Simulizi: Tafadhali baba usitufanye misukule

Simulizi: Tafadhali baba usitufanye misukule

Sehemu ya 09

“Nani kasema?”
“Aliyekuwa akikaa na dada Monika ndiye anayeeneza habari hizi”
“Yeye kajuaje?”

“Mama ina maana ninapozungumza na wewe unakuwa wapi? Nilikueleza kuwa kabla ya kufa dada Monika alimpa siri kubwa ya maisha yetu na sababu ya kifo chake. Pia alimueleza kuwa alikuwa na siri nzito ambayo asingemwambia zaidi yangu mimi.”

ILIPOISHIA;

“Mmh, sasa huyo kijana kinamuhusu nini kututangaza vibaya?”
“Kinacho muuma ni kumuulia mtoto wake asiye na hatia.”
“Hivi baba yako akijua kuwa ndiye anayetutangaza vibaya kwa watu kutakuwa na usalama kweli?”

“Atamfanya nini?”
“Masalu wee acha baba yako hana dogo anaweza hata kumkata kichwa”
“Akimuua atapata faida gani si ndiyo atakuwa anaongeza chuki kwa watu.”

“Masalu mwanangu kwa umri wako hata nikueleza kitu hutanielewa, nakuomba kila ulilosikia liache lilivyo bado mtoto mdogo litakuchanganya”
“Sawa nimekuelewa, ila naomba ukweli wa jambo moja.”

“Jambo gani gani?”
”Kuhusu ukweli wa dada Monika”
“Ukweli upi?”
”Ni kweli amekufa?”
“Ndiyo”
“Amezikwa wapi?”
“Mmh! Si Makaburini”
“Makaburini gani?”

SASA ENDELEA.....
“Kwa kweli siwezi kujua makaburi gani sikwenda kuzika”
“Mama kuna makaburi tofauti na

tuliyoyazoea?”
“Hakuna”
“Na misiba yote huanzia kanisani kisha kupelekwa kuzikwa?”
“Ndiyo”
“Sasa msiba wa dada Monika mliupeleka kanisa gani?”

“Masalu hata ukijua itakusaidia nini, aliyekufa amekufa huwezi kumfufua.”
“Hata kama siwezi kumfufua da Monika ndiye kipenzi changu, kaburi lake kwangu ni kielelezo cha kumuona kipenzi changu”
“Masalu nakuomba suala hilo uachane nalo”
“Yote nitaachana nayo si la dada Monika”
“Masalu akitaka kujua mengi utakosana na baba yako”
“Kwa hiyo ukweli dada Monika maiti yake haikuzikwa?”

“Masalu nakuomba mwanangu chonde chonde achana na hayo ili maisha yako yawe salama”
“Kwa hiyo nikitaka kujua baba ataniua?”
“Hawezi kukuua ila utakuwa matatizoni”
“Mmh! Sawa mama,” nilikubali kwa shingo upande kutokana na kuonekana kumuweka mama katika wakati mgumu.

Sikutaka kumsumbua sana mama yangu kutokana na maelezo ya dada Monika, kila nilipomtazama nilimuonea huruma. Nilimuahidi mama toka moyoni mwangu sitaulizia lolote kuhusiana na dada Monika wala kitu chochote kuhusiana na familia yetu.

Kauli yangu ilimfurahisha mama na kuonekana hawezi kuamini nilichokisema.
“Kweli Masalu”

“Kweli mama, nakupenda sana mama yangu”
“Asante Masalu, nakuomba kila unachokijua huenda hata mimi mama yako sivijui kwa vile baba yako alimpenda sana Monika hata siri zingine sizijui ambazo alikueleza wewe na pengine kabla ya kufa angekueleza,” maskini mama yangu alisema huku akitokwa na machozi kitu kilichozidi kuniumiza nami machozi yalianza kunitoka kwa mbali.
“Nimekuelewa mama yangu, nimekuelewa sina budi kukusikiliza.”

“Asante Masalu, siku zote niliamini wewe na Monika ndio watoto wangu wanaonijali, endelea kunijali mwanangu wewe ndiye tegemeo langu soma unikomboe”
“Nitafanya hivyo mama yangu, nakuahidi kuwa kimbilio lako”

“Asante mwanangu”
Baada ya mazungumzo marefu tulirudi nyumbani, lakini bado yaliniacha na maswali lukuki moyoni mwangu, nilijikuta nakubaliana na shemeji, bwana ya Monika kuwa mwili wa dada umefichwa ndani pamoja na mtoto wa dada Mihayo.


SIKU TATU BAABAYE


Siku tatu baadaye nilipata taarifa za kusikitisha za kifo cha utata cha shemeji aliyekuwa bwana wa Monika. Taarifa zilizonitisha na kuamini mazungumzo yangu na mama juu ya taarifa zinazoisambwazwa na shemeji zilimfikia baba na kuamua kufanya umaruhuni wake.

Ndugu walisema aliporudi nyumbani alianza kusema anasumbuliwa na kichwa huku akisema kama akifa atakuwa ni baba. Na usiku alipiga kelele akimtaja jina la baba kitu kilichozidi kuaminisha kwamba anahusika moja kwa moja ili kumukomoa baada ya kusikia akitutangazia sifa mbaya familia yetu.

Kifo kile kiliongeza sifa mbaya kufikia hatua familia ya aliyekuwa mpenzi wa marehemu dada Monika kuja kutushambulia kwa maneno ya kutuita wachawi.

Siku hiyo nilikuwepo, mama wa marehemu alikuja nyumbani na kuanza kutoa shutuma nzito kusema kwa sauti ya juu huku watu wakisikiliza”

“Mmeniulia mwanangu kwa imani zenu za kichawi ili muwe matajiri, kumuua mtoto wa Mihayo hamkuridhika mmemuua Monika na kumficha ndani kama chama bado tu mmeona haitoshi mmemuua mwanangu.

Nawaambia damu ya mwanangu haiendi bure.”
Taarifa zile zilipelekwa kwa baba ambaye aliita polisi na kumchukua yule mama na kumpeleka kituoni. Kwa kweli kilichoendelea sikujua zaidi ya kumsikia baba akitamba atamuonesha.

Pamoja na yule mama kupelekwa polisi familia yetu ilitawaliwa na sifa mbaya ambazo wengi walizisikia na kuzisambaza kwa watu kuwa maisha yetu yametawaliwa na utajiri wa kishirikina ulikuwa ukipitia kidonda cha marehemu dada.

Nilijikuta nikiishi maisha ya kukosa amani hata tembea yangu ilikuwa ya mashaka kwa kuhofia maneno ya watu. Siku zilikatika walisema mchana, usiku wakalala. Walizungumza sana mwisho wakanyamaza na kusahaulika na maisha yakaendelea.

Katika maisha yetu hakuna kilichobadilika, nilimaliza kidato cha nne kwa kupata matokeo mabaya. Niliamini kufanya vibaya kulitokana na migongano ya mawazo iliyotokana na kuchanganywa na mambo yote yaliyotokea yakihusu familia yetu, na taarifa nilizopewa na dada Monika kifo chake na matukio mengi ya kishirikina yaliyoilenga familia yetu.

Wazo la kurudia mtihani wa kidato cha nne, lilipingwa na baba na kusema atanipatia shughuli nyingine. Roho iliniuma kwani ndoto zangu zilikuwa kusoma kwa bidii ili siku moja nimkomboe mama kwenye mateso ya kuwekwa kifungoni na baba.

Miezi sita baada ya matokeo mbaya ya kidato cha nne, baba alionesha mapenzi makubwa tofauti na zamani hata kuzunguka naye kila kona kwenye shughuli zake. Siku nyingine alinipa pesa za matumizi ambazo alinieleza ninunue kitu chochote nikitakacho.

Kwa akili za kitoto nilianza kubadilika na kuyaona yote niliyoelezwa juu ya ukatili wa baba ni uongo. Baba alikuwa mtu mzuri kwa kuninunulia nguo za thamani, nilionekana kweli mtoto wa mtu mwenye pesa tofauti na mwanzo nilivyokuwa nasoma shule.

Baba siku zote alinisikifia kuwa mimi ndiye mtoto anipendaye kuliko wote, kauli zile za baba zilinifanya nisahau hata wazo la kumuuliza juu ya dada Monika.

Siku moja tulikuwa tumekaa kwenye moja ya hoteli ya baba huku akiniruhusu kula nikitakacho, baada ya chakula baba alinichukua na kuingia naye kwenye ofisi yake iliyokuwa ndani ya hoteli ile ambayo sikuwahi kuingia siku za nyuma.

Baada ya kuingia ofisini baba aliendelea kunimwagia sifa.
“Masalu unajua nakupenda sana kuliko watoto wangu wote”
“Najua baba”

“Hebu niambie unataka nini nikufanyie ili ujue napenda sana”
“Cha kwanza kunipa nafasi ya kurudia masomo niliyoanguka katika mtihani wangu ili nifanye vizuri bado nina hamu ya kuendelea kusoma”

“Tofauti na hilo?”
“Siwezi kusema kwa sasa mpaka nitakapofanya mtihani wangu wa marudio.”
“Masalu, kusoma si muhimu sana kwako, kama pesa zipo nitakufungulia mradi wako ili uendeleze maisha yako”
“Lakini...”

“Masalu hakuna haja ya kubishana, naomba ujiandae kuna duka moja nimelifungua na kuanza kazi wewe ndiye msimamizi mkubwa “
Nilijikuta nakosa cha kuzungumza na kukubaliana na baba japo nafsi yangu ilitaka kusoma ili nimkomboe mama yangu.

Nilijua kukubali mradi ule japo utakuwa chini yangu bado utakuwa wa nguvu za kishirikina kwa ,kuhofia huenda siku za mbele baada ya kuoa na kupata mtoto akatolewa kafara.

Baba alinitolea hati za kumiliki duka lile lenye jina langu na kunionesha sehemu ya kusaini, Nilisaini na kuniahidi kunifanyia mambo makubwa kuliko ndugu zangu wote. Baada ya kutoka pale aliniingiza kwenye gari lake na kunipeleka mjini barabara ya Pamba kwenye duka langu.

Nililikuta duka lipo wazi na watu wakiendelea na mauzo ya vitu, lilikuwa duka kubwa la kuuza vitu vya jumla na rejareja. Tulipofika dada mmoja ambaye alikuwa akinifahamu aliniuliza:

“Leo Masalu ndiyo umeamua kuja?”
“Alikuwa anamalizia masomo,” baba alijibu.

“Karibu bosi”
“Asante,”
Nilijibu huku nikiingia dukani na kwenda kukaa kwenye kiti changu kilichoandaliwa kwa ajili ya kukalia niwapo kazini. Baada ya kukagua duka lililokuwa likilingana na maduka ya ndugu zangu. Baba aliondoka na kuniacha nisimamie duka langu.

Alinipitia jioni na kunirudisha nyumbani, nilipofika nyumbani nilimueleza mama kuwa nimepewa duka na baba. Ajabu mama badala ya kufurahi alitokwa na machozi
 
Sehemu ya 10

Alinipitia jioni na kunirudisha nyumbani, nilipofika nyumbani nilimueleza mama kuwa nimepewa duka na baba. Ajabu mama badala ya kufurahi alitokwa na machozi, kwa vile tulikuwa peke yetu nilimuuliza:
“Mama unalilia nini?”
“Mmh, najua hukufurahi na inaweza usifurahi”

“Kwa nini mama?”
“Ni vigumu kunielewa kwa sasa lakini tumuombe Mungu aepushe mbali.”
“Mama mbona sikuelewi?”
“Suala la shule limeishia wapi?”
“Baba amekataa na kusema tayari ameisha nifungulia duka, na leo ndiyo nimekabidhiwa rasmi”

“Mmh! Haya”
“Kwani kuna nini?”
“Hakuna ubaya”
“Mama kuna kitu hutaki kuniambia”
“Hakuna kitu kikubwa zaidi ya kukatika kwa ndoto yako ya kusoma”
“Mama nitasoma tu”

“Kwa duka lako, si unawaona ndugu zako walivyo bize na maduka yao hata muda wa kunikumbuka hawana”
“Mama nitajipanga, siku hizi kuna masomo ya jioni.”

Siku zilikatika biashara nayo ilizidi kushika kasi, hata mwili wangu ulibadilika na kuonekana mtu mzima kutokana na kunenepa hata sauti yangu ilibadilika.

Lakini ilikuwa tofauti na wenzangu, mimi nilibakia nyumbani na mama pamoja na mfanyakazi mmoja, niliamua kumpumzisha mama kazi za shamba, lakini mama aling’ang’ania kwa kusema kama akiacha kwenda shamba atafukuzwa na baba.

Nilipomuuliza baba naye alinijia juu na kunionya nisingilie mambo yake, sikuwa na jinsi, nilimuacha mama aendelee kulima huku nikitumia vijana kumsaidia mama, ambaye alifanya kazi ndogo ndogo. Kingine ambacho sikukubaliana na baba ni kuhusu mavazi ya mama yaliyokuwa yamechoka.

Hapo sikukubali hata kidogo na nilikuwa tayari kwa lolote.
“Masalu unataka tubishane,” baba alinikalipia.

“Kwa hili baba sikubaliani nawe hata kidogo.”
“Umeanza kuvimba kichwa kwa vipesa unavyopata?”

“Si kuvimba kichwa, nipo sahihi, kama mali zako chukua lakini nimechoka kuiona hali hii mpaka lini?”

Sikuogopa chochote cha baba mpaka tulipokubaliana kumnunulia mama nguo mpya, pamoja na mzozano huo bado baba hakuonekana kukasirika sana. Mama alibadilika kuvaa vitenge vya gharama hata kandambili alivaa mpya.

Ndugu zangu walipokuja nyumbani hawakuamini kumkuta mama yetu kapendeza. Walipomuuliza aliwaeleza ni kwa ajili yangu, walinifuata kutaka kujua nimewezaje kumbadili baba kukubali mama kuvaa nguo mpya. Niliwaeleza ni msimamo hakuna kitu kingine, maisha yaliendelea.

Katika vitu ambavyo baba alinionya ni kutembea na wanawake, nilikumbuka kauli za dada Monika kuwa alianza kuelezwa asijihusishe na wanaume na mwisho wa siku alipata kidonda cha kichawi.

Nilimkubalia kumridhisha tu, lakini niliendelea kuwa na mahusiano na binti mmoja ambaye ndiye tuliyepanga kuoana siku za mbeleni. Siku zote mambo yangu nilikuwa nayafanya kwa siri kubwa bila baba kujua kwa kuamini sina uhusiano wa kimapenzi na mwanamke.

Siku moja nikiwa nimelala niliota kitu kama nyoka, lakini sikukielewa vizuri kikiniuma kwenye mguu wa kulia kwa ndani juu ya jicho la mguu. Nilishtuka lakini hakukuwa na kitu chochote, niliendelea kulala. Kesho yake nilikwenda dukani kama kawaida na kuendelea na shughuli zangu.

Wiki moja baadaye nilianza kusikia muwasho sehemu niliyoota nimeumwa na kitu kama nyoka. Nilimueleza mama asubuhi baada ya kujikuna mpaka kukaleta weusi sehemu iliyokuwa ikiniwasha. Mama alishtuka kitu kilichonitisha.

”Mama mbona umeshtuka?”
“Baba yako alikueleza nini?”
“Kuhusu nini?”

“Huo muwasho wako.”
“Hata, sijazungumza lolote.”
“ Mmh!” Mama aliguna.
“Unaguna nini?” nilimuuliza.

“Hapana”
“Mbona kama inanitisha, unakuwa hauna tofauti na wa dada Monika?”
“Ni kweli.”
“Unataka kuniambia ndiyo huu?”
“Ndiyo.”

“Mungu wangu nimekwisha,”
“Wala hujaisha, ukifuata masharti yake hauna tatizo.”
“Kwa hiyo na mimi nitakuwa na kidonda kama dada Monika?”

“Ndiyo lakini hakiumi”
“Na nikikosea nitakufa kama dada Monika?”
“Monika kafa na yake”
“Mamaa, juzi tulizungumza nini, leo unanibadilikia,” nilimuona mama akitaka kuficha mambo.

“Masalu nakuomba suala hili muulize baba yako na usimueleze kuwa tumezungumza.”
“Sawa mama.”

Niliachana na mama huku mwili wote ukininyongea kwa kujua niliyoelezwa na dada Monika yametimia.

Siku ile hata hamu ya kwenda kwenye duka langu sikuwa nayo, kwa kuamini nilikuwa nimeisha haribika. Nilishinda ndani huku nikilia lakini mama alitumia muda wake kunibembeleza kuwa sijaharibika kama ninavyo fikiria.

“Masalu usilie mwanangu.”
“Mama kwa nini mnanitendea unyama kama huu kosa langu nini?”

“Huna kosa mwanangu, kidonda hiki humfuata yule aliyeteuliwa na mizimu.”
“Wataniteua vipi wakati mimi sitaki?”
“Huwezi kukataa.”
“Mama nina malengo yangu wewe unajua.”
“Ni kweli, lakini hakuna wa kumzuia baba yako uamuzi wake.”

“Mama na mimi nitakufa kama dada Monika?”
“Kwa nini?’
”Siwezi kufuata masharti ni magumu.”
“Si magumu akizingatia.”

“Siwezi mama siwezi...,” nilikatwa kauli na sauti ya baba aliyekuwa akimwita mama. Nilimuona mama akishtuka na kuanza kutetemeka na kijasho mbali kilimvuja.
“Mama vipi?”

“Naomba usimwambie baba yako niliyokueleza, ataniua.”
“Siwezi kumwambia.”
“Ng’wana Manoni.”
“Lama,” mama aliitikia huku akitoka chumbani kwangu.

“Vipi mbona unatoka chumbani kwa mtoto?”
“Hajisikii vizuri.”
“Na shamba hujaenda?”
“Baba Mihayo nimwache Masalu anaumwa niende shamba.”

“Kwani anaumwa sana?”
“Toka asubuhi analia tu.”
“Kafanya nini?”
“Mmh, nenda ndani ukamuone.”
“Masalu,” baba aliniita.

“Naam baba.”
“Eti kuna nini?”
“Kuna vitu ambavyo sielewi.”
“Vitu gani?” Baba alisema huku akiingia ndani.

Alipoingia ndani alinikuta nimeshikilia mguu.
“Kuna nini?”
“Baba sehemu hii inaniwasha sana kufikia hatua ya kunikosesha raha.”
“Hebu nione,” nilimuonesha baba baada ya kuona alisema.

“Kumbe hiki?”
“Ndiyo baba.”
“Sasa tatizo nini?”
“Kinaniwasha.”
“Usikikune kitapoa chenyewe.”
“Hapana baba bora niende hospitali.”
“Masalu usiende hospitali, ugonjwa juu si wa kawaida.”

“Wa nini?”
“Utajua tu baadaye, lakini chonde usiende hospitali.”
“Au ndiyo kama wa dada Monika.”
“Eti?” Kauli yangu ilimshtua baba na kunitazama mara mbili kama ndiyo siku yangu ya kwanza kuniona.

“Eti umesemaje?”
“Baba mbona umeshtuka hivyo?”
“Sijakuelewa, hebu rudia swali lako.”
“Nauliza, kisiwe kidonda kama cha dada Monika.”

“Mama yako ndiyo kwakwambia leo atanitambua,” baba alikuja juu.
“Baba badala ya kunijibu swali langu unakimbilia kutaka kumpiga mama au ndiyo umemuona gunia lako la mazoezi,” nilizidi kumchanganya baba na maneno yangu ambayo akufikiria hata siku moja nitayatamka.

“Masalu mbona unanikosea heshima.”
“Sijakukosea heshina ila nataka kujua ukweli wa muwasho huu kwa vile nilibashiliwa kipindi kirefu.”

“Na nani?”
“Na dada Monika”
“Alikubashiria nini?’
“Alinieleza kuwa kifo chake kimetokana na kukikataa kidonda hiki, na ulichomuahidi ndicho kilichotokea.”
“Muongo unamsingizia Monika wakati uongo wote kakupa mama yako.”

“Baba utamuonea mama bure, mama hajanieleza chochote zaidi ya kunifanya mtoto mdogo mambo ninayoyajua.”
“Mambo gani?”

“Kuhusu chanzo cha utajiri kidonda cha dada Monika mpaka kifo chake kilisababishwa nini na utabiri wake kidonda kikitoka kwake kinakuja kwangu.”

“Mmh,” baba aliguna, kisha alinitazama kwa muda na kuangalia juu kabla ya kushusha tena pumzi.

“Masalu.”
“Naam.”
“Niambie ukweli mama yako kakuambia nini juu ya huu muwasho?”
“Kaniambia ni muwasho wa kawaida, utakao poa wenyewe.”

“Hakukuambia kitu kingine?”
“Hajaniambia, ndiyo maana nilijua ananidanganya, dada Monika alinipa siri nyingi, zingine hata mama hajui na bahati mbaya wakati anakufa nilikuwa mbali lakini kuna mengi mazito alitaka kunipa juu ya familia yetu.”

“Monika alikuambia nini?”
“Alinieleza jinsi kidonda chake kilianza kama muwasho na mwisho wa siku kilikuwa kidonda kisichouma zaidi ya kutoka maji na kukatazwa asiyafute.”

“Mmh, pamoja na uongo wake nakuomba usimuamini ni mfitini yule.”
“Baba unataka kunihakikishia kidonda hiki sio kama cha dada Monika?”
“Nimekueleza usimfuate Monika ni muongo.”
“Kama muongo naomba na mimi uniondolee masharti ya kuwa na mke.”

“Masalu, umri wako bado.”
“Baba mimi si mdogo, ukweli ni kwamba huu muwasho mwisho wake ni kidonda ambacho kitaingiza pesa kwa njia ya kumwagika maji. Baada ya dada Monika kuyashindwa na masharti yako uliamua kumuua na mimi nahofia utaniua.”

“Narudia tena kukueleza Monika ni muongo.”
“Baba nasema kama ndicho kidonda hiki basi nami nitakufa kama dada Monika.”
“Masalu kuna sababu ya kuzungumza kwa kituo.”

“Sawa baba lakini kaa ukijua kama muwasho huu mwisho wake ni kidonda cha utajiri sikitaki nakuomba unirudishe shuleni.”
“Nikurudishe shuleni fedha za shule utazipata wapi?”

“Kwani lazima nipate kidonda ili nisome?”
“Utasoma, lakini kumbuka fedha zinatafutwa na njia zake pesa zipo nyingi.”

“Moja wapo ni kidonda changu?”
“Masalu tutazungumza, hebu vaa kuna mali mpya nimeituma dukani mwako twende ukaiangalie.”

“Sawa baba,” nilikubali shingo upande na kukubali kuondoka na baba kwenda dukani kwangu. Nilipanga kutokwenda dukani baada ya kupata uhakika wa mwasho wangu.

Niliondoka na baba hadi dukani ambako alinionesha baadhi ya bidhaa alizoniagizia toka China, vilikuwa vitu vingi sana ambavyo vilifanya duka langu liongezeke.

Kwa muda mfupi hata ndugu zangu walianza kunionea wivu. Wazo la haraka lilikuwa huenda aliyoyafanya dada Monika ya kutaka naye awe na maisha yake ndiyo yaliyosababisha hali ile.

Hali ya muwasho iliendelea kupungua na kuweka kitu kama gamba kwenye weusi ule. Siku moja asubuhi ilipoamka nilikuta lile gamba limetoka kutokana na kujigeuza na kuweka kidonda.

Moyo wangu ulilipuka na kujua kazi imeanza, kutokana na maelezo ya awali kidonda kile hakikutakiwa kutibiwa.
Nilijikuta nikikosa raha pamoja na mali zote alizonipa baba sikuwa na furaha yoyote moyoni mwangu kuishi na kidonda kisicho wekewa dawa mpaka mwisho wa maisha yangu.

Nilipoamka na kukuta hali ile nilimweleza mama, naye alinipa jibu jepesi.
“Aliyokueleza dada yako yametimia.”
“Mama nitafanya nini, nitaishi hivi mpaka lini?”

“Masalu, ondoa wasiwasi kama nilivyokueleza toka mwanzo usishtuke sana kwa vile hali hii niliisha kueleza mapema uishi vipi baada ya kutokea kwa hali hii.”

“Mama kusema ni rahisi, lakini haivumiliki, nitaishi vipi na watu wakijua nina kidonda kama cha dada Monika nitauweka wapi uso wangu?”

“Nani atajua, labda utawaonesha wewe.”
“Duniani hakuna siri”
“Ukitaka iwe siri itakuwa siri.”
“Lakini kwa nini umenifanya hivi si mngeniuliza kuliko kunipa kidonda bila idhini yangu?”
“Mimi utanilaumu bure wa kumlalamikia ni baba yako.”

“Mama nami nitakufa kama dada siwezi kuishi maisha ya mipaka.”
Nilimuhakikishia mama sitakubali kuishia maisha yale bali nitakayo amua mwenyewe.
Siku ile mama aliniomba nisivae viatu na soksi bali nivae sandoz ili nisikibuguzi kidonda ambacho kilikuwa kimeanza kutoa maji.

Ugumu wa kuishi maisha ya kidonda nilianza kuuona kwa kuamini mabadiliko yangu ya mavazi lazima watu watataka kujua kumetokea kitu gani kilichopelekea hali ile.
Siku ile nilishinda ndani nikilia japo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom