SIMULIZI: Sura Ya Kivuli

SIMULIZI: Sura Ya Kivuli

daaah yale yale ya arosto[emoji41][emoji41][emoji41][emoji58][emoji58][emoji58]
 
MKUU UMEAMUA KUIBA STORY YANGU


Samahani naomba i story uisome na uiache kule kule ulipo itoa. watu tume tumia akiri na mda mwingi sana kuandika afu wewe una kuja ku copy tu











[emoji23] [emoji23] [emoji23] ayo yalikua maneno ya member mmoja wa JF kweny story kama ii

Sent from my VFD 301 using JamiiForums mobile app
 
Sehemu ya sita °06°


...tumsubiri CAPTAIN tujue tunamfanya nin huyu mjingamjinga...!!??? Hadi hapo bado nilikua nikiomba mungu ili anitoe kwenye janga hili na haya majangili na baada ya muda mfupi alikuja mtu mnene na aliyefunika sura ake na wote wakasema "karibu CAPTAIN" Sasa nikajua muda wangu umefika na yule dereva akamkabidhi yule CAPTAIN vitu vyangu vyote na kumuuliza tumfanye nini huyu... Aliniangalia na kisha kunisogelea na kisha kunishika mabega yangu na hapo nilikua nikitetemeka kutokana na uzito wa mikono ake na kufikiria kitu gani kinachofuata na kisha akasema kwa sauti ya chini " fungua uso wangu " nilitoa kitambaa alichovaa usoni na kwa kweli sikuamini macho sura ambayo niliokua nikiona machoni mwangu....!!!!!

Baada ya kushuka kwenye ndege 24-KEYBOARD alikwenda kwanza kukodisha chumba katika nyumba ya wageni iliyokua karibu na stendi ya mabasi ili asubuhi ake aanze safari ya kuelekea kijijini kwao, anapata chumba na kujipumzisha na kuanza kukumbuka ni jinsi gani hadi alifika kwenye jumba lile walikotoka, yeye alikua ni mtaalamu wa maswala ya tehama lakini tofauti na nurdin huyu alikua amesoma katika chuo kikubwa duniani cha tehama na alikua ni 1 kati ya vijana waliokua na ujuzi mkubwa katika maswala ya kudukua kitu chochote kwa haraka. Alizaliwa katika familia yenye kipato kikubwa na aliweza kusoma katika mazingira mazuri kutokana na baba yake kufanya kazi katika taasisi ya fedha serikalini na aliishi miaka mingi nje ya nchi na aliporudi nchini ndipo alipokutana na mwanadada mmoja aitwae Nuru na walianza mahusiano na kwa muda mfupi Keyboard alionekana kumpenda Nuru sana kutokana na jinsi alivyokua akifanyiwa vitu ambavo ughaibuni hakuwahi kukutana navyo na ilimfanya yeye kutotamani kurudi huko alikotoka na hadi hapo alifikia maamuzi ya kwenda kuwataarifu wazazi wake kuwa anataka kuoa. Baba yake mzee Zuru Mbini akamwambia kijana wake SHAM (keyboard) kuwa kabla ya kutafuta mke wa kuishi nae kwanza alitakiwa kutafuta juu ukweli uliofichika kuhusu kifo tata cha babu yake mzee Mbini sham ambacho hadi leo hajajulikana ni nani alihusika na kwanini babu yake aliuwawa kikatili na hakupatikana muuaji na njia pekee ya kuweza kujua ukweli huo ilikua ni kujiunga idara ambayo babu yake alikua akiifanyia kazi na ilikua ni idara ya usalama wa nchi. Sham (keyboard) aliambiwa hawezi kuruhusiwa kua na mke mpaka atakapoweza kujua sababu ya kifo tata cha babu yake. Na hadi sham anarudi tayari baba yake alikua ashatumia kila njia kijana wake nae awepo katika vijana watakaochukuliwa na idara hiyo. Hapa keyboard anakua anajiunga ili tu kujua sababu ya babu yake kuuwawa...Ghafla mlango ubagongwa na Keyboard anastuka kutoka katika vitu ambavo alikua akifikiria na kuuliza ni nani wewe na sauti ya mwanaume ikajibu ni muhudumu nimekuletea taulo na anafungua mlango na kupokea taulo na kurudi ndani na kuangalia saa anaona mda wa kupata chakula cha usiku unakaribia na anatoka nje ya nyumba ya wageni akiwa amebeba begi lake na kwenda kutafuta chakula. Alifika kwenye mgahawa mmoja na akaagiza aletewe chipsi na wakati alikua anakula alisikia mabishano ya vijana wawili wakibishana kuhusu simu waliokua wameishika wakisema hii simu haitoweza kutoka neno la siri na mwingine akisema inawezekana na hapo mmoja wao akasema yeyote atakaweza kutoa neno la siri kweny simu hiyo angegawa chipsi bure siku yote. Kutokana na upweke aliokua nao keyboard aliamua kumwita kijana muuza chipsi na kumwambia ampe simu hiyo na kijana yule akauliza unaweza kufanya simu hii itoke neno la siri..!?? Keyboard alijibu ndio na akafungua begi lake na kutoa kompyuta ndogo na kutoa waya na kuunganisha kutoka kwenye kompyuta hadi kwenye simu na baada ya dakika 4 alimrudishia ile simu na akasimama na kuongea kwa sauti kubwa..."CHIPSI BUREEEEEEEEEE..!!!!" na watu walianza kusogea na kuanza kuchukua chipsi za bure na alirudisha ile kompyuta kwenye begi na kumwambia yule kijana amfuate lakini bado yule kijana aliendelea kutoa macho katika sehemu ya chipsi jinsi watu walivyokua wakigombania zile chipsi na keyboard alianza kuondoka na yule alimfuata na kumuuliza je huoni kama umeniharibia biashara yangu na keyboard alimjibu "thamani ya simu ulioshika ni mara tatu ya biashara ako na akampa namba ya simu akamwambia piga hii na namba na utauza simu hiyo kwa bei kubwa sana.
Anarudi hadi alipokua na analala na asubuhi yake anakwenda kwenye stendi ya mabasi kwa ajili ya kurudi nyumbani.

Itaendelea...
 
asante kiongozi ila ongezea ongezea kidogo umetupunja[emoji52][emoji52]
 
Sehemu ya saba •07•

....Anarudi hadi alipokua analala na asubuhi yake ankwenda kwenye stendi ya mabasi kwa ajili ya kurudi nyumban. Baada ya basi kuwasili katika mji ambao sham anaishi anapiga simu kwa dereva aliyemfuata na kumwambia amewasili na yupo nje ya stand ya mabasi na anafuatwa na kuingia ndani ya gari na kuelekea nyumbani kwao.
Nurdin anapofungua sura ya CAPTAIN anabaki na mshangao na tabasamu lilianza kuonekana na kumwambia kumbe ni wewe KAMBI, wanakumbatiana na kusalimiana na huku wale wafuasi wengine walianza kushangaa kilichokua kinatokea pale na CAPTAIN anaanza kwa kusema "huyu ni ndugu yetu na huyu mmoja kati ya waanzilishi wa kikundi hiki huko nyuma", anamkabidhi vitu vyake na kumwambia hakikisha kam vipo salama vimetimia na dereva atakufikisha salama hadi nyumbani. Anafika nyumbani na kupokelewa na wazazi wake na baada kupumzika na kupata chakula anaitwa faragha na baba yake na kuulizwa kuhusu barua ambayo alituma siku chache za nyuma, Nurdin anamjibu baba yake kuwa yote ni kweli na amebakiza wiki mbili kurudi huko kwenye maisha yake mapya na baba yake anamtakia kila la heri kijana wake na kumwambia afuate kile moyo wake unachopenda. Baada ya wiki anawaaga nyumbani kwao na kuwaambia kuwa amepata nafasi ya kuendeleza elimu yake nje ya nchi, anapanda basi kurudi alipokua anaishi na kuwasili jioni na anapofika kwenye chumba chake anashusha begi na kujilaza kitandani na kuanza kufikiria majukumu atayokuja kukutana nayo huko mbeleni, akiwa anaanza kusinzia mara ghafla simu yake inaita na anapopekea inasikika sauti ya kiume ..." hallo nina simu aina ya [emoji768] na nimeambiwa unatafuta na anataja na bei. [emoji768] ni aina ya simu ambayo nilikua naipenda na aliponiambia bei yake ilikua ni ndogo na nilimjibu kesho aniletee na ntainunua. Baada ya siku mbili nilihamisha vitu vyote na kuviuza na vingine niligawa kwa wapangaji wenzangu mule ndani na nilienda kupanga nyumba ya wageni kwa ajili ya siku zilizobakia na baada ya wiki kuisha nilipigiwa simu kufika mahala fulani kwa ajili ya kuanza maisha mapya.
.....Katika mtaa mmoja kulionekana kikundi cha watu kikiwa kinamvuta vuta kijana mmoja huku wengine wakiwa wanampiga makofi na mateke wakidai ni mwizi na adhabu yake yafaa auwawe lakini kikundi kile kilidai wao ni mwizi wao na watamalizana nae wenyewe na wanaenda nae kuingia katika nyumba fulani na kumwambia wanahitaji warudishiwe gari yao aliokua anafanyia kazi ya tax na anawajibu kuwa atawalipa gharama za gari yao na fidia lakini hawakutaka kumsikiliza na kumwambia tutakachokufanyia leo hutosahau, mmoja kati ya watu wale anasema hebu tumpeni nafasi ya kuongea huyu Dulla. Wanamwachia na anaanza kuongea kwa tabu na sauti ya chini na kusema " nimeanza kazi ya udereva tax kabla yenu nyinyi wote hapa na nimeenda kukaa jela mara 3 kwa makosa ambayo sikuwahi kufanya lakini nilijipa moyo na hadi hadi kifungo cha mwisho kupata msamaha wa raisi na niliporudi hapa kijiweni niliapa kuwa mwadilifu na dereva bora kuwahi kutokea lakini mara nyingi nakutana na mitihani ambayo mungu hunipa na pamoja na mara ya mwisho nilikua na gari yenu na nitawalipa gari yenu na mmoja kati yenu atoke nyuma ya nyumba hii atafute sehemu ambayo ilichimbwa na kufukiwa na afukue na atakuta kiasi cha pesa na mchukue na mniache na maisha yangu" ...Mmoja ya watu wale anatoka na baada ya dakika kadhaa aarudi akiwa ameshika mfuko uliokua na hela na anwaambia humu kuna fedha nying zinatosha hata kununua magari mawili kama lililopotea na wote wanabaki na mshangao na kumwambia wewe hizi fedha zote umetoa wapi lakini dulla anawajibu kama mmepata fedha zenu naomba mniache na maisha yangu. Wanaamua kumuacha na kuondoka watu wote wakimwambia una bahati umelipa na fidia za usumbufu. Huyu ni DEREVA na anakjikaza na kwenda nyuma ya jumba lile na kufukua sehemu na kutoa simu na anaiwasha na kupiga namba moja na kusema "nipo tayari mnifuate"........

Inaendelea
 
Sehemu ya saba •07•

....Anarudi hadi alipokua analala na asubuhi yake ankwenda kwenye stendi ya mabasi kwa ajili ya kurudi nyumban. Baada ya basi kuwasili katika mji ambao sham anaishi anapiga simu kwa dereva aliyemfuata na kumwambia amewasili na yupo nje ya stand ya mabasi na anafuatwa na kuingia ndani ya gari na kuelekea nyumbani kwao.
Nurdin anapofungua sura ya CAPTAIN anabaki na mshangao na tabasamu lilianza kuonekana na kumwambia kumbe ni wewe KAMBI, wanakumbatiana na kusalimiana na huku wale wafuasi wengine walianza kushangaa kilichokua kinatokea pale na CAPTAIN anaanza kwa kusema "huyu ni ndugu yetu na huyu mmoja kati ya waanzilishi wa kikundi hiki huko nyuma", anamkabidhi vitu vyake na kumwambia hakikisha kam vipo salama vimetimia na dereva atakufikisha salama hadi nyumbani. Anafika nyumbani na kupokelewa na wazazi wake na baada kupumzika na kupata chakula anaitwa faragha na baba yake na kuulizwa kuhusu barua ambayo alituma siku chache za nyuma, Nurdin anamjibu baba yake kuwa yote ni kweli na amebakiza wiki mbili kurudi huko kwenye maisha yake mapya na baba yake anamtakia kila la heri kijana wake na kumwambia afuate kile moyo wake unachopenda. Baada ya wiki anawaaga nyumbani kwao na kuwaambia kuwa amepata nafasi ya kuendeleza elimu yake nje ya nchi, anapanda basi kurudi alipokua anaishi na kuwasili jioni na anapofika kwenye chumba chake anashusha begi na kujilaza kitandani na kuanza kufikiria majukumu atayokuja kukutana nayo huko mbeleni, akiwa anaanza kusinzia mara ghafla simu yake inaita na anapopekea inasikika sauti ya kiume ..." hallo nina simu aina ya [emoji768] na nimeambiwa unatafuta na anataja na bei. [emoji768] ni aina ya simu ambayo nilikua naipenda na aliponiambia bei yake ilikua ni ndogo na nilimjibu kesho aniletee na ntainunua. Baada ya siku mbili nilihamisha vitu vyote na kuviuza na vingine niligawa kwa wapangaji wenzangu mule ndani na nilienda kupanga nyumba ya wageni kwa ajili ya siku zilizobakia na baada ya wiki kuisha nilipigiwa simu kufika mahala fulani kwa ajili ya kuanza maisha mapya.
.....Katika mtaa mmoja kulionekana kikundi cha watu kikiwa kinamvuta vuta kijana mmoja huku wengine wakiwa wanampiga makofi na mateke wakidai ni mwizi na adhabu yake yafaa auwawe lakini kikundi kile kilidai wao ni mwizi wao na watamalizana nae wenyewe na wanaenda nae kuingia katika nyumba fulani na kumwambia wanahitaji warudishiwe gari yao aliokua anafanyia kazi ya tax na anawajibu kuwa atawalipa gharama za gari yao na fidia lakini hawakutaka kumsikiliza na kumwambia tutakachokufanyia leo hutosahau, mmoja kati ya watu wale anasema hebu tumpeni nafasi ya kuongea huyu Dulla. Wanamwachia na anaanza kuongea kwa tabu na sauti ya chini na kusema " nimeanza kazi ya udereva tax kabla yenu nyinyi wote hapa na nimeenda kukaa jela mara 3 kwa makosa ambayo sikuwahi kufanya lakini nilijipa moyo na hadi hadi kifungo cha mwisho kupata msamaha wa raisi na niliporudi hapa kijiweni niliapa kuwa mwadilifu na dereva bora kuwahi kutokea lakini mara nyingi nakutana na mitihani ambayo mungu hunipa na pamoja na mara ya mwisho nilikua na gari yenu na nitawalipa gari yenu na mmoja kati yenu atoke nyuma ya nyumba hii atafute sehemu ambayo ilichimbwa na kufukiwa na afukue na atakuta kiasi cha pesa na mchukue na mniache na maisha yangu" ...Mmoja ya watu wale anatoka na baada ya dakika kadhaa aarudi akiwa ameshika mfuko uliokua na hela na anwaambia humu kuna fedha nying zinatosha hata kununua magari mawili kama lililopotea na wote wanabaki na mshangao na kumwambia wewe hizi fedha zote umetoa wapi lakini dulla anawajibu kama mmepata fedha zenu naomba mniache na maisha yangu. Wanaamua kumuacha na kuondoka watu wote wakimwambia una bahati umelipa na fidia za usumbufu. Huyu ni DEREVA na anakjikaza na kwenda nyuma ya jumba lile na kufukua sehemu na kutoa simu na anaiwasha na kupiga namba moja na kusema "nipo tayari mnifuate"........

Inaendelea

Go on nimeipenda hii stori
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom