SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

SIMULIZI: Tembele la uwani (EDGAR MBOGO)

TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA THELATHINI NA TATU
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA THELATHINI NA MBILI: Wakati mzee Mahamud anatoka ndani ndio muda ambao alisikia simu yake inaita, alipotazama akaona kuwa mpigaji alikuwa ni bwana Mahadhi, kwanza akamtazama mke wake ambae alikuwa anaongozana nae kutoka nje, “Mahadhi huyo anapiga simu” alisema Mahamud kwa sauti ya kuhitaji ushauri, “pokea msikilize anataka kusema nini, mimi nilitaka tumfumanie huko huko msikitini” alisema mama Soraya, ambao sasa walikuwa wametokea nje na kuwakuta wakina Talib wakiwa wana subiria kuingia kwenye gari……… SONGA NAYO SASA
Mzee Mahamud akapokea simu ile na kuiweka sikioni, huku anasogea pembeni akipishana na Soraya aliekuwa anakuja toka ndani, akiwa amependeza kweli kweli kwa gauni lake refu la kijivu na shungi (kilemba) cheupe na niqab ya kijivu aliyoishia mikononi, viatu leo alivaa vya kudumbukiza vyeusi, lakini vya chini, “hallow assalam alaykum” alisalimia bwana Mahamud, kwa sauti nzito na tulivu, “waalaykum salaam bwana Mahamud, kwanza uniwie radhi mzee mwenzangu, maana muda unapiga simu nilikuwa nimeisahau nyumbani nahangaika mitaani kumtafuta Idd, maana alikumbwa na balaa kubwa” alisema bwana Mahadhi, huku akijichekesha chekesha, hapo Mahamud akakunja sura kwa mshangao, “balaa lipi bwana Mahadhi zaidi ya lile alilomsababishia binti yangu?” alisikika akiuliza bwana Mahamud kwa sauti ya ukali kiasi cha watu wote kugeuka kumtazama kwa mshangao, maana walizoea kumuona mzee huyu akiongea kwa sauti ya upole siku zote, “ukisema alimsababishia utakuwa umekosea mzee mwenzangu, kama mwanao alipata tatizo, basi hilo tatizo limewakuta wote wawili” alisema Mahadhi kwa sauti ya upole, lakini hakuacha kujichekesha kidogo, “ni matatizo gani aliyapata kijana wako bwana Mahadhi?” bado sauti ya Mahamud ilikuwa ni ile iliyojaa hasira, “kwa kweli ni hatari ndugu yangu, kijana wangu jana alishindwa hata kurudi nyumbani, aliokotwa asubuhi akiwa amelala kwenye gari hajitambui hata kidogo, anasema jana walienda sehemu kununua Juice ya mabungo kwaajili ya huyo mwenzie Soraya na yeye akanunua maji, kumbe walitegeshewa vilevi kwenye juice na maji, yeye akajikuta amelewa na kukimbilia kwenye gari, hakujuwa Soraya ameenda wapi, hivyo nikasema nikupigie simu ili nijuwe na yeye ilikuwaje?” aliuliza Mahadhi kwa sauti ya upole kama vile ana masikitiko fulani, hapo Mahamud alishusha pumzi kidogo kama ile pumzi ya kushusha hasira, “nadhani tukutane baada ya swala ili tuongee vizuri, lakini kwa kifupi na yeye aligundua kuwa juice alieyoletewa ilikuwa na kilevi” alisema Mahamud na wakakubaliana hivyo.
Naam Mahamud na familia yake iliingia kwenye gari ambalo lilikuwa linaendeshwa na Soraya, huku safari ikaanza kuelekea msikitini, wakiburudishwa na qaswida, huku Mahamud aliekaa mbele akimsimulia mke wake pamoja na mwanae Soraya aliokuwa nao kule mbele ya gari, kilicho tokea kwa Idd jana jioni, “lakini baba mbona ile harufu ya pombe ilikuwa ni kali sana, ina maana hakuisikia hata kidogo mpaka anywe na alewe?” alisema Soraya akipingana na utetezi wa bwana Mahadhi, yaani baba yake Idd, ok! wacha nikawasikilize kwanza” alisema Mahamud, ambae alionekana kuwa hasira zimesha muondoka, “lakini hata kama watasema nini ukaribu na mwanangu sihitaji tena”, alisisitiza mama Soraya.******
Kwa upande wa Higgno leo yeye ndie alieenda nyumbani kwao, maana toka jana hakuwahi kuonana na baba yake, ni baada ya kutembea kwenye mitego michache ya wanyama wa porini, akaona ni bora akienda kwanza kwa baba yake kisha akirudi aende kutazama mitego ya kanga kwale na samaki, Higgno alifika nyumbani kwao akiwa amebeba nyama ya wanyama kama Sungura na digi digi, ikiwa ni moja ya vitu ambavyo mzee Frank alijivunia kutokana na mwanae kukaa kule shambani, maana alisha sahau mambo ya kwenda buchani kununua nyama au utumbo, “mwanangu afadhali umekuja, maana umenipunguzia safari ya kuja huko” alisema bwana Frank mara baada ya kusalimiana na mwanae Higgno, “niliona kuna umuhimu wa kuja kuonana leo, kwasababu kesho nitakuwa na kazi ya kumalizia sehemu fulani pale shambani, jumapili nitakuwa nafua nguo kwa maandalizi ya kwenda kwenye kuomba kazi kule mjini” alisema Higgno, “basi umefanya vyema, ila kwa kifupi nadhani umejionea mwenyewe hali halisi kwa yaliyo tokea jana kule kwa shangazi yako?” alisema mzee Frank kwa mtindo wa kuuliza, na Higgno akaitikia kwa kichwa kukubali kuwa ameshuhudia mwenyewe, “sasa mimi nakuomba wewe jitahidi utafute mwanamke, ujue katika jamii yetu haipendezi kijana mkubwa kama wewe uonekane hauna mwanamke hata wakuongozana nae” aliongea mzee Frank kwa sauti ya chini na tulivu, huku Higgno akimsikiliza kwa umakini mkubwa, “kuna kitu hujui Higgno, unajua hawa wakina mama inafikia wakati wanapenda kuona au kusikia kesi ndogo ndogo toka kwa wenzao wakilalamika kuhusu mabinti zao” alisema bwana Frank na kuendelea kumsisitiza mwanae, “hivyo Higgno wewe tafuta mwanamke hata kama ukiona umependa mwanamke fulani na unashindwa la kufanya njoo uniambie” alisema mzee Frank, kwa sauti ya chini iliyojaa msisitizo, “lakini baba wanawake wanapenda hela mi naona nisubiri kwanza nipate kazi, nikiwa na hela nguo nzuri viatu vizuri lazima watanipenda wenyewe”alisema Higgno, akionekana kukatishwa tamaa na maisha ya wanawake aliowahi kuwaona kwa macho yake mfano Hilda.
Hapo baba yake Higgno alitabasamu kidogo, “Higgno kama ulikuwa hujui basi wacha nikueleze na unisikilize kwa umakini” alisema mzee Frank kwa sauti iliyojaa umakini mkubwa, Higgno nae akaongeaza umakini kumsikiliza baba yake, “najuwa kama asilimia kubwa ya wanawake hasa wale wenye maisha ya chini wanapenda kuishi au kuwa na mwanaume mwenye fedha na uwezo mkubwa ili watatue shida walizoshindwa kuzitatua, japo kuna wengine hupanda kuishi maisha ambayo wamekuwa wakiya shuhudia kwa wenzao” alisema baba Higgno ikiwa ni mwanzo wa maelezo yake, lakini pia wapo wanawake haijalishi ni kutoka kwenye familia za hali ya chini kama zetu au kutoka kwenye maisha bora wao hupenda mwanaume mwenye mapenzi ya kweli, japo asilimia kubwa ni huwa wale wenye maisha mazuri” alisema baba Higgno akimpa somo kijana wake aliekuwa anamsikiliza kwa umakini mkubwa, “cha kuzingatia kwanza usitumie kitu kumpata mwanamke, hilo litakusumbua sana maishani, hasa utakapo kosa kuwa na kitu, pili hakikisha unamuonyesha upendo mwanamke wako, mchukulie kama rafiki na mwenzako, sio adui au kijakazi wako pale nyumbani, ujuwe siku zote wanawake wanapenda sana kuonyeshwa upendo, kudekezwa kama wao wanavyo wadekeza watoto” alimaliza kueleza baba Higgno na hapo ni kama somo lilimuingia Higgno, “sasa baba nitaanzaje kumuonyesha mwanamke kuwa nampenda, si mpaka anipe nafasi ya kuwa karibu yake na mimi niweze kumuambia?” aliuliza Higgno na kumfanya baba yake acheke kidogo, tena kicheko cha huzuni, “ina maana huwezi kumueleza mwanamke unachotaka kwake?” aliuliza kwa mshangao mzee Frank, na Higgno akatulia kimya, “ok! kwanza kabisa lazima utambue kuwa penzi halijifichi, na huwa linakuja lenyewe, asilimia themanini na tano ya mwanamke unae mtongoza tayari anakuwa amesha kuandalia jibu kabla huja mueleza chochote, (sijui kama mzee Frank alikuwa sahihi) iwe mwenye mapenzi juu ya wewe ulivyo au mwenye mapenzi juu ya fedha au ulicho nacho, ukweli anakupenda au kukuchukia mara tu baada ya kukufahamu, cha msingi weka hisia zako wazi” alisema mzee Frank, na hapo Higgno akakubaliana nae kwa kutikisa kichwa juu chini, akionyesha ameleewa alichoambiwa.********
Wakati huo huku mjini, tayari ibada ilishamalizika kwenye msikiti wa mkoa wa Ruvuma, Mahamud akiwa nje ya msikiti anatazama kama angemuona bwana Mahadhi na kumkaba maswali juu ya kitendo cha jana, mara akamuona kijana mmoja ambae hujihusisha na kufundisha mafundisho ya dini kwa watoto wadogo na wakubwa wasio na ufahamu wa dini, yaani madrasa, akimjia na kumueleza kuwa anaitwa kwenye ofisi ya baraza la wazee pale pale msikitini, hapo Mahamud ambae hakutegemea kuwa atamkuta bwana Mahadhi akiwa na wazee wengi namna ile, maana licha ya kuwa pamoja na kijana wake Idd pia alikuwa pamoja na wazee wengine watano, akaingia ofisini na kukaa kitako kwenye mazuria mazuri ambayo baadhi yake alinunua yeye mwenyewe.
Naam baada ya kusalimiana maongezi yakaanza, na mwanzilishi alikuwa ni bwana Mahadhi, “samahani wazee wenzangu, kuna jambo ambalo limetokea jana jioni baina ya vijana wetu wawili, yaani kijana wangu Idd, na binti wa bwana Mahamud” hapo kila mmoja akaonekana kumtazama mwenzie, wakionyesha kuwa walijawa na maswali vichwani mwao juu ya jambo ambalo bwana Mahadhi alitaka kuwaeleza, jambo ambalo limemfanya awakusanye mahali hapa, “kifupi nimeona kuwa endapo nitaongea na bwana Mahamud tukiwa wawili peke yetu haita kuwa vyema, yaani pengine asingeweza kunielewa kutokana na mazingira ya tukio lenyewe ambalo naimani kwa upande wa mwenzangu hakukuwa na madhara makubwa kama ilivyokuwa kwangu” alieleza bwana Mahadhi, ambae alianza kwa kueleza kama alivyo mueleza bwana Mahamud kuwa kijana wake alitoka na Soraya kwenda sehemu aliyowatuma, lengo likiwa ni kuwa weka vijana hawa karibu ikibidi watengeneze urafiki ambao utawaweka kwenye ndoa, “lakini kwa bahati mbaya katika matembezi yao wakajikuta wameingia kwenye mitengo ya kuwekewa kilevi kwenye vinywaji vyao” alieleza bwana Mahadhi, ambae alidai kuwa pengine lengo la watu hao lilikuwa ni kuwaibia, “lakini bahati nzuri Soraya aliwahi kuondoka, naimani alifika salama nyumbani kama nilivyo muona leo amehudhuria ibada vizuri kabisa, na kijana wangu Idd aliwahi kujifungia kwenye gari ambapo aliokoa vitu vyao vyote ikiwa na bengi la Soraya, hivyo naomba ifahamike kuwa hawakuwa wametumia kilevi kwa makusudi, isipokuwa waliwekewa kilevi bila wao kujuwa” alimaliza bwana Mahadhi kueleza simulizi ambayo alikuwa ameibadilisha maudhui kidogo kwa lengo la kuficha uovu wa mwanae Idd, “mh! nadhani wote tumesikia jamani, kwa upande wangu naona ni kisa cha kusikitisha kwa kweli, pole kwa vijana wetu kwa mtihani uliowafika” alisema mmoja wa wazee ambae ndie mwenyekiti wa baraza lile kwa mkoa wa Ruvuma, huku wenzie wakimuunga mkono kwa kuonyesha masikitiko yao kwa kilicho watokea Idd na Soraya wakiamini kuwa waliwekewa vilevi kwaajili ya kuibiwa, “kijana hii songea ni mpya sio ile uliyoiacha miaka ile” alisema mmoja wa wazee wale akimtazama Idd, ambae muda wote alikuwa anakenua meno kwa tabasamu, “sijui bwana Mahamud kama umeelewa alichokueleza mzee mwenzio?” aliuliza yule mzee wa kwanza huku anamtazama bwana Mahamud, “kiukweli mimi bado nina utata na maelezo ya bwana Mahadhi, Soraya anasema baada ya kuanza kulewa huyu Idd aliondoka pale mezani, na yeye akaona bora anywe maji haraka ili aondoe ulevi ule aliowekewa kwenye juice na maji ya haraka yalikuwa ni yale aliyokuwa anakunywa Idd, lakini alipoyafungua na kuyasogeza mdomoni akagunduwa kuwa ni pombe tena ilikuwa na harufu mbaya, sasa Idd alishindwa vipi kujuwa kama wametegeshewa kilevi?” aliuliza bwana Mahmudu akionyesha kuwa hakuwa na imani na Idd, “lakini kama mwanao hakuweza kusikia harufu Idd angewezaje bwana Mahamud, tusimhukumu kijana pasipo ukweli” alishauri yule mzee na wengine wakiendelea kuchangia maoni yao, wakimtetea Idd kuwa hakufanya hivyo, na kama angefanya hivyo basi wasingekuja kufafanua mbele ya baraza la wazee, wengine wakawalaumu wazee hawa wawili kwa mpango wao mbaya, “halafu kwa upande mwingine nyie ndio mlikosea hamuwezi kufanya hivyo, ni sawa na kukaribisha zinaa kwa vijana wetu, mlichotakiwa kufanya ni kuwaita wazee waende pale kwa Mahamud kutoa barua ya posa, ndivyo wazee wetu walivyofanya, sasa nyie mnafanya mambo ya wapi?” aliongea yule mwekiti na hapo wote wakakaa kimya, ikiwa ni pamoja na wakina Mahadhi na mwanae Idd na bwana Mahamud, kila mmoja akilitafakari kwa namna yake swala lile, wakati bwana Mahamud akiona kuwa ni jambo la kweli kabisa, maana hata baadhi ya hadithi kwenye vitabu vya dini vimesimulia hivyo.
Tofauti na upande wa Mahadhi na mwanae, walifurahia mioyoni mwao kwa kuona kuwa mwenyekiti ana warahisishia mipango yao ya kumnasa Soraya kuwa mke wa Idd, na mwisho wao ndio wawe watawala wa mali za Mahamud, “tena nilicho wasifu hamja angalia hali ya mtu zaidi ya kuangalia kuwa kijana ni mcha mungu na binti ni mchamungu, kwakweli juu ya swala hilo ninawaunga mkono” alisema mwenyekiti, akionyesha ana maanisha anachokisema, na amekiunga mkono kwa moyo wake wote.
Hapo Mahamud akahisi kijasho chembamba kina churuzika kwenye paji la uso wake, kwanza ataanzaje kumueleza mwanae Soraya mpaka amuelewe pia mke wake atamuelezaje, “ok! kama ni kweli alichoeleza bwana Mahadhi, mimi sina neno juu ya wazo lenu” alisema bwana Mahamud, huku kila mmoja anasikiliza kwa umakini, “ila kwa kweli nisiwafiche ndugu zangu sina uwezo wa kuileza familia yangu hasa Soraya mwenyewe juu ya jambo la ndoa kati yake na Idd na akanielewa, kama kweli mtaweza kumshawishi Soraya kwa namna yoyote mimi sina maneno” alisema Mahamud na wakakubaliana kuwa siku ya jumapili saa saba mchana baada ya swala kuna wazee wataenda nyumbani kwa bwana Mahamud ili kufikisha ujumbe wa uchumba, wakipanga kuwa iwe ni jambo la kushtukiza………… ITAENDELEA
Sema kidini ni mpaka binti mwenyewe akubali tofauti na hapo hakuna Ndoa, sitegemei kama Mzee Mahamoud anaweza kumlazimisha bintiye kuolewa.
 
Sema kidini ni mpaka binti mwenyewe akubali tofauti na hapo hakuna Ndoa, sitegemei kama Mzee Mahamoud anaweza kumlazimisha bintiye kuolewa.
Hamna ndoa hapo, Binti mwenyewe ameanza msako wa kumtafuta kijana mpole wake
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA THELATHINI NA NNE
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA THELATHINI NA TATU: alisema bwana Mahamud, huku kila mmoja anasiliza kwa umakini, “ila kwa kweli nisiwafiche ndugu zangu, sina uwezo wa kuileza familia yangu hasa Soraya mwenyewe juu ya jambo la ndoa kati yake na Idd na akanielewa, kama kweli mtaweza kumshawishi Soraya kwa namna yoyote mimi sina maneno” alisema Mahamud na wakakubaliana kuwa siku ya jumapili saa saba mchana baada ya swala, kuna wazee wataenda nyumbani kwa bwana Mahamud ili kufikisha ujumbe wa uchumba, wakipanga kuwa iwe ni jambo la kushtukiza… ENDELEA
Basi mzee Mahamud alikabidhiwa mkoba wa mwanae Soraya, kisha wakaogozana kutoka nje, wakiongea kwa furaha na amani kiasi cha kuwashangaza wakina Soraya waliokuwa wana mngojea mzee Mahamud, hakika usingejua kama kuna tatizo lilikuwepo kati yao, kilichowafanya Soraya na mama yake wajuwe kuwa walikuwa katika maongezi ya tukio la jana ni ule mkoba wa Soraya uliobebwa na mzee Mahamud, ambae alimkabidhi yeye mwenyewe, “angalia kama vitu vyako kama vipo vyote” alisema mzee Mahamud.******
Wakati huo nyumbani kwa mzee Komba, mama Hilda alimuwahi Hilda kabla hajaenda kusaka mtu wa kumnunulia pombe pasipo kujari gharama ya malipo yake itakuwa nini na kwa kiasi gani, maana hutokea wakati mwingine akanywa pombe nyingi, hata kununuliwa mishikaki na kupewa elfu mbili au moja ya kuondoka nayo, lakini kwenye malipo angetoa kitumbua na mlaji angetumia hata dakika mbili angekuwa amesha maliza na kuondoka zake, huku wakati mwingine hutokea mtu akampatia bia mbili au kopo nne za ulanzi wa mia tano tano, lakini malipo yake yaka chukuwa nusu saa nzima, akigawa kila kona ya mwili wake, ambayo ingesuguliwa kweli kweli, “mwanangu njoo nikuambie kitu, huko unakoenda utaenda baadae” alisema mama Hilda na kuanza kumueleza Hilda juu ya uamuzi wake yeye na baba yake wa kwenda kutengeneza mambo kwa mganga ili kuwa komoa wakina Higgno, na kumsaidia yeye kufanikiwa katika maisha haswa katika swala la kutulia na mwanaume wake ambae ni Talib.
Mwanzo Hilda alitaka kukataa mpango huo, kwasababu alikuwa anajuwa fika kuwa mambo yanayo mkuta sababu sio familia ya bwana Frank, ila ni yeye mwenyewe na ujinga wake, lakini aliposikia swala la kutulia na Talib hapo akakubali mara moja, kwasababu aliona akifanikiwa kumtuliza Talib basi maisha yake yatakuwa mazuri, “hapo mama umeongea, sasa tunaenda kwa mganga gani” aliuliza Hilda kwa shauku, “tutaenda kule mshambani Ngwendema, kuna kile kibabu Mabudi, kile kinaweza sana” alisema mama Hilda na hapo wakakubaliana kuwa wajiandae ili waondoke zao, yaani Hilda mama yake na mtoto wa Hilda.********
Naam huku mjini maeneo ya msikiti wa mkoa, Familia iliingia ndani ya gari na safari ikaanza kuelekea nyumbani, huku Soraya aliekuwa anaendesha gari lile pamoja na mama yake wakisubiri kwa hamu kusikia kilichozungumzwa huko ndani huku Talib akiwa kama wengine, hakujuwa kilichokuwa kinaendelea, alitulia akionekana kijana safi anatoka msikitini kufanya ibada, “hawa wana mipango gani?” alijiuliza Talib, ambae kwa haraka ungejuwa kuwa amekuja pale msikitini kwaajili ya swala, lakini ukweli safari hii ilikuwa mahususi kwaajili ya kuchunguza ratiba ya Soraya, ambae mara nyingi ijumaa huwa anaenda shaambani kwake, “vipi huko wamesemaje?” aliuliza mke wa Mahamud ambae alikuwa amekaa seat ya mbele katikati pembeni ya mume wake aliekaa upande wa kushoto, hapo Talib na wengine wakatega sikio kunasa umbea, “wamefafanua ilivyokuwa, kumbe kuna mtu ambae alifanya hivyo kwa lengo la kuwaibia maana waliwekewa wote wawili” alisema mzee Mahamud, huku safari inaendelea, “nani aliesema hivyo Idd au baba yake?” aliuliza Soraya kwa sauti ya hamaki, “alielezea baba yake, lakini alielezwa na Idd mwenyewe, kwasababu na yeye ameokotwa asubuhi akiwa amelala kwenye gari hajitambui” alisema Mahamud, ambae licha ya mashaka aliyokuwa nayo juu ya Idd, lakini alijifanya kuwa ameamini maneno ya Mahadhi na kijana wake, ili kusikia maoni ya mwanae Soraya, “hapana baba, na uhakika yeye tu, ile chupa yake ilikuwa inanuka pombe kabisa, ina maana mpaka analewa hakujuwa kama ni pombe?” aliuliza Soraya, huku Talib akijitahidi kutafsiri mazugumzo yale ili apate maana kamili ya maongezi yale yanayo muhusisha Idd, na akichanganya na mashaka yake juu ya ukimya na kuto kuonekana kwa Soraya jana usiku, “wameeleza mbele ya baraza la wazee, hivyo kuna mambo wameshauri na wamesisitiza tuelewe” alisema mzee Mahamud, “lakini baba Soraya, hata kama tuna potezea lakini ukaribu wa Soraya na Idd mwisho ilikuwa jana” aliongea mama Soraya akimaanisha anacho sema, kisha kikapita kimya kirefu huku gari likiendelea na safari, sauti ya redio ikiendelea kuwapa mwaidha ya ijumaa ile.*******
Baada ya kumaliza maongezi na baba yake na kupata chakula cha mchana kwa pamoja na wazazi wake, Higgno aliaga kuanza kuondoka kurudi nyumbani kwake kule shambani akipanga kwenda kumalizia kukagua mitego ya kanga na samaki na mingine ambayo hakuwa ameikagua asubuhi.
Higgno alitembea kwa haraka huku anakumbuka tukio la jana jioni kule bomba mbili alipomsaidia yule mschana aliekuwa amelewa sana, mschana ambae licha ya kuvaa mavazi nadhifu ya kiislam na kuonekana kuwa ametokea kwenye familia ya kitajiri lakini alionekana kuwa hakuwa anajitambua kwa ulevi, “dah! eti twende nyumbani, halafu wazazi wako wange ni bananisha na kusema mimi ndie niliekunywesha pombe” aliwaza Higgno huku akiendelea kutembea kwa speed, “ila mimi inabidi niache tabia ya kupiga piga watu, naweza kuuwa siku moja halafu kesi iwe kwangu… alafuuuu mbona yule aliemuita mama ni mweusi sio mweupe kama yeye” aliwaza Higgno ambae hakumaliza hata kijiji, mara akashtuka akikutana na wakina Hilda mama yake na mtoto wa Talib, yaani ile ghafla hawa hapa uso kwa uso, “shikamoo mama” alisalimia Higgno, huku akimtazama mama Hilda ambae alikuwa anatazama chini kama mwanae Hilda kwa macho ya aibu, “marahaba” aliitikia kifupi, huku akikwepesha macho yake yasikutane na macho ya Higgno sio tu mama Hilda hata Hilda mwenywe alikuwa hivyo hivyo.
Higgno hakuweza kuhoji lolote, kwssababu licha ya kukumbuka kilichotokea baina yao, pia hakuona sababu ya kufanya hivyo, akapiga hatua kuwaacha, lakini alikuwa amemsahau mmoja wao ambae kwa namna moja au nyingine hausiki, na wala hajui chochote, “baba umeniletea pipi?” aliuliza mtoto wa Hilda aliezaa na Talib, huku akionekana mwenye furaha baada ya kumuona Higgno baba yake wa hiyari, hapo mama Hilda na Hilda wakainua nyuso zao kumtazama Higgno, kuona ana muonekano upi wa sura yake, yaani kama ni hasira, na atamjibu nini yule mtoto, wakitegemea jibu baya na kali toka kwa Higgno, lakini baada yake wakashangaa kuona tabasamu usoni kwa Higgno, “sijabeba pipi, lakini utaenda kununua dukani” alisema Higgno huku anaingiza mkono mfuni kwake na kuibuka na noti kadhaa za elfu mbili mbili, akaichomoa moja na kumkabidhi yule mtoto ambae licha ya kukaa pamoja na Higgno na mama yake na kushuhudia mengi lakini hakuwa anayatambua maana yake, na yeye kuendelea kumchukulia Higgno kama baba yake.
Naam sio Hilda wala mama yake, hakuna aliekumbuka kumkumbusha mtoto yule mdogo kusema asante kwa Higgno, zaidi ya kutoa mcho yao kwa mshangao wa kuto kuamini, wakimtazama Higgno akiondoka zake na kutokomea mwishoni mwakijiji, wao wakija taratibu huku Hilda akiwaza na kuuchanganua moyo wa Higgno, ambae siku zote amemuonyesha moyo wa kibinadamu kama ilivyo kuwa leo, ame toa fedha ambayo yeye hutafuta kwa jasho na kuvumilia atakachofanyiwa na walevi kwa Elfu mbili hiyo, lakini leo imetoka bure kabisa, “hivi mama baada ya Talib kwanini tusimwambie mganga amfanye Higgno awe mwanaume wangu” aliuliza Hilda baada ya kufikiria kwa dakika kadhaa, “hata mimi naona hilo kama linafaa, maana huyu kijana ana moyo mzuri sana” alisema mama Hilda ambae alitulia kidogo, akiwaza jambo kabla hajacheka, tena mwenzio hapa nilikuwa na waza tutatoa wapi hela ya lamri, bahati nzuri tumeipata kiulaini kabisa, tutafute sehemu tuchenji” alisema mama huyu akionyesha kufurahia ile hela ya Higgno, “mama bwana ina maana Higgno ametoa hela ya kwenda kumtengenezea mwenyewe” alisema Hilda na wote wakacheka, “kwani hujui ng’ombe huwa anapikwa na mafuta yake” alifafanua mama Hilda.*******
Baada ya kufika nyumbani na kupata chakula cha mchana Soraya na Laylah wakaingia kwenye Land Rover discover na kuanza kuzunguka mtaani pengine wange kutana na Kijana mpole, mtaa wa kwanza kabisa ulikuwa ni bomba mbili, ambako walizunguka kila kona, wakidhania kuwa pengine kijana yule anaishi kule bomba mbili kwa sasa, lakini mpaka adhana ya magharibi ina adhiniwa hawa kuwa wamemuona kijana huyu, hivyo hawa kuwa na budi kurudi nyumbani, ambapo waliswali kwa pamoja, kisha Soraya akamsindikiza Laylah kwa gari na kurudi mwenyewe, kwasasa ni kama walikuwa marafiki tu.
Wakati huo huo Talib nae alishaenda kukutana na rafiki zake wakina Vitus na Zido, alienda kuwapa taarifa ya kughairishwa kwa safari ya Soraya kwenda shambani, hivyo wakaambizana kusubiri hiyo jumapili.********
Ukweli maisha yalikuwa magumu sana kwa yule mwanamke muhudumu wa pale Kuchile bar, ambae alilala na Idd usiku kucha, alishinda kutwa nzima akishindwa kuhudumia vizuri kutokana na kuto kueleweka vizuri kwa wateja, kutokana na meno yake kukanyagwa na Idd, na alipoona mambo yamezidi akaomba ruksa kwa manager wake akakimbia mtaani na kununua super glue, ambayo alijitahidi kuyanunganisha yale meno mpaka alipoweza na kurudi tena kazini na kuendelea na kazi zake, huku akikumbuka jinsi alivyo fanyiwa na Idd ambae alimfanyia mambo ambayo hakuwahi kufanyiwa na mlevi yoyote kwa miaka ya karibuni, “kunyonywa kitumbua” hakika mwanamke huyu alijikuta anatabasamu kila alipo kumbuka tukio hilo, hakufikiri kero ambayo mwenzie aliipata mara baada ya kugundua hali yake ya vidonda sehemu zake za siri, yeye alichowaza kuwa ikitokea akakutana nae basi itakuwa burudani kwake, kuanzia pommbe na kufaidi dudu.********
Hilda na mama yake wakiwa na mtoto mdogo wa Hilda alie
zaa na Talib, mida hii walikuwa mashambani, huko Ngwendema kilomita sita toka Luhila seko, ndani ya kibanda kimoja cha udongo ambacho kuta zake zilikuwa zime egama upande, kosa kushikizwa na miti kama kiegemeo basi mpaka sasa ingekuwa imeanguka, nyumba hiyo ambayo ilikuwa imezungukwa na vichwaka virefu vya nyasi na miti iliyo achiana nafasi, kilitundikwa tunguli zenye vijikamba vyekundu na vyeusi huku mipaka (paka/nyau) ya kila rangi ikiranda randa mida yote kuzunguka nyumba ile ambayo ukiachia Mganga mabudi Hilda mama yake na mtoto mdogo wa Talib, hakukuwa na mtu mwingine upweke ulizizima.
Hali ilionyesha kuwa tayari matibabu yalishaanza na yalikuwa yanaelekea kwenye hitimisho, “kwahiyo unataka bwana Frank na mke wake wawe masikini na wachukiwe na kila mtu pale mtaani, halafu binti yako aolewe na mtoto wa bwana Frank” aliuliza babu Mabudi mwenye umri wa miaka sabini, ambae alikuwa amekaa kwenye jiwe ambalo ndilo hutumia kama kiti chake, huku akiwa amejifunga kijinguo fulani ambacho kiukweli lengo lake ni kuziba sehemu muhimu za siri, japo hakikuweza kufanya hivyo na kusababisha wakina mama Hilda na Hilda, mwenyewe waliokaa chini kwenye kipande cha ngozi, wajionee wazi wazi sehemu nyeti za mzee huyu, “ndiyo baba yangu, yaani amekuwa kero kubwa katika maisha yangu na familia yangu” alijibu mama Hilda, “lakini mama mbona inaonyesha huyu bwana hana matizo yoyote na wewe, kiasi cha nyie kuhitaji binti yenu kwenda kuishi na kijana wake?” aliuliza babu Mabudi, “hata kama babu, lakini wamekuwa wakijidai sana na kutunyanyasa na umsikini wetu” alisisitiza mama Hilda.
Hapo mzee Mabudi alitulia kidogo, kama kuna kitu anatafakari, kabla hajainua uso wake na kumtazama Hilda, kisha akamtazama mama yake halafu akamtazama tena Hilda, “haya mama nitawasaidia, kwanza nimchanje huyu binti ili akionekana mbele ya kijana mwenyewe ampende hapo hapo na asimuachie hata kidogo, na hilo la kuwa susha hao wengine nitakupa dawa, utaenda kuweka karibu na kwao, ili wanapokanyaga tu iwe ndio umasikini wao” alisema Mabudi na hapo akamtaka mama Hilda aondoke nje na yule mtoto mdogo ili yeye aweze kubakia na Hilda mule ndani aweze kumchanja.
Mama Hilda alimchukuwa mjukuu wake na kutoka nae nje ya kibanda, akimuacha Hilda amekaa kwenye kipande cha ngozi mbele ya babu Mabudi “haya simama mjukuu wangu” alisema babu Mabudi huku na yeye anasimama na kusogea kwenye mkoba mmoja uliotundikwa kwenye mti uliokuwepo kati kati ya kibanda kile, “vua nguo zote mjukuu wangu wala usiogope” alisema babu Mabudi, ambae hakugeuka nyuma zaidi kuanza kupekuwa mkoba wake na kuibuka na kisu kidogo na kijifuko fulani kidogo kilichofungwa pia, kisha akageuka na kumtazama Hilda ambae alikuwa amevua gauni lake na kubakia na chupi na sidiria, mjukuu wangu wala usiogope vua tu tukamilishe dawa” alisema babu Mabudi, huku anasogea pale alipokuwepo Hilda ambae alikuwa anajiuliza avue au asivue…. ITAENDELEA
 
Sema kidini ni mpaka binti mwenyewe akubali tofauti na hapo hakuna Ndoa, sitegemei kama Mzee Mahamoud anaweza kumlazimisha bintiye kuolewa.
Team idd tumejipanga mara hii usicheze na mzee mahadhi
 
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA THELATHINI NA TANO
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA THELATHINI NA NNE: “haya simama mjukuu wangu” alisema babu Mabudi, huku na yeye anasimama na kusogea kwenye mkoba mmoja uliotundikwa kwenue mti uliokuwepo katikati ya kibanda kile, “vua nguo zote mjukuu wangu wala usiogope” alisema babu Mabudi, ambae hakugeuka nyuma zaidi kuanza kupekuwa mkoba wake na kuibuka na kisu kidogo na kijifuko fulani kidogo kilichofungwa pia, kisha akageuka na kumtazama Hilda ambae alikuwa amevua gauni lake na kubakia na chupi na sidiria, mjukuu wangu wala usiogope vua tu tukamilishe dawa” alisema babu Mabudi huku anasogea pale alipokuwepo Hilda, ambae alikuwa anajiuliza avue au asivue…. ENDELEA
Lakini hakuwa na sababu ya kuacha kuvua nguo zake mbele ya babu mabudi, kwasababu ukiachilia alishawahi kuvua nguo zake mbele ya wanaume wengi sana, pia alitakiwa kuvua nguo kwasababu ya kumpata mwanaume ambae atamsaidia kwenye maisha yake, hivyo akavua mara moja bila kusita sita, kisha akamtazama Babu Mabudi, akamuona anaenda kwenye kona ya chumba kile ambapo palikuwa na mtungi akaufunua na kutoa chupa fulani chenye maji yenye rangi nyekundu ya kupauka, ambayo aliifungua na kuinywa kwa kuigugumia kidogo kwa awamu mbili, kisha akaifunga na kuiweka ndani ya kile chungu, halafu akachukuwa kipande fulani cha mzizi na kuking’ata kidogo na kuanza kutafuna kama vile mtu atafunavyo muwa, yaani akimeza mate yake na sio mzizi wenyewe, (ATAKAETAKA HUO MZIZI MI NINAO NAUZA) huku akiondoa kilichobakia akakirudisha kwenye mtungi, halafu akarudi kwa Hilda aliekuwa amesimama huku akiwa uchi wa mnyama, akafungua kile kijifuko mkononi mwake ambacho kilikuwa na vitu kama unga fulani mweusi ambao babu alijipakaza mikononi mwake, “haya tanua mikono” alisema babu, na Hilda akanyayua mikono yake na kuacha kwapa zake zikiwa wazi na kumfanya babu Mabudi ashuhudie msitu wa nywele kwenye kwapa za mwanamke huyu, lakini hakuzijali yeye akaanza kazi yake.
Kwanza babu alianza kutembeza viganja vyake kwenye kwapa za Hilda akipaka ule unga mweusi, na kuanza kumpaka Hilda kwenye makwapa yake, akitembeza mkono taratibu huku Hilda akisikilizia mikono hiyo ambayo katika hali asiyoielewa, akaanza kusikia mtekenyo fulani ambao ulimpa msisimko uliosababisha raha ambayo hakuitarajia katika mazingira yale, hakujuwa kama ile hali aliyoisikia ilikuwa mwanzo tu, na alikuja kuligundua hilo mara baada ya babu kupakaza tena ule unga mweusi kwenye viganya vyake na kuhamia kifuani ambapo alipeleka mikono kwenye maziwa ya Hilda ambayo muonekano wake na umri wake vilikuwa tofauti, maana tayari yalishafanana na vile viatu vya kuogea.
Hilda akiwa bado ameinuwa kwapa zake aliweza kuhisi msisimko zaidi, ambao ulifanya ashushe mikono yake maana alihisi kuchoka kwa msisimko ambao ulishuka kuanzia shingoni kupitia kwenye uti wa mgongo mpaka kwenye makalio na kuzungukia kwenye kitumbua chake, hivyo akajikuta akihisi kitu kama mkojo ukimbana na kumfanya abane miguu yake hasa sehemu za mapaja ambazo ndizo zilizofuatia kupakwa dawa.
Sasa basi wakati babu anapaka dawa kwenye mapaja ya Hilda, Hilda mwenyewe alijikuta akitanua miguu na kumpa nafasi nzuri babu apake dawa huku Hilda akiomba japo babu aguse kitumbua chake hata kwa bahati mbaya, pengine angekisugua na kumpuguzia ile hali aliyokuwa anaisikia, lakini babu hakufanya hivyo baada yake alipitisha mikono kwenye uvungu wa Hilda na kutemmbeza taratibu huku akiendelea kutafuna kijiti chake kama anakula bazoka, hakika Hilda aliona wazi kuwa anahitaji dudu kwa wakati ule, hivyo akajikuta yeye mwenyewe anapeleka mkono kwenye usawa wa kile kijinguo cha babu alichojifunga kiunoni na kupapasa kwenye dudu akaikuta ilisha simama, “babu kumbe na wewe umo” alisema Hilda kwa sauti ya chini, yaani ya kunong’ona huku anapekenyuwa kile kijinguo na kuikamata dudu yenyewe, kisha akaanza kuichezea, “vipi mjukuu wangu, unataka hogo?” aliuliza babu huku anapitisha mkono kwenye mpasuko wa kitumbua na hapo ni kama alikuwa amemchokoza Hilda, ambae alianza kuchezesha kiuno chake na kusababisha kitumbua chake kijisugue kwenye mkono mkomavu wenye dawa wa babu Mabudi.*******
Higgno alifika salama kule shambani na kuanza kutembelea mitego yake, huku akiendelea kuwaza na kuchanganua maneno ya baba yake kuhusu kupata mwanamke “kwahiyo hata kama sina hela kama wakina Talib nitaweza kupata mwanamke mzuri” alijisema Higgno, ambae alikumbuka yule mwanamke ambae alionyesha kumzoea kwa ghafla jana jioni pale alipomsaidia, mschana ambae baadae aligundua kuwa nyumbani kwao wanauwezo mkubwa kifedha, “ningempataga yule mwanamke wa siku zile pale TTC, halafu ndiyo anakuwa demu wangu, mbona ningejisikia raha sana” aliwaza Higgno akiendelea kukagua mitego yake ambayo ilionyesha kuwa alikuwa amenasa mawindo yake kwa wingi sana, akimkumbuka mschana wa kiarabu ambae alimsaidia miaka mingi iliyopita, “lakini yule hata ukimuonyesha unampenda yeye ataanzaje kukupenda na vile walivyo matajiri” alijisemea Higgno, ambae mpaka anamaliza kukagua mitego yake alikuwa amenasa kanga kumi wa porini wote wakiwa wazima, samaki wakubwa wa kawaida sita na kambale wanne, huku wadogo wadogo wakiwa zaidi ya ishirini, hakika ilikuwa kazi kubwa kidogo, ambayo aliikamilisha saa mbili za usiku na kuwahifadhi wale kanga wa porini, huku akianza kuwabanika wale samaki kwenye moto mdogo, alifanya hivyo kwasababu alihitaji kuwa hifadhi vizuri mpaka juma tatu jioni akitoka kwenye maombi ya kazi, maana kesho asingeweza kwenda nyumbani kuwapelekea mboga kwa kuwa jumapili alipanga iwe siku ya maandalizi ya siku inayofuata ya kwenda kwenye masailiano, (interveiw)
Higgno alikaa kibandani kwake akisimamia ukaushaji wa samaki, huku wale kanga akiwa amewafungia kwenye banda dogo ambalo lilitengenezwa maalumu kwaajili ya kuku, huku anasikiliza redio yake na kuendelea kuwaza jinsi maisha yake mapya yatakavyokuwa mara baada ya kupata kazi kwa mwarabu tajiri, ambae alisha ahidi kumpatia kazi mwaka mmoja uliopita, ni mara baada ya kumsaidia kumuokoa toka kwa wanyang’anyi, “sijui atanikumbuka yule mzee” aliwaza Higgno akiona kuwa ni muda mrefu umepita toka akutane na Mahamud.******
Higgno aliwaza mengi sana pale nje ya kibanda chake, huku akiwaza zaidi kuhusu kupata mwanamke na sura ya mwanamke mzuri ambayo ilimjia ni ile ya mschana mzuri aliekuwa anataka kubakwa na yeye akamsaidia, “ninge kuwa na gari langu pale ningemwambia ingia kwenye gari huku nawapiga wale jamaa” aliwaza Higgno, huku akivuta picha kuwa amekaa pembeni ya yule mschana wa kiarabu kwenye gari, Higgno akajicheka kidogo huku anainuwa uso wake na kutazama mwezi, “tena kama nikipata safari za dar, natafute mwanamke mzuri kama yule mtoto wa kiarabu, yule mwarabu dah! sijui huko aliko alishaolewa au hajaolewa, sijui amelala peke yake au na yeye anatazama mwezi kama mimi” yalikuwa mawazo ya kipuuzi ya bwana Higgno, ambae bado alikuwa amekaa pale nje anatazama mwezi uliokuwa unaangaza vyema kabisa katika usiku wenye amani tele.******
Kule Ngwindimba yaani kwa babu Mabudi, hatukujua kilichoendelea mule ndani ya kibanda, zaidi ni kwamba Dakika kumi zilitosha kwa Hilda kupewa dawa mule ndani ya kibanda cha babu Mabudi, ambae aliwapatia pia dawa ya kwenda kumwaga karibu na nyumba ya bwana Frank, akimtaka mama Hilda kurudi tena jumapili, yaani siku ya pili iliyofuata ili wakamilishe dawa.
Hilda na mama yake pamoja na mtoto mdogo waliondoka zao kurudi kijijini, huku mama Hilda akiamini kuwa muda mfupi ujao wataanza kuyaona mafanikio, kabla yeye hajarudi kukamilisha dawa, “amekuchanja wapi na wapi?” aliuliza mama Hilda wakiwa njiani wanarudi, “amenichanja kwenye kwapa kifuani na kwenye mapaja” alisema Hilda, akimdanganya mama yake akichelea kumueleza ukweli kuwa alipakwa dawa ambayo ilimwongezea hamu ya kupewa dudu na akapewa dudu na yule babu mganga Mabudi, “huyu babu namuamini sana yaani akikuambia kitu kina kuwa hivyo hivyo” alisifia mama Hilda pasipo kujuwa kuwa mwanae alikuwa anatafakari utamu alioupata siku ile mule ndani ya kibanda kile, “anaonekana yupo vizuri” alichangia Hilda, huku safari inaendelea, Hilda akivuta kumbukumbu jinsi yule babu alivyomshika na kumgeuza atazame mbele kisha kumwambia ainame huku yeye akitamani dudu kuliko kitu kingine utadhani mfungwa wa kike alietoka gerezani, Hilda hakusuburi babu aongee mara mbili aliinama kwanguvu akibidua vijikalio vyake na kutanua miguu kwa nguvu kiasi cha kitumbua kile kufunguka ungesema babu anataka kuchungulia tumboni, na babu ambae alishajiandaa kwaajili ya mechi hii ya ghafla, akajipimia uroda bila kujivunga, japo shughuri ilikuwa ya muda mfupi lakini ukweli Hilda alifurahia show kiasi cha kutamani ile nafasi ya mama yake ya kurudi kwa babu jumapili kule Ngwendimba ingekuwa ya kwake ili akapewe tena dudu, laiti angelijua sasas.
Hata walipofika nyumbani mida ya saa mbili za usiku wakimkuta mzee Komba akiwa anasubiri kwa hamu wampe habari za kwa Mabudi, nao waliunga nae wakitumia ile efu moja iliyobakia kununua ulanzi na kuanza kuunywa, huku wakisimuliana habari za huko, “yaani amesema hilo kwake tatizo dogo sana, muda mfupi wanapukutisha mali zote wanabakia weupe” alisema mama Hilda huku akimueleza pia mume wake juu ya uamuzi waliouchukuwa wa kumpumbaza Higgno ampende Hilda, “hapo mmecheza maana watakoma na roho zao, wao si walimuona Hilda hafai” aliunga mkono bwana Komba, “tena kesho kutwa ameniambia nirudi kumalizia dawa” alikumbusha mama Hilda pasipo kujuwa kilichomtokea mwanae Hilda kule kwa babu Mabudi, “haina tatizo mke wangu hata akisema ulale huko huko haina shida ilimradi hawa watu wakome na kushika adabu” alisema mzee Komba pasipo kujuwa kitakachoenda kumkuta mke wake.******
Bwana Mahamud hakuweza kukaa kimya, huku akiwaza peke yake juu ya ushauri wa mwenyekiti wa baraza la wazee wa dini la kuja kutoa posa kwa ajili ya Soraya, ukiwa ni mpango ambao wao waliubariki hapo mwanzo kabla ya tukio la jana, na baada ya kukaa kwa muda mrefu juu ya kitanda akiwaza juu ya mambo yale huku mke wake anaanza kuutafuta usingizi ndipo alipo amua kuvunja ukimya na kumueleza mke wake kama walivyo jadili kule baraza la wazee, “kwa kweli nimeshidwa kukataa, kwasababu kila mmoja anaamini kuwa Soraya na Idd waliwekewa dawa na sio kwamba Idd aliweka dawa kwenye juice” alisema mzee Mahamud kwa sauti tulivu iliyozidiwa na uchovu wa kufikiria kwa muda mrefu, “mh! kama wamesema wale wazee kwa kweli hapo inabidi tuwe makini katika kutoa maamuzi, maana tunaweza kuonekana tuna mnyima mtoto haki yake ya kuolewa, na kama tukimuachia Soraya mwenywe atoe maamuzi, itaonekana kuwa tumeshindwa kumlea mtoto kimaadili na kwamba maamuzi yote ni ya kwake na sisi hatuna maamuzi na mtoto” alisema mama Soraya kwa sauti ya kuishiwa pose, “lakini naamini kama Soraya ataongea kwa kuweka pingamizi mbele ya wazee wa baraza lazima atakuwa na point ambazo zitawafanya wazee hao wakubaliane nae” alisema mzee Mahamud, “mh! ila kumbuka pia Soraya hajawahi kukutana na wazee wale katika maamuzi kama haya, hivyo anaweza kujikuta anakubali pasipo kutegemea” alisema mama Soraya na bada ya mjadala wa muda mrefu wakakubaliana hivi, “tumuache tuone ataamua nini, hata akiolewa na Idd akimshinda basi atarudi nyumbani” alisema baba Soraya “lakini kumbuka binti alijitunza muda mrefu kwaajili ya mwanaume mwenye upendo wa dhati na mwenye kujiheshimu” alikumbusha mama Soraya akionyesha msisitizo, “mke wangu kilichobakia tumuombe mwenyezi mungu kila kitu kiende kwa haki” alisema bwana Mahamud, huku wakipanga kufanya siku ile kuwa kama surprise kwa Soraya, hawakutaka kumuuza roho yake kwa muda siku mbili nzima akiwaza ujio wa wazee hao, hivyo wakapanga kuwa siku ya jumapili kumuacha Soraya aende shambani huku nyuma yaanze maandalizi ya wageni, atakaporudi saa saba kwaajili ya swala ya saa saba anakutana na wageni, hapo ndipo tutakapo msikia atasemaje” alisema Mahamud.******
Wakati baba na mama wanawaza hayo huku nako Soraya alikuwa chumbani kwake amejilaza kitandani, uwa jekundu likiwa kifuani kwake, katikati ya maziwa yake mazuri yaliyosimama vyema na chuchu za kuchingoka, amezima taa na wala haja washa TV kama kawaida yake, macho yapo dirishani anatazama mwezi mkubwa uliokuwa unaangaza vyema kabisa na kufanya miale ya nuru zake kupenya dirishani na kumpiga usoni, nadhani na yeye atakuwa anauona huu mwanga wa mbala mwezi, maana nyumba yake haina mlango, si ndivyo alivyo mueleza mama” aliwaza Soraya, ambae mara kwa mara alikuwa anajitabasamulia peke yake, akionyesha kujawa na matumaini fulani, “kesho pia nitaingilia upande wa majengo mpaka mfaranyaki pengine nitamuona” aliwaza Soraya ambae kuna wakati alikuwa anashangaa kwanini kijana yule hakuwahi hata kuota kama kuna mschana anampenda na kujaribu kumfuatilia, ina maana toka miaka ile hajui mimi ni nani na ninakaa wapi, japo aje abishe hodi na kusema kuwa nimekuja kumuoa Soraya?” alijiuliza Soraya ambae mara kwa mara alikuwa anarudisha macho yake kwenye dirisha na kutazama mwezi, ambao ulikuwa umetulia kutokana na utulivu wa anga usiku ule, lakini naamini nitamuona tu, kama nilivyo muona jana” alisema Soraya, au mpaka nipate tatizo jingine ndipo nimuone tena?” aliwaza Soraya na kucheka kidogo, “kwanini isiwe kwenye wakati wa raha, maana wanasema rafiki wa kweli ni yule akufaae kwa dhiki na faraja, sasa mtu mwenyewe kazi yake ni kunisaidia kwenye matatizo tu!” alilalamika Soraya ambae aliona siku inayofuata inachelewa kukucha ili aingie mtaani kumsaka kijana mpole wakati ukweli higgno hana ratiba ya kutoka siku hiyo.******
Siku iliyofuata yaani siku ya jumamos, ilipita kwa haraka sana kila mmoja akiendelea na shughuli zake, wakati Talib alienda mwembe chai kupanga mpango kabambe wa jumapili juu ya kumteka na kumuuwa Soraya wakiwa wameshapata fedha, lengo likiwa ni kumpatia nafasi Taliba ya kuwa mtu pekee wakutegemewa katika familia ya bwana Mahamud, huku Higgno akimalizia kulima kipande kidogo cha shamba huku akiendelea kukausha samaki, Soraya yeye alikuwa anazunguka mtaani akitumia gari lake aina ya Disicovery Land Rover, akiendeshwa na Laylah, walizunguka karibu mji mzima wa songea mjini pasipo mafanikio, wakiambulia mengine kabisa ambayo hawa kuyategemea, kama vile kuna wakati walikuwa wanakatiza maeneo ya mwembe chai wakitokea Lizborn, wakamuona Talib akiwa na vijana watatu wakiwa wamesimama pembeni ya kituo cha daladala cha mwenye chai, huko wote wakiwa na sigara zao mkononi, “mh! kumbe Talib bado anavuta sigara?” aliuliza Laylah, kwa mshangao, “we unajua leo, mwenzio nimejua siku nyingi kuwa anavuta mpaka bangi” alisema Soraya, ambae hakuacha kutazama huku na huko kuangalia kama anaweza kumuona kijana mpole akiwa katika matembezi yake, “weeee! kumbe ujuwe ameniambia kuwa kesho anataka kuniagiza shamba” alisema Laylah kwa mshangao, “hawezi kukuagiza upuuzi wake, we msikilize tu” alisema Soraya akimuondoa wasi wasi dereva na rafiki yake Laylah, hiyo ilikuwa ni safari ya kurudi nyumbani maana muda ulishaenda sana.
Hilda yeye hakuwa na shida zaidi ya kwenda kwenye kilabu cha ulanzi na kujiegesha, maana alijuwa fika lazima atapata mwanaume wa kumnunulia ulanzi, kisha na yeye alipie fadhila, Higgno yeye jioni aliishia kufanya mazoezi na kuendelea kubanika samaki wake akipanga kesho kuwa akitoka kwenye usail atengeneze wale kanga na wengine apeleke nyumbani kwa baba yake.
Wakati huo upande wa bwana Mahadhi na kijana wake Idd walikuwa katika mipango ya kufanya utaratibu wa kupelekea barua ya posa nyumbani kwa bwana Mahamud, pamoja na wazee wa baraza huku mipango ikiwa mingi sana, “yaani wewe nakukubali sana, unajuwa kuweka mambo sawa, sio toto lingine linavuruga halafu linakaa kimya, haliwezi hata kutoa ushauri au mbinu ambayo tunaweza kutumia kuweka mambo sawa” alisema Mahadhi, “lakini baba tusubiri kesho tuone inakuwaje?” alishauri Idd, ambae alikuwa na kachupa kake kadogo ka pombe wanyewe wanaita kaschana, akikakamua pale pale nyumbani kama alivyo shauriwa na baba yake kuepuka macho ya watu, “weweee, unamjuwa yule mwenyekiti atatoa aya pale hata kama mtoto analega lega yeye mwenyewe ataelewa somo na kukubali tu” alisema mzee Mahadhi Salum kwa kujisifu, ambae alionekana kuwa na asilimia zote za kufanikisha mpango ule, “lakini usije kunifanyie ujinga, mimi nahangaika hapa halafu unafanikiwa unanisahau, hakika nitakupiga uchizi” alisema Mahadhi akitania.********
Naam ulikuwa mchana ukawa usiku, ikawa asubuhi, hatimae siku ya jumapili siku ambayo kuna watu walikuwa wanaisubiri kwa hamu sana, sijakutaja msomaji ila ni wakina Talib na wenzake, ambao walipanga siku hiyo isipite bila kukamilisha mpango wao wa kumteka Soraya, wengine waliokuwa wanatamani sana, siku hii ifike ni Mahadhi na kijana wake Idd, ambao waliamini kuwa ungekuwa mwanzo wa mafanikio ya maisha ya Idd, babu Mabudi pia aliitamani siku hii kwa kuwa ni siku nzuri kwake, kwasababu alitarajia mgeni toka Luhila mbae ni mke wa bwana Komba yaani mama Hilda, wapo pia walioisubiri kwa hamu siku hii kwa sababu zao binafsi, siku ambayo naomba niisimulie vyema pasipo kurukaruka kama juma mosi, ahsanteni wale ambao mumetuwezesha leo kuwepo hewani, kama kuna yule ambae angependa kuendelea kutuwezesha kwaajili ya jioni na kuendelea siku zijazo anaweza kutuchangia chochote kwa kuanzia Tsh 500/= kwa namba 0717924403 asanteni kwa msaada wenu wasomaji ndio wadhamini wetu..., Endelea Kufuatilia mkasa huu hapa hapa jamii forums ujue nini kilijiri siku ya jumapili.
 
Back
Top Bottom