TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA THELATHINI NA SITA
MTUNZI
Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA THELATHINI NA TANO: Naam ulikuwa mchana ukawa usiku ikawa asubuhi hatimae siku ya jumapili siku ambayo kuna watu walikuwa wanaisubiri kwa hamu sana, sijakutaja msomaji, ila ni wakina Talib na wenzake ambao walipanga siku hiyo isipite bila kukamilisha mpango wao wa kumteka Soraya, wengine waliokuwa wanaitamani sana siku hii ifike ni Mahadhi na kijana wake Idd, ambao waliamini kuwa ungekuwa mwanzo wa mafanikio ya maisha ya Idd, babu Mabudi pia aliitamani siku hii kwa kuwa ni siku nzuri kwake, kwasababu alitarajia mgeni toka Luhila ambae ni mke wa bwana Komba yaani mama Hilda, wapo pia walio isubiri kwa hamu siku hii kwasababu zao binafsi... ENDELEA
Mida ya saa nne ndio mida ambayo pilika zilianza, ni baada ya Laylah kufika nyumbani kwa kina Soraya yaani nyumbani kwa mzee Mahamud, nyumba ambayo baadhi ya vijana na watu wazima walipenda kupaita ikulu ya mwarabu, akiwa amevalia maalumu kwa safari ya shamba, yaani suruali ya jinsi na tishet ndani ya gauni refu, bila kusahau ushungi kama wavaavyo wanawake wa kiislam, pia chini alivalia viatu vya ngozi vya kudumbukiza.
Naam ile anaingia tu kwenye lango la jumba hili la kifahari, akakutana na babu mlinzi ambae alimpa ujumbe “mjukuu naona ndio unaingia kwa safari ya shamba” aliongea yule babu huku anajichekesha chekesha, “ndiyo babu si unajua safari mapema” alisema Laylah, ambae nae sio wa polepole, kwa maana ya kuwa alikuwa ni mzuri wa sura na umbo, “basi Talib amesema kuwa ukija upitie pale kwake akakuagize huko huko shamba” alisema babu mlinzi, huku akiendelea kujichekesha chekesha, “ok! tena nilishasahau kabisa” alisema Laylah, huku anaenda kwenye nyumba kubwa na kutoa taarifa kuwa ameshafika, ili ujumbe umfikie Soraya halafu akatoka na kulekea kwenye nyumba ndogo inayokaliwa na Talib, kisha akagonga mlango kama mara tatu hivi, ndipo alipo jibiwa na sauti toka ndani, “karibu na wewe” ilikuwa ni sauti ya Talib sambamba na vishindo vya kitu kinachi kung’utwa mfano wa mtu anaefukuza hewa mbaya au vumbi, “kaka talib ni mimi Laylah” alisema Laylah na hapo akasikia vishindo vya mtu akija mlangoni, “hooo! Laylah karibu” alisikika Talib, huku mlango ukifunguliwa na Talib alievalia kijikaptura kifupi bila shati, akatokea pale mlangoni akiwa na glass yenye juice nzuri ya embe, akitanguliwa na harufu nzuri ya marashi ya udi, “asante kaka Talib, lakini mimi sikai sana nimekuja kuchukuwa hayo maagizo, maana muda sio mrefu tunaondoka kuelekea shambani” alisema Laylah huku macho yake yakiikodolea glass ya juice iliyopo mkononi mwa Talib, aliekuwa anaipeleka mdomoni na kuinywa funda moja kisha akatanua mdomo wake na kuruhusu hewa itoke na kumfanya Laylah kumeza mate kwa uchu, “hooo! kumbe ndio munaondoka sasa hivi?” aliuliza Talib akiwa katika hali fulani ya mshangao, lakini iliyochanganyika na furaha fulani, huku anamtazama Laylah na kumuona kama angeingia kwenye mtego wake, akamuona anameza mate ya pili kwa uchu, “ndio tunaondoka sio muda mrefu, si unajua saa saba inabidi tuwahi adhuhuri” alisema Laylah huku akiendelea kuikodolea macho ile Juice ya embe mkononi kwa Talib, “ok! Haina shida basi njoo upate juice kidogo wakati nacheki hela yenyewe” alisema Talib na hapo Laylah akatabasamia moyoni.
Laylah aliingia ndani kwa Talib ambako licha ya miaka mingi aliyofanya kazi hapa kwa mzee Mahamud hakuwahi kuingia, akakaa sebuleni kwenye moja kati ya makochi matatu mazuri, yaliyopo pale sebuleni, na haraka sana Talib aliingia chumbani ambako hakukaa sana akatoka na glass yenye juice kibao akaiweka mezani, “nisubiri kidogo nakuja sasa hivi” alisema Talib, kisha akaingia chumbani akimuacha Laylah pale sebuleni akiinua glass ya juice na kuiweka mdomoni, akipiga funda dogo kama vile anaionja, alisikilizia ladha yake na kujikuta anatabasamu kwa utamu wa juice ile, huku anaisogeza tena mdomoni na kugugumia mafunda matatu kwa mkupuo, kisha akaiweka mezani halafu akaanza kuangalia huku na huku kama vile anakagua mule ndani.*******
Mida hii huko Luhila nyumbani kwa mzee Komba, mama Hilda alikuwa anajiandaa kwa safari ya kwenda Kwendimba kwa mganga Mabudi, “tatizo la nyie wanawake bwana mambo yenu taratibu, hapo utajichelewesha mpaka ukute watu kibao” alisema mzee Komba aliekuwa amekaa kwenye kitanda anamtazama mke wake alikuwa anaendelea kujiandaa, “baba Hilda umeanza jamani, sasa ningeondoka bila kuosha vyombo kuchemsha hiyo mihogo halafu juzi hatukukuta hata watu” alisema mama Hilda yani mke wa mzee Komba, “kwahiyo unataka urudi saa mbili za usiku kama juzi?” aliuliza mzee Komba, “wala sifiki hata saa nane kabla sijarudi” alisema mama Hilda ambae sasa alikuwa ana malizia kuvaa na kuchukuwa upande wa kanga akautundika begani na kuvaa kandambili zake kisha akatoka nje, “jitahidi umsikilize vizuri mganga ili tusikosee mashariti” alisema mzee Komba ambae kama angejuwa kinachoenda kufanyika huko Ngwendemba hakika angemzuia mke wake asiende, “hilo tu wala usiwe na wasi wasi na hivi ninavyo taka kuona wale washenzi wa filisika” alisema mama Hilda, ambae alianza safari mara moja kuelekea huko Ngwendemba kwa mganga mabudi.*******
Mzee Mahadhi Salum akiwa nyumbani na mwanae mida hii alikuwa akiwasiliana na wazee ambao walitakiwa kwenda nae kwa mzee Mahamud kupeleka barua ya posa ya mschana mrembo Soraya, “sasa ngoja nimpigie mwenyekiti maana yule kama hatoenda basi inabidi tughairi, maana bila yule mambo yanaweza kuvurugika” alisema mzee Mahadhi mwenyewe huku anabofya bofya simu yake kutafuta namba ya mwenyekiti wa baraza la wazee, “ila yule mzee nimemkubali kwa jinsi alivyo badili matokeo” alisema Idd ambae huwezi amini kuwa mida hii alikuwa ana chupa kubwa ya pombe kali akijinywea taratibu, “we unadhani kwanini niling’ang’ania kupeleka kwenye baraza, nilijuwa akiwepo mwenyekiti lazima mwarabu aelewe somo” alisema Mzee Mahadhi huku anaibofya namba ya mwenyekiti, “nikifanikiwa lazima niwe namtoa sana yule mzee, maana….” alisema Idd na baba yake akamuonyesha ishara ya kumzuia asiendelee kuongea, “hallow, mwenyekiti assalamu Alaykum ” alisalimia mzee Mahadhi kwa sauti ya uchangamfu, waalaykum salaam, bwana Mahadhi lete habari” alisikika mwenyekiti ambae kiukweli ni mzee wa makamo, “habari kubwa hakuna ila nilikuwa na taka nikukumbushe kuhusu ile safari ya kwenda kwa bwana Mahamud” alisema mzee Mahadhi, “hoo! nakumbuka bwana Mahadhi si tumepanga kukutana baada ya adhuhuri ili tuelekee huko” alisema mwenyekiti, “si unajua tena mchecheto wa kijana wako kila saa ananisisitiza nikupigie simu” alisema Mahadhi akimtupia kesi mwanae Idd, “asiwe na shaka mke ameshampata” alisema Mwenyekiti na hapo wakaongea mawili matatu na kukata simu, kisha Mahadhi akamtazama kijana wake Idd, “sasa hiyo pombe usinywe sana kiasi cha kushtukiwa kuwa umelewa” alisema mzee Mahadhi huku uso wake ukiwa umetawaliwa na tabasamu la furaha za wazi kabisa, “kweli kabisa mzee, hii inatosha hapa nikuondoa harufu tu! ila kama mambo yakienda fresh nikirudi nitapiga mtungi kinyama” alisema Idd kwa sauti ya kupania, “sio yakienda fresh, we jiandae kwa kushangilia mwenyekiti hajawahi kuniangusha” alijinasib mzee Mahadhi ambae alionekana wazi kufurahia kwa tukio la wao kwenda kupeleka barua akiamini kuwa wakitumia mgongo wa dini lazima wangefanikiwa.******
Upande wa kijana Higgno, mida hii alikuwa anatoka kanisani huku njia nzima akiwaza kuhusu kupata kazi na mwanamke mzuri wa maisha yake, hiyo ni tabia yake mpya ambayo sasa imeonekana kumshika sana na kumletea hamu ya kuwa na mwanamke wake, “yaani nakuwa na demu wangu, sijui kama usiku tutapumzika” aliwaza Higgno akiwa njiani anarudi nyumbani, “angekuwaga Hilda lakini ndio hivyo tena, wamemchukuwa wenye fedha” alijiwazia Higgno huku anaendelea chanja mbuga kueleka nyumbani kwake, “wacha nikafue nguo zangu niziweke fresh kwaajili ya kesho” aliwaza Higgno, akimaanisha kuwa akafanyie usafi nguo za kuvaa kesho kule kwenye maombi ya kazi, akiwa na uhakika kuwa mzee Mahamud atampatia kazi endapo atamkumbuka, “akinisahau nitamkumbusha” alijiwazia Higgno, ambae aliendelea kuwaza akiwa njiani na hata baada ya kufika sehemu ambayo kwasasa ni kama nyumbani kwake, yaani kule shambani, aliendelea kuwaza.
Higno alibadili nguo zake na kuvaa nguo ambazo hutumia kwaajili ya kilimo na shughuri mbali mbali za shamba, kisha akachukuwa nguo chafu pamoja na zile ambazo alitakiwa kwenda kuzifua kwaajili ya kesho kisha akaziweka kwenye ndoo, akachukuwa sabuni yake na kuelekea sehemu ya kufulia ambako ni darajani, hakufuata barabara badala yake alifuata njia ya mkato ambayo huitumia mara zote anapoenda kuoga au kufua au kuchota maji ya kunywa au kupikia, pia njia hii ndio anayoitumia kwenda mtoni kutega samaki.
Dakika kumi zilitumika kwa Higgno kufika mtoni, ambako aliwakuta vijana wawili wakiwa wanamalizia kufua na kuoga, “oya dogo vipi?” ilikuwa ni kama salam toka kwa mmoja kati ya vijana wale, “safi blaza mambo vipi?” alijibu Higgno kwa salamu dhidi ya wale jamaa wawili waliomzidi umri, ambao alikuwa anawafahamu vizuri tu, ni jamaa ambao walikuwa wanafanya kazi kwenye shamba la tajiri fulani ambae yeye binafsi hakuwa anamjua, “fresh dogo, sisi ndio tunatimka” alisema mmoja kati ya wale jamaa wawili, “poa mimi ndio naingia, naona leo muliwahi sana” alisema Higgno ambae licha ya upole alionao lakini alikuwa anaongea na kila mmoja bila kubagua wala kiburi, na kama ungemtazama kwa haraka usingefikiria kuwa kijana huyu ana uwezo mkubwa wa kupigana, “tulikuja mapema kwasababu baadae tuna kazi” alifafanua mmoja wao huku wanaondoka zao na kumuacha Higgno anaanza kazi ya kufua nguo zake chache alizokuja nazo mtoni, huku akiendelea kuwaza juu ya mapenzi na maisha.*******
Laylah aliendelea kutazama mule ndani, mlimokuwa muna nukia harufu ya udi huku ana kunywa juice yake ambayo sasa ilishabakia robo kwenye glass yake, sasa basi wakati anandelea kutazama tazama akaona kuna kitu kama jivu karibu na miguu yake, na alipotazama vizuri lile jivu ni la nini ndipo alipoona kitu ambacho kilifanana na kipisi cha tumbaku, “kumbe kweli huyu bado anvuta…” alisema Laylah na kabla hajamaliza kuongea akahisi maumivu makali ya tumbo juu ya kitovu, akajaribu kuvumilia akajuwa ni maumivu ya kupita lakini haikuwa hivyo, ndio kwanza akaanza kuona maumivu hayo yana anza kushuka toka juu ya kitovu na kuhamia chini ya kitovu na kuzidi kushuka mpaka kiunoni yakielekea kwenye makalio, hapo hakuwa na muda wa kusubiri, “kaka Talib nakuja sasa hivi” alisema Laylah huku anainuka na kukimbilia nje, huku akiona dalili zote za kuweza kuchafua mazingira, hakujua kuwa mwenzie Talib alikuwa anamchungulia na kumsindikiza kwa macho na alipotoweka nje tu! Talib akatoa simu yake na kupiga sehemu na haikuchukuwa muda mrefu akaanza kuongea, ikionyesha kuwa imeshapokelewa, “oya! huyu demu tayari nimesha mkalisha, hao jamaa wawe tayari, Soraya akiondoka tu! nitakupigia ili waondoke haraka kuelekea kule shambani” alisema Talib kwa sauti ya chini huku akisogea mlangoni na kuchungulia nje akimuona, Laylah jinsi anavyo kimbia huku amejishika tumbo na makalio, “poa usiwe na wasi wasi, wote wanne wameshakuja na pikipiki mbili, mimi na Vitus tutakuwa na gari tuna wasikilizia wakisha mkamata tu! sisi tunaenda kumchukua” alisema mtu wa upande wa pili ambae ni Zido.******
Yap! sasa twendeni, Ngwendimba, eneo hili la mashambani tunaelekea kwenye eneo la babu mabudi, mzee ambae kiukweli licha ya kuwa ni mganga aliepewa sifa nyingi sana za kuwasaidia watu wenye imani hiyo, lakini pia mganga huyu ana sifa mbili za kipekee, moja huwa hakubali kumzuru mtu kwa uonevu, hiyo ni sifa njema, lakini pia babu huyu alikuwa na sifa nyingine ya kupenda ngono, hasa kwa wateja ambao aliwaona wana akili za kujinga kama vile mama Tatu, mke mdogo wa bwana Kazembe, (
tafuta simulizi yetu ya MWALIMU NAE ANATAKA).
Hivyo basi baada ya kumpata Hilda siku ile ya ijumaa na kula kitumbua chake na kuweka mtego kwa mama Hilda, basi siku ya leo babu Mabudi toka asubuhi alikuwa anajiandaa kwa mchezo, ambao aliupanga uwe wakutwa nzima, maana kikawaida siku ya jumapili ilikuwa ni siku yake ya kupumzika ndio maana akamueleza mama huyu aje siku hiyo.
Ukiachilia maandalizi ya kutafuna tuvijiti twake, tunatojulikana kwa jina la Lunjumbwi, ambavyo aliamini kuwa vina muongezea uwezo wa kudumu kwenye mchezo kwa muda mrefu na kurudia mara kadhaa bila kuchoka, pia alikuwa ameandaa chakula cha kutosha ikiwa ni kande za kunde na dawa ya kumshawishi mama yule kuingia kwenye mchezo na kudumu kwa muda mrefu, akitamani kila mara dudu iwe ndani ya kitumbua chake ikiwa ni dose kubwa kuliko ile aliyompati mwanae Hilda.
Sasa mzee Mabudi alikuwa amekaa nje ya kibanda chake, pembeni ya jiko lake lililobeba sufuria kubwa la kande lililokuwa linachemka, na yeye kuchochea vijikuni ili kande zizidi kuiva na kuwa laini sana, kutokana na uhaba wa meno mdomoni mwake, yeye mwenye akiwa amevalia kile kijipande cha nguo ambacho kilikuwa kimeelemewa na dudu, ambayo ilikuwa imeshaanza kuleta fujo kwa kusimama muda wote ikitamani kitumbua ambacho kilikuwa kinatarajiwa kufika muda wowote, “akija tu! cha kwanza naingia nae ndani” aliwaza babu mabudi ambae sasa alikuwa anahisi kama vile amebanwa na mkojo kwa jinsi ngale zilivyo mshika.
Naam akiwa anawaza hayo kwa mbali akaanza kumuona mama Hilda yaani mke wa mzee Komba anakuja, hapo mzee huyu mweye akiba ya meno machache mdomoni mwake akatabasamu na kusababisha vijimate vimdondoke mdomoni mwake akishindwa kuvizuwia kutokana na mapengo yaliyo tawala mdomoni mwake.*******
Tatizo la ghafla la kuumwa tumbo la kuhara la Laylah liliwashtua wazazi wa Soraya, yaani bwana Mahamud na mke wake ambao sio tu kwa uendeshaji wa binti yule ambae pia wamefanya nae kazi kwa muda mrefu, ambae alikuwa anarudi chooni kila mara na huko angekaa dakika kumi na tano mpaka ishirini, pia walishtuka kwasababu waliona wazi tumbo la Laylah linge vuruga mpango wa kupokea wageni, maana endapo Soraya angegundua mapema kwa kuona maandalizi lazima angehoji na wao wangelazimika kumueleza ukweli, hapo ndipo mtafaruku ungeanzia, “mama Soraya hebu fanya ujanja wowote Soraya aondoke, bora akirudi akute kuna wageni na sisi tutamuambia walitoa taarifa baada ya yeye kuondoka” alisema mzee Mahamud akiwa chumbani na mke wake,
Mama Soraya hakuwa mbishi, alitoka chumbani nakumfuata mwanae aliekuwa nje amesimama pembeni ya gari lake huku ameshajiandaa kwa safari ya shamba, nae alivaa gauni refu jeusi lililoficha suruali nyepesi ya kitambaa na kitambaa kikubwa kichwani mwake, yaani hijab nayo nyeusi, “Soraya vipi bado, Laylah yupo chooni?” aliuliza mama Soraya, ndio bado yupo chooni yaani sijui amekula nini huko kwao” alijibu Soraya kwa sauti ya kinyoge kweli kweli, “sasa kwanini usimpleke mwenzio hospital na wewe ukaelekea shambani, maana usipoipanda hii miti leo inaweza kuharibika” alishauri mama Soraya, “basi ngoja nimsubiri atoke chooni” alisema Soraya huku akitazama muda kwenye simu yake.*****
Mama Hilda alipokelewa vizuri na babu Mabudi, “karibu mwanangu, karibu sana, tena umekuja mapema itakuwa vizuri sana” alisema Babu Mabudi, huku akimuonyeshea mama Hilda aingie ndani, “asante babu, si unajua mambo mapema” alijibu mama Hilda, huku anaingia ndani pasipo kujuwa ameandaliwa nini siku ile, na baada ya kuingia ndani babu nae akafuatia nyuma yake huku anamtathmini kwa kumtazama maeneo ya mgongo mpaka makalio, mpaka mama huyu alipokaa kwenye kipande cha ngozi, nadhani ndicho ambacho hutumika pia kama kitanda cha mzee mabudi, maana hakukuwa na kitanda wala godoro mule ndani ya kibanda cha udongo cha babu Mabudi, “haya! mwanangu habari za huko nyumbani?” alisalimia mzee Mabudi huku anakaa kwenye kigoda pembeni ya kile kipande cha ngozi, na kufanya kile kijinguo alicho jifunga kishindwe kuhifadhi dudu ambayo kiukweli ilikuwa inaleta vurugu kwa kusimama hovyo hovyo na kuyafanya macho ya mama Hilda yapate nafasi ya kuiona dudu ya mzee huyu iliyo kuwa imeinuka na kuacha kengere zina ning’inia, “nyumbani salama, nimekuja kama ulivyo sema” alisema mama Hilda, huku macho yake ya wizi, yakiitazama dudu ya babu huyu, ambae kwa haraka haraka hata yeye alifaa kuwa babu yake, “sawa kabisa, ni vyema umekuja mapema” alisema Mabudi huku anainuka na kuelekea kwenye kona ya chumba kile na kufunua mtungi ambao ulikuwepo eneo lile na kutoa vyupa viwili, akakichagua kimoja akafungua na kuyanywa maji yalipo ndani ya chupa kile na kukirudisha mtungini, kisha akachukua chupa cha pili na kurudi nacho pale alipokuwepo mama Hilda, “haya mwanangu hebu kunywa maji haya mara mbili” alisema mzee Mabudi, huku anampatia maam Hilda ile chupa ya maji, nae akaifungua na kunywa mafunda mawili kama alivyoambiwa, kisha akamtazama babu mabudi ambae sasa alikuwa anaelekea kwenye mti wa katikati na kufungua mkoba fulani uliotundikwa kwenye nguzo ile, “tayari babu” alisema mama Hilda ambae alishangazwa na utamu wa dawa ile, ambayo pia licha ya utamu wake ulimfanya hata midomo yake ijisikie vizuri sana, “ongeza tena mafunda miwili” alisema babu Mabudi, ambae kimoyo moyo alijisema, “shauri yako, tembo mwenyewe huwa anapga magoti hapo” aliwaza huku anamtazama mama Hilda kwa jicho la pembeni na kumuona akinywa ile dawa safari hii akiongeza mara mbili zaidi, nadhani kutokana na utamu wake, babu akatabasamu, “tayari babu niongeze nyingine” aliuliza mama Hilda, “hapana utaongeza baadae” alijibu babu Mabudi kwasababu alikuwa anajuwa tabia ya juice ile ya matunda ya mbura, ambayo mama Hilda alidhania kuwa ni dawa, ni matunda ambayo hupatikana kwa wingi kusini mwa afrika, kuanzia ukanda wa mkoa wa ruvuma kwenye mbuga ya Selous, hupendwa sana na wanyama kama tembo nyati na faru, ni tunda ambalo huwa ongezea wanyama hao hasa wakike hamu ya kuhitaji dudu, hasa kipindi chao cha kupandwa na joto, “kwani hauna nyingne ya baadae babu?” aliuliza mama Hilda, huku anavizia nafasi ya kunywa tena, “hiyo haitakiwi kuzidisha” alisema babu Mabudi huku anapekuwa mkoba wake alio utundika na kuibuka na kijifuko cha ngozi, yaani kile cha juzi chenye dawa nyeusi, huku mama Hilda akitumia nafasi hiyo kunywa ile juice ambayo yeye aliichukulia kuwa ni dawa tamu, safari hii akigugumia kwa nguvu sana, hata babu alipogeuka yeye tayari alishaiweka chini na kujikausha, “haya mama tulia hapo dawa ifanye kazi” alisema babu Mabudi huku anaweka kile kijifuko cha ngozi kwenye kipande cha ngozi alicho kuwa amekalia mama Hilda na kutoka nje akimiacha mama Hilda akiwa amekaa pale ndani akilitazama kopo la dawa na kutabasamu kama vile fisi ameona mfupa, kisha akamtazama babu mabudi aliekuwa anapotelea nje ya banda lake, na ile kupotea tu likawa kosa, mama Hilda akakamata ile chupa na kuipeleka mdomoni, mpaka anaishusha tayari lilikuwa limesha kwisha.*****
Huku nyumbani kwa bwana Mahamud mara baada ya Soraya kuondoka na Laylah, yeye akiwa anaendesha gari haraka sana pilika za maandalizi ya wageni zikaanza, hasa kwa maandalizi ya chakula na vinywaji, maana ukiachilia ugeni wa heshima wa viongozi wa baraza la wazee wa mkoa, pia tukio lililokuwa linafuatia la kuleta barua ya posa lilikuwa ni tukio muhimu sana kwao, maana aliekuwa analetewa barua ni binti yao wapekee.
Wakati nyumba kubwa yanaendelea hayo, huku nako Talib alishapiga simu kwa kina Vitus kuwa tayari Soraya amesha toka anaelekea Hospital na akitoka hapo ataenda shambani yeye peke yake, “sasa fanyeni faster muwahi kule shamba” alisisitiza Talib,ambae alikuwa ana uona utajiri ukimjia kwa kasi, wakati akifanya mawasiliano ndipo akasikia mlango unagongwa, akakata simu na kwenda kufungua mlango na mgongaji wa mlango hakuwa mwingine ila alikuwa ni mlinzi, “unaitwa na mzee kuna mbuzi wawili wanatakiwa kuchinjwa na kutengenezwa” alisema mlinzi na hapo Talib akaenda kujiandaa kwaajili ya kazi hiyo, “kuna nini leo mpaka wanachinja mbuzi wawili?” alijiuliza Talib, ambae hakuwa anajua taarifa ya binamu yake Soraya kuletewa barua.*****
Kijana Higgno Frank, au kijana mpole mwenye mdomo mzito katika kutongoza wanawake, hakutumia muda mrefu sana kufua nguo zake chache alizoenda nazo mtoni, alimaliza kufua kisha akaoga huku anawaza vitu vyake vya ajabu, akivuta picha kuwa yupo na mwanamke mzuri sana kwenye maji yale ya mtoni anaogelea nae, huku wana rushiana maji kwa michezo ya kimapenzi kama ya kwenye video, hata alipomaliza kuoga na kujikuta yupo peke yake aliongeza ndoto ya kijinga kwa kuvuta picha yupo na mschana wake mzuri kweli kweli, wanatoka kule mtoni na kueleka nyumbani, huku yeye amemsaidia mpenzi wake kubeba maji kichwani, huku mpenzi wake akiwa amebeba nguo walizozifua, nasema ya kipumbavu kwasababu vitu hivyo vyote alikuwa amebeba yeye mwenye, akiwa mkono wa kushoto ameshika ndoo na mkono wa kulia ameshika kijifurishi kidogo cha nguo kama saba hivi.
Higgno safari hii aliona haitakuwa vyema akipita barabarani, maana kule vichakani nyasi zina muwasha sana kutokana na kuwa tayari ameshaoga, na huo ndio ulikuwa utaratibu wake wa siku zote, lakini leo aliongeza na katabia kakujivutia taswira ya kwamba yupo na mwanamke mmoja mzuri sana, “tena amevalia nguo nzuri nilizo mnunulia dar” aliwaza Higgno, ambae katika mawazo yake ni kwamba wakati anatembea na barabarani na huyo mpenzi wake, watu waliokuwa wanapita njiani walikuwa wanawashangaa na kuwatazama kwa matamanio.
Hakika mawazo ya kijana huyu yalitaka kumpelekea kuwa chizi, maana hata wakati alitengeneza taswira ya kuwa magari yanakuja na kuwapita huku madereva au abiria wa magari hayo wakiwashangaa yeye na mpenzi wake, na hata aliposikia ngurumo ya gari la kweli likija yeye akaivutia taswira ya dunia yake ya kufikirika.*******
Dakika kumi zilikatika, mama Hilda akiwa ndani ya banda la babu Mabudi peke yake, akisubiri dawa ifanye kazi kama alivyo ambiwa, “kama Hilda nae alikunywa hii dawa siku ile mbona alifaidi sana” aliwaza mama Hilda akitamani dawa itakayo fuata iwe kama ile, aliwaza mama Hilda ambae ni kama alianza kuona hali fulani isio ya kawaida kwenye mwili wake hasa kuanzia kwenye kinena mpaka chini kwenye kitumbua, ni kama alihisi hali fulani ya kutekenya na msisimko wa ajabu kiasi kwamba hata nguo yake mwenyewe ilikuwa inamtekenya.
Naam kila dakika zilivyo zidi kusonga, ndivyo hali hiyo ilivyozidi sambamba na sehemu mbali mbali za mwili wake, kuanzia shingoni mpaka kwenye uti wa mgongo na kusambaa kwenye mbavu na kifuani kwake zikigota kwenye chuchu za maziwa yake makongwe, hakika mama Hilda alijikuta katika hali ya ajabu, hali ambayo ilimfanya amkumbuke mume wake aliemuacha nyumbani, “mh! mbona leo nanyegeka sana” aliwaza mama Hilda huku anapeleka mkono wake kwenye kifua chake na kulikama ziwa lake moja, kisha kuibinya chuchu yake mwenywe, lakini haikusaidia lolote, zaidi alijikuta anaongeza msisimko uliokimbilia kwenye kitumbua chake, “huwwwi mimi yoyoooo, leo mbona nimeshikwa namna hii” alijishangaa mama Hilda, huku anakaa vizuri na kuinua nguo yake upande wa chini kisha kuanza kupaa chupi yake juu ya kitumbua, akifanya kama anakipooza joto au kukifuta, “jamani, mbona naweza kubaka sasa” aliwaza mama Hilda ambae aliona kukipapasa kitumbua kilichokuwepo ndani ya nguo yake ilikuwa ni kazi bure, hivyo akapekenyuwa chupi yake na kukiweka kitumbua wazi kabisa na kuanza kujichezea kunde huku anaanza kuvuta picha ya dudu ya babu aliyoiona muda mfupi uliopita, “babuuu tayari dawa imefanya kazi” alipiga kelele mama Hilda, ambae sasa alianza kuona hata koo lake mwenye linakauka kwa kutamani maji.
Mama Hilda hakusikia jibu lolote la babu Mabudi zaidi, alimuona anaingia ndani tena hakushtuka kumuona akiwa katika hali ile ya kujipapasa kitumbuani, zaidi alimuona akitabasamu na hapo ndipo mama Hilda alipogundua kuwa leo hakuitiwa dawa ila aliitiwa dudu, “haya mwanangu kaa vizuri tukamilishe dawa, alisema babu Mabudi, huku anafungua kile kijipande cha nguo iliyofubaa kwa uchafu na kukitupa chini akibakia uchi wa mnyama na dudu ikiwa imesimama utadhania kijana anae barehe leo, kuona hivyo mama Hilda hakusubiri kuambiwa mara ya pili, akalala chali na kuipandisha zaidi ile nguo yake huku akiipekenyuwa zaidi chupi yake na kutanua miguu, “kamilisha babu, kamilisha dawa babu, kamilisha unavyo weza, leo mimi ni wa kwako babu, nifanye unavyo taka” alisema mama Hilda akijikabidhi kwa babu, ambae alishuka juu yake na kujipachika kati kati ya mapaja ya mama huyu huku dudu kichwa wazi, ikitangulia na kuingia kwenye shimo lake.*****
Baada ya kumuacha Hosptali binafsi dereva wake Laylah akipatiwa vipimo, Soraya aliondoka mwenyewe kueleka mashariki mwa mji wa songea, huku njiani akiamisha mawazo toka kwa mgonjwa wake na kuyapeleka kwenye maisha yake binafsi, hasa akiwaza juu ya kunusurika kuingiliwa mara mbili bila ridhaa yake, yaani kubakwa, na sababu ya kunusurika ni kuokolewa na mtu huyo huyo mmoja, aliwaza juu ya uchungu ambao angeupata kwa kuondokewa na uschana wake kwa kubakwa, tena katika nyakati ngumu kama ile ya kwanza ya kubakwa na vijana wanne na hii ya kuleweshwa, “lakini kijana mpole akanisaidia” aliwaza Soraya huku anaendesha gari kwa mwendowa kasi, kwasababu alikuwa ameshachelewa kutokana na kutumia muda mwingi kumsubiri Laylah na kumpeleka hospital.
Soraya alikanyaga pedor ya mafuta ya hili Land Rover Discover TDI nalo likakanyagika na kuvuta mwendo, “hivi kwanini yule kijana siku ile alikataa kuja nyumbani?” alijiuliza Soraya, huku analipita gari moja dogo aina ya Toyota carina, lilikuwa lina tembea taratibu nyuma ya pikipiki mbili zilizo beba abiria wa kiume mmoja mmoja kila moja, “hawezi kuwa hanipendi, mbona wanaume wengi wananipenda au ananiogopa” aliwaza Soraya, kisha akajicheka kidogo, huku anapunguza mwendo kukata kona ya mwisho ya chem chem, mita chache toka shule ya msingi chem chem iliyopo mwishoni kabisa mwa kijiji hiki cha Chemchem na kuingia kwenye njia inayopita pembezoni mwa milima ya matogoro na kufanya zile pikipiki zimsogelee na gari likibakia nyuma likija taratibu, “aniogope mi nani, nikimuona nitamng’ang’ania” aliwaza Soraya, huku anaongeza mwendo na kutimua vumbi kiasi cha kuto kuziona zile pikipiki nyuma yake kwa uwingi wa vumbi.
Soraya alikanyaga mafuta kwa nguvu kiasi cha kuanza kujiogopa, hasa alipoiacha ile safu ya milima na kuingia usawa wa mashamba ya Mahilo na kuukamata mteremko wa kuelekea daraja la mto Mahilo, “ hivi hapa akitokea mtu au mnyama wa porini si namgonga jamani….” hakumaliza hata kauli yake, macho yake yakaona kitu ambacho hakuamini kama ni kweli au ni wenge lake, alikuwa ni kijana alievalia kaptura ya jinsi iliyokatwa kwa kitu ambacho sio rasmi, juu hakuvaa shati lolote na kufanya kifua chake kipana kilicho jengeka kimazoezi kionekane vizuri kabisa machoni pake, hilo sio tatizo kwa Soraya, tatizo ni sura ya kijana huyu, “ni yeye” alipayuka Soraya,m huku akimpita kijana yule kwa speed ya ajabu kiasi cha mkufanya kijana yule aruke pembeni ya barabara na kumwaga maji aliyokuwa ameyabeba kwenye ndoo huku nguo zake nazo zikigala gala kwenye vumbi... ITAENDELEA USIKU