fenisher
JF-Expert Member
- Apr 27, 2017
- 339
- 733
Sehemu ya kwanza °01°
Asubuhi na mapema foru anapoamka na kufungua macho yake anaangaza huku na kule anagundua sehemu alipokua amelala si mahala pake na anapoinuka anashindwa kusimama na anaanza kuhisi maumivu ya mwili mzima na kichwa kinauma sana, anakaa na kuanza kuangalia chumba chote na anagundua pembeni ake kuna watu wawili wamelala wakiwa karibu karibu,mmoja alionekana mwanamke na mwingine mwanaume, hadi mda huo akili yake ilikua haijakaa sawa na anaamua kutuliza akili na kufikiria kabla ya kulala alikua wapi?!!, alikua na nani? na alikua anafanya nini? Lakini cha ajabu anashindwa kukumbuka kitu chochote kutoka katika ubongo wake na hali hiyo inamfanya mapigo yake ya moyo kwenda kasi ghafla na anagundua hakumbuki kitu chochote kutoka kwenye ubongo wake. Anaamua kujikaza na kuinuka kuelekea mlangoni kwa mwendo wa polepole na anapokaribia mlangoni anagundua ameipita kamera iliyokua bado inaendelea kurekodi vidio ikiwa imesimamishwa katika stendi yake, akili ake inapata kumbukumbu ya kuwa yeye ndiye aliyekua anaiweka kamera hiyo pale ilipo na kumbukumbu kukata, swala hilo linamfanya abadili mawazo ya kutoka ndani ya chumba iko na kuifata kamera ili aone matukio ambayo kamera imechukua toka mwanzo kwani hiyo ingemsaidia katika kurudisha kumbukumbu zake kichwani na anapoikaribia na kuishika kamera GHAFLA..!! Mlango unavunjwa na kuingia watu wakiwa wamevaa suti wote pamoja na miwani meusi na kila mmoja wao akiwa ameshika silaha aina ya bunduki na kutamka maneno kwa sauti ya juu " ukisogeza hata ukucha nakudungua risasi" Kauli hiyo inamfanya foru agande kama roboti na kudondosha kamera chini, hapo inamrudia kumbukumbu ya yeye akiwa anakabidhiwa bunduki na mtu na anaambiwa amtwange risasi mtu ambaye aliyekua mbele ake na nafsi yake inakataa na kudondosha bunduki chini kuashiria hawezi kufanya jambo hilo. Anaporudi kutoka katika kumbukumbu bado alikua amewapa kisogo watu wale walioingia ndani kwa kuvunja mlango na wanamwambia ageuke nyuma huku mikono yake ikiwa juu, anapogeuka na kuwaangalia watu hao ila kitu cha ajabu watu wote wanaanza kumshangaa na mmoja wao akisema kwa sauti ya chini " haiwezekani mtu huyu yupo hai" watu wale walionekana kuogopa kumkaribia moja kwa moja na hali hiyo inamfanya aanze kufikiria ni kwanini watu wenye miili iliyoshiba na wanaonekana wako sawa kiafya wanaogopa kumsogelea yeye ambaye ni mwembamba na dhoofu kwa anavyookana. " K.. mfunge pingu mimi nakulinda" alisikika mmoja wa watu wale akiwa anamwangalia mwenzake aliyekua upande wake wa kushoto na kumuonyesha ishara ya kusogea alipokua amesimama Foru na anamwambia wa upande wa kulia akawaangalie watu waliokua wamelala pale chini. Foru anapowaangalia watu wale anagundua wapo makini kwa kila hatua wanayokanyaga na anapowahesabu anagundua wapo watu saba lakini kila mmoja wao akiwa katika sehemu yake katika hali ya utulivu na ukakamavu,.. " mheshimiwa waziri amefariki na mkewe pia" alisema yule aliyeambiwa akague watu wale waliolala pale....kumbukumbu inarudi kukumbuka nikiwa nakabidhiwa nishani ya maua na mwanaume nikiwa nimevalia joho na mkononi nikiwa nimeshika cheti pamoja na kofia ya joho nililovaa na kumbukumbu inakatika tena. Yule aliyeambiwa aje kunifunga pingu alikua ameshanifikia na alikua ni mtu mwenye tahadhari kubwa na kunigeuza na akaanza kunifunga pingu huku akisema " uaijaribu kufany upumbavu wowote" Wakati ananiinua na kunisamamisha niliweza kuona nje kupitia dirisha la vioo kuwa tuko juu milima yani nje kote kulikua na milima na nikagundua sehemu tuliokuepo ni mlimani juu kabisa ...Jambo la kushangaza niliweza kupiga mahesabu ya kujirusha dirishani lakini kabla ya hapo nilitakiwa kuchukua begi lililo karibu na dirisha na kudondokea chini ya milima hiyo, ndani ya sekunde kadhaa nilipata jibu na haraka kumsukuma yule mtu mmoja aliyeniweka pingu na kuchukua bag na kujitupa kwenye dirisha lenye vioo na milio ya risasi ilinifuata kwa nyuma na kuvaa begi hewani nikiwa nadondoka kwenda chini ya milima hiyo. Hapa kuna kitu Foru alikua anawaza akiwa anadondoka kwanini!!? yule jamaa alimfunga pingu kwenye mkono mmoja na alimfinya mara mbili na yeye ndio akapata akili ya kuchukua begi na kujirusha kupitia dirishani......
Asubuhi na mapema foru anapoamka na kufungua macho yake anaangaza huku na kule anagundua sehemu alipokua amelala si mahala pake na anapoinuka anashindwa kusimama na anaanza kuhisi maumivu ya mwili mzima na kichwa kinauma sana, anakaa na kuanza kuangalia chumba chote na anagundua pembeni ake kuna watu wawili wamelala wakiwa karibu karibu,mmoja alionekana mwanamke na mwingine mwanaume, hadi mda huo akili yake ilikua haijakaa sawa na anaamua kutuliza akili na kufikiria kabla ya kulala alikua wapi?!!, alikua na nani? na alikua anafanya nini? Lakini cha ajabu anashindwa kukumbuka kitu chochote kutoka katika ubongo wake na hali hiyo inamfanya mapigo yake ya moyo kwenda kasi ghafla na anagundua hakumbuki kitu chochote kutoka kwenye ubongo wake. Anaamua kujikaza na kuinuka kuelekea mlangoni kwa mwendo wa polepole na anapokaribia mlangoni anagundua ameipita kamera iliyokua bado inaendelea kurekodi vidio ikiwa imesimamishwa katika stendi yake, akili ake inapata kumbukumbu ya kuwa yeye ndiye aliyekua anaiweka kamera hiyo pale ilipo na kumbukumbu kukata, swala hilo linamfanya abadili mawazo ya kutoka ndani ya chumba iko na kuifata kamera ili aone matukio ambayo kamera imechukua toka mwanzo kwani hiyo ingemsaidia katika kurudisha kumbukumbu zake kichwani na anapoikaribia na kuishika kamera GHAFLA..!! Mlango unavunjwa na kuingia watu wakiwa wamevaa suti wote pamoja na miwani meusi na kila mmoja wao akiwa ameshika silaha aina ya bunduki na kutamka maneno kwa sauti ya juu " ukisogeza hata ukucha nakudungua risasi" Kauli hiyo inamfanya foru agande kama roboti na kudondosha kamera chini, hapo inamrudia kumbukumbu ya yeye akiwa anakabidhiwa bunduki na mtu na anaambiwa amtwange risasi mtu ambaye aliyekua mbele ake na nafsi yake inakataa na kudondosha bunduki chini kuashiria hawezi kufanya jambo hilo. Anaporudi kutoka katika kumbukumbu bado alikua amewapa kisogo watu wale walioingia ndani kwa kuvunja mlango na wanamwambia ageuke nyuma huku mikono yake ikiwa juu, anapogeuka na kuwaangalia watu hao ila kitu cha ajabu watu wote wanaanza kumshangaa na mmoja wao akisema kwa sauti ya chini " haiwezekani mtu huyu yupo hai" watu wale walionekana kuogopa kumkaribia moja kwa moja na hali hiyo inamfanya aanze kufikiria ni kwanini watu wenye miili iliyoshiba na wanaonekana wako sawa kiafya wanaogopa kumsogelea yeye ambaye ni mwembamba na dhoofu kwa anavyookana. " K.. mfunge pingu mimi nakulinda" alisikika mmoja wa watu wale akiwa anamwangalia mwenzake aliyekua upande wake wa kushoto na kumuonyesha ishara ya kusogea alipokua amesimama Foru na anamwambia wa upande wa kulia akawaangalie watu waliokua wamelala pale chini. Foru anapowaangalia watu wale anagundua wapo makini kwa kila hatua wanayokanyaga na anapowahesabu anagundua wapo watu saba lakini kila mmoja wao akiwa katika sehemu yake katika hali ya utulivu na ukakamavu,.. " mheshimiwa waziri amefariki na mkewe pia" alisema yule aliyeambiwa akague watu wale waliolala pale....kumbukumbu inarudi kukumbuka nikiwa nakabidhiwa nishani ya maua na mwanaume nikiwa nimevalia joho na mkononi nikiwa nimeshika cheti pamoja na kofia ya joho nililovaa na kumbukumbu inakatika tena. Yule aliyeambiwa aje kunifunga pingu alikua ameshanifikia na alikua ni mtu mwenye tahadhari kubwa na kunigeuza na akaanza kunifunga pingu huku akisema " uaijaribu kufany upumbavu wowote" Wakati ananiinua na kunisamamisha niliweza kuona nje kupitia dirisha la vioo kuwa tuko juu milima yani nje kote kulikua na milima na nikagundua sehemu tuliokuepo ni mlimani juu kabisa ...Jambo la kushangaza niliweza kupiga mahesabu ya kujirusha dirishani lakini kabla ya hapo nilitakiwa kuchukua begi lililo karibu na dirisha na kudondokea chini ya milima hiyo, ndani ya sekunde kadhaa nilipata jibu na haraka kumsukuma yule mtu mmoja aliyeniweka pingu na kuchukua bag na kujitupa kwenye dirisha lenye vioo na milio ya risasi ilinifuata kwa nyuma na kuvaa begi hewani nikiwa nadondoka kwenda chini ya milima hiyo. Hapa kuna kitu Foru alikua anawaza akiwa anadondoka kwanini!!? yule jamaa alimfunga pingu kwenye mkono mmoja na alimfinya mara mbili na yeye ndio akapata akili ya kuchukua begi na kujirusha kupitia dirishani......