TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA SITA
MTUNZI
Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA TANO: Higgno alifanya hivyo hata wakati shule ilipofunguliwa, alipotoka shule alipitia moja kwa moja jeshini akiwa na Yohane ambae alikuwa ni mmoja wa wakufunzi wa sanaa hiyo ya mapigano, yaani Sen Sei (kwa kijipan), ambae alijitahidi kutumia uwezo wake wote kuhakikisha kijana Higgno ana wiva katika mavunzo hayo ya mapigano.******Week tatu baada ya kufungua shule, wanafunzi wote wakike walipelekwa kwenye zahanati ya jeshi la ulinzi kwaajili ya kupima ujauzito, ikiwa ni utaratibu uliowekwa na shule hiyo, mara wanafunzi wanapotoka likizo na siku tatu mbele ndipo majibu ya vipimo hivyo yalivyoletwa na kusomwa mbele ya wanafunzi wote pale shuleni………ENDELEA…….
Na kati ya wanafunzi wakike mia moja na arobain na sita, wa shule hii ya Luhuwiko ni mschana mmoja tu aliekutwa na ujauzito wenye miezi miwili, “kutokana na sheria za shule hii Hilda Komba sio mwanafunzi wetu tena, amefukuzwa shule, na iwe fundisho kwa wanafunzi wengine” alisikika mwalimu mkuu,l aliesimama mbele ya mkusanyiko wa wanafunzi wote wa Luhuwiko sekondari, “na hili liwe fundisho kwa wanafunzi wengine ambao wanashiriki ngono” alisema yule head master alieonekana wazi kuwa ni mwanajeshi kwa sauti ya ukali.
Taarifa hii ilimuumiza sana Higgno, ambae alikuwa anaamini kuwa ipo siku Hilda angerudi kwake, tena aliamini kuwa sikucahe zijazo, ni mara baada ya Talib kumaliza shule, “lakini sasa kama amesha pata mimba si ndio mwanzo wa kuishi pamoja” mawazo hayo yalimjia Higgno, mara kwa mara akiwa njiani anaelekea jeshini kwenye mazoezi.*****
Hilda baada ya kusomewa hukumu yake ya kufukuzwa shule, aliingiwa na simanzi kubwa sana, moja kuwa na ujauzito, ambao aliamini unaweza kuwa chanzo cha kuachana na Talib, pili kufukuzwa shule, ingekuwa aibu kubwa kwake na wazazi wake, tatu alihofia kuchekwa na Higgno, lakini mara baada ya kukutana na Talib ambae alimuonya asimtaje pale shuleni kuwa yeye ndio muhusika na kumuaidi kuwa akimaliza shule na kukabidhiwa biashara na mjomba wake atamchukuwa na kuishi nae, hapo Hilda alianza kupata furaha na faraja, ongeza bangi na ulanzi, akasahau kabisa kuwa kuna jambo limemkuta shuleni, hata alipofika nyumbani, Hilda aliwanunulia ulanzi wazazi wake ambao walisha zoea swala hili kila siku.
Na wakati wanaendelea kunywa ulanzi, ambao siku za hivi karibuni walisha anza tabia ya kunywa pamoja na binti yao, ndipo Hilda alipoanza kuwasimulia kilicho mtokea.******
Naam saa tatu na nusu, ndio muda ambao mzee Frank akiwa na mwanae Higgno, walikuwa wanafunga duka ili waingie ndani, mara wakamuona mzee Komba anaingia pale nyumbani kwao, nao wakashangaa kumuona mzee huyu nyumbani kwao, “mh! ananini huyu bwana halafu amelewa vibaya sana” aliuliza mzee Frank kwa sauti ya chini, huku yeye na mwanae Higgno wakimtazama kwa tahadhari wakati huo
Higgy Wizzy aliekuwa anajua tukio lililo mtokea Hilda, akiwa ana jiuliza mzee Komba amekuja kufanya nini, isije kuwa Hilda amemsingizia yeye ndie aliempa mimba, ……….. endelea
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA SABA
MTUNZI
Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA SITA: Naam saa tatu na nusu, ndio muda ambao mzee Frank akiwa na mwanae Higgno, walikuwa wanafunga duka ili waingie ndani, mara wakamuona mzee Komba anaingia pale nyumbani kwao, nao wakashangaa kumuona mzee huyu nyumbani kwao, “mh! ana nini huyu bwana halafu amelewa vibaya sana” aliuliza mzee Frank kwa sauti ya chini, huku yeye na mwanae Higgno wakimtazama kwa tahadhari, wakati huo
Higgy Wizzy alie kuwa anajuwla tukio lililo mtokea Hilda, akiwa ana jiuliza mzee Komba amekuja kufanya nini, isije kuwa Hilda amemsingizia yeye ndie aliempa mimba, endelea…….
“mbona mnafunga mapema duka au mme ridhika na visent mulivyo vipata?” aliuliza mzee Komba kwa sauti ya kilevi iliyo jaa jeuri na dharau, hapo Higgno na baba yake wakatulia kimya wakimtazama mzee Komba, “we dogo hebu nipatie sport mbili, alisema mzee Komba, huku akimpatia Higgno shilingi thelathini, kwa mgao wa sarafu ya shilingi ishirini moja na shilingi tano tano mbili, Higgno alimtazama baba yake, ambae alimuonyesha ishara kuwa aende akamchukulie, nadhani mzee Frank alichelea kusemewa vibaya na mzee Komba, maana toka siku ile alipomjia asubuhi kumshtakia Higgno urafiki wao ulipotea hapo hapo, Higgno akapokea ile fedha na kuelekea kwenye mlango wa duka na kuufungua, “unajua bwana Frank, sisi masikini huwa tuna ridhika z na vitu vidogo sana, mfano wewe saizi unafunga duka wakati watu kama wakina Mahamud ndio kwanza kama kuna kucha” alisema mzee Komba kwa sauti ambayo kama ungekuwepo na kuisikia ungejua ni mtu mwenye fedha na uwezo mkubwa wa kiuchumi, “ni kweli kabisa, bwana Komba, lakini sasa unawezaje kukesha wakati wateja wenyewe wamesha lala” alisema mzee Frank kwa sauti tulivu.
Mzee Frank akamsikia bwana Komba anaguna huku anatikisa kichwa kwa maskikitiko, “hizo ni dharau bwana Frank, inamaana mimi sio mteja?” aliuliza mzee Komba kwa sauti ya kilevi iliyoonyesha kusikitishwa, huku bado anatikisa kichwa kwa masikitiko na kufanya kama vile mtu anaita paka aje kukuchukua chakula, “sina maana hiyo Komba, na maanisha watu wengi wanakuwa wamelala” alirekebisha kauri yake mzee Frank, wakati huo Higgno alikuwa anatoka dukani akiwa na sigara mbili aina ya sport mkononi mwake, akampatia mzee Komba, “unaona dharau nyingine hii, kibiriti kikowapi?” aliuliza mzee Komba, hapo bila kuuliza Higgno akarudi dukani haraka, “unajua bwana Frank unamuharibu huyu mtoto, na atakuja kukupa shida sana hapo baadae” alisema mzee Komba kwa sauti ya kilevi, “kivipi bwana Komba?” aliuliza Frank, kwa sauti tulivu huku akimtazama kwa umakini mzee Komba, watu wanasema ukiona mlevi kaja kwako kwa shari, ujue alidhamilia, “huwezi kujua, lakini nadhani unakumbuka kipindi cha karibia na mavuno, huyu kijana wako alitaka kupigana na wakina Hilda, ukajifanya hujui sababu ni nini” alisema bwana Komba, na hapo mzee Frank akajua kuwa huyu bwana Komba bado alikuwa na kisa chake kile kile, “inamaana bado una yale yale?” aliuliza Frank kwa sauti ya tulivu, iliyoonyesha kuhuzunishwa kwake, “sikiliza Frank nikueleze kijana wako alivyo mbinafsi, huyu, aliona mwenzie amepata mwanaume mwenye fedha, mtoto wa tajiri ndio alitaka kuwatengenisha, sijui yeye angepata faida gani?” aliongea mzee Komba na kumshangaza mzee Frank, mwanaume! binti wa kidato cha kwanza!
Wakati huo tayari Higgno alikuwa ameshasimama karibu na mzee Komba akamkabidhi kibiriti, “niskie vizuri bwana Frank” alisema mzee Komba alieibana sigara yake mdomoni na kuiwasha, “nakusikiliza unieleze ubinafsi wa kijana wangu” alisema mzee Frank ambae alikuwa anajitahidi kuzuia jazba zake, bwana Komba akiwa asie na uharaka wote, alipiga pufu moja la sigara yake na kutoa moshi mrefu, ambao ulisambaa na kuwa fikia wakina Higgno na baba yake, ambao hawakuwa na budi ya kuvumilia, “huyu dogo ni mbinafsi sana, hakutaka mwenzie apate mwanaume tajiri, sasa kiko wapi, hapa tunasubiri ndoa muda wowote kuanzia mwezi wa kumi na mbili” alisema mzee Komba kwa majisifu na kumfanya mzee Frank ashangae kwa kuachama mdomo, “samahani bwana Komba najua mambo ya familia yako hayanihusu, lakini unamaanisha kuwa Hilda anaacha shule anaolewa…” kabla hajamaliza swali lake bwana Frank, mzee Komba akamdaka juu kwa juu, “kumbe sasa, hivi mwanamke hata akiwa waziri au rais wa nchi bila mume si anaonekana ni muhuni tu!, tena anaolewa na mtoto wa tajiri Mahamud” alisema kwa sauti ya kujisifu na majivuno ya hali ya juu.
Mzee Frank akamtazama Higgno, ambae kauli ya mzee Komba ni kama ili mtonesha kidonda, hivyo alitazama chini kwa huzuni ambayo mzee Frank aliiona wazi wazi, “nitafungua duka kubwa sana hapa kijijini, na sitokuwa na majivuno kama nyie” mzee Komba aliyasema hayo huku anaondoka zake na kuanza kuimba kilevi kwa sauti ya juu kabisa, “vandu vava mwenga (watu hawa jamani) “ alirudia mara kadhaa na alipofikia kipengere cha mbele yake akaimba, “vatu makoko, vandu makoko (watu ni mbwa)” aliimba huku ana kanya miguu chini kwa nguvu.
Frank na mwanae Higgno walimsindikiza kwa macho mpaka alipotoweka na kubakia wakisikia sauti yake kwa mbali ikizidi kutokomea kuelekea upande wa nyumbani kwake, ndipo bwana Frank alipohitaji ufafanuzi wa jambo hili, na Higgno akamueleza vyema kabisa kuwa Hilda amefukuzwa shule kwaajili ya ujauzito, aliopewa na Talib, ambae inasemekana kuwa ni mtoto wa tajiri mkubwa sana pale mjini songea, mwarabu Mahamud, “hata hivyo hainiingii akilini kama Mahamud ambae anasomesha mtoto wake wakike akubali kijana wake amuachishe binti wa watu shule” alisema mzee Frank wakiwa wanaingiza ndani ya nyumba yao, maana hata kibiriti walikisahau mzee Komba akaondoka nacho.*****
Naam siku iliyo fuata zikaanza kusambaa taarifa za Hilda kuacha shule kwaajili ya ujauzito, taarifa zilizo sambazwa na wazazi wake mwenyewe, sio kwa ubaya, ila kwa majisifu ya kuwa binti yao anaolewa na mtoto wa tajiri, mwarabu Mahamud, taarifa hizo ambazo ziliambatana na shutuma nzito kwa familia ya bwana Frank, shutuma ya kuwa familia hii haipendi binti yao aolewe na mtoto wa tajiri, ndio maana hata Higgno aliwahi kujaribu kuwavamia na kuwapiga, bahati nzuri aliambulia kipigo.
Wapo waliounga mkono jambo hilo, lakini wapo waliotia shaka juu ya hili, wakiamini kuwa kwa muonekano wa Talib hakuwa muoaji, swala hilo lilianza kuthibitishwa na Hilda ambae hakuwahi kuwaelekeza wazazi wake mambo yalivyokuwa yakienda, ikiwa ni pamoja kupungua kwa mapenzi yao na Talib, ambae sasa alikuwa anamkwepa mara kwa mara kila Hilda alipojaribu kumtafuta, na hata kuonekana kwake kulikuwa ni kwa nadra sana.
Siri iliwekwa wazi mwezi wa pili mwaka 1998, mwezi mmoja toka Higgno aingie kidato cha pili, miezi mitatu toka Talib amalize shule, ukimya ukiwa umetawala, hata zile mia mbili mia mbili za ulanzi na mishkaki hazikuonekana tena, tumbo la Hilda lilisha kuwa pevu, kiasi cha kuwa muda wowote mwezi huu wa pili alikuwa anatarajia kujifungua.
Baada ya kuona hakukuwa na dalili ya kuja kwa ujumbe wowote juu ya swala la kuolewa kwa Hilda ndipo mzee Komba alipoamua kujibeba yeye na mke wake na mwanae kwenda kwa mzee Mhamud kujieleza na kutafuta muafaka juu ya ujauzito na ndoa ya mwanae Hilda.****
Ilikuwa juma mosi, mida ya saa tano asubuhi, binti Soraya binti wa pekee wa tajiri mkubwa mjini songea bwana Mhamud, akiwa amesimama nje ya gate kubwa la shule sekondar ya waschana ya songea, huku amevalia nguo nadhifu za kiraia, gauni refu jekundu, kilemba hijab nyeusi viatu virefu vya mchuchumio, mkononi alikuwa na madaftari manne kama kawaida yake, mara likaonekana gari aina ya Land Rover discover likija na kusimama karibu yake, akaingia kwenye seat ya nyuma ya gari hilo na gari likaondoka kueleka upande wa mjini, likipitia RMA, “Laylah baba umemuacha nyumbani?” aliuliza Soraya, kwa sauti yake laini ambayo ukiisikia mara moja ungependa uisikie kila mara, “wote pamoja na mama wapo nyumbani, na nina imani ya kuwa bado wapo nyumbani kwasababu wakati natoka niliona kuna wageni wanaongea na mlinzi pale getini”, alijibu dereva wake ambae alikuwa makini sana kwenye kazi yake ya udereva, “wageni wa mama au baba?” aliuliza Soraya ambae alikuwa amebadilika kidogo tofauti na mwaka jana alivyokuwa anaonekana kuwa binti mdogo, sasa alionekana kuwa mschana angalau hata kifua chake kilichomoza maziwa mazuri yenye ukubwa wastani, hips zilizidi kutanuka na makalio yake kuongezeka ukubwa, urefu pia uliongezeka na kumfanya azidi kuwa mzuri wa sura na umbo pia.
Safari iliendelea kimya kimya kama dakika mbili hivi, ndipo Laylah akavunja ukimya, “Sora, vipi uliutazama ule mkanda jana” aliuliza Laylah huku akijichekesha kidogo, “kweli bwana umenikumbusha, niliutazama ni mzuri, mimi huwa natazamaga tu mikanda ya kihindi kumbe na ile ya wazungu ni mizuri” alisema Soraya akionyesha furaha, inaonyesha sasa alisha zoeana sana na dereva wake Layla “nimekubebea mwingine, lakini ni wa wamarekani weusi” alisema Layla, aliekuwa anaendelea kuendesha gari kwa umakini mkubwa sana, “afadhari niitazame leo usiku” alisema Soraya na sasa gari lilikuwa linaingia nyumbani kwao na kusimama nje ya gate na kupiga honi.
Gate lika funguliwa na hapo hapo wakawaona watu watatu, wakilisogelea gari lao, huku mwanaume mzee akiwa mbele anakimbilia gari na nyuma yake wanawake wawili wakimfuata, mama akiwa mtu mzima akiwa amemshika mkono mschana mjamzito, ambae mimba yake ilionyesha muda wowote anaweza kujifungua kwa ukubwa wake, “samahani mama naomba ninashida na wewe” alisikika yule mzee akiongea kwa sauti ya kuomboleza, huku akilikimbilia gari nusu aaguke kwa mbio alizotimua, lililokuwa linaanza kuingia ndani, lakini Layla hakusimamisha gari akaingiza gari ndani na lango likafungwa, “hebu simamisha gari” alisema Soraya, na Layla akasimamisha gari, “hivi umemsikia huyo mzee alikuwa anasema anashida na wewe vipi una mfahamu?” aliuliza Soraya kwa ile sauti yake nyororo ya kiarab, “siwafahamu, ila hao ndio niliokuambia kuwa ni wageni wa baba, nimewaona wanaongea na mlinzi” alisema Laylah, hapo Soraya akashuka toka kwenye gari, “we mlinzi, hao wazee hapo nje wanahitaji nini?” aliuliza Soraya, huku anatembea kumsogelea mlinzi, ambae kiukweli siku zote amezoea kumuona kwa mbali akiwa kwenye bustani ya mauwa anajisomea au amepumzika, vinginevyo hakuweza kumuona kwa ukaribu licha ya kukaa hapa getini kwa mezi saba sasa, siku zote alikuwa akipita getini huku amepandisha vioo vya gari, “boss haaa! wamesema wanataka kumuona baba au mama” alijibu kwa sauti ya uoga uoga yule mlinzi
Hapo Soraya akatazama kwenye maegesho ya magari na kuona magari yote yapo, ikionyesha kuwa watu wote wapo, ukiachilia Hyundai ambalo sasa lilikuwa halitumiwi na mtu, ni baada ya Talib kuzuiliwa kutumia gari hilo ambalo baada ya kumaliza shule na kupata daraja ziro kwenye matokea ya mtihani huo wa taifa, Nissan ambalo hutumiwa na baba yake lilikuwepo, Pajero la mama yake lilikuwepo, hata Suzuki maruti la kuendea sokoni pia lilikuwepo, sasa kwanini huja waruhusu, ina maana baba amekataa?” aliuliza Soraya huku amemkazia macho mlinzi, ambae alitazama kwanza upande wa kushoto wa jumba lile la kifahari, ambako kulikuwa na vijumba vinne vidogo vidogo, vijumba ambavyo kimoja wapo alikuwa anaishi Talib kwa sasa, ni mara baada ya kuzuiliwa kuingia nyumba kubwa kutokana na tabia yake ya udokozi iliyosababishwa na ulevi na uvutaji wa bangi.
Mlinzi hakumuona mtu yoyote, “Talib amenizuia nisiwafungulie” alijibu mlinzi….
Naam nini kitajili? Endelea Kufuatilia hapa hapa
jamii forums.