SEHEMU (18)
ILIPOISHIA.
"Nilikuwa nashirikiana na Wenzangu wawili Manyege
na Mgusi "
Jumanne alisema. Alimsahau Faustin kabisa
kumsema kwenye kundi lile la watu wenye Hasira.
"Na Faustin?"
Uliulizwa tena kuusu Faustin.
"Huyo alikuwa ajui Chochote kuusu mauaji ya watu,
alikuwa anashirikiana nasi kwa vingine tu lakini
alikuwa auwi kabisa"
Jumanne alisema.
SONGA NAYO.
Faustin anamungu wake Hakutajwa kabisa kama
naye alikuwa muhusika katika mauwaji.
"Jamani ameficha kitu?"
Kidume kilichokuwa mbele kama kiongozi
kiliwauliza, mkononi kilikuwa kimeshikilia panga.
"Bado kaficha hajatwambia ni wapi walikuwa
wanawapereka baada ya kuwaua"
Wananchi walisema.
"Umesikia Kumbe bado hujasema wapi huwa
mnawapereka"
Kidume kile kiliinama na kumuuliza Jumanne.
"Tulikuwa tunawakata matiti na kuyaperekea
mashetani wa Kisiwa cha Shetani. Huko ndiko
tuliyachukua madini, na ndiko tulimchinjia Mtoto wa
Dada yangu. Yeye yumo humo ndani, naye nilitaka
kumuua, Mimi mwenyewe ndiye nilimuua na Mume
wake"
Jumanne alisema na alizidi kuufungukia ukweli.
"Aaaaaa!"
Watu hawakuamini kabisa kabisa alichokizungumza
Jumanne.
"Sasa baada ya kufanya hivyo miili yao mlikuwa
mnaipereka wapi?"
"Humo ndani ya majumba yetu na Guest pamoja na
Hoteli yetu kuna mashimo marefu ambayo huwa
tunaitumbukiza miili tukiisha maliza kukata maziwa"
Jumanne alisema tena kipindi hiki hakuacha hata
kimoja, aliusema ukweli wote, ukweli ambao kila
mtu alistaajabu sana, wengine wakawa wanajiuliza
kaupata wapi Ujasiri wa kuweza kumchinja mtoto
wa dada yake, Mume wa Dada yake halafu pia
alitaka kumchinja Dada yake.
Baada ya ukweli wote Jumanne alinyanyuliwa na
Bausa lile mpaka ndani akawaoneshe shimo hilo
lilivyo. Waliingia mpaka kwenye Chumba
kilichokuwa na Shimo, bado Mama Fatuma alikuwa
ndani ya chumba hicho ajitambui kabisa hata
kamba alizokuwa amefungwa mikononi zikiwa bado
zimemfunga. Kitendo kile kiwasikitisha sana watu
waliofanikiwa kufika chumbani, walimfungilia Mama
Fatuma kamba alizokuwa amefungwa kisha
wakamtoa inje kwenye upepe na kuanza kumpepea
kama angeweza kurudi katika hali ya kawaida.
Ndani Chumbani walikisogeza kitanda pembeni,
walipokisogeza walikuta kuna visu viwili vikubwa na
vilikuwa ni visu kweli kweli.
"Mh! Kweli ninyi mlikuwa ni wauwaji"
Mwanaume mmoja alisema.
Haya na hilo Shimo liko wapi?"
Jumanne aliulizwa, Kwa Jinsi mfuniko wa shimo lile
ulivyokuwa umedizainiwa kama sura ya vigae
vilivyokuwa ndani ya Chumba hicho, ilikuwa si rahisi
kwa mtu kuiligundua kwa kukurupuka, umakini
uliitajika sana ili kuligundua shimo hilo.
Alipoulizwa alionesha na mwenyewe akalifungua.
Alipolifungua shimo hilo, kidogo watu wakimbie
ndani ya Chumba hicho ilifumuka harufu nzito kweli
kweli kutoka katika miili ya Marehemu.
Watu waliziba pua zao ilimradi tu wapate
kuchungulia ndani ya Shimo hilo ili wapate
kushuudia urefu wa shimo hilo na miili mingapi
ilikuwemo. Ndani ya shimo hilo kulikuwa Giza,
ilikuwa si rahisi kuona mwisho wa shimo hilo bila
mwanga. Watu walifuata tochi zao kwenye miji zao
kwa ajili ya kumlikia ili wapate kushuudia ndani ya
shimo. tochi moja nayo ilikuwa haitoshi walitumia
tochi zaidi ya tatu, walichokutana nacho mule kweli
walisikitika sana, miili ya watu ndiyo ilikuwa
ikionekana ikiwa inatembelewa na Funza tu,
kwakweli watu waliumia sana, hapo Hapo baadhi
wakajigawa wengine wakaenda nyumbani kwa
Manyege na kwa Mgusi,
Haikupita hata Robo saa Mgusi naye akaletwa pale
pale kwa Jumanne, akaungaunganiswa. Mgusi naye
tayari alikuwa na kesi mbili za kujibu kwasababu
alikutwa na mwili wa Dada yake, ukiwa na kisu
tumboni kwa maana hiyo watu walijua moja kwa
moja kuwa yeye ndiye aliyeua. Halafu kwa Mgusi
watu hawakusumbuka kabisa kumkamata kwani
mpaka anakamatwa yeye bado alikuwa yupo kama
zezeta. Watu walijikusanya wengi sana nyumbani
kwa Jumanne. Japo kuwa viwanja vyao vilikuwa
vikubwa havikutosha watu kuingia ndani ya uzio wa
ukuta uliokuwa umelizunguka jengo la Jumanne,
hivyo watu walipanda juu kwenye ukuta wakakaa ili
wapate kuwashuudia watumwa wa shetani. Kama
kawaida hata waandishi wa habari nao walikuwa ni
miongoni mwa watu waliokuwepo kwenye tukio hilo
wakichukua taarifa zao. Police hakurusiwa kusogea
pale, watu walikuwa tayari wapigwe mabomu ya
machozi lakini watu wao wawafaidi wenyewe.
Manyege hakupatika kwake kwa muda huo lakini
watu walijua kabisa kakimbia. Kukimbia kwake
hakukuwa na tiketi ya watu kumwacha. Kila mmoja
alisema.
"Ndani ya Ukelewe hii utaenda wapi Shetani
manyege, utakamatwa kabla hujafika popote" muda
huo waliwapigia simu watu wa sehemu tofauti
katika vijiji vilivyokuwa Jirani na Nansio ili waanze
kumsaka, hasa hasa waliopewa taarfa walikuwa ni
dareva Bodaboda. Kwani hata taarifa za kukamatwa
zilichelewa, mule mule ndani ya Nansio alikamatwa
hata kabla hajaivuka.
Baada ya kukanatwa naye alishushiwa kipigo cha
maana kisha akaletwa kwa wenzake. Bahati mbaya
zaidi muda huo huo Dada yake Jumanne (mama
Fatuma) aliamka kutoka katika kupoteza fahamu.
Alipo amka alishangaa kukuta mkusanyiko mkubwa
wa watu wengi nyumbni kwa kaka yake.
Hakiamungu mwanamke yule alikuwa Kama vile
ameshituka kutoka usingizini baada ya kuota ndoto
kama vile mwanaye anachinjwa, alipiga kelele za
kumuomba mwanaye huku akilitaja jina la kaka yake
amrudishe mwanaye. Mama Fatuma alijikuta
anapiga makelele mengi huku akisogea alipokuwa
kaka yake, alikuwa akitembea huku akiyumba
yumba, kwasababu ya alichokuwa amekisikia kutoka
kwa watu wale kuwa mwanaye kaisha fariki kilimpa
hasira sana, alipomuona tena kaka yake, Mama
Fatuma kwa hasira alizokuwa nazo alijikuta
anaanguka chini mzima mzima kama mzigo wa
kumi ndiyo uliotupwa chini na kupoteza tena
fahamu kwa mala nyingine. Pale pale watu
wakambeba na kuanza kumpepea tena, lakini
haikusaidia hali yake ilionekana kuwa mbaya zaidi
ndipo walipochukua maamuzi ya kumkimbiza
hospitali pale Nansio kwa ajili ya matibabu.
Nyumbani kwa Fausitin Dada yake naye alikuwa
kaisha jiua kwa sababu halijihofu kuwa hata yeye
anaweza kuunganishwa kwenye kesi ya Mauwaji.
Watu walipokwenda ili kijithitibitishia walikuta Dada
mtu kaisha fariki, lakini walipofanya upekuzi napo
pia walilikuta Shimo ndani ya Nyumba yake, harafu
miili ya watu ikiwa mule mule. Mbali na hilo hata
Chumba cha kuwasiliana na shetani nacho
walikinasa.
"Hapa hakuna cha Faustin naye lazima akamatwe
aunganishwe."
Wanaume wa kazi waliokuwa wanaifanya kazi ya
upekuzi walisema.
Lakini kilichokuwa kinaleta utata ni wapi Faustin
yupo, muda huo huo walijaribu kufuatilia
wakagundua kuwa Faustin yupo Mwanza.
"Mwanza! Kumbe mwanza hapo tu ngoja
tutamuibukia"
Bausa aliyekuwa kama ndiye kiongozi wa watu wote
pale alisema. Baada ya kusema hivyo aliamuru
Jumanne na wenzake wafungwe kamba ndefu kisha
wawafunge kwenye pikipiki halafu wawavurute
kutoka nyumbani pale mpaka eneo la wazi kabisa
kwa ajili ya zoezi lingine lililokuwa linawafaa.
Walivutwa Mpaka kwenye eneo zuri lilokuwa pana
kisha wakafungwa kamba wote kwa pamoja, halafu
kilicho fuata kila mtu aliamuriwa achukue Jiwe
Dogo Dogo ambalo siyo zito lenye uzani kama
Nusu kilo kisha asogee na kuwaponda mpaka
watakapo kufa. Lilikuwa ni zoezi Gumu sana lakini
kwa watu wenye hasira lilikuwa ni Zoezi jepesi tu,
watu waliyakusanya mawe tena mengine yalikuwa
na zaidi ya kilo mbili na kusogea kuwaponda,
walipondwa na kundi kubwa la watu waliokuwa zaidi
ya Elfu moja na mia tano.
Kwa kiasi hicho kikubwa cha watu kilichotokea pale
ni Maiti tu ndizo zilisalia. Lakini bado watu
hawakurizika walikusanya kuni na matairi ya kwenye
magari yao yakachomolewa kisha wakawakunjia
kwenye hayo hayo matairi, wakawamwagia mafuta
wakawaunguza. Watu waliamini kuwa bila
kuwaunguza watu kama wale wanaweza kurudi tena
katika Dunia na kuyafanya waliyokuwa wanayafanya.
"Bado Faustin ajiandae lazima naye akipate
kilichowakuta wenzake"
Bausa aliyekuwa anawaongoza wenzake alisema.
Baada ya kumaliza kuuwasha moto, watu waliamia
tena kwenye majengo ya watu wale nayo
yakawashwa moto, palikuwa hapatoshi ndani ya
Nansio. Walibomoa kila kitu kilichowahusu watu
wale, Hoteli, majumba yao, Magari yao, maguest
yao, hata ambayo yalikuwa yamesambaa sehemu
zingine nao yaliunguzwa, mitumbwi na makokoro
yao ya kuvulia dagaa navyo viliunguzwa ndani ya
Nusu saa.
Kufikia mida ya saa nane kilichokuwa kimesalia
kwenye vichwa vya watu ni hadithi tu kuusu vifo vya
Jumanne na timu yake.
Kwa bahati mbaya kilichotokea usiku wa siku hiyo
ni kwamba Mama Fatuma alifariki. Kesho yake watu
walizipokea taarifa za kifo cha mama huyo kwa
masikitiko makubwa sana, hawakuamini kama kweli
mama yule alifariki, iliwauma na ikawauma sana,
tena kilichowauma watu sana ni kwamba kifo chake
kilisababishwa na ushetani wa kaka yake.
"Mungu ailaze roho yake mahara pema peponi"
"Amiin, kaacha watoto wawili wa kike na wakiume"
"Mimi kaniuma sana Mama Fatuma, kwakweli
alikuwa mwanamke mwenye moyo wa aina yake"
Hayo yalikuwa ni baadhi tu ya mazungumzo ya watu
waliozipokea taarifa za msiba wa Mama Fatuma.
Yalikuwa ni maumivu makubwa hasa kwa watoto
wake Sadick na Sauda walipozipata taarifa za kifo
Cha mama yao.
Watoto wale walikuwa wanalia tu muda wote, hasa
Sauda yeye alizimia mala mbili katika siku hiyo,
Mama yao aliwaaga kuwa anaenda kwa kaka yao na
aliwaahidi kuwa angerudi siku hiyo hiyo lakini
kumbe alikuwa anaenda kufa. Watoto wale iliwauma
iliwauma.
Mbali na watoto wake hata Baba na Mama yake
ambao umri ulikuwa ushawaacha na walijaaliwa
kuwa na watoto hawo wawili Mama Fatuma na
Jumanne au Shetani.
Wengi sana waliudhulia katika mazishi ya Mama
Fatuma, Mama aliyewaumiza watu karibu wote
kwasababu kifo chake kilisabishwa na kudai haki
yake.
Kutokana na hasira ambazo watu walikuwa nazo
waliamua moja kwa moja wakapanda mitumbwi yao
wakaingia majini, moja kwa moja kuelekea mwanza
kumtafuta Faustin hawakuwa na mzaa kabisa,
kwasababu ushetani wao ndiyo ulio sababisha
kuawa kwa watu ambao hawakuwa na hatia.
Walikuwa ni kikundi cha watu zaidi ya amsini
waliokwenda mwanza kumtafutaFaustin. Watu wale
walifika mwanza salama. Taarifa za watu hao
Faustin alizipata vizuri sana hata kabla hawajafika
Mwanza, hapo faustin aliomba aende akawapokee
wakerewe wenazake.
"Faustin mpenzi wangu utauliwa"
Loveness alimwambia faustin kipindi faustin
anamwambia kuwa anaenda kuipokea timu
iliyokuwa imekuja kumsaka.
"Usijali loveness kipenzi changu, kama nikifa basi
mungu atakuwa ametaka kwasababu mimi nilikuwa
mfanya dhambi, kwahio dhambi zangu ngoja
zikalipwe kwa damu yangu, lakini kama mungu
hajapenda nitarudi na nitaishi na wewe"
Hilo ndilo jawabu ambalo Faustin alimwambia
Loveness kisha akaenda kuwapokea. Yeye ndiye
alikiwa wa kwanza kufika kirumba mwaloni.
Kweli fauatin alikuwa amejiandaa kuwapokea vizuri
tu. Watu kutoka Ukerewe walipo fika kirumba
mwaloni, Faustin aliwaona akawasogelea, ilimuuma
hata yeye lakini alilazimika ili kuilipa dhambi yake,
kwakuwa muda huyo alikuwa kaisha kuwa mrokore
safi tena ndani ya muda mfupi wa siku mbili.
Faustin akisogea kuwapokea watu wale, Loveness
naye alikuwepo pale ila mbali kidogo akimuombea
mchumba wake kwa mungu aweze kuepukika na
kifo kwani aliamini kabisa kuwa kaisha kuwa
mtumikiaji wa mungu. Richa ya kuwa Faustin
aliwasogelea watu wale na kuwasalimia tena kwa
kiruga cha kwao lakini watu wale walishindwa
kumtambua kabisa kama ni yeye badala yake wao
walimfanya msaada kwao wa kumtafuta Faustin.
Faustin mwenyewe alijishangaa kabisa, mpaka
akawauliza mnaye mtafuta mnamjua. Wao
wakasema ndiyo, hapo Faustin alipata ujasiri wa
kuwambia kuwa hakuwahi kumuona. Hiyo ndiyo
ikawa ponapona ya Faustin, imani yake ilimponya,
watu walimtafuta sana Faustin bila mafanikio,
Mwisho wakarudi zao Ukerewe wakiamini kabisa
kuwa Faustin huwenda alijiua.
Baada ya matukio hayo Faustin na Loveness
walimua nao kusafiri mpaka Ukerewe kwao na
Jumanne kwa ajili ya kuwapa pole. Kwa machungu
waliyokuwa nayo Faustin na Loveness walijitolea
kuwasaidia watoto wa Marehemu kwa hatua yeyote
ile ambayo wangeifikia. Maisha ya Faustin
yalibadilika yakawa kwa mungu kitu ambacho
kilisababisha hata ndugu zake kutomtambua kabisa,
alichokuwa anakifanya yeye aliwasaidia ndugu zake
na wazazi wake kwa moyo wake wote huku akiamini
siku moja mungu atawafunulia ukweli. IAMINI
IMANI YAKO ITAKUPONYA KWA MUNGU.
ALLAH YU PAMOJA NASI KWA NJIA NJEMA.
Mwisho.