yake walivyo kuja ofisini kwa akina Soraya, ikiwa imepita miaka zaidi ya mitano.
Mzee Mahadhi, licha ya kuwa mmoja kati ya wazee wa baraza la dini hapa mkoani Ruvuma, lakini pia, mzee huyu mwenye asili ya visiwani Zanzibar unguja mjini magharibi, kitongoji cha Mombasa, alikuwa anajihusisha na biashara ya nguo, kama vile kanzu mabaibui, baraghashia, magauni mazuri ya heshima, na nguo nyinginezo, za kawaida kwa wanaume na wanawake, “ok! karibu bwana Idd, naona umekuwa kijana sasa, vipi umeshaoa huko south afrika?” aliuliza mzee Mahamud kwa namna ya utani, Idd na baba yake wakatazamana na kucheka, huku Soraya, akimkata jicho baba yake akiamini kitachofuata ni kuzungumzia mambo ya kuoa na kuolewa tu! “aowe wapi, amesema anakuja kuolea nyumbani” aliwahi kujibu Mahadhi mwenyewe, ni jambo la kheri kuoa nyumbani, japo haijakatazwa kuolea mbali” alisema Mahamud.
Naam yalipita maongezi mawili matatu, kabla ya mzee Mahadhi salum hajaomba faragha kidogo na mzee Mahamud, “haina shida twende sebuleni, basi, tuwaache hawa huku ofisini” alisema Mahamud, nao wakatoka mule ofisini na kuwaacha Soraya na Idd mule ofisini, “niambie Soraya, unanikumbuka lakini?” aliuliza Idd mara tu baada ya wazazi wao kutoka mule ofisini, huku akimtazama Soraya usoni, na kama ujuavyo msomaji, Soraya licha ya kuwa mrembo pia ni mzuri wa sura na mwili, maana kila alivyozidi kukuwa ndivyo alivyo zidi kuwa na umbo matata, “nakukumbuka sana” alijibu Soraya huku ana jitahidi kukwepesha macho yake yasitazamane na macho ya Idd, “unanikumbuka kwa lipi Soraya?” aliuliza tena Idd kwa sauti nzito na tulivu, tofauti na mwanzo, “nikukumbuke kwa lipi kaka Idd?” aliuliza Soraya, huku ana jaribu kumtazama Idd usoni, akamuona anajilamba midomo huku amelegeza macho, “kwa lile ulilo nifanyia, najua ulikuwa ni utoto tu, lakini sasa umeshakuwa mkubwa” alisema Idd, kwa sauti ile ile nzito ya makusudi huku anaendelea kujiramba midomo yake, na macho yake kulegeza akiwa ameyaelekeza kwa Soraya ambae aliyakwepesha ya kwake, “we unakumbuka mambo ya zamani, kwani wewe ulikuwa mkubwa?” aliuliza Soraya huku akiwa anaanza kupekuwa pekuwa barua zilizopo mezani, “yah! kwani unaona nilikuwa mdogo?” aliuliza Idd, kwa sauti ile nzito iliyojaa majivuno, “hongera yako” alisema Soraya, huku akizidi kutawaliwa na aibu, maana alishindwa kukabiliana na mtu ambae anaonyesha wazi matamanio juu yake, “hongera ya nini Soraya, mbona vitu vya kwawaida tu!” alisema Idd kwa sauti ya kurahisisha, “wewe ndio unaona kawaida, lakini mwenzio… mh!” alisema Soraya huku anaichukuwa barua ya Higgno na sijuwi kwa kuchangachikiwa na maongezi akajikuta anaiweka kwenye kundi la barua za kundi la kwanza zilizopewa kipaumbele.
Naam wakati huo huo huku sebuleni kulikuwa na maongezi ambayo Soraya kama ange yasikia hakika, sijuwi kama angekubaliana nayo, “ndiyo hivyo bwana Mahamud, kijana wangu akasema hapana hawezi kuoa mwanamke yoyote sehemu yoyote, wakati kuna mschana mwenye kujiheshimu, alielelewa akaleleka na mschana mwenyewe ni mwanao Soraya, na ukiangalia watoto umri ndio unaenda hivyo” alisema bwana Mahadhi, kwa sauti ya chini iliyojaa msisitizo, muda huu mama Soraya alikuwa ameenda mjini, kuangalia vitu vya jikoni na wafanyakazi wake wawili, “hilo jambo kwa kweli hata mimi lina niumiza kichwa bwana Mahadhi, natamani sana binti yangu aolewe na mimi nipate mjukuu, lakini tatizo huyu Soraya, amekuwa mchaguzi sana wa wanaume, mapaka sasa anasema bado hajamuona mwanaume ambae atafaa kuwa mume wake, wote ni kama wana tamaa” alisema Mahamud kwa suti ya chini pia, “unajua kwanini Mahamud, ni kwasababu hajapata nafasi ya kuchunguza mwanaume wa kumfaa, naimani tukiwaweka karibu, basi watazoeana na kuchunguzana, ujuwe ndoa za sasa hivi, uanza na urafiki” alisema Mahadhi, kwa sauti ile ile ya chini, “sasa tutawawekaje karibu?” aliuliza Mahamud, kwa sauti ile ya chini, ungesema kuna mtu hawataki asikie, “hilo ni jambo rahisi, hebu niachie mimi nikupe mbinu, lazima tujitahidi kuwa tuna waweka karibu mara kwa mara na njia rahisi ni kuwa tuna watuma kwa pamoja mara kwa mara, mpaka watajikuta wanaingia kwenye urafiki ambao utasababisha ndoa” alisema Mahadhi, na wakaanza kupanga jaribio la kwanza, kabla ya kuagana na kuondoka zao********
Upande wa pili, kijana Talib, hakuwa tena na mtaji wa biashara, sio mtaji tu, hakuwa hata na fedha yoyote, kiasi cha kushindwa kuweka mafuta kwenye gari alilokuwa anatumia, yaani Hyundai, na kumlazimu kutembea kwa miguu kwenye baadhi ya matembezi yake, au kutumia daladala, kwenye matembezi ya mbali kama vile mwembe chai kwa bwana Zido na Vitus, ambako alilazimika kwenda kwaajili ya kufuata bangi na kupanga mipango ya kumteka Soraya ili wajipatie fedha nyingi, japo yeye alikuwa anawashauri wenzake kuwa, itafaa endapo watamuuwa kabisa, na yeye Talib kujinyakulia nafasi ya binti huyu wa pekee katika familia ile na kuwa msimamizi wa biashara ya mzee Mahamud.
“tunaweza kufanya hivyo, lakini wacha kwanza tuchukuwe mkwanja wa haraka, kisha tumuuwe, maana itasaidia pia kutunza siri, anaweza kututambua halafu ikawa shida” alisema Zido, siku tatu kabla ya tukio, “na nikifanikiwa kukamata nafasi hiyo, kwanza kila mmoja atatupiwa gari moja la maana, halaf nawakabidhi vitengo kwenye kampuni” moja ya ahadi ambayo Talib aliitoa kwa wenzake.*****
Naam zilipita siku tatu, juma moss moja, Soraya akiwa chumbani kwake akijaribu kutazama filamu moja ya kihindi, ambayo kiukweli ni kama hakuwa anaifuatilia, maana ukweli ni kwamba, maongezi ya siku ile usiku akiwa na baba yake na mama yake wanakula, ni kama yali mtonesha mschana huyu, ambae kila alipokumbuka maneno ya baba yake kuwa, endapo angempata kijana yule aliemsaidia kumuokoa mikononi mwa wanyang’anyi, ambae yeye alimfananisha kitabia na yule kijana mpole, alitamani sana ile bahati ingemkuta kijana mpole aliemsaidia sibakwe, “sijuwi kwanini niliondoa gari haraka siku ile, pengine angekuwa rafiki yangu” aliwaza Soraya, ambae hata yeye hakujuwa ni kwanini anawaza sana juu ya kijana ambae ametokea kumpenda na kuamini kuwa anafaa kuwa mume wake, “sijuwi nawaza nini mimi mtu sijamuona miaka na miaka, halafu hata hanijuwi na mimi simjuwi” alijisemea Soraya ambae aliona kama anawaza jambo ambalo lisinge wezekana, hivyo akaamua kulipotezeana kuwaza kuhusu miche ya matunda, ambayo ilibidi kesho kutwa akaichukuwe kule Seed farm ya Lumecha, ili ijumaa waipeleke kule shambani ikapandwe, lakini licha ya kujitahidi kupotezea bado akajikuta anavuta taswira ya sura ya kijana mpole, ambae kila alipomkumbuka aliona kama amekosa kitu muhimu sana, utazani alishawahi kuwa mpenzi wake na wakapotezana ghafla, kumbe ni watu ambao hawakuwahi kuongea hata kufahamiana majina, “sijuwi nikimuona atakuwa na mke tayari?” alijiuliza Soraya ambae ni kama alikuwa anaamini kuwa ipo siku atamuona yule kijana mpole.
Wakati Soraya anaendelea kupambana na mawazo juu ya kijana mpole, mara akasikia mlango wa chumba chake unagongwa, “ingia” alisema Soraya huku akijiweka vizuri na mlango ukafunguliwa akaingia mama yake, “mwanangu, na wewe kwa kutazama filamu, hebu jiandae anakuja rafiki yako Idd, baba yako anataka awatume sehemu” alisema mama Soraya, kwa sauti ya furaha na ucheshi, huku anatabasamu, “Idd?” aliuliza Soraya ka mshangao, “unashangaa nini mwanangu, nenda katembee saa kumi na mbili uwahi nyumbani” alisema mama Soraya, kwa sauti ya kubebembeleza na kumfanya Soraya akubaliane na mama yake.... Haya sasa soraya anawekwa karibu na idd ambae sio chaguo lake, ila lengo la wazazi wawe karibu wazoeane kisha ndoa, nini kitajiriiiii? Atakutana na kijana mpoleeee au ndio anaenda kuolewa na idd? Vip kuhusu talibu na mipango yake? Vip mama hilda na safari yake ya kwenda kwa mganga? Basi usiache Kufuatilia mkasa huu hapa hapa
jamii forums.