TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA KUMI
MTUNZI
Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA TISA : ghafla akawaona vijana wawili wakiibuka mbele yake, ilikuwa ghafla kwasababu vijana hawa waliovalia kama wale aliowaona barabarani, yaani suruali za shule na mashati ya kiraia, walitokea kwenye kichaka na kuanza kumfuata huku wamemkazia macho, hapo Soraya akajua dawa ni kurudi alikotoka, ile anageuka akashangaa kuona wale vijana wawili aliowaona barabarani, nao walikuwa mita chache nyuma yake, “mungu wangu nini kina nitokea, ni ndoto au kweli” alijiuliza Soraya, ambae alianza kuhisi miguu yake inakosa nguvu, akitabiri kinachokuja kumtokea, ni wazi sio kitu kizuri kwake……...……… endelea……..
Lakini hakusubiri wale watu wamkute akiwa amesimama pele pale, akaona bora arudi alikotoka, pengine angepata msaada toka kwa Laylah, hivyo akaanza kurudi alikotoka huku mikono yake ameikumbatia kifuani ameshikilia kile kitabu chake cha dini, na wakati huo huo akasikia gari lake likiwashwa na ile alipowakaribia wale wavulana wawili ambao ni wazi kabisa kuwa ni wanafunzi wa songea Boys, waliokuwa wanatokea barabara kuu, akaamua awapishe kwa kupita kwenye nyasi kabisa, huku uso wake ukiwa umetawaliwa na uoga wa hali ya juu, lakini ni kama alikuwa amewarahisishia kazi wale vijana, hapo hapo mmoja wao akamsukuma kwa nguvu na Soraya akijikwaa kwenye nyasi na vile viatu vyake virefu, akajibwaga chinii puu, hapo Soraya akaachia kilio cha mwaka, lakini akakutana na kofi zito la usoni, “kimya wewe ukipiga kelele tutakuuwa hapa hapa” alisema mmoja huku wale wengine nao wakija na kuungana nao, hebu tulieni jamani, huyu demu mimi nilikuwa namtamani kinyama, nyie pigeni alafu mimi nitamalizia” alisema mmoja kati ya wale wanafunzi wawili walioongezeka, “jamani msinifanye hivyo nitawapa hela” alisema Soraya kwa sauti ya uoga na yakuomboleza, lakini hakuna hata mmoja alieonyesha kumsikiliza, ndio kwanza walianza kumshika viziri wawili wakimshika miguu mmoja akiamshika mikono, pale pale chini, halafu mmoja wao akashika gauni tayari kulipandisha juu, hapo Soraya akajua leo anatolewa uschana wake katika njia mbaya kuliko alivyotegemea tena kwa namna ya aibu kwa mtoto wa tajiri kama yeye,
Hapo Soraya akiwa ameshakata tamaa, alibakia ana toa mchozi wa kimya kimya na kufumba macho japo siweze kushuhudia kile kinachotaka kufanywa kwenye kitumbua chake, lakini kabla hata yule jamaa haja mfunua gauni lake, mara akasikia, “mwacheni huyo mwanamke” hapo Soraya akafumbua macho na kuwaona wale jamaa ambao walionyesha kushtuka na kumuachia Soraya, huku wakisimama na kumtazama aliewaambia wamuachie, hapo Soraya pia akainuka na kumtazama mtu huyo mwenye sauti ya upole, akamuona ni yule kijana aliewasalimia pale kwenye gari, ambae sio yeye tu alieona kuwa msaada unaweza kuwa mdogo sana kwa kumtegemea kijana huyu, kwasababu asilimia kubwa ya wale vijana wanne walimzidi kwa umri na maumbo yao makubwa, wakionyesha kuwa ni wanafuzi wa kati ya Kidato cha tatu mpaka cha sita, na huyu kama anasoma basi ni kidato cha kwanza au cha pili, maana hata kwa mtazamo walikuwa wanaendana kwa umri, hata wale vijana wanne walimdharau, “kum.. tutakukamua na wewe mwenyewe, hebu ondoka haraka” alisema mmoja wao kwa sauti ya kibabe, yenye mkwara mzito, hapo Soraya ambae alisha kata tama na utetezi uliokuja akaona kuwa mtetezi wake aliebakia ni mbio pekee, lakini viatu alivyovaa ndivyo vilivyo kuwa kikwazo kwake,
Lakini akatumia ujanja wa kuvua viatu kwa kutumia mguu, lakini hakumaliza hata kutoa kiatu kimoja, akadakwa mkono na mmoja wa wale vijana, Soraya hakuwa na ujanja, akabakia ana mtazama yule kijana mpole mwenye kujiamini, ambae ndiyo mtu pekee anaeweza kumsaidia, japo alishakata tamaa juu ya kijana huyu mdogo, “mugu wangu tenda miujiza” alijisemea Soraya, huku akijiona kuwa bado yupo kwenye hatari ya kubakwa na wanaume wanne, Soraya akamtazama yule kijana mpole kwa macho ya huruma, akamuona ametulia anawatazama wale vijana wa songea boys kwa zamu, “kama mnajua wazazi wenu waliwatuma kuja kusoma nasema muacheni huyo mschana haraka” alisema tena yule kijana mdogo, kwa sauti ile ile ya upole yenye kujiamini kiasi cha kuwafanya wale vijana wanne watazamane kwa mshangao, huku Soraya akianza kumuona yule kijana kuwa ni wakipekee kwa jinsi anavyojiamini, lakini wale vijana walimtazama kwa sekunde chache, waliachia kicheko cha nguvu kilichojaa dharau, “anasemaje huyu fala, anatujua sisi wakina nani?” aliuliza mmoja huku anawatazama wenzake.
Hapo Soraya, alijikuta anaomba japo kijana huyu, angekuwa na mwili mkubwa kidogo ange msaidia kuepukana na kibako hiki, na wakati huo huo ikasikika sauti ya Laylah, “we! Sorayaaaaaa” ilionyesha wazi kuwa tayari Laylah alijua kinacho taka kutokea kwa boss wake, maana hata gari tayari alishaliwasha, lakini soraya hakuweza kuitikia, maana alikumbuka kofi alilotandikwa usoni wakati ule, sasa Soraya akamuona kijana mmoja kati yao akimsogelea yule kijana mpole kwa hasira huku anasema,“mbona mnamkawiza huyu, mseng…” na kabla hajamalizia kauli yake, Soraya alimuona yule kijana mpole ghafla na kwa haraka akikifyetuwa kichwa chake kwanguvu kukivurumisha kwa mwanafunzi yule aliemsogelea, ambapo kilitua kati kati ya pua na macho, hakika hakikumuacha salama yule mwanafunzi, ambae alitoa mguno wa maumivu huku anajishika usoni kwa mikono yote miwili, muda huo huo tayari damu zilishatapakaa eneo lote la matundu ya pua mpaka kwenye mdomo na kidevu, hapo kijana mpole ni kama alichokoza nyuki, maana vijana wawili wengine walimvamia kijana huyu huku mmoja akibakia amemshikilia yeye Soraya, na yule mwingine akijishangaa damu zilizotapakaa usoni mwake, sasa Soraya akajua kuwa kijana mpole anapokea kipogo kizito.
Hapo Soraya akashuhudia kijana mpole akimkwepa mwanafunzi wa kwanza aliekuwa amerusha konde kwenda usoni, kijana mpole hakuangaika na huyu aliemkwepa, kwanza alirusha ngumi ya maana iliyotuwa usawa wa chembe ya moyo wa kijana wa pili na kumfanya ainame huku akijishika kwa maumivu makali huku akimuona yule mwingie na yeye akimvamia tena kijana mpole kwa kumrushia teke, hapo Soraya akamuona yule kijana anafanya kama vile anavyoona kwenye video, yani alikwepa kidogo na kuvulumisha ngumi nzito kwenye shavu la yule mwanafunzi wa pili, ambae alitema damu na kitu kama punje ya muhindi iliyochafuliwa na damu.
Mpaka hapo Soraya akapata matumaini ya kutoka salama mikononi mwa watu hawa waliokosa huruma, japo hawakuonekana kukubali matokeo,ni baada ya kuamua kumvamia tena wote watatu kwa pamoja, huku mwenzao akiwa bado amemshika Soraya, lakini kilichotokea ndicho ambacho kilimfanya Soraya amtazame vizuri kijana huyu usoni, maana aliwakwepa kwa ustadi na kuwashambulia kama mtu aliepata mafunzo ya kimapigano, na mashambulizi yake yalikuwa mazito.
Soraya ambae aliendelea kumsikia Laylah akiita kwa sauti ya juu, akamuona yule mmoja aliekuwa amemshika mkono akimuachia yeye mwenyewe, na kujaribu kwenda kuongeza nguvu ya kuwa saidia wenzake, hapo ndipo Soraya alipovua viatu na kuanza kukimbia kuelekea barabarani akiacha mapigano yanaendaelea, huku yule kijana akiwatandika wale wanafunzi kwa ngumi nzito za kikatili.
Pasipo kujua kilichotokea nyuma, Soraya aliingia kwenye gari na Laylah akaondoa gari kwa speed kurudi mjini, ambapo mita kama mia nne mbele, wakawaona polisi wengi wakiwa na magari mawili yaliyo simama na gari la baba yake soraya, yaani Nissan patrol, na hapo Soraya akamuambia Layla asimamishe gari.
Waliposimamisha gari tu! ndipo walipomuona mzee Mahamud akishuka toka kwenye gari lake na kuwafuata kwenye gari lao, “vipi mwanangu upo salama” aliuliza mzee Mahamud kwa sauti iliyojaa pupa na wasi wasi, ndipo Soraya alipo anza kumsimulia jinsi ilivyo kuwa.******
Wakati huo tayari
Higgy wizzy alishawatandika vibaya sana wale wanafunzi wanne, akiwa amesha mvunja mmoja mkono mwingine mguu na yule aliempasua pua na mwingine alimtoa jino, sasa walikuwa hoi na Higgno akaanza kusikia saauti ya wanafunzi wengine wanakuja upande huo hivyo akaondoka zake, akijua kuwa wakiongezeka zaidi kuna hatari ya yeye kushindwa kuwamudu kimapigano.
Higgno alipofika barabarani hakutaka tena kufuata barabara, hivyo alivuka barabara na kuingia kwenye mashamba ya mahindi akapotelea huko kuelekea bondeni, yaani mtoni ili avukie kwao Luhuila, na hakufika mbali akasikia miungurumo ya magari yakiongozana kuja kule alikotoka na kusimama pale kwenye usawa wa kituo cha dala dala.******
Ilikuwa hivi, mara baada ya kumsimulia baba yake, jinsi alivyovamiwa na vijana wale wahuni, na kuokolewa na kijana yule asiemfahamu, ambae alimuacha bado anaendelea kupambana na wale vijana wahuni, ndipo mzee Mahamuda alipo waeleza polisi kuwa waelekee huko wakamsaidie kijana huyo muokozi wa binti yake, hata Soraya ambae alitamani kumuambia asante kijana yule mpole akaingia kwenye gari lake na Laylah akaendesha kuwafuata polisi na baba Soraya, ambapo dakika mbili zilitosha wao kufika eneo husika na kusimamisha magari yao.
Polisi wakashuka Haraka na kelekea kwenye ile njia ambayo Soraya alisema alikuwa amepita na kukutana na wale wanafunzi wahuni, hapo polisi kumi waliofuata ile barabara waliwaona vijana kama kumi na saba wakianza kukimbia maporini, huku wakiwaacha wenzao wanne wakiwa wanashindwa kukimbia vizuri kutokana na kujeruhiwa vibaya na kijana mpole, hata walipo kamatwa Soraya aliwatambua kama ni wale vijana waliotaka kumbaka.
Licha ya yote, lakini Soraya alisikitika kuto kumuona yule kijana mpole, na katika hali ambayo hata yeye mwenyewe hakuielewa alijikuta ana tamani kukutana na kijana yule, ambae sio jina tu! hata sehemu anayoweza kumpata hakuijua, hivyo akabaki akishindwa kuondoa kumbu kumbu ya kijana yule kwa muda mrefu sana, “Layalah, hivi wewe una mwanaume wako?” kuna siku Soraya akiwa kidato cha tatu, anatoka shule na Dereva wake, alimuuliza swali hilo, ambae alianza kwa kucheka kidogo, “ndio ninae lakini sijafunga nae ndoa” alijibu Laylah huku anacheka cheka, “na huwa unazini nae” aliuliza tena Soraya na kumfanya Laylah acheke kicheko cha aibu, “ndiyo huwa tunafanya mara moja moja” alijibu Laylah, akiendelea kuachia kucheko chake, “kwani ukiwa na mwanaume lazima mfanye?” aliuliza Soraya, hapo Laylah akashusha pumzi nzito, “mh! inategemea na mtu mwenyewe, kwani… kuna mwanaume unafikilia kumkubali?” aliuliza Laylah, kwa sauti ya mashaka, maana hakujua kama lile swali lita kuwa zuri kwa Soraya, itaendelea……..
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA KUMI NA MOJA
MTUNZI
Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA KUMI : “na huwa unazini nae” aliuliza tena Soraya na kumfanya Laylah acheke kicheko cha aibu, “ndiyo huwa tuna fanya mara moja moja” alijibu Laylah, akiendelea kuachia kucheko chake, “kwani ukiwa na mwanaume lazima mfanye?” aliuliza Soraya, hapo Laylah akashusha pumzi nzito, “mh! inategemea na mtu mwenyewe, kwani… kuna mwanaume unafikiria kumkubali?” aliuliza Laylah, kwa sauti ya mashaka, maana hakujua kama lile swali lita kuwa zuri kwa Soraya, endelea……..
Ambae alitulia kwa sekunde kadhaa kama vile anatafuta jibu la kumpa dereva wake, yaani Laylah “mh! mi sijui” hilo ndilo lililokuwa jibu la Soraya, ambae mpaka anafika kidato cha tatu na miaka yake kumi na saba, hakuwa ameruhusu mwanaume aguse kitumbua chake, japo alishangaa kuona anatamani kumuona kijana mpole na kuwa nae karibu, “mh! akitaka tufanye nitamwambiaje” aliwaza Soraya.
Naam mschana huyu ambae ilisemekana kwa kipindi hicho alikuwa ndie mschana mrembo, zaidi aliepata kutokea mkoani Ruvuma kabla ya wakian Eveline (mwalimu nae anataka) au Malaika (bibi harusi mtarajiwa), aliendelea kusoma kwa juhudi huku taratibu siku zilivyo enda ndivyo alianza kusahau juu ya kijana mpole, aliemsaidia asibakwe, japo alianza kupata hisia za kuwa na mwanaume, lakini alijizuia kufanya hivyo kwasababu aliona kuwa, aina ya mwaume aliemuhitaji, pia alisaidiwa na maadili ya dini na heshima ya wazazi wake.
Soraya aliendelea kusoma kwa juhudi, huku burudani yake kubwa ikiwa ni filamu za kihindi za kizungu na zile za vichekesho za Kiswahili za wakina marehemu king Majuto, mzee small na wengine, (walazwe mahali pema pepon).*******
Higgno ambae licha ya kumsaidia mschana yule chotara kwa lengo la kumuokoa asifanyiwe udhalilishaji na wale wanafunzi watukutu, lakini kiukweli alishangazwa sana na uzuri wa mschana yule, huku akiombea japo amuote kwenye ndoto japo hata usku mmoja tu na roho yake itulie, lakini huwezi amini, hakuweza kuota hata ndoto inayofanana.
Ukweli Higgno hakuwahi kuwaza kuwa anaweza hata kupata nafasi ya kumsogelea mschana yule chotara ambae ukiachilia uzuri wake, pia hata hali ya kimaisha aliyonayo mschana yule, ambae hakumfahamu anatokea wapi na anasoma wapi, yeye Higgno alijiona kuwa asingefaa hata kuwa house boy wake, Higgno alitamani angezaliwa akiwa tajiri, maana hata Hilda asingemkimbia na kwenda kwa Talib, ambae sio kwamba ni mtoto wa tajiri ila ni ndugu wa tajiri, lakini kadiri siku zilivyo songa ndivyo Higgno alivyozidi kumsahau mschana yule chotara, ambae aliamini kuwa hatokaa akutana nae tena katika maisha yake, zaidi aliendelea kujituma katika mazoezi na masomo na kumsaidia baba yake kazi mbali mbali, akiamini kuwa juhudi zake ndizo zitakazo muokoa katika maisha yake na kuondokana na kudharauliwa.*******
Upande wa pili Hilda aliendelea kulea mwanae kwa shida, huku anajutia kitendo cha kujiingiza kwenye mapenzi na Talib, akimuacha Higgno, ambae alionyesha kumpenda na kumjali toka wakiwa wadogo, hawajui hata maana ya kupeana dudu, “Joan mshenzi sana, kweli nimeamini kuna watu wamezaliwa kuwaharibia wenzao maisha” alijisemea Hilda, ambae hakuweza kuvumulia kukutana na Higgno uso kwa uso, na kila alipomuona kwa mbali alimkwepa kwa kumkimbia, ni kutokana na aibu aliyokuwa nayo.
Mwanzo Hilda alikuwa mtu wa kujificha ficha kwa aibu, lakini siku zilivyozidi kwenda akaanza kuzoea na kujionea kawaida tu, hivyo akaanza kujiachi mitaani na kufanya kazi za nyumbani na shambani kama kawaida, huku akiendelea kulea mwanae, lakini yote kwa yote bado hakuweza hakuwai kukutana na Higgno uso kwa uso, ukiachilia kumkwepa mara chache anapomuona, pia ni kutokana na Higgno kutokushinda nyumbani, maana muda mwingi aliutumia shuleni na mazoezini.******
Naam Higgno alifanikiwa kumaliza kidato cha nne mwaka 2000, bahati haikuwa kwake, aliambulia division four ya point 28, ambayo inge muwezesha kujiunga na chuo cha ualimu, lakini katika za kitoto Higgno hakupenda kuwa mwalimu, hivyo akajiunga na chuo cha ufundi, akijiweka kwenye ufundi wa magari kwenye chuo kidogo cha ufundi kinacho milikiwa na kanisa catoriki, akiamini kuwa elimu hiyo inaweza kumsaidia kupata kazi itakayo muingizia kipato, lakini hakuwahi kuacha mazoezi ya karate, ni kama ulishakuwa ulevi wake.
Wakati huo huo mschana mrembo mwenye urembo wake akipata division one na kuendelea na kidato cha tano hapo hapo songea Girls, ni kutokana na wazazi wake kuomba asome shule hiyo ambayo ingemuweka karibu yao, hawakutaka wakae mbali na binti yao.
Kwa upande wa kijana Talib, maisha yalizidi kuwa magumu kwake, maana sasa hata vile vitu vidogo vidogo vya kuiba ili akauze apate fedha ya bangi alikosa, sasa alikuwa anaenda kujikalisha kwenye vijiwe vya wauzaji na wavutaji wa bangi, ili wenzake wanapo nunua na yeye adowee (agongee), maana hata rafiki yake Vitus hakujua yupo wapi toka walipomaliza shule na Talib kusitishiwa huduma za fedha na usafiri, Vitus nae akatoweka, sio Vitus peke yake hata marafiki wengine wakike na wakiume waliokuwa wanamfuata Talib kwaajili ya hela zake nao walitoweka, japo baadhi yao alikuwa anakutana nao, lakini hawakuwa na mpango nae, walimpita kama mtu ambae hawakuwa wanamjua.
Lakini siku moja Talib akiwa amewahi kweli kweli kwenye viwanja vya RMA, sehemu ambayo wavuta bangi wengi hutumia kama sehemu ya kununulia na kuvutia sigara hiyo, ambayo mpaka sasa nchini kwetu haijapata kibali cha kutumika, akiwapeke yake huku kiu ya kilevi hicho ambacho toka alipopewa jana kwa ule utaratibu wa mwenge hauvuki kijiji, akuwa amevuta tena mpaka leo, alijaribu kutafuta pisi pale chini, pengine angeweza kuviunganisha na kupata angalau kidogo ya kuvuta muda ule (wenyewe wanaita chaukucha), lakini hakupata hata mbegu ya mmea huo wenye majina mengi duniani.
Naam Talib akiwa amekosa bangi na kiu kali sana, wenyewe wanaita alosto, aliwaza mengi sana pale pembezoni mwa uwanja huu mkubwa wa michezo, ukweli alijiona kuwa anaonewa sana na kunyanyaswa na mjomba wake, ukweli hakuangalia matendo yake mabaya yaliyo sababisha hayo yote, ikiwa ni ulevi na utumiaji wa bangi, wizi na matukio mengine ya kuchukiza, Talib aliumia sana jinsi binamu yake Soraya alivyokuwa analelewa na kuhudumiwa kama malkia fulani, hakuna kitu alihitaji hakupewa, japo hakuwa na mambo mengi ya ziada zaidi ya mahitajio ya shule, nguo mpya na matoleao ya viatu na mapambo ya kisasa, hakuzuiliwa kutumia gari muda wowote alioutaka, japo hakuwa mtu wa safari za ovyo, likizo zake alikuwa anasafiri kwenye dar es salaam au dubai ambako ndiko nyumbani asili ya mzee Mahamud.
Naam wakati Talib anaendelea kuwaza na kunung’unika ndipo alipo shangaa kumuona Vitus akiingia sehemu ile, ukweli Talib alipatwa na mashangao mkubwa sana kumuona Vitus, sio kwasababu alikuwa hajamuona muda mrefu, la hasha, ni kwasababu Vitus aliingia pale akiwa na vijana wengine watatu wakitumia usafiri wa Toyota crester lenye music mkubwa sana, huku wao pia wakiwa wamevalia mavazi nadhifu ya kupendeza kuanzia matisheti suruali zao za jinsi rangi ya blue ya kuiva na mipauko, na raba kali sana miguuni mwao, wengine kati yao walivalia pete na cheni za dhahabu.
“Duh! Talib! ni wewe? mbona upo hivyo?” aliuliza vitus kwa mshangao huku anamtazama Talib kwa jinsi alivyochafuka na mavazi dhaifu, “ebwahee! Vitus una michongo gani siku hizi, mbona unawaka na pamba nyepesi” aliuliza Talib kwa mshangao, huku anamtazama Vitus ambae kiukweli ungedhania yeye ndie anatokea kwenye lile jengo la kifahari la mwarabu tajiri bwana Mahamud, “maisha tu mwanangu, vipi wewe mbona umechoka hivyo?” aliuliza Vitus swali ambalo Talib hakuweza kulijibu, Vitus akamtazama jamaa mmoja kati ya wale aliokuja nao, ambae alionekana kuwa ndie mmiliki wa lile gari, maana hata umri aliwazidi wakina Vitus, “Zido una mfahamu huyu jamaa?” aliuliza Vitus, na yule jamaa anaeitwa Zido ni kama hakumjari sana, lakini akajibu, “nisimjue huyu dogo fala wa pale kwa mwarabu” alijibu zido huku anazunguka gari kwenda kwenye buti na kulifungua, kisha mwingine akatoa mfuko mkubwa kama ule wa kuwekea unga wa sembe au mahindi wa kilo kumi, “sio fea bro, unamuitaje fala” alilalamika Vitus, huku wengine wakicheka, huku talib akishangaa na kutulia kinyonge, maana hakuwa na la kufanya, “kwani uongo huyu ni fala, anakaa kwa tajiri kama yule anashindwa kupiga hela mpaka anaishi kiboya kama hivi?” alisema Zido, huku ana ingiza mkono mfukoni mwake na kutoa lizzler huku wengine wakitulia na kushindwa kuchangia neno, “unadhani Vitus, huyu dogo fala sana, we unakuwaje hivi wakati yule mzee anamawe kibao anasaidia mpaka masikini wa mtaani, halafu we unakuja kuvuta cha ukucha hapa kijiwe” alisema Zido ambae sasa aliingiza mkono kwenye kile kiroba na kuibuka na kiasi fulani cha bangi, “hebu nyonga hii ushtue kidogo nikupe mchongo wa kufaidika, sio unaishi kindezi ndezi” alisema Zido, huku anampatia Talib ile bangi na lizzler (kiaratasi maalumu kwaajili ya kuviligia tumbaku ya asili, local sigaret, hapo sasa hata Talib mwenyewe akatabasamu huku anapokea ile bangi na karatasi ya kusokotea, mara moja akaanza kusokota bangi, huku tabasamu la fisi likitawala mdomoni mwake, ungesema anaandaa paja la kuku wa kienyeji.
Naam sijui Zido aliongea nini na Talib, lakini ghafla Talib alionyesha mabadiliko makubwa sana katika maisha yake, alianza kuwa msafi wa mwili na mavazi, alitumia muda mwingi kushinda nyumbani, pengine angetoka kidogo mchana na kurudi nyumbani, ambapo angesaidia kufanya kazi ndogo ndogo za pale nyumbani, kilichomfurahisha mjomba wake ni kitendo cha kushiriki swala zote tano pamoja na yeye, kwenye chumba ambacho kiliandiliwa kwaajili hiyo, mfano alfajiri na mapema angeamka na kuchukuwa udhu, kisha angeenda kugonga nyumba kubwa na kushiriki swala ya alfajil pamoja na mzee Mahamud shangazi yake na Soraya mwenyewe, pamoja na wafanya kazi wa mule ndani, mchana pia ingekuwa hivyo hivyo kwenye swala ya adhuhuri, hapo ange toka kidogo hakuna aliejua anakoenda, ila saa tisa na nusu angekuwa nyumbani anachukuwa udhu kwaajili ya swala ya alaasiri, ingekuwa hivyo swala ya magharibi na swala ya inshaa na kurudi chumbani kwake, ambako angejifungia kimya kabisa, huku muda wote ungesukia harufu nzuri ya manukat ya ubani au udi.
Ukweli Mahamud na mke wake walijikuta wanaanza kumuamini Talib na kumchulia kama kijana alieamua kubadilika, hivyo na wao wakaamua kuanza kumchukulia kama mwanafamilia wa kawaida, ambapo sasa ukiachilia kumruhusu kuingia nyumba kubwa kama zamani, pia alitumwa sehemu mbali mbali akitumia lile gari dogo aina ya Hyundai, yeye mwenyewe akiwa ni dereva, kamwe hakuacha kuswali na kuhudhuruia ibada ya ijumaa nakuzidi kuwa karibu na bwana Mahamud, ambae sasa alimueka karibu sana mtoto huyu wa shemeji yake, na kumshirikisha katika baadhi ya majukumu yake ya siri ikiwa ni pamoja na kwenda nae kwenye ukusanyaji wa fedha toka kwenye miradi mbali mbali,.
Kitu ambacho bwana Mahamud hakuwa anakijua ni kwamba, Talib alikuwa anakutana kwa siri na wakina Zido na Vitus, “vipi mipango inaendaje?” hilo lilikuwa swali la kila siku la Zido... Itaendelea……