Simulizi: Scaila Michael

Simulizi: Scaila Michael

Ndio maana kesi za mapenzi hua siziingilii.... hapo namuona Hiza akiwa katika wakati mgumu.
 
SEHEMU YA 42

Nikakata simu na kukaa kwenye kiti. Yaani ni ghafla tu uso wangu ukaanza kuwa na tabasamu pana, nilihisi kuridhika, nilihisi kama dunia nzima mimi ndiye niliyekuwa nikipendwa kuliko wote.

“Inawezekana hata Hiza atakuwa amenidanganya, anakuwaga na masihara sana yule,” nilijisemea, yaani mapenzi yalikuwa si mchezo mpaka Hiza nilimuona kama muongo fulani hivi.

Niliendelea kuwa kazini lakini akili yangu ilikuwa nyumbani, sikutaka kupoteza muda sana, ni majira ya saa kumi na mbili, nikarudi na kuelekea huko.

Nilikuwa na presha kubwa, sikutaka kuendelea kukaa muda wote huo pasipo kuonana na msichana huyo. Nikiwa njiani, niliona gari likianza kuchemka sana, haikuwa kawaida hata kidogo.

Ilinishangaza mno na hata nilipokuwa nikisikilizia taili la mbele, nilihisi lilipata pancha, hivyo nikaanza kumuomba Mungu nifike salama nyumbani.

Nilipofika, Grace akafungua geti na kuliingiza gari ndani. Haraka sana nikaliangalia lile taili, ni kweli lilipata pancha hivyo nisingeweza kutoka nalo.

Nikaliacha na kuelekea ndani, kwanza nilitaka nimuone Scaila, kipenzi cha moyo wangu, nilitamani nimkumbatie baada ya kuhusu alikuwa akinidanganya kwa kunisaliti.

“Waooo! Mpenzi...” alinikaribisha kwa mbwembwe, akanisogelea, akanikumbatia na kunimwagia mabusu mfululizo.

Hayo yote yalifanyika na kuzidi kumuona Hiza kuwa mtu mbaya sana kwani alitaka kunichonganisha na Scaila kwa kuniambia alikuwa malaya! Malaya gani alikuwa na mapenzi namna hii.
“Ngoja nikakuandalie maji!” aliniambia.
“Nitashukuru sana!”

Akaenda na kuniandalia maji. Nilikaribishwa kwa mbwembwe zote kiasi cha kunichanganya kabisa. Nilioga kwa dakika kadhaa na kutoka, nikamkuta amekaa kitandani, kama kawaida yake alikuwa na simu yake.

Hapo nikaanza kujiuliza maswali kama lingekuwa jambo zuri kuchukua laptop yangu na kufungua WhatsApp Web ama la! Nilihitaji kujua kila kitu kilichokuwa kikiendelea huko kwani ndipo ambapo uovu wake wote alikuwa akiufanya.
“Ngoja niingie! Abiria chunga mzigo wako!” nilijisemea.
 
SEHEMU YA 43

Haraka sana nikafungua laptop na kumwambia kuna kazi ya mahesabu nilitaka kuifanya, hakunishangaa kwani ilikuwa kawaida sana hasa kwa mfanyabiashara kama mimi.

Kweli nikaingia na kuanza kufanya kazi hiyo lakini upande mwingine nikafungua WhatsApp Web na kuanza kuangalia. Niliona jinsi alivyokuwa akiwasiliana na marafiki zake kitu ambacho kiliendelea kuniumiza.

Penny: Jana ilikuwa si mchezo! Katika maisha yangu nimemchukua mwanaume mwenye garden love kifuani.

Scaila: Ikawaje shoga yangu.
Penny: Yaani ilikuwa si mchezo. Uwiiiii....Jamani yule kaka anajua, yaani alinichanganya kupita kawaida.
Scaila: Wacha weeeee.

Penny: Akanikuna sana. Halafu nikamuona yule mwanaume wako wa Kiarabu, alikuja na kukuulizia.

Scaila: Munir?
Penny: Ndiyo! Nikamdanganya unaumwa, ila leo utakuwepo.

Scaila: Haiwezekani! Lazima nije klabu leo, lazima nije kwa gharama yoyote ile.

Akili yangu ni kama ilikuwa imezibuka na kurudi katika ile hali ya kwanza kabisa kwamba huyu Scaila hakuwa mwanamke wa kuishi naye kabisa.

Nilichukia mno kuwa ndani ya nyumba hiyo, ilikuwa yangu lakini kuna wakati nilijikuta nikianza kuchukia hata kuwa humo ndani.

Nikatoka chumbani na kuelekea sebuleni, nilibaki nikizungukazunguka tu, sikutulia, akili yangu ilishindwa kabisa kufanya maamuzi, nilimpenda sana Scaila na sikutaka kabisa kuona akifanya kitu chochote kile kibaya na ndiyo maana nilikuwa radhi kufanya lolote lile kwa ajili yake.

Wakati nikiwa sebuleni, nikasikia simu yangu ikiita, nilikuwa nimetoka nayo kwani kuna wakati nilihisi nilihitaji kuwasiliana na Ally na kumuomba ushauri kwani kwa kile kilichokuwa kikiendelea, kilinivuruga sana.

“Halo!” niliita, yaani kwa jinsi nilivyochanganyikiwa, nilipokea simu pasipo kujua mpigaji alikuwa nani, yaani nililiona jina lakini ubongo wangu ulishindwa kung’amua ni mtu gani alikuwa amenipigia simu muda huo.
“Halo!” niliita, sauti ilikuwa ya mwanamke.
|
|
|

Je, nini kitaendelea?
Tukutane Alhamisi.
 
Asante Shunie Kazi Nzuri.
SEHEMU YA 43
Haraka sana nikafungua laptop na kumwambia kuna kazi ya mahesabu nilitaka kuifanya, hakunishangaa kwani ilikuwa kawaida sana hasa kwa mfanyabiashara kama mimi.
Kweli nikaingia na kuanza kufanya kazi hiyo lakini upande mwingine nikafungua WhatsApp Web na kuanza kuangalia. Niliona jinsi alivyokuwa akiwasiliana na marafiki zake kitu ambacho kiliendelea kuniumiza.
Penny: Jana ilikuwa si mchezo! Katika maisha yangu nimemchukua mwanaume mwenye garden love kifuani.
Scaila: Ikawaje shoga yangu.
Penny: Yaani ilikuwa si mchezo. Uwiiiii....Jamani yule kaka anajua, yaani alinichanganya kupita kawaida.
Scaila: Wacha weeeee.
Penny: Akanikuna sana. Halafu nikamuona yule mwanaume wako wa Kiarabu, alikuja na kukuulizia.
Scaila: Munir?
Penny: Ndiyo! Nikamdanganya unaumwa, ila leo utakuwepo.
Scaila: Haiwezekani! Lazima nije klabu leo, lazima nije kwa gharama yoyote ile.
Akili yangu ni kama ilikuwa imezibuka na kurudi katika ile hali ya kwanza kabisa kwamba huyu Scaila hakuwa mwanamke wa kuishi naye kabisa.
Nilichukia mno kuwa ndani ya nyumba hiyo, ilikuwa yangu lakini kuna wakati nilijikuta nikianza kuchukia hata kuwa humo ndani.
Nikatoka chumbani na kuelekea sebuleni, nilibaki nikizungukazunguka tu, sikutulia, akili yangu ilishindwa kabisa kufanya maamuzi, nilimpenda sana Scaila na sikutaka kabisa kuona akifanya kitu chochote kile kibaya na ndiyo maana nilikuwa radhi kufanya lolote lile kwa ajili yake.
Wakati nikiwa sebuleni, nikasikia simu yangu ikiita, nilikuwa nimetoka nayo kwani kuna wakati nilihisi nilihitaji kuwasiliana na Ally na kumuomba ushauri kwani kwa kile kilichokuwa kikiendelea, kilinivuruga sana.
“Halo!” niliita, yaani kwa jinsi nilivyochanganyikiwa, nilipokea simu pasipo kujua mpigaji alikuwa nani, yaani nililiona jina lakini ubongo wangu ulishindwa kung’amua ni mtu gani alikuwa amenipigia simu muda huo.
“Halo!” niliita, sauti ilikuwa ya mwanamke.
|
|
|
Je, nini kitaendelea?
Tukutane Alhamisi.
[/QUOTE]
 
Niko mzima mm kidogo tu flue imenibana sana mobutu hofu kwako tu

Samahani sana kwa kutoka nje ya mada, naomba unisaidie link ya ile stori ya fadhili humu iliandikwa na Irene Mbowe,asante
 
Kama kweli alichokiandika nyemo kuna wanawake wanafanya hivyo basi kuni zitakazo wachoma naomba shetani aendelee kuziwekea mbolea ...
so sad
 
SEHEMU YA 20

Yaani nilivyokuwa nikiwaangalia marafiki wa Scaila niligundua walikuwa ‘malaya’ tu lakini kwa jinsi nilivyokuwa nikimpenda msichana huyo, nilimuona kama malaika vile, yaani eti malaika alikuwa kwenye kundi la mashetani.

Baada ya kuwasindikiza, akarudi na nikaanza kuongea naye mambo mengi sana. Alionekana kuwa mtu aliyechangamka sana, alinisifia kwa jinsi nilivyokuwa na mambo mengine mengi.
“Kwanza naomba namba yako,” nilimwambia.

“Tena afadhali! Jana nilitaka tuongee lakini ilishindikana!” aliniambia.
Tukabadilishana namba na mambo mengine kuendelea. Sikufichi, kipindi hicho nilijisikia furaha isiyo kifani, kuwa karibu na Scaila ilionekana kuwa bahati moja kubwa mno.

Pale kochini alipokuwa, nikamsogelea, nikamwangalia usoni na kuanza kutoa tabasamu pana ambalo lilikuwa ni kama matayarisho ya kitu fulani.

“Unataka kufanya nini? Hapana! Hapana Nye...” aliniambia huku akitoa tabasamu lakini hata kabla hajamaliza, alichokuwa akitaka kunikataza tayari nikaanza kukifanya, tukaanza kubadilishana mate kwa sekunde kadhaa, halafu tukaanza kuangaliana.

“Oh! It my fault, I’m sorry...” (Oh! Ni kosa langu, samahani...) nilimwambia huku tukiangaliana.

“Kwa nini umenifanyia hivi?” aliniuliza.
“Ndiyo maana nimesema samahani! Nilizidiwa!” nilijitetea, nikaona haitoshi, kulikuwa na kiumbe kingine nilikuwa sijakisingizia kesi, haraka sana nikakisingizia.

“Shetani alinipitia...”
Scaila akatabasamu, hapohapo haraka sana akanisogelea na kuanza tena. Niliona mtoto alidhamiria hivyo kumshika zaidi kwa dakika moja na kuachiana.

Naweza kusema huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa mapenzi yetu. Nikatokea kumpenda Scaila kuliko mwanamke yeyote yule. Niliona kama malaika fulani ambaye Mungu aliamua kunishushia, kumbe sikujua kama mwanamke huyu alikuwa na roho mbaya, ya kikatilia hata zaidi ya shetani.

Nilihisi kama nimeokota embe chini ya muarobaini kumbe niliopata shubiri chini ya mkomamanga.


|
|
|


Hii hadithi itakuwa inatoka Jumatatu na Alhamisi.
Stori nzuri nimeipenda bure kama kuna kitabu chake nitakua wa kwanza kununua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom