Nephew
JF-Expert Member
- Jun 29, 2014
- 333
- 395
Hukosei mkuu Abou Shaymaa. Kazi nzuri sana, weka vitu tuendelee kuburudika
Jana alieweka mida ya kesho kasoro(saa sita kasoro hivi) au anaweza akaweka usiku wakesho saa sita au Saba haeleweki anapenda tuchunguliechungulie🤓Leo usiku wa saa ngapi sasa
Ngoja nikuulize:Idd kayatimba
mmh sijajua mtoa mada amasema leo tunafurahi, mpaka sasa ni epsod ya piliNgoja nikuulize:
Kwaleo hii ndio episode ya mwisho?
Nitachungulia tena saa 6 usiku:mmh sijajua mtoa mada amasema leo tunafurahi, mpaka sasa ni epsod ya pili
Huyu Idd ana laaaanaaaIdd ni mtoto mwenye sura ya kibandidu Idd ni mtoto wa kwanza wa mzee Hamidu 🎶
Team Idd tunakuja na mpango mwingine mara hii hachomoki soraya, japo kuwa team idd kunahitaji moyo walai 😅 sina muda nitaungana na Mahimbo Jr kuwa team mzee komba.Huyu Idd ana laaaanaaa
wapi
Sasahivi nahakikisha nakuwa upande wa watu wenye akili.Team Idd tunakuja na mpango mwingine mara hii hachomoki soraya, japo kuwa team idd kunahitaji moyo walai 😅 sina muda nitaungana na Mahimbo Jr kuwa team mzee komba.
Nasubiria kitumbua cha soraya hapa mpka kieleweke😂TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA THELATHINI: Idd alitamani kupata cha asubuhi kabla hajaondoka lakini aliona itakuwa vyema kama wakioga kwanza ilikuondoa uchafu uliowajaa miilini mwao, hivyo idd akainuka toka kitandani ila anakanyaga chini akakutana na meno manne ya bandia ya pamoja tena machafu kwa rangi yake, hapo akashtuka na kugeuka kumtazama mwanamke huyu alielala kitandani, akamsogelea na kumfunua shuka, kwanza kabisa macho yake yalitua kwenye makalio madogo ya mschana huyu ambae licha ya kuchafuka kwa kinyesi pia vilionekana vidonda vingi vilivyo pauka kweli kweli, vikishindana ukubwa na upya, “mama yangu nipo salama kweli” alijiuliza Idd huku ana jishika kichwa kwa masikitiko……… ENDELEA SASA
Akageuka na kuelekea bafuni huku akikanyaga tena yale meno ya plastic na safari hii akiyavunja kabisa na kujiumiza unyayoni kwa waya ulio baniwa yale meno, “ass kum.. make...” alilalamika Idd huku anainua mguu mmoja ule ulioumia na kujishika kwa kujipooza huku anaruka ruka kwa mguu mmoja, ambao pia alishtuka akinasa kwenye nguo fulani ambayo mwanzo hakuitambua na kuanguka chini, akainasua na kuinuka nayo ikiwa mkononi, ndipo alipoitazama, mwanzo alidhania kuwa kuna kitambaa cha kufutia vumbi madirishani kiliachwa mule chumbani kwa bahati mbaya, jinsi kilivyo kwa uchafu wake, maana licha ya kuwa kime kakamaa kama vile kilinyunyuziwa uji wa kupikia pombe ya kienyeji, wao wanaita ubaga, au uji wa mhogo, Idd akashawishika kukitazama kile kijinguo na kilicho mvuta au kumshawishi kukiangalia ni harufi yake mbaya kama vile nyama iliyo sahaulika na kuanza kuonza, “mamaaaa” alipiga kelele Idd huku anaitupa chini ile nguo, ilikuwa ni chupi ya kike ambayo muonekanano wake ungesema kuna mtu aliipengea kamasi week nzima bila kuiosha, hapo Idd akashika pua yake kwa haraka sana na kuitupa chini, “huff!!! masikini mimi nimeokota weee! lakini leo nimeokotwa” alijisemea Idd huku anaelekea bafuni kuoga.*******
Saa moja na nusu siku hii ya ijumaa, mida ambayo Soraya alisha maliza kuoga na kujilaza kitandani kwake huku kichwa chake kikiwa kizito kidogo, akiwa anatafakari mambo yaliyo mtokea jana, hasa akivuta kumbukumbu alivyo kutana na yule kijana aliemtafuta kwa muda mrefu, hata alivyo msaidia kwa mara nyingine na kumfikisha nyumbani, maana alipokuwa anaoga alijikagua na kujiona kuwa yupo salama kabisa, “ina maana hanipendi, mbona hakuonyesha kunipenda?” alijiuliza Soraya kabla hajajipatia jibu, “Hooo! nilivaa niqab, ina maana hakunifunua! ni heshima kiasi gani aliyo nayo yule mwanaume?” alijiuliza Soraya, “sasa itakuwaje wakati mimi nampenda jamani” safari hii Soraya aliwaza kwa sauti, “kama hakunitambua mbona aliniachia zawadi” aliwaza Soraya, ambae sasa alikumbuka kile kijifuko cha zawadi na kukichukuwa kisha akalala nacho kitandani na kukifungua,kisha akaingiza mkono na kutoa kitu kimoja baada ya kingine huku akijikuta anatabasamu kwa kila kile alichokitoa ndani ya mfuko, “ananipenda ndio maana ameniletea chupi” aliwaza Soraya ambae huku anaachia tabasamu lililochanganyika na aibu fulani kutokana na aina ya ile chupi, hakujuwa kuwa ile chupi sidiria na uwaridi vyote vya rangi nyekundu havikuwa vya kwake, ila ni kama alivipora kwa mwenyewe Kijana mpole, Soraya alijikuta akitabasamu kwa furaha, “inamaana aliniona toka siku ile nilivyoenda na Idd ndio akaamua kuninunulia zawadi, sasa mbona hakuonyesha kama ananijuwa au ameshikwa na wivu, alidhania Idd ni mchumba wangu?” aliwaza Soraya, ambae hakuwaza jambo alilofanyiwa na Idd kuwekewa kilevi kwenye juice ya mabungo, “mama atakuwa ameshanifahamu, hivyo rahisi mimi kumpata” aliwaza Soraya na wakati huo huo mlango wachumba chake, ukagongwa “ingia” alisema Soraya na mlango ukafunguliwa na mama Soraya akaingia chumbani kwa Soraya na kumkuta binti yake huyu ameshaoga na kujilaza kitandani, akionekana kutafakari jambo kwa kina, “assalaam alaykum” alisalimia mama Soraya huku anakaa kwenye kitanda cha Soraya, “waalaykum salaam, shikamoo mama” aliitikia Soraya huku anajiinua na kukaa kitandani pembeni ya mama yake, “marhaba pole mwanangu, unajisikiaje sasa?” aliuliza mama Soraya, huku akiweka kiganja chake cha mkono kwenye paji la uso la binti yake na kuligusa kama anatazama joto la mwili, “nipo safi mama, japo kichwa bado kizito kidogo” alijibu Soraya kwa sauti tulivu, na kabla mama Soraya hajauliza kitu, Soraya akawahi kuuliza, “samahani mama ulikutana na yule kijana mpole?” aliuliza Soraya kwa sauti iliyojaa shauku, “mh! sijawahi kuona kijana mstaarabu kama yule, hivi unamfahamu toka zamani?” aliuliza mama Soraya kabla hajajibu swali la mwanae, “kwahiyo ulimwambiaje?” aliuliza Soraya kwa shauku, “mh! nilimwambia aje nyumbani nimpe japo hela kidogo ya ansante, lakini alikataa alisema anawahi nyumbani kwao kibanda chake hakina mlango anaogopa wataiba” alijibu mama Soraya, akionyesha kupenda tabia ya Kijana mpole, “kwahiyo mama ulimwambiaje?” aliuliza tena Soraya akionyesha kuhitaji sana habari za kijana mpole kuliko yaliyotokea jana akiwa na Idd, “nilimwambia aje nyumbani achukuwe japo fedha kidogo za shukurani, lakini alikataa alisema haitaji malipo kwasababu alikusaidia kama dada yake” alijibu mama Soraya, akionyesha alistaajabishwa na tabia ya kijana mpole, “kwahiyo mama huku chukuwa hata namba yake ya simu?” aliuliza Soraya kwa sauti ya kulalamika, “mh! mama nisamehe kwanza ningeanzaje, maana niliogopa jinsi nilivyopakuta pale, yaani nimekuta amempiga yule kijana mwenye lile Taxi, amelala chini hajiwezi” alisema mama Soraya, na hapo Soraya akacheka kidogo, “mshenzi yule eti alikuwa anamwambia yule mvulana kuwa mjinga bora anifanye” alisema Soraya,”kwani ilikuwaje ulewe vile mpaka ukakutana na yule kijana wakati ulikuwa na Idd?” aliuliza mama Soraya na kutaka kujuwa kila kitu kilivyo kuwa, “yaani mama, msiniambie tena kuhusu kumsindikiza kaka Idd, kwanza anakunywa mipombe halafu sijui aliniwekea nini kwenye juice” Soraya alimsimulia mama yake, kuanzia alipo muona yule kijana wakati anavuka barabara na kupanda pikipiki, na walipoenda kunywa juice ya mabungo ambayo iliwekewa kilevi, huku akigundua kuwa maji aliyokuwa anakunywa Idd yalikuwa sio maji ni pombe, alieleza jinsi alivyo toka pale bar na kukutana na Kijana mpole, ambae alimsaidia mpaka akafika salama, pia alimueleza mama yake kuwa kijana huyu mpole ndie yule aliewahi kumsaidia miaka iliyopita asibakwe na wanafunzi watukutu wa songea boys, “tena Idd amebakia na mkoba wangu kwenye gari lake na una hela zangu na vitambulisho” alimaliza kusimulia Soraya, “kumbe Idd mshenzi kwa hiyo alitaka akufanye nini?” aliuliza mama Soraya kwa sauti iliyojaa Hasira, huku anainuka toka kitandani na kutoka nje ya chumba cha Soraya.
Moja kwa moja akaelekea chumbani kwake ambako alimkuta mume wake akiwa anajiandaa kuelekea kwenye kalakana ya uchoraji na upakaji wa ragi magari ya Mbogo Edgar CAR SHINE COMP, ambako magari yake yalikuwa yana pigwa chapa ya kampuni yake, ikiwa na maandishi makubwa ya SORAYA EXPRESS, na rangi waliyoichagua blue yenye fito nyekundu na nyeupe kwa upande wa nyuma “baba Soraya, naomba iwe mwisho kumkaribisha Idd hapa nyumbani, kwa kitendo alichokifanya jana anaweza kuja hata kutuibia hapa nyumbani” alisema mama Soraya, kwa sautiliyojaa jazba, “vipi amemuharibu mtoto?” aliuliza mzee Mahamud huku anasogea kwenye kabati lake na kuvuta drow akitoa bastora yake, “hata kama hajamuharibu we unadhani kilichokuwa kina fuatia ni kitu gani?” alisema mama Soraya, na kumsimulia mume wake kama alivyo simuliwa na Soraya, “kwahiyo huyo kijana ndiyo yule aliemsaidiaga kipindi kile” alisema mzee Mahamud, huku anachukuwa simu yake na kumpigia Mahadhi ……….. ITAENDELEA
TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA THELATHINI NA MOJA
MTUNZI Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA THELATHINI: “baba Soraya naomba iwe mwisho kumkaribisha Idd hapa nyumbani, kwa kitendo alichokifanya jana anaweza kuja hata kutuibia hapa nyumbani” alisema mama Soraya, kwa saut iliyojaa jazba, “vipi amemuharibu mtoto?” aliuliza mzee Mahamud huku anasogea kwenye kabati lake na kuvuta drow akitoa bastora yake, “hata kama hajamuharibu we unadhani kilicho kuwa kina fuatia ni kitu gani?” alisema mama Soraya, na kumsimulia mume wake kama alivyo simuliwa na Soraya, “kwahiyo huyo kijana ndiyo yule aliemsaidiaga kipindi kile” alisema mzee Mahamud huku anachukuwa simu yake na kumpigia Mahadhi……….. ENDELEA NAYO SASA
Huku anaweka bastora yake mezani, simu iliita mpaka inakatika yenyewe pasipo kupokelewa, “hawezi kupokea simu kwasababu anajuwa alicho kifanya huyo mlevi wake” alisema mzee Mahamud huku anapiga tena simu kwa namba hiyo hiyo, lakini safari hii akaambiwa simu ile ilikuwa inatumika, “mpuuzi sana, anajifanya anatumika nitakunasa kwenye ibada” alisema mzee Mahamud ambae alionekana kujawa na hasira, “kwani ulitaka kumuambia nini?” aliuliza mke wa bwana Mahamud, “kwanza atume mtu alete begi la Soraya, pili sihitaji yeye wala mwanae wakanyage hapa nyumbani wala kujenga mazoea ya kijinga” hakika Mahamud hakuwahi kuonekana mwenye hasira za wazi kama alivyoonekana wakati huo, hakika cheza na kitu chochote lakini sio mwanae Soraya, “mume wangu unahitaji kupunguza hasira, cha kushukuru ni kwamba Soraya yupo salama” alisema mama Soraya, kwa sauti ya upole akijaribu kumtuliza mume wake, “lakini kwanini huyu kijana amekataa kuja hapa nyumbani, amenisaidia mara mbili na bado hataki hata kitu chochote cha shukrani?” aliuliza mzee Mahamud kwa sauti ya kutia shaka, “hata mimi nilishangaa kwa kweli, eti anawahi kwake kibanda chake hakina mlango, ila nimemwambia akiwa na shida aje hapa nyumbani” alisema mama Soraya, “unajuwa bado sijaelewa ni kwanini kijana huyu aliweza kutoa msaada kwa Soraya pasipo kuomba wala kukubali kitu chochote kama ahsante?” aliuliza Mahamud, akimtazama mke wake ambae sasa alimsogelea na kuanza kumsaidia kumfunga vishkizo vya shati, “tena kwa vijana wa sasa na hivi wanavyo mtamani huyu mtoto jamani, huyu kijana sijui ana moyo wa aina gani, yaani msaada alioutoa kijana huyu naweza kusema ni zaidi ya ambavyo kaka angepaswa kumfanyia dada yake au mume kumfanyia mke wake, yaani alikuwa makini sana” alisema mama Soraya kwa msisitizo” alisema mama Soraya na hapo kikapita kimya kidogo, kabla mzee Mhamud hajasema “siku akipatikana huyu kijana nitamuuliza swali, nikiridhika na jibu lake itabidi tumjengee nyumba ndogo nzuri, na kama akiwa ni fundi au dereva basi nitampatia kazi, maana inaonyesha kuwa ni muaminifu” alisema mzee Mahamud, huku anaendelea kujiandaa.******
Idd alimaliza kuoga, huku muda wote akijilaumu kwa kilealichokifanya usiku kucha, hasa kitendo cha kuonyesha ufundi wa kumnyonya kitumbua cha mwanamke huyu, ambacho ni wazi kabisa kina tatizo kutokana na muonekanano wa sehemu za siri za mwanamke mwenyewe, alijilaumu kwa kuingia njia isiyo rasmi na kuacha kitumbua, maana huku kwa jirani ndio tatizo kubwa, hapo akajikuta akitema mate kama mjazito, yaani mara kwa mara, kwasababu alikuwa na uhakika kuwa alishabugia sana uchafu wa mwanamke huyu, wakati akimuingilia kinyume na maumbile yake, hasa kipindi alipokuwa ana toa dudu yake kwenye makalio ya mwanamke huyu na kupakaza mate kisha kuendelea, hapo angepump mara kadhaa kisha angefanya tena hivyo na alifanya hivyo mara kwa mara pasipo kujuwa kuwa alikuwa anabugia uchafu ambao alipoamka aliukuta umetapakaa kila kona ya mwili wake na kuchafua mashuka ya chumba kile cha hotel.
Ile anatoka bafuni akakimbilia kwenye nguo zake ambazo nazo zilikuwa chini akazizoa zoa na kuanza kuvaa kwa pupa, hakutaka tena kumtazama yule mwanamke ambae bado alikuwa amelala kwa kujifunika gubi gubi pale kitandani, na wakati anavaa suruali ndipo aliposikia simu yake inatetemeka, akagundua kuwa ilikuwa inaita akaitoa haraka huku mapigo yake ya moyo yanaenda kasi, akihofia kukutana na simu toka kwa Soraya au baba yake au mama yake, lakini alipoitazama akakuta kuwa ilikuwa ni simu toka kwa baba yake hivyo akaipokea haraka huku “ndio baba kuna usalama huko” aliuliza Idd kwa sauti iliyojaa wasi wasi na pupa, huku anaendelea kuvaa, “usalama utoke wapi wakati mpaka sasa hujarudi nyumbani toka jana jioni, halafu ulitoka na mtoto wa watu baba yake amenipigia simu nimeshindwa kuipokea” alisema mzee Mahadhi kwa sauti ya chini, kama vile hakuwa anahitaji mtu mwingine asikie, “dah! baba ni story ndefu, sijui tunafanyaje, yaani kuna mchezo nilitaka kumchezea Soraya sasa umeferi, halafu akanitoroka, sasa sijui kama aliweza kufika nyumbani kwao maana mchezo wenyewe ulikuwa wa hatari vibaya sana” alisema Idd ambae sasa alikuwa anamilizia kuvaa viatu ili aondoke zake, “bwasheee! umesha vuruga kila kitu, unadhani mzee yule atanielewa kweli, njoo haraka tupange jinsi ya kumaliza tatizo” alisema Mahadhi ambae alionekana wazi kuwa upande wa mwanae, kama walivyo wazazi wengi wa sasa ambao hujitahidi kuwasaidia vijana wao, pale wanapo kuwa wameingia kwenye matatizo, hata kama alie ya sababisha ni kijana mwenyewe, “nakuja sasa hivi” alisema Idd na kukata simu, kisha akamaliza kuvaa na kuinuka tayari kuondoka, lakini ile anainuka tu akashangaa ameshikwa bega na kutulizwa kidogo, “mpehi habar ya asupuhi” ilisikika sauti ambayo mwanzo, Idd hakuwa ameelewa ina maanisha nini, akageuka na kutazama huyu aliemshika bega ambae yeye alikuwa anajuwa kuwa ni yule mwanamke alielala nae usiku kucha, alipo geuka na kumtazama akakutana na sura ya ajabu, ambayo hakutegemea kama ndiyo ya mtu aliekuwa amelala pale kitandani, “weeee! yule mwanamke niliekuwa nae jana usiku aliondoka?” aliuliza Idd kwa mshangao na kuinuka haraka kwa mshtuko toka pale kitandani alipokuwa amekaa akivaa viatu, huku macho yamemtoka kwa kumtazama yule mwanamke mzee mwenye sura iliyozeeka kweli kweli, ambayo sasa ilikuwa katika muonekano fulani ambao Idd hakujuwa kuwa lilikuwa ni tabasamu, zaidi yeye alizidi kushtushwa na muonekano ule, ambao ulimfanya atambue kuwa mwana mama huyu hakuwa na meno ya mbele, “mpehi upigi ya asuhuhi” aliuliza tena yule mwanamke, akishindwa kutamka kiufasaha, kuwa “mpenzi haupigi cha asubuhi” kutokana na kukosa meno ya mbele ambayo mpaka sasa yalisha tawanyika pale chini kwa kukanyagwa na Idd, hapo Idd hakujibu kitu zaidi alianza kutembea kuufuata mlango, “bai nihaie ela ya upu” alisema yule mwanamke akimaanisha “basi niachie hela ya supu” lakini Idd sijui hakumuelewa au alifanya makusudi, maana aliondoka zake bila kugeuka nyuma akafungua mlango na kutoka zake.
Moja kwa moja Idd alienda kwenye gari lake na kuingia ndani akaliwasha na kuondoka zake, huku anawaza mambo yaliyo mtokea jana usiku, “niliwezaje kugonga yule mwanamke tena usiku kucha” aliendelea kuwaza Idd akijilaumu kwa kile alicho kifanya, na wakati huo akatazama pembeni ya seat yake akaona mkoba wa Soraya, na hapo ndipo lilipomjia wazo la kuwa ana jambo la kujibu kwa mzee Mahamud, hasa endapo binti yake hakufika nyumbani kwake salama jana usiku, maana kuhusu kulewa hilo alikuwa na uwezo wa kujibu, tena jibu ambalo lingemtetea hata yeye mwenyewe, lakini je aliweza kufika nyumbani na kama alifika, alifika fikaje, yaani alifika salama? hilo ndilo swali lililo mchanganya Idd, kwasababu kwa kilevi alicho muekea Idd alishawahi kuwafanyia hivyo wanawake kadhaa na wote alifanikiwa kulala nao akiwafanyia michezo, michafu kuliko uchafu aliouacha chumba cha hotel, “ila leo nimeingia choo cha wanawake” aliwaza Idd, ambae hofu yake ilikuwa kubwa sana juu ya afya yake kutokana na muonekano wa mwanamke yule, usiulize kuhusu kutumia mipira, huo haukuwa utamuduni wa Idd kutumia vitu kama hivyo.******
Mida ya saa nne Laylah, aliingia nyumbani kwa boss wake akiwa amevaa gauni lake refu baibui, tayari kwa kueleka msikitini hapo baadae kabla hawajaenda shamba kupeleka na kupanda miti ile ya matunda waliyoichukuwa lumecha, akipishana na Talib mlangoni, “vipi kaka Talib, mbona siku hizi hutumii gari lako” aliuliza Laylah, mara baada ya kusalimia na Talib aliekuwa anatoka nje ya geti, “wakati mwingine nahitaji kujizowesha kutembea kwa miguu, si unajuwa magari yenyewe ya watu haya” alisema Talib huku anatabasamu, akionyesha kijiuso cha urafiki, “mh! ni kweli lakini kwa jinsi mjomba wako anavyokupenda hawezi kukunyang’anya” alisema Laylah, ambae alianza kutembea kuingia ndani, “subiri kwanza Laylah, hivi mwenzio jana kilimtokea nini?” aliuliza Talib kwa sauti ya chini, huku akimtazama Laylah na kumsogelea pale aliposimama, “mh! kumtokea nini!, saa ngapi, maana tulivyo toka Lumecha mimi nilienda nyumbani” alisema Laylah, maongezi yao yakiwa ni ya sauti ya chini, “jioni bwana si alitoka na yule fala aliekimbiliaa south” alisema Talib kwa dharau, “nani Idd, ndio alitoka nae, walitumwa bomba mbili, kwani kimetokea nini?” aliuliza Laylah, , ambae sasa hofu ilianza kumtawala moyoni kwake, kwasababu yeye ndie wa kwanza kujuwa kuwa Idd sio kijana mwema, “hata mimi naelewa basi naona vikao vya siri tu, halafu hata Soraya mwenyewe sijamuona toka jana usiku” alisema Talib kwa sauti ya kutokujari, “mh! Idd…” aliguna Laylah, huku anaanza tena kutembea, lakini Talib akamzuwia tena, “mtaenda shambani kweli leo” aliuliza Talib, kwa sauti ile ile ya chini, “kwa kweli sijui, kama kuna jambo baya lilimtokea nadhani hatutoweza kwenda shambani” alisema Laylah kwa sauti ya kutia shaka, “poa basi kama mutaenda shamba utanijulisha nikuagize matogoro, mchana nitakuwa pale chumbani kwangu” alisema Talib, kwa kusisitiza kisha huyooo akaondoka zake na kutokomea mitaani, huku akilini mwake akipanga kutekeleza mpango wake haraka iwezekanavyo.
Wakati Laylah yeye alitembea haraka kuufuata mlango wa nyumba kubwa ya mzee Mahamud, huku moyoni mwake akiwaza ni jambo gani lilimkuta Soraya, Laylah alipomuulizia boss wake nae akaenda kujulishwa, ndipo Soraya akaagiza kuwa Laylah aingie chumbani kwake, ni mara chache sana hutokea Laylah kuingia chumbani kwa Soraya, labda itokee Soraya anaumwa au kuna kitu cha kupeleka, “nimekutana na Talib hapo nje akaniuliza eti Soraya amepatwa na nini?” alisema Laylah, mara baada ya Soraya kumaliza kumsimulia kilicho tokea jana, “kumbe Idd ni mshenzi, kwa hiyo alitaka ukilewa akufanyeje?” aliuliza Laylah, na hapo wote wakacheka kidogo, “ameshindwa na hanipati ng’o” alisema Soraya, ambae sasa alikuwa anamuamini Laylah kuwa ndie rafiki wa pekee aliebakia nae, “kwahiyo una uhakika kuwa yule mkaka ndie mwenyewe kabisa” aliuliza Laylah, “tena sjui hata kwanini najikuta nampenda tu yule mkaka, lakini kwanini anajifanya hanijui” aliuliza Soraya, kwa sauti ya masikitiko, “Dah! Soraya si umesema kuwa ulikuwa umevaa niqab” aliuliza Laylah, na hapo ni kama Soraya alikumbuka jambo, “kweliii nilivaa niqab, ina maana hakunifunua kunitazama usoni” aliuliza Soraya kwa masikitiko, “mh! hata hivyo unadhani akikuona mara moja atajuwa kama wewe ni mtoto wa Mahamud, ujuwe ni watu wachache sana ndio wanajuwa hivyo” alisema Laylah akimgutua Soraya, “mh! kweli Laylah, sasa inabidi leo tusiende shambani tutaenda jumapili, baada yake leo na kesho tuzunguke mitaani, kumsaka huyu kijana” alisema Soraya, hapo Laylah akatabasamu kidogo, “ukimpata utamwambia nini?” aliuliza Laylah, na hapo Soraya akatulia kidogo kama anafikiria cha kumuambia kijana huyo mara atakapo kutana nae, akitumia sekunde kadhaa kisha akaongea akiwa ametazama chini, “hata mimi sijui” alijibu Soraya, kisha hapo kikapita kimya tena, kabla Soraya hajaongea tena, “kwani mimi si mzuri?” aliuliza Soraya, “hakuna asiefahamu hilo, alijibu Lalyah, ambae akauliza swali ambalo Soraya hakulitegemea, “kwahiyo unampenda yule kijana na upo tayari kuwa nae?” aliuliza Laylah kwa sauti tulivu huku akimtazama Soraya usoni, lakini Soraya hakuweza kumtazama Laylah, hata kuitikia kwake aliitikia kwa kichwa akikubari kuwa alikuwa anampenda kijana mpole, “kama amesha oa, itakuwaje?” aliuliza Laylah, “sijui itakuwaje” alijibu Soraya kwa sauti iliyo jaa unyonge.********
Idd alifika nyumbani kwao na kumkuta baba yake akiwa ametulia sebuleni anamsubiri, “haya nieleze imekuwaje, maana nimeshindwa kupokea simu ya bwana Mahamud, kwasababu sijui lolote, na wewe hukuniambia chochote, alisema mzee Mahadhi Salum, mara baada ya mwanae kuingia ndani, “asikuambie mtu baba, ni tatizo lakini nimesha pata jibu” alisema Idd, na kuanza kumueleza kuhusu jinsi ilivyokuwa na ukweli ni kwamba hakuficha hata kitu kimoja, zaidi ya ule ushenzi alioufanya kwa mwamamke muhudumu, pia akampa wazo lake yaani njia ya kutatua lile tatizo, “hapo baba inabidi usimame kama kiungo namba nane ili kuhakikisha mzee Mahamud, anaelewa somo” alisema Idd baada ya kumpa mbinu baba yake, “wala usiwe na wasi wasi, tena mbinu hiyo itaniondoa kwenye aibu kubwa” alisema Mahadhi akiukubali mpango wa mwanae Idd, mpango ambao aliamini ungefaa katika kuweka mambo sawa, “sasa mpigie kabisa mzee Mahamud” alisema Idd, ambae alijihisi kuwa bado anatoa harufu mbaya kwa uchafu alioupata kule Hotelini, “lakini na wewe wakati mwingine, unapo fanya kitu lazima uwe makini bwana” alisema mzee Mahadhi huku anachukuwa simu yake na kupiga kwa mzee Mahamud.*******
Naam habari ya kununuliwa baisker kwa mzee Frank, zilitapakaa mtaa mzima wa Luhila seko, wapo waliomuita mwenye bahati, wapo walio msema vibaya kwamba alisukumwa kidogo na kudai fidia akimuonea yule mschana mdogo mwenye kujiziba uso, hakuna aliemfahamu yule mschana kuwa ni mtoto wa mzee Mahamud, kama ujuwavyo siku zote mschana huyu hujificha sana, kiasi cha watu wengi kutokumfahamu zaidi ya watu wa pale mjini.
Taarifa hizi hazikuwa nzuri kwa mzee Komba na familia yake, sijui kwanini walijikuta wanaichukia baiskeli wanamchukia mzee Komba pia wanamchukia hata mke wa mzee Frank, hawakumbakiza kijana wao, hawakuacha kuwaombea mabaya kila kukicha, walitamani hata siku moja waamke wakute mzee huyu amefilisika na kubakia masikini zaidi yao, hakika maombi yao yalikuwa makubwa sana kiasi kwamba wangetumia kujiombea wao wenyewe ili wafanikiwe yangewasaidia sana.
“Mama Hilda hivi unadhani haya yanayotukuta kuhusu Hilda ni kawaida kweli?” aliuliza mzee Komba aliekuwa na mke wake wanatoka shambani, “mwenzio nilishajuwa mapema sana, tatizo letu huwa tuna tangaza mapema mafanikio yetu, tunasahau kuna watu wanatuonea vijicho” alisema mke wa mzee Komba, yaani mama Hilda, “inabidi na sisi tuhangaike haiwezekani kila mtoto anapo patana na mwenzie wanavurugana ghafla namna hii” alisema mzee Komba akiongea kwa sauti iliyojaa chuki na kuonyesha kuwa alikuwa katika maamuzi ya ukweli, “yaani baba Hilda, sio siri na nikimbaini anaefanya hivyo hakika nitamwambia mganga ampe pigo takatifu” alisema mama Hilda akionyesha kukamia pia, “sio akimbaini, kwani mpaka sasa hatumjui, hapa dawa ni kwenda kwa mganga na kumueleza kuwa amtungue tu” alisema mzee Komba aliekuwa ametangulia mbele mke wake aliebeba vijikuni akifatia kwa nyuma, “kwani wewe unamuhisi nani?” aliuliza mama Hilda kama vile anamtega mumewe, “kuna mwingine zaidi ya wale chuma ulete waliojaza ndondocha dukani” aliongea mzee Komba kwa sauti iliyojaa chuki, akimaanisha ni mzee Frank na familia yake, “hapo umepatia, mi jioni nitaenda kule kwa Mabudi akamkaange mtu!” alisema mama Hilda, akionyesha kuwa alipania kumchawia mzee Frank na familia yake.*****
Kikawaida siku ya ijumaa familia ya mzee Mahamud na wafanyakazi wake wote hutumia gari moja aina ya Toyota hiace kwenda msikitini, kuna wakati dereva anaweza kuwa mama Soraya, au Soraya au baba Soraya huku wengine wote pamoja na Laylah hukaa kama abiria wengine, yaani wale wafanyakazi wa ndani.
Naam leo ikiwa ni siku ya pekee, baada ya kupita miezi mingi sana pasipo kuhudhuria swala yoyote pamoja na familia hii, nae leo alikuwa mmoja kati ya watu waliokuwepo pale nyumbani wakijiandaa kuingia kwenye gari safari ya msikitini, huyu alikuwa ni Talib ambae muda wote alikuwa karibu na Laylah, akivizia kupata habari za safari yao ya kwenda shamba, maana ilikuwa kawaida kwa Soraya kwenda shamba mara baada ya kutoka msikitini, “vipi mtaenda shamba kweli?” aliuliza Talib wakiwa nje ya nyumba hii kubwa ya kifahari ya mzee, wanawasubiria wakina mzee Mahamud mke wake pamoja na Soraya, “leo hatuendi, tutakuwa hapa hapa mjini” alisema Laylah, ambae hakujuwa kuwa lengo la kuulizia kwa Talib halikuwa jema, maana tayari alisha andaa mpango wa hatari dhidi ya Soraya, “kwahiyo mutaenda lini?” aliuliza Talib, kwa sauti ya chini, “amesema tutaeda jumapili” alisema Laylah, na hapo wakakubaliana kuwa kama kweli wataenda jumapili basi Talib atamuagizia Laylah kitu fulani ambacho hakukitaja, “poa basi utanishtua nikupe hela” alisema Talib, wakiendelea kuwasubiri wengine waje ili waondoke.
Wakati mzee Mahamud anatoka ndani ndio muda ambao alisikia simu yake inaita, alipotazama akaona kuwa mpigaji alikuwa ni bwana Mahadhi, kwanza akamtazama mke wake ambae alikuwa anaongozana nae kutoka nje, “Mahadhi huyo anapiga simu” alisema Mahamud kwa sauti ya kuhitaji ushauri, “pokea msikilize anataka kusema nini, mimi nilitaka tumfumanie huko huko msikitini” alisema mama Soraya, ambao sasa walikuwa wametokea nje na kuwakuta wakina Talib wakiwa wana subiria kuingia kwenye gari………… ITAENDELEA
N
Nasubiria kitumbua cha soraya hapa mpka kieleweke😂
[/QUOTE
Kitumbua kimevuka mengi