Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 153,020
- 454,039
Mtunzi: Ally Katalambula
Katika dunia ya Mungu kuna mambo mengi ambayo ukihadithiwa unaweza kuona na simulizi ya kutunga na kusisimua. Lakini siku zote kila isifue mvua basi imemnyea. Dunia umezungukwa na siri nzima ndani ya majumba ya watu kuna mambo mazito ambayo ni chukizo la muumba.
Si kila mwenye maisha mazuri au matajiri mali aliyopata kaipata kihalali, wengi wao utajiri wao unatokana na nguvu za kiza utajiri anaoambatana na kutoa kafara ya kitu. Wapo wanaotoa watoto, wake au waume zao, pia wapo wanaowageuza watoto, wake au waume zao kuwa mandondocha kama chuma ulete wa kuwaongezea kipato.
Nyumba nyingi huwa na vyumba vya siri ambavyo huwa havifunguliwi kutokana na masharti ya mganga na kufanya watu wabaki na maswali.
Pia nyumba nyingine unakuta kuna mtoto ambaye akili zake si nzuri akikaa yupoyupo mate yanamtoka ovyo kumbe ni dawa ya utajiri. Ajabu huyo ndiye anakuwa kipenzi cha baba ambaye anajua siri yake.
Wapo ambao huambiwa kama mtoto huyo atakufa basi na utajiri nao unayeyuka, ni mambo mengi yaliyoizunguka jamii na uchafu wa tamaa za watu kutaka utajiri kwa njia ya mkato na kujikuta wakifanya uchafu au ukatiri mkubwa bila kuwa na huruma ili tu wapate utajiri.
Nayasema haya nikiwa na uchungu mkubwa baada ya baba yangu kutugeuza chumaulete kumuingizia pesa bila kujua. Nayasema haya baada ya kuteseka zaidi ya miaka saba bila kujua kumbe mateso yangu ndiyo yalikuwa chachu ya utajiri wa familia yangu.
Toka nilipoanza kupata matatizo yaliyopelekea mateso kila kukicha hata siku moja sikuruhusiwa kwenda hospitali zaidi ya kutumia dawa za kienyeji zisizo punguza maumivu na si kuponesha.
Miaka saba nyuma tatizo kama langu alikuwa nalo dada yangu ambaye nilimfuata mara ya nne ambaye sasa hivi ni marehemu.
Mwanzo nilipomuona dada nilijua ni kidonda cha kawaida japo kilinishangaza kichukua muda mrefu toka nikiwa na miaka sita mpaka nilipokuwa na utambuzi kujua kuwa dada yangu anateseka na kidonda kile ambacho kilikuwa hakiponi.
Miaka tatu baadae nilisikia ugomvi mkubwa kati ya baba na dada, nilijificha na kumsikia dada akisema.
“Nimechoka siwezi kuteseka wakati wenzangu wanafaidi kwa mateso yangu, siolewi sina maisha mazuri kama wenzangu niponipo tu.
Haya maisha mpaka lini? Nasema sasa hivi naondoka na hili sasa mtafutie mwingine, nakwenda kuishia maisha yangu kama pesa nimekuingizia sana naomba niondeke.”
“Monika mwanangu kuondoka kwako utaharibu kila kitu.”
“Baba wacha viharibike nimechoka.”
“Mwanangu unajua kabisa dawa hii haitaki uchafu ukikutana na mwanaume tu umeharibu kila kitu.”
“Ndiyo maana nimekwambia tafuta wengine, baba wewe ni kiumbe gani usiye na huruma. Miaka yote nateseka peke yangu wakati wengine wanafaidika, watu wana majumba wana magari ya kifahari lakini mimi bado naishi maisha duni kuna faida gani kuendelea kuteseka.”
“Basi nipe muda nivifanyie kazi.”
”Sina muda huo nimechoka.”
Kwa kweli kutokana na uchanga wangu wa akili sikujua baba na dada walikuwa wanabishana nini, pia nilijiuliza dada ana mateso gani ambayo anamlalamikia baba.
Lakini baada na mimi kunikuta nilielewa dada alikuwa akimaanisha nini. Maisha tuliyokuwa tukiishi yalikuwa ya ajabu sana, kwa sisi tuliokuwa tukiishi nyumbani tuliishi maisha ya dhiki sana tofauti na utajiri mkubwa tulikuwa nao.
Tulikuwa na majumba kila kona ya jiji la Mwanza, pia tulikuwa na mashine za kusaga na kukoboa ambazo ziliingiza pesa nyingi sana. Kaka zangu na dada zangu wote kila mmoja alikuwa na duka kubwa gari na majumba makubwa. Lakini sisi tuliobakia maisha yetu hayakulingana na utajiri wa baba yetu.
Kitu kingine wakati ule kilichonishangaza ni hali ya mama pamoja na kuwa na utajiri mkubwa kama ule. Kila siku mama alikuwa akiamka asubuhi na kwenda shamba ambako alilima mpaka jioni na kurudi nyumbani. Kila mama aliporudi nyumbani alikuwa akirudi na kuni ambazo alipikia katika jiko la mafiga.
Kwa vile mwanzo zilikuwa akili za kitoto sikuelewa nini kinaendelea wala wakati huo sikujua faida ya utajiri tuliokuwanao. Kitu kingine ambacho sikukielewa muda ule kilikuwa ni nyumba tuliyokuwa tukiishi ilikuwa ni ya zamani ambayo baba aliinunua wakati anaanza maisha.
Lakini haikuwa na mabadiliko yoyote pamoja na mabadiliko ya kimaisha kwa baba kuwa na pesa kama mchanga. Dada baada ya kubishana na baba alikaa kwa wiki mbili.
Siku moja niliporudi sikumkuta alikuwa ameamua kuondoka, sikujua amehamia wapi. Lakini baada ya siku tatu nilipata taarifa kuwa dada amehamia Mkuyuni ambako alikuwa amepanga na kufungua duka lake. Kuondoka kwa dada nyumba iligeuka kama pametokea msiba kitu ambacho kilinishangaza sana.
Kuondoka kwa dada hakukuwa kitu cha ajabu kwa vile dada na kaka zangu wote walipotaka kuanza maisha yao waliondoka lakini hakukuwa na mabadiliko yoyote. Baba alionekana kukosa raha, mama naye muda mwingi mkono ulikuwa shavuni. Kitu kile kwa kweli kilinishangaza sana.
Nakumbuka siku moja ndugu wote walikutana nyumbani kasoro dada Monika na kuwa na kikao kizito, cha ajabu mimi nilitolewa nje hivyo kilichoendelea sikujua kwa vile nilibaguliwa kutokana na kuonekana mdogo nisiye na mchango wowote.
Baada ya kikao kilichochukua masaa zaidi ya manne ndugu zangu waliondoka.
Kuondoka kwao kidogo kulifanya baba achangamke kidogo bila kujua walikuwa wamezungumza nini na nini chanzo cha wazazi wangu kuwa katika hali ya majonzi.
Nilijiuliza ilikuwa ni dada kuondoka au kulikuwa na jambo kubwa zaidi, katika akili yangu nilifikilia kuna umuhimu wa kumtafuta dada Monika ili nijue kwa nini ameondoka nyumbani na vile vile ni mateso gani aliyoyapata.
Kuna kitu kimoja ambacho kilikuwa kikinishangaza toka nilipopata akili ni donda la mguu la dada ambalo lilikuwepo kila siku wala halikupata dawa ya kuliponesha.
Nilijikuta nikipata hamu ya kutaka kujua kwa nini dada aliyasema yale maneno ambayo yalionesha machungu kwa kuonekana akizuiwa nyumbani asiondoke lakini wengine wote waliruhusiwa.
Kingine kilichoacha maswali kichwani mwangu ambacho kilikuwa hakijakomaa akili ni hali ya dada kuonekana kama hajaliwi na baba tofauti na ndugu zangu tokea kwenye elimu mpaka maisha ya kawaida.
Wote walikuwa na maisha mazuri kasoro yeye, lakini sikutaka kujua zaidi kwa vile nilikuwa mtoto mdogo nisiye na uwezo wa kuhoji jambo. Nilipeleleza anapokaa dada, mama alinieleza anakaa pembeni ya soko la Mkuyuni duka lake linatazamana na soko. Siku moja baada ya kutoka shule nilipitia moja kwa moja hadi kwa dada.
Kufika kwake sikupotea nilifika bila tatizo kutokana na duka lake kuonekana pia ndilo lililokuwa kubwa. Nilipofika dukani dada aliponiona alifurahi sana.
“Karibu mdogo wangu.”
“Asante dada.”
“Umekuja na nani?”
“Peke yangu.”
“Umepajuaje hapa?” Dada alinishangaa.
“Amenielekeza mama, sehemu yenyewe si ya kupotea.”
“Ni sehemu nyeupe, karibu mdogo wangu.”
“Asante.”
“Nyumbani hawajambo?”
“Hawajambo mama anakusalimia.”
“Baba anajua umekuja huku?”
“Walaaa.”
“Karibu soda upoze koo,”nilipokea soda na kuanza kunywa, wakati huo dada alikuwa akihudumia wateja waliokuwa wakinunua bidhaa dukani kwake, baada ya kumaliza kuwauzia alinigeukia.
“Mmhu, za shule?”
“Nzuri tu dada.”
“Umetumwa au?”
“Dada siji kwako mpaka nitumwe?”
“Siwajahi kukuona ndio maana nashangaa ni muda gani toka niondoke nyumbani. Najua wote mlinichukukia kwa kujua nataka kuwanyang’anya utajiri wenu.”
Sehemu ya 01
Katika dunia ya Mungu kuna mambo mengi ambayo ukihadithiwa unaweza kuona na simulizi ya kutunga na kusisimua. Lakini siku zote kila isifue mvua basi imemnyea. Dunia umezungukwa na siri nzima ndani ya majumba ya watu kuna mambo mazito ambayo ni chukizo la muumba.
Si kila mwenye maisha mazuri au matajiri mali aliyopata kaipata kihalali, wengi wao utajiri wao unatokana na nguvu za kiza utajiri anaoambatana na kutoa kafara ya kitu. Wapo wanaotoa watoto, wake au waume zao, pia wapo wanaowageuza watoto, wake au waume zao kuwa mandondocha kama chuma ulete wa kuwaongezea kipato.
Nyumba nyingi huwa na vyumba vya siri ambavyo huwa havifunguliwi kutokana na masharti ya mganga na kufanya watu wabaki na maswali.
Pia nyumba nyingine unakuta kuna mtoto ambaye akili zake si nzuri akikaa yupoyupo mate yanamtoka ovyo kumbe ni dawa ya utajiri. Ajabu huyo ndiye anakuwa kipenzi cha baba ambaye anajua siri yake.
Wapo ambao huambiwa kama mtoto huyo atakufa basi na utajiri nao unayeyuka, ni mambo mengi yaliyoizunguka jamii na uchafu wa tamaa za watu kutaka utajiri kwa njia ya mkato na kujikuta wakifanya uchafu au ukatiri mkubwa bila kuwa na huruma ili tu wapate utajiri.
Nayasema haya nikiwa na uchungu mkubwa baada ya baba yangu kutugeuza chumaulete kumuingizia pesa bila kujua. Nayasema haya baada ya kuteseka zaidi ya miaka saba bila kujua kumbe mateso yangu ndiyo yalikuwa chachu ya utajiri wa familia yangu.
Toka nilipoanza kupata matatizo yaliyopelekea mateso kila kukicha hata siku moja sikuruhusiwa kwenda hospitali zaidi ya kutumia dawa za kienyeji zisizo punguza maumivu na si kuponesha.
Miaka saba nyuma tatizo kama langu alikuwa nalo dada yangu ambaye nilimfuata mara ya nne ambaye sasa hivi ni marehemu.
Mwanzo nilipomuona dada nilijua ni kidonda cha kawaida japo kilinishangaza kichukua muda mrefu toka nikiwa na miaka sita mpaka nilipokuwa na utambuzi kujua kuwa dada yangu anateseka na kidonda kile ambacho kilikuwa hakiponi.
Miaka tatu baadae nilisikia ugomvi mkubwa kati ya baba na dada, nilijificha na kumsikia dada akisema.
“Nimechoka siwezi kuteseka wakati wenzangu wanafaidi kwa mateso yangu, siolewi sina maisha mazuri kama wenzangu niponipo tu.
Haya maisha mpaka lini? Nasema sasa hivi naondoka na hili sasa mtafutie mwingine, nakwenda kuishia maisha yangu kama pesa nimekuingizia sana naomba niondeke.”
“Monika mwanangu kuondoka kwako utaharibu kila kitu.”
“Baba wacha viharibike nimechoka.”
“Mwanangu unajua kabisa dawa hii haitaki uchafu ukikutana na mwanaume tu umeharibu kila kitu.”
“Ndiyo maana nimekwambia tafuta wengine, baba wewe ni kiumbe gani usiye na huruma. Miaka yote nateseka peke yangu wakati wengine wanafaidika, watu wana majumba wana magari ya kifahari lakini mimi bado naishi maisha duni kuna faida gani kuendelea kuteseka.”
“Basi nipe muda nivifanyie kazi.”
”Sina muda huo nimechoka.”
Kwa kweli kutokana na uchanga wangu wa akili sikujua baba na dada walikuwa wanabishana nini, pia nilijiuliza dada ana mateso gani ambayo anamlalamikia baba.
Lakini baada na mimi kunikuta nilielewa dada alikuwa akimaanisha nini. Maisha tuliyokuwa tukiishi yalikuwa ya ajabu sana, kwa sisi tuliokuwa tukiishi nyumbani tuliishi maisha ya dhiki sana tofauti na utajiri mkubwa tulikuwa nao.
Tulikuwa na majumba kila kona ya jiji la Mwanza, pia tulikuwa na mashine za kusaga na kukoboa ambazo ziliingiza pesa nyingi sana. Kaka zangu na dada zangu wote kila mmoja alikuwa na duka kubwa gari na majumba makubwa. Lakini sisi tuliobakia maisha yetu hayakulingana na utajiri wa baba yetu.
Kitu kingine wakati ule kilichonishangaza ni hali ya mama pamoja na kuwa na utajiri mkubwa kama ule. Kila siku mama alikuwa akiamka asubuhi na kwenda shamba ambako alilima mpaka jioni na kurudi nyumbani. Kila mama aliporudi nyumbani alikuwa akirudi na kuni ambazo alipikia katika jiko la mafiga.
Kwa vile mwanzo zilikuwa akili za kitoto sikuelewa nini kinaendelea wala wakati huo sikujua faida ya utajiri tuliokuwanao. Kitu kingine ambacho sikukielewa muda ule kilikuwa ni nyumba tuliyokuwa tukiishi ilikuwa ni ya zamani ambayo baba aliinunua wakati anaanza maisha.
Lakini haikuwa na mabadiliko yoyote pamoja na mabadiliko ya kimaisha kwa baba kuwa na pesa kama mchanga. Dada baada ya kubishana na baba alikaa kwa wiki mbili.
Siku moja niliporudi sikumkuta alikuwa ameamua kuondoka, sikujua amehamia wapi. Lakini baada ya siku tatu nilipata taarifa kuwa dada amehamia Mkuyuni ambako alikuwa amepanga na kufungua duka lake. Kuondoka kwa dada nyumba iligeuka kama pametokea msiba kitu ambacho kilinishangaza sana.
Kuondoka kwa dada hakukuwa kitu cha ajabu kwa vile dada na kaka zangu wote walipotaka kuanza maisha yao waliondoka lakini hakukuwa na mabadiliko yoyote. Baba alionekana kukosa raha, mama naye muda mwingi mkono ulikuwa shavuni. Kitu kile kwa kweli kilinishangaza sana.
Nakumbuka siku moja ndugu wote walikutana nyumbani kasoro dada Monika na kuwa na kikao kizito, cha ajabu mimi nilitolewa nje hivyo kilichoendelea sikujua kwa vile nilibaguliwa kutokana na kuonekana mdogo nisiye na mchango wowote.
Baada ya kikao kilichochukua masaa zaidi ya manne ndugu zangu waliondoka.
Kuondoka kwao kidogo kulifanya baba achangamke kidogo bila kujua walikuwa wamezungumza nini na nini chanzo cha wazazi wangu kuwa katika hali ya majonzi.
Nilijiuliza ilikuwa ni dada kuondoka au kulikuwa na jambo kubwa zaidi, katika akili yangu nilifikilia kuna umuhimu wa kumtafuta dada Monika ili nijue kwa nini ameondoka nyumbani na vile vile ni mateso gani aliyoyapata.
Kuna kitu kimoja ambacho kilikuwa kikinishangaza toka nilipopata akili ni donda la mguu la dada ambalo lilikuwepo kila siku wala halikupata dawa ya kuliponesha.
Nilijikuta nikipata hamu ya kutaka kujua kwa nini dada aliyasema yale maneno ambayo yalionesha machungu kwa kuonekana akizuiwa nyumbani asiondoke lakini wengine wote waliruhusiwa.
Kingine kilichoacha maswali kichwani mwangu ambacho kilikuwa hakijakomaa akili ni hali ya dada kuonekana kama hajaliwi na baba tofauti na ndugu zangu tokea kwenye elimu mpaka maisha ya kawaida.
Wote walikuwa na maisha mazuri kasoro yeye, lakini sikutaka kujua zaidi kwa vile nilikuwa mtoto mdogo nisiye na uwezo wa kuhoji jambo. Nilipeleleza anapokaa dada, mama alinieleza anakaa pembeni ya soko la Mkuyuni duka lake linatazamana na soko. Siku moja baada ya kutoka shule nilipitia moja kwa moja hadi kwa dada.
Kufika kwake sikupotea nilifika bila tatizo kutokana na duka lake kuonekana pia ndilo lililokuwa kubwa. Nilipofika dukani dada aliponiona alifurahi sana.
“Karibu mdogo wangu.”
“Asante dada.”
“Umekuja na nani?”
“Peke yangu.”
“Umepajuaje hapa?” Dada alinishangaa.
“Amenielekeza mama, sehemu yenyewe si ya kupotea.”
“Ni sehemu nyeupe, karibu mdogo wangu.”
“Asante.”
“Nyumbani hawajambo?”
“Hawajambo mama anakusalimia.”
“Baba anajua umekuja huku?”
“Walaaa.”
“Karibu soda upoze koo,”nilipokea soda na kuanza kunywa, wakati huo dada alikuwa akihudumia wateja waliokuwa wakinunua bidhaa dukani kwake, baada ya kumaliza kuwauzia alinigeukia.
“Mmhu, za shule?”
“Nzuri tu dada.”
“Umetumwa au?”
“Dada siji kwako mpaka nitumwe?”
“Siwajahi kukuona ndio maana nashangaa ni muda gani toka niondoke nyumbani. Najua wote mlinichukukia kwa kujua nataka kuwanyang’anya utajiri wenu.”