Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,998
- 453,891
- Thread starter
- #81
Sehemu ya 13
“Masalu kwa nini hutaki kumsikiliza baba”
“Nimsikilize kwa lipi?”
“Juu ya wewe kuwa na mwanamke.”
“Mna uhakika gani?”
“Sisi hatuna uhakika ila kasema mwenyewe.”
“Ninyi mna wapenzi?” Niliwauliza.
“Tunao.”
“Sasa mimi nazuiwa na nini?”
“Si unajua hali yako haitaki uwe na mwanamke?”
“Kwa hiyo kidonda niwe nacho mimi maisha mazuri muwenayo ninyi, sikilizeni kila mtu ataubeba mzigio wake mwenyewe.”
“Masalu utakuja kuijutia kauli yako.”
“Sijuitii mbona dada Monika hakuijutia na mkiniua na ninyi mnafirisika kazi kwenu.”
Maneno yangu yaliwazima mdomo waliondoka na kuniacha wakiwa hawana hamu na mimi.
Tokea siku ile nikawa adui yao mkubwa, niliwashangaa kunikasirikia mimi kuwa na mwanamke wakati wao walikuwa na kila kitu. Kama mateso ya kidonda nimeyakubali bado hawaridhiki walitaka nikose na raha za dunia.
Ukali wa baba ulipogonga mwamba na kumtumia mama kunibembeleza, nani msimamo wangu ulikuwa pale pale wa kukataa kulala na mwanamke.
“Masalu jihurumie usije kufa kama dada yako Monika.”
“Mama mkiniua nani atakayebeba kidonda, dada Monika alinieleza kuwa wote mliotaka kuwapa kidonga mizimu iliwakataa.”
“Ni kweli, lakini unatakiwa uionee huruma familia yako.”
“Mama ninyi hamnionei huruma, mimi nitawaonea vipi?”
“Kumbuka kama utaendelea kufanya kama usipokufa wewe basi utampoteza baba yako.”
“Mama kila mwanadamu hufa kwa ahadi yake na wala si kwa ajili yangu.”
“Kwa hiyo una mwanamke?”
“Nilikuwa naye lakini sasa hivi kabakia rafiki.”
“Mbona baba yako kaelezwa kuwa unautia mwili wako uchafu ndicho chanzo wa kidonda chako kukauka na kufanya mambo yote yaanze kusimama?”
“Lakini mama kama kidonda nimekubali kwa nini mniwekee vikwazo kwenye maisha yangu?”
“Si vikwanzo bali masharti ya mizimu.”
“Kama ni masharti ya kunyanyasana mimi siyawezi, kama mali zenu chukueni na mimi niacheni na maisha yangu.”
“Masalu unajiamini nini mwanangu?”
“Sina cha kujiamini bali ukweli ndiyo huo.”
“Basi baba nakuomba nipo chini ya miguu yako kama una mwanamke achana naye.”
“Nikueleze mara ngapi kuwa sina.”
“Najua tumekufanyia kitu kibaya lakini mabadiliko ya kidonda chako ni hayo hayo.”
Niliachana na mama ambaye niliona na yeye ananizingua, sikutaka kukosa vyote, mavazi nilibadilika kuvaa siku zote nilivaa suruali za kitambaa ili kuogopa kukitonesha kidonda, sikuruhusiwa tena kuvaa viatu zaidi ya sandoz. Kila mmoja alinihoji uwezo wangu wa kifedha na mavazi yangu.
Nilikuwa na duka kubwa kuliko ndugu zangu, lakini wao ndio walionekana wana maisha mazuri. Nami sikutaka kushindana nao, kwa vile kidonda nilijua hakitoki mwilini mwangu nami niliamua kutumia kilicho ndani ya uwezo mwangu.
Nilianzisha tabia ya kumuhonga pesa mpenzi wangu ili naye afaidi kama ndugu zangu kutokana na kuonekana wao ndiyo wenye thamani. Siku moja niliamka asubuhi nyumbani kwangu kama kawaida na kushangazwa kukuta baba yangu na ndugu zangu wakiwa nje ya nyumba yangu.
Eti shida yao kubwa kunifumania na mwanamke, niliwashangaa watu wazima kama wale kuacha kazi zao ya msingi kutaka kunifumania mimi. Ajabu ya Mungu siku ile mpenzi wangu hakulala nyumbani, sikutaka kupigizana nao kelele. Niliwaruhusu wamtafute, walifanya upekuzi bila kuona lolote.
“Jamani kama bado hamharidhika semeni niwafungulie wapi mkatafute?”
“Wee chonga lakini lazima utakumbuka siku moja kuwa sisi tulitangulia kuzaliwa.”
“Hilo ni dua la kuku ambalo halitanipa asilani.”
Wote waliondoka na kuniacha nikijiuliza kama wangemkuta na mwanamke wangenifanya nini maana walionekana kabisa walikuja kishari.
Baada ya kuondoaka niliapa kufanya ninachokiweza sikuwa tayari kugeuzwa kitega uchumi cha watu. Niliendelea kufanya mapenzi na mpenzi wangu kama kawaida japo hata biashara kwenye duka langu zilidoda hazikwenda kama mwanzo.
Yote hayo sikuyafikiria zaidi ya kusubiri litakalo tokea japo mama alijitahidi kunibembeleza niachane na yote yanayoonekana yanaharibu biashara za familia yetu ikiwemo na yangu. Baada ya kuona maneno yamezidi nilianza kuwa mlevi kila muda nilikuwa nimelewa kitu kilichozidi kuichanganya familia yangu.
Siku moja nikiwa faragha na mpenzi wangu nilishangaa kuziona sehemu zangu za siri zimeingia ndani nilishtuka sana. Hali ile ilinifanya nikose raha kwa kuamini zile zilikuwa njama za familia yangu kutaka kuona sifanyi mapenzi na mwanamke.
“Masalu kwa nini hutaki kumsikiliza baba”
“Nimsikilize kwa lipi?”
“Juu ya wewe kuwa na mwanamke.”
“Mna uhakika gani?”
“Sisi hatuna uhakika ila kasema mwenyewe.”
“Ninyi mna wapenzi?” Niliwauliza.
“Tunao.”
“Sasa mimi nazuiwa na nini?”
“Si unajua hali yako haitaki uwe na mwanamke?”
“Kwa hiyo kidonda niwe nacho mimi maisha mazuri muwenayo ninyi, sikilizeni kila mtu ataubeba mzigio wake mwenyewe.”
“Masalu utakuja kuijutia kauli yako.”
“Sijuitii mbona dada Monika hakuijutia na mkiniua na ninyi mnafirisika kazi kwenu.”
Maneno yangu yaliwazima mdomo waliondoka na kuniacha wakiwa hawana hamu na mimi.
Tokea siku ile nikawa adui yao mkubwa, niliwashangaa kunikasirikia mimi kuwa na mwanamke wakati wao walikuwa na kila kitu. Kama mateso ya kidonda nimeyakubali bado hawaridhiki walitaka nikose na raha za dunia.
Ukali wa baba ulipogonga mwamba na kumtumia mama kunibembeleza, nani msimamo wangu ulikuwa pale pale wa kukataa kulala na mwanamke.
“Masalu jihurumie usije kufa kama dada yako Monika.”
“Mama mkiniua nani atakayebeba kidonda, dada Monika alinieleza kuwa wote mliotaka kuwapa kidonga mizimu iliwakataa.”
“Ni kweli, lakini unatakiwa uionee huruma familia yako.”
“Mama ninyi hamnionei huruma, mimi nitawaonea vipi?”
“Kumbuka kama utaendelea kufanya kama usipokufa wewe basi utampoteza baba yako.”
“Mama kila mwanadamu hufa kwa ahadi yake na wala si kwa ajili yangu.”
“Kwa hiyo una mwanamke?”
“Nilikuwa naye lakini sasa hivi kabakia rafiki.”
“Mbona baba yako kaelezwa kuwa unautia mwili wako uchafu ndicho chanzo wa kidonda chako kukauka na kufanya mambo yote yaanze kusimama?”
“Lakini mama kama kidonda nimekubali kwa nini mniwekee vikwazo kwenye maisha yangu?”
“Si vikwanzo bali masharti ya mizimu.”
“Kama ni masharti ya kunyanyasana mimi siyawezi, kama mali zenu chukueni na mimi niacheni na maisha yangu.”
“Masalu unajiamini nini mwanangu?”
“Sina cha kujiamini bali ukweli ndiyo huo.”
“Basi baba nakuomba nipo chini ya miguu yako kama una mwanamke achana naye.”
“Nikueleze mara ngapi kuwa sina.”
“Najua tumekufanyia kitu kibaya lakini mabadiliko ya kidonda chako ni hayo hayo.”
Niliachana na mama ambaye niliona na yeye ananizingua, sikutaka kukosa vyote, mavazi nilibadilika kuvaa siku zote nilivaa suruali za kitambaa ili kuogopa kukitonesha kidonda, sikuruhusiwa tena kuvaa viatu zaidi ya sandoz. Kila mmoja alinihoji uwezo wangu wa kifedha na mavazi yangu.
Nilikuwa na duka kubwa kuliko ndugu zangu, lakini wao ndio walionekana wana maisha mazuri. Nami sikutaka kushindana nao, kwa vile kidonda nilijua hakitoki mwilini mwangu nami niliamua kutumia kilicho ndani ya uwezo mwangu.
Nilianzisha tabia ya kumuhonga pesa mpenzi wangu ili naye afaidi kama ndugu zangu kutokana na kuonekana wao ndiyo wenye thamani. Siku moja niliamka asubuhi nyumbani kwangu kama kawaida na kushangazwa kukuta baba yangu na ndugu zangu wakiwa nje ya nyumba yangu.
Eti shida yao kubwa kunifumania na mwanamke, niliwashangaa watu wazima kama wale kuacha kazi zao ya msingi kutaka kunifumania mimi. Ajabu ya Mungu siku ile mpenzi wangu hakulala nyumbani, sikutaka kupigizana nao kelele. Niliwaruhusu wamtafute, walifanya upekuzi bila kuona lolote.
“Jamani kama bado hamharidhika semeni niwafungulie wapi mkatafute?”
“Wee chonga lakini lazima utakumbuka siku moja kuwa sisi tulitangulia kuzaliwa.”
“Hilo ni dua la kuku ambalo halitanipa asilani.”
Wote waliondoka na kuniacha nikijiuliza kama wangemkuta na mwanamke wangenifanya nini maana walionekana kabisa walikuja kishari.
Baada ya kuondoaka niliapa kufanya ninachokiweza sikuwa tayari kugeuzwa kitega uchumi cha watu. Niliendelea kufanya mapenzi na mpenzi wangu kama kawaida japo hata biashara kwenye duka langu zilidoda hazikwenda kama mwanzo.
Yote hayo sikuyafikiria zaidi ya kusubiri litakalo tokea japo mama alijitahidi kunibembeleza niachane na yote yanayoonekana yanaharibu biashara za familia yetu ikiwemo na yangu. Baada ya kuona maneno yamezidi nilianza kuwa mlevi kila muda nilikuwa nimelewa kitu kilichozidi kuichanganya familia yangu.
Siku moja nikiwa faragha na mpenzi wangu nilishangaa kuziona sehemu zangu za siri zimeingia ndani nilishtuka sana. Hali ile ilinifanya nikose raha kwa kuamini zile zilikuwa njama za familia yangu kutaka kuona sifanyi mapenzi na mwanamke.