TEMBELE LA UWANI
SEHEMU YA TISINI
MTUNZI
Mbogo EDGAR
ILIPO ISHIA SEHEMU YA THEMANINI NA TISA : Naam ni kweli swala hili liliwashtua vibaya sana, Mahamud na mke wake, na kuanza kujutia kile walicho kifanya kwa haraka haraka bila kuchunguza na kabla hawaja juwa wafanye nini wakasikia ngurumo ya gari nje ya nyumba yao, hapo wakatazamana kwa macho ya mshangao na wasi wasi, maan wao walishajuwa kuwa wakina Soraya wanakuja na wazazi wazi wa Higgno na Higgno mwenyewe.… ENDELEA………..
“Tunafanyaje?” aliuliza Mahamud kwa sauti ya kunong’ona, huku anamtazama mke wake, “tulia kwanza tusiwaonyeshe kama tuna watilia shaka, si unakumbuka hata nyuma tuliwashuku hivi hivi, lakini tukaja kukuta vingine” alisema mama Soraya kwa sauti ya chini, huku Talib akiwasikiliza kwa umakini japo hakuwa anawaelewa kwanini wanaongea vile, “tatizo shangazi we endelea kuwalea lea, yaani unaongea kwa sauti ya chini kwaajili ya Soraya” aliongea kwa sauti ya juu Talib, ambae hakujuwa kijacho, “hebu funga mdomo wako we mjinga…” alisema mama Soraya kwa sauti ya chini yenye kukalipia, na kabla hajamaliza wakashtuka kusikia nyanyo za watu zikikaribia mlango wa kuingilia sebuleni na wote wakatazama upande ule wa mlango, huku Talib mapigo ya moyo yakianza kumuenda kasi, maana alianza kuhisi kuwa vishindo vile sio vya watu wawili yaani Soraya na Laylah.
Ni kweli macho ya Talib yaliweza kuthibitisha hilo mara baada ya mlango kufunguliwa, aliefungua alikuwa ni Soraya akifuatiwa na Laylah, ambao walivua viatu vyao vya mikanda kwa kutumia miguu yao, nadhani unaweza kuvuta picha kamili, huku nyuma yao wakionekana wageni wengine watatu ambao walikuwa wanavua viatu vyao vya kutumbukiza, nao ni wanaume wawili na mwanamke mmoja, “msala” alinong’ona Talib, huku anainuka toka kwenye kiti pale kwenye meza kubwa ya chakula, akisahau hata kunawa na kuanza kutoka kuelekea upande wa mlango wa nyuma, “we! Talib unaenda wapi baada ya kusubiri kuwasalimia wageni” aliuliza mama Soraya, kwa sauti iliyojaa mshangao, lakini Talib aliekuwa kama amekimbizwa au teja aliemuona polisi hakugeuka wala kusimama, ndio kwanza akaongeza speed ya kuufuata mlango ule, ambao aligunduwa kuwa umeshafungwa mara baada ya kuufikia, ni kwamba mlango ulifungwa na kutolewa funguo toka lilipotokea lile utukio la jana usiku.
Hivyo Talib akageuka na kutazama alikotoka, akawaona wageni wale watatu ambao aliwafahamu mara moja kuwa ni Higgno na wazazi wake, hapo Talib akaona kuwa akizubaa anaumbuka kweupe kabisa, akatazama kushoto na kulia kama kuna mlango anaweza kuingilia ili asikutane na mzee Frank, ambae aliamini kuwa lazima atamkumbuka kuwa alienda kumsumbua pale dukani kabla ya kwenda kuchoma moto duka lake usiku, lakini hakuona mlango ambao anaweza kuingia kujificha, maana kila mlango alio uona ulikuwa ni wachumba cha mtu tena ambacho hatakiwi kuingia hata kwa bahati mbaya, na vilivyo bakia ni vya wageni, ambavyo lazima vilikuwa vime fungwa na funguo, hivyo akaona kama mbwai na iwe mbwai.
Talib aligeuka na kutazama sebuleni alikotoka, ambako aliwaona wageni wao wakiwa wanaingia sebuleni na kuanza kusalimia na shangazi yake na mjomba wake, ambao bado walionekana kuwa katika mshangao juu ya yeye Talib kwa kile alicho kionyesha, Talib akaona atumie nafasi hiyo kupita pale sebuleni na kutokea mlango mkubwa kuelekea nje, hivyo akapiga hatua za haraka kueleka sebuleni kwa lengo la kupita haraka sebuleni huku akisikia wageni wale wakisalimiana kwa sauti za furaha na kusimuliana mambo ya huko kijijini, “kwa kweli leo nimejiona kama mke wa mfalme jinsi watu walivyojaa barabarani kutushangaa” alisimulia mama Soraya, kwa sauti iliyochangamka kweli kweli.
Naam Talib alipokaribia pale sebuleni akakutana na wakina Soraya na Laylah, ambao walikuwa wanaelekea chumbani kwa Soraya, “we kaka Talib vipi mbona kama unahangaika?” aliuliza Soraya kwa sauti iliyoonyesha mshangao wa kudhihaki, ila ukweli hakuwa anashangaa, maana alikuwa anajuwa ni kwanini Talib alikuwa katika hali ile, swali hili japo alikujibiwa na Talib ambae aliendelea kutembea kuelekea sebuleni liliwashtua wakina mzee Mahamud na kuwafanya wote waliokuwepo pale sebuleni kutazama kule alikotokea Talib.
Naam hapo macho ya mzee Frank yalikutana na na macho ya Talib, na kumfanya Talib akwepeshe macho kwa mashaka makubwa aliyo kuwa nayo, huku mzee Frank akitoa macho ya mshangao na wakati huo Soraya na Laylah walikuwa wamesimama wanatazama mwisho wa Talib, “we! Talib hebu simama hapa, kwani una nini wewe unashindwa kuwasalimia wageni” alisema mama Soraya kwa sauti kali zaidi, yaani alimkalipia mtoto huyu wa kaka yake pasipo kujari wageni, lakini bado Talib hakutaka kusimama, “kwani huyu ni kijana wako pia?” aliuliza mzee Frank kwa mshangao, na hapo Talib akaona kuwa mzee Frank anataka kuharibu kabisa, hivyo akazidi kutembea kuondoka eneo lile, ambalo sasa alikuwa kati kati anakatiza, hisia zikiwa tofauti kwa Mahamud na mke wake, ambao walihisi kuwa Talib na mzee Frank ni kweli wanafahamiana na ni kweli mzee huyu ni tapeli kama anavyosema Talib, “kwani unamfahamu huyu?” aliuliza mzee Mahamud kwa mshangao wa tahadhari, “ndiyo ni yeye kabisa, ndie kijana aliekuja kunitishia na mwisho kuchoma duka langu” alisema mzee Frank na hapo ghafla mama Soraya akasimama, “weee! Talib hebu simama, na uje ukae hapa, ukitoka humu ndani na uondoke moja kwa moja nisikuone tena” ilikuwa ni sauti kali iliyojaa hasira kali sana, “tatizo shangazi unamsikiliza huyu tapeli” alisema Talib huku anapunguza mwendo na kusimama, watu wote wakaachama midomo kwa mshangao, hasa wakina Higgno na wazazi wake, “we Talib, huoni hata aibu, huyu baba amekutapeli nini, wewe si ulisema Higgno alikuvurugia mipango yako ndio maana umechoma duka lake moto” alisema Soraya, ambae aliunganisha simulizi na matukio ya kijana alie enda kumtishia mzee Frank dukani kwake, “we! Soraya lazima umtetee huyu mzee si wamesha kuroga” alisema Talib kwa sauti ya kali yenye upinzani, “hebu tulieni kwanza jamani mbona munatuchanganya, mara tapeli, mara kuchoma duka la watu, samahani mzee wangu hebu tuelezee ulikuwa unamfahamu vipi huyu Talib” alisema mzee Mahamud na hapo mzee Frank akaanza kueleza jinsi ilivyo kuwa siku ile ambayo duka lake lilichomwa moto, huku soraya akisogea sebuleni kusikiliza mkasa huo.*******
Naam Mzee Mahadhi akiwa hajuwi kilichotokea usiku, aliamka na kujiandaa kuelekea dukani kwake na alipotoka nje kutazama gari hakuliona, hivyo hakutaka kuhoji na kuondoka zake kuelekea kazini kwake, kitu ambacho hakukijuwa ni kwamba kijana wake Idd alikuwa anamsubiri atoke ili na yeye awasiliane na Talib ili wakawaone wale vijana wengine kama walifanikiwa kuondoka na fedha ili wakagawane na wao wakimbilie msumbiji.
Mahadhi alifika dukani kwake na kufungua kama ilivyo kawaida, huku akiwa na hamu kubwa ya kikao cha mchana wa saa saba, ambacho kingemsimanga Mahamud kwa kukubali kijana ambae sio muisilam kumchumbia binti yake, ukweli muda kila ulipozidi kwenda ndipo alipoanza kusikia habari za kuwa kuna tukio lilitokea jana usiku nyumbani kwa Mahamud, na kwamba jaribio limeshindwa la kumvamia na kumuibia, pia alizidi kupata habari ambayo ilianza kumchoma moyo wake kama ile ya kuwa mkwe wa mzee Mahamud ndie aliefanikisha kuwazuia wale majambazi, ambao mmoja kati yao alifanikiwa kumbia huku wengine sita wakitiwa mbaroni pamoja na vyombo vya usafiri walivyo vitumia ikiwa ni gari moja na pikipiki mbili.
Huwezi amini kama Mahadhi hakuhisi chochote kuhusu mwanae na gari lake kuhusika kwenye tukio lile, mpaka aliposhtuka kuona gari la polisi likija na kusimama dukani kwake, kisha polisi kumtangazia kuwa kuanzia muda huo yupo chini ya ulinzi wa jeshi la polisi, “kwalepi tena jamani, mbona fitina zishaanza jamaaa” alilalamika mzee Mahadhi, huku mawazo yake yakimpeleka kwenye kitendo cha kuandika ujumbe mfupi wa simu na kuutawanya kwa lengo la kumchafua Mahamud, “mzee unatuhumiwa kuhusika na tukio la uvamizi wa nyumba ya bwana Mahamud na kujaribu kuiba, baada ya gari lako kukutwa eneo la tukio na jitihada zinafanywa kumnasa Idd Mahadhi, ambae inasemekeana alikuwa ndie dereva wa gari hilo” alifanuliwa bwana Mahadhi kama ilivyo sheria na hapo ndipo akili ilipomkaa sawa, kwanza alikumbuka kuwa kijana wake ni muharifu kweli kweli, maana hata huko msumbiji alikuwa anaishi kwa kufanya uharifu, pia akakumbuka kuwa sio tu kuliona gari lake hata Idd hakuwa amemuona toka alipo achana nae jana asubuhi wakati anaenda dukani, na mara ya mwisho kuwasiliana nae ilikuwa ni jioni ya jana alipo mueleza kuhusu kuchumbiwa kwa Soraya.
Mahadhi alipewa nafasi ya kufunga duka lake na kupandishwa kwenye gari la polisi, safari ya ikaanza kueleka nyumbani kwake kumfuata Idd, huku njia nzima Mahadhi akiijutia nafsi yake kwa kumuendekeza Idd kijana wake, ambae nae alikuwa ndio kwanza bado amejikunyata kitandani huku anaugulia maumivu ya ng’olewa jino, kwa ngumi, nae bila kusita akamtaja Talib, kuwa ndie msusi wa mipango yote ya kumwibia mjomba wake, hivyo polisi mala baada ya kuwaacha wakina Mahadhi kituoni, wakaanza safari ya kueleka nyumbani kwa Mahamud, wakiwaacha Idd na baba yake wanachukuliwa maelezo, ambayo yalimsaidia Mahadhi kuachiwa muda mfupi baadae, baada ya kujieleza kuwa yeye akuwa anajuwa lolote kuhusu mpango huo, na kwamba gari alikuwa nalo kijana wake na akujuwa kama anaenda kulitumia kwenye uharifu.********
Naam baada ya mzee Frank kueleza jinsi alivyo kutana na Talib, huku mzee Mahamud akikumbuka kuwa siku hiyo tajwa, alimuona Talib akirudi nyumbani usiku kwa mwendo wa kuvizia, lakini Talib alipinga vibaya sana, “anko huyu mzee nimuongo sana tena tapeli, anajuwa kupanga uongo wake mpaka munaweza kumuamini” alisema Talib huku anaanza kuondoka, “usiondoke Talib, ukiondoka tu usije ukarudi kwenye nyumba hii” alifoka mama Soraya na wakati huo Soraya ametulia kimya kabisa anawasikiliza, “hebu niambie siku ile usiku ulikuwa unatokea wapi?” aliuliza Mahamud kwa sauti ya upole, mara nyingi hakupenda kumfokea Talib, “anko mimi nilikuwa na mishe zangu tu! wala sikwenda huko, nyie hamuwajuwi hawa ni waongo sana” alisema Talibu macho yakiwa makavu kabisa, usinge dhania kuwa alikuwa anahusika kwa asilimia mia moja na uharifu uliotokea kwenye duka hilo la mzee Frank, “hakika Talib unanishangaza sana, ni kitu gani kina kufanya uchome duka la watu” aliuliza Mahamud kwa mshangao na masikitiko makubwa, hapo Talib hakuweza kujibu lolote, akabakia ameinamisha kichwa chini, “ona sasa, leo hii unao wafanyia hivyo ndio wanakuja kuwa ndugu zako, umepata faida gani? au Higgno alikuvurugia mipango gani?” aliuliza tena Mahamud na hapo japo Talib alijuwa jibu sahihi la swala hilo, lakini alitoa jibu lake, “anko tatizo hamtaki kunisikiliza, hawa kuna watu watakuwa waligombana nao tu katika utapeli wao ndio wakawalipizia kisasi, na kwa kuwa mimi nilipita mchana wanaamua kuni singizia” alijitetea Talib bila hata chembe ya aibu, “hivyo ndiyo utakavyoenda kueleza polisi?” aliuliza mama Soraya kwa sauti ya ukali, na kuona hivyo mzee Frank akaona isiwe shida, “lakini mzee Mahamud, nadhani tufanye kama yamepita, maana tumesha kuwa familia moja, siwezi tena kwenda kutoa taarifa polisi kuwa nime muona kama nilivyo agizwa, ila naomba tu kijana ajirekebishe” alisema mzee Frank kwa sauti ya upole, unaona wenzako walivyo na moyo wa kusamehe, sasa wewe ni kitu gani ambacho Higgno alikukosea mpaka ukachome duka la baba yake?” aliuliza mama Soraya kwa sauti ya kusimanga iliyojaa masikitiko, “shangazi nilisha sema toka mwanzo huyu mzee ni bingwa wa kugeuza maneno, huyu ni tapeli, na alichotaka ni Higgno amuoe Soraya, anasema mimi nilisema amenivurugia mipango yangu anaweza kunivurugia mipango gani huyu masikin….” alisema Tarib kwa sauti iliyojaa ujeuri na ukizingatia alikuwa na hasira na Higgno, ambae ni mara ya pili alikuwa anamvurugia mipango yake, hapo kwa mara ya kwanza Soraya akafungua mdomo, “unajifanya hujui ni mipango gani alikuvurugia, sema unajifanya huijui niitaje” aliuliza Soraya huku anatoa simu kwenye mkoba wake, nilie ambayo iliokotwa kwenye tukio la uvamizi kule shambani, kisha akaipiga namba ya Talib mwarabu, ambayo ilikuwa juu kabisa, huku kila mmoja akidhania kuwa Soraya alikuwa anapiga simu kwa mtu ambae anaweza kutoa ushahidi, na hapo simu ya Talib ikaanza kuita kutokea mfukoni mwake, unajuwa nini kilifuata?
Ni katika hali ambayo Talib hakutegemea kabisa, kuwa simu ile aliyopiga Soraya ndio ilikuwa inaita mfuko mwake, na yeye akidhania kuwa ni Idd au mtu mwingine anampigia akatoa simu yake na kuitazama haraka haraka akaona jina Zido, akukumbuka kuwa simu ile ilisha potea kule shamba, unajuwa nini wewe sema kama unajuwa” alisema Talib, huku anaikata simu ile na kuiweka tena mfukoni, kwasababu asingeweza kuongea na Zido huku akiwaza kuwa wenzake wamesha achiwa au Zido hakukamatwa kama wenzake, “sema mbona kimya sasa” aliongea Talib huku watu wote wakimtazama, maana walishaona kuwa amepigiwa simu na Soraya na kuikata.
Na kama haitoshi Soraya akapiga tena, na ile simu ya Talib ikaanza kuita tena toka mfukoni mwake, Talib akaitoa tena na kuitazama akaona jina lile lile Zido, na hapo ndipo akili ilipomkaa na kukumbuka kuwa simu ile ilishapotea muda mrefu, tena ilipotea kwenye tukio la utekaji wa Soraya, akili ikamtuma kumtazama Soraya na alipomtazama akamuona ameishikilia simu mkononi, huku simu ile ikiendelea kuita, Talib akawatazama shangazi na mjomba wake, akawaona wanamtazama kwa macho ya sitofahamu, akawatazama wakina Higgno na wazazi wake pamoja na Laylah, nao walikuwa wanamtazama yeye ambae alikuwa ameishikilia simu ambayo ilikuwa inaendelea kulia, “ndio nini, sasa hiyo simu inanihusu nini?” alisema Talib kwa sauti ya kufoka, “unajifanya huijui? sema sasa unajifanya huijui? kwa taarifa yako hii ndio simu ambayo ulikuwa unatumia kupanga mipango ya kuniteka na kuniuwa, na ndio mpango ambao unasema Higgno alikuvurugia, kataa sasa kama nakusingizia” alisema Soraya kwa sauti ya juu na ya ukali pia, akiwaacha wazazi wake midomo wazi huku wakimtazama Talib kwa mshangao mkubwa, “we Soraya unaongea nini?” aliuliza mama Soraya kwa sauti iliyojaa mshangao na butwaa, “mama jana sikutaka kuongea mbele ya polisi, kwasababu ungesema namuonea” alisema Soraya huku ana weka sehemu ya messeji kwenye ile simu, “hii ndio simu ambayo wale watekaji walikuwa wanawasiliana na baba siku ile, tazameni hizi messeji halafu angalieni namba iliyo zituma hizo messeji” alisema Soraya huku anamkabidhi mama yake simu ile.
na hapo Talib akaanza kukumbuka jinsi alivyokuwa anatuma sms kwa zido kusisitiza kumuuwa Soraya mara tu watakapo kamilisha mpango wao, pia alipo wajulisha kuhusu mpango wa mjomba wake kuwajulisha polisi, Talib akawatazama shangazi yake na mjomba wake, ambao wote kwa pamoja waliinamia simu na kuanza kusoma sms zile zilizotumwa na mtu alieseviwa kwa jina la Talib mwarabu, “jamani jamani, hebu njooni muone huyu mtu, kweli unaweza kufanya hivi kwa ndugu yako” alilalamika mama Soraya, huku wakiwaita wakina mzee Frank nao wasogee, nao wakavutika pamoja Higgno na wakina Soraya, “huyu ni muuwaji mkubwa, na hiyo ya mwisho aliwaambia kuhusu funguo si munaona” alisema Soraya kwa sauti iliyojawa na msisitizo, “kaka atanisamehe kwahili, huyu namfunga akaozee jela maisha yake yote” alisema mama Soraya huku wanainuwa nyuso zao kumtazama Talib pale alipokuwa amesimama, hakika mtu sio panzia ya kwamba unalifunua unavyotaka..... ITAENDELEA