Simulizi: Scaila Michael

SEHEMU YA 27

Wakati mwingine nilimchukua na kwenda naye huko ilipokuwa nyumba hiyo, mafundi walikuwa wakiendelea kuijenga kwa nguvu kubwa, kila siku ilikuwa ni lazima wafike hapo na kuendelea na mambo yao.

Nilipanga kuhamia ndani ya nyumba hiyo siku ambayo nitafunga ndoa na Scaila. Nilimueleza hilo kabisa lakini sikutaka kumwambia ni siku gani nilitamani sana kumuoa.

Nakumbuka siku hiyo ilikuwa ni Jumapili ya mwezi wa tatu, nilipokea simu kutoka kwa Hiza na Ally ambao waliniambia walikuwa wakija nyumbani kumuona shemeji yao maana kila siku niliwaambia waje kumuona ila walikuwa na mambo mengi.

Nilimwambia Scaila, nikamwambia ni lazima ahakikishe anavaa vizuri, anapendeza ili marafiki hao watakapokuja basi wachanganyikiwe na kuona nimekuwa mwanaume ninayejua kuchagua mwanamke mzuri.

Hawa wawili huwa wananijua, sikuwa mtu mwepesi kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi, ninapenda sana kukaa singo kwa kipindi kirefu nikifanya mambo yangu binafsi ila ninapoamua kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi, huwa ninamchagua mwanamke mzuri mno.
Walinizoea hivyo tangu tulipokuwa chuo mpaka kipindi hicho.

Katika kipindi chote huko nyuma waliniambia siku ambayo ningeoa, basi ningemuoa mwanamke mbaya kuliko wote katika dunia hii kwa sababu tu nilipenda kutembea na wanawake wazuri.

“Huyo mkeo, najua atakuwaje! Nishapata picha yale,” aliniambia Hiza huku akicheka, kipindi hicho tulikuwa chuo.
“Mke wangu atakuwa mkali sana, zaidi ya mkeo, zaidi ya mke wa Ally, yaani atakuwa pini, pini kweli,” nilimwambia.
“Hahaha! Mzee baba utachagua koroma!” alisema Ally.

“Mtaona tu.”
Maneno hayo niliyakumbuka vilivyo, niliwatambia sana na sasa ulikuwa muda wa kuwaonyeshea nilikuwa makini kwa kile nilichowaambia miaka ya nyuma, niliamini kila mmoja angemkubali huyu Scaila kwani hakuwa na uzuri wa kawaida.

Ilipofika majira ya saa tisa alasiri, wakanipigia simu na kuniambiwa walikuwa njiani wakija. Nikawakaribisha na kumwambia Scaila ajiandae.

“Wanakuja!” nilimwambia.
“Haina shida. Nawasubiri!” alisema Scaila, hapohapo akamwambia Grace aandae chakula kabisa kwani muda si mrefu wageni wangeingia.
Yatakayotokea ni kwamba kina Ally wanamjua scaila ndani nje
 
SEHEMU YA 31

Maisha baina yangu na Scaila yalikuwa matamu sana, tulipendana kwa dhati na muda mwingi tulikuwa pamoja.

Sikuyaona madhaifu yake kwa wakati huo, kila nilipokuwa nikirudi nyumbani nilipokelewa kwa mbwembwe nyingi na mahaba tele.

Kiukweli hapo ndipo niligundua unapokuwa kwenye mapenzi mazito una nguvu ya kufanya kitu chochote kile.

Scaila aliuteka moyo wangu, alilifahamu hilo na alihakikisha kila siku ninakuwa mtu wa furaha katika maisha yangu yote.

Kwa kweli sikutaka kumfuatilia kabisa hasa kwenye simu yake, nilihitaji awe huru, afanye lolote analolitaka lakini aniheshimu na kujua kwamba mimi ni mume wake mtarajiwa.

Mambo yalikuwa mazuri mpaka pale ambapo niliona anakuwa bize sana na simu. Kama ni kuchati, basi kwa Scaila ilikuwa si mchezo, kila wakati aliishikilia simu yake na kuandika meseji kwenda kwa watu wengine.

Kwa sababu nilimpenda, sikutaka kabisa kumfuatilia, sikutaka kuona akikasirika kwani yeye ndiye alikuwa furaha yangu katika maisha yangu kipindi hicho.

Nilianza kuingiwa na shaka kuhusu simu yake, ila wakati mwingine nilijiambia sikutakiwa kuwa hivyo kwa sababu nilipenda, na mtu ukimpenda, jambo la kwanza kabisa unatakiwa kumwamini.

Hivyo ilikuwa ni hivyo, hata alipokuwa akiiacha simu yake hapo, iwe inaita au ujumbe wa maneno kuingia wala sikujishughulisha nao hata kidogo.

Nakumbuka kuna siku nilirudi nyumbani majira ya saa kumi, siku hiyo niliwahi kwa sababu nilimaliza biashara zangu mapema sana hasa kwenye kukusanya mahesabu na hivyo nilihitaji muda mwingi wa kupumzika.

Nilipofika nyumbani, nilimkuta Grace lakini Scaila hakuwepo nyumbani. Sikutaka kuwa na wasiwasi naye kwa sababu nilimwamini sana.

Nilikaa sebuleni huku nikiendelea kufanya mambo yangu kwenye kompyuta yangu ya mapajani.

Muda ulikwenda lakini hakurudi nyumbani, nilianza kuingiwa na wasiwasi, ikanibidi nifanye maamuzi ya kumpigia simu na kumuuliza alipokuwa. Kabla ya kufanya hivyo, kitu cha kwanza nikaona lingekuwa jambo jema nijue mahali alipokuwa, nikamuita Grace na kumuuliza.

“Wifi yako yupo wapi?” nilimuuliza.
“Alikwenda kwa mama!” alinijibu.
 
SEHEMU YA 32

Hapo nikaona sikutakiwa kumpigia simu. Sijui kwa nini ilikuwa hivyo, nilijiona kuwa na wasiwasi mwingi sana, sikuwa nikijiamini kwa kweli.

Ndani hakukukalika, nikaondoka na kuelekea nyumbani kwao huko Tababa. Nilipofika, nikapaki gari nje na kuingia ndani. Hakukuwa na haja ya kugonga geti, nilizama moja kwa moja, nikagonga mlango wa sebuleni na mama yake kunikaribisha.

Nilipoingia, mama yake akashtuka mno, ni kama hakutarajia kuniona mahali hapo. Nilishangaa hali hiyo lakini sikutaka kumuonyeshea kama nilishangaa, hivyo nikamtolea tabasamu pana.

“Shikamoo mama!” nilimsalimia kwa unyenyekevu.
“Marahaba mwanangu! Karibu!” alinikaribisha.

Nilikaa na kuanza kuzungumza naye! Sikujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea mahali hapo, wakati mama akijiandaa kuinuka kuelekea chumbani, ghafla nikamsikia Scaila akija kutokea ukumbini huku akiongea na mtu ambaye sikujua alikuwa nani, ila alikuwa mwanaume kwa kuwa sauti yake niliisikia vilivyo.

Walipofika sebuleni na macho yake kuniona, alishtuka mno! Ni kama mtu aliyeshtuliwa na jambo fulani kubwa. Sikujua kilichokuwa kikiendelea, nilishangaa sana.

Mwanaume yule aliponiangalia, hakushtuka, akanisalimia kisela huku kila nilipokuwa nikimwangalia Scaila, niliona kabisa hakuwa sawa.

“Karibu mpenzi!” alisema Scaila, akaja na kunikumbatia, nikaanza kuisikia harufu ya manukato mengine ambayo sikuwahi kuyasikia.

Alipotoka kifuani mwangu, akili yangu ikacheza haraka sana, nikamsogelea mwanaume yule na kumpa mkono, yale manukato ambayo niliyasikia kwa Scaila yalikuwa ya huyu jamaa kwani naye alinukia vilevile.

“Karibu sana!” aliniambia.
Haraka sana mama yake Scaila akanyanyuka na kuanza kutoa utambulisho. Akaniambia ni jambo jema nimekuja muda muafaka kwani yule kaka yake Scaila aliyewahi kuniambia alikuwa huyo.

Niseme ukweli kwanza! Huyu mwanamke hakuwahi kuniambia kuhusu kaka yake Scaila, nilishangaa, kwa haraka sana nikaanza kuvuta kumbukumbu kwamba inawezekana kweli aliwahi kuniambia kuhusu kaka huyo lakini sikupata jibu lolote lile.
“Anaitwa Alfred!” alisema.
 
SEHEMU YA 33

Hapo akili yangu ikapiga kengele. Jina hilo halikuwa geni, niliwahi kulihisi kabla. Siku ile nilipokuwa nikila chakula na Scaila, namba hiyo ilipiga kwenye simu yake, sikuwa na uhakika kama jina lilikuwa Alfred ama Albert, ila leo nikapata uhakika kwamba mtu aliyepiga alikuwa huyo Alfred, ila yeye aliniambia alikuwa Janeth.

Hapo nikashikwa na machale zaidi, nikahisi kabisa kulikuwa na kitu kilichokuwa kikiendelea, ila kwa sababu nilikuwa mwanaume, sikutaka kujali sana, nikajifanya kupotezea na hapo ndipo nilipoanza kazi rasmi ya kumchunguza huyu Scaila.

Niligundua inawezekana alikuwa na michezo mingi nje ya kumi na nane aliyokuwa akiicheza ila sikuwa nikiijua kwa undani. Ilikuwa ni lazima nifanye kila linalowezekana kuhakikisha naujua ukweli kabisa.

Scaila hakuwa demu, alikuwa mchumba wangu ambaye nilipanga kufunga naye ndoa, hivyo kupoteza muda wangu kwa lengo la kumchunguza halikuwa tatizo hata kidogo.

“Akitoka Alfred ndiyo anaingia Scaila,” aliniambia mama yake bila kuona aibu hata kidogo.

“Nimefurahi kumfahamu!” nilisema huku nikiwa nimetoa tabasamu pana kweli, yaani sikutakiwa kuonekana nikiwa na shaka hata kidogo.

Basi tukaongea mambo mengi, muda mwingi nilikuwa na furaha mno, nilihitaji kuwaaminisha kwamba sikuwa na wasiwasi na Alfred hata kidogo, hivyo ilikuwa ni lazima nionekane nipo kawaida kumbe upande wa pili niliamua kuanza kazi yangu ya kumpeleleza huyu Scaila, alikuwa nani na alijishughulisha na nini?
Nikamchukua na kuanza kurudi naye nyumbani.

Nilimletea unafiki mwingi, stori zilikuwa nyingi mno, nilichangamka kupita kawaida kumbe moyo wangu ulikuwa na maumivu makali mno.

Tukafika nyumbani na kuelekea sebuleni. Tukaingia na kuendelea kupiga stori, tulicheka pamoja na kula kisha kuelekea chumbani.

Siku hiyo nilihitaji kujifanya kuwa bize na mambo yangu kumbe nilihitaji kufanya jambo fulani kubwa. Nilijua kuhusu mambo ya kompyuta, jinsi application ya WhatsApp ilivyokuwa ikifanya kazi kwenye kompyuta kupitia kitu kiitwacho WhatsApp Web.
 
SEHEMU YA 31

Maisha baina yangu na Scaila yalikuwa matamu sana, tulipendana kwa dhati na muda mwingi tulikuwa pamoja.

Sikuyaona madhaifu yake kwa wakati huo, kila nilipokuwa nikirudi nyumbani nilipokelewa kwa mbwembwe nyingi na mahaba tele.

Kiukweli hapo ndipo niligundua unapokuwa kwenye mapenzi mazito una nguvu ya kufanya kitu chochote kile.

Scaila aliuteka moyo wangu, alilifahamu hilo na alihakikisha kila siku ninakuwa mtu wa furaha katika maisha yangu yote.

Kwa kweli sikutaka kumfuatilia kabisa hasa kwenye simu yake, nilihitaji awe huru, afanye lolote analolitaka lakini aniheshimu na kujua kwamba mimi ni mume wake mtarajiwa.

Mambo yalikuwa mazuri mpaka pale ambapo niliona anakuwa bize sana na simu. Kama ni kuchati, basi kwa Scaila ilikuwa si mchezo, kila wakati aliishikilia simu yake na kuandika meseji kwenda kwa watu wengine.

Kwa sababu nilimpenda, sikutaka kabisa kumfuatilia, sikutaka kuona akikasirika kwani yeye ndiye alikuwa furaha yangu katika maisha yangu kipindi hicho.

Nilianza kuingiwa na shaka kuhusu simu yake, ila wakati mwingine nilijiambia sikutakiwa kuwa hivyo kwa sababu nilipenda, na mtu ukimpenda, jambo la kwanza kabisa unatakiwa kumwamini.

Hivyo ilikuwa ni hivyo, hata alipokuwa akiiacha simu yake hapo, iwe inaita au ujumbe wa maneno kuingia wala sikujishughulisha nao hata kidogo.

Nakumbuka kuna siku nilirudi nyumbani majira ya saa kumi, siku hiyo niliwahi kwa sababu nilimaliza biashara zangu mapema sana hasa kwenye kukusanya mahesabu na hivyo nilihitaji muda mwingi wa kupumzika.

Nilipofika nyumbani, nilimkuta Grace lakini Scaila hakuwepo nyumbani. Sikutaka kuwa na wasiwasi naye kwa sababu nilimwamini sana.

Nilikaa sebuleni huku nikiendelea kufanya mambo yangu kwenye kompyuta yangu ya mapajani.

Muda ulikwenda lakini hakurudi nyumbani, nilianza kuingiwa na wasiwasi, ikanibidi nifanye maamuzi ya kumpigia simu na kumuuliza alipokuwa. Kabla ya kufanya hivyo, kitu cha kwanza nikaona lingekuwa jambo jema nijue mahali alipokuwa, nikamuita Grace na kumuuliza.

“Wifi yako yupo wapi?” nilimuuliza.
“Alikwenda kwa mama!” alinijibu.
@shunie mamaa ya 30 mbonaa siionii
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom