SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA THELATHINI NA NANE
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA THELATHINI NA SABA: Naam hapo wote wakamuona mama soraya akija mbiombio ana simu ya mume wake mkononi, huku uso wake ukionyesha wazi kuwa alikuwa katika mashaka makubwa sana, “huuuwi baba Soraya najuta kupokea simu yako mume wangu, majambazi wame mkamata Soraya” alisema mama Soraya huku sauti yake ikiambatana na kilio, mzee Mahamud akainuka haraka na kumsogelea mke wake aliekuwa anakuja pale sebuleni na kuichukua yake toka kwa mke wake, “wanataka kuongea na wewe” alisema mama Soraya kwa saui ile ile ya kilio huku mikono akiipeleka kichwani, “kelele za nini sasa, mna mwaga mchele kwenye kuku wengi” alijisemea Talib kimoyo moyo huku usoni akijifanya kuwa katika mshangao…… ENDELEA
Mahamud akiwa wenye hofu na wasi wasi akaiweka simu sikioni na kuongea mara moja, “hallow mnashida gani na binti yangu” kisha akaonekana kutulia kimya akisikiliza kinacho ongelewa na mpigaji wa simu hiyo, na baada ya sekunde kama thelathini hivi akasikika tena mzee Mahamud akiongea kwa mara ya pili, “fedha nitawapatia lakini nawaomba msimdhuru mwanangu, pili naomba nusu saa nikusanye hiyo fedha” alisema Mahamud na kusikiliza jibu la ombi lake, inaonekana alisha kubaliwa maana alikata simu na kumtazama Talib, kisha akamuonyeshea ishara ya kumuita.
Talib akiwa anajuwa kuwa sasa anaenda kupewa fedha ya maana akainuka haraka na kumfuata mjomba wake huku akijitahidi kuficha furaha yake isionekane wazi usoni mwake, huku mama Soraya akiendelea kumporomosha kilio na tayari wanawake wengine ambao walikuwa wameshafika katika kundi la wegeni na wafanyakazi wake walishafika na kumchukua mama huyu kumpeleka kwenye chumba cha wageni kumtuliza, japo ilikuwa kazi bure kwasababu aliendelea kutiririsha kilio.
Wageni walio kuwa sebuleni ambao walishahisi kinachoendelea hivyo wakainuka wawili watatu wakajiunga na Talib kuongozana pamoja na mzee Mahamud wakaingia ndani ya ofisi ya pale nyumbani ya mzee Mahamud, “nini kimetokea bwana Mahamud” aliuliza mmoja kati ya wale ndugu na jamaa walio jiunga pamoja na Talib na mjomba wake, yaani bwana Mahamud alieonekana kubeba sura ya fadhaha na yenye wasiwasi kwa ghafla sana, “mwanangu ametekwa na majambazi wanahitaji million kumi ndani ya nusu saa, wameagiza nisimuambie mtu yoyote wala kuoa taarifa kituo chochote cha polisi, nikifanya hivyo watamuuwa mwanangu” alisema Mahamud kwa sauti iliyoonyesha wazi kuchanganyikiwa na tukio la kutekwa mwanae, huku anaelekea ukutani na kwenye picha yake kubwa na kuitoa ile picha, na hapo wote wakaona kipande cha mbao kilicho pachikwa mfano wa kizibo cha dirisha la kabati hata Talib ambae alishawahi kuingia mule ofisini mata kadhaa akaonekana kushangazwa na muonekano wa ile taswira, “wewe unaonaje Mahamud ni vyema kufuata maagizo hayo au utumie muda huo kuwa taarifu polisi ili….” alisema mmoja kati ya wale watatu walio ingia mule ofisini, lakini Talib akadakia haraka, “mh! anko usijaribu kuwazunguka wanaweza kummaliza kabisa” alisema Talib kwa sauti ya kukurupuka, kiasi cha wote kumtazama kasoro mzee Mahamud mwenyewe, ambae alikuwa anafungua kile kimfuniko cha mbao pale ukutani na kukuta kimlango cha chuma chenye funguo ya namba, “sikieni jamani, hata kama una mpango wa kupeleka hiyo fedha ni muhimu kushirikisha jeshi la polisi, inawezekana watekaji wanaamua kumuua Soraya mara baada ya kupata fedha zao ikiwa ni kufuta ushahidi wakihofia atakuwa amesha wagundua” alisema yule mzee alieshauri mwanzo, “ni kweli hilo ni wazo zuri, maana wamesema kuwa nimkabidhi Talib hizo fedha, hivyo basi Talib akiondoka kuwapekelekea na polisi nao waanze kumfuata Talib” alisema Mahamud, huku akimtazama yule mzee alietoa ushauri, wakati huo Talib alikuwa ana chezea simu yake kwa haraka sana kisha akaiweka mfukoni.
Naam wazo lile lilikuwa zuri sana kwa Mahamud ambae alifungua lile kabati na kutoa maburungutu ya fedha, zikiwa ni noti elfu kumi kumi, kila fungu likiwa na jumla ya million moja, na kuweka mezani akisaidiwa na Talib na wale wazee, alipomaliza akatoa simu yake na kuanza kutafuta namba ya mkuu wa polisi ambae angemsaidia katika swala lile la kumuokoa mwanae, huku Talib akionekana kuingiwa na uso wa mashaka, “nadhani huyu anaweza kuni saidia” alisema Mahamud, ambae alikuwa ameipata namba ya simu ya RTO, (Region Treffick Officer/kamanda wa usalama wa barabarani mkoa) ndie mtu aliemzoea kupita kiasi kutokana na kazi zake za kibiashara za usafirishaji, hapo Talib akajua kuwa mpango wake wa kwanza wa kupata fedha ambazo alikuwa anaziona mezani unaweza kushidwa, na pengine kufanikisha mpango wa pili, ambao ni wakumuuwa Soraya, “lakini anko…” kabla Talib hajamaliza neno lake mara simu ya Mahamud mkononi mwake ikaita, na alipoitazama ikaonyesha kuwa ni namba ile ile ya watekaji, “haooo wanapiga tena” alisema Mahamud kwa sauti iliyojawa na mashaka, huku anaipokea ile simu na kuiweka sikioni, “lakini nilisema mnipe muda wa kukusanya fedha sasa mbona…” alisema Mahamud kwa sauti iliyojaa wasi wasi, “sikia we mzee, najua una mpango wa kuwaambia polisi, sasa ukifanya hivyo usilete fedha ila subiri taarifa ya polisi ya kuokotwa kwa mwili wa Soraya” iliskika sauti nzito ya kiume ambayo iliambatana na kilio cha mbali cha Soraya akilalamika “niacheni jamani niacheni” hapo mzee Mahamud aliingiwa na hofu kubwa zaidi, “tafadhari usimdhuru mwanangu, sijaenda polisi wala kutoa taarifa polisi, nampa Talib fedha anazileta sasa hiv…” aliongea Mahamud na kabla hajamaliza kuongea mara akasikia kishindo cha kama vile simu ikidondoka chini na hapo ikakatika, hizi ni million nane wacha nipige simu msamala stendi walete million mbili ili Talib aende haraka, wamesema watamuuwa mwanangu” alisema Mahamud huku ana bofya simu yake kupiga kwenye ofisi yake ya msamala stendi.******
Wakati huo huo mzee Mahadhi na mwanae Idd, walikuwa wameshakutana na wazee wabaraza, wanaingia kwenye gari yao kuanza safari ya kuelekea kwa bwana Mahamud, “kijana umechukuwa maamuzi mazuri sana kumchumbia Soraya binti Mahamud, ni mschana mzuri anajiheshimu na wala hajawahi kusika hata mara moja amefanya yale ya kipuuzi yakuchukiza” alisema mmoja wa wazee waliopanda gari la bwana Mahadhi na Idd alikuwepo ndani yake akicheka cheka kicheko cha ushindi, “tena ni heshima kubwa sana kwa Idd kumchumbia binti wa Mahamud, nimepata kesi nyingi sana za vijana walioshindwa kupata nafasi hiyo” alisema mwingine, manaa mule ndani ya gari walikuwa wanne, yaani Mahadhi wazee wengine wawili na kijana Idd, ambae kama sio karafuu alizotafuna, basi mule ndani ya gari dogo wote wangekuwa wameshalewa kwa harufu ya pombe, “ni kweli bwana ilisadikika kuwa mzee Mahamud ndie anae mshawishi mwanae awakatae vijana wa Kiswahili ikiwa ni sehemu ya ubaguzi wa rangi” alisema mzee yule wa kwanza, “lakini mbele ya mwenyekiti sidhani kama ataleta ujanja wake” alisema Mahadhi, ambae ndie alikuwa dereva wa gari hili ambalo lilikuwa ni la pili toka nyuma, katika magari matano waliyokuwa nayo katika msafara ule, mbona yeye mke wake ni mngoni, kwanini yeye amzuie mwanae” alisema Idd, ambae uongeaji wake na sauti yake kama wale wazee wange kuwa makini basi wange gundua kuwa Idd alikuwa amelewa, baada yake walicheka kwa kumuunga mkono, “wala usiwe na wasi wasi kijana, kwa mwenyekiti amekwama, namfahamu yule mzee kwa maneno yake ya busara na mitego” alisema mzee mwingine huku safari inaendelea pasipo kujua kuwa huko kwa mzee Mahamud mambo yalisha haribika.******
Tayari Laylah alishapata nafuu na maumivu kuisha kabisa, hivyo akaruhusiwa kuondoka pale hospital, nae akaona itakuwa vyema akielekea nyumbani kwa boss wake akawajulishe hali yake, kisha aende nyumbani akapumzike, Laylah akiwa njiani aliendelea kutafakari hili na lile juu ya sabuni aliyokula na kumvuruga tumbo, hakika licha ya kuwaza kwa muda mrefu lakini alikosa jibu.
Lakini Laylah alipofika nyumbani kwa mzee Mahamud au ikulu ya mwarabu kama wanavyo paita na kukuta kuna mambo mengi yanaendelea pale nyumbani, kwanza maandalizi kama ya sherehe ndogo, hivyo akamtafuta Subira mfanyakazi wa Soraya, yaani yaya, na kumuuliza, “ndugu yangu kuna makubwa yametokea leo, mwenzio leo yule kijana Idd anakuja kuleta barua ya posa, wakati huo huo Soraya mwenyewe ametekwa na majambazi” alisema Subira kwa sauti iliyojaa masikitiko, ujue Subira ndie yaya wa Soraya toka Soraya akiwa mtoto mdogo sana, “mh! mbona makubwa Soraya kutolewa barua na Idd, Soraya kutekwa na majambazi” alishangaa Laylah na hapo kwa haraka akaanza kuchezesha akili, “mh! nimetoka nyumbani nikiwa mzima kabisa, nikashikwa na tumbo la ghafla na kushindwa kumpeleka Soraya shambani, Soraya kutekwa nyara, mbona kama kuna mchezo umechezeka,” aliwaza Laylah, “kwani Soraya mwenyewe ana fahamu kama leo anatolewa barua?” aliuliza Laylah, “ajue wapi wenzio wanataka wamshtukize ili ashindwe kukataa” alisema Subira na kumfadhaisha Laylah, “ina maana boss ameshindwa kuelewa kuwa Idd ni kijana mbaya kwa Soraya” alisema Laylah, “lakini mimi nina mashaka na Soraya, unadhani amesha gundua na kujisingizia ametekwa?” aliuliza Subira kwa sauti ya chini, “eti eeh! hebu ngoja kwanza nijaribu kumpigia” alisema Laylah huku anatoa simu yake na wote waka sogea pembeni zaidi huku Laylah anabofya simu yake na kuipiga namba ya Soraya.******
Sio kwamba tumewasahau babu mabudi na mama Hilda, hapana wakati kule mambo yanaendela hebu twendeni shambani kwa Soraya ambako mambo yalikuwa hivi.
Mara baada ya wale wakulima wake kukimbia na kutokomea upande wa mtoni, baada ya kuwafanyia ujanja na kuwatoroka wale watu alio wahisi ni majambazi, ambao walijiondoa lile vumbi na kumsogelea yeye Soraya ambae alikuwa amekamatwa na mmoja wao, “oya jamani eeh, huyu mtoto mimi simuachi hivi hivi, lazima nitoe gundu la kumla mtoto wa kiarabu” alisema mmoja wao na Soraya kusikia hivyo hata mwili ulimsisimka, maana alianza kuvuta picha ya maumivu atakayo yapata huku akisikilizia jibu atakalopewa na wenzake, “weweeee unaongea sasa hivi wakati mwenzio Zido alishapanga toka nyumbani, yaani akimaliza tu na mimi naingia” alisema mwingine huku Soraya akishindwa kuwatambua kwa sura vijana hawa
ambao bado walikuwa wamejiziba sura yao, “msinifanye hivyo nitawapa hela muniachie” alisema Soraya kwa sauti ya kinyonge iliyoambatana na kilio, hawa jamaa vipi si waje basi tumalize kazi” alisema mmoja wao na wakati huo huo wakasikia ngurumo ya gari, wakageuka kutazama upande ule na wakaliona Toyota carina likiibuka toka upande wa daraja la mahilo, “haooo! wanakuja” alisema mmoja wao huku wanaendelea kulitazama lile gari dogo ambalo lilisimama upande ule wa barabara, na wakashuka jamaa wawili ambao pia walivaa sox kama za wenzao, ambao waliwasogelea mpaka pale walipo, na walipowafikia Zido ambae bado aliziba uso alimsogelea kabisa Soraya aliekuwa bado ameshikwa na yule jamaa, “safi sana, sasa tuwasiliane na baba yake” alisema Zido huku akimtazama Soraya kwa macho ya tamaa na uchu, kisha akatoa simu yake na kupiga kwa mzee Mahamud na ndipo simu ilipo pokelewa na mama Soraya, hata hivyo alipewa Mahamud mwenyewe na kisha Zido akatoa maelekezo, kuwa wakitaka amuachie Soraya apewe million kumi na fedha hizo apewe Talib asiongozanae na mtu yoyote, na wala taarifa isifike polisi, “kwasababu kufanya hivyo ni kumpoteza Soraya” alisema Zido kwa msisitizo huku Soraya mwenye akisikia kwa masikio yake.
Kama tulivyosoma kwenye kipande kilichopita nyumbani kwa Mahamud, ni kwamba wakati wakiwa wanasubiri mpangilio wa fedha, huku wanapanga kumuingilia kimwili Soraya, Zido akipanga kuwa wakwanza kisha Vitus halafu wale wengine wanne kila mmoja akitaka kufanya hivyo, hakika Soraya alikuwa katika mashaka makubwa sana, wasi wasi na machungu makubwa, Soraya alililia kwa sauti akiomba wasi mfanyie kile walichohitaji kukifanya kwenye mwili wake, lakini hawa jamaa hawakuonyesha dalili ya kumuelewa Soraya.
Lakini wakati wanataka kumpeleka kwenye kibanda kidogo kilichopo pale shambani kwa lengo la kumuingilia kimwili mschana huyu mrembo wa kupindukia, mschana ambae alikuwa ndoto ya kila kijana mwenye fedha mjini Songea, mara ukaingia ujumbe kwenye simu Zido, ambao aliufungua na kuanza kuusoma kwa sauti “oya sikia, “jamaa anasema mwarabu anataka kututumia polisi hivyo tumpigie simu kumtisha” alisema Zido na kuanza kupiga simu kwa mzee Mahamud.
Hapo ndipo Soraya alipoanza kugundua kuwa mpango wa kumteka umeanzia kwa mtu wa karibu wa familia yao, ambao moja kwa moja alihisi kuwa ni wafanyakazi wa pale nyumbani kwao, na wakati Zido anaongea na simu yeye wakaanza kumkokota kumpelaka kwenye kibanda huku anapiga kelele za kuomba msaada, lakini wakati huo huo akasikia kishindo cha “guh!” kilichotokea pale alipokuwepo Zido, wote wakageuka kutazama wakamuona Zido akiwa ameanguka chini huku simu yake ikiwa pembeni imeanguka, karibu yake amesimama kijana mmoja alievalia kaptura ya jinsi bila ya shati “kijana mpole” alinong’ona Soraya, ambae uso wake ulianza kuachama kwa tabasamu la matumaini na furaha, tabasamu ambalo lilipochanua usoni mwake lilianzia tumboni kifuani mpaka usoni kwake…… ITAENDELEA
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA THELATHINI NA NANE
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPOISHIA SEHEMU YA THELATHINI NA SABA: Naam hapo wote wakamuona mama soraya akija mbiombio ana simu ya mume wake mkononi, huku uso wake ukionyesha wazi kuwa alikuwa katika mashaka makubwa sana, “huuuwi baba Soraya najuta kupokea simu yako mume wangu, majambazi wame mkamata Soraya” alisema mama Soraya huku sauti yake ikiambatana na kilio, mzee Mahamud akainuka haraka na kumsogelea mke wake aliekuwa anakuja pale sebuleni na kuichukua yake toka kwa mke wake, “wanataka kuongea na wewe” alisema mama Soraya kwa saui ile ile ya kilio huku mikono akiipeleka kichwani, “kelele za nini sasa, mna mwaga mchele kwenye kuku wengi” alijisemea Talib kimoyo moyo huku usoni akijifanya kuwa katika mshangao…… ENDELEA
Mahamud akiwa wenye hofu na wasi wasi akaiweka simu sikioni na kuongea mara moja, “hallow mnashida gani na binti yangu” kisha akaonekana kutulia kimya akisikiliza kinacho ongelewa na mpigaji wa simu hiyo, na baada ya sekunde kama thelathini hivi akasikika tena mzee Mahamud akiongea kwa mara ya pili, “fedha nitawapatia lakini nawaomba msimdhuru mwanangu, pili naomba nusu saa nikusanye hiyo fedha” alisema Mahamud na kusikiliza jibu la ombi lake, inaonekana alisha kubaliwa maana alikata simu na kumtazama Talib, kisha akamuonyeshea ishara ya kumuita.
Talib akiwa anajuwa kuwa sasa anaenda kupewa fedha ya maana akainuka haraka na kumfuata mjomba wake huku akijitahidi kuficha furaha yake isionekane wazi usoni mwake, huku mama Soraya akiendelea kumporomosha kilio na tayari wanawake wengine ambao walikuwa wameshafika katika kundi la wegeni na wafanyakazi wake walishafika na kumchukua mama huyu kumpeleka kwenye chumba cha wageni kumtuliza, japo ilikuwa kazi bure kwasababu aliendelea kutiririsha kilio.
Wageni walio kuwa sebuleni ambao walishahisi kinachoendelea hivyo wakainuka wawili watatu wakajiunga na Talib kuongozana pamoja na mzee Mahamud wakaingia ndani ya ofisi ya pale nyumbani ya mzee Mahamud, “nini kimetokea bwana Mahamud” aliuliza mmoja kati ya wale ndugu na jamaa walio jiunga pamoja na Talib na mjomba wake, yaani bwana Mahamud alieonekana kubeba sura ya fadhaha na yenye wasiwasi kwa ghafla sana, “mwanangu ametekwa na majambazi wanahitaji million kumi ndani ya nusu saa, wameagiza nisimuambie mtu yoyote wala kuoa taarifa kituo chochote cha polisi, nikifanya hivyo watamuuwa mwanangu” alisema Mahamud kwa sauti iliyoonyesha wazi kuchanganyikiwa na tukio la kutekwa mwanae, huku anaelekea ukutani na kwenye picha yake kubwa na kuitoa ile picha, na hapo wote wakaona kipande cha mbao kilicho pachikwa mfano wa kizibo cha dirisha la kabati hata Talib ambae alishawahi kuingia mule ofisini mata kadhaa akaonekana kushangazwa na muonekano wa ile taswira, “wewe unaonaje Mahamud ni vyema kufuata maagizo hayo au utumie muda huo kuwa taarifu polisi ili….” alisema mmoja kati ya wale watatu walio ingia mule ofisini, lakini Talib akadakia haraka, “mh! anko usijaribu kuwazunguka wanaweza kummaliza kabisa” alisema Talib kwa sauti ya kukurupuka, kiasi cha wote kumtazama kasoro mzee Mahamud mwenyewe, ambae alikuwa anafungua kile kimfuniko cha mbao pale ukutani na kukuta kimlango cha chuma chenye funguo ya namba, “sikieni jamani, hata kama una mpango wa kupeleka hiyo fedha ni muhimu kushirikisha jeshi la polisi, inawezekana watekaji wanaamua kumuua Soraya mara baada ya kupata fedha zao ikiwa ni kufuta ushahidi wakihofia atakuwa amesha wagundua” alisema yule mzee alieshauri mwanzo, “ni kweli hilo ni wazo zuri, maana wamesema kuwa nimkabidhi Talib hizo fedha, hivyo basi Talib akiondoka kuwapekelekea na polisi nao waanze kumfuata Talib” alisema Mahamud, huku akimtazama yule mzee alietoa ushauri, wakati huo Talib alikuwa ana chezea simu yake kwa haraka sana kisha akaiweka mfukoni.
Naam wazo lile lilikuwa zuri sana kwa Mahamud ambae alifungua lile kabati na kutoa maburungutu ya fedha, zikiwa ni noti elfu kumi kumi, kila fungu likiwa na jumla ya million moja, na kuweka mezani akisaidiwa na Talib na wale wazee, alipomaliza akatoa simu yake na kuanza kutafuta namba ya mkuu wa polisi ambae angemsaidia katika swala lile la kumuokoa mwanae, huku Talib akionekana kuingiwa na uso wa mashaka, “nadhani huyu anaweza kuni saidia” alisema Mahamud, ambae alikuwa ameipata namba ya simu ya RTO, (Region Treffick Officer/kamanda wa usalama wa barabarani mkoa) ndie mtu aliemzoea kupita kiasi kutokana na kazi zake za kibiashara za usafirishaji, hapo Talib akajua kuwa mpango wake wa kwanza wa kupata fedha ambazo alikuwa anaziona mezani unaweza kushidwa, na pengine kufanikisha mpango wa pili, ambao ni wakumuuwa Soraya, “lakini anko…” kabla Talib hajamaliza neno lake mara simu ya Mahamud mkononi mwake ikaita, na alipoitazama ikaonyesha kuwa ni namba ile ile ya watekaji, “haooo wanapiga tena” alisema Mahamud kwa sauti iliyojawa na mashaka, huku anaipokea ile simu na kuiweka sikioni, “lakini nilisema mnipe muda wa kukusanya fedha sasa mbona…” alisema Mahamud kwa sauti iliyojaa wasi wasi, “sikia we mzee, najua una mpango wa kuwaambia polisi, sasa ukifanya hivyo usilete fedha ila subiri taarifa ya polisi ya kuokotwa kwa mwili wa Soraya” iliskika sauti nzito ya kiume ambayo iliambatana na kilio cha mbali cha Soraya akilalamika “niacheni jamani niacheni” hapo mzee Mahamud aliingiwa na hofu kubwa zaidi, “tafadhari usimdhuru mwanangu, sijaenda polisi wala kutoa taarifa polisi, nampa Talib fedha anazileta sasa hiv…” aliongea Mahamud na kabla hajamaliza kuongea mara akasikia kishindo cha kama vile simu ikidondoka chini na hapo ikakatika, hizi ni million nane wacha nipige simu msamala stendi walete million mbili ili Talib aende haraka, wamesema watamuuwa mwanangu” alisema Mahamud huku ana bofya simu yake kupiga kwenye ofisi yake ya msamala stendi.******
Wakati huo huo mzee Mahadhi na mwanae Idd, walikuwa wameshakutana na wazee wabaraza, wanaingia kwenye gari yao kuanza safari ya kuelekea kwa bwana Mahamud, “kijana umechukuwa maamuzi mazuri sana kumchumbia Soraya binti Mahamud, ni mschana mzuri anajiheshimu na wala hajawahi kusika hata mara moja amefanya yale ya kipuuzi yakuchukiza” alisema mmoja wa wazee waliopanda gari la bwana Mahadhi na Idd alikuwepo ndani yake akicheka cheka kicheko cha ushindi, “tena ni heshima kubwa sana kwa Idd kumchumbia binti wa Mahamud, nimepata kesi nyingi sana za vijana walioshindwa kupata nafasi hiyo” alisema mwingine, manaa mule ndani ya gari walikuwa wanne, yaani Mahadhi wazee wengine wawili na kijana Idd, ambae kama sio karafuu alizotafuna, basi mule ndani ya gari dogo wote wangekuwa wameshalewa kwa harufu ya pombe, “ni kweli bwana ilisadikika kuwa mzee Mahamud ndie anae mshawishi mwanae awakatae vijana wa Kiswahili ikiwa ni sehemu ya ubaguzi wa rangi” alisema mzee yule wa kwanza, “lakini mbele ya mwenyekiti sidhani kama ataleta ujanja wake” alisema Mahadhi, ambae ndie alikuwa dereva wa gari hili ambalo lilikuwa ni la pili toka nyuma, katika magari matano waliyokuwa nayo katika msafara ule, mbona yeye mke wake ni mngoni, kwanini yeye amzuie mwanae” alisema Idd, ambae uongeaji wake na sauti yake kama wale wazee wange kuwa makini basi wange gundua kuwa Idd alikuwa amelewa, baada yake walicheka kwa kumuunga mkono, “wala usiwe na wasi wasi kijana, kwa mwenyekiti amekwama, namfahamu yule mzee kwa maneno yake ya busara na mitego” alisema mzee mwingine huku safari inaendelea pasipo kujua kuwa huko kwa mzee Mahamud mambo yalisha haribika.******
Tayari Laylah alishapata nafuu na maumivu kuisha kabisa, hivyo akaruhusiwa kuondoka pale hospital, nae akaona itakuwa vyema akielekea nyumbani kwa boss wake akawajulishe hali yake, kisha aende nyumbani akapumzike, Laylah akiwa njiani aliendelea kutafakari hili na lile juu ya sabuni aliyokula na kumvuruga tumbo, hakika licha ya kuwaza kwa muda mrefu lakini alikosa jibu.
Lakini Laylah alipofika nyumbani kwa mzee Mahamud au ikulu ya mwarabu kama wanavyo paita na kukuta kuna mambo mengi yanaendelea pale nyumbani, kwanza maandalizi kama ya sherehe ndogo, hivyo akamtafuta Subira mfanyakazi wa Soraya, yaani yaya, na kumuuliza, “ndugu yangu kuna makubwa yametokea leo, mwenzio leo yule kijana Idd anakuja kuleta barua ya posa, wakati huo huo Soraya mwenyewe ametekwa na majambazi” alisema Subira kwa sauti iliyojaa masikitiko, ujue Subira ndie yaya wa Soraya toka Soraya akiwa mtoto mdogo sana, “mh! mbona makubwa Soraya kutolewa barua na Idd, Soraya kutekwa na majambazi” alishangaa Laylah na hapo kwa haraka akaanza kuchezesha akili, “mh! nimetoka nyumbani nikiwa mzima kabisa, nikashikwa na tumbo la ghafla na kushindwa kumpeleka Soraya shambani, Soraya kutekwa nyara, mbona kama kuna mchezo umechezeka,” aliwaza Laylah, “kwani Soraya mwenyewe ana fahamu kama leo anatolewa barua?” aliuliza Laylah, “ajue wapi wenzio wanataka wamshtukize ili ashindwe kukataa” alisema Subira na kumfadhaisha Laylah, “ina maana boss ameshindwa kuelewa kuwa Idd ni kijana mbaya kwa Soraya” alisema Laylah, “lakini mimi nina mashaka na Soraya, unadhani amesha gundua na kujisingizia ametekwa?” aliuliza Subira kwa sauti ya chini, “eti eeh! hebu ngoja kwanza nijaribu kumpigia” alisema Laylah huku anatoa simu yake na wote waka sogea pembeni zaidi huku Laylah anabofya simu yake na kuipiga namba ya Soraya.******
Sio kwamba tumewasahau babu mabudi na mama Hilda, hapana wakati kule mambo yanaendela hebu twendeni shambani kwa Soraya ambako mambo yalikuwa hivi.
Mara baada ya wale wakulima wake kukimbia na kutokomea upande wa mtoni, baada ya kuwafanyia ujanja na kuwatoroka wale watu alio wahisi ni majambazi, ambao walijiondoa lile vumbi na kumsogelea yeye Soraya ambae alikuwa amekamatwa na mmoja wao, “oya jamani eeh, huyu mtoto mimi simuachi hivi hivi, lazima nitoe gundu la kumla mtoto wa kiarabu” alisema mmoja wao na Soraya kusikia hivyo hata mwili ulimsisimka, maana alianza kuvuta picha ya maumivu atakayo yapata huku akisikilizia jibu atakalopewa na wenzake, “weweeee unaongea sasa hivi wakati mwenzio Zido alishapanga toka nyumbani, yaani akimaliza tu na mimi naingia” alisema mwingine huku Soraya akishindwa kuwatambua kwa sura vijana hawa
ambao bado walikuwa wamejiziba sura yao, “msinifanye hivyo nitawapa hela muniachie” alisema Soraya kwa sauti ya kinyonge iliyoambatana na kilio, hawa jamaa vipi si waje basi tumalize kazi” alisema mmoja wao na wakati huo huo wakasikia ngurumo ya gari, wakageuka kutazama upande ule na wakaliona Toyota carina likiibuka toka upande wa daraja la mahilo, “haooo! wanakuja” alisema mmoja wao huku wanaendelea kulitazama lile gari dogo ambalo lilisimama upande ule wa barabara, na wakashuka jamaa wawili ambao pia walivaa sox kama za wenzao, ambao waliwasogelea mpaka pale walipo, na walipowafikia Zido ambae bado aliziba uso alimsogelea kabisa Soraya aliekuwa bado ameshikwa na yule jamaa, “safi sana, sasa tuwasiliane na baba yake” alisema Zido huku akimtazama Soraya kwa macho ya tamaa na uchu, kisha akatoa simu yake na kupiga kwa mzee Mahamud na ndipo simu ilipo pokelewa na mama Soraya, hata hivyo alipewa Mahamud mwenyewe na kisha Zido akatoa maelekezo, kuwa wakitaka amuachie Soraya apewe million kumi na fedha hizo apewe Talib asiongozanae na mtu yoyote, na wala taarifa isifike polisi, “kwasababu kufanya hivyo ni kumpoteza Soraya” alisema Zido kwa msisitizo huku Soraya mwenye akisikia kwa masikio yake.
Kama tulivyosoma kwenye kipande kilichopita nyumbani kwa Mahamud, ni kwamba wakati wakiwa wanasubiri mpangilio wa fedha, huku wanapanga kumuingilia kimwili Soraya, Zido akipanga kuwa wakwanza kisha Vitus halafu wale wengine wanne kila mmoja akitaka kufanya hivyo, hakika Soraya alikuwa katika mashaka makubwa sana, wasi wasi na machungu makubwa, Soraya alililia kwa sauti akiomba wasi mfanyie kile walichohitaji kukifanya kwenye mwili wake, lakini hawa jamaa hawakuonyesha dalili ya kumuelewa Soraya.
Lakini wakati wanataka kumpeleka kwenye kibanda kidogo kilichopo pale shambani kwa lengo la kumuingilia kimwili mschana huyu mrembo wa kupindukia, mschana ambae alikuwa ndoto ya kila kijana mwenye fedha mjini Songea, mara ukaingia ujumbe kwenye simu Zido, ambao aliufungua na kuanza kuusoma kwa sauti “oya sikia, “jamaa anasema mwarabu anataka kututumia polisi hivyo tumpigie simu kumtisha” alisema Zido na kuanza kupiga simu kwa mzee Mahamud.
Hapo ndipo Soraya alipoanza kugundua kuwa mpango wa kumteka umeanzia kwa mtu wa karibu wa familia yao, ambao moja kwa moja alihisi kuwa ni wafanyakazi wa pale nyumbani kwao, na wakati Zido anaongea na simu yeye wakaanza kumkokota kumpelaka kwenye kibanda huku anapiga kelele za kuomba msaada, lakini wakati huo huo akasikia kishindo cha “guh!” kilichotokea pale alipokuwepo Zido, wote wakageuka kutazama wakamuona Zido akiwa ameanguka chini huku simu yake ikiwa pembeni imeanguka, karibu yake amesimama kijana mmoja alievalia kaptura ya jinsi bila ya shati “kijana mpole” alinong’ona Soraya, ambae uso wake ulianza kuachama kwa tabasamu la matumaini na furaha, tabasamu ambalo lilipochanua usoni mwake lilianzia tumboni kifuani mpaka usoni kwake…… ITAENDELEA
mwanangu Higno kama ananawa hivi
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA THELATHINI NA TISA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA THELATHINI NA NANE: lakini wakati huo huo akasikia kishindo cha “guh!” kilichotokea pale alipokuwepo Zido, wote wakageuka kutazama, wakamuona Zido akiwa ameanguka chini huku simu yake ikiwa pembeni imeanguka, karibu yake amesimama kijana mmoja alievalia kaptura ya jinsi bila ya shati “kijana mpole” alinong’ona Soraya, ambae uso wake ulianza kuachama kwa tabasamu la matumaini na furaha, tabasamu ambalo lilipo chanua usoni mwake lilianzia tumboni kifuani mpaka usoni kwake ……ENDELEA……
Tabasamu lililo ashiria ushindi, japo kichwani mwake alikuwa anaona ni kama kimuujiza fulani kuibuka kwa mtu huyu katika hali kama hii, wakati Soraya ana waza hayo aliweza kushuhudia wale vijana watano walio kuwa wamesimama wana mshangaa mwenzao aliekuwa ana ongea na simu akiwa chini amejibwaga kama kifurushi, akamuona yule kijana mpole ambae siku tatu zilizopita ametoka kumsaidia kuchomoka kwenye mtego wa Idd akigeuka na kuwatazama wale wangine watano waliobakia, “we! fala umeingia kwenye anga zetu leo” aliongea mmoja kati ya wawili waliokuja na gari, yaani Vitus, na sauti hii ni kama Kijana mpole aliitambua na kumtazama mtu huyu ambae alikuwa karibu yake kidogo, wakati huo vijana wawili kati ya wale waliokuja na pikipiki walichomoka wangu wangu kumfuata kijana mpole, ambae hakuangaika kuwa kabili zaidi ya kuwakwepa pale walipo mvamia na kujikuta wakipitiliza na kwenda kusimama pembeni, “sikieni jamani, mi sipendi kuwaumiza, muacheni huyo mwanamke aondoke zake” aliongea Kijana mpole kwa sauti yake ya upole, ungesema anaongea na watoto wa chekechea au mpenzi, huku kijana huyu ambae mimi na wewe tuna mtambua kama kijana Higgno, mtoto wa mzee Frank, akiwatazama vijana wale kwa awamu, “anaongea nini huyo fala, hebu mfanyieni mjinga tu nina mfahamu huyo” alipiga kelele Vitusi na hapo kijana mmoja akachomoa kisu kirefu kidogo chenye makali ya kuonekana hata kwa macho.
Soraya akaingiwa na hofu kwa kujuwa kuwa leo kijana mpole asinge kuwa na ujanja wa kuwakabili wale jamaa, kwanza ukiachilia uwingi wao pia tayari mmoja alikuwa na kisu mkononi, hivyo akakodoa macho ya hofu kumtazama kijana mpole, ambae hakuonyesha hofu yoyote usoni kwake zaidi ya kuwatazama watu hawa kwa macho yake tulivu, “unasubiri nini wewe, mkalishe mjinga huyo” alisema Zido, ambae alikuwa anajizoa zoa pale chini, hapo ndio kama vile alimkumbusha kijana mpole yaani Higgno kuwa alikuwa karibu yake, maana alimshindilia teke la usoni na kumrudisha chini.
Naam! kwa kitendo kile ni kama Higgno aliwachokoza wale jamaa, maana kwanza kabisa akachomoka yule mwenye kisu mkononi, akamsogelea Higgno kwa kasi na kuchoma kisu mbele usawa wa tumbo, hapo Soraya akafumba macho kwani hakutaka kushuhudia mtu ampendae akichomwa na kisu, lakini kabla hata hajafumba macho yake, akamuona yule kijana ananesea pembeni kidogo na kuudaka mkono wa yule jamaa ulioshikilia kisu, kisha akaukita kwenye goti lake usawa wa kiwiko cha mkono ule (yaan higgon akaukita ule mkono ulioshika kisu kwenye goti lake), na hapo ikasikika guh!, huku mkono ukipindia upande wa pili kama muwa ulio kosa maji (bua) unaposhindwa kuvunjika vizuri, “mamaaaa!” alipiga kelele yule kijana huku akiachia kishu, wakati huo huo kumbe vitus alisharusha ngumi na kumtwanga Kijana mpole eneo la shavu, nayo ikaingia sawa sawa, cha kushukuru haikuwa na nguvu ya kumpeleka chini kijana mpole, kuona hivyo wale wengine watatu ukiacha mmoja aliemshika Soraya, wakamvamia Higgno huku tayari Vitus ambae alikuwa anajua kuwa Higgno ni mzembe wa siku zote kama walivyo mtandika kule pacha nne ya liza born kipindi wanasoma akarusha ngumi nyingine kwa Higgno, lakini ile Vitus anarusha nyingine akashtuka akidakwa mkono wake aliourusha ngumi na kuzibuliwa mawash kakato, ( kijapan, ikiwa na maana ya ngumi kofi la usawa wa juu) lililotuwa usawa wa uso wa Vitus, ambae bahati mbaya yake licha ya kuona nyota za kila rangi lakini hakuachiwa mkono, na hata mwenzie mmoja aliporuka juu akitanguliza teke la usawa wa kifua, Higgno alikwepa kidogo na kumvuta Vitus aliejaa kwenye targert ya mguu wa yule mwenzie na lile teke likatuwa kwake, ile wana jiuliza kilicho tokea mpaka kumpiga msaidizi wa bossi wao zido tayari Higgono alikuwa hewani amesha tawanya teke na ngumi zilizotuwa sambamba kwa vijana wawili, wakushoto akisukumiwa ngumi ya mkono wa kulia iliyotuwa shavuni na kumfanya ateme mchuzi mzito wa damu, sambamba na kitu kama punje ya hindi, huku wakushoto akiambulia teke zito la kifuani lililomsukuma na kwenda kumbamiza Zido aliekuwa anajiinua toka chini na kuwafanya wote wawili waende tena chini.
Hapo likaonekana tabasamu jipya usoni kwa Soraya ambae alikuwa ameshikwa na yule jamaa, huku wakina Vitus wakiugulia maumivu ndipo Soraya akapiga kelele, “njoo umpige na huyu alinipiga kofi” alisema Soraya ambae alisemelea lile kofi la mgongoni alilopigwa mwanzo kabisa, Higgno akageuka na kumtazama yule jamaa aliemshika Soraya, ambae aliona kuwa sasa ni zamu yake, hivyo haraka sana akamuachia Soraya na kuchomoa kisu kama kile cha yule mwingine alievunjwa mkono, kisha akaanza kumfuata Higgno na wakati huo wale wengine pia walikuwa wanainuka na kuanza kutafua silaha za jadi, nazo ni vigongo vya miti, Higgno akatulia na kuwatazama kwa awamu, kabla haja mtazama Soraya, “ondoka haraka” alisema Higgno, lakini Soraya ni kama akusikia kauri ile, maana alionekana kutulia.
Fumba na kufumbua, Soraya ambae leo hakutaka kuondoka mpaka akutane na kijana mpole aongee nae, aliwaona wale vijana wote wa tano, kasoro yule alievunjwa mkono wakimvamia Higgno kwa pamoja na kuanza kumshambulia kwa kutumia yale mapande ya miti waliyo iokota, tunaweza kuita virungu, huku Higgno akijitahidi kuwa kwepa na umakini wake mkubwa ulikuwa kwenye kisu, japo moja moja ilikuwa inamkuta na kujitahidi kuzuwia kwa bloack za mikono, huku Soraya akianza kuingiwa wasi wasi kwa kuona Kijana mpole sasa amepatikana, “ondoka wewe mwanamkeee” Soraya alisikia sauti ya kijana mpole ikimshauri akimbie na hapo akaona ni kweli kuna umuhimu wa kukimbia, japo alitamani kukaa mpaka mwisho ili aonane na kijana huyu ambae ni kama moja ya malengo yake katika maisha, hivyo kwa roho shingo upande Soraya akaanza kukimbia kuelekea kwenye gari lake, lakini kabla hajafika mbali Zido akamuona, “oya mzuie huyu demu” alisema Zido, huku akimtazama yule alievunjwa mkono, ambae alianza kujikongoja kumfuata Soraya huku ameupakatia mkono wake ulio degejuliwa (ulio vunjwa) Soraya nae aliongeza mwendo, huku wale wengine pia wakiangalia kule ambako mwenzao alikuwa ana kimbilia.
Naam hapo ndipo Higgno alipo pata nafasi na kumkamata mmoja wao alieshika gongo na kumtwisha ngumi nzito ya usoni, ambayo ni kama ilimpa wenge, ile wengine wanashtuka tayari Higgno alikuwa anachukuwa lile gongo mkononi kwa yule aliemtandika ngumi na kulivurumisha kichwani kwa yule mwenye kisu, ambae alikuwa ana mpunguzia kasi na uwezo wa kupambana kutokana na muda wote kuwa makini kukwepa kisu kile.
Ni kweli bwana lengo likatimia, mwenye kisu alipigwa rungu la kichwa usawa wa sikio na kuonekana akizunguka mara kadhaa kisha akaanguka chini akitanguliza kichwa na kuacha makalio juu kama mlevi wa pombe moja ya mikoa ya tabora na Rukwa yaani Kimpumu, kisu kikiwa kimeshamtoka kitambo, wakati wenzake wanalishangaa hilo, Higgno akamtazama yule aliekuwa anamkimbiza Soraya, ambae sasa alikuwa anakaribia kumkamata huku Soraya akionekana kukata tamaa, Higgno akarusha lile pande la mti na kuelekea kwa yule jamaa ambae hakutarajia jambo hilo na kujikuta akitandikwa miguuni na kujibwaga chini na kutanguliza mkono ule ule ulioteguliwa mwanzo, hapo Soraya akaona kuwa kweli alikuwa na umuhimu wa kukimbia, maana kuendelea kuwepo kwake pale ni kuzidi kumpa majukumu mazito kijana yule ambae alikuwa na kazi ya kupambana na watu sita, hivyo alikimbilia kwenye gari lake akaingia na kuondoka zake kwa speed kali huku akimuachia msala kijana wake mpole.
Na baada ya kutembea na gari lake kwa mwendo wa mita kama mia nane au mia tisa hivi na kuanza kijiji cha Mahilo, Soraya ambae hakuamini jinsi alivyo pona pona toka kwenye mikono ya wale vijana sita ambao walitaka kumuingilia kimwili huku wakidai fedha kwa baba yake, aliendesha gari kwa speed akiingia kijiji cha mahilo huku kichwani mwake akiwaza juu ya kijana mpole aliemuacha kule shambani anapambana na wale jamaa sita, “mungu wangu msaidie kaka wa watu atoke salama” alisema Soraya ambae kama unge uona uso wake basi unge tambua kuwa alikuwa katika hofu na mashaka makubwa.
Na wakati anaendelea na safari yake mara akasikia simu yake ambayo ilikuwa kwenye dash board inaita, hapo akakumbuka kuwa kulikuwa na umuhimu wa kuongea na nyumbani kwao kuwajulisha kuwa alikuwa amesha toka mikononi mwa majambazi na kwamba wasitishe mpango wa kutoa fedha kwa watu hapo ambao waliagiza kuwa fedha hizo apewe Talib ili awapelekee sehemu watakayo elekeza, Soraya akapunguza mwendo na kuchukua simu yake, hakuwa na haja ya kutazama ni nani alikuwa anampigia, kwasababu namba ya simu yake walikuwa nayo watu wachache ukiachilia Idd alieipata siku za hivi karibuni, basi ni wazazi wake na dereva wake Laylah, Talib, na wafanyakazi wa nyumbani kwao, na marafiki wachache wa kike ambao wengi walishaga ondoka pale mkoani, “hallow nimesha toka yule kijana wanamshambulia sijui kama atatoka salama” aliongea Soraya kwa sauti ya kuchanganyikiwa pasipo kujua alikuwa anaongea na nani, “we da’Soraya ni kweli ulitekwa?” ilikuwa ni sauti ya Laylah alieuliza kwa mshangao, “ndio Laylah, nimeokolewa na yule mkaka sijui kama atakuwa salama wana mshambulia wapo wengi” alisema Soraya na kukata simu ni kama aliona inamchelewesha, “bora nikamuambie baba awaambie polisi waende kuwashika wale majambazi kabla hawaja muua yule kijana wangu” alijisemea Soraya akiongeza mwendo wa gari lake.******
Huwezi amini, Hilda alikuwa nyumbani kwao amejifungia chumbani kwake kukwepa vurugu za mwanae mdogo, ambae alikuwa anadai apelekwe kwa baba akampatie tena pipi, yaani kwa bwana Higgno, Hilda alikuwa anawaza na kuwazua jinsi mambo yalivyo kuwa ile siku kwa babu Mabudi, “mh! mbona sikuile nilishikwa na hamu ya ghafla sana” aliwaza Hilda, ambae hakuhitaji kukumbuka kama alipewa dawa yoyote au maelezo ya kuhusu dawa ambayo ingemfanya Higgno ampende, “halafu kumbe hata vibabu vina wezankuliko hata Talib” aliwaza Hilda ambae leo hakuwa ana hata shilingi ya kuanzia kwenye kilabu cha pombe ya ulanzi, au siku ile alibahatika tu!, ngoja nitaenda tena ili nione kama siku ile alibahatisha au kweli anaweza” aliwaza Hilda, ambae pia baada ya kuwaza sana akajikuta anaenda mbali zaidi, “mh! halafu mbona leo amemuambia mama aende peke yake au na yeye anataka akamfanye?” alijiwazia Hilda, huku kidalili cha wivu kikimjia, “lakini hata kama si kila mmoja kwa muda wake” alijisema Hilda ambae hakutaka kukumbuka kuwa lengo la kwenda kule kwa babu kwa mara ya kwanza ilikuwa ni kwenda kumloga Higgno ampende yeye na pili ni kuwaloga wazazi wa Higgno wafilisike, “we muache leo afaidi mpaka hamu yake iishe lakini mimi zamu yangu kesho” alijisemea Hilda, ambae ni kama alihisi kidudu fulani kinatekenya kwenye kitumbua chake hasa sehemu za kikundeni, “mh! wacha nikatembee kidogo na weza kupata hata robo ya ulanzi” alijisemea Hilda huku anainuka toka kitandani na kuanza kuvaa tayari kuelekea kwenye vilabu vya pombe za kienyeji, akijuwa kuwa endapo atavuka vilabu viwili vitatu basi lazima atakuwa amepata mtu wakumpatia angalau kopo moja la ulanzi, ambalo gharama yake yeye huiona ni ndogo sana, malipo yake hutoaga kitumbua ambacho ni moja ya bidhaa ambayo hakuipa thamani kama wanavyo fanya wengine wakina Soraya.*****
Yap, msafara wa magari matano uliingia malangoni pa mzee Mahamud na kupokelewa na watu maalumu ambao waliandaliwa kwaajili ya mapokezi na kuwaelekeza ndani, huku wakishangaa kuona kama shamrashamra zimepungua na walipoingia ndani waliwakuta wale wageni wengine wa upande wa ndugu wa Mahamud ambao walikuwa wamekaa wanapata shurubati na kababu, ikiwa ni kizugio cha kusubiria muda wa chakula na maongezi, lakini hawa kumuona mzee Mahamud mwenyewe, hawa kuwa na wasi wasi kuhusu Soraya, keasababu ni lazima mschana anaechumbiwa, afichwe na kuibuliwa baadae wakati maakuli, ambapo angekaa akimuandalia mchumba wake na kula nae pamoja, sehemu maalumu waliyotengewabkwaajili ya chakula.
Hapo mtu mmoja akainuka kuelekea ofisini kwa mzee Mahamud kupeleka ujumbe wa ugeni uliofika pale nyumbani, wakiwaacha wageni wanasalimiana na wenyeji walio wakutabna kisha kukaa kwa sehemu zao, nao wakiletewa shurubati (juice) ya matunda na kababu au vileja, na wakati wanaanza kula na kunywa wakisubiri aitwe mwenyeji wao bwana Mahamud huku muda wote kijana Idd akitabasamu kwa kuona dalili za wazi kuwa lengo lake linakaribia kufanikiwa, maana kwa ugeni na maandalizi yale hata Soraya mwenyewe angeona aibu kukataa.
Haikuchukuwa muda akaja mmoja kati ya wale wazee walikuwepo kule ndani ya ofisi na bwana Mahamud, “assalaam alaykum” alisalimia yule mzee na wakina mzee Mahadhi na wezake, wakiongozwa na mwenye kiti wakaitikia kwa pamoja, “waalaykum salaam” lakini walipomtazama yule jamaa walimuona akiwa katika hali tofauti kidogo, kama uso wake ulitwaliwa na huzuni kidogo, “karibuni sana jamani, lakini samahani kidogo tutaomba uvumilivu wenu maana kuna tatizo lime jitokeza kidogo” alisema yule mzee kwa sauti tulivu iliyo onyesha kukata tamaa, hapo wageni wa awamu ya pili yaani wakina mzee Mahadhi wakaonekena wakinong’onezana jambo, huku Idd akitaka kulitoa neno zito, na mmoja wa wazee akamzuia, ni yule aliekuwa amekaa nae gari moja na kubashiri kuwa mzee Mahamud huwa ana sababisha mwanae asiolewe, lakini walishachelewa maana mzee Mahadhi alisha ongea, “lakini jamani hee!, swala hili lilikuwa la hiyari, kama kulikuwa na kipingamizi ni vyema mungetua…” aliongea bwana Mahadhi, lakini yule mzee akamdaka juu kwa juu, “mzee mbona sikuelewei, inamaana hili swala lililotokea hapa, unaliona ni la kawaida kuliko posa ya mwanao?” aliuliza yule mzee alietoka ofisini na hapo mwenyekiti akadakia, “samahani bwana, msamehe bure huyu mzee mwenzio ameghafirika kidogo, hebu tujuze kidogo kulikoni” alisema mwenyeti kwa sauti iliyojaa busara, “ni kwamba binti wa bwana Mahamud, yaani Soraya ametekwa akiwa shambani alikokuwa ameenda asubuhi ya leo” aliongea yule mzee na hapo akajikuta anasababisha sinto fahamu, ambayo ilipokelewa na kicheko cha dharau na ung’amuzi toka kwa mzee Mahadhi na wale wazee wengine wawili waliokuwa wanajadili pamoja ndani ya gari la bwana Mahadhi wakati wakiwa njiani wanakuja, “eti ametekwa, munaona jamani” alisema mzee Mahadhi…….. ITAENDELEA MUWE NA JION NJEMA
 
Back
Top Bottom