Simulizi: Tafadhali baba usitufanye misukule

Simulizi: Tafadhali baba usitufanye misukule

Sehemu ya 06

“Aliyoyataka mwanao yametimia.”
Unataka kuniambia Monika ame...”
“Ishia hapo hapo na sitaki utoe chozi unajua nini tuliambiwa.”

Nilishtuka na kutoka nje na kuwakuta baba na mama sebuleni, mama aliponiona alishtuka tofauti na baba.
“Mama, dada Monika kafanya nini?”
“Kwani umesikia nini?” Baba aliniuliza.
“Sijui...ame..”

“Amefanya nini?”
“A..me..mee,” nilijikuta nikipata kigugumizi.
“Hebu ondoka hapa asubuhi yote nini kimekuamsha,” baba alinifokea.

Nilirudi chumbani kwangu nikiwa bado sielewi dada Monika kafanya nini japo bado wasiwasi wangu ulikuwa labda amefariki kutokana na maelezo ya dada Monika na kauli ya baba juu ya dada Monika. Kwa kulia ya baba ambayo aliifunga, niliamini kabisa dada Monika huenda kweli amefariki.

Kwa vile muda wa kujiandaa kwenda shule ulikuwa umekaribia nilikwenda kuoga ili nijiandae na shule. Baada ya kuoga nilirudi chumbani kwangu kujiandaa kwenda shule, nikiwa bado nipo katika maandalizi nilishtuka kusikia sauti za ndugu zangu.

Ujio wao wa asubuhi ile ulinishtua sana, nilijiuliza kuna kitu gani kimetokea au ndiyo niliyokuwa nayafikiria ya kifo cha dada Monika. Sikutaka kutoka haraka nilimalizia kuvaa nguo za shule baada ya kuvaa nilitoka ili nijiandae.
Nilishtuka kuwaona dada na kaka zangu wamekaa sebuleni, waliponiona walishtuka na kuniuliza.

“Masalu unakwenda wapi?’
”Shule.”
“Unakwenda shule hujui hapa nyumbani kumetokea nini?’
”Sijui.”
“Mmh, makubwa, Monika amefariki.”
“Eti?

“Monika amefariki.”
“Dada Monika?” Bado sikuamini.
“Eeeh, huyohuyo.”
“Hapana hapana sitaki kuamini ..siamini,” nilipingana na maneno yao.

Bila kujielewa nilijizoa mzima mzima na kujipiga chini na kupoteza fahamu, baada ya huduma ya kwanza nilipata fahamu na kuangua kilio tofauti na wenzangu hakuna hata mtu mmoja aliyemwaga chozi. Juhudi za kunibembeleza zilishindikana.

Bila kujielewa nilijikuta nikisema kwa sauti ya juu, yote uliyonieleza dada yangu nilifikiri utani kumbe kweli wamekuua.”

“Alikueleza nini?”
”Baba kwa nini umemuua dada Monika?”
“Wee Msalu maneno gani hayo?” wote walishtuka.

“Maskini dada yangu kumbe ulikuwa na siri nzito moyoni mwako ambayo imenifumbua leo ungekufa dada yangu bila kujua lakini Mungu mkubwa.”

“Masalu hebu ondoa uchuro hapa.”
“Siwezi.. siwezi, kwa nini lakini umemuua dada Monika?” Niliendelea kulia kwa uchungu huku nikijipigiza chini.

“Nani kamuua Monika?”
“Nyinyi wote kwa tamaa za mali.”
“Masalu unatukosea adabu.”
“Siwakosei adabu bali ukweli ni huo.”

Kaka mkubwa alinichukua na kutoka na mimi uani huku nikiendelea kulia, roho iliniuma kumpoteza kipenzi dada yangu Monika mtu aliyenipenda kuliko yeyote. Kutokuonesha ndugu zangu kuguswa na kifo cha Monika niliamini ndoto niliyoota ilikuwa na maana kubwa.

Kama dada Monika wamemla nyama nini maana ya kidonda mguuni kwangu chenye kutoa wadudu. Tulipofika nje kaka alinibembeleza na kunieleza maneno ya busara kuhusiana na kifo cha Monika kuwa kilitokana na uzazi wala hakihusiani na masuala ya ushirikina.

Na kutokuonesha kuguswa kila mmoja alikuwa akililia moyoni kwa vile hakuna aliyetegemea. Kwa vile nilikuwa namheshimu nilimkubalia ili kumridhisha lakini siri ilibakia moyoni mwangu. Wengi walishtuka maneno yangu na kunionya nisiyasikilize ya Monika kwa vile alikuwa ni muongo na mgombanishi, nao nilikubaliana nao ili yaishe.

Ajabu ya mwaka ambayo baada ya akili ya ufahamu kukomaa niligundua kuna kitu kilitendeka mpaka leo hii sijui. Baada ya taarifa za msiba wa dada Monika ambao hakuna aliyefunua mdomo wake kulia zaidi yangu mwenyewe.

Taarifa za msiba ule hata majirani hawakujua nyumbani kulitokea msiba,
Mwili wa dada ulifuatwa na kurudishwa nyumbani.

Gari lililouleta mwili wa dada ilipita mpaka uani, waliuteremsha na kuingiza chumbani kisha ndugu wote walitawanyika kwenda kuendelea na kazi zao kama kawaida. Kitu kile kilinishtua iweje kuwepo na msiba hakuna mtu aliyeguswa wala taarifa kuwafikia majirani.

Usiku nilipelekwa kwa kaka ambako nilililala siku mbili na kurudishwa nyumbani, niliporudi hali ilikuwa ile ile na kunifanya niwe na mawazo ni kweli dada alikufa au taarifa zile zilikuwa mgonjwa mahututi. Kwa hiyo yupo hospitali, sikutaka kuhoji haraka baada ya wiki sikuona mabadiliko wala taarifa zozote za dada Monika.

Hata majirani waliotuzunguka hawakujua kitu zaidi ya ndugu wa mpenzi wa dada Monika kuulizia dada alizikwa wapi. Maswali yale kwa kweli yalinichanganya sana. Kila nilivyojitahidi kuchunguza sikupata taarifa zozote zaidi ya watu kufurahia maisha.

Mwezi ulikatika nikiwa bado njia panda kuhusu maswali dada Monika wakiulizia mazishi yake yalifanyika lini na kwa nini baba hakuwataarifu kama kuna msiba, kama majirani wajumuike pamoja katika msiba ule. Siku moja nilikwenda hadi Mkuyuni nyumba aliyokuwa akikaa dada Monika.

Nilikuta mlango umefungwa, kuuliza nilishindwa kutokana na kuogopa maswali huenda amekufa na kunifahamu mimi ni nani.

Niliamua kurudi bila kupata jibu kuhusiana na kupotea kwa dada Monika amekufa kweli au hali yake ni mbaya. Lakini nilikumbuka kaka mkubwa aliniambia kuwa Monika alikufa kutokana na uzazi.

Nilijiuliza kama alikufa alizikwa wapi na kwa nini majirani hawajui lolote, na kama kweli alikuwa amekufa mazishi yake yalifanyika wapi. Kutokana na kuja mjini muda mrefu mazishi yote tuliyafanyia mjini. Ingekuwa kama wengine mazishi huyafanyia vijiji walikozaliowa lakini dhana ile baba aliikataa.

Bado sikutaka kukubali nilizunguka kwenye makaburi labda nitaliona kaburi jipya la dada Monika, lakini sikuona kitu chochote. Zaidi ya makaburi mapya yenye majina tofauti na la dada Monika. Nilibakia njia panda siku zote kujiuliza ni kweli dada Monika alikufa au yupo kwa mganga.

Siku moja nilikutana na shemeji bwana aliyekuwa akikaa na dada Monika, nilimuulizia kitu ambacho kilionekana kituko mbele yake.
 
Duh! Kama kweli watu wana roho ngumu..endelea kudondosha tuone mwisho wake.
 
Sehemu ya 07

Bado sikutaka kukubali nilizunguka kwenye makaburi labda nitaliona kaburi jipya la dada Monika, lakini sikuona kitu chochote. Zaidi ya makaburi mapya yenye majina tofauti na la dada Monika. Nilibakia njia panda siku zote kujiuliza ni kweli dada Monika alikufa au yupo kwa mganga.

Siku moja nilikutana na shemeji bwana aliyekuwa akikaa na dada Monika, nilimuulizia kitu ambacho kilionekana kituko mbele yake.
“Shemu za siku?”

“Nzuri sijui zako?”
“Eti shemu, dada Monika yupo wapi?”
“Masalu swali gani hilo? Ina maana mtu akifa huwa anakwenda wapi?”

“Una maana ni kweli dada Monika amekufa?”
“Masalu kioja gani unataka kunionesha, ina maana wakati Monika anakufa wewe ulikuwa wapi?”
“Sasa kama amekufa maiti yake imezikwa wapi?”

“Mimi nitajua wapi, wakati nilifukuzwa?”
“Kama kazikwa mbona hakuna kaburi lake?”
“Masalu upo sawa?”
“Kwani wewe unanionaje?”
“Nakuona haupo sawa.”
“Nipo sawa na akili timamu.”
“Kama kweli una akili timamu usingeniuliza suala la kifo cha Monika.”

“Shemu kama dada alikufa mbona wewe mumewe haukuwepo msibani?”
“Masalu, nilifukuzwa kama mbwa na kutishiwa maisha, kwanza nikionekana nimesimama na wewe nitajitafutia balaa.”
“Shemu una uhakika Monika amekufa?”
“Ndiyo.”

“Ulimshuhudia kabisa amekufa?”
“Monika amefia mikononi mwangu na kuna mengi alinieleza ya kukueleza lakini sikupata muda wa kuonana na wewe. Kama ni kweli aliyosema Monika basi familia yetu itakuwa ina hatari kubwa.”

“Kuhusu utajiri?” Nijikuta naropoka.
“Nalo hilo alilizungumzia, ila wamemtesa sana mke wangu mpaka kifo chake.

Kibaya wamemuua hata mtoto wangu aliyekuwa tumboni bila kosa, yaani siamini familia yako kuna na roho mbaya kiasi hicho. Kama mtu kawapatia utajiri akisema amechoka na yeye anataka maisha yake kuna ubaya gani?” Maskini shemeji yangu alizungumza huku akitokwa na machozi, nilijikuta nikitokwa na mimi machozi bila kupenda.

“Masalu familia yetu haifai unafikiri maisha ya kuongozwa na nguvu za kishirikina mwisho wake nini. Haya sasa wamemuua Monika nani atafuata na kwa taarifa kidonda alicho kikataa dada yako kitahamia kwako.

Kabla ya kufa kaitaja familia yenu wote kuwa wanagombania roho yake kasoro wewe pake yako na kuonesha jinsi gani uhusiki na mateso ya mke wangu.”

“Mungu wangu!”
“Huo ndio ukweli wenyewe, hujiulizi kwa nini mama yako bado analima kama sio ushirikina, hivi baba yako hana pesa ya kuwapa watu walime na mama yako na utu uziuma wake apumzike?”

“Anaweza.”
“Kama anaongeza majumba na magari kwa nini mama yako usipumzike, hebu angalia ndugu zako wakubwa. Nao wana roho ya tamaa ya mali kushindwa kumuonea huruma mama yenu. Nasikia ndani mwenu kuna chumba kisicho funguliwa unajua kuna nini?”
“Hata sijui!”

“Kwa taarifa yako kuna maiti ya mtoto mchanga ambayo kila siku tatu hupakwa mafuta ili isiharibike.”
“Shemuuuu! Umejuaje?” Nilishtuka kusikia habari zile, chumba alichokisema kweli kilikuwepo ambacho sikuwahi kukiona kikifunguliwa.

“Dada yako Monika alikuwa na siri nzito moyoni mwake, nyingine alisema hawezi kuniambia labda ungekuwepo kabla ya kufa kwake.”
“Sasa yeye alijuaje kama kuna maiti ya mtoto?”

“Mara nyingi kazi ile aliifanya yeye baba na mama yenu hakuna mtu mwingine aliyeruhusiwa kuifanya.”
“Mmh! Maiti na mtoto wa nani?”
“Kama una kumbukumbu, nasikia mtoto wa kwanza wa dada yako ambaye ndiye aliye na pesa kuliko wote alimtoa mtoto wake kafara ili kuongeza utajiri.”

Kauli ile ilinirudisha nyuma na kukumbuka miaka sita iliyopita dada mkubwa alifiwa na mwanaye lakini mazishi yake sikuyaelewa japo msiba ulikuwa nyumbani.

Kingine kilichonifungua macho hakikuwa na tofauti na msiba wa Monika kilikuwa cha kifamilia tena ya ndani hata wana ndugu hawakujulishwa. Taratibu nilianza kufunguka akili na kuamini kila lililosemwa na Monika lilikuwa na ukweli mkubwa.

“Asante shemu kwa kunifumbua macho,” nilimshukuru ili tuagane, nilipotaka kuondoka aliniuliza kitu.

“Masalu unataka kuniambia hukuwa na habari Monika amekufa au ulitaka kunitega akili?”
“Shemu, huwezi kuamini kila dakika nimekuwa nikichanganyikiwa juu ya taarifa za msiba wa dada Monika. Kweli niliuona mwili ukiteremshwa kwenye gari. Lakini tokea hapo sikuweza kujua nini kilichoendelea mpaka leo hii.”

“Ulipouliza walikujibu nini?”
“Sijauliza bali nilifanya upelelezi wangu, kila kona nilifika lakini sikupata kuona chochote.”
“Ulichunguza nini?”

“Sehemu za makaburi au kupata taarifa kama hajafa yupo wapi?”
“Una uhakika Monika hakuzikwa?”
“Nina uhakika.”
“Basi kuna sehemu wamemuweka isiwe naye wamemuweka kwenye hicho chumba na kumpaka mafuta?”

“Mmh! Sijui.”
“Unaweza kuingia?”
“Mmh! Nitajitahidi kuhakikisha napata ukweli.”
“Basi utakacho kipata usikose kunijulisha.”

“Nakuahidi kukuletea kila kitu.”
“Haya shemu kwa heri”
“Ya kuonana.”
Niliagana na shemu na kurudi zangu nyumbani nilizidi kuchanganyikiwa na maneno ya pande mbili juu ya ukweli juu ya kifo cha dada Monika. Moyoni niliapa nikipata muda lazima mama ananiambia ukweli.

Siku zilikatika bila kujua taarifa za uhakika kuhusiana na habari tata juu ya kifo cha dada Monika ni kweli amekufa? kitu ambacho moyo wangu haukukubaliana nacho.

Uvimilivu ulinishinda siku moja nilimfuata mama shamba kutaka kujua ukweli wa dada Monika. Kama kawaida yangu nilidanganya naumwa.

Baada ya kuondoka na kuniacha nyumbani na mfanyakazi, majira saa nne asubuhi nilikwenda hadi shamba.

Nilimkuta mama akipiga jembe kama hana akili nzuri. Moyoni nilimuonea huruma jinsi alivyohenyeka japo tuna pesa, kila dakika niliyakumbuka maneno ya dada Monika kuwa maisha yetu yanaongozwa na ushirikina.

Nilimwita mama ambaye alishtuka kuniona, niliamini kabisa alijiandaa kutokana na kumuuliza maswali mazito siku ya kwanza.

“Wee Masalu mbona huku si unaumwa?”
“Kidogo nimepata nafuu.”
“Haya ulikuwa unasemaje?”
“Kuna kitu mama kinanisumbua kila siku naomba msaada wako wanaweza kuwa chizi”
“Wee mwana mbona una mambo kuna nini tena?”

Mama alisema huku akiweka jembe pembeni na kunifuata nilipokuwa nimesimama.
“Masalu kuna nini tena?” Mama aliniuliza huku akifuta jasho kwenye paji la uso kwa mkono.

“Mama toka kifo cha dada Monika kuna mambo yamekuwa yakinichanganya na kunifanya kila siku nisijielewe.”
“Masalu mambo gani tena mwanangu kila siku huishi vioja?”

“Kuhusu dada Monika.”
“Monika kafanya nini tena?”
“Mama ni kweli dada Monika amefariki?”
”Masalu wewe si mtoto mdogo sasa, kila mtu anajua Monika amefariki wewe ukiwemo.”
“Mamaa, kama dada Monika amefariki mbona sikuona mazishi wala kaburi lake.”

“Masalu uyaone hayo ili ikusaidie nini?”
“Mama unajua majirani wanatusema vibaya toka taarifa za kifo cha dada Monika.”
“Nani aliwaambia Monika amekufa?”
“Mamaa, kwani kifo cha dada Monika kilikuwa cha siri?”

“Hata kama sio cha siri sio lazima wajue.”
“Hivi mama watu wakiniuliza dada Monika yupo wapi mimi niwajibu nini?”
“Wanyamazie usiwajibu chochote.”

“Lakini mama, kumbe hata yule shemeji aliyekuwa anakaa na dada Monika mlimfukuza asihudhurie mazishi.”
“Ahudhurie ametoa kiasi gani cha pesa kwa dada yako, zaidi ya kutuchanganya kifamilia.”

“Lakini mama tuachane na hayo, kaburi la babu na bibi nalifahamu, kaburi la kaka mkubwa nalifahamu. Makaburi yote yanayotuhusu nayafahamu na kila mwisho wa mwaka huenda kuyazuru familia yote na pia huenda kila mwezi kusafisha na kuyaweka katika hali ya usafi. Lakini kaburi la dada Monika lipo wapi, japo sikuhudhuria mazishi yake.?”

“Masalu, wee mtoto mdogo hujui lolote elewa kuwa dada yako Monika amefariki.”
“Mama, bado hayajaniingia akilini.”
“Masalu hebu niondokee nilifikiri jambo la maana kumbe ni upumbavu,” mama alisema huku akijiandaa kurudi shambani.
“Mama unaniona mtoto lakini mambo yetu yote yapo hadharani.”

“Mambo gani?” Mama alishtuka na kunigeukia ili kutaka kujua.
“Dada Monika alinieleza mengi kuhusiana kifo chake alichotishiwa na baba kwa ajili ya kukikataa kidonda na kunitisha kidonda kile kitahamia kwangu.”

“Masalu nikueleze mara ngapi kuwa dada yako Monika alikuwa muongo aliyetaka aonekane alichokifanya ni sahihi cha ukosefu wa adabu.”

“Lakini mama mbona mengi aliyonieleza yanatokea uongo wake nini?”
“Kama nini?”
“Kuhusu wewe kuteseka na kilimo wakati familia ina uwezo mkubwa?”
”Kulima si kujitesa bali kujipa mazoezi.

“Mama, juzi uligombana na baba akikulazimisha uje shamba wakati ulikuwa hujisikii vizuri hata juzi uliniambia hukulala kutokana na maumivu ya mgongo. Mama naona umejisahau pale uliponiambia kuwa baba atakuua kwa vitu vya kulazimishana, bado tu unasema mazoezi.

“ Mama unaweza kuona mnafanya siri lakini kila kitu kipo wazi. Unaweza kuona watu wapo kimya, lakini kuna maneno mengi sana juu ya kifo cha dada Monika, hakina tofauti na kifo cha mtoto wa dada Mihayo.”

“Masalu! Hakina tofauti ya nini?”
“Wanasema hata mtoto wa dada Mihayo alipokufa hakuzikwa.”
“Hakuzikwa alifanywa nini?” Maskini mama aliniuliza huku macho yakimtoka pima na kujasho chembamba kilimvuja.

“Eti wanasema kile chumba ambacho hakifunguliwi ndani kuna maiti ya mtoto ambayo huwa mnaipaka mafuta kila baada ya siku tatu ndicho chanzo cha dada Mihayo kuwa na utajiri mkubwa kuliko wenzake.”
“Wee mtoto, haya yote umeyasikia wapi?” Mama alishtuka.

“Shemeji aliniambia kuwa kabla dada hajakata roho alimweleza mambo mengi juu ya ushirikina wa familia yetu kutumia kidonda chake kujipatia utajiri na hata alipotoka nyumbani kukataa kuendelea na kidonda ilisababisha kifo chake.”

“Masalu! Alimueleza kuwa hicho chumba kuna maiti ya mtoto?”
“Ndiyo, tena alimueleza kuwa watu waliokuwa wakiipaka maiti mafuta ni wewe baba na yeye dada Monika.”

“Mungu wangu, kayasema hayo Monika?”
“Na wasiwasi mwingine wanasema maiti ya dada Monika huenda nayo haikuzikwa imefichwa kwenye chumba kile cha siri”
“Ooh..Mungu wangu ...

Ooh moyo wangu,” mama alisema huku akishikilia kifua na kuanguka chini. Nilipojaribu kumuamsha hakuamka, nilipiga kelele kwa majirani wa shamba la pili. Sauti yangu iliwakusanya watu ambao walifika na kumpa huduma ya kwanza mama aliyekuwa amepoteza fahamu.

Alipopata fahamu aliwaomba wampe msaada wa kumrudisha nyumbani, jirani yetu mama Kusekwa alimsindikiza mama hadi nyumbani. Tulipofika alituacha na yeye kurudi shambani. Nikiwa nimejawa na wasiwasi huku nikijilaumu kwa kumueleza mama mambo ambayo niliyaona mazito.

Nilikuwa pembeni ya mama aliyekuwa bado amejilaza kwenye zuria huku akipuliziwa upepo wa feni aliniita.
“Masalu,” mama aliniita.
“Naam mama”
“Kuna mtu aliuliza sababu ya kuanguka kwangu?”

“Ndiyo mama.”
“Aliwajibu nini?”
“Niliwaeleza kuwa ulianguka ghafla.”
“Awakukuhoji zaidi?”
“Hawakunihoji zaidi ya kukupa huduma ya haraka.”

“Ooh, afadhari.”
“Unajisikiaje kwa sasa?” Nilimuuliza mama kwa huruma.
“Mmh, sijambo kidogo ila nakuomba tuliyozungumza yote usimwambie mtu.”
“Sawa mama.”

Nilimkubalia ili tu kuiacha siku ile ipite pia kutokana na hali yake, lakini bado sikupata jibu la dada Monika amekufa kweli, japo shemeji alinihakikishia amekufa. Na kama amekufa amezikwa wapi au ndio yaleyale niliyoelezwa kuwa mwili wake umefichwa ndani.
 
Sehemu ya 08

Nilimkubalia ili tu kuiacha siku ile ipite pia kutokana na hali yake, lakini bado sikupata jibu la dada Monika amekufa kweli, japo shemeji alinihakikishia amekufa. Na kama amekufa amezikwa wapi au ndio yaleyale niliyoelezwa kuwa mwili wake umefichwa ndani.

Moyoni nilibakia njia panda kutaka kujua ukweli kuhusu dada Monika, nilipanga kama mama atashindwa kunieleza basi nitamvaa baba na ukali wake ili nijue amekufa au mzima na kama amekufa amezikwa wapi.
Sikutaka kuliulizia jambo lile haraka kutokana na hali ya mama, niliamua kukaa kimya, lakini moyoni sikuwa na raha kutaka kujua ukweli wa kifo cha dada Monika.

Siku moja asubuhi kabla ya kwenda shule mama alinifuata chumbani kwangu na kunieleza nisiende shule kuna sehemu anataka kunituma.
Nilibadilisha nguo zangu za shule na kuvaa za nyumbani, wakati huo alikuwa akijiandaa kwenda shambani. Lakini siku ile hakuwahi kama ilivyokawaida yake.

Tuliondoka nyumbani pamoja kuelekea shamba, baada ya muda wa chai, kutoka nyumbani mpaka shambani ni mwendo wa dakika 45. Tulikwenda huku tukizungumza, mama aliniulizia habari za shule, nilimuelezea maendeleo yangu japo hakuwahi hata siku moja kushika madaftari yangu kuyaangalia.

Katika kumbukumbu zangu nilielezwa kuwa mama aliishia darasa la sita baada ya kupewa ujauzito na baba kisha kumtorosha. Taarifa hizo alinipa marehemu ambaye sina uhakika kama kweli amekufa au maiti yake imefungiwa katika chumba kisichofunguliwa.

Dada Monika alinieleza kuwa mama yetu alitengwa na familia yake baada ya kubebeshwa ujauzito na baba na kutoroshwa. Kitendo kile ndicho kilichofanya mama aishi maisha ya peke yake bila ndugu, ndugu yake mkubwa alikuwa baba kitu kilichofanya baba amnyanyase kwa kujua hana pa kwenda.

Sababu ile ndiyo iliyomfanya mama aishi kama mtumwa kwa vile kila alipofanya kosa baba alimtishia kumfukuza. Kwa kweli kitendo cha baba nilikiona cha kikatili sana, kila dakika nilijikuta nikimchukia baba kwa roho mbaya ya kuitesa familia yake kwa ajili ya mali.

Niliamini mateso ya muda mrefu na shuruba zote, baada ya kupata utajiri wa kushirikina, basi alitakiwa mama atulie na kufaidi matunda ya uchawi wao.

Lakini imekuwa tofauti mama kila kukicha amekuwa mtu wa kusurubika. Kilichonishangaza ni ndugu zangu kushindwa kumsimamia mama, mateso ya kulima kupasua kuni. Kila nilipomtazama mama yangu roho iliniuma na kujiapiza kama Mungu atanisaidia kupata kazi na kuwa na maisha mazuri basi nitamuondoa kwa baba.

Moyoni nilijiapiza kutokukubali kuishi maisha machafu ya ndugu zangu ya kutoa familia zao kwa ajili ya kafara ya hatari na kujiona kama wataishi milele. Nilijiuliza dada Mihayo atamwambia nini mwanaye mbele ya Mungu, aliyemtoa kafara kwa ajili ya utajiri na baadaye kuendelea kuteza kwa kumlaza kwenye chumba.

Kuna kitu alinieleza dada Monika juu ya mama na kuniomba nimchunguze, nakumbuka siku hiyo alinieleza:

“Masalu, mama yetu anaishi maisha ya mateso makubwa sana, baba ni shetani asiyefaa mbele ya jamii. Nataka nikueleze kitu kimoja ambacho mimi wananikataza. Kwa taarifa yako nilikatazwa kulala na mwanaume lakini baba ana mwanamke kamjengea nyumba ya gharofa moja.”
Dada Monika aliendelea kunieleza jinsi watu wanavyotumia pesa huku mama akiteseka, alinieleza:

“Mdogo wangu familia yetu yote tutateketea kwa moto wa kiama, hebu ona maisha ya mama yanalingana na utajiri tulionao, hata kama kuyumba hatuwezi kuishiwa kiasi cha kutisha, sawa na tembo kuugua maralia hawezi kukonda kama mbwa.

“Masalu, sema tu mama mbishi, nilimueleza mapema tuondoke pamoja ili aepukane na maisha ya mateso, lakini mama kama amerogwa na baba haelewi hasikii.

Hivi kweli mama yetu ni wakuvaa kandambili za kufunga na kamba?” Nakumbuka siku hiyo dada Monika alizungumza huku akibubujikwa machozi.

Mama anateseka dada Mihayo anamuhonga bwana wa pembeni gari, Masalu inauma lakini sina uwezo. Kama kidonda hiki angekuwa nacho mtu mwingine na mimi kuwa na uwezo wa dada Mihayo hata kwa kutoa kafara ya mtoto mama yangu angeishi kama malaika.

Lakini sina uwezo, hata hili kidogo ninachokipata nikimpelekea mama hatakitumia zaidi ya kugeuzwa ndondocha na baba.”

Kila nilipoyakumbuka maneno ya dada nilijikuta nikitokwa na machozi. Nilikumbuka neno moja ambalo dada Monika alinieleza nilifanyie kazi, aliniambia:

“Masalu, mchunguze mama muda mwingi akiwa peke yake mkono huwa shavuni, na kama utamfuatilia kwa muda baada ya kutoa mkono shavuni utikisa kichwa na kufuta machozi. Katika maisha yetu toka tupate utajiri wa kishirikina furaha ya mama umetoweka, kutabasamu kumekuwa kama ajali lakini kulia kumekuwa kitu cha kawaida.

Mara nyingi mama amekuwa kila akiwa peke yake kanga huwa mkononi ili kufuta machozi. Vitu vile nilivifanyia kazi na kumueleza dada Monika yote aliyonieleza ni kweli. Aliniuliza swali lingine:

“Masalu umeisha muona mama akivaa nguo mpya?”
“Hapana,” nilimjibu.
“Hebu jifikirie mama yetu ni wa kuvaa nguo zilizoachwa na wanawe?”

“Nilikuwa sijui.”
“Kama hujui, hata macho yako hayaoni, Masalu sasa hivi wewe si mtoto unaona vitu ambavyo baadaye vinataka majibu kwa kile ulichokiona.”

“Huwezi kuamini dada nilikuwa kama nimefungwa akili, unachonieleza sasa hivi ndiyo kama kwangu kunapambazuka baada ya kukaa kizani kwa muda mrefu. Kama usingenieleza haya ningekufa kibudu.”

Niliamini kabisa kama dada Monika kama kweli amekufa, basi alikuwa amekufa na mengi moyoni sawa na samaki mwenye mengi ya kuzungumza lakini kila alipofumbua mdomo maji yalimjaa mdomoni. Kama alivyonieleza shemeji kabla ya kufa kutokana na maelezo yake mengi angenieleza mengi mazito.

Tulipofika shambani mama hakuonesha kama anataka kulima, aliniweka chini ya mti huku akionekana mwingi wa mawazo. Baada ya ukimya mfupi mama aliniita jina langu.

“Masalu”
“Naam mama.”
“Najua umesikia mengi juu ya maisha yetu, lakini hakuna ukweli kwa yote uliyosikia nakuomba uwapuuze, sawa baba.”
“Lakini mama mbona yote niliyoelezwa yana ukweli.”

“Ukweli upo?
”Mama kwanza naanza na wewe, toka nipate akili sijawahi kukuona ukifurahi kila siku mtu wa masikitiko na kutokwa na machozi”
“Ha! Masalu umejuaje?”
“Mama dada Monika kanieleza mambo mengi sana ambayo niliyafanyia kazi na kuupata ukweli juu yako.”

“Ukweli gani?”
“Kuhusu muda mwingi kuweka mkono shavuni na kutokwa na machozi, nilikufuatilia bila wewe kujijua na kuupata ukweli, pia uvaaji wako wa nguo mama toka nipate akili sijakuona akivaa nguo mpya au zilizo nzuri pia mama hebu angalia ndala zako. Kwa maisha tunayoishi wewe si wa kuvaa ndala za kufunga na waya”

Niliposema vile mama alijiangalia kama hakujua alichokivaa wakati wakutoka nyumbani.
“Mama najua yote haya yanatokea kwa ajili ya nini.”

“Kwa ajili gani?”
“Haya ni mateso anayokupa baba, baada ya kutengwa na ndugu yako, na chanzo cha yote ni yeye. Kutokuwa na ukaribu na familia yako, katumia ni fimbo ya kukuadhibia. Hivi mama hata wanao wengine wanajijali wao na kukusahau , bila wewe wangeijuaje dunia?

“Mama maisha haya unayoishi siyo mazuri, nilisikia eti baba alikutishia maisha kama utataka mambo makubwa. Haya ndiyo aliyoyakataa dada Monika kidonda akitunze yeye wengine wale maisha mazuri. Matokeo yake mnaamua kumuua na kuificha maiti yake”

“Masalu nani kaificha maiti ya Monika”
“Ipo wapi?”
“Masalu swali gani hilo , kila anayekufa si uzikwa”

“Mbona mtoto wa dada Mihayo hakuzikwa?”
“Masalu una uhakika gani?”
“Dada Monika hakunificha yote nisemayo ni yeye aliyeniambia ni mengi sana nayajua kuliko mtu mwingine.”

“Masalu yote usemayo ni kweli, nakuomba usimwambie mtu yoyote habari hizi”
“Kama ni kweli naomba kuanzia leo kazi ya kulima aachiwe mtu mwingine, uvae nguo nzuri ili ulingane na utajiri wa familia yetu.”
“Masalu hilo haliwezekani”

“Kwa nini?”
“Baba yako ataniua, naomba mwanangu yote unayoyaona yaache kama yalivyo, na ukizidi kumchokonoa anaweza kukuua”
“Kama alivyomuua dada Monika?”
“Usiseme hivyo Masalu”

“Mama tunafichana nini, hivi utajiri ndiyo unaotufanya tukose huruma kwa wenzetu?”
“Masalu nakuomba usichimbe sana.”
“Hapana mama huwezi kujua sasa hivi tunaonekana vipi mbele ya macho ya watu, kwa taarifa yako inasemekana Monika hajazikwa amewekwa ndani kwa imani za kishirikina”

“Nani kasema?”
“Aliyekuwa akikaa na dada Monika ndiye anayeeneza habari hizi”

“Yeye kajuaje?”
“Mama ina maana ninapozungumza na wewe unakuwa wapi? Nilikueleza kuwa kabla ya kufa dada Monika alimpa siri kubwa ya maisha yetu na sababu ya kifo chake. Pia alimueleza kuwa alikuwa na siri nzito ambayo asingemwambia zaidi yangu mimi.”
 
Sehemu ya 08

Nilimkubalia ili tu kuiacha siku ile ipite pia kutokana na hali yake, lakini bado sikupata jibu la dada Monika amekufa kweli, japo shemeji alinihakikishia amekufa. Na kama amekufa amezikwa wapi au ndio yaleyale niliyoelezwa kuwa mwili wake umefichwa ndani.

Moyoni nilibakia njia panda kutaka kujua ukweli kuhusu dada Monika, nilipanga kama mama atashindwa kunieleza basi nitamvaa baba na ukali wake ili nijue amekufa au mzima na kama amekufa amezikwa wapi.
Sikutaka kuliulizia jambo lile haraka kutokana na hali ya mama, niliamua kukaa kimya, lakini moyoni sikuwa na raha kutaka kujua ukweli wa kifo cha dada Monika.

Siku moja asubuhi kabla ya kwenda shule mama alinifuata chumbani kwangu na kunieleza nisiende shule kuna sehemu anataka kunituma.
Nilibadilisha nguo zangu za shule na kuvaa za nyumbani, wakati huo alikuwa akijiandaa kwenda shambani. Lakini siku ile hakuwahi kama ilivyokawaida yake.

Tuliondoka nyumbani pamoja kuelekea shamba, baada ya muda wa chai, kutoka nyumbani mpaka shambani ni mwendo wa dakika 45. Tulikwenda huku tukizungumza, mama aliniulizia habari za shule, nilimuelezea maendeleo yangu japo hakuwahi hata siku moja kushika madaftari yangu kuyaangalia.

Katika kumbukumbu zangu nilielezwa kuwa mama aliishia darasa la sita baada ya kupewa ujauzito na baba kisha kumtorosha. Taarifa hizo alinipa marehemu ambaye sina uhakika kama kweli amekufa au maiti yake imefungiwa katika chumba kisichofunguliwa.

Dada Monika alinieleza kuwa mama yetu alitengwa na familia yake baada ya kubebeshwa ujauzito na baba na kutoroshwa. Kitendo kile ndicho kilichofanya mama aishi maisha ya peke yake bila ndugu, ndugu yake mkubwa alikuwa baba kitu kilichofanya baba amnyanyase kwa kujua hana pa kwenda.

Sababu ile ndiyo iliyomfanya mama aishi kama mtumwa kwa vile kila alipofanya kosa baba alimtishia kumfukuza. Kwa kweli kitendo cha baba nilikiona cha kikatili sana, kila dakika nilijikuta nikimchukia baba kwa roho mbaya ya kuitesa familia yake kwa ajili ya mali.

Niliamini mateso ya muda mrefu na shuruba zote, baada ya kupata utajiri wa kushirikina, basi alitakiwa mama atulie na kufaidi matunda ya uchawi wao.

Lakini imekuwa tofauti mama kila kukicha amekuwa mtu wa kusurubika. Kilichonishangaza ni ndugu zangu kushindwa kumsimamia mama, mateso ya kulima kupasua kuni. Kila nilipomtazama mama yangu roho iliniuma na kujiapiza kama Mungu atanisaidia kupata kazi na kuwa na maisha mazuri basi nitamuondoa kwa baba.

Moyoni nilijiapiza kutokukubali kuishi maisha machafu ya ndugu zangu ya kutoa familia zao kwa ajili ya kafara ya hatari na kujiona kama wataishi milele. Nilijiuliza dada Mihayo atamwambia nini mwanaye mbele ya Mungu, aliyemtoa kafara kwa ajili ya utajiri na baadaye kuendelea kuteza kwa kumlaza kwenye chumba.

Kuna kitu alinieleza dada Monika juu ya mama na kuniomba nimchunguze, nakumbuka siku hiyo alinieleza:

“Masalu, mama yetu anaishi maisha ya mateso makubwa sana, baba ni shetani asiyefaa mbele ya jamii. Nataka nikueleze kitu kimoja ambacho mimi wananikataza. Kwa taarifa yako nilikatazwa kulala na mwanaume lakini baba ana mwanamke kamjengea nyumba ya gharofa moja.”
Dada Monika aliendelea kunieleza jinsi watu wanavyotumia pesa huku mama akiteseka, alinieleza:

“Mdogo wangu familia yetu yote tutateketea kwa moto wa kiama, hebu ona maisha ya mama yanalingana na utajiri tulionao, hata kama kuyumba hatuwezi kuishiwa kiasi cha kutisha, sawa na tembo kuugua maralia hawezi kukonda kama mbwa.

“Masalu, sema tu mama mbishi, nilimueleza mapema tuondoke pamoja ili aepukane na maisha ya mateso, lakini mama kama amerogwa na baba haelewi hasikii.

Hivi kweli mama yetu ni wakuvaa kandambili za kufunga na kamba?” Nakumbuka siku hiyo dada Monika alizungumza huku akibubujikwa machozi.

Mama anateseka dada Mihayo anamuhonga bwana wa pembeni gari, Masalu inauma lakini sina uwezo. Kama kidonda hiki angekuwa nacho mtu mwingine na mimi kuwa na uwezo wa dada Mihayo hata kwa kutoa kafara ya mtoto mama yangu angeishi kama malaika.

Lakini sina uwezo, hata hili kidogo ninachokipata nikimpelekea mama hatakitumia zaidi ya kugeuzwa ndondocha na baba.”

Kila nilipoyakumbuka maneno ya dada nilijikuta nikitokwa na machozi. Nilikumbuka neno moja ambalo dada Monika alinieleza nilifanyie kazi, aliniambia:

“Masalu, mchunguze mama muda mwingi akiwa peke yake mkono huwa shavuni, na kama utamfuatilia kwa muda baada ya kutoa mkono shavuni utikisa kichwa na kufuta machozi. Katika maisha yetu toka tupate utajiri wa kishirikina furaha ya mama umetoweka, kutabasamu kumekuwa kama ajali lakini kulia kumekuwa kitu cha kawaida.

Mara nyingi mama amekuwa kila akiwa peke yake kanga huwa mkononi ili kufuta machozi. Vitu vile nilivifanyia kazi na kumueleza dada Monika yote aliyonieleza ni kweli. Aliniuliza swali lingine:

“Masalu umeisha muona mama akivaa nguo mpya?”
“Hapana,” nilimjibu.
“Hebu jifikirie mama yetu ni wa kuvaa nguo zilizoachwa na wanawe?”

“Nilikuwa sijui.”
“Kama hujui, hata macho yako hayaoni, Masalu sasa hivi wewe si mtoto unaona vitu ambavyo baadaye vinataka majibu kwa kile ulichokiona.”

“Huwezi kuamini dada nilikuwa kama nimefungwa akili, unachonieleza sasa hivi ndiyo kama kwangu kunapambazuka baada ya kukaa kizani kwa muda mrefu. Kama usingenieleza haya ningekufa kibudu.”

Niliamini kabisa kama dada Monika kama kweli amekufa, basi alikuwa amekufa na mengi moyoni sawa na samaki mwenye mengi ya kuzungumza lakini kila alipofumbua mdomo maji yalimjaa mdomoni. Kama alivyonieleza shemeji kabla ya kufa kutokana na maelezo yake mengi angenieleza mengi mazito.

Tulipofika shambani mama hakuonesha kama anataka kulima, aliniweka chini ya mti huku akionekana mwingi wa mawazo. Baada ya ukimya mfupi mama aliniita jina langu.

“Masalu”
“Naam mama.”
“Najua umesikia mengi juu ya maisha yetu, lakini hakuna ukweli kwa yote uliyosikia nakuomba uwapuuze, sawa baba.”
“Lakini mama mbona yote niliyoelezwa yana ukweli.”

“Ukweli upo?
”Mama kwanza naanza na wewe, toka nipate akili sijawahi kukuona ukifurahi kila siku mtu wa masikitiko na kutokwa na machozi”
“Ha! Masalu umejuaje?”
“Mama dada Monika kanieleza mambo mengi sana ambayo niliyafanyia kazi na kuupata ukweli juu yako.”

“Ukweli gani?”
“Kuhusu muda mwingi kuweka mkono shavuni na kutokwa na machozi, nilikufuatilia bila wewe kujijua na kuupata ukweli, pia uvaaji wako wa nguo mama toka nipate akili sijakuona akivaa nguo mpya au zilizo nzuri pia mama hebu angalia ndala zako. Kwa maisha tunayoishi wewe si wa kuvaa ndala za kufunga na waya”

Niliposema vile mama alijiangalia kama hakujua alichokivaa wakati wakutoka nyumbani.
“Mama najua yote haya yanatokea kwa ajili ya nini.”

“Kwa ajili gani?”
“Haya ni mateso anayokupa baba, baada ya kutengwa na ndugu yako, na chanzo cha yote ni yeye. Kutokuwa na ukaribu na familia yako, katumia ni fimbo ya kukuadhibia. Hivi mama hata wanao wengine wanajijali wao na kukusahau , bila wewe wangeijuaje dunia?

“Mama maisha haya unayoishi siyo mazuri, nilisikia eti baba alikutishia maisha kama utataka mambo makubwa. Haya ndiyo aliyoyakataa dada Monika kidonda akitunze yeye wengine wale maisha mazuri. Matokeo yake mnaamua kumuua na kuificha maiti yake”

“Masalu nani kaificha maiti ya Monika”
“Ipo wapi?”
“Masalu swali gani hilo , kila anayekufa si uzikwa”

“Mbona mtoto wa dada Mihayo hakuzikwa?”
“Masalu una uhakika gani?”
“Dada Monika hakunificha yote nisemayo ni yeye aliyeniambia ni mengi sana nayajua kuliko mtu mwingine.”

“Masalu yote usemayo ni kweli, nakuomba usimwambie mtu yoyote habari hizi”
“Kama ni kweli naomba kuanzia leo kazi ya kulima aachiwe mtu mwingine, uvae nguo nzuri ili ulingane na utajiri wa familia yetu.”
“Masalu hilo haliwezekani”

“Kwa nini?”
“Baba yako ataniua, naomba mwanangu yote unayoyaona yaache kama yalivyo, na ukizidi kumchokonoa anaweza kukuua”
“Kama alivyomuua dada Monika?”
“Usiseme hivyo Masalu”

“Mama tunafichana nini, hivi utajiri ndiyo unaotufanya tukose huruma kwa wenzetu?”
“Masalu nakuomba usichimbe sana.”
“Hapana mama huwezi kujua sasa hivi tunaonekana vipi mbele ya macho ya watu, kwa taarifa yako inasemekana Monika hajazikwa amewekwa ndani kwa imani za kishirikina”

“Nani kasema?”
“Aliyekuwa akikaa na dada Monika ndiye anayeeneza habari hizi”

“Yeye kajuaje?”
“Mama ina maana ninapozungumza na wewe unakuwa wapi? Nilikueleza kuwa kabla ya kufa dada Monika alimpa siri kubwa ya maisha yetu na sababu ya kifo chake. Pia alimueleza kuwa alikuwa na siri nzito ambayo asingemwambia zaidi yangu mimi.”
Dogo anachana ukweli tu hafichi neno

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shemeji ana uwawa


Sent from my iPhone using JamiiForums
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom